02-Imaam Ibn Baaz: Amenyoa Kwapa Akiwa Katika Hali Ya Ihraam

 

Amenyoa Kwapa Akiwa Katika Hali Ya Ihraam

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

  

SWALI:

 

Hujaji ameingia katika Ihraam ya 'Umrah, kisha akakumbuka kuwa ni waajib kunyoa kwapani. Akanyoa akiwa katika ihraam. Kisha akaelekea kufanya 'Umrah. Tunaomba mutuelezee hukmu ya hili, na Allaah Awalipe.

 

JIBU:

 

Kunyoa kwapani au kunyofoa nywele zake sio waajib kwa ajili ya kuingia katika ihraam. Bali ni jambo la kupendeza kunyoa na kubakia msafi kabla ya kuingia katika ihraam, kama inavyopendekezeka kupunguza masharubu, kukata kucha, kunyoa nywele za sehemu za siri ikihitajika (yaani ikiwa zimekuwa nyingi kiasi cha kuhitaji kupunguzwa) Sio lazima kufanya hivyo mtu anapoingia katika ihraam, bali inatosheleza akifanya kabla ya kuingia katika ihraam akiwa bado nyumbani kwake au njiani. Na hawajibiki kufanya lolote (kulipa kafara) yule anayekumbuka kunyoa kwapa kwani ni ukosefu wa kutambua hukmu ya jambo hili. Hali kadhalika haiwajibiki lolote kwa aliyekwishaingia katika ihraam kisha akasahau na kufanya lolote ambalo limetajwa kufanywa kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:

رَبَّنَا لاَ تُؤَاخِذْنَا إِن نَّسِينَا أَوْ أَخْطَأْنَا

“Rabb wetu Usituchukulie tukisahau au tukikosea. [Al-Baqarah:286]

 

Na imethibitika kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa Allaah Aliikubali du'aa hii. 

 

 

[Majmuw' Fataawa Samaahat  Shaykh Ibn Baaz – Mjalada 6, Uk. 96, Fatwa Namba 48]

  

 

 

Share