04-Buluwgh Al-Maraam: Kitabu Cha Zakaah: Mlango Wa Ugawaji Wa Swadaqah

 

 

بُلُوغُ الْمَرام

 

Buluwgh Al-Maraam

 

كِتَابُ اَلزَّكَاةُ

Kitabu Cha Zakaah

 

بَابُ قَسْمِ اَلصَّدَقَاتِ

04-Mlango Wa Ugawaji Wa Swadaqah

 

 

 

 

 

520.

عَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه  قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لَا تَحِلُّ اَلصَّدَقَةُ لِغَنِيٍّ إِلَّا لِخَمْسَةٍ: لِعَامِلٍ عَلَيْهَا، أَوْ رَجُلٍ اِشْتَرَاهَا بِمَالِهِ، أَوْ غَارِمٍ، أَوْ غَازٍ فِي سَبِيلِ اَللَّهِ، أَوْ مِسْكِينٍ تُصُدِّقَ عَلَيْهِ مِنْهَا، فَأَهْدَى مِنْهَا لِغَنِيٍّ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَأُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ

Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Swadaqah si halali kwa anayejitosheleza isipokuwa kwa mambo matano: Mtu anayeikusanya, au mtu anayeinunua kwa pesa zake, au alielemewa, au mtu anayepigania Dini ya Allaah, au mtu masikini ambaye baada ya kupewa Swadaqah humpa sehemu yake mtu tajiri kama zawadi.”[1] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na Ibn Maajah, na akaisahihisha Al-Haakim]

 

 

 

521.

وَعَنْ عُبَيْدِ اَللَّهِ بْنِ عَدِيِّ بْنِ اَلْخِيَارِ، {أَنَّ رَجُلَيْنِ حَدَّثَاهُ أَنَّهُمَا أَتَيَا رَسُولَ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم يَسْأَلَانِهِ مِنَ اَلصَّدَقَةِ، فَقَلَّبَ فِيهِمَا اَلْبَصَرَ، فَرَآهُمَا جَلْدَيْنِ، فَقَالَ: "إِنْ شِئْتُمَا، وَلَا حَظَّ فِيهَا لِغَنِيٍّ، وَلَا لِقَوِيٍّ مُكْتَسِبٍ".} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَقَوَّاهُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ

Kutoka kwa ‘Ubaydullaah bin ‘Adiyy bin Al-Khiyaar[2] amesema kuwa: “Watu wawili walituarifu kuwa walikwenda kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuomba Swadaqah. Akawatazama juu mpaka chini, na alipowaona wako imara, akawaambia: “Mkitaka nitawapa, lakini kitu hicho hakipati mtu yeyote ambaye ni tajiri au mtu ambaye ana nguvu mwenye uwezo wa kuchuma.”[3] [Imetolewa na Ahmad na ikaimarishwa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy]

 

 

 

522.

وَعَنْ قَبِيصَةَ بْنِ مُخَارِقٍ اَلْهِلَالِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ  صلى الله عليه وسلم {إِنَّ اَلْمَسْأَلَةَ لَا تَحِلُّ إِلَّا لِأَحَدِ ثَلَاثَةٍ: رَجُلٌ تَحَمَّلَ حَمَالَةً، فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَهَا، ثُمَّ يُمْسِكَ، وَرَجُلٌ أَصَابَتْهُ جَائِحَةٌ، اِجْتَاحَتْ مَالَهُ، فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَ قِوَامًا مِنْ عَيْشٍ، وَرَجُلٌ أَصَابَتْهُ فَاقَةٌ حَتَّى يَقُومَ ثَلَاثَةٌ مِنْ ذَوِي الْحِجَى مِنْ قَومِهِ: لَقَدْ أَصَابَتْ فُلَانًا فَاقَةٌ; فَحَلَّتْ لَهُ اَلْمَسْأَلَةُ حَتَّى يُصِيبَ قِوَامًا مِنْ عَيْشٍ، فَمَا سِوَاهُنَّ مِنَ اَلْمَسْأَلَةِ يَا قَبِيصَةُ سُحْتٌ يَأْكُلُهَا  صَاحِبُهَا‏ سُحْتًا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ

Kutoka kwa Qabiyswah bin Mukhaariq Al-Hilaaliyy[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuomba hakuruhusiwi isipokuwa kwa moja kati ya matatu: (a) Mtu aliyeweka dhamana, ambaye huruhusiwa kuomba hadi amepata kisha ajizuie (b) Mtu ambaye mali zake zimeteketezwa na maafa yaliyomsibu. Ameruhusiwa kuomba hadi atakapopata kiasi cha kumkimu. (c) Mtu aliyefilisika na akawa maskini anayethibitishwa na watu watatu werevu, anaruhusiwa kuomba hadi atakapopata cha kumkimu. Sababu yoyote nyingine ya kuomba Ee Qabiyswah ni haramu na mtu anayeomba hivyo, atakuwa anakula haramu.” [Imetolewa na Muslim, Abuu Daawuwd, Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]

 

 

 

523.

وَعَنْ عَبْدِ اَلْمُطَّلِبِ بْنِ رَبِيعَةَ بْنِ اَلْحَارِثِ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {إِنَّ اَلصَّدَقَةَ لَا تَنْبَغِي لِآلِ مُحَمَّدٍ، إِنَّمَا هِيَ أَوْسَاخُ اَلنَّاسِ}

وَفِي رِوَايَةٍ: {وَإِنَّهَا لَا تَحِلُّ لِمُحَمَّدٍ وَلَا آلِ مُحَمَّدٍ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa ‘Abdul Mutwalib bin Rabiy’ah bin Al-Haarith[5] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hizi Swadaqah hazifai kwa watu wa Rasuli wa Allaah kwani hizo uchafu wa watu.”[6]

Katika Riwaayah nyingine: “Hizo si halaal kwa Muhammad wala familia yake.” [Imetolewa na Muslim]

 

 

 

524.

وَعَنْ جُبَيْرِ بْنِ مُطْعِمٍ رضى الله عنه قَالَ: {مَشَيْتُ أَنَا وَعُثْمَانُ بْنُ عَفَّانَ  رضى الله عنه إِلَى اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقُلْنَا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ، أَعْطَيْتَ بَنِي اَلْمُطَّلِبِ مِنْ خُمُسِ خَيْبَرَ وَتَرَكْتَنَا، وَنَحْنُ وَهُمْ بِمَنْزِلَةٍ وَاحِدَةٍ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم  "إِنَّمَا بَنُو اَلْمُطَّلِبِ وَبَنُو هَاشِمٍ شَيْءٌ وَاحِدٌ".} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ

Kutoka kwa Jubayri bin Mutw’im (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “’Uthmaan bin ‘Affaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na mimi tulimuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) tukamuambia: “Ee Rasuli wa Allaah! Umewapa wana wa Al-Mutwalib Khumus (moja ya tano) ya ngawira ya vita vya Khaybar na hukutupa sisi, na sisi na wawo ni daraja moja.”[7] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Wana wa ‘Abdul-Mutwalib na wana wa Haashim wote ni wamoja tu.”[8] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]

 

 

 

525.

وَعَنْ أَبِي رَافِعٍ رضى الله عنه {أَنَّ اَلنَّبِيَّ  صلى الله عليه وسلم بَعَثَ رَجُلًا عَلَى اَلصَّدَقَةِ مِنْ بَنِي مَخْزُومٍ، فَقَالَ لِأَبِي رَافِعٍ: اِصْحَبْنِي، فَإِنَّكَ تُصِيبُ مِنْهَا، قَالَ: حَتَّى آتِيَ اَلنَّبِيَّ  صلى الله عليه وسلم فَأَسْأَلَهُ.‏ فَأَتَاهُ فَسَأَلَهُ، فَقَالَ: " مَوْلَى اَلْقَوْمِ مِنْ أَنْفُسِهِمْ، وَإِنَّا لَا تَحِلُّ لَنَا اَلصَّدَقَةُ ".} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالثَّلَاثَةُ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ

Kutoka kwa Abuu Raafi’[9] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtuma mtu wa Banuw Makhzuwm kwenda kukusanya Swadaqah na akamtaka Abuu Raafi’ aende naye ili akapate sehemu ya hiyo. Abuu Raafi’ akasema: “Hapana siendi hadi nikamuulize Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alipokwenda kumuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Swadaqah imeharamishwa kwetu sisi, na mtumwa[10] wa watu ni mmoja wapo.” [Imetolewa na Ahmad, na Ath-Thalaathah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd), Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]

 

 

 

526.

وَعَنْ سَالِمِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عُمَرَ، عَنْ أَبِيهِ، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُعْطِي عُمَرَ اَلْعَطَاءَ، فَيَقُولُ: أَعْطِهِ أَفْقَرَ مِنِّي، فَيَقُولُ: "خُذْهُ فَتَمَوَّلْهُ، أَوْ تَصَدَّقْ بِهِ، وَمَا جَاءَكَ مِنْ هَذَا اَلْمَالِ، وَأَنْتَ غَيْرُ مُشْرِفٍ وَلَا سَائِلٍ فَخُذْهُ، وَمَا لَا فَلَا تُتْبِعْهُ نَفْسَكَ".} رَوَاهُ مُسْلِمٌ

Kutoka kwa Saalim bin ‘Abdillaah bin ‘Umar kwa upokezi wa baba yake amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpa zawadi ‘Umar, naye akamuambia: “Mpe mtu ambaye ni maskini kuliko mimi.” Aliposikia hivyo, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aksema: “Wewe chukua, na uifanye mali yako, au uigawe kama Swadaqah. Chukua kinachokuja katika mali hii wala wewe huna uroho wala huombi, lakini isiyokuwa hiyo usiuache moyo wako uitamani.” [Imetolewa na Muslim]

 

[1] Imekatazwa kwa mtu tajiri kuchukua pesa zozote kutoka katika Zakaah lakini ikiwa mtu maskini atapata pesa za Zakaah, akanunua kitu kwa pesa hizi na akampa hicho mtu tajiri, inaruhusiwa.

[2] ‘Ubaydullaah bin ‘Adiyy bin Al-Khiyaar alikuwa Mkuraishi kutoka Banuw Nawfal. Alizaliwa wakati Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) bado yu hai, lakini anahesabika miongoni mwa Taabi’iyn. Alisimulia Hadiyth kutoka kwa ‘Umar na ‘Uthmaan na wengine. Inasemekana kuwa babake aliuawa kule Badr kama kafiri. ‘Ubaydullaah anasemekana kuwa alikuwa kijana mkubwa wakati Makkaah ilipotekwa, na kwa hivyo alikuwa Swahaba. Alikuwa miongoni mwa utawala wa Al-Waliyd bin Abdil-Maalik mnamo mwaka wa 90 A.H.

[3] Watu wengine wanaitafsiri Hadiyth hii kwamba, mtu anayeweza kufanya kazi ya kipato, hata kama yeye ni maskini, asipokee Swadaqah. Tafsiri hii siyo sahihi. Hadiyth nyingine inaweka wazi kwa kusema, mtu ambaye yuko karibu na kufa kwa njaa anaweza kuomba Swadaqah.

[4] Qabiyswah bin Mukhaariq Al-Hilaaliyy ndiye Abuu Bishr Qabiyswah bin Al-Mukhaariq bin ‘Abdillaah bin Shaddaad Al-‘Aamir Al-Hilaal, alikuwa ni Swahaba aliyelowea Basra. Alimzuru Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na akasimulia Hadiyth kutoka kwake. Yeye ni msimulizi wa Hadiyth sita.

[5] ‘Abdul Mutwalib bin Rabiy’ah bin Al-Haarith ndiye mwana wa ‘Abdul-Mutwalib bin Haashim Al-Qurayashiy. Alilowea Al-Madiynah, kisha akahamia Damascus ambako alifia.

[6] Imekatazwa kwa kila kizazi cha Muhammad (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kukubali malipo ya Zakaah. Hukmu  hii imeafikiwa. Hata hivyo, kuna tofauti ya maoni juu ya hali ya Swadaqah ya khiari. Hawa siyo vizazi vya Muhammaad (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) peke yake wanaoharamishiwa kupokea malipo za Zakaah, bali wamo pia vizazi vya ‘Aliy, ‘Abbaas, Ja’far, ‘Aaqil, ‘Abdul-Mutwalib bin ‘Abd-Manaaf ambayo inamaanisha kuwa wote hawa wamo katika familia ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).

[7] Usemi wa Jubayr bin Mutw’im na ‘Uthmaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) kuwa wao wako sawa au daraja zao sawa una maana mbili: (a) Wote wanamtii Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa njia ile ile kama vizazi vya Al-Mutwalib wanavyomtii. (b) Banuw Mutwalib hawawapiti wao katika kustahili kutokana na miungano ya mahusiano na udugu kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). ‘Uthmaan baki ya kupewa heshima ya kuwa mkwe wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) pia anatoka katika ukoo wa Banuw Umayiyyah. Banuw Umayiyya na Banuw Haashim walihisabika kuwa makabila yaliyo sawa kwa mujibu wa hadhi yao miongoni mwa vizazi vya Maquraishi.

 

[8] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) Amesema hivi: “Hakuna ubishi kuwa kuhusu daraja, na ukoo, Banuw Haashim na Banuw Umayiyyah wako sawa kabisa. Lakini Banuw Mutwalib waliungana na upande wa Waislam, wakati Banuw Nawfal na Banuw Abdish-Shams waliwapinga Waislam. Kwa sababu hiyo Banuw Haashim na Banuw Mutwalib wako sawa, na wakati ulipofika, walipewa Khumus ya pesa lakini ninyi hamkupewa chochote.”

[9] Abuu Raafi’ alikuwa mtumwa wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), na jina lake ni Aslam au Hurmuz au Thaabit au Ibraahiym. Alikuwa Mkipti wa Misri na alimilikiwa na Al-‘Abbaas aliyemzawadia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alisilimu kabla ya Badr, na hakuwahi kuishuhudia vita ile. Alishuhudia vita za Uhud na zilizofuata. Al-‘Abbaas aliposilimu, Abuu Raafi’ ndiye aliyempa habari hizo njema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ambaye alimuacha huru. Alikufa mwanzo mwanzo wa Ukhalifa wa ‘Aliy mnamo mwaka wa 36 A.H. kule Al-Madiynah.

[10] Mtu ambaye kaharamishiwa kupokea Zakaah hata mtumwa wake ni haraam kupokea

 

Share