12-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Mifano Ya Ukarimu Wake: Akitoa Bila Kukhofia Umasikini

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

12-Mifano Ya Ukarimu Wake: Akitoa Bila Kukhofia Umasikini

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitoa swadaqah kila mara bila ya kukhofu umasikini:

 

 

 

عَنْ مُوسَى بْنِ أَنَسٍ، عَنْ أَبِيهِ، قَالَ: مَا سُئِلَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَلَى الإِسْلاَمِ شَيْئًا إِلاَّ أَعْطَاهُ. قَالَ: فَجَاءَهُ رَجُلٌ فَأَعْطَاهُ غَنَمًا بَيْنَ جَبَلَيْنِ فَرَجَعَ إِلَى قَوْمِهِ فَقَالَ: "يَا قَوْمِ أَسْلِمُوا فَإِنَّ مُحَمَّدًا يُعْطِي عَطَاءً لاَ يَخْشَى الْفَاقَةَ"

Imepokelewa kutoka kwa Muwsaa bin Anas kutoka kwa baba yake kwamba: Hakupata kuombwa kitu Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa ajili ya Uislamu isipokuwa alitoa.”  Akasema:  “Alimjia mtu akampa kundi la mifugo ya (kondoo na mbuzi). Akarudi kwa watu wake na kusema: “Enyi watu wangu! Silimuni katika Uislamu kwani Muhammad anatoa swadaqah bila ya kukhofia ufukara.” [Muslim]

 

 

Share