08-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Twahaarah: Mlango Wa Ghuslu (Kuoga) Na Hukumu Ya Janaba

 

بُلُوغُ الْمَرام

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتابُ الطَّهارَة

Kitabu Cha Twahaarah

 

بَابُ اَلْغُسْلِ وَحُكْمِ اَلْجُنُبِ

Mlango Wa Ghuslu (Kuoga) Na Hukumu Ya Janaba

 

 

 

 

 

92.

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {اَلْمَاءُ مِنْ اَلْمَاءِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ وَأَصْلُهُ فِي اَلْبُخَارِيِّ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Maji (ya ghuslu) ni kutokana na maji (ya kutoka manii)[1].”” [Imetolewa na Muslim, na chanzo chake ni Al-Bukhaariy]

 

 

 

93.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِذَا جَلَسَ بَيْنَ شُعَبِهَا اَلْأَرْبَعِ، ثُمَّ جَهَدَهَا، فَقَدْ وَجَبَ اَلْغُسْلُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

زَادَ مُسْلِمٌ: "وَإِنْ لَمْ يُنْزِلْ "

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “(Mwanamume) atakapokaa baina ya sehemu nne za mwanamke, kisha akamfanyia bidii kuingiza dhakari yake[2], itampasa ghuslu.”” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

Na katika Muslim aliongeza yafuatayo: “Hata kama hakutokwa na manii.”

 

 

 

94.

وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ; أَنَّ أُمَّ سُلَيْمٍ وَهِيَ اِمْرَأَةُ أَبِي طَلْحَةَ قَالَتْ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ اَللَّهَ لَا يَسْتَحِي مِنْ اَلْحَقِّ، فَهَلْ عَلَى اَلْمَرْأَةِ اَلْغُسْلُ إِذَا اِحْتَلَمَتْ؟ قَالَ: "نَعَمْ.‏ إِذَا رَأَتِ الْمَاءَ"} اَلْحَدِيثَ.‏ مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) kuwa: “Ummu Sulaym[3], mke wa Abuu Twalhah amesema: “Ee Rasuli wa Allaah! Allaah Haionei haki aibu. Je mwanamke inamlazimu afanye ghuslu akiota ndoto ya kujimai[4]?” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ndiyo! Akiona maji maji.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

 

95.

وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ  رضى الله عنه  قَالَ: {قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم فِي اَلْمَرْأَةِ تَرَى فِي مَنَامِهَا مَا يَرَى اَلرَّجُلُ قَالَ: "تَغْتَسِلُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

 

زَادَ مُسْلِمٌ: فَقَالَتْ أُمُّ سُلَيْمٍ  {وَهَلْ يَكُونُ هَذَا؟ قَالَ: "نَعَمْ فَمِنْ أَيْنَ يَكُونُ اَلشَّبَهُ؟ }

Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuhusu mwanamke anayeota usingizini kujimai[5] kama aotavyo mwanamume: “Basi aoge.”” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na katika Muslim aliongeza yafuatayo: “Ummu Salamah aliuliza: “Hii hutokea (kwa mwanamke pia)?”  Akasema:  “Ndiyo! Kwani inatoka wapi kushabihiana (kwa mtoto na mama yake)?”

 

 

 

96.

وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ اَلنَّبِيَّ  صلى الله عليه وسلم يَغْتَسِلُ مِنْ أَرْبَعٍ: مِنْ اَلْجَنَابَةِ، وَيَوْمَ اَلْجُمُعَةِ، وَمِنْ اَلْحِجَامَةِ، وَمِنْ غُسْلِ اَلْمَيِّتِ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akioga kutokana na mambo manne: Kutoka na janaba, siku ya Ijumaa, baada ya hijaamah (kuumika), na baada ya kuosha maiti[6].” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah]

 

 

 

97.

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  رضى الله عنه  {فِي قِصَّةِ ثُمَامَةَ بْنِ أُثَالٍ، عِنْدَمَا أَسْلَم وَأَمَرَهُ اَلنَّبِيُّ  صلى الله عليه وسلم أَنْ يَغْتَسِلَ} رَوَاهُ عَبْدُ اَلرَّزَّاقِ

وَأَصْلُهُ مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuhusu kisa cha Thumaamah bin Uthaal[7] aliposilimu, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuamrisha aoge[8].” [Imetolewa na ‘Abdur-Razzaaq, na chanzo chake ni kutoka Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

98.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ  رضى الله عنه  أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم قَالَ: {غُسْلُ اَلْجُمُعَةِ وَاجِبٌ عَلَى كُلِّ مُحْتَلِمٍ} أَخْرَجَهُ اَلسَّبْعَةُ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ghuslu (kuoga) siku ya Ijumaa ni waajib kwa kila mtu aliyebaleghe.”” [Imetolewa na As-Sab’ah (Al-Bukhaariy, Muslim, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad, At-Tirmidhiy]

 

 

 

99.

وَعَنْ سَمُرَةَ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {مَنْ تَوَضَّأَ يَوْمَ اَلْجُمُعَةِ فَبِهَا وَنِعْمَتْ، وَمَنْ اِغْتَسَلَ فَالْغُسْلُ أَفْضَلُ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ

Kutoka kwa Samurah[9] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutawadha siku ya Ijumaa anafanya jambo jema, na yule anayeoga, basi ghuslu (kuoga) ni bora zaidi.” [Imetolewa na Maimaam watano na akaipa daraja la Hasan At-Tirmidhiy]

 

 

 

100.

وَعَنْ عَلِيٍّ  رضى الله عنه  قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم يُقْرِئُنَا اَلْقُرْآنَ مَا لَمْ يَكُنْ جُنُبًا} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَهَذَا لَفْظُ اَلتِّرْمِذِيِّ وَحَسَّنَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ

Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akitufundisha Qur-aan, isipokuwa alipokuwa katika janaba[10].” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, na Musnad Ahmad) na hili ni tamshi la At-Tirmidhiy aliyeipa daraja la Hasan na akaisahihisha Ibn Hibbaan]

 

 

 

101.

وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِذَا أَتَى أَحَدُكُمْ أَهْلَهُ، ثُمَّ أَرَادَ أَنْ يَعُودَ فَلْيَتَوَضَّأْ بَيْنَهُمَا وُضُوءًا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

زَادَ اَلْحَاكِمُ: { فَإِنَّهُ أَنْشَطُ لِلْعَوْدِ }

وَلِلْأَرْبَعَةِ عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم يَنَامُ وَهُوَ جُنُبٌ، مِنْ غَيْرِ أَنْ يَمَسَّ مَاءً} وَهُوَ مَعْلُولٌ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu akijimai na mkewe, na akataka kurudia, basi na atawadhe[11] baina ya mara hizo mbili.” [Imetolewa na Muslim]

 

Na akaongezea Al Haakim: “Kwani huo (wudhuu) humchangamsha kwa ajili ya kurudia (jimai).”

 

Na Maimaam wanne wamepokea Hadiyth ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا): “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa analala na huku ana janaba bila ya kugusa maji[12].” [Imetolewa na Al-Arba’h, Hadiyth hii ina dosari]

 

 

 

102.

وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم إِذَا اِغْتَسَلَ مِنْ اَلْجَنَابَةِ يَبْدَأُ فَيَغْسِلُ يَدَيْهِ، ثُمَّ يُفْرِغُ بِيَمِينِهِ عَلَى شِمَالِهِ، فَيَغْسِلُ فَرْجَهُ، ثُمَّ يَتَوَضَّأُ، ثُمَّ يَأْخُذُ اَلْمَاءَ، فَيُدْخِلُ أَصَابِعَهُ فِي أُصُولِ اَلشَّعْرِ، ثُمَّ حَفَنَ عَلَى رَأْسِهِ ثَلَاثَ حَفَنَاتٍ، ثُمَّ أَفَاضَ عَلَى سَائِرِ جَسَدِهِ، ثُمَّ غَسَلَ رِجْلَيْهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ

وَلَهُمَا فِي حَدِيثِ مَيْمُونَةَ: {ثُمَّ أَفْرَغَ عَلَى فَرْجِهِ، فَغَسَلَهُ بِشِمَالِهِ، ثُمَّ ضَرَبَ بِهَا اَلْأَرْضَ}

وَفِي رِوَايَةٍ: {فَمَسَحَهَا بِالتُّرَابِ}

وَفِي آخِرِهِ: {ثُمَّ أَتَيْتُهُ بِالْمِنْدِيلِ} فَرَدَّهُ، وَفِيهِ: { وَجَعَلَ يَنْفُضُ الْمَاءَ بِيَدِهِ }

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akioga janaba, akianza kuosha mikono, kisha anamimina kwa kulia kwake juu ya kushoto kwake na anaosha tupu yake, kisha anatawadha, kisha alichukua maji akapitisha vidole vyake kwenye mizizi ya nywele zake, kisha alitia mafumba matatu ya maji kichwani, kisha anamimina maji sehemu zingine za mwili wake, kisha anaosha miguu yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]

 

Nao wawili (Al-Bukhaariy na Muslim) wamesimulia Hadiyth ya Maymuwnah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimwagia tupu yake na akaiosha kwa mkono wake wa kushoto. Kisha akapiga mkono wake ardhini.”

 

Katika Riwaayah nyengine: “Akaupangusa ardhini.”

 

Na mwisho inasema: “Kisha nikamletea kitambaa[13], akakirudisha, na akaendelea kujipangusa maji kwa mkono wake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

 

103.

وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ إِنِّي اِمْرَأَةٌ أَشُدُّ شَعْرَ رَأْسِي، أَفَأَنْقُضُهُ لِغُسْلِ اَلْجَنَابَةِ؟

 

وَفِي رِوَايَةٍ: وَالْحَيْضَةِ؟ فَقَالَ: "لَا، إِنَّمَا يَكْفِيكِ أَنْ تَحْثِي عَلَى رَأْسِكِ ثَلَاثَ حَثَيَاتٍ"} رَوَاهُ مُسْلِم

Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nilisema, Ee Rasuli wa Allaah! Mimi ni mwanamke nasuka nywele kichwa changu, Je! Nizifumue ili nipate kuoga janaba?”

 

Katika Riwaayah nyengine: “Na mwisho wa hedhi?” akasema: “Hapana, inatosha kumwagia mafumba matatuya maji kichwani kwako[14].” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

104.

وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِنِّي لَا أُحِلُّ اَلْمَسْجِدَ لِحَائِضٍ وَلَا جُنُبٌ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Siruhusu  Msikiti kwa mwenye hedhi[15] wala mwenye janaba[16].”” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah]

 

 

 

105.

وَعَنْهَا قَالَتْ: {كُنْتُ أَغْتَسِلُ أَنَا وَرَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم مِنْ إِنَاءٍ وَاحِدٍ، تَخْتَلِفُ أَيْدِينَا فِيهِ مِنَ اَلْجَنَابَةِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ

زَادَ ابْنُ حِبَّانَ: وَتَلْتَقِي أَيْدِينَا

Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema tena: “Mimi na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) tulikuwa tukioga (ghuslu ya) janaba katika chombo kimoja huku mikono yetu ikipishana.” [Al-Bukhaariy, Muslim]

 

Na akaongezea Ibn Hibbaan: “Na (mikono yetu) ilikuwa inakutana.”

 

 

 

106.

 

وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ  رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِنَّ تَحْتَ كُلِّ شَعْرَةٍ جَنَابَةً، فَاغْسِلُوا اَلشَّعْرَ، وَأَنْقُوا اَلْبَشَرَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَضَعَّفَاهُ

وَلِأَحْمَدَ عَنْ عَائِشَةَ نَحْوُهُ، وَفِيهِ رَاوٍ مَجْهُولٌ

Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuna janaba chini ya kila unywele[17], kwa hivyo osheni nywele na osheni ngozi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na wote waliidhoofisha]

 

Na katika Riwaayah ya Ahmad, Hadiyth sawa na hiyo imesimuliwa na ‘Aaishah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na katika Isnaad yake kuna mpokezi mmoja Majhuwl (asiyejulikana).

 

 

[1] Inamaanisha baada ya kutokwa na manii, kuoga ni lazima na muhimu. Hadiyth hii inahusiana na “kutokwa kwa usiku” tu, siyo kwa kujamiiana. Wanazuoni wengi wanaamini hivyo. ‘Ubayy bin Ka’b alisema: “Katika siku za mwanzo za Uislaam, watu wakijamiiana, kuoga hakukuwa lazima hadi manii yawe yametoka; lakini baadaye amri hii ikabatilishwa. Baadhi ya watafiti wameripoti maafikiano ya Muslim juu ya kadhia hii, kwamba, mara kujamiiana kunapoanza, kuoga kunakuwa lazima, hata manii yasipotoka.”

 

[2] Hii inamaanisha kuwa kujamiiana kukianza tu, kuoga kunakuwa lazima. Hadiyth hii inaibatilisha hiyo iliyopita, ikihusiana na kujamiiana.

 

[3] Umm Sulaym ni Ar-Rumaysa au Al-Ghumaysa bint Milhaan, Mama wa Anas bin Maalik. Alikuwa miongoni mwa Swahabiyyah waadilifu. Aliolewa na Maalik bin An-Nasr. Kisha akasilimu, na akamualika aingie Uislaam. Lakini yeye alichukia na akaenda zake Shaam ambako alifia. Kisha akachumbiwa na Abuu Twalha Al-Anaswaariy wakati bado ni mshirikina, lakini yeye akampa sharti kuwa awe Muislaam kwanza, kwa hivyo akasilimu na akamuoa. Alifariki zama za Ukhalifa wa ‘Uthmaan.

 

[4] Kama walivyo wanaume, wanawake pia hupata “Ndoto za kulowana.”

 

[5] Inamaanisha kuwa wanawake pia hutokwa na maji maji kama manii ya mwanamme, ama sivyo watoto wangekuwa hawafanani na mama zao. Kufanana kwa watoto na wazazi wao kunategemea ukali wa hayo manii.

 

[6] Kati ya mambo hayo manne, kuoga baada ya kujamiiana ni fardhi (lazima), kuoga siku ya Ijumaa ni Sunnah (kufuata matendo ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)), na mawili yanayobaki ni Mustahab (yanapendeza). Ahaadiyth kuhusu ulazima wa kuoga siku ya Ijumaa ni sahihi zaidi, kwa hivyo zifuatwe hizo.

 

[7] Thumaamah bin Uthaal alikuwa anatoka kwa Banu Hanifa na Sultani wa watu wa Al-Yamaama. Alikuenda kuhiji Hijjah ndogo (‘Umrah) wakati akiwa bado mushrik na akakamatwa na wapanda farasi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Walimpeleka Al-Madiynah na wakamfungia katika nguzo ya Msikiti. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuachia huru baada ya siku tatu. Basi akawa Muislaam muadilifu sana na imara sana, zama zile za ukanaji dini, dhidi ya watu wake ambao walighilibiwa na Musailima Al-Kadhdhaab.

 

[8] Mtu asiyekuwa Muislaam anaposilimu, sharti aoge. Abuu Daawuwd aliripoti kuwa, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuamuru Thumaamah aoge aliposilimu.

 

[9] Samurah bin Jundub ni Swahaba maarufu ambaye alipewa jina la utani la Abuu ‘Abdillaah. Alikuwa ni Fazari na alikuwa rafiki wa Answaar. Pia alikuwa mmoja wa mahaafidh waliohifadhi Ahaadiyth nyingi. Alilowea Basra, na alikuwa mkali sana dhidi ya Al-Haruriya. Alifariki mwishoni mwa mwaka 59 A.H.

 

[10] Kutokana na Hadiyth hii na zingine, inathibitika kwamba kusoma Qur-aan Tukufu kwa mtu anayepasa kuoga josho la baada ya kujamiiana, siyo sawa.

 

[11] Kutawadha huku kunapendeza lakini siyo lazima. Pia kunaleta raha na uchangamfu au upya katika hali ya tendo. Inasemekana kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akienda kulala na wakeze mbalimbali katika usiku mmoja, alikuwa akioga kabla ya kuenda kwa kila mmoja. Imeripotiwa pia kuwa mara nyingine alikuwa akitawadha baina yao na mara nyingine hakufanya hivyo. Kwa hivyo katika jambo hili, mtu aweza kuchagua mtindo wowote.

 

[12] Inamaanisha kwamba, kabla ya kuenda kulala, kuoga siyo lazima kwa mtu mwenye janaba. Kuna Hadiyth kutoka kwa Bukhaariy kuhusu kadhia hii kwamba Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akitawadha kabla ya kula, kunywa au kulala. Kwa hiyo ni ubora kufuata njia za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), ingawa jambo hili linapendeza tu (lakini siyo lazima).

 

[13] Suala la kukausha viungo baada ya kutawadha ni la hiari, kwa hivyo ni hiari ya mtu kujikausha au laa.

 

[14] Hadiyth hii inaweka wazi kwamba, kwa mwanamke mwenye hedhi na kwa mwanamume mwenye janaba, siyo lazima kuzifumua nywele. Kuna Hadiyth nyingine kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) ambayo inataja kufumua nywele. Hadiyth zote mbili ni kwa mazingira au nyakati tofauti.

 

[15] Mwanamke mwenye hedhi haruhusiwi kuingia Msikiti wowote wala kutufu (kuizunguka) Ka’bah, na asiswali wala kufunga akiwa katika hedhi. Swalaah anazozikosa nyakati hizi anasamehewa, lakini ni sharti alipe Swawm baada ya hedhi. Wanazuoni wamekhitilafiana kuhusu mwanamke mwenye hedhi kusoma na kugusa Qur-aan, lakini rai iliyo na nguvu zaidi ni kuwa anaruhusika kuisoma kwani hawezi kuharamika kuihifadhi Qur-aan. Na wengineo wameona pia anaruhusika hata kuigusa wakatoa dalili kadhaa ikiwemo Hadiyth ya ‘Aaishah pindi alipokwenda Hajj ikamjia hedhi akaamrishwa na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) atekeleze yote wanayoyatekeleza Hujaji isipokuwa kutufu Ka'bah. Ama wengineo wamekubali aisome lakini asiiguse bali anaweza kuikamata kwa kushikia kitambaa au glavu. Kumdhukuru Allaah (عز وجل) imeruhusiwa kwake.   Anaruhusiwa kuenda mahali pa kuswalia ‘Iyd.

 

[16] Inamaanisha kuwa mwanamke mwenye hedhi na mwanamume mwenye janaba hawaruhusiwi kukaa Msikitini lakini kupita tu wanaruhusiwa. Mtu akiwa kalala Msikitini na akaota na akajikojolea huku bado yumo Msikitini, ni lazima atoke nje.

 

[17] Tunaelewa kuwa Hadiyth hii kwamba, ni lazima kuosha mwili mzima baada ya tendo la ndoa, isipokuwa kusukutua mdomo na kuweka maji puani kwa kuwa haya mawili yana ubishi.

 

Share