كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu)
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu)[1]
بَابُ حَدِّ اَلزَّانِي
01-Mlango Wa Adhabu Ya Uzinifu
1033.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ وَزَيْدِ بْنِ خَالِدٍ اَلْجُهَنِيِّ رَضِيَ اَللَّهُ عنهما {أَنَّ رَجُلًا مِنَ اَلْأَعْرَابِ أَتَى رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَنْشُدُكَ بِاَللَّهِ إِلَّا قَضَيْتَ لِي بِكِتَابِ اَللَّهِ، فَقَالَ اَلْآخَرُ وَهُوَ أَفْقَهُ مِنْهُ نَعَمْ. فَاقَضِ بَيْنَنَا بِكِتَابِ اَللَّهِ، وَأْذَنْ لِي، فَقَالَ: "قُلْ". قَالَ: إنَّ اِبْنِي كَانَ عَسِيفًا عَلَى هَذَا فَزَنَى بِاِمْرَأَتِهِ، وَإِنِّي أُخْبِرْتُ أَنْ عَلَى اِبْنِي اَلرَّجْمَ، فَافْتَدَيْتُ مِنْهُ بِمَائَةِ شَاةٍ وَوَلِيدَةٍ، فَسَأَلَتُ أَهْلَ اَلْعِلْمِ، فَأَخْبَرُونِي: أَنَّمَا عَلَى اِبْنِيْ جَلْدُ مَائَةٍ وَتَغْرِيبُ عَامٍ، وَأَنَّ عَلَى اِمْرَأَةِ هَذَا اَلرَّجْمَ، فَقَالَ رَسُولُ ا للَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ، لَأَقْضِيَنَّ بَيْنَكُمَا بِكِتَابِ اَللَّهِ، اَلْوَلِيدَةُ وَالْغَنَمُ رَدٌّ عَلَيْكَ، وَعَلَى اِبْنِكَ جَلْدُ مِائَةٍ وَتَغْرِيبُ عَامٍ، وَاغْدُ يَا أُنَيْسُ إِلَى اِمْرَأَةِ هَذَا، فَإِنْ اِعْتَرَفَتْ فَارْجُمْهَا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، هَذَا وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah na Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema: Mtu mmoja katika mabedui alimjia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Nakuomba kwa Allaah unihukumu kwa Kitabu Cha Allaah”. Mwingine ambaye ni mjuzi kuliko yeye akasema: “Ndio, hukumu baina yetu kwa Kitabu Cha Allaah, na uniruhusu niseme.” Akasema Rasuli wa Allaah: “Sema.” Akasema: “Mwanangu alikuwa ni muajiriwa wa huyu, akazini na mkewe, nami nilikuwa nimeambiwa kuwa mwanangu atarujumiwa, nimemtolea fidia ya mbuzi mia na mjakazi. Nikawauliza wenye ilmu wakaniambia kuwa mwanangu achapwe mijeledi mia na atolewe mjini mwaka mmoja na mke wa huyu arujumiwe. Akasema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Naapa kwa Ambaye nafsi yangu imo Mkononi mwake! Nitahukumu baina yenu kwa Kitabu Cha Allaah. Mjakazi na mbuzi warudishwe kwako. Na mwanao achapwe mijeledi mia na kutolewa mjini mwaka mmoja. Ee Unays, nenda hadi kwa mke wa bwana huyu, akiungama umrajimu (umpige mawe).”[2] [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
1034.
وَعَنْ عُبَادَةَ بْنِ اَلصَّامِتِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {خُذُوا عَنِّي، خُذُوا عَنِّي، فَقَدْ جَعَلَ اَللَّهُ لَهُنَّ سَبِيلاً، اَلْبِكْرُ بِالْبِكْرِ جَلْدُ مِائَةٍ، وَنَفْيُ سَنَةٍ، وَالثَّيِّبُ بِالثَّيِّبِ جَلْدُ مِائَةٍ، وَالرَّجْمُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ.
Kutoka kwa ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Chukueni kutoka kwangu, chukueni kutoka kwangu. Allaah Amewajaalia (wanawake) kupata njia.[3] Mume asiye na mke, na mke asiye na mume (watakapozini) watapigwa mijeledi mia na kutolewa mjini mwaka mmoja. Mume aliyeowa na mke aliyeolewa (wakizini) watapigwa mijeledi mia[4] na kupigwa mawe (Rajm).” [Imetolewa na Muslim]
1035.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أَتَى رَجُلٌ مِنْ اَلْمُسْلِمِينَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَهُوَ فِي اَلْمَسْجِدِ فَنَادَاهُ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنِّي زَنَيْتُ، فَأَعْرَضَ عَنْهُ، فَتَنَحَّى تِلْقَاءَ وَجْهِهِ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنِّي زَنَيْتُ، فَأَعْرَضَ عَنْهُ، حَتَّى ثَنَّى ذَلِكَ عَلَيْهِ أَرْبَعَ مَرَّاتٍ، فَلَمَّا شَهِدَ عَلَى. نَفْسِهِ أَرْبَعَ شَهَادَاتٍ. دَعَاهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ "أَبِكَ جُنُونٌ ؟" قَالَ. لَا. قَالَ: "فَهَلْ أَحْصَنْتَ ؟". قَالَ: نَعَمْ. فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "اِذْهَبُوا بِهِ فَارْجُمُوهُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Mtu mmoja katika Waislamu alimjia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akiwa Msikitini, akamnadia: “Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nimezini.” Rasuli wa Allaah akampa mgongo, akamuendea akamuambia: “Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nimezini!” Rasuli wa Allaah akampa mgongo, hata akaikariri kauli hiyo mara nne. Alipojishuhudia zinaa yeye mwenyewe mara nne, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuita akamuuliza: “Una wazimu?” Akasema: “Laa (hapana).” Akasema: “Umehifadhika (una mke)?” Akasema: “Ndio.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Mchukueni na mumrajimu.”[5] [Bukhaariy, Muslim]
1036.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {لَمَّا أَتَى مَاعِزُ بْنُ مَالِكٍ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ لَهُ: "لَعَلَّكَ قَبَّلْتَ، أَوْ غَمَزْتَ، أَوْ نَظَرْتَ ؟" قَالَ: لَا يَا رَسُولَ اَللَّهِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Maa’iz bin Maalik alipokuja kwa Nabiy[6] (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Pengine ulibusu au uligusa au ulitazama.” Akasema Maa’iz: “Sivyo Ee Rasuli wa Allaah!” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1037.
وَعَنْ عُمَرَ بْنِ اَلْخَطَّابِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّهُ خَطَبَ فَقَالَ: إِنَّ اَللَّهَ بَعَثَ مُحَمَّدًا بِالْحَقِّ، وَأَنْزَلَ عَلَيْهِ اَلْكِتَابَ، فَكَانَ فِيمَا أَنْزَلَ اَللَّهُ عَلَيْهِ آيَةُ اَلرَّجْمِ. قَرَأْنَاهَا وَوَعَيْنَاهَا وَعَقَلْنَاهَا، فَرَجَمَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَرَجَمْنَا بَعْدَهُ، فَأَخْشَى إِنْ طَالَ بِالنَّاسِ زَمَانٌ أَنْ يَقُولَ قَائِلٌ: مَا نَجِدُ اَلرَّجْمَ فِي كِتَابِ اَللَّهِ، فَيَضِلُّوا بِتَرْكِ فَرِيضَةٍ أَنْزَلَهَا اَللَّهُ، وَإِنَّ اَلرَّجْمَ حَقٌّ فِي كِتَابِ اَللَّهِ عَلَى مَنْ زَنَى، إِذَا أُحْصِنَ مِنْ اَلرِّجَالِ وَالنِّسَاءِ، إِذَا قَامَتْ اَلْبَيِّنَةُ، أَوْ كَانَ اَلْحَبَلُ، أَوْ اَلِاعْتِرَافُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alihutubia akasema: “Kwa hakika Allaah Alimtuma Muhammad (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa haki, Akamteremshia Kitabu, ikawa katika Aliyomteremshia ni Aayah ya Rajmi, tuliisoma tukaihifadhi na tukaizingatia. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akapiga kwa mawe (Rajm), na sisi baada yake tukapiga kwa mawe. Kwa hivyo nachelea isije zama zikawa ndefu kwa watu akaja kusema mwenye kusema: “Mbona hatuoni kupiga kwa mawe (Rajm) katika Kitabu Cha Allaah!” Kwa ajili hiyo wakapotea kwa kuacha faradhi Aliyoiteremsha Allaah. Na kwa hakika Rajm kumethubutu katika Kitabu Cha Allaah[7] kwa mwenye kuzini aliyeoa au ameolewa miongoni mwa wanaume na wanawake utakaposimama ubainifu au kwa kushika mimba au kwa kukiri.” [Bukhaariy, Muslim]
1038.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {"إِذَا زَنَتْ أَمَةُ أَحَدِكُمْ، فَتَبَيَّنَ زِنَاهَا، فَلْيَجْلِدْهَا اَلْحَدَّ، وَلَا يُثَرِّبْ عَلَيْهَا، ثُمَّ إِنْ زَنَتْ فَلْيَجْلِدْهَا اَلْحَدَّ، وَلَا يُثَرِّبْ عَلَيْهَا، ثُمَّ إِنْ زَنَتِ اَلثَّالِثَةَ، فَتَبَيَّنَ زِنَاهَا، فَلْيَبِعْهَا وَلَوْ بِحَبْلٍ مِنْ شَعَرٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ وَهَذَا لَفْظُ مُسْلِمٍ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Atakapozini mjakazi wa mmoja wenu[8] na uzinifu wake ukabainika, basi ampe adhabu kwa kumchapa mijeledi wala asimkaripie. Atakapozini tena amchape mijeledi wala asimkaripie. Atakapozini mara ya tatu uzinifu wake ukabainika basi amuuze japo kwa kamba ya nywele.” [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
1039.
وَعَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَقِيمُوا اَلْحُدُودَ عَلَى مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wasimamishieni adhabu iliyowamiliki mikono yenu.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd]
1040.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حَصِينٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اِمْرَأَةً مِنْ جُهَيْنَةَ أَتَتْ نَبِيَّ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَهِيَ حُبْلَى مِنْ اَلزِّنَافَقَالَتْ: يَا نَبِيَّ اَللَّهِ! أَصَبْتُ حَدًّا، فَأَقِمْهُ عَلَيَّ، فَدَعَا نَبِيُّ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَلِيَّهَا. فَقَالَ: "أَحْسِنْ إِلَيْهَا فَإِذَا وَضَعَتْ فَائْتِنِي بِهَا" فَفَعَلَ. فَأَمَرَ بِهَا فَشُكَّتْ عَلَيْهَا ثِيَابُهَا، ثُمَّ أَمَرَ بِهَا فَرُجِمَتْ، ثُمَّ صَلَّى عَلَيْهَا، فَقَالَ عُمَرُ: أَتُصَلِّي عَلَيْهَا يَا نَبِيَّ اَللَّهِ وَقَدْ زَنَتْ ؟ فَقَالَ: "لَقَدْ تَابَتْ تَوْبَةً لَوْ قُسِّمَتْ بَيْنَ سَبْعِينَ مِنْ أَهْلِ اَلْمَدِينَةِ لَوَسِعَتْهُمْ، وَهَلْ وَجَدَتْ أَفَضَلَ مِنْ أَنْ جَادَتْ بِنَفْسِهَا لِلَّهِ ؟} ". رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Mwanamke wa kabila la Juhaynah (Al-Ghamidiya) alienda kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akiwa na mimba ya zinaa, akamuambia: “Ee Nabiy wa Allaah! Nimestahiki haddi (adhabu) kwa hivyo nisimamishie.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuita msimamizi wake akamuambia: “Mfanyie wema, atakapojifungua[9] mlete.” Akafanya hivyo akaja naye, akaamuru, akafungwa kwa nguo zake kisha akaamuru akarajumiwa kisha akamswalia. ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) akamuambia: “Ee Nabiy wa Allaah! Unamswalia na hali amezini?” Akasema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) : “Kwa yakini ametubia tawbah ambayo lau ingaligawanyiwa kwa watu sabini mongoni mwa watu wa Madiynah, ingaliwatosha. Je ushawahi kuona lililo bora kuliko yeye kujileta mwenyewe kwa Allaah?” [Imetolewa na Muslim]
1041.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {رَجَمَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ رَجُلًا مَنْ أَسْلَمَ، وَرَجُلًا مِنْ اَلْيَهُودِ، وَاِمْرَأَةً} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَقِصَّةُ رَجْمِ اَلْيَهُودِيَّيْنِ فِي "اَلصَّحِيحَيْنِ" مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عُمَرَ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimpiga mawe (Rajm) mtu wa kabila la Aslam, na mtu mwigine wa Kiyahudi na mwanamke.[10] [Imetolewa na Muslim]
Kisa cha Mayahudi wawili kiko katika Swahiyh mbili; Swahiyh Al-Bukhaariy na Swahiyh Muslim kutoka katika Hadiyth ya ‘Ibn Umar
1042.
وَعَنْ سَعِيدِ بْنِ سَعْدِ بْنِ عِبَادَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {كَانَ بَيْنَ أَبْيَاتِنَا رُوَيْجِلٌ ضَعِيفٌ، فَخَبَثَ بِأَمَةٍ مِنْ إِمَائِهِمْ، فَذَكَرَ ذَلِكَ سَعْدٌ لِرَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: "اِضْرِبُوهُ حَدَّهُ". فَقَالُوا: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّهُ أَضْعَفُ مِنْ ذَلِكَ، فَقَالَ: "خُذُوا عِثْكَالًا فِيهِ مِائَةُ شِمْرَاخٍ، ثُمَّ اِضْرِبُوهُ بِهِ ضَرْبَةً وَاحِدَةً". فَفَعَلُوا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ . لَكِنْ اخْتُلِفَ فِي وَصْلِهِ وَإِرْسَالِهِ
Kutoka kwa Sa’iyd bin Sa’d bin ‘Ubaadah[11] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Katika nyumba zetu kulikuwa na mtu dhaifu akazini na kijakazi miongoni mwa vijakazi vyao. Sa’d akamueleza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) khabari hiyo, akasema Rasuli wa Allaah: “Mmpigeni haddi (adhabu) yake.”[12] Maswahaba wakamuambia: “Ee Rasuli wa Allaah! Yeye ni dhaifu mno kuliko hiyo (haddi).” Rasuli akasema: “Chukueni shina la mtende lenye vitawi mia na mumpige nalo mara moja.” Maswahaba wakafanya hivyo. [Imetolewa na Ahmad, An-Nasaaiy na Ibn Maajah. Sanad ya wapokezi wake ni Hasan. Hata hivyo wametofautiana kama ni mawsuwl au mursal]
1043.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ وَجَدْتُمُوهُ يَعْمَلُ عَمَلَ قَوْمِ لُوطٍ، فَاقْتُلُوا اَلْفَاعِلَ وَالْمَفْعُولَ بِهِ، وَمَنْ وَجَدْتُمُوهُ وَقَعَ عَلَى بَهِيمَةٍ، فَاقْتُلُوهُ وَاقْتُلُوا اَلْبَهِيمَةَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالْأَرْبَعَةُ، وَرِجَالُهُ مُوَثَّقُونَ، إِلَّا أَنَّ فِيهِ اِخْتِلَافًا
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtakayemkuta akifanya kitendo cha uliwati muuweni mwenye kufanya na kufanyiwa,[13] na mtu akimkuta akimuingilia mnyama basi muuweni yeye na muuweni mnyama.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah). Wapokezi wake ni madhubuti lakini ndani yake kuna ikhtilafu]
1044.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا: {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ ضَرَبَ وَغَرَّبَ وَأَنَّ أَبَا بَكْرٍ ضَرَبَ وَغَرَّبَ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، إِلَّا أَنَّهُ اخْتُلِفَ فِي رَفْعِهِ، وَوَقْفِهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alichapa mijeledi na akawatoa[14] mjini. Abuu Bakr alichapa na akatoa mjini. [Imetolewa na At-Tirmidhiy na wapokezi wake ni madhubuti, isipokuwa wamekhitilafiana kuwa ni mawquwf au Marfuw’]
1045.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلْمُخَنَّثِينَ مِنْ اَلرِّجَالِ، وَالْمُتَرَجِّلَاتِ مِنْ اَلنِّسَاءِ، وَقَالَ: {أَخْرِجُوهُمْ مِنْ بُيُوتِكُمْ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amewalaani wanaume wanaojifananisha na wanawake, na wanawake wanaojifananisha na wanaume.[15] Na akasema: “Watoeni majumbani mwenu.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1046.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اِدْفَعُوا اَلْحُدُودَ، مَا وَجَدْتُمْ لَهَا مَدْفَعًا} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَإِسْنَادُهُ ضَعِيفٌ
وَأَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِمُ: مِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا بِلَفْظِ {ادْرَأُوا اَلْحُدُودَ عَنْ اَلْمُسْلِمِينَ مَا اِسْتَطَعْتُمْ} " وَهُوَ ضَعِيفٌ أَيْضًا
وَرَوَاهُ اَلْبَيْهَقِيُّ: عَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ (مِنْ) قَوْلِهِ بِلَفْظِ:{ادْرَأُوا اَلْحُدُودَ بِالشُّبُهَاتِ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Zuieni adhabu mnapopata njia ya kuzizuia.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa isnaad dhaifu]
Na At-Tirmidhiy amepokea na Al-Haakim kutoka katika Hadiyth ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) kwa tamshi: “Waepushieni adhabu[16] Waislam kadiri muwezavyo.” [nayo pia ni dhaifu]
Al-Bayhaqiyy amepokea kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kwa kauli yake: “Epusheni haddi (adhabu) kwa shubha (utata).”
1047.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اِجْتَنِبُوا هَذِهِ اَلْقَاذُورَاتِ اَلَّتِي نَهَى اَللَّهُ تَعَالَى عَنْهَا، فَمَنْ أَلَمَّ بِهَا فَلْيَسْتَتِرْ بِسِتْرِ اَللَّهِ تَعَالَى، وَلِيَتُبْ إِلَى اَللَّهِ تَعَالَى، فَإِنَّهُ مَنْ يَبْدِ لَنَا صَفْحَتَهُ نُقِمْ عَلَيْهِ كِتَابَ اَللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ} رَوَاهُ اَلْحَاكِمُ، وَهُوَ فِي "اَلْمُوْطَّإِ" مِنْ مَرَاسِيلِ زَيْدِ بْنِ أَسْلَمَ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Jiepusheni na machafu haya Aliyokataza Allaah. Atakayetenda basi ajisitiri kwa sitara ya Allaah na atubu kwa Allaah, kwani atakayetudhihirishia hakika yake tutamsimamishia Kitabu Cha Allaah.” [Imetolewa na Al-Haakim, hadiyth hii iko katika kitabu cha Al-Muwatwa ya Imaam Malik kutoka katika Ahaadiyth za Zayd bin Aslama[17]]
[1] Huduwd ni wingi wa Hadd, ambayo ina maana ya ‘Kuzuia’. Ni adhabu ya kishariy’ah kwa wazinifu na mfano wa adhabu hizo huitwa kuwa ni Huduwd kwani zinaonesha adhabu kwa aina za watu waliotajwa. Wakati mwingine neno Hadd hutumika kutaja aina fulani ya tendo la dhambi.
[2] Hadiyth hii inaonesha hukumu ya mtu aliyezini kwa Bikra awe ni mwanamme au mwanamke ni mijeledi mia moja na kuhamishwa kwenye nje ya dola ya Kiislam kwa muda wa mwaka mmoja. Kupigwa mijeledi mia moja ni kutokana na hukumu ya Qur-aan wakati adhabu kuhamishwa ni ziada inayokubaliwa na wapokezi wote wa Hadiyth. Adhabu ya mzinifu aliyekuishaoa au kuolewa ni Rajm (adhabu ya kupigwa mawe mpaka kufa) hadi kufa kulingana na makubaliano ya ‘Ulamaa. Hii inathibitisha vile vile kuwa kukiri kwa mmoja katika wazinifu kunatosha kusimamisha adhabu.
[3] Hii inakusudia maelezo ya Allaah katika Suwrah Al-Maaidah (5) Aayah 15:
يَا أَهْلَ الْكِتَابِ قَدْ جَاءَكُمْ رَسُولُنَا يُبَيِّنُ لَكُمْ كَثِيرًا مِّمَّا كُنتُمْ تُخْفُونَ مِنَ الْكِتَابِ وَيَعْفُو عَن كَثِيرٍ ۚ قَدْ جَاءَكُم مِّنَ اللَّـهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾
“Enyi Ahlal-Kitaab! Hakika amekwishakujieni Rasuli Wetu anayekubainishieni mengi katika yale mliyokuwa mkiyaficha katika Kitabu, na anasamehe mengi. Kwa yakini imekufikieni kutoka kwa Allaah Nuru na Kitabu kinachobainisha”
[4] Hadiyth hii inamaanisha kuwa mzinifu wa kike na mzinifu wa kiume watapigwa mijeledi kisha wapigwe mawe (Rajm) hadi kufa. Hata hivyo, maoni ya ‘Ulamaa wengi ni kuwa suala la kupigwa mijeledi mia moja halina haja bali Rajm itatosheleza. Wamesema kuwa suala hili halina nguvu kwa sababu Nabiy hakumpiga Maa’iz na wengine, bali ni kupigwa mawe tu.
[5] Mtu ambaye alitoa uthibitisho huu alikuwa ni Maa’iz Aslami. Hadiyth hii inaelezea kuwa Qadhi ni lazima afanye uchunguzi wa kutosha kabla ya kutoa hukumu yake kuhusu adhabu fulani, kwani huenda maisha ya mtu yakakatishwa kwa hukumu yenye makossa.
[6] Maa’iz ndiye aliyekiri kufanya kosa hili wakati akiwa na mke.
[7] Hadiyth hii imetajwa na Muhadithina wote isipokuwa An-Nasaai, kadhalika imepokewa na Maswahaba wengi wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Iliripotiwa na Ubay bin Ka’ab kuwa Suwrah Ahzaab ilikaribiana na Suwrah Baqarah. Nyingi katika Aayah za Suwrah hizo zilifanywa Nasikh au zilikuwa Mansuwkh. Ubay bin Ka’ab anahadithia: “Tulikuwa tunasoma Aayah hizi katika Suwrah hii hadi tunapofikia katika Aayah:
‘Pindi mwanamme aliyeowa na mwanamke aliyeolewa wanapozini warujumuni’ baadae, usomaji wa Aayah hii ukafutwa lakini hukumu yake ikabaki pale pale, ambayo vile vile ni aina ya naskh.
Hukumu ya uzinifu unahitaji ushahidi ufuatao: (a) mashahidi wane, (b) kukiri kwa mhusika, na (c) mimba. Sharti hili la tatu linawahusu wanawake tu, lakini Imaam Shaafi’iy na Imaam Abuu Haniyfah hawakubaliani nalo. Kwa wanaolikubali kama ni ushahidi, mwanamke ambaye hakuolewa (asiyekuwa mtumwa) ataadhibiwa ikiwa mimba yake itakuwa wazi.
[8] Suala la mamlaka ya mtumwa mwanamke au mwanamme limeachwa kwa anayemmiliki. Watu wote walobakia wanahukumiwa na Dola. Ikiwa mtumwa mwanamme alikuwa ameshaoa, hapa kutakuwa na rai tofauti miongoni mwa ‘Ulamaa ya kuwa mamlaka ya kumpa adhabu yatakuwa kwenye Dola au kwa mwenyewe mwenye kummiliki. Ama kijakazi akizini basi atachapwa mijeledi na adhabu ya kumpiga mawe haitotekelezwa kwake. Hata kupigwa kwake mijeledi haitozidi hamsini. Ushahidi wa hili ni Aayah katika Qur-aan inayosema:
فَإِذَا أُحْصِنَّ فَإِنْ أَتَيْنَ بِفَاحِشَةٍ فَعَلَيْهِنَّ نِصْفُ مَا عَلَى الْمُحْصَنَاتِ مِنَ الْعَذَابِ
Na watakapohifadhiwa katika ndoa, kisha wakafanya uchafu basi adhabu yao itakuwa ni nusu ya adhabu ya waliyowekewa wanawake walio huru (wasioolewa).
[An-Nisaa: 4: 25]
[9] Hadiyth hii inabainisha kuwa suala la adhabu la uzinifu halitakiwi kufanyika mapema kwa mwanamke ili iangaliwe kwanza kama ana mimba. Ikiwa kama ana mimba anatakiwa asubiriwe hadi atakapojifungua. Pindi mwanamke atakapojifungua, mwanamke anaweza kupewa adhabu kwa sharti kuwa suala la kumnyonyesha mtoto na kumlea limekadhibiwa mwanamke mwingine. Ikiwa mwanamke huyo hajapatikana suala la adhabu litaakhirishwa hadi mtoto atakapoachishwa ziwa. Hata kama mwanamke huyo hakuwahi kuolewa adhabu itaakhirishwa mpaka atakapojifungua. Katika hali hiyo inatakiwa atendewe wema na jamaa zake na si vizuri kumshutumu na kumtukana ambapo Shariy’ah hairuhusu.
[10] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwahukumu watu wane kupigwa Rajm katika wakati wake. Wa kwanza ni lile tukio la mwanamke, wa pili alikuwa mtu wa kabila la Banu Aslam (Maa’iz bin Maalik) na Mayahudi wawili (mwanamke na mwanamme). Hili linamaanisha kuwa hukumu za Shariy’ah zinahusika pia kwa makafiri kama zinavyotekelezwa kwa Waislam.
[11] Sa’iyd bin Sa’d bin ‘Ubaadah Al Answaar As-Sa’iyd alikuwa ni Swahaba. Inasemekana kwa wengine alikuwa ni Taabi’i, alikuwa ni madhubuti aliyepokea baadhi za Ahaadiyth. Alikuwa gavana wa Yemen wakati wa Ukhalifa wa ‘Aliy bin Abi Twaalib.
[12] Hadiyth hii inaelezea ikiwa mtu ambaye hajaoa akazini, lakini kulingana na hali yake ya udhaifu au maradhi, na pindi itakaposimamishwa adhabu kwake anaweza kufa kama atapigwa mijeledi mia moja, inatakiwa upole katika kutekeleza adhabu yenyewe. Idadi ya mijeledi mia moja haitopunguzwa, bali huenda fimbo ya kupigia ikawa ni ndogo zaidi. Hata hivyo kunaweza kuwa na tofauti ya kupiga na isiwe kwa nguvu zaidi kama katika hali ya kawaida.
[13] Kuna rai tofauti kwa ‘Ulamaa kuhusu adhabu ya liwati kwa mwanamme kumfanyia mwanamke, pamoja na kuwa hakuna Hadiyth maalum inayoainisha hilo zaidi ya adhabu ya kifo. Hii ina maana tofauti iliyopo ni jinsi ya kutekeleza adhabu yenyewe tu. Baadhi wanaona kuwa adhabu ni Rajm (kupigwa kwa mawe). Wengine wanaona kuwa watupwe kutoka umbali wa juu na kurushwa chini. Kundi lingine linaona kuwa wawashiwe moto. Rai nyingine inaona kuwa hukumu ya mzinifu ipite kwake; Kama ameoa arajimiwe; vinginevyo, apigwe mijeledi mia moja na atolewe nje ya mji. Allaah ndiye Mjuzi.
[14] Baadhi ya ‘Ulamaa wana muono kuwa adhabu ya kuhamishwa mji imefutwa na haifanyi kazi tena. Hadiyth hii inapinga ile rai ya kuwa ikiwa wazinifu walihamishwa miji wakati wa Makhalifa waongofu, dalili ipi inayoonesha kuwa hukumu hii imefutwa?
[15] Hadiyth hii inathibitisha kuwa mwanamke au mwanamme ambaye anaiga tabia ya jinsia ya pili ni watu wenye kulaaniwa na jambo hili ni katika madhambi. Matowashi wapo wa aina mbili: ni wale matowashi ambao maumbile yao ya kiwiliwili yanafanana na wanawake na wakati wengine wanafanana na wanaume. Matowashi lazima wavae nguo zinazofanana na jinsia yao na kufanana nao zaidi.
[16] Ikiwa kuna shaka kuhusu ukweli fulani wa ushahidi unaopelekea katika hukumu ya adhabu, hukumu ile inabidi itenguliwe. Hadiyth hii haikusudii kuwa hakuna hukumu itakayotolewa, bali inamaanisha kuwa hukumu ya adhabu haitopitishwa hadi tatizo liwe la wazi uwazi usio na shaka. Watu wanashauriwa kuwa wasipeleke kesi yoyote mahakamani hadi wajenge ushahidi wa kutosha unaowaunga katika madai yao ili kuthibitisha kuwa fulani ni mwenye kosa.
[17] Alikuwa ni Swahaba kutoka kabila la Al-Balawi. Alikuwa katika ukoo wa Banuu Al-‘Ajlan, washirika wa Banuu ‘Amr bin ‘Awf katika Al-Answaar. Alishuhudia Badr na kadhalika Swiffiyn akiwa pamoja na ‘Aliy. Hata hivyo, Hishaam Al-Kalabi amesema, (Zaid) aliuwawa na Twulayha bin Khuwaylid Al-Asad katika siku ya Bazakha katika mwaka wa 11 Hijriyyah mwanzoni mwa Ukhalifa wa Abuu Bakr.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu)
بَابُ حَدِّ اَلْقَذْفِ
02-Mlango Wa Adhabu Ya Kusingizia
1048.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {لَمَّا نَزَلَ عُذْرِي، قَامَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَلَى اَلْمِنْبَرِ، فَذَكَرَ ذَلِكَ وَتَلَا اَلْقُرْآنَ، فَلَمَّا نَزَلَ أَمَرَ بِرَجُلَيْنِ وَاِمْرَأَةٍ فَضُرِبُوا اَلْحَدَّ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ وَالْأَرْبَعَةُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: Udhuru wangu ulipoteremka (kutoka mbinguni)[1] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisimama juu ya mimbari akaeleza hilo akasoma Qur-aan, alipoteremka aliamuru wanaume wawili na mwanamke mmoja[2] wapigwe haddi (adhabu).[3] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah)]
1049.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أَوَّلَ لِعَانٍ كَانَ فِي اَلْإِسْلَامِ أَنَّ شَرِيكَ بْنُ سَمْحَاءَ قَذَفَهُ هِلَالُ بْنُ أُمَيَّةَ بِاِمْرَأَتِهِ، فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "اَلْبَيِّنَةَ وَإِلَّا فَحَدٌّ فِي ظَهْرِكَ "} اَلْحَدِيثَ أَخْرَجَهُ أَبُو يَعْلَي، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
وَهُوَ فِي اَلْبُخَارِيِّ نَحْوُهُ مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عَبَّاسٍ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Kulaaniana kwa kwanza katika Uislam ni Hilaal bin Umayyah[4] alipomsingizia mke wake kuzini na Shariyka bin Samhaa,[5] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Leta ushahidi vinginevyo utapigwa mijeledi mgongoni mwako…”[6] mpaka mwisho wa Hadiyth [Imetolewa na Abuu Ya’laa na wapokezi wake ni madhubuti, na katika Al-Bukhaariy kuna Hadiyth kama hii kutoka kwa Ibn ‘Abbaas]
1050.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَامِرٍ بْنِ رَبِيعَةَ قَالَ: {لَقَدْ أَدْرَكَتُ أَبَا بَكْرٍ، وَعُمَرَ، وَعُثْمَانَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمْ، وَمِنْ بَعْدَهُمْ، فَلَمْ أَرَهُمْ يَضْرِبُونَ اَلْمَمْلُوكَ فِي اَلْقَذْفِ إِلَّا أَرْبَعِينَ} رَوَاهُ مَالِكٌ، وَالثَّوْرِيُّ فِي "جَامِعِهِ"
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Aamir bin Rabiy’ah amesema: Nilimkuta Abuu Bakr, ‘Umar na ‘Uthmaan (رضيَ اللهُ عَنْهُمْ) na waliokuja baada yao sikuwaona wakimpiga mtumwa katika adhabu ya kusingizia uzinifu isipokuwa mijeledi arubaini tu.[7] [Imetolewa na Maalik na Ath-Thawriy katika kitabu chake cha Al-Jaami’i]
1051.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مِنْ قَذْفَ مَمْلُوكَهُ يُقَامُ عَلَيْهِ اَلْحَدُّ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، إِلَّا أَنْ يَكُونَ كَمَا قَالَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakaemsingizia (uzinifu) mtumwa wake atasimamishiwa haddi Siku Ya Qiyaamah[8] isipokuwa iwe ni kama alivyosema.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Soma Suwrah An-Nuwr Aayah ya 11 (na zinazofuatia)
إِنَّ الَّذِينَ جَاءُوا بِالْإِفْكِ عُصْبَةٌ مِّنكُمْ ۚ لَا تَحْسَبُوهُ شَرًّا لَّكُم ۖ بَلْ هُوَ خَيْرٌ لَّكُمْ ۚ لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُم مَّا اكْتَسَبَ مِنَ الْإِثْمِ ۚ وَالَّذِي تَوَلَّىٰ كِبْرَهُ مِنْهُمْ لَهُ عَذَابٌ عَظِيمٌ ﴿١١﴾
“Hakika wale walioleta singizo la kashfa; (kumzulia mama wa waumini ‘Aaishah رضي الله عنها) ni kundi miongoni mwenu. Msiichukulie kuwa ni shari kwenu, bali ni khayr kwenu. Kila mtu katika wao atapata yale aliyochuma katika dhambi. Na yule aliyejitwika sehemu yake kubwa miongoni mwao atapata adhabu kuu.”
[2] Mwanamme anayetajwa hapa ni Mistwah bin Uthaathah na Hassan bin Thaabit na mwanamke aliyekuwa akiitwa Hamna bin Jahsh.
[3] Ikiwa mtu kamtuhumu mtu kwa uzinifu na akashindwa kuthibitisha, itabidi alete mashahidi wane, adhabu yake itakuwa mijeledi themanini. Baadhi ya wanafiki walimsingizia Mama ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) kwa uzinifu. Walitangaza na jambo hilo likawaathiri watu wengi na minong’ono ikawa mingi kuhusu jambo hilo. Pindi ‘Aaishah alipokoshwa na Aayah za Allaah, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alitangaza adhabu kali kwa Waumini lakini hakusema chochote kuhusu wanafiki, kwani aliacha adhabu yao wapewe na Allaah. Waumini watatu walioadhibiwa kwa kusingizia huku walikuwa ni Hassan bin Thaabit, Mistwah bin Uthaathah na Hamna bint Jahsh (Radhwiya-Allaahu ‘anhum).
[4] Alikuwa katika Al-Answaar, Aws na Waqifi alikuwa Swahaba mashuhuri. Alisilimu mapema na alikuwa na tabia ya kuyavunja masanamu ya Baniy Waqifu. Alishuhudia vita vya Badr, Uhud na alibeba bendera ya Banu Waqifu katika siku ya Fat-hu Makkah. Alikuwa mmoja kati ya watatu walioshindwa kuhudhuria vita vya Tabuwk ambae altengwa kwa muda wa siku hamsini na baadae walisamehewa na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ)
[5] Alikuwa katika kabila la Balawi waliokuwa na ushirika na Answaar. Hilaal bin Umayyah alimtuhumu kuzini na mke wake. Inasemekana kuwa alishiriki katika vita va Uhud na baba yake. Alikuwa na udugu upande wa mama ni pamoja na Baraa bin Maalik, jina la baba yake ni ‘Abaadah bin Mu’tib na As-Sahma lilikuwa ni jina la mama yake.
[6] Ikiwa mtu atamtuhumu mke wake kuzini ni lazima athibitishe kwa ushahidi, vinginevyo au apate laana ya Allaah kwake kwa kumsingizia mke wake. Vinginevyo ataadhibiwa kwa kusingizia. Akimtaja mtu kama ndio mshirika wake katika jinai ile, anatakiwa atoe ushahidi hadi mwisho wake. Kwa kuwa ni mke wake anaweza kukwepa adhabu ya mijeledi lakini hatokwepa laana ya Allaah kwake (ikiwa atakuwa amemsingizia). Nini hali ya mtu aliyetuhumiwa kuwa mshirika wa jinai hii? Hana uchaguzi isipokuwa: (a) Atoe ushahidi kuunga madai yake, au (b) awe tayari kukabiliana na adhabu ya kusingizia.
[7] Hii inathibitisha kuwa adhabu anayopewa mtumwa mwanamme au mwanamke ni nusu ya adhabu apewayo mtu aliyekuwa huru, na hii ni kwa mujibu wa Jamhuri ya ‘Ulamaa.
[8] Hii ina maana kama mtu atamsingizia mtumwa au kijakazi wake kwa uzinifu hatoadhibiwa hapa duniani.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Al-Huduwd (Adhabu)
بَابُ حَدِّ اَلسَّرِقَةِ
03-Mlango Wa Adhabu Ya Kuiba
1052.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ : {لَا تُقْطَعُ يَدُ سَارِقٍ إِلَّا فِي رُبُعِ دِينَارٍ فَصَاعِدًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ. وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ . وَلَفْظُ اَلْبُخَارِيِّ: "تُقْطَعُ اَلْيَدُ فِي رُبُعِ دِينَارٍ فَصَاعِدًا "
وَفِي رِوَايَةٍ لِأَحْمَدَ "اِقْطَعُوا فِي رُبُعِ دِينَارٍ، وَلَا تَقْطَعُوا فِيمَا هُوَ أَدْنَى مِنْ ذَلِكَ"
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mkono wa mwizi haukatwi ila kwa robo dinari na zaidi.”[1] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Na Matini ya Bukhaariy inasema: “Mkono wa mwizi unakatwa kwa robo dinari na zaidi.”
Na katika riwaayah nyingine ya Ahmad: “Kateni (mkono) katika robo dinari wala msikate chini ya hiyo.”
1053.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا: {أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَطَعَ فِي مِجَنٍ، ثَمَنُهُ ثَلَاثَةُ دَرَاهِمَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikata (mkono) katika (kuiba) ngao thamani yake ni dirhamu tatu.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1054.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَعَنَ اَللَّهُ السَّارِقَ ؛ يَسْرِقُ الْبَيْضَةَ ، فَتُقْطَعُ يَدُهُ ، وَيَسْرِقُ الْحَبْلَ ، فَتُقْطَعُ يَدُهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ أَيْضًا
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah Amlaani mwizi! Anaiba yai mkono wake ukakatwa, na anaiba kamba mkono wake ukakatwa.”[2] [Al-Bukhaariy, Muslim]
1055.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا ؛ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {أَتَشْفَعُ فِي حَدٍ مِنْ حُدُودِ الْلَّهِ ؟ " ثُمَّ قَامَ فَاخْتَطَبَ ، فَقَالَ : " أَيُّهَا النَّاسُ ! إِنَّمَا هَلَكَ الَّذِينَ مِنْ قَبْلِكُمْ أَنَّهُمْ كَانُوا إِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الشَّرِيفُ تَرَكُوهُ ، وَإِذَا سَرَقَ فِيهِمُ الضَّعِيفُ أَقَامُوا عَلَيْهِ الْحَدَّ . . .} الْحَدِيثَ . مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ وَلَهُ مِنْ وَجْهٍ آخَرَ : عَنْ عَائِشَةَ : كَانَتِ امْرَأَةٌ تَسْتَعِيرُ الْمَتَاعَ ، وَتَجْحَدُهُ ، فَأَمَرَ الْنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِقَطْعِ يَدِهَا
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema (kwa Usaamah Bin Zayd): “Unaombea[3] katika haddi (adhabu) miongoni mwa haddi za Allaah? Halafu akasimama kuwakhutubia watu: ‘Enyi watu! Kwa yakini waliangamia waliokuwa kabla yenu, kwani anapoiba mtukufu wao wanamuacha, na akiiba mnyonge wanamsimamishia haddi.”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Naye Muslim amepokea kwa njia nyingine kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا): “Mwanamke alikuwa akiazima vyombo na anakanusha, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamuru akatwe mkono.”
1056.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ ، عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَيْسَ عَلَى خَائِنٍ وَلَا مُنْتَهِبٍ ، وِلَا مُخْتَلِسٍ ، قَطْعٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ ، وَالْأَرْبَعَةُ ، وَصَحَّحَهُ التِّرْمِذِيُّ ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jabair (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kufanya khiyana, mwenye kudokoa na mwenye kunyang’anya, hawakatwi mkono.”[5] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan]
1057.
وَعَنْ رَافِعِ بْنِ خَدِيجٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ ، قَالَ سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {لَا قَطْعَ فِي ثَمَرٍ وَلَا كَثَرٍ} رَوَاهُ اَلْمَذْكُورُونَ، وَصَحَّحَهُ أَيْضًا اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Raafi’ bin Khadiyj (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Hakuna kukata mkono kwa aliyechukua matunda wala joyo la mtende.”[6] [Imetolewa na hao waliotajwa, vile vile At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan wameisahihisha]
1058.
وَعَنْ أَبِي أُمَيَّةَ الْمَخْزُومِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أُتِيَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بِلِصٍّ قَدِ اعْتَرَفَ اعْتِرَافًا، وَلَمْ يُوجَدْ مَعَهُ مَتَاعٌ، فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "مَا إِخَالَكَ سَرَقْتَ". قَالَ: بَلَى، فَأَعَادَ عَلَيْهِ مَرَّتَيْنِ أَوْ ثَلَاثًا، فَأَمَرَ بِهِ فَقُطِعَ. وَجِيءَ بِهِ، فَقَالَ: "اسْتَغْفِرِ اللَّهَ وَتُبْ إِلَيْهِ"، فَقَالَ: أَسْتَغْفِرُ اللَّهَ وَأَتُوبُ إِلَيْهِ، فَقَالَ: "اللَّهُمَّ تُبْ عَلَيْهِ" ثَلَاثًا} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَأَحْمَدُ، وَالنَّسَائِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
وَأَخْرَجَهُ الْحَاكِمُ مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ، فَسَاقَهُ بِمَعْنَاهُ، وَقَالَ فِيهِ: {اذْهَبُوا بِهِ، فَاقْطَعُوهُ، ثُمَّ احْسِمُوهُ}. وَأَخْرَجَهُ الْبَزَّارُ أَيْضًا، وَقَالَ: لَا بَأْسَ بِإِسْنَادِهِ
Kutoka kwa Abiy Umayyah Al-Makhzuwmiy[7] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliletewa mwizi aliyeungama kuwa aliiba lakini hakuwa na alichoiba, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: ‘Sidhani kama umeiba’ yule mtu akasema: ‘Nimeiba,[8] akarudia kusema hivyo mara mbili au mara tatu. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamrisha akatwe mkono kisha akaletwa, akamuambia: ‘Omba msamaha kwa Allaah na utubie Kwake’ yule mtu akasema: ‘Naomba msamaha kwa Allaah na natubia Kwake’ Rasuli wa Allaah akasema: ‘Ee Allaah! Mkubalie tawbah yake’ alisema hivyo mara tatu.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na matini ya hadiyth ni yake, vile vile imepokewa na Ahmad na An-Nasaaiy na wapokezi wake ni madhubuti]
Pia Al-Haakim ameipokea kutoka katika hadiyth ya Abuu Hurayrah akayieleza ki maana, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaambia: “Mchukueni mumkate kisha mumpisheni.” Vile vile Al-Bazzaar ameipokea na amesema: Isnaad yake haina ubaya.
1059.
وَعَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ بْنِ عَوْفٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ؛ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَغْرَمُ السَّارِقُ إِذَا أُقِيمَ عَلَيْهِ الْحَدُّ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَبَيَّنَ أَنَّهُ مُنْقَطِعٌ. وَقَالَ أَبُو حَاتِمٍ: هُوَ مُنْكَرٌ
Kutoka kwa ‘Abd Ar-Rahmaan bin ‘Awf (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwizi harudishi alichokiiba atakaposimamishiwa[9] haddi.” [Imetolewa na An-Nasaaiy na ameeleza kuwa Hadiyth hii ni Munqatwi’. Na amesema Abuu Haatim: “Hadiyth hii ni Munkar.”]
1060.
وَعَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ رَسُولِ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ ؛ {أَنَّهُ سُئِلَ عَنِ التَّمْرِ الْمُعَلَّقِ؟ فَقَالَ: "مَنْ أَصَابَ بِفِيهِ مِنْ ذِي حَاجَةٍ، غَيْرَ مُتَّخِذٍ خُبْنَةً، فَلَا شَيْءَ عَلَيْهِ، وَمَنْ خَرَجَ بِشَيْءٍ مِنْهُ، فَعَلَيْهِ الْغَرَامَةُ وَالْعُقُوبَةُ، وَمَنْ خَرَجَ بِشَيْءٍ مِنْهُ بَعْدَ أَنْ يُؤْوِيَهُ الْجَرِينُ، فَبَلَغَ ثَمَنَ الْمِجَنِّ فَعَلَيْهِ الْقَطْعُ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ الْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr bin Al-‘Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliulizwa kuhusu tende zilizotundikwa, akasema: “Mwenye haja akila kiasi cha haja bila ya kuchukua hana lawama. Na mwenye kutoka na kitu basi atapata kulipa na kuadhibiwa. Na mwenye kuchukua sehemu (katika hiyo tende) baada ya kuingizwa sehemu inayokaushiwa na ikafikia thamani ya tende zinazotiwa sehemu hiyo, basi atakatwa (mkono).” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Al-Haakim]
1061.
وَعَنْ صَفْوَانَ بْنِ أُمِّيَّةٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ لَهُ لَمَّا أَمَرَ بِقَطْعِ اَلَّذِي سَرَقَ رِدَاءَهُ، فَشَفَعَ فِيهِ: {هَلَّا كَانَ ذَلِكَ قَبْلِ أَنْ تَأْتِيَنِي بِهِ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةَ. وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْجَارُودِ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Swafwaan bin Ummiyyah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipoamrisha kukatwa mkono wa aliyeiba shuka yake (Safwaan). Safwaan alimuombea yule mwizi asikatwe. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: ‘Ungalifanya hivyo kabla ya kumleta kwangu).” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Ibn Al-Jaaruwd na Al-Haakim]
1062.
وَعَنْ جَابِرٍ قَالَ: جِيءَ بِسَارِقٍ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: {"اُقْتُلُوهُ". فَقَالُوا يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّمَا سَرَقَ. قَالَ: "اِقْطَعُوهُ" فَقَطَعَ، ثُمَّ جِيءَ بِهِ اَلثَّانِيَةِ، فَقَالَ "اُقْتُلُوهُ" فَذَكَرَ مِثْلَهُ، ثُمَّ جِيءَ بِهِ اَلرَّابِعَةِ كَذَلِكَ، ثُمَّ جِيءَ بِهِ اَلْخَامِسَةِ فَقَالَ: "اُقْتُلُوهُ"} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنِّسَائِيُّ، وَاسْتَنْكَرَهُ
وَأَخْرُجَ مِنْ حَدِيثِ اَلْحَارِثِ بْنِ حَاطِبٍ نَحْوَهُ. وَذَكَرَ اَلشَّافِعِيُّ أَنَّ اَلْقَتْلَ فِي اَلْخَامِسَةِ مَنْسُوخٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliletewa mwizi akasema: ‘Muuweni’. Maswahaba wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Ameiba. Akasema: ‘Mkateni (mkono)’ akakatwa mkono, kisha akaletwa mara ya pili akasema: ‘Muuweni’. Akataja mfano wake. Kisha akaletwa mara ya tatu. Akaeleza kama alivyotangulia. Kisha akaletwa mara ya nne. Akataja mfano wake. Alipoletwa mara ya tano, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: ‘Muuweni’.”[10] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na amesema ni Munkar]
An-Nasaaiy alipokea mfano wake kutoka kwa Al-Haarith bin Haatwib.[11] Ash-Shaafi’iy amesema kuwa kuuwawa kwa mara ya tano kumefutwa (mansuwkh)
[1] Kuna rai tofauti miongoni mwa ‘Ulamaa kuhusu kiasi cha thamani ya kitu kilichoibiwa ili mkono wa mwizi ukatwe. Tukisoma Ahaadiyth mbali mbali na maelezo ya ‘Ulamaa mbali mbali kinathibitisha kuwa wizi wa bidhaa zenye thamani chini ya moja ya nne ya dinari (ambayo ni sawa na dirhamu 3 wakati wa Maswahaba wa Nabiy) haihalalishi mkono wa mwizi ule kukatwa. Robo dinari ni chini ya gramu moja na nusu ya dhahabu.
[2] Hadiyth ikamalizikia: “Ikateremka Aayah:
إِنَّ الَّذِينَ يَشْتَرُونَ بِعَهْدِ اللَّـهِ وَأَيْمَانِهِمْ ثَمَنًا قَلِيلًا أُولَـٰئِكَ لَا خَلَاقَ لَهُمْ فِي الْآخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّـهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيْهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٧٧﴾
“Hakika wale wanaobadilisha ahadi ya Allaah na viapo vyao kwa thamani ndogo; hao hawana sehemu yoyote katika Aakhirah na wala Allaah Hatowasemesha na wala Hatowatazama Siku Ya Qiyaamah na wala Hatowatakasa na watapata adhabu iumizayo” [Aal-‘Imraan: 77]
[3] Tukio hili lilitokea kwa bibi mmoja aitwae Faatwimah bint Aswad Makhzuwmiyah, ambae ni mwanamama kutoka katika familia kubwa inayoheshimika aliyeiba. Ilipotajwa hukumu ya kumkata mkono, watu wakaanza kutafuta wa kumuombea msamaha. Usaamah alionekana wa kutumika kumuombea. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alitoa khutbah kali ambayo baadhi yake ipo katika hadiyth hii. Kishariy’ah mtu aliyeibiwa ana haki ya kumsamehe mwizi wake kabla ya jambo lile kupelekwa mahakamani. Hata hivyo kesi ikishapelekwa mahakamani hakuna njia ya kumsamehe tena mhusika. Mkono wake ni lazima ukatwe, na kumuombea kwa wakati huu haina maana kwani hairuhusiwi.
[4] Yaani wote watakuwa ni wamiliki wa mnyama huyo.
[5] Wizi wa kutumia silaha, ubadhirifu wa mali na udanganyifu haviingii katika adhabu ya kukata mkono. Udanganyifu unakusudia mtu aliyepatiwa amana kwa kuilinda anaitumia na kuondoka na mali ile huku akionesha sura nyingine. Ama wizi kwa njia ya ujambazi ni kuchukua mali ya mtu kwa nguvu na kwa uwazi kabisa. Ubadhirifu ni kutumia mali ya mtu mwingine vibaya kwa kutokuwepo kwake. Hata hivyo, ikiwa mtu ataazima kitu kwa mtu na mwisho akakana kuwa hajaazima, mtu huyu atachukuliwa kama ni mwizi na atakatwa mkono.
[6] Kuiba matunda hailazimishi mtu kukatwa mkono maadamu katika shamba lile hakukuwa na ukuta uliyozungushiwa. Likiwa shamba au bustani lenyewe lina ukuta uliozungushwa basi atawajibika na adhabu ile. Hivyo, msafiri ambae ameshaanza kupewa chakula na watu wa mji anaruhusiwa kula katika bustani iliyo na matunda pembezoni mwa ukuta.
[7] Ni Swahaba kutoka Al-Hijaaz ambae amepokea Hadiyth moja tu. Hammaad bin Salamah anamuelezea: “Alikuwa ni katika ukoo wa Al-Makhzuwm” wakati wa Humam bin Yahya amesema: ‘Alikuwa ni Answaar’
[8] Hadiyth hii inaelezea mambo mawili yaliyozingatiwa katika kutoa hukumu ya adhabu ya mwizi. Kwanza mali ya wizi ikombolewe kutoka kwake, au mwenyewe kukiri kuhusu hilo, siyo lazima kukiri mara mbili, mara moja inatosha kumuingiza hatiani na hukumu kutekelezwa kwake. Kuna tofauti ya rai ikiwa ushahidi unahitajika katika suala la wizi unapotokea. Kwa maneno mengine ni kuwa ikiwa mtuhumiwa hajakiri kuiba na hakuna kidhibiti kilichopatikana kwake na mashahidi wakapatikana kuwa ndie aliyeiba. Hukumu ya kesi kama hiyo siyo katika makubaliano ya ‘Ulamaa. Baada ya mkono kukatwa mafuta ya moto humwagwa ili kuzuia kutoka kwa damu. Ikiwa katika hali kama hii damu ikaendelea kumiminika na mtu akafa, kwa ajili hiyo ni jukumu la Hazina ya dola (Baytul-Maal) kulipa fidia kwa warithi wa aliyefariki.
[9] Ikiwa vitu vilivyoibwa vitapatikana kwa mwizi, vitarejeshwa kwa mwenyewe na mkono wa mwizi utakatwa kwa makubaliano ya ‘Ulamaa. Katika hali ya vitu vilivyoibwa kuharibika, hapa kuna tofauti ya rai kwa ‘Ulamaa kama alipe faini au laa.
[10] ‘Ulamaa wengi wanaona kuwa njia iliyoelezwa ya kumkata mwizi mkono na mguu ni kuwa kwa mara ya kwanza akiiba atakatwa kiganja cha mkono wa kuume. Kwa mara ya pili atakatwa fundo la mguu wa kushoto, mara ya tatu kiganja cha mkono wa kushoto na mara ya nne ni kifundo cha mguu wa kushoto.
[11] Huyu alikuwa Jumahi, Mqurayshi aliyezaliwa Ethiopia. Alikuwa gavana wa Makkah mwaka wa 66 Hijriyyah wakati wa ‘Abdullaah bin Az-Zubayr. Alimtumikia kwa muda wa miaka 6 na baada ya hapo akawa msimamizi wa Al-Masai wakati wa Marwaan alipokuwa gavana wa Madiynah wakati wa Mu’aawiyah.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Haddi (Adhabu)
بَابُ حَدِّ اَلشَّارِبِ وَبَيَانِ اَلْمُسْكِرِ
04-Mlango Wa Adhabu Ya Mnywaji Pombe Na Kubainisha Kileo (Ni Nini)
1063.
عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَتَى بِرَجُلٍ قَدْ شَرِبَ اَلْخَمْرَ، فَجَلَدَهُ بِجَرِيدَتَيْنِ نَحْوَ أَرْبَعِينَ. قَالَ: وَفَعَلَهُ أَبُو بَكْرٍ، فَلَمَّا كَانَ عُمَرُ اِسْتَشَارَ اَلنَّاسَ، فَقَالَ عَبْدُ اَلرَّحْمَنِ بْنُ عَوْفٍ: أَخَفَّ اَلْحُدُودِ ثَمَانُونَ، فَأَمَرَ بِهِ عُمَرُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: عَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ فِي قِصَّةِ اَلْوَلِيدِ بْنِ عَقَبَةَ {جَلَدَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَرْبَعِينَ، وَأَبُو بَكْرٍ أَرْبَعِينَ، وَعُمَرُ ثَمَانِينَ، وَكُلٌّ سُنَّةٌ، وَهَذَا أَحَبُّ إِلَيَّ}
وَفِي هَذَا اَلْحَدِيثِ: {أَنَّ رَجُلًا شَهِدَ عَلَيْهِ أَنَّهُ رَآهُ يَتَقَيَّأْ اَلْخَمْرَ، فَقَالَ عُثْمَانُ: إِنَّهُ لَمْ يَتَقَيَّأْهَا حَتَّى شَرِبَهَا}
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Mtu mmoja aliletwa kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akiwa amekunywa khamr[1] (pombe), akamtandika kwa matawi mawili ya mtende mara arubaini hivi. Na Abuu Bakr naye alifanya hivyo. Ulipokuwa wakati wa ‘Umar aliwashauri watu. ‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf amesema: ‘Adhabu hafifu zaidi ni mijeledi themanini.’ ‘Umar akaamuru iwe hivyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Katika Riwaayah ya Muslim kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) katika kisa cha Al-Waliyd bin ‘Uqbah[2]: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipiga mijeledi arubaini, Abuu Bakr alipiga mijeledi arubaini, ‘Umar alipiga mijeledi thamanini. Yote hayo ni Sunnah na hii yapendeza mno kwangu.”
Na katika hadiyth hii: “Mtu mmoja alimshuhudia (Al-Waliyd) akitapika pombe. ‘Uthmaan akasema: ‘Yeye hakutapika pombe ila baada ya kuwa amekunywa.’
1064.
وَعَنْ مُعَاوِيَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنَّهُ قَالَ فِي شَارِبِ اَلْخَمْرِ: {إِذَا شَرِبَ فَاجْلِدُوهُ، ثُمَّ إِذَا شَرِبَ اَلثَّانِيَةِ فَاجْلِدُوهُ، ثُمَّ إِذَا شَرِبَ اَلثَّالِثَةِ فَاجْلِدُوهُ، ثُمَّ إِذَا شَرِبَ اَلرَّابِعَةِ فَاضْرِبُوا عُنُقَهُ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ وَهَذَا لَفْظُهُ، وَالْأَرْبَعَةُ
وَذَكَرَ اَلتِّرْمِذِيُّ مَا يَدُلُّ عَلَى أَنَّهُ مَنْسُوخٌ، وَأَخْرَجَ ذَلِكَ أَبُو دَاوُدَ صَرِيحًا عَنْ اَلزُّهْرِيِّ
Kutoka kwa Mu’aawiyah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alisema kuhusu mnywaji pombe: “Atakapokunywa (mara ya kwanza) mtandikeni, kisha atakapokunywa mara ya pili mtandikeni, kisha atapokunywa mara ya tatu mtandikeni, kisha atakapokunywa mara ya nne mkateni shingo yake.” [Imetolewa na Ahmad, matini hii ni ya Maimaam wane (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah). At-Tirmidhiy amesema kuwa ni mansuwkh.[3] Abuu Daawuwd pia amepokea kwa uwazi kutoka kwa Az-Zuhriyy]
1065.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {" إِذَا ضَرَبَ أَحَدُكُمْ فَلْيَتَّقِ اَلْوَجْهَ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakapopiga mmoja wenu aepuke kupiga uso.”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim]
1066.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {" لَا تُقَامُ اَلْحُدُودُ فِي اَلْمَسَاجِدِ"} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِم
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haddi (adhabu) hazitekelezwi ndani ya Msikiti.”[5] [Imetolewa na At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
1067.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {لَقَدْ أَنْزَلَ اَللَّهُ تَحْرِيمَ اَلْخَمْرِ، وَمَا بِالْمَدِينَةِ شَرَابٌ يَشْرَبُ إِلَّا مِنْ تَمْرٍ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Allaah Ameteremsha kuharamisha pombe na Madiynah hakuna pombe inayonywewa ila pombe ya tende.” [Imetolewa na Muslim]
1068.
وَعَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {نَزَلَ تَحْرِيمُ اَلْخَمْرِ، وَهِيَ مِنْ خَمْسَةِ: مِنْ اَلْعِنَبِ، وَالتَّمْرِ، وَالْعَسَلِ، وَالْحِنْطَةِ، وَالشَّعِيرِ. وَالْخَمْرُ: مَا خَامَرَ اَلْعَقْلَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Imeteremka amri ya kuharamisha pombe, inayotokana na vitu vitano: Zabibu, tende, asali, ngano na shayiri.[6] Pombe ni kila kinachofunika akili.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
1069.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {" كُلُّ مُسْكِرٍ خَمْرٌ، وَكُلُّ مُسْكِرٍ حَرَامٌ"} أَخْرَجَهُ مُسْلِمُ.
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kila kileo ni pombe na kila kileo ni haraam.” [Imetolewa na Muslim]
1070.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {" مَا أَسْكَرَ كَثِيرُهُ، فَقَلِيلُهُ حَرَامٌ"} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Chochote kinacholewesha kwa wingi, uchache wake[7] ni haraam.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1071.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يُنْبَذُ لَهُ اَلزَّبِيبُ فِي اَلسِّقَاءِ، فَيَشْرَبُهُ يَوْمَهُ، وَالْغَدَ، وَبَعْدَ اَلْغَدِ، فَإِذَا كَانَ مَسَاءُ اَلثَّالِثَةِ شَرِبَهُ وَسَقَاهُ، فَإِنْ فَضَلَ شَيْءٌ أَهْرَاقَهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akitengenezewa kinywaji cha (kurowekwa) zabibu na akitiliwa katika chombo akinywa siku ile, siku inayofwatia na siku baada yake. Inapofika jioni ya siku ya tatu alikuwa akinywa na akimpa mtu mwingine anywe kinapobakia kitu anamwaga.”[8] [Imetolewa na Muslim]
1072.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {" إِنَّ اَللَّهَ لَمْ يَجْعَلْ شِفَاءَكُمْ فِيمَا حَرَّمَ عَلَيْكُمْ"} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika Allaah Hakujaalia ponyo lenu katika Alivyoharamisha.”[9] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1073.
وَعَنْ وَائِلٍ اَلْحَضْرَمِيِّ، أَنَّ طَارِقَ بْنَ سُوَيْدٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {سَأَلَ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ اَلْخَمْرِ يَصْنَعُهَا لِلدَّوَاءِ ؟ فَقَالَ: " إِنَّهَا لَيْسَتْ بِدَوَاءٍ، وَلَكِنَّهَا دَاءٌ"} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ. وَأَبُو دَاوُدَ وَغَيْرُهُمَ
Kutoka kwa Waa-il Al-Hadhwramiyy amesema kuwa Twaariqa bin Suwayd[10] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا): Alimuuliza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu pombe inayotengenezwa kwa ajili ya dawa? Akasema: “Hiyo (pombe) sio dawa lakini ni ugonjwa.” [Imetolewa na Muslim na Abuu Daawuwd na wengineo]
[1] Khamr kwa Kiarabu maana yake ni kuficha, kufinika. Mtu anapolewa kile kilevi hufunika akili yake na hii ndio maana ya Khamr. Katika istwilaah ya Shariy’ah kila kilevi ni haraam. Na kila kinachopelekea katika kilevi ni haraam. Kuna makubaliano ya ‘Ulamaa kwa athari ya kilevi na adhabu ya mtu anayopewa. Hata hivyo, kuna rai tofauti kwa mnywaji pombe. Wakati wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na Abuu Bakr, adhabu kwa mnywaji pombe ilikuwa ni mijeledi arubaini. ‘Umar aliongeza kufikia themanini na ndio uliyokuwa msimamo uliokuja chukuliwa. Kwa hivyo basi baadhi ya Maimaam wametoa hukumu zao adhabu ya mijeledi themanini. Kwa kuwa adhabu ya mijeledi themanini haikuwepo wakati wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), baadhi ya ‘Ulamaa wanaona kuwa adhabu ni mijeledi arubaini tu. Nukta nyingine ya tafaruku baina ya ‘Ulamaa kulingana na adhabu ni je, suala la adhabu ni lazima kutumia mijeledi au kopo au kiatu kinatosheleza. Kulingana na muono wa ‘Ulamaa wengi, ni sawa kutumia chombo chochote (mjeledi, kiatu, kopo na kadhalika) wakati wa kumuadhibu mtu mwenyewe.
[2] Al-Waliyd bin ‘Uqbah bin Abiy Mu’ait Al-Qurayshiy alikuwa ni ndugu wa ‘Uthmaan bin ‘Affaan upande wa mama. Alisilimu siku ya Fat-h Makkah. Alikuwa miongoni mwa ma-Quraysh wacheshi, mvumilivu, jasiri na mshairi. ‘Uthmaan alimfanya gavana wa mji wa Kufa nchini ‘Iraaq kisha akamuuzulu kwa tuhuma za kunywa pombe. Alijzuia kuingia katika fitnah baada ya kuuwawa kwa ‘Uthmaan, aliishi Ruqa na alifia huko na kuzikwa kwa maeneo ya Bulaykh.
[3] Imam Shaafi’iy anaripoti makubaliano ya ‘Ulamaa (isipokuwa madhehebu ya Zuhri na Imaam Ibn Hazm) kuwa mnywa pombe kwa hali yoyote hawezi kuuwawa, bila kujali amekunywa mara ngapi. Vivyo hivyo, kila atakapokamatwa akinywa pombe hukumu mpya itatolewa dhidi yake, bila kujali kama aliadhibiwa kabla ya hapo na hukumu hiyo hiyo. Kuna makubaliano ya hukumu hii kwa ‘Ulamaa.
[4] Muda wowote pindi mtu anapopigwa kwa adhabu yoyote iliyotolewa dhidi yake, mtu huyo anayetekeleza hukumu ile asipige usoni kwa yeyote atakayeadhibiwa.
[5] Hii ni kwa sababu Misikiti imesimamishwa kwa lengo maalum la kumuabudu Allaah. Hivyo basi, inatakiwa iwe safi muda wote kwa ajili ya jukumu lile la kumuabudu Allaah. Damu ya mtu aliyeadhibiwa (aliyehukumiwa) haitakiwi kutapakaa maeneo ya Msikiti. Maeneo haya ni matukufu na sehemu ya kusubiri Rahmah za Allaah, wakati adhabu iliyotolewa ni kulipa kisasi cha Allaah.
[6] Lengo la kutaja Hadiyth hii ni kuelezea kuwa sio tu kwamba pombe inayotokana na mzabibu ndio iliyoharamishwa bali zote zinazolewesha ni haraam.
[7] Ina maana chochote kinacholewesha kwa kunywa kwa wingi wake basi ni haraam kukichukuwa kwa uchache wake. Hata kama kichache chake hakilevi.
[8] Huenda kile kilichobaki kikawa kilevi baada ya muda. Kinywaji kile kinapoanza kubadilika ni lazima kimwagwe. Haswa ikiwa ni zaidi ya siku tatu, kinywaji kile kisitumike kikianza kuonekana kimeharibika hata kama ni siku ya pili.
[9] Hii inamaanisha kuwa ni haraam kutumia vitu vilivyoharamishwa, hata kwa ajili ya tiba. Vitu hivi ni kama vile pombe, bangi, madawa ya kulevya na mfano wake.
[10] Huyu ni Swahaba aliyekuwa akijulikana kwa jina la Twaariqa bin Suwayd. Alikuwa mhadharami na inasemekana alikuwa Ju’fi. Ana Hadiyth moja ambayo watu wa mji wa Kufa walikuwa wakipokea kutoka kwake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلْحُدُودِ
Kitabu Cha Haddi (Adhabu)
بَاب اَلتَّعْزِيرِ وَحُكْمِ اَلصَّائِلِ
05-Mlango Wa Ta’ziyr[1] Na Hukumu Ya Mshambuliaji
1074.
عَنْ أَبِي بُرْدَةَ اَلْأَ نْصَارِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {" لَا يُجْلَدُ فَوْقَ عَشَرَةِ أَسْوَاطٍ، إِلَّا فِي حَدِّ مِنْ حُدُودِ اَللَّهِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Burdah[2] Al-Answaariyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alisema kuwa alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Asichapwe mtu zaidi ya mijeledi kumi[3] isipokuwa katika haddi (adhabu) miongoni mwa haddi za Allaah.” [Bukhaariy, Muslim]
1075.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {" أَقِيلُوا ذَوِي اَلْهَيْئَاتِ عَثَرَاتِهِمْ إِلَّا اَلْحُدُودَ"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wasameheni wenye tabia nzuri[4] kuteleza kwao isipokuwa katika haddi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy]
1076.
وَعَنْ عَلِيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {مَا كُنْتُ لِأُقِيمَ عَلَى أَحَدٍ حَدًّا، فَيَمُوتُ، فَأَجِدُ فِي نَفْسِي، إِلَّا شَارِبَ الْخَمْرِ، فَإِنَّهُ لَوْ مَاتَ وَدَيْتُهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Msimamishieni haddi yeyote na akifa nikahuzunika isipokuwa mnywaji pombe, kwani lau atakufa nitamtolea diya.”[5] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1077.
وَعَنْ سَعِيدِ بْنِ زَيْدٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {" مِنْ قُتِلَ دُونَ مَالِهِ فَهُوَ شَهِيدٌ"} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Sa’d bin Zayd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayeuwawa kwa kutetea mali zake huyo ni Shahidi.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
1078.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ خَبَّابٍ قَالَ: سَمِعْتَ أَبِي رَضِيَ اللهُ عَنْهُ يَقُولُ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ: {" تَكُونُ فِتَنٌ، فَكُنْ فِيهَا عَبْدَ اَللَّهِ اَلْمَقْتُولَ، وَلَا تَكُنْ اَلْقَاتِلَ"} أَخْرَجَهُ ابْنُ أَبِي خَيْثَمَةَ. وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ
وَأَخْرَجَ أَحْمَدُ نَحْوَهُ: عَنْ خَالِدِ بْنِ عُرْفُطَةَ
Kutoka kwa ‘Abdillaah[6] bin Khabbaab[7] amesema amemsikia Baba yangu (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) akisema kuwa alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Kutakuwa na fitnah,[8] kuwa mja wa Allaah mwenye kuuwawa wala usiwe mwenye kuua.”[9] [Imetolewa na Abiy Khaythamah na Ad-Daaraqutwniy]
Na Ahmad ameipokea Hadiyth kama hii kutoka kwa Khaalid bin ‘Urfutwah[10]
[1] Kuadhiri na kuadhibu.
[2] Huyu ni Hani bin Niyaar aliyekuwa Swahaba kutoka katika kabila la Balawi. Alikuwa ni mshirika wa Al-Answaar na alishuhudia vita vya Badr na vita vinginevyo. Alifariki mwaka 41, na inasemekana 42 na wengine 45 Hijriyyah.
[3] Hadiyth hii imefahamika na baadhi ya Fuqahaa kuwa ni dalili hawezi mtu kuchapwa zaidi ya mijeledi kumi isipokuwa mtu huyo ameingia katika adhabu ya haddi. Imaam Shaafi’iy na Maalik kuongeza inaruhusiwa ilimradi isifikie kile kiwango cha haddi kilichotajwa. Wengine wanaona kuwa huwezi kuongeza maadamu adhabu imetajwa. Wengine wanaona kuwa inaweza kuongezeka zaidi ya mijeledi kumi ikiwa ni adhabu ya kosa kubwa, wakati makosa madogo huwezi kzidisha zaidi ya mijeledi kumi.
[4] Katika adhabu za haddi zilizoainishwa kulingana na makatazo, adhabu hizo zitawahusu wote bila kubagua, tajiri au masikini, mtu wa kawaida au yule mwenye nafasi kubwa katika jamii. Katika makosa madogo madogo hali inaangaliwa kulingana na muda, aina ya kosa, na mtu aliyehusika na kosa lenyewe.
[5] Hadiyth hii inaonesha pia kuwepo kwa tofauti ya rai baina ya Maswahaba wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ikiwa kumchapa mnywa pombe kwa mijeledi arubaini ilikuwa ni adhabu ya haddi au ilikuwa ni Ta’ziyr (kumuadhibu kwa kumuadhiri). Hilo vile vile lilikuwa ni adhabu ya kumuadhiri mtu mzima kwa sababu adhabu ile haipo katika Qur-aan. Hakuna cha kufanya kwa wale ambao watakufa kwa kutekelezewa adhabu ile kwao. Hata hivyo, ikiwa kama mtu atakufa akipitishiwa hukumu hiyo ya kumwadhiri ni juu ya Dola kutoa fidiya kutoka katika hazina wa warithi wa aliyefariki. Tokea hapo, ikawa kila mnywa pombe atakapoadhibiwa na akafa katika adhabu ile, Fuqahaa wana rai kuwa itolewe fidia walipwe warithi wake.
[6] ‘Abdullaah alikua ni miongoni mwa Taabi’iyna na mkazi wa Madiyna. Hururiya (Khawaarij) walimuuwa katika mwaka wa 27 Hijriyyah baada ya kumuasi ‘Aliy na alikuwa njiani akielekea An-Naharwaan. Baada ya kumuuwa waliingia nyumbani kwake, walimuuwa mjakazi wake na kukatakata kichanga kilichokuwa tumboni mwake. Hili lilipelekea vita maarufu vya An-Naharwaan ambapo ‘Aliy aliwauwa Khawaarij wote isipokuwa tisa miongoni mwao ambao walisababishia fitnah kubwa huko mbele.
[7] Khabbaab bin Al-Arat bin Jandala At-Tamiymi alikuwa mmoja wa Maswahaba walioteswa kwa ajili ya Dini yao. Alishiriki katika vita vya Badr. Alikufa katika mji wa Kufa uliopo ‘Iraaq alipokataa kushiriki katika vita vya Siffin katika mwaka wa 37 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 73.
[8] Fitnah ni mitihani mbalimbali ni ule mtafaruku uliokuwa ukitokea katika Ummah na katika Dini.
[9] Imetajwa katika Hadiyth iliyotangulia kuwa mwenye kufa akitetea nafsi yake, mali na familia yake atakuwa amekufa Shahidi. Akimuua adui kwa njia ya kujilinda hatopata dhambi kwa mauaji yale. Hukumu hii hutekelezwa ikiwa hali ipo kwa uwazi na sababu zimefahamika. Ikiwa jambo halipo wazi na kuna ukinzani na ugomvi hatakiwi mtu kunyanyua mkono wake kuuwa. Njia nzuri kwa mtu za kuwa salama ni kuacha kuuwa, kwa kuwa muuwaji hukabiliwa na adhabu ya moto, ama aliyeuliwa huingia Jannah. Ikiwa wote watapigana na kila mmoja kupupia kumuuwa mwenzake wote watakabiliwa na adhabu ya moto atakapo Allaah.
[10] Huyu ni Swahaba kabila lake ni Quda katika koo za ‘Udhr. Alikuwa ni mwakilishi wa Sa’d bin Abiy Waqqaas katika mji wa Kufa. Alifariki mwaka 61 Hijriyyah na inasemekana kuwa Al-Mukhtar bin Abuu ‘Ubayd alimuuwa baada ya kifo cha Yaziyd mwaka 64 Hijriyyah.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10042&title=10-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%20%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D8%AD%D9%8F%D8%AF%D9%8F%D9%88%D8%AF%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10043&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%3A%20Mlango%20Wa%20Adhabu%20Ya%20Uzinifu
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10044&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%3A%20Mlango%20Wa%20Adhabu%20Ya%20Kusingizia
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10050&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%3A%20Mlango%20Wa%20Adhabu%20Ya%20Kuiba
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10135&title=04-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%3A%20Mlango%20Wa%20Adhabu%20Ya%20Mnywaji%20Pombe%20Na%20Kubainisha%20Kileo%20%28Ni%20Nini%29
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10161&title=05-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Al-Huduwd%20%28Adhabu%29%3A%20Mlango%20Wa%20Ta%E2%80%99ziyr%20%20Na%20Hukumu%20Ya%20Mshambuliaji