080-Aayah Na Mafunzo: Makatazo Ya Kupinduka Mipaka Kumtukuza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Makatazo Ya Kupinduka Mipaka Kumtukuza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

www.alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

وَلَا يَأْمُرَكُمْ أَن تَتَّخِذُوا الْمَلَائِكَةَ وَالنَّبِيِّينَ أَرْبَابًا ۗ أَيَأْمُرُكُم بِالْكُفْرِ بَعْدَ إِذْ أَنتُم مُّسْلِمُونَ ﴿٨٠﴾ 

80. Na wala hakuamuruni kuwachukua Malaika na Manabii kuwafanya miola. Je, anakuamrisheni ukafiri baada ya nyinyi kuwa mmejisalimisha kwa Allaah? [Aal-'Imraan: 80]

 

Mafunzo:

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amekataza kutukuzwa kupindukia kiasi amesema: “Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Rasuli Wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim].

 

 

Share