003-Aayah Na Mafunzo: Mayahudi Kuithamini Aayah Leo Nimekukamilishieni Dini yenu…

Aayah Na Mafunzo

Al-Maaidah

Mayahudi Kuithamini Aayah Leo Nimekukamilishieni Dini yenu…

Alhidaaya.com

 

 

حُرِّمَتْ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةُ وَالدَّمُ وَلَحْمُ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ لِغَيْرِ اللَّـهِ بِهِ وَالْمُنْخَنِقَةُ وَالْمَوْقُوذَةُ وَالْمُتَرَدِّيَةُ وَالنَّطِيحَةُ وَمَا أَكَلَ السَّبُعُ إِلَّا مَا ذَكَّيْتُمْ وَمَا ذُبِحَ عَلَى النُّصُبِ وَأَن تَسْتَقْسِمُوا بِالْأَزْلَامِ ۚ ذَٰلِكُمْ فِسْقٌ ۗ الْيَوْمَ يَئِسَ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن دِينِكُمْ فَلَا تَخْشَوْهُمْ وَاخْشَوْنِ ۚ الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ فَمَنِ اضْطُرَّ فِي مَخْمَصَةٍ غَيْرَ مُتَجَانِفٍ لِّإِثْمٍ ۙ فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣﴾

Mmeharamishiwa nyamafu, na damu, na nyama ya nguruwe, na kilichotajiwa asiyekuwa Allaah katika kuchinjwa kwake, na (pia) mnyama aliyekufa kwa kukosa hewa au aliyepigwa akafa, au aliyeporomoka toka juu, au aliyepigwa pembe, na aliyeliwa na mnyama mwitu, isipokuwa mliyewahi kumchinja kihalali (kabla ya kufa), na waliochinjwa kwa ajili ya ‘ibaadah ya waabudiwa, na kupiga ramli kwa mishale. Hayo kwenu ni ufasiki. Leo wamekata tamaa wale waliokufuru na Dini yenu, basi msiwaogope, bali Niogopeni Mimi. Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislamu uwe Dini yenu. Basi atakayelazimika katika njaa kali bila kulalia kwenye dhambi (akala vilivyoharamishwa), basi hakika Allaah Ni Mwingi wa Kughufuria, Mwenye Kurehemu. [Al-Maaidah (5:3)]

 

Mafunzo:

 

Aayah Ambayo Ingeliteremshwa Kwa Mayahudi, Wangelisherehekea Siku Iliyoteremshwa:

 

‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  amehadithia kwamba Myahudi mmoja alimwambia: Ee Amiri wa Waumini, lau ingeliteremka kwetu sisi Aayah hii:

 

الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الْإِسْلَامَ دِينًا ۚ

Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na Nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekuridhieni Uislamu uwe Dini yenu.  (5:3).

 

basi tungeliifanya kuwa ni siku ya kusherehekea. ‘Umar akasema: Wa-Allaahi, naijua siku gani imeteremka Aayah hii. Imeteremka Siku ya ‘Arafah siku ya Ijumaa. [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share