07-Imaam Ibn ‘Uthyamiyn: Akimeza Maji Bila Kukusudia Kutokana Na Kusukutua Swawm Yake Inabatilika?

Akimeza Maji Bila Kukusudia Kutokana Na Kusukutua Swawm Yake Inabatilika?

 

Imaam Ibn ‘Uthyamiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

SWALI:

 

Je, Swawm ya mfungaji inabatilika ikiwa atasukutua kinywa au pua na kwa bahati mbaya akameza maji?

 

JIBU:

 

Aliyekuwa katika swawm akaukutua kinywa au pua na maji yakamuingia, Swawm yake haibatiliki, kwa kuwa hakukusudia hilo. Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema:

 

وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ ۚ

lakini isipokuwa katika yale yaliyoyakusudia nyoyo zenu  [Al-Ahzaab 33;5]

 

[Imaam Muhammad  Swaalih Ibn 'Uthaymiyn -  Fiqhul-'Ibaadat, uk. 253]

 

Share