086-Asbaabun-Nuzuwl: Aal-'Imraan Aayah 086: كَيْفَ يَهْدِي اللَّـهُ قَوْمًا كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ وَشَهِدُوا

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

Aal-‘Imraan 086-Vipi Allaah Atawaongoza watu waliokufuru baada ya kuamini

 

 

كَيْفَ يَهْدِي اللَّـهُ قَوْمًا كَفَرُوا بَعْدَ إِيمَانِهِمْ وَشَهِدُوا أَنَّ الرَّسُولَ حَقٌّ وَجَاءَهُمُ الْبَيِّنَاتُ ۚ وَاللَّـهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٦﴾ 

Vipi Allaah Atawaongoza watu waliokufuru baada ya kuamini kwao na wakashuhudia kwamba Rasuli ni haki na zikawajia hoja bayana? Na Allaah Hawaongozi watu madhalimu.

 

 

 أُولَـٰئِكَ جَزَاؤُهُمْ أَنَّ عَلَيْهِمْ لَعْنَةَ اللَّـهِ وَالْمَلَائِكَةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ﴿٨٧﴾

Hao jazaa yao ni kwamba juu yao ipo Laana ya Allaah na ya Malaika na ya watu wote.

 

 

خَالِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنْهُمُ الْعَذَابُ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ ﴿٨٨﴾

Wadumu humo milele, hawatopunguziwa adhabu wala hawatopewa muda wa kuakhirishwa adhabu.

 

 

إِلَّا الَّذِينَ تَابُوا مِن بَعْدِ ذَٰلِكَ وَأَصْلَحُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٨٩﴾

Isipokuwa wale waliotubu baada ya hayo na wakatengeneza, kwani hakika Allaah Ni Mwingi wa Kughufiria, Mwenye Kurehemu. [Aal-‘Imraan (3:86-89)]

 

 

 

Sababun-Nuzuwl

 

Aayah hizi (3:86-89) ziliteremka kumzungumzia mtu mmoja katika Answaar ambaye alisilimu kisha akaritadi na akaingia katika shirki. Halafu akajuta kwa tendo lake hilo la kuritadi. Akatuma watu wake ili wamfikishie swali lake kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa je, anaweza kuleta tawbah kwa tendo lake hilo? Baada ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuulizwa swali hilo, zikateremka Aayaat hizo, mtu huyo akatumiwa, na akasilimu. [Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما). Aathaar hii imepokelewa na Ibn Jariyr, na pia imesimuliwa na Ahmad, Ibn Hibbaan na wengineo. Adh-Dhahabiy ameiwafiki pamoja na Al-Albaaniy katika Asw-Swahiyhah (3066)]

 

 

  

Share