075-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Anfaal Aayah 075: وَالَّذِينَ آمَنُوا مِن بَعْدُ وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا مَعَكُمْ فَأُولَـٰئِكَ مِنكُمْ

 

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

Al-Anfaal: 75

 

 

 

075- Na wale walioamini baada (ya hijra) na wakahajiri na wakafanya Jihaad pamoja nanyi, basi hao..

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَالَّذِينَ آمَنُوا مِن بَعْدُ وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا مَعَكُمْ فَأُولَـٰئِكَ مِنكُمْ ۚ وَأُولُو الْأَرْحَامِ بَعْضُهُمْ أَوْلَىٰ بِبَعْضٍ فِي كِتَابِ اللَّـهِ ۗ إِنَّ اللَّـهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ﴿٧٥﴾

Na wale walioamini baada (ya hijra) na wakahajiri na wakafanya Jihaad pamoja nanyi, basi hao ni miongoni mwenu. Na ndugu wa uhusiano wa damu wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe (kwa kurithiana), katika Shariy’ah ya Allaah. Hakika Allaah Ni Mjuzi wa kila kitu. [Al-Anfaal: 75]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

 

Amesimulia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) : Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliwaunga undugu Swahaba wakawa wanarithiana mpaka ilipoteremka:

 

وَأُولُو الْأَرْحَامِ بَعْضُهُمْ أَوْلَىٰ بِبَعْضٍ

Na ndugu wa uhusiano wa damu wanastahikiana wenyewe kwa wenyewe (kwa kurithiana).

 

Wakaacha kurithiana wakawa wanarithiana kwa uhusiano wa damu. [Atw-Twabaraaniy, na amesema Al-Haythamiy katika Majma’u Az-Zawaaid (7/28) Watu wake ni Swahiyh. Na imepokelewa na Ibn Abiy Haatim (4/25) Hadiyth ya Az-Zubayr bin Al-‘Awwaam (4/24) na imepokelewa na Ibn Jariyr (10/58)]

 

 

 

Share