Vipai Vya Nyama (Meat Rolls)

Vipai Vya Nyama (Meat Rolls)

Vipimo

Siagi - Kikombe 1

Unga - Vikombe  2 (ufute, usijaze mlima)

Maji - Kiasi

Nyama ya kusaga - Kikombe 1

Pilipili manga ya unga - ½ kijiko cha chai

Kitunguu saumu(thomu) iliyosagwa -  ½ kijiko cha chai

Tangawizi iliyosagwa - ½ kijiko cha chai

Chumvi - kiasi

Namna ya kutayarisha na kupika

Kutayarisha nyama:

  1. Changanya nyama, pilipili manga, thomu, tangawizi na chumvi ndani ya sufuria, ipike bila ya kutia mafuta wala maji huku unaikoroga koroga mpaka iwe kavu.
  2. Epua weka pembeni
  3. Changanya unga na siagi mpaka uchanganyike vizuri.
  4. Changanya na maji ili ushikane, lakini usiukande.
  5. Kata madonge na usukume kama unataka kufanya chapati, lakini usifanye mwembamba sana.
  6. Kata vipande virefu virefu. (rectengular)
  7. Weka nyama juu ya kila kipande, halafu kunja upande mmoja ufunike ile nyama, kisha kunja upande wa pili kufunika ile sehemu ya kwanza uliyoikunja.
  8. Chukua uma choma choma juu yake ili kuweka nakshi, pia utadidimiza ile sehemu ya mwisho iliyokunjwa kwa kuzuwia isifunuke wakati wa kuchoma.
  9. Fanya hivyo  mpaka umalize zote.
  10. Chukua tray na kupaka siagi na uzipange humo.
  11. Washa overn na uzichome (Bake)  350 Deg C  mpaka zibadilike rangi  zikiwa tayari kuliwa.

 

Share