133-Aayah Na Mafunzo: Unapoomba Jannah, Omba Jannatul-Firdaws

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Unapoomba Jannah Omba Jannatul-Firdaws

Alhidaaya.com

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَسَارِعُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ﴿١٣٣﴾ 

Na kimbilieni maghfirah kutoka kwa Rabb wenu na Jannah upana wake ni wa mbingu na ardhi imeandaliwa kwa wenye taqwa.  [Aal-Imraan: 133]

 

Mafunzo:

 

قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: إِنَّ فِي الْجَنَّةِ مِائَةَ دَرَجَةٍ أَعَدَّهَا اللَّهُ لِلْمُجَاهِدِينَ فِي سَبِيلِ اللَّهِ، مَا بَيْنَ الدَّرَجَتَيْنِ كَمَا بَيْنَ السَّمَاءِ وَالأَرْضِ، فَإِذَا سَأَلْتُمُ اللَّهَ فَاسْأَلُوهُ الْفِرْدَوْسَ، فَإِنَّهُ أَوْسَطُ الْجَنَّةِ وَأَعْلَى الْجَنَّةِ، أُرَاهُ فَوْقَهُ عَرْشُ الرَّحْمَنِ، وَمِنْهُ تَفَجَّرُ أَنْهَارُ الْجَنَّةِ ‏"‏‏.‏  

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Kuna daraja mia moja za Jannah ambazo Amezitayarisha Allaah kwa ajili ya Mujaahidiyn wanaopigana kwa ajili Yake. Baina ya sehemu moja na sehemu nyingine, ni masafa sawa ya baina ya ardhi na mbingu. Unapomuomba Allaah, muombe Al-Firdaws, kwa sababu ipo katikati ya Jannah na ni sehemu ya Juu kabisa (Msimuliajia amesema: Nadhani pia amesema: ”Juu yake kuna Arsh ya Ar-Rahmaan) na humo mnabubujika  mito ya Jannah.” [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share