05-Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kurudia Kufanya Umrah Baada Ya Muda Mfupi Kutoka Makkah

 

Kurudia Kufanya Umrah Baada Ya Muda Mfupi Kutoka Makkah

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Amefanya 'Umrah, alipomaliza amekwenda Twaaif kwa kazi fulani. Kisha alipomaliza kazi zake Twaaif alitaka kufanya tena 'Umrah kwa ajili ya mtu aliyefariki. Je, inaruhusiwa?

 

JIBU:

 

Hakuna ubaya kwake kufanya hivyo. Anapofanya mtu 'Umrah kisha akaondoka Makkah kwenda Twaaif au Jeddah kwa sababu fulani, akapenda kumfanyia 'Umrah mtu aliyefariki, hakuna ubaya, hata kama akirudia tena kufanya hivyo.

 

Iliyokatazwa ni kubakia Makkah kisha kwenda Tan'iym (Masjid 'Aaishah, penye kutilia Ihraam) ili kurudi Makkah kufanya 'Umrah nyingine. Hii imeharamishwa.

 

[Liqa-aat al-Baab Al-Maftuwh – Mjalada 1, Uk. 51, Namba 86]

 

 

 

 

Share