216-Aayah Na Mafunzo: Muumini Khasa Ni Mwenye Kuamini Majaaliwa Ya Khayr Na Shari

Aayah Na Mafunzo

Al-Baqarah

 

Muumini Khasa Ni Mwenye Kuamini Majaaliwa Ya Khayr Na Shari

 

www.alhidaaya.com

 

 

 كُتِبَ عَلَيْكُمُ الْقِتَالُ وَهُوَ كُرْهٌ لَّكُمْ ۖ وَعَسَىٰ أَن تَكْرَهُوا شَيْئًا وَهُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ وَعَسَىٰ أَن تُحِبُّوا شَيْئًا وَهُوَ شَرٌّ لَّكُمْ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ وَأَنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿٢١٦﴾

216. Mmeandikiwa shariy’ah kupigana vita nako kunachukiza mno kwenu. Na asaa mkachukia jambo na hali lenyewe ni khayr kwenu. Na asaa mkapenda jambo na hali lenyewe ni la shari kwenu. Na Allaah Anajua na nyinyi hamjui.

 

 

Mafunzo:

 

قال رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم:" عَجَبًا لأمرِ المؤمنِ إِنَّ أمْرَه كُلَّهُ لهُ خَيرٌ وليسَ ذلكَ لأحَدٍ إلا للمُؤْمنِ إِنْ أصَابتهُ سَرَّاءُ شَكَرَ فكانتْ خَيرًا لهُ وإنْ أصَابتهُ ضَرَّاءُ صَبرَ فكانتْ خَيرًا لهُ ". رواهُ مُسْلِمٌ.

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Ajabu ya hali ya Muumini kuwa mambo yake yote ni khayr; anapofikwa na furaha hushukuru na huwa khayr kwake, na anapofikwa na matatizo husubiri na huwa ni khayr kwake, na haiwi hivyo (sifa hiyo) ila kwa Muumini)) [Muslim]

 

 

Share