08 - Mambo Ya Haramu Kwa Vinyozi: Wanawake Kuwaosha Wanaume Nywele, Kuchuliwa (Massage)

Mambo ya Haramu yanayofanyika katika kazi ya Unyozi:

 

 

8. Baadhi Ya Vinyozi Kuweka Wanawake Wa Kuwaosha Wanaume Nywele Zao Na Hata Wengine Kuchuliwa (Massage) Na Wanawake

 

Ingawa nasaha hizi zilikusudiwa vinyozi wa nchi za Ulaya na mazingira mfano wake, lakini si vibaya kuchanganya na mazingira ya vinyozi walioko Afrika ambao ndio wengi hufanya jambo hili. Ifahamike kuwa hili ni jambo lisilofaa na kukubalika kishariy’ah, achilia mbali kidini, bali japo kimaadili na hayaa za kiuana Aadam ni jambo lililo kinyume na murua.

Ikiwa tu Rasuli katoa makemeo makali mno kwa mwanamme na mwanamke kupeana mikono au kugusana, ijekuwa kuoshwa mwanamme na mwanamke asiye mahram wake!

Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa alihi wa sallam):

“Mmoja wenu kudungwa kichwa kwa sindano ya chuma ni bora kwake kuliko kumgusa mwanamke asiyeruhusiwa kwake.” [At-Twabaraaniy katika Al-Mu’jam Al-Kabiyr na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Al-Jaami’]

 

Ee mja wa Allaah, jiweke mbali na makaripio hayo makali na epuka ukharibifu huo wa shariy’ah na maadili kwa tamaa za kuvuta wateja dhaifu walitawaliwa na matamanio ya nafsi. Usiwe wewe ndio kichocheo cha maasi na uchafu.

 

 

Share