51-Kitaab At-Tawhiyd: Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo

Mlango Wa 51

باب: وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ

Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo


 

 

قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

 

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ  

((Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) [Al-A’raaf (7: 180)]

 

ذَكَرَ اِبْنُ أَبِي حَاتِمٍ عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ: ((يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ)): يُشْرِكُونَ.

Ibn Haatim ametaja kwamba Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema kuhusu: ((Wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) yaani: wanafanya shirki.

وَعَنْهُ: سَمُّوا اَللاَّتَ مِنَ الإِلَهِ وَالْعُزَّى مِنَ الْعَزِيزِ.

Na kasema pia: “Wamewaita Al-Laata – kutokana na ‘Ilaah’. Na Al-Uzzah kutokana na ‘Al-‘Aziyz’.

 

وَعَنِ الأَعْمَشِ: يُدْخِلُونَ فِيهَا مَا لَيْسَ مِنْهَا

Na Al-A’mash kasema: “Wanaingiza humo (katika Majina ya Allaah, Majina) yasiyokuwemo.”

 

 

Masuala Muhimu Yaliyomo:

 

1-Kuthibitisha Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyosema (Al-A’raaf 7: 180).

 

2-Majina yote ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni mazuri.

 

3-Maamrisho ya kumuomba Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Majina Yake Mazuri.

 

4-Amri ya kuepukana na majahili na wakanushaji.   

 

5-Maelezo ya wanavyopotoa na kuharibu Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

6-Adhabu imeahidiwa kwa wapotoshaji Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).

 

 

 

Share