Magimbi (Eddoes) Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Magimbi Kwa Nyama Ya Ng’ombe

 

Vipimo 

Majimbi (Eddoes) kiasi 6 au 7

Nyama ng’ombe ½ kilos

Tangawizi ilosagwa 1 kijiko cha kulia

Haldi (bizari manjano/turmeric) ½ kijiko cha chai

Tui zito la nazi vikombe 2

Chumvi kiasi

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

 

  1. Safisha nyama kisha weka chumvi, bizari ya manjano, tangawizi mbichi, ukaushe kwanza katika sufuria kwa kukaanga kaanga.
  2. Ikianza kukauka, weka maji funika uchemshe iwive.
  3. Menya majimbi ukate kate na uweke katika sufuria nyengine.
  4. Mimina supu na nyama katika majimbi uchemshe yawive majimbi.
  5. Mwisho weka tui zito la nazi uchanganye vizuri kisha weka katika moto kidogo tu bila kufunika yakiwa tayari.

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)  

 

 

Share