47-Kitaab At-Tawhiyd: Kuheshimu Majina Ya Allaah Na Kubadilisha Jina Lake Mtu Kwa Ajili Hiyo

Mlango Wa 47

بَابٌ اِحْتِرَامُ أَسْمَاءِ اللَّهِ تَعَالَى وَتَغْيِيرُ الِاسْمِ لِأَجْلِ ذَلِكَ

Kuheshimu Majina Ya Allaah Ta’aalaa Na Kubadilisha Jina Lake Mtu Kwa Ajili Hiyo


 

 

 

عَنْ أَبِي شُرَيْحٍ: أَنَّهُ كَانَ يُكَنَّى: أَبَا الْحَكَمِ. فَقَالَ لَهُ النَّبِيُّ (صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ): ((إِنَّ اللَّهَ هُوَ الْحَكَمُ وَإِلَيْهِ الْحُكْمُ)) فَقَالَ: إِنَّ قَوْمِي إِذَا اِخْتَلَفُوا فِي شَيْءٍ أَتَوْنِي فَحَكَمْتُ بَيْنَهُمْ فَرَضِي كِلا الْفَرِيقَيْنِ فَقَالَ: ((مَا أَحْسَنَ هَذَا، فَمَا لَكَ مِنَ الْوَلَدِ؟)) قُلْتُ: شُرَيْحٌ وَمُسْلِمٌ وَعَبْدُ اللَّهِ. قَالَ: ((فَمَنْ أَكْبَرُهُمْ؟))  قُلْتُ: شُرَيْحٌ. قَالَ: ((فَأَنْتَ أَبُو شُرَيْحٍ))  رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ وَغَيْرُهُ

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Shurayh(رضي الله عنه)  kwamba: alikuwa akiitwa Abuu Al-Hakam. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: ((Hakika Allaah ndiye Hakimu na Kwake kuna hukmu zote)) Akasema: Hakika watu wangu wanapokhitilafiana katika jambo, hunijia kisha nikawahukumu baina yao, hapo pande mbili zote zinaridhika. Akasema: ((Uzuri ulioje huo! Je, unao watoto?)) Nikajibu: [Ndio] Shurayh na Muslim na ‘Abdullaah. Akauliza: ((Nani mkubwa wao?)) Nikasema: Shurayh.  Akasema: ((Basi wewe ni Abuu Shurayh)) [Abuu Daawuwd na wengineo].

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuheshimu Majina na Sifa za Allaah (سبحانه وتعالى) japokuwa    maana yake halisi haikukusudiwa kujisifia nayo (na Abuu Shurayh)  

 

2-Mtu kubadili jina lake kwa ajili hiyo.

 

3-Kutumia jina la mtoto mkubwa kwa ajili ya kun-yah.

 

 

Share