Shaykh Fawzaan: Wanaoghafilika Na Kauli Ya Laa Ilaaha Illa-Allaah

 

Wanaoghafilika Na Kauli Ya Laa Ilaaha Illa-Allaah

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu-Allaah)

www.alhidaaya.com

 

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu-Allaah) amesema:

 

“Kuna watu ambao shaytwaan anawaghafilisha na kauli ya:

 

لا إله إلاَّ الله

Laa ilaaha illa-Allaah

 

Hawatamki isipokuwa kwa uchache wala hawamdhukuru Allaah kwayo isipokuwa kidogo wala hawaikariri juu ya kuwa hiyo ni nzito katika Mizani. Basi hiyo ni kauli nzito kabisa lakini imekuwa ni wachache wanaoitanabahi na kuikumbuka na kuzoesha ulimi kuitamka na kuikariri isipokuwa yule ambaye Allaah Amejaaliwa tawfiyq.”

 

[Tafsiyr Kalimah At-Tawhiyd (77)]

 

 

 

Share