01-Imaam Ibn Baaz: Akiwa Ndani Ya Ihraam Amechezea Nywele Kisha Zimeng'oka

 

 

Akiwa Ndani Ya Ihraam Amechezea Nywele Kisha Zimeng'oka

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Nina tabia ya kuchezea nywele ninapoikuwa na fikra. Nilipokwishaingia katika ihraam, bila ya kujitambua, nilifanya hivyo na baadhi ya nywele ziling'oka na kuanguka. Je, napaswa kulipa kafara?

 

JIBU:

 

Hakuna haja kufanya hivyo (kulipa kafara) kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametaja kuhusu Waumini kwamba wamesema:  

رَبَّنَا لاَ تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا

“Rabb wetu Usituchukulie tukisahau au tukikosea. [Al-Baqarah:286]

 

Kisha Allaah Akawajibu du'aa yao hii kama ilivyotajwa katika Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  Aliitikia kwa kusema:

((قَدْ فَعَلْت))  

(Nimeiitikia [du'aa]) [Muslim katika Swahiyh yake]

 

[Fataawa Al-Hajj Wal 'Umrah waz-Ziyaarah Uk. 58]

 

 

 

Share