Tafsiyr Gani Anatakiwa Awe Nayo Mtafutaji Elimu?
Imaam Muhammad bin Swaalih Al-‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)
Alhidaaya.com [2]
SWALI:
Allaah Awahifadhi na Azinyooshe hatua zenu, Twaalib Al-‘Ilm (Mwanafunzi, Mtafutaji elimu) anataka kusoma Tafsiyr, ni zipi Tafsiyr mashuhuri ambazo anahitaji kuwa nazo mwanafunzi?
JIBU:
Maona amiliki Tafsiyr ya Ibn Kathiyr (Rahimahu Allaah), na Tafsiyr ya Shaykh wetu ‘Abdur-Rahmaan As-Sa’diy, kwani hizo mbili ni Tafsiyr bora nilizozipitia katika vitabu vya Tafsiyr.
Vilevile kuna Tafsiyr zingine kwa mtafutaji elimu mwenye shauku na kutaka (kusoma), kama vile Tafsiyr ya Al-Qurtwubiy na Tafsiyr Ash-Shawkaaniy. Na’am.
[Al-Mawqi’ Ar-Rasmiy li-Fadhwiylah Ash-Shaykh Al-'Allaamah Muhammad bin Swaalih Al-'Uthaymiyn] [3]
N.B. Katika sehemu nyingine, Imaam Ibn ‘Uthaymiyn vilevile aliitaja Tafsiyr ya Ibn Jariyr Atw-Twabariy kuwa ni katika Tafsiyr bora ila inahitaji mwenye maarifa kutokana na upana wa ufafanuzi wake na wingi wa maelezo ya wapokezi wa Ahaadiyth, Athaar na Isnaad.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/206
[2] http://www.alhidaaya.com/
[3] http://binothaimeen.net/content/12924
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7386&title=Imaam%20Ibn%20%27Uthaymiyn%3A%20Tafsiyr%20Gani%20Anatakiwa%20Awe%20Nayo%20Mtafutaji%20Elimu%3F