012-Aayah Na Mafunzo: Rahma Za Allaah Zinashinda Ghadhabu Zake

Aayah Na Mafunzo

 

www.alhidaaya.com

 

 

Al-An’aam 12

 

 

012-Rahma Za Allaah Zinashinda Ghadhabu Zake

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

 

قُل لِّمَن مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۖ قُل لِّلَّـهِ ۚ كَتَبَ عَلَىٰ نَفْسِهِ الرَّحْمَةَ ۚ لَيَجْمَعَنَّكُمْ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ لَا رَيْبَ فِيهِ ۚ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٢﴾

Sema: Ni vya nani vilivyomo mbinguni na ardhini? Sema: Ni vya Allaah. Amejiwajibishia Nafsi Yake Rahmah. Bila shaka Atakukusanyeni Siku ya Qiyaamah, hapana shaka yoyote ndani yake. Wale ambao wamekhasiri nafsi zao basi wao hawaamini. [Al-An'aam: 12]

 

 

 

 

Mafunzo:

 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: (( لَمَّا قَضَى اللَّهُ الْخَلْقَ كَتَبَ فِي كِتَابِهِ عَلَى نَفْسِهِ فَهُوَ مَوْضُوعٌ عِنْدَهُ إِنَّ رَحْمَتِي تَغْلِبُ غَضَبِي)) البخاري   مسلم  النسائي وابن ماجه

Kutoka kwa Abu Hurayrah (رضي الله عنه)  ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Allaah Alipoumba viumbe Aliandika katika kitabu Chake Alichonacho katika Nafsi Yake: Rahmah Zangu zinashinda ghadhabu Zangu)) [Al-Bukhaariy, Muslim, an-Nasaaiy na Ibn Maajah]

 

 

 

 

 

Share