Macaroni Ya Express Ya Kidari Cha Kuku Na Jibini
Vipimo
Makaroni - 500 gm
Kidari cha kuku katakata vipande - ½ kilo
Kitunguu katakata kidogodogo - 1
Nyanya/tungule katakata ndogo ndogo - 3
Thomu (garlic) ilosagwa - 1 kijiko cha chai
Nyanya kopo (paste) - 1 kijiko cha kulia
Pilipili nyekundu ya unga - ½ kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia - 3 vijiko cha kulia
Jibini (Cheese) iliyokunwa ya cheddar - ½ kikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Tia thomu (kitunguu saumu) endelea kukaanga kwa dakika moja.
Tia kuku, chumvi, pilipili na endelea kukaanga au kukoroga. Acha ipikike bila kuifunika mpaka kuku aive.
Tia nyanya, changanya ukoroge mpaka nyanya ziive na kuwa laini kisha tia nyanya kopo.
Tia macaroni, koroga, kisha tia maji kiasi yafunike macaroni. Koroga kisha funika na punguza moto uwe mdogo.
Pika kwa dakika 15, koroga kisha tazama kama macaroni yameiva na maji yamekauka. Yakiwa hayakuiva bado ongezea maji lakini yasizidi ¼ kikombe. Na yakiwa yameiva na bado yana maji, funua mfuniko upike wazi ili maji yakauke.
Zima moto, kisha changanya na jibini (cheese) kisha pakua katika chombo yakiwa tayari.
Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/84
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F7428&title=Macaroni%20Ya%20Express%20Ya%20Kidari%20Cha%20Kuku