Sababu Za Kuteremshwa
(Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Suwrah Al-An’aam
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [2]
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
Al-An’aam: 52
06Al-An'aam: 52-Na wala usiwafukuze wale wanaomwomba Rabb wao asubuhi na jioni
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَلَا تَطْرُدِ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ مَا عَلَيْكَ مِنْ حِسَابِهِم مِّن شَيْءٍ وَمَا مِنْ حِسَابِكَ عَلَيْهِم مِّن شَيْءٍ فَتَطْرُدَهُمْ فَتَكُونَ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٥٢﴾
52. Na wala usiwafukuze wale wanaomwomba Rabb wao asubuhi na jioni wanataka Wajihi Wake. Si juu yako hisabu yao hata kidogo, na wala hisabu yako si juu yao hata kidogo, hata uwafukuze ukaja kuwa miongoni mwa madhalimu. (6:52).
Sababun-Nuzuwl:
Sa’ad (رضي الله عنه) amehadithia: Tulikuwa watu sita pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), na Ibn Mas’uwd alikuwa mmoja wao. Washirikina wakamwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Usiwaweke watu hawa karibu yako.” (Katika riwaayah nyingine ya Muslim): “Wafukuze.” Hapo ikateremka Aayah hii:
وَلَا تَطْرُدِ الَّذِينَ يَدْعُونَ رَبَّهُم بِالْغَدَاةِ وَالْعَشِيِّ يُرِيدُونَ وَجْهَهُ ۖ مَا عَلَيْكَ مِنْ حِسَابِهِم مِّن شَيْءٍ وَمَا مِنْ حِسَابِكَ عَلَيْهِم مِّن شَيْءٍ فَتَطْرُدَهُمْ فَتَكُونَ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٥٢﴾
52. Na wala usiwafukuze wale wanaomwomba Rabb wao asubuhi na jioni wanataka Wajihi Wake. Si juu yako hisabu yao hata kidogo, na wala hisabu yako si juu yao hata kidogo, hata uwafukuze ukaja kuwa miongoni mwa madhalimu. (6:52).
أسْبابُ النُّزُول
Asbaabun-Nuzuwl
Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)
Imekusanywa na: Alhidaaya.com [4]
Al-An’Aam 121
121- Na wala msile katika ambavyo halikutajwa Jina la Allaah (wakati wa kuchinjwa)...
Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):
وَلَا تَأْكُلُوا مِمَّا لَمْ يُذْكَرِ اسْمُ اللَّـهِ عَلَيْهِ وَإِنَّهُ لَفِسْقٌ ۗ وَإِنَّ الشَّيَاطِينَ لَيُوحُونَ إِلَىٰ أَوْلِيَائِهِمْ لِيُجَادِلُوكُمْ ۖ وَإِنْ أَطَعْتُمُوهُمْ إِنَّكُمْ لَمُشْرِكُونَ ﴿١٢١﴾
Na wala msile katika ambavyo halikutajwa Jina la Allaah (wakati wa kuchinjwa), kwani huo ni ukiukaji wa utiifu kwa Allaah. Na hakika mashaytwaan wanawashawishi marafiki wao wandani wabishane nanyi. Na kama mtawatii basi hakika mtakuwa washirikina. [Al-An’aam (6:121)]
Sababun-Nuzuwl:
Amehadithia Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kuhusu Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):
وَإِنَّ الشَّيَاطِينَ لَيُوحُونَ إِلَىٰ أَوْلِيَائِهِمْ
Na hakika mashaytwaan wanawashawishi marafiki wao wandani. (6:121).
Walikuwa washirikina wakisema: Kilichochinjwa kwa ajili ya Allaah msile! Lakini mnachochinja nyinyi basi kuleni! Hapo Allaah Akateremsha:
وَلَا تَأْكُلُوا مِمَّا لَمْ يُذْكَرِ اسْمُ اللَّـهِ عَلَيْهِ وَإِنَّهُ لَفِسْقٌ ۗ
Na wala msile katika ambavyo halikutajwa Jina la Allaah (wakati wa kuchinjwa), kwani huo ni ukiukaji wa utiifu kwa Allaah. (6:121). [Imepokelewa na Abuu Daawuwd]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/238
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8994&title=006-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-An%27aam
[4] http://alhidaaya.com
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8995&title=052-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-An%27aam%20Aayah%20052%3A%20%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D8%A7%20%D8%AA%D9%8E%D8%B7%D9%92%D8%B1%D9%8F%D8%AF%D9%90%20%D8%A7%D9%84%D9%91%D9%8E%D8%B0%D9%90%D9%8A%D9%86%D9%8E%20%D9%8A%D9%8E%D8%AF%D9%92%D8%B9%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20%D8%B1%D9%8E%D8%A8%D9%91%D9%8E%D9%87%D9%8F%D9%85%20%D8%A8%D9%90%D8%A7%D9%84%D9%92%D8%BA%D9%8E%D8%AF%D9%8E%D8%A7%D8%A9%D9%90%20%D9%88%D9%8E%D8%A7%D9%84%D9%92%D8%B9%D9%8E%D8%B4%D9%90%D9%8A%D9%90%D9%91%20%D9%8A%D9%8F%D8%B1%D9%90%D9%8A%D8%AF%D9%8F%D9%88%D9%86%D9%8E%20%D9%88%D9%8E%D8%AC%D9%92%D9%87%D9%8E%D9%87%D9%8F%20%DB%96
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F8996&title=121-Asbaabun-Nuzuwl%3A%20Al-An%27aam%20Aayah%20121%3A%20%D9%88%D9%8E%D9%84%D9%8E%D8%A7%20%D8%AA%D9%8E%D8%A3%D9%92%D9%83%D9%8F%D9%84%D9%8F%D9%88%D8%A7%20%D9%85%D9%90%D9%85%D9%91%D9%8E%D8%A7%20%D9%84%D9%8E%D9%85%D9%92%20%D9%8A%D9%8F%D8%B0%D9%92%D9%83%D9%8E%D8%B1%D9%90%20%D8%A7%D8%B3%D9%92%D9%85%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%91%D9%8E%D9%80%D9%87%D9%90%20%D8%B9%D9%8E%D9%84%D9%8E%D9%8A%D9%92%D9%87%D9%90%20%D9%88%D9%8E%D8%A5%D9%90%D9%86%D9%91%D9%8E%D9%87%D9%8F%20%D9%84%D9%8E%D9%81%D9%90%D8%B3%D9%92%D9%82%D9%8C%20