13-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Zinazokubalika: Thanaa Na Kumswalia Nabiy

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Zinazokubalika

 

13-Kutawassal Kwa Thanaa Ya Allaah 

Na kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)

 

 

 

Thanaa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) maana yake ni kumtaja Allaah Ta'aalaa kwa majina Yake mazuri na Sifa Zake Zilizotukuka, na Matendo Yake adhimu  na kumsifu, kumhimidi, kumpwekesha na kumtukuza Allaah kwa maneno yenye kudhihirisha utukufu Wake ('Azza wa Jalla) na neema na fadhila Zake. Nayo yanapatikana katika Aayah nyingi za Qur-aan na katika Hadiyth za Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Mifano michache katika Qur-aan ni kama kumwita Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kusema

“Yaa…

بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ

Mwanzilishi wa mbingu na ardhi [Aayaat kadhaa katika Suwraa kadhaa imetaja]

 

 عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْكَبِيرُ الْمُتَعَالِ ﴿٩﴾

Mjuzi wa ghayb na dhahiri, Mkubwa wa dhati vitendo na sifa, Mwenye Uluwa Aliyejitukuza kabisa. [Ar-Ra’d: 9]

 

 

اللَّـهُمَّ مَالِكَ الْمُلْكِ

“Ee Allaah Mfalme Uliyemiliki ufalme wote, [Aal-‘Imraan: 26]

 

رَبُّ الْعَرْشِ الْعَظِيمِ ۩﴿٢٦﴾

Rabb wa Al-‘Arsh adhimu” [An-Naml: 26]

 

 

Inafaa pia mwombaji kuanza kwa thanaa ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa mfano kusema:

 

‘Allahumma inniy as-aluka bianna Lakal-Hamdu laa ilaaha illa Anta Wahdaka laa shariyka Laka, (Ee Allaah, hakika mimi nakuomba kwamba Himdi ni Zako, hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, Huna mshirika.” Na kadhaalika.

 

Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapoamka usiku akimhimidi Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kumtukuza kwa kusema:

 

اللَّهُمَّ لَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ نُورُ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ ، وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ قَيِّمُ السَّمَوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَنْ فِيهِنَّ ، وَلَكَ الْحَمْدُ أَنْتَ الْحَقُّ ، وَوَعْدُكَ حَقٌّ ، وَقَوْلُكَ حَقٌّ ، وَلِقَاؤُكَ حَقٌّ ، وَالْجَنَّةُ حَقٌّ ، وَالنَّارُ حَقٌّ ، وَالسَّاعَةُ حَقٌّ ، وَالنَّبِيُّونَ حَقٌّ ، وَمُحَمَّدٌ حَقٌّ ، اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ ، وَعَلَيْكَ تَوَكَّلْتُ ، وَبِكَ آمَنْتُ ، وَإِلَيْكَ أَنَبْتُ ، وَبِكَ خَاصَمْتُ ، وَإِلَيْكَ حَاكَمْتُ : فَاغْفِرْ لِي مَا قَدَّمْتُ وَمَا أَخَّرْتُ ، وَمَا أَسْرَرْتُ وَمَا أَعْلَنْتُ ، أَنْتَ الْمُقَدِّمُ وَأَنْتَ الْمُؤَخِّرُ ، لَا إِلَهَ إِلَّا أَنْتَ - أَوْ لَا إِلَهَ غَيْرُكَ  

Allaahumma Lakal-Hamdu Anta Nuwrus-samaawati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Anta Qayyimus-samaawaati wal ardhwi waman fiyhinna. Walakal-Hamdu Antal-Haqqu, wa wa’dukal-haqqu, wa qawlukal-haqqu, wa liqaaukal-haqqu, wal-Jannata haqqun, wan-naaru haqqun, was-saa’atu haqqun,  wan-nabiyyuwna haqqun, wa Muhammadun  haqqun, Allaahumma Laka aslamtu, wa ’Alayka tawakkaltu, wabika aamantu, wa Ilayka anabtu, wabika khaaswamtu, wa Ilayka haakamtu, faghfir liy maa qaddamtu wamaa akh-khartu, wamaa asrartu, wamaa a’lantu, Antal-Muqaddimu wa Antal-Muakh-khiru laa ilaaha illa Anta. (Au) laa ilaaha ghayruka

 

Ee Allaah Himdi ni Zako  Wewe Ndiye Nuru ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Himdi ni Zako Wewe Ndiye Wewe Ndiye Msimamizi wa  mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, na Himdi ni Zako Wewe ni Haki na ahadi Yako ni ya kweli, na neno Lako ni la kweli, na kukutana na Wewe ni kweli, na Jannah ni kweli, na moto ni kweli, na Manabii ni kweli, na Muhammad ni kweli, na Qiyaamah ni kweli.  Ee Allaah, Kwako nimejisalimisha, na kwako nimetawakali, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimerejea kutubia. Na kwa ajili Yako (au kwa hoja na dalili Zako) nimetetea (maadui Wako). Na nimeelekea Kwako kukufanya Wewe ni Hakimu Wangu (kuhukumu baina yetu). Basi nighufurie  niliyoyatanguliza na niliyoyachelewesha, na niliyoyaficha na niliyoyatangaza; Wewe Ndiye Al-Muqaddimu (Mwenye kutanguliza) na Al-Muakh-khiru (Mwenye kuchelewesha), hapana Muabudiwa wa haki ila Wewe; Wewe Ndiye Ilaah wangu, hapana mwabudiwa wa haki ila Wewe (au) Hapana mwabudiwa wa haki ghairi Yako.” [Al-Bukhaariy (1120), Muslim (769) na wengineo]

 

Inafaa pia kumhimidi na kumtukuza kwa kauli au maneno mengineyo yenye kudhihirisha utukufu Wake Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) lakini yawe maneno ambayo hayavuki mipaka yakatoka nje ya ’Aqiydah sahihi.

  

Kisha unamswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyothibiti katika Hadiyth zifuatazo:

 

 عن فَضَالَةَ بْنَ عُبَيْدٍ (رضي الله عنه) يَقُولُ: سَمِعَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) رَجُلاً يَدْعُو فِي صلاَتِهِ لَمْ يُمَجِّدْ اللَّهَ تَعَالَى وَلَمْ يُصَلِّ عَلَى النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((عَجِلَ هَذَا)) ثُمَّ دَعَاهُ فَقَالَ لَهُ أَوْ لِغَيْرِهِ: ((إِذَا صَلَّى أَحَدُكُمْ فَلْيَبْدَأْ بِتَمْجِيدِ رَبِّهِ جَلَّ وَعَزَّ وَالثَّنَاءِ عَلَيْهِ ثُمَّ  يُصَلِّي عَلَى النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ ثُمَّ يَدْعُو بَعْدُ بِمَا شَاءَ))

Kutoka kwa Fadhwaalah bin ‘Ubayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimsikia mtu akiomba katika Swalaah yake hamtukuzi Allaah (Ta’aalaa) wala hamswalii Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Ameharakiza huyu)). Kisha akamwita akamwambia yeye au mwengine: ((Anaposwali mmoja wenu basi aanze kwa kumtukuza Rabb wake (‘Azza wa Jalla) amsifu kisha amswalie Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kisha aombe baadaye anachokitaka)) [Abuu Daawuwd, Ahmad na ameipa daraja ya Swahiyh Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (1481)]

 

Na katika riwaaya nyingine pia: 

 

عن فَضَالَةَ بْنَ عُبَيْدٍ (رضي الله عنه)  يَقُولُ: "سَمِعَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) رَجُلاً يَدْعُو فِي صَلاَتِهِ لَمْ يُمَجِّدْ اللَّهَ وَلَمْ يُصَلِّ عَلَى النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ), فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّم)َ: ((عَجِلْتَ أَيُّهَا الْمُصَلِّي)) ثُمَّ عَلَّمَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ ( صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ).  وَسَمِعَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) رَجُلاً يُصَلِّي فَمَجَّدَ اللَّهَ وَحَمِدَهُ وَصَلَّى عَلَى النَّبِيِّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((ادْعُ تُجَبْ وَسَلْ تُعْطَ))

Kutoka kwa Fadhwaalah bin ‘Ubayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kamsikia mtu akiomba katika Swalaah yake hamtukuzi Allaah (Ta’aalaa) wala hamswalii Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Umeharakiza ee mwenye kuswali)). Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akawafunza. Na akamsikia mtu anaswali akamtukuza Allaah na Akamsifu, na akamswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Omba du’aa utakaitikiwa, na omba utapewa)) [Swahiyh An-Nasaaiy (1283)]

 

 

 

 

Share