017-Hiswnul-Muslim: Du’aa Za Wakati Wa Kurukuu

Hiswnul-Muslim

017-Du’aa Za Wakati Wa Kurukuu

www.alhidaaya.com

 

 

Bonyeza Hapa Usikilize

 

 

 

[33]

سُبْـحانَ رَبِّـيَ الْعَظـيم

 

Subhaana Rabbiyal ’Adhwiym

 

Ametakasika Rabb wangu aliye Mtukufu[1]  (mara 3)

 

 

[34]

سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ رَبَّـنا وَبِحَـمْدِك، اللّهُـمَّ اغْفِـرْ لي

 

Subhaanaka Allaahumma Rabbanaa wabihamdika, Allaahummaghfir liy

 

Utakasifu ni Wako Ee Allaah Rabb wetu na Himdi ni Zako Ee Allaah, nighufurie[2]

 

 

[35]

سُبـّوحٌ قُـدّْوس، رَبُّ الملائِكَـةِ وَالـرُّوح

 

Subbuwhun Qudduwsun  Rabbul-Malaaikati war-Ruwh

 

Mwingi wa kutakaswa, Mtakatifu, Rabb wa Malaika na Jibiriyl[3].

 

 

[36]

اللّهُـمَّ لَكَ رَكَـعْتُ، وَبِكَ آمَـنْت، ولَكَ أَسْلَـمْت، خَشَـعَ لَكَ سَمْـعي، وَبَصَـري، وَمُخِّـي، وَعَظْمـي، وَعَصَـبي، وَما استَقَـلَّ بِهِ قَدَمي

 

Allaahumma Laka raka’-tu, wabika aamantu, walaka aslamtu. Khasha’a Laka sam-’iy, wabaswariy, wamukh-khiy, wa ’adhwmiy, wa ‘aswabiy, wamas-taqalla bihi qadamiy

 

Ee Allaah Kwako nimerukuu, na Wewe nimekuamini, na Kwako nimejisalimisha, umenyenyekea Kwako usikizi wangu, na uwoni wangu, na ubongo wangu, na mfupa wangu, na hisia zangu, na ambacho kimesimama juu ya miguu yangu[4].

 

 

[37]

سُبْـحانَ ذي الْجَبَـروت، والمَلَـكوت، وَالكِبْـرِياء، وَالْعَظَـمَه

 

Subhaana dhil-Jabaruwti wal-malakuwti, wal-kibriyaai, wal-‘adhwamah

 

Ametakasika Mwenye Ujabari (Utawala, Utukufu), na Ufalme, na Ukubwa, na Uadhama [5].

 

 

 

[1]Hadiyth ya Hudhayfah bin Al-Yamaan (رضي الله عنه) - Ahlus-Sunan: Abu Daawuwd [871], At-Tirmidhiy [262], An-Nasaaiy (1/190), ibn Maajah [888], Ahmad (394, 382/5) na angalia: Swahiyh At-Tirmidhiy (1/83)

 

[2]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)   - Al-Bukhaariy (1/99), Muslim (1/350)

 

[3]Hadiyth ya ‘Aaishah (رضي الله عنها)   - Muslim (1/353), Abu Daawuwd (1/230)

 

[4]Hadiyth ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (رضي الله عنه)  - Muslim (1/534) na Maimamu wane wa Hadiyth isipokuwa ibn Maajah. Isipokuwa kauli ya Wamastaqalla bihi qadamiy haikupokelewa na Muslim wala Maimamu wanne, bali ametamka Ibn Hibbaan. Angalia: Swahiyh ibn Hibbaan [1901] na Swahiyh Ibn Khuzaymah [607]

 

[5]Hadiyth ya ‘Awf bin Maalik Al-Ashja’iyy (رضي الله عنه) - Abu Daawuwd (1/230), An-Nasaaiy (2/191), Ahmad (6/24) na isnadi yake ni Hasan.

 

 

 

Share