03-Imaam Ibn Baaz: Amesahau Kutamka Talbiyah katika Hajj ya Tamattu'

 

Amesahau Kutamka Talbiyah katika Hajj ya Tamattu'

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

   

 

SWALI:

 

Hajji ameingia katika ihraam alipofika Miyqaat lakini kasahau kutamka talbiyah kwa ajili ya Hajj ya Tammattu'. Je amalize taratibu zake kama ni Hajji wa Tammattu’? Afanye nini ikiwa atavua ihraam yake na kuvaa ihraam ya Hajj akiwa Makkah? 

 

JIBU:

 

Ikiwa ametia niyyah ya kutekeleza 'Umrah alipoingia katika ihraam kisha akasahau kutamka talbiyah huku akiwa na niyyah ya 'Umrah, atahesabika kama aliyetamka talbiyah. Anatakiwa afanye twawaaf, sa’ay na kukata nywele kisha avue ihraam yake. Anaruhusiwa kutamka talbiyah akiwa njiani. Ikiwa hakutamka talbiyah basi hakuna kimpasacho kufanya (kama kafara) kwani kutamka talbiyah ni Sunnah iliyothibiti. Afanye twawaaf, sa’y, akate nywele zake ili amalize 'Umrah yake. Hii ni kwa sababu alikuwa na niyyah ya 'Umrah. Ikiwa ametia niyyah ya Hajj wakati alipoingia katika ihraam na muda unatosheleza, inapendekezeka kubadilisha niyyah yake kufanya 'Umrah ambayo ni kufanya twawaaf, sa’y, kukata nywele ili kujitoa katika ihraam.

 

Himdi Anastahiki Allaah, atahesabika kuwa kama ni Mutamatti'

 

 

[Fataawa Muhimmah tata'allaq bil-Hajji wal-‘Umrah – Uk. 16, Fatwa Namba 4]

 

Share