05-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Twahaarah:Mlango Wa Kupangusa Juu Ya Khuff Mbili (Soksi)

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتابُ الطَّهارَة

Kitabu Cha Twahaarah

 

بَابُ اَلْمَسْحِ عَلَى اَلْخُفَّيْنِ

05-Mlango Wa Kupangusa Juu Ya Khuff Mbili (Soksi Za Ngozi)

 

 

 

Tanbihi: Soksi za aina yoyote zinafaa ikiwa za sufi, pamba au katani na mifano hivyo.  

 

 

 

53.

عَنْ اَلْمُغِيرَةِ بْنِ شُعْبَةَ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {كُنْتُ مَعَ اَلنَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏فَتَوَضَّأَ، فَأَهْوَيْتُ لِأَنْزِعَ خُفَّيْهِ، فَقَالَ: "دَعْهُمَا، فَإِنِّي أَدْخَلْتُهُمَا طَاهِرَتَيْنِ" فَمَسَحَ عَلَيْهِمَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْه

وَلِلْأَرْبَعَةِ عَنْهُ إِلَّا النَّسَائِيَّ: {أَنَّ اَلنَّبِيَّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏مَسَحَ أَعْلَى اَلْخُفِّ وَأَسْفَلَهُ} وَفِي إِسْنَادِهِ ضَعْف

Kutoka kwa Mughiyra bin Shu’bah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilikuwa na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akatawadha, nikaharakia kumvua soksi zake. Akasema: “Ziache, kwani nilizivaa zikiwa twahaara[1].” Akapungusa juu yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na kutoka kwa Al-Arba’ah isipokuwa An-Nasaaiy: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipangusa sehemu ya juu na chini ya soksi za ngozi.” [Katika Isnaad yake kuna udhaifu].

 

 

 

54.

وَعَنْ عَلِيٍّ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {لَوْ كَانَ اَلدِّينُ بِالرَّأْيِ لَكَانَ أَسْفَلُ اَلْخُفِّ أَوْلَى بِالْمَسْحِ مِنْ أَعْلَاهُ، وَقَدْ رَأَيْتُ رَسُولَ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏يَمْسَحُ عَلَى ظَاهِرِ خُفَّيْهِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ بِإِسْنَادٍ حَسَن

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Lau Dini ingekuwa kwa rai[2], basi ingelikuwa kupangusa chini ya khuff ni bora zaidi kuliko juu yake. Na kwa yakini mimi nimemuona Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akipangusa juu ya khuff zake.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]

 

 

 

55.

وَعَنْ صَفْوَانَ بْنِ عَسَّالٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏يَأْمُرُنَا إِذَا كُنَّا سَفْرًا أَنْ لَا نَنْزِعَ خِفَافَنَا ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ وَلَيَالِيَهُنَّ، إِلَّا مِنْ جَنَابَةٍ وَلَكِنْ مِنْ غَائِطٍ، وَبَوْلٍ، وَنَوْمٍ} أَخْرَجَهُ النَّسَائِيُّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ وَصَحَّحَاه ُ 

Kutoka kwa Swafwaan bin ‘Assaal (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akituamrisha pindi tukiwia safarini, tusivue khuff zetu siku tatu mfululizo mchana na usiku wak[3]e isipokuwa tukiwa katika janaba, lakini kwa haja kubwa, mkojo na usingizi (tulikuwa hatuvui).” [Imetolewa na An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy, na tamshi hili ni lake, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah]

 

 

 

56.

وَعَنْ عَلِيِّ بْنِ أَبِي طَالِبٍ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {جَعَلَ اَلنَّبِيُّ ‏صلى الله عليه وسلم ‏ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ وَلَيَالِيَهُنَّ لِلْمُسَافِرِ، وَيَوْمًا وَلَيْلَةً لِلْمُقِيمِ.‏ يَعْنِي: فِي اَلْمَسْحِ عَلَى اَلْخُفَّيْنِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِم

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alifanya kuwa siku tatu; mchana na usiku wake kwa msafiri, na siku moja; mchana na usiku wake kwa mkaazi yaani katika kufuta juu ya khuff.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

57.

وَعَنْ ثَوْبَانَ ‏ رضى الله عنه ‏ قَالَ: {بَعَثَ رَسُولُ اَللَّهِ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏سَرِيَّةً، فَأَمَرَهُمْ أَنْ يَمْسَحُوا عَلَى اَلْعَصَائِبِ ‏ يَعْنِي: اَلْعَمَائِمَ ‏وَالتَّسَاخِينِ‏ يَعْنِي: اَلْخِفَافَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِم

Kutoka kwa Thawbaan[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alituma kikosi cha jeshi na akawaamrisha wapanguse juu ya vilemba[5] na khuff.” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd, na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

58.

وَعَنْ عُمَرَ ‏مَوْقُوفًا‏ وعَنْ أَنَسٍ ‏مَرْفُوعًا‏: {إِذَا تَوَضَّأَ أَحَدُكُمْ وَلَبِسَ خُفَّيْهِ فَلْيَمْسَحْ عَلَيْهِمَا، وَلْيُصَلِّ فِيهِمَا، وَلَا يَخْلَعْهُمَا إِنْ شَاءَ إِلَّا مِنْ جَنَابَةٍ"} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَالْحَاكِمُ وَصَحَّحَه

Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) katika Hadiyth Mawquwfaa na kutoka kwa Anas katika Hadiyth Marfuw’aa kuwa: “Pindi mmoja wenu akitawadha na akavaa khuff zake mbili, afanye mas-h (kupangusa kwa maji) juu yake na aswali nazo, na asizivue akipenda[6], isipokuwa kwa janaba.” [Imetolewa na Ad-Daarqutwniy na Al-Haakim, na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

59.

وَعَنْ أَبِي بَكْرَةَ ‏ رضى الله عنه ‏ عَنْ اَلنَّبِيِّ ‏ صلى الله عليه وسلم ‏{أَنَّهُ رَخَّصَ لِلْمُسَافِرِ ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ وَلَيَالِيَهُنَّ، وَلِلْمُقِيمِ يَوْمًا وَلَيْلَةً، إِذَا تَطَهَّرَ فَلَبِسَ خُفَّيْهِ: أَنْ يَمْسَحَ عَلَيْهِمَا} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَة

Kutoka kwa Abuu Bakrah[7] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameruhusu msafiri kupangusa juu ya khuff siku tatu na usiku wake, na kwa mkaazi siku moja; mchana na usiku wake, atakapochukua wudhuu akavaa khuff zake mbili.” [Imetolewa na Ad-Daaruqutwniy na akaisahihisha Ibn Khuzaymah]

 

 

 

60.

وَعَنْ أُبَيِّ بْنِ عِمَارَةَ ‏ رضى الله عنه ‏ أَنَّهُ قَالَ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ أَمْسَحُ عَلَى اَلْخُفَّيْنِ؟ قَالَ: "نَعَمْ" قَالَ: يَوْمًا؟ قَالَ: "نَعَمْ"، قَالَ: وَيَوْمَيْنِ؟ قَالَ: "نَعَمْ"، قَالَ: وَثَلَاثَةً؟ قَالَ: "نَعَمْ، وَمَا شِئْتَ" أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَقَالَ: لَيْسَ بِالْقَوِيِّ

Kutoka kwa Ubayy bin ‘Imaarah[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, naweza kupangusa juu ya khuff mbili?” Akasema: “Ndiyo.” Akauliza tena: “Siku moja?” Akasema: “Ndiyo.” Akauliza tena: “Siku mbili je?” Akasema: “Ndiyo.” Akauliza tena: “Na siku tatu?: Akasema: “Ndiyo, na utakavyo[9].” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na akasema: “Hadiyth haina nguvu[10].”]

 

 

[1] Kupangusa (Mas-h) juu ya soksi kuna masharti. Hizo soksi lazima uwe ulizivaa ukiwa twahara. Ikiwa ulivaa soksi hizo hauko tohara, basi kupangusa juu yake hakuruhusiwi.

 

[2] Hadiyth hii inamaanisha kuwa amri za kidini (katika Uislaam) za maamrisho na makatazo hutegemea Wahyi. Mtu huwezi kukubali au kukataa amri kwa sababu ya kuzielewa au kutozielewa. Lakini hii haimaanishi kuwa maamrisho au makatazo hayo ya kidini huenda kinyume na akili na busara. Pia inathibitisha kuwa, pakiwepo Hadiyth Swahiyh, kutoa uamuzi kinyume na Hadiyth hiyo hairuhusiwi. Hili limebainishwa na Shariy’ah ya Kiislaam.

 

[3] Hadiyth hii inamaanisha kuwa, kupangusa (Mas-h) kunaruhusiwa kwa msafiri mpaka siku tatu, na kwa mkazi wa pale mpaka saa thelathini na nne. Kipindi cha Mas-h huhesabika tangu wudhuu unapobatilika na siyo tangu kuzivaa soksi. Njia ya kupangusa (Mas-h) ni kulowanisha mikono kwa maji, na kuanzia kwenye vidole kuupandisha mpaka chini ya magoti. Baada ya wakati unaoruhusiwa kwisha au ukijamba, ukikojoa, n.k., mas-h hubatilika. Na pia inabatilika kwa mambo yote yanayobatilisha wudhuu.

[4] Huyu Thawbaan ni Thawbaan bin Bujdud bin Jahdar, ambaye alipewa jina la utani la Abuu ‘Abdillaah. Alikuwa mkazi wa As-Surat, ambapo ni mahali kati ya Makkah na Al-Madiynah. Ilisemekana pia kuwa yeye alitoka Himyaar. Aliishi na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) maisha yake yote, baadaye akalowea Sham, na baadaye akahamia Hims alikofia mnamo mwaka 54 A.H.

 

[5] Katika maandishi ya Kiarabu neno ‘Aswaa-ib maana yake ni bendeji inayotumiwa kufungia vidonda, au ukivunjika mguu au mkono, kufungia juu ya vipande vya mbao viwekwavyo kuuzunguka mfupa uliovunjika.

 

[6]  “Akipenda” maana yake iwapo bado yumo katika wakati ulioruhusiwa kupangusa (Mas-h). Lakini mara wakati huo unapokwisha, lazima azivue soksi zake, akatawadhe upya pamoja na kuosha miguu yake, ndipo azivae tena hizo soksi zake, na kipindi cha kupangusa (Mas-h) kianze upya.

 

[7] Huyu Abuu Bakrah ndiye Nufai bin Al-Haarith au bin Al-Masruwh. Alishuka kutoka katika ngome ya Twaaif pamoja na kundi la watumwa na akasilimu, ndipo Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuacha huru. Alikuwa mmoja wa Swahaba wenye taqwa na akafia Basra manmo mwaka 51 au 52 A.H.

 

[8] Ubay bin ‘Imaarah alikuwa Swahaba wa Kianswaar (wa kutoka Al-Madiynah). Alilowea Misr. Ibn Hibbaan alisema: “Aliswali kwa Qiblah mbili, lakini sichukulii ripoti yake kuwa ni mlolongo kamili wa wapokezi.”

 

[9] Isnaad ya Hadiyth hii si Swahiyh. Hadiyth ile inayotaja siku moja (saa 24) kwa mkazi, na siku tatu kwa msafiri ni Swahiyh.

 

[10] Hadiyth hii haikuchukuliwa kama ni ushahidi kwa udhaifu wake na kwa kuipinga Hadiyth Hasan na Swahiyh ambayo imetaja vipindi. An-Nawawi ametaja katika Sharh Al-Muhadhdhab kwamba, Imaam wamekubaliana juu ya udhaifu wa Hadiyth hii, na Ahmad alisema: “Wapokezi wake hawajulikani.”

 

Share