06-Mukhtasari Aqiydah Ya Muislamu: Nini Tawhiyd ya Ilaah?

 Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

 

 

 

06-Nini Tawhiyd ya Ilaah?

 

Tawhiyd ya Ilaah ni kumfanyia ‘ibaadah Pekee Yeye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama du’aa, kuchinja, kuweka nadhiri na kadhaalika.

فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ

Basi jua kwamba laa ilaaha illa-Allaah, hapana Muabudiwa wa haki ila Allaah [Muhammad: 19]

Yaani: Hakuna apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah.

 

((فَلْيَكُنْ أَوَّلَ مَا تَدْعُوهُمْ إِلَيْهِ شَهَادَةَ أَنلاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ))  متّفق عليه  

أَيْ إِلَى أَنْ يوحّدوا الله

((Basi liwe jambo la kwanza la kuwalingania wao Kwake ni "Shahaadah kwamba hapana Muabudiwa wa haki isipokuwa Allaah)) [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Yaani; Wampwekeshe Allaah.

 

 

 

Share