04-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Nini Ihsaan katika ‘Ibaadah?

Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 04-Nini Ihsaan katika ‘ibaadah?

 

Maana ya Ihsaan katika i’baadah ni kujichunga kuwa makini katika ‘ibaadah kwa ajili Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee.

إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُمْ رَقِيبًا ﴿١﴾ 

Hakika Allaah daima Amekuwa juu yenu Mwenye kuchunga [An-Nisaa: 1]

الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ ﴿٢١٨﴾

Ambaye Anakuona wakati unaposimama. [Ash-Shu’araa: 218]

 

((الإحسانُ أَنْ تعبُدَ اللهَ كأنّك تراه فإن لَمْ تكن تراهُ فإنَّه يراك))  رواه مسلم

 ((Ihsaan ni kumuabudu Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama vile unamuona, na kama humuoni basi Yeye Anakuona)). [Muslim]

 

 

 

Share