27-Zawadi Kwa Wanandoa: Kubusu Kabla Ya Kuingiliana

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

27-Kubusu Kabla Ya Kuingiliana

 

القبلة قبل الجماع

 

'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha)  amesema:

“Hakika Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)  alikuwa akiwabusu wake zake kisha akitoka kuelekea kuswali na hakuwa akitawadha.”

(Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na Ahmad)

 

Tendo la kubusu lina athari muhimu sana katika mapenzi na hukurubisha zile hisia za mapenzi na mwisho hupelekea kugandana kwa kiwiliwili, na jinsi lilivyo muhimu ni kuwa mwenyewe Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alikuwa haliachi hata kama amefunga saumu, kwani alikuwa akibusu na akiwakumbatia wake zake hali ya kuwa amefunga.” (Al-Bukhaariy na Muslim) Ummu Salama (Radhiya Allaahu 'anha)  amesema: Hakika Mtume wa Allah alikuwa akiwabusu wake zake hali ya kuwa amefunga.

 

Busu linakuwa katika hali nzuri na yenye kufidisha na kusisimua likiwa ni ndefu na haswa linapokuwa ni mdomo kwa mdomo hali ya kuwa wamefunga macho mawili na kufungua kidogo kidogo mara kwa mara. Wakati huo inapokuwa miili imegandana na pumzi kubadilishana hali zikiwa moto moto, ukianzia kuvuta kwa ndani kabisa na macho yenu yakiwa yanaangaliana kwa huruma. Yote haya huzipa raha nafsi za wanandoa na ni vitangulizi vizuri kwa kutayarisha mazingira mazuri ya kuanza kwa Jimai.

 

Kubusiana hakuishii katika midomo miwili tu, lakini huweza kuendelezwa katika maeneo mengine ya kiwiliwili ambayo yanaweza kusisimshwa na na hivyo  matamaniwa yakasimama.

Share