كِتَاب اَلْقَضَاءِ
Kitabu Cha Kuhukumu
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْقَضَاءِ
00-Kitabu Cha Kuhukumu
1188.
عَنْ بُرَيْدَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"اَلْقُضَاةُ ثَلَاثَةٌ: اِثْنَانِ فِي اَلنَّارِ، وَوَاحِدٌ فِي اَلْجَنَّةِ. رَجُلٌ عَرَفَ اَلْحَقَّ، فَقَضَى بِهِ، فَهُوَ فِي اَلْجَنَّةِ. وَرَجُلٌ عَرَفَ اَلْحَقَّ، فَلَمْ يَقْضِ بِهِ، وَجَارَ فِي اَلْحُكْمِ، فَهُوَ فِي اَلنَّارِ. وَرَجُلٌ لَمْ يَعْرِفِ اَلْحَقَّ، فَقَضَى لِلنَّاسِ عَلَى جَهْلٍ، فَهُوَ فِي اَلنَّارِ"} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Buraydah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Maqaadhwi ni watatu, wawili[1] ni wa motoni na mmoja ni wa katika Jannah. (Wa kwanza) Ni mtu amejua haki akahukumu kwayo; huyo ni wa katika Jannah. (Wa pili) ni mtu amejua haki wala hakuhukumu kwayo, na akafanya jeuri katika hukumu, huyo ni wa motoni. (Wa tatu) ni mtu ambaye hakujuwa haki, akahukumu watu kwa ujinga, huyo ni wa motoni.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Al-Haakim]
1189.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم : {"مَنْ وَلِيَ اَلْقَضَاءَ فَقَدْ ذُبِحَ بِغَيْرِ سِكِّينٍ"} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutawalia ukadhi, kwa hakika amechinjwa bila ya kisu.”[2] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]
1190.
وَعَنْهُ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"إِنَّكُمْ سَتَحْرِصُونَ عَلَى اَلْإِمَارَةِ، وَسَتَكُونُ نَدَامَةً يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، فَنِعْمَ اَلْمُرْضِعَةُ، وَبِئْسَتِ اَلْفَاطِمَةُ"} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika nyinyi mtapupia uongozi, na utakuwa majuto siku ya Qiyaamah. Ni neema iliyoje (kwa mnyonyeshaji (duniani)! Na ubaya ulioje wa muachishaji (kunyonya).”[3] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1191.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ رضى الله عنه أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {"إِذَا حَكَمَ اَلْحَاكِمُ، فَاجْتَهَدَ، ثُمَّ أَصَابَ، فَلَهُ أَجْرَانِ. وَإِذَا حَكَمَ، فَاجْتَهَدَ، ثُمَّ أَخْطَأَ، فَلَهُ أَجْرٌ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Amr bin Al-‘Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Hakimu akihukumu akajitahidi akapatia, ana (malipo mawili), na akihukumu akajitahidi akakosea, ana ujira mmoja.” [Bukhaariy, Muslim]
1192.
وَعَنْ أَبِي بَكْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {" لَا يَحْكُمُ أَحَدٌ بَيْنَ اِثْنَيْنِ، وَهُوَ غَضْبَانُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Asihukumu yoyote baina ya wawili huku ameghadhibika.”[4] [Bukhaariy, Muslim]
1193.
وَعَنْ عَلِيٍّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {" إِذَا تَقَاضَى إِلَيْكَ رَجُلَانِ، فَلَا تَقْضِ لِلْأَوَّلِ، حَتَّى تَسْمَعَ كَلَامَ اَلْآخَرِ، فَسَوْفَ تَدْرِي كَيْفَ تَقْضِي" . قَالَ عَلِيٌّ: فَمَا زِلْتُ قَاضِيًا بَعْدُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحَسَّنَهُ، وَقَوَّاهُ اِبْنُ اَلْمَدِينِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
وَلَهُ شَاهِدٌ عِنْدَ اَلْحَاكِمِ: مِنْ حَدِيثِ اِبْنِ عَبَّاسٍ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Watu wawili wakishtakiana kwako, usimhukumu wa kwanza mpaka usikie maneno ya mwingine[5] pengine ndio utajua utakavyo hukumu. ‘Aliy akasema ‘baada ya mafundisho haya nikawa nahukumu hivyo.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy ameifanya ni Hasan na akaipa nguvu Ibn Al-Madaniyy. Na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
Na ina ushahidi kwa Al-Haakim kutoka katika Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas
1194.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم: {" إِنَّكُمْ تَخْتَصِمُونَ إِلَيَّ، وَلَعَلَّ بَعْضَكُمْ أَنْ يَكُونَ أَلْحَنَ بِحُجَّتِهِ مِنْ بَعْضٍ، فَأَقْضِيَ لَهُ عَلَى نَحْوٍ مِمَّا أَسْمَعُ، مِنْهُ فَمَنْ قَطَعْتُ لَهُ مِنْ حَقِّ أَخِيهِ شَيْئًا، فَإِنَّمَا أَقْطَعُ لَهُ قِطْعَةً مِنَ اَلنَّارِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika nyinyi mnakuja kwangu kushtakiana na huenda mmoja wenu akawa fasaha zaidi katika hoja yake kuliko mwingine, hivyo nikamhukumu yeye kulingana na nilivyosikia. Basi nitakayemkatia chochote katika haki ya nduguye hakika ninamkatia kipande cha moto.”[6] [Bukhaariy, Muslim]
1195.
وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه قَالَ: سَمِعْتُ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {" كَيْفَ تُقَدَّسُ أُمَّةٌ، لَا يُؤْخَذُ مِنْ شَدِيدِهِمْ لِضَعِيفِهِمْ ؟"} رَوَاهُ اِبْنُ حِبَّانَ
وَلَهُ شَاهِدٌ: مِنْ حَدِيثِ بُرَيْدَةَ، عِنْدَ اَلْبَزَّارِ
وَآخَرُ: مِنْ حَدِيثِ أَبِي سَعِيدٍ عِنْدَ اِبْنِ مَاجَه
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema nimemsikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Vipi ummah utasafishwa ilhali haki ya mnyonge haichukuliwi kutoka kwa mwenye nguvu?”[7] [Imetolewa na Ibn Hibbaan]
Na ina ushahidi kutoka katika Hadiyth ya Buraydah kwa Al-Bazzaar.
Na ina ushahidi mwingine kutoka katika Hadiyth ya Abuu Sa’iyd kwa Ibn Maajah.
1196.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {" يُدْعَى بِالْقَاضِي اَلْعَادِلِ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، فَيَلْقَى مِنْ شِدَّةِ اَلْحِسَابِ مَا يَتَمَنَّى أَنَّهُ لَمْ يَقْضِ بَيْنَ اِثْنَيْنِ فِي عُمْرِهِ"} رَوَاهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَأَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ، وَلَفْظُهُ: { فِي تَمْرَةٍ }
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Siku ya Qiyaamah ataitwa Qadhwi muadilifu, kutokana na ugumu wa hesabu atatamani kuwa asingehukumu baina ya watu wawili katika umri wake.” [Imetolewa na Ibn Hibbaan,na Al-Bayhaqiyy ameitaja kwa tamko: ‘hata kama ni tende’]
1197.
وَعَنْ أَبِي بَكْرَةَ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"لَنْ يُفْلِحَ قَوْمٌ وَلَّوْا أَمْرَهُمْ اِمْرَأَةً"} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Watu hawatafaulu watakapomtawalisha mwanamke jambo lao.”[8] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1198.
وَعَنْ أَبِي مَرْيَمَ اَلْأَزْدِيِّ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم أَنَّهُ {قَالَ: "مَنْ وَلَّاهُ اَللَّهُ شَيْئًا مِنْ أَمْرِ اَلْمُسْلِمِينَ، فَاحْتَجَبَ عَنْ حَاجَتِهِمْ وَفَقِيرِهِم، اِحْتَجَبَ اَللَّهُ دُونَ حَاجَتِهِ"} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Abuu Maryam Al-Azdiyy[9] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuwa: “Ambaye Allaah Atamtawalisha katika chochote cha Waislaam, akajificha dhidi ya haja zao na mafukara wao, Allaah Atajitenga naye katika haja zake.”[10] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
1199.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: {لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم اَلرَّاشِيَ وَالْمُرْتَشِيَ فِي اَلْحُكْمِ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
وَلَهُ شَاهِدٌ: مِنْ حَدِيثِ عَبْدِ اَللَّهِ بنِ عَمْرٍو. عِنْدَ اَلْأَرْبَعَةِ إِلَّا النَّسَائِيَّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amemlaani[11] mtoa rushwa na mchukua rushwa katika hukumu.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na At-Tirmidhiy amesema ni Hasan. Na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
Na ina ushahidi wa Hadiyth ya Abdullaah bin ‘Amr kwa Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy.
1200.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بنِ اَلزُّبَيْرِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {قَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنَّ اَلْخَصْمَيْنِ يَقْعُدَانِ بَيْنَ يَدَيِ اَلْحَاكِمِ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Az-Zubayr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amehukumu kuwa watesi wawili wanakaa[12] mbele ya hakimu.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Al-Haakim]
[1] Hadiyth hii inaelezea nukta mbili: Nukta ya kwanza, mtu ambaye hajui ukweli. Na mtu mwingine, ambaye hatekelezi ukweli ule pamoja na kuujua, mtu huyu ataadhibiwa. Hii ina maana kuwa elimu isiyokuwa na utekelezaji haina maana. Pili, kuna uwezekano wa kukosea katika kutoa hukumu. Kama isingekuwa hivyo basi watu wasingegawanyika katika hali ile na kila mmoja kujiona yuko sawa.
[2] Kwa kusoma Hadiyth hii adhabu na ukali ulio dhidi ya Qadhwi anayekwenda kinyume na maamrisho. Kila anayepewa nafasi ya Qadhwi ameiweka nafsi yake katika kichinjo. Ikiwa Qadhwi ni mwenye taqwa ni juu yake kutafuta hukumu yenye uadilifu zaidi. Vinginevyo anatarajiwa kupata hukumu kali mbele ya Allaah huko Aakhirah. Hadiyth nyingine inaelezea kuwa Qadhwi mwenye taqwa ataitwa na kuulizwa maswali katika Siku ya Hukmu, kiasi cha yule Qadhwi kusema: ‘Wa-Allaahi ni bora ningehukumu walau kati ya watu wawili’. Ikiwa Qadhwi huyo atakuwa ni dhalimu, mla rushwa, mara noja atatupwa motoni.
[3] Hii ina maana kuwa utawala huo unawaridhia watawala wengi hapa duniani. Hata hivyo, anapokufa anaachishwa, anakosa raha zile na anasubiri hukumu yake. Ubaya ndio mwisho wake kwa aliyeshindwa kutekeleza majukumu yake.
[4] Qadhwi au jaji asitoe hukumu yake akiwa ameghadhibika, au mfano wa hali kama hizo; kusikia kiu, njaa, ugonjwa, wasiwasi, kusikia usingizi na mfano wa hayo. Akifanya hivyo huenda akatoa hukumu isiyo adilifu. Jambo hili ni katazo la uharaam katika istwilahi ya kishariy’ah. Ikiwa Qadhwi ametoa hukumu katika hali ya ghadhabu hukumu hiyo itakuwa na utata wa kuzingatiwa uhalaal wake.
[5] Hadiyth hii inatahadharisha kutoa hukumu kwa kumsikiliza mlalamikaji pekee kuwa si sahihi, ila atakapopewa anayelalamikiwa nafasi ya kujitetea. Katika kesi ambayo mlalamikiwa amekaa kimya, anakataa kujibu maswali au hajibu, kujieleza na hajali chochote na haji kusikiliza kesi yake hapo ni ruhusa kwa Qadhwi, hakimu au jaji kutoa hukumu ya kesi ile.
[6] Hadiyth hii inabainishia nukta muhimu zifuatazo: ikiwa Qadhwi atatoa hukumu kinyume na hukumu yenyewe basi Allaah Ataiandika kuwa ni hukumu batili na hukumu sahihi Allaah Ataitoa siku ya Hukmu (Aakhirah). Pili, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hakuwa na elimu ya ghaibu. Vinginevyo, asingetoa maneno kama hayo.
[7] Hadiyth hii inasisitiza haki za wanyonge kutoka kwa watu wenye nguvu na mamlaka kuwa haki zao ni wajibu kupewa. Ikiwa kuna dhuluma inayofanyika katika nchi, basi watu wote watawajibika na dhulma ile.
[8] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema maneno hayo pindi watu wa Iran walipomtawalisha Khosru (binti wa Kisrah) akiwa kama mtawala wao. Suala la mwanamke kutawazwa kuwa ni jaji katika mahakama ni suala lenye utata miongoni mwa Wanazuoni. Hata hivyo, Wanazuoni wengi wana rai kuwa mwanamke hawezi kuwa jaji katika mahakama ya jinai.
[9] Swahaba anaitwa Al-Asadi, alikuwa Mhadhramiy. Alimtembelea Mu’aawiyah Shaam na akamsomea Hadiyth hii.
[10] Hadiyth hii inatupa fundisho kuwa ni haraam kwa mtawala kuwazuia watu wake na haja zao. Vivyo hivyo, hatakiwi kufunga milango ya hukumu kwao, badili yake watu wote, maskini kwa tajiri waweze kuingia kwake katika mashauri yao bila kuzuiwa.
[11] Wote kwa pamoja mtoa rushwa na mpokea rushwa wamelaaniwa. Hali hii inajumuisha hali zote. Hali ya kwanza kwa anayetoa rushwa ili apate haki zake zinazomuhusu. Katika hali hii uharaam ni kwa anayechukuwa si kwa anayetoa. Hali ya pili ni ya yule mtu anyetoa rushwa ili apate zaidi ya kile anachostahiki kupata na kwa hiyo anatwaa haki ya mwingine. Rushwa katika hali hii inakuwa ni haraam kwa anayetoa na anayepokea.
[12] Tunapata mafundisho yafuatayo: (a) Kuwa mlalamikaji na mlalamikiwa wafanyiwe usawa, yeyote asipendelewe. (b) Kila mmoja kati ya mlalamikaji na mlalamikiwa watoe maelezo yao kwa hakimu hali wakiwa wamekaa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْقَضَاءِ
Kitabu Cha Kuhukumu
بَابُ اَلشَّهَادَاتِ
01-Mlango Wa Ushahidi
1201.
عَنْ زَيْدِ بْنِ خَالِدٍ اَلْجُهَنِيِّ رضى الله عنه أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"أَلَا أُخْبِرُكُمْ بِخَيْرِ اَلشُّهَدَاءِ ؟ اَلَّذِي يَأْتِي بِشَهَادَتِهِ قَبْلَ أَنْ يُسْأَلَهَا"} رَوَاهُ مُسْلِم ٌ
Kutoka kwa Zayd bi Khaalid Al-Juhaniyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Je nikuambieni shahidi bora? Ni yule anayetoa ushahidi kabla hajaulizwa.”[1] [Imetolewa na Muslim]
1202.
وَعَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"إِنَّ خَيْرَكُمْ قَرْنِي، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ اَلَّذِينَ يَلُونَهُمْ، ثُمَّ يَكُونُ قَوْمٌ يَشْهَدُونَ وَلَا يُسْتَشْهَدُونَ، وَيَخُونُونَ وَلَا يُؤْتَمَنُونَ، وَيَنْذُرُونَ وَلَا يُوفُونَ، وَيَظْهَرُ فِيهِمْ اَلسِّمَنُ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika wabora wenu ni karne yangu, kisha wanaowafuatia, kisha wanaowafuatia. Kisha kutakuwa na watu wanaotoa ushahidi (wa uongo) wala hawakutakiwa kutoa ushahidi,[2] wanakhini wala hawaaminiwi, wanaweka nadhiri wala hawatekelezi, unene utadhihiri ndani yao.” [Bukhaariy, Muslim]
1203.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"لَا تَجُوزُ شَهَادَةُ خَائِنٍ، وَلَا خَائِنَةٍ، وَلَا ذِي غِمْرٍ عَلَى أَخِيهِ، وَلَا تَجُوزُ شَهَادَةُ اَلْقَانِعِ لِأَهْلِ اَلْبَيْتِ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haufai ushahidi wa mfanya khiyana mwanamme wala mwanamke, wala mwenye chuki dhidi ya nduguye, wala haufai ushahidi wa mtumishi wa nyumbani.”[3] [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd]
1204.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"لَا تَجُوزُ شَهَادَةُ بَدَوِيٍّ عَلَى صَاحِبِ قَرْيَةٍ"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Ushahidi wa bedui dhidi ya mtu wa kijijini (au mjini) haufai.”[4] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ibn Maajah]
1205.
وَعَنْ عُمَرَ بْنِ اَلْخَطَّابِ رضى الله عنه {أَنَّهُ خَطَبَ فَقَالَ: إِنَّ أُنَاسًا كَانُوا يُؤْخَذُونَ بِالْوَحْيِ فِي عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَإِنَّ اَلْوَحْيَ قَدْ اِنْقَطَعَ، وَإِنَّمَا نَأْخُذُكُمْ اَلْآنَ بِمَا ظَهَرَ لَنَا مِنْ أَعْمَالِكُمْ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) alikhutubia akasema: “Hakika baadhi ya watu katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) walipatilizwa kutokana na Wahyi. Na Wahyi umekatika si vinginevyo. Sasa tutawapatiliza kutokana na matendo yenu yanayotudhihirikia.”[5] [Imetolewa na Al-Bukaariy]
1206.
وَعَنْ أَبِي بَكْرَةَ رضى الله عنه {عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم أَنَّهُ عَدَّ شَهَادَةَ اَلزُّورِ فِي أَكْبَرِ اَلْكَبَائِرِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ فِي حَدِيثٍ
Kutoka kwa Abuu Bakr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Aliuhesabu ushahidi wa uzushi katika dhambi kubwa.” [Bukhaariy, Muslim katika Hadiyth]
1207.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ لِرَجُلٍ: "تَرَى اَلشَّمْسَ ؟" قَالَ: نَعَمْ. قَالَ: "عَلَى مِثْلِهَا فَاشْهَدْ، أَوْ دَعْ"} أَخْرَجَهُ اِبْنُ عَدِيٍّ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ فَأَخْطَأ َ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alimuambia mtu mmoja: Unaona jua? Akasema: ‘Ndiyo’ akamuambia: kwa mfano wake toa ushahidi au wacha.”[6] [Imetolewa na Ibn ‘Adiyy kwa isnaad dhaifu. Akaisahihisha Al-Haakim lakini alikosea]
1208.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَضَى بِيَمِينٍ وَشَاهِدٍ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ. وَأَبُو دَاوُدَ. وَالنَّسَائِيُّ وَقَالَ: إِسْنَادُهُ جَيِّد ٌ
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه مِثْلَهُ. أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّان َ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alihukumu kwa yamini na wa shahidi mmoja.”[7] [Imetolewa na Muslim na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na amesema: ‘Isnaad yake ni nzuri’
Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amepokea Hadiyth kama hii. Imepokewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan
1209.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه مِثْلَهُ. أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّان َ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) Hadiyth mfano wake imepokewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan
[1] Hawa ni wale wanaotoa ushahidi kwa ajili ya Allaah na kwa lengo la kupatikana kwa haki. Hawasubiri hadi dhalimu awakabili na kutoa ushahidi.
[2] Hawa ni wale wenye kutoa ushahidi tu kwa njia yoyote iwe ni haki au batili. Haya yanatoka katika undani wao ili kuupoteza ukweli. Hawa ni mashahidi wa aina mbaya sana.
[3] Ushahidi unaotolewa na mtu asiyekuwa mwaminifu haukubaliki, adui au mtu atakayetoa ushahidi kwa kumpendelea jamaa yake haukubaliki, kwani ushahidi kama huo mara nyingi unaelemea upande mmoja. Vivyo hivyo, hairuhusiwi kwa mtu kutoa ushahidi kwa mtu anayemkirimu kwa uwezekano mkubwa wa kumpendelea katika ushahidi wake. Ushahidi unatakiwa utolewe na mtu mwaminifu ambaye hatompendelea mmoja dhidi ya mwengine.
[4] Hii ni kwa sababu bedui hajui hali na mazingira ya watu wa mjini au kijijini na ndiyo maana wamekatazwa kutoa ushahidi kwao (kwa ajili au dhidi yao). Kwa mtu wa mjini kutoa kwa watu wa mjini mfano wao inaruhusiwa kwa kufahamu kwao mazingira ya wenzao wanaokaa mjini. Ikiwa bedui anafahamu vizuri mazingira ya watu wa mjini basi anaruhusiwa kutoa ushahidi.
[5] Hadiyth hii inaelezea kuwa hukumu itatolewa kwa lililodhaniwa kuwa ni sawa. Ikiwa katika mashahidi kuna aliyesema uongo (pamoja na kuwa aliapa kuwa atasema kweli) dhambi itakuwa ni kwa yule aliyesema uongo. Kadhi au jaji hatohusika na makosa yale.
[6] Mtu anatakiwa atoe ushahidi kwa kile alichokuwa na hakika nacho au vinginevyo aache kutoa ushahidi wake. Kwa hali hiyo hatakiwi atoe ushahidi kwa kukisia au kudhania au kwa kusikia maneno yasiyokuwa ya uhakika.
[7] Tunapata uthibitisho wa Hadiyth hii kuwa kama hakuna mashahidi wawili basi mmoja anatosheleza pamoja na kiapo cha mdai. Ikiwa katika hali ambayo hakuna shahidi, wakati huo kiapo cha madai hakitotosheleza katika kusimamisha madai yake. Katika hali hiyo, mdaiwa atatakiwa kuleta kiapo cha kukana mashtaka dhidi yake.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَاب اَلْقَضَاءِ
Kitabu Cha Kuhukumu
بَابُ اَلدَّعْوَى وَالْبَيِّنَاتِ
02-Mlango Wa Madai na Ushahidi[1]
1210.
عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"لَوْ يُعْطَى اَلنَّاسُ بِدَعْوَاهُمْ، لَادَّعَى نَاسٌ دِمَاءَ رِجَالٍ، وَأَمْوَالَهُمْ، وَلَكِنِ اَلْيَمِينُ عَلَى اَلْمُدَّعَى عَلَيْهِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ وَلِلْبَيْهَقِيِّ بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ: {"اَلْبَيِّنَةُ عَلَى اَلْمُدَّعِي، وَالْيَمِينُ عَلَى مَنْ أَنْكَرَ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Lau watu wangepewa kulingana na madai yao, basi watu wengine wangedai damu za watu na mali zao.[2] Lakini yamini ni juu ya mdaiwa.” [Bukhaariy, Muslim]
Na amepokea Al-Bayhaqiyy kwa isnaad sahihi: “Ushahidi ni juu ya mdai na yamini ni juu ya aliyekana.”
1211.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم عَرَضَ عَلَى قَوْمٍ اَلْيَمِينَ، فَأَسْرَعُوا، فَأَمَرَ أَنْ يُسْهَمَ بَيْنَهُمْ فِي اَلْيَمِينِ، أَيُّهُمْ يَحْلِفُ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Aliwaambia watu fulani waape, wakaharakisha. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamrisha kupiga kura[3] baina yao nani kati yao aape.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
1212.
وَعَنْ أَبِي أُمَامَةَ اَلْحَارِثِيُّ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {" مَنْ اِقْتَطَعَ حَقَّ امْرِئٍ مُسْلِمٍ بِيَمِينِهِ، فَقَدْ أَوْجَبَ اَللَّهُ لَهُ اَلنَّارَ، وَحَرَّمَ عَلَيْهِ اَلْجَنَّةَ" . فَقَالَ لَهُ رَجُلٌ: وَإِنْ كَانَ شَيْئًا يَسِيرًا يَا رَسُولَ اَللَّهِ؟ قَالَ: "وَإِنْ قَضِيبٌ مِنْ أَرَاكٍ"} رَوَاهُ مُسْلِم ٌ
Kutoka kwa Abuu Umaamah Al-Haarithiy[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakayejichukulia haki ya mtu Muislaam kwa kiapo chake, hakika Allaah Amekwishamuajibishia moto na Amemharamishia Jannah. Mtu mmoja akasema: ‘Ee Rasuli wa Allaah! Hata kama ni kitu kidogo? Akasema: hata kama ni kipande cha mswaki.”[5] [Imetolewa na Muslim]
1213.
وَعَنِ الْأَشْعَثِ بْنِ قَيْسٍ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ، يَقْتَطِعُ بِهَا مَالَ امْرِئٍ مُسْلِمٍ، هُوَ فِيهَا فَاجِرٌ، لَقِيَ اَللَّهَ وَهُوَ عَلَيْهِ غَضْبَانُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Al-Ash’ath bin Qays[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakayeapa yamini ili ajikatie mali ya mtu Muislaam ilihali katika hilo ni muovu; atakutana na Allaah ilihali Amemghadhibikia.” [Bukhaariy, Muslim]
1214.
وَعَنْ أَبَى مُوسَى اَلْأَشْعَرِيِّ رضى الله عنه {أَنَّ رَجُلَيْنِ اِخْتَصَمَا إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم فِي دَابَّةٍ، لَيْسَ لِوَاحِدٍ مِنْهُمَا بَيِّنَةٌ، فَقَضَى بِهَا رَسُولُ اَللَّهِ بَيْنَهُمَا نِصْفَيْنِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ وَهَذَا لَفْظُهُ، وَقَالَ: إِسْنَادُهُ جَيِّدٌ
Kutoka kwa Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Watu wawili waligombania mnyama, wala hakuna yeyote kati yao mwenye ushahidi. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akahukumu baina yao nusu mbili.”[7] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy, Hadiyth hii ni tamshi lake na akasema: Isnaad yake ni nzuri]
1215.
وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {"مَنْ حَلَفَ عَلَى مِنْبَرِي هَذَا بِيَمِينٍ آثِمَةٍ، تَبَوَّأَ مَقْعَدَهُ مِنْ اَلنَّارِ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Atakayeapa juu ya mimbari yangu hii kwa yamini ya dhambi, basi ameandaa makazi yake motoni.”[8] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
1216.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {"ثَلَاثَةٌ لَا يُكَلِّمُهُمْ اَللَّهُ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، وَلَا يَنْظُرُ إِلَيْهِمْ، وَلَا يُزَكِّيهِمْ، وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ: رَجُلٌ عَلَى فَضْلِ مَاءٍ بِالْفَلَاةِ، يَمْنَعُهُ مِنْ اِبْنِ اَلسَّبِيلِ; وَرَجُلٌ بَايَعَ رَجُلاً بِسِلْعَةٍ بَعْدَ اَلْعَصْرِ، فَحَلَفَ لَهُ بِاَللَّهِ: لَأَخَذَهَا بِكَذَا وَكَذَا، فَصَدَّقَهُ، وَهُوَ عَلَى غَيْرِ ذَلِكَ; وَرَجُلٌ بَايَعَ إِمَامًا لَا يُبَايِعُهُ إِلَّا لِلدُّنْيَا، فَإِنْ أَعْطَاهُ مِنْهَا، وَفَى، وَإِنْ لَمْ يُعْطِهِ مِنْهَا، لَمْ يَفِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Watu watatu[9] Allaah Hatawasemesha Siku ya Qiyaamah wala Hatawatazama wala Hatawatakasa na wana adhabu kali: (a) mtu mwenye maji ya ziada jangwani na anamyima msafiri, (b)mtu aliyeuziana bidhaa na mtu baada ya Al-‘Aswr akaapa kwa kadha wa kadha, akamuamini na yeye si hivyo, (c) na mtu aliyembai kiongozi kwa ajili ya dunia tu akimpa kitu hutekeleza na asipompa kitu hatekelezi.” [Bukhaariy, Muslim]
1217.
وَعَنْ جَابِرٍ رضى الله عنه {أَنَّ رَجُلَيْنِ اِخْتَصَمَا فِي نَاقَةٍ، فَقَالَ كُلُّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا نُتِجَتْ عِنْدِي، وَأَقَامَا بَيِّنَةً، فَقَضَى بِهَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم لِمَنْ هِيَ فِي يَدِهِ}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Watu wawili waligombania ngamia, kila mmojawapo akasema: ‘Ngamia huyu amezaliwa kwangu’ na wao wakaleta uthibitisho. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akahukumu ngamia huyo ni wa ambaye yuko mkononi mwake.”
1218.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا،{أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم رَدَّ اَلْيَمِينَ عَلَى طَالِبِ اَلْحَقِّ} رَوَاهُمَا اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَفِي إِسْنَادِهِمَا ضَعْفٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alirudisha yamini ya mwenye kutafuta haki.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy na katika isnaadi zake kuna udhaifu]
1219.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {قَالَتْ: دَخَلَ عَلَيَّ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ مَسْرُورًا، تَبْرُقُ أَسَارِيرُ وَجْهِهِ. فَقَالَ: "أَلَمْ تَرَيْ إِلَى مُجَزِّزٍ اَلْمُدْلِجِيِّ ؟ نَظَرَ آنِفًا إِلَى زَيْدِ بْنِ حَارِثَةَ، وَأُسَامَةَ بْنِ زَيْدٍ، فَقَالَ: " هَذِهِ أَقْدَامٌ بَعْضُهَا مِنْ بَعْضٍ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliingia kwangu hali ni mwenye furaha, uso wake wameremeta. Akasema: “Je umemuona Mujazzizin Al-Mudlijiyy?[10] Muda mfupi amemtazama Zayd bin Haarithah na Usaamah bin Zayd akasema: “Hakika nyayo hizi baadhi yake zinatokana na baadhi nyingine.” [Bukhaariy, Muslim]
[1] Maana ya Da’waa (mashtaka au ulingano) ni kuweka madai ya mtu katika kitu kwa kusema: “Ni haki ya kitu kadha wa kadha.” Bila kujali madai hayo yaliyowekwa ni kweli au si kweli. Bayyinah ina maana ya jambo lililo wazi, bayana, maadamu inathibitisha haki ya kishariy’ah ya mmiliki katika kitu kinachogombewa.
[2] Moja katika kanuni za msingi za shariy’ah ni kuwa mdai ni lazima athibitishe ukweli wa madai yake kwa kuleta vithibitisho, kuleta mashahidi n.k. mdaiwa au mshtakiwa ni lazima athibitishe ukweli wa madai yake kwa kuthibitisha au kwa kukana. Kama hili halijafanyika, mdaiwa anatakiwa alete ushahidi wa kukana madai au aape. Katika kesi ya mtuhumiwa mauaji ni kuwa mdaiwa (kama hali itaruhusu) anatakiwa alete mashahidi 50 watakaotoa kiapo. Akishindwa mdaiwa kufanya hivyo, au mdai kutoamini viapo vile, basi wakati huo anaweza kuleta viapo kama vile na kutaka alipwe fidia.
[3] Ikiwa mazingira ya madai ni imetokea kuwa makundi yote hasimu kila kimoja ni mdai na mdaiwa kwa wakati huo mmoja, basi makundi yote yanawajibika kutoa kiapo. Ikiwa kundi moja limekataa kutoa kiapo, kundi hasimu linatakiwa lifanye hivyo na kuchukua kinachogombaniwa. Kama hali itakuwa ni kwa makundi yote kuwa tayari kutoa viapo, mwenye kustahiki ataamuliwa kwa kura. Jina lolote litakalotokeza katika utaratibu huo atachukua kiapo kisha atachukuwa kitu kinachogombewa.
[4] Huyu ni Abuu Umaamah Iyaas bin Tha’labah Al-Answaar Al-Haarith Al-Khazraji. Inasemekana ni katika kabila la Balawi lililokuwa mshirika na Answaar. Alikuwa ni Swahaba wa kitambo, hakushiriki Badr kwa kuwa alikuwa akimuuguza mama yake.
[5] Hadiyth hii inathibitisha kuwa mtu akitoa kiapo cha uongo na kuchukua kitu cha mtu (hata kikiwa ni kidogo kiasi gani) au akamkosesha mtu mwenye haki na kitu chake, mtu huyo ataharamishiwa Jannah.
[6] Al-Ash’ath bin Qays bin Ma’dikarib Al-Kindi, Abuu Muhammad kwa jina lingine alikuwa ni Swahaba aliyeishi katika mji wa Kufa ‘Iraq. Alipoteza macho yake mawili katika vita vya Yarmuk. Alikuwa ni mtu karimu na mwema. Alichaguliwa kuwa ni gavana wa Azerbaijan na alihudhuria Siffin akiwa na ‘Aliy. Alifariki baada ya siku arubaini ya kifo cha ‘Aliy katika mwaka 40 Hijriyyah akiwa na umri wa miaka 63.
[7] Hii ni hali ambayo makundi yote mawili yanadai kitu kimoja. Ima hawakuwa tayari kuapa, au hawakuwa na mashahidi wa kuthibitisha madai yao. Hii ina maana walikuwa katika hadhi moja kuhusu madai yao. Ikiwa jambo katika mazingira kama haya litatokea, basi kitu kinachogombewa kitabaki kwa aliye nacho. Ikiwa hakuna aliyekuwa nacho, au kitu hicho kipo katika umiliki wa nusu kwa nusu, basi hukumu ni kukigawa kitu kinachogombewa mara mbili na kila mmoja kupata nusu yake.
[8] Hadiyth hii inaonesha kuwa uzito wa dhambi unategemea ni sehemu mtu aliyefanyia kitu kile na wakati alioufanya.
[9] Hadiyth hii inalinganisha watu wenye madhambi, kuwa hali zao zitakuwa mbaya sana, na wanastahiki ghadhabu za Allaah.
[10] Imepokelewa kuwa Zayd bin Haarith muachwa huru wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alielekea kuwa mweupe zaidi ilihali mwanae Usaamah alikuwa mweusi. Kwa ajili ya hili baadhi ya makafiri wakashuku nasaba ile. Mujazzizin Al-Mudlijiyy aliwaona wakiwa wamelala, wamejifunika nyuso zao na miguu yao ikiwa wazi. Alipoona miguu yao alisema maneno hayo ambayo yalimfurahisha Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Hii ni dalili ya kuwa mtu anapopata mashaka na kitu ni bora akapata ushauri wa wataalamu kama huyo bwana mtaalamu wa nasaba alivyofanya.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10256&title=14-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Kuhukumu%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%92%D9%82%D9%8E%D8%B6%D9%8E%D8%A7%D8%A1%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10257&title=00-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Kuhukmu
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10258&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Kuhukumu%3A%20Mlango%20Wa%20Ushahidi
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10260&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Kuhukumu%3A%20Mlango%20Wa%20Madai%20na%20Ushahidi