كِتَابُ اَلصِّيَامِ
Kitabu Cha Swiyaam
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلصِّيَامِ
05-Kitabu Cha Swiyaam[1]
527.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لَا تَقَدَّمُوا رَمَضَانَ بِصَوْمِ يَوْمٍ وَلَا يَوْمَيْنِ، إِلَّا رَجُلٌ كَانَ يَصُومُ صَوْمًا، فَلْيَصُمْهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msitangulie Ramadhwaan kwa Swawm siku moja au mbili[2] isipokuwa mtu alikuwa ana Swawm basi afunge.”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
528.
وَعَنْ عَمَّارِ بْنِ يَاسِرٍ رضى الله عنه قَالَ: {مَنْ صَامَ اَلْيَوْمَ اَلَّذِي يُشَكُّ فِيهِ فَقَدْ عَصَى أَبَا اَلْقَاسِمِ صلى الله عليه وسلم} وَذَكَرَهُ اَلْبُخَارِيُّ تَعْلِيقًا، وَوَصَلَهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa ‘Ammaar bin Yaasir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mwenye kufunga siku ambayo inatiliwa mashaka,[4] atakuwa amemuasi Abul-Qaasim (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).” [Al-Bukhaariy aliitaja kuwa ni Mu’allaq, lakini Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) waliifuatilia Hadiyth hii kuwa ni Mawsuwl, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]
529.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: {إِذَا رَأَيْتُمُوهُ فَصُومُوا، وَإِذَا رَأَيْتُمُوهُ فَأَفْطِرُوا، فَإِنْ غُمَّ عَلَيْكُمْ فَاقْدُرُوا لَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: {فَإِنْ أُغْمِيَ عَلَيْكُمْ فَاقْدُرُوا لَهُ ثَلَاثِينَ}
وَلِلْبُخَارِيِّ: {فَأَكْمِلُوا اَلْعِدَّةَ ثَلَاثِينَ}
وَلَهُ فِي حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه {فَأَكْمِلُوا عِدَّةَ شَعْبَانَ ثَلَاثِينَ}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Nilimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema: “Mkiuona mwezi mpya fungeni, na msifungue hadi mmeuona. Lakini ikiwa anga ina mawingu, basi ukadirieni.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na Muslim amesema: “Ikiwa kuna mawingu, basi hesabuni siku thelathini (ambapo mwezi sharti uandame).”
Na Al-Bukhaariy amesema: “Kamilisheni hesabu siku thelathini.”
Naye amenukuu Hadiyth ya Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) kuwa: “Kamilisheni hesabu ya siku thelathini[5] za mwezi wa Sha’baan.”
530.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {تَرَاءَى اَلنَّاسُ اَلْهِلَالَ، فَأَخْبَرْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنِّي رَأَيْتُهُ، فَصَامَ، وَأَمَرَ اَلنَّاسَ بِصِيَامِهِ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Watu waliuona mwezi mwandamo, nikamuarifu Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuwa nimeuona. Kwa hivyo yeye akafunga na akawaamrisha watu wafunge.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd, na wakaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
531.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ أَعْرَابِيًّا جَاءَ إِلَى اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: {إِنِّي رَأَيْتُ اَلْهِلَالَ، فَقَالَ: " أَتَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اَللَّهُ ؟ " قَالَ: نَعَمْ. قَالَ: " أَتَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اَللَّهِ ؟ " قَالَ: نَعَمْ. قَالَ: " فَأَذِّنْ فِي اَلنَّاسِ يَا بِلَالُ أَنْ يَصُومُوا غَدًا"} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ وَرَجَّحَ النَّسَائِيُّ إِرْسَالَهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Bedui mmoja alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Nimeona mwezi, Akasema: “Unashahadia kuwa hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah?” Akasema “Ndiyo.” Akasema: “Unashahadia pia kuwa Muhammad ni Rasuli wa Allaah?” Akasema: “Ndiyo.” Akasema: Bilaal! Watangazie watu wafunge kesho.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan, na An-Nasaaiy aliipa daraja ya Mursal]
532.
وَعَنْ حَفْصَةَ أُمِّ اَلْمُؤْمِنِينَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ لَمْ يُبَيِّتِ اَلصِّيَامَ قَبْلَ اَلْفَجْرِ فَلَا صِيَامَ لَهُ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَمَالَ النَّسَائِيُّ وَاَلتِّرْمِذِيُّ إِلَى تَرْجِيحِ وَقْفِهِ، وَصَحَّحَهُ مَرْفُوعًا اِبْنُ خُزَيْمَةَ وَابْنُ حِبَّانَ
وَلِلدَّارَقُطْنِيِّ: {لَا صِيَامَ لِمَنْ لَمْ يَفْرِضْهُ مِنَ اَللَّيْلِ}
Kutoka kwa Hafswah[7] Ummul Mu-uminiyna (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asiyelaza niyyah[8] kabla ya alfajiri hana Swawm.”[9] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad), At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy wakaisahihisha na kuipa daraja la Mawquwf. Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan wakaipa daraja la Marfuw’]
Na Ad-Daaraqutwniyy amesema: “Hana Swawm ambaye hakuifaradhisha tangu usiku.”
533.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {دَخَلَ عَلَيَّ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ يَوْمٍ. فَقَالَ: " هَلْ عِنْدَكُمْ شَيْءٌ ؟ " قُلْنَا: لَا. قَالَ: " فَإِنِّي إِذًا صَائِمٌ " ثُمَّ أَتَانَا يَوْمًا آخَرَ، فَقُلْنَا: أُهْدِيَ لَنَا حَيْسٌ، فَقَالَ: " أَرِينِيهِ، فَلَقَدْ أَصْبَحْتُ صَائِمًا " فَأَكَلَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliingia kwangu siku moja akasema: “Una kitu chochote cha kula?” Tukasema: “Hapana.” Na akasema (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Basi mie ninafunga leo.”[10] Kisha akanitembelea siku nyingine nami nikamuambia kuwa nimepewa zawadi ya Hays[11], Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hebu nionyeshe, kwani nimeamka nikiwa na Swawm.” Kisha Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akala.”[12] [Imetolewa na Muslim]
534.
وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَا يَزَالُ اَلنَّاسُ بِخَيْرٍ مَا عَجَّلُوا اَلْفِطْرَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِلتِّرْمِذِيِّ: مِنْ حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {قَالَ اَللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ أَحَبُّ عِبَادِي إِلَيَّ أَعْجَلُهُمْ فِطْرًا}
Kutoka kwa Sahl bin Sa’d (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Watu wataendelea kuwa katika khayr ilimradi wanaharakisha kufuturu.”[13] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika At-Tirmidhiy kwa upokezi wa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah amesema Mja Nimpendaye sana kati ya waja Wangu ni anayeharakisha kufuturu.”
535.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {تَسَحَّرُوا فَإِنَّ فِي اَلسَّحُورِ بَرَكَةً} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kuleni sahuwr (daku) kwani katika sahuwr kuna Baraka.”[14] [Al-Bukhaariy, Muslim]
536.
وَعَنْ سَلْمَانَ بْنِ عَامِرٍ اَلضَّبِّيِّ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {إِذَا أَفْطَرَ أَحَدُكُمْ فَلْيُفْطِرْ عَلَى تَمْرٍ، فَإِنْ لَمْ يَجِدْ فَلْيُفْطِرْ عَلَى مَاءٍ، فَإِنَّهُ طَهُورٌ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ وَابْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Salmaan bin ‘Aamir Adhw-Dhwabbiyy[15] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Endapo mmoja wenu anafuturu, afuturu kwa tende, asipopata (tende), basi kwa maji,[16] kwani maji yanatakasa.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad), akaisahihisha Ibn Khuzaymah, Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
537.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم عَنِ اَلْوِصَالِ، فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ اَلْمُسْلِمِينَ: فَإِنَّكَ يَا رَسُولَ اَللَّهِ تُوَاصِلُ ؟ قَالَ: " وَأَيُّكُمْ مِثْلِي ؟ إِنِّي أَبِيتُ يُطْعِمُنِي رَبِّي وَيَسْقِينِي". فَلَمَّا أَبَوْا أَنْ يَنْتَهُوا عَنِ اَلْوِصَالِ وَاصَلَ بِهِمْ يَوْمًا، ثُمَّ يَوْمًا، ثُمَّ رَأَوُا اَلْهِلَالَ، فَقَالَ: " لَوْ تَأَخَّرَ اَلْهِلَالُ لَزِدْتُكُمْ " كَالْمُنَكِّلِ لَهُمْ حِينَ أَبَوْا أَنْ يَنْتَهُوا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikataza kufunga Swawm mfululizo,[17] akasema mtu mmoja: “Wewe hufunga mfululi’zo Ee Rasuli wa Allaah! Akasema: “Nani kati yenu yuko kama Mimi? Wakati wa usiku Rabb Wangu Hunilisha na Kuninywesha. Walipokataa wakataka kuendelea kufunga mfululizo, alifunga pamoja nao kwa siku moja na kisha siku moja tena, kisha wakaona mwezi, Akasema: “Mwezi ungechelewa, ningewazidishia”. Alielekea kutaka kuwaadhibu walipokataa kusitisha.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
538.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَنْ لَمْ يَدَعْ قَوْلَ اَلزُّورِ وَالْعَمَلَ بِهِ، وَالْجَهْلَ، فَلَيْسَ لِلَّهِ حَاجَةٌ فِي أَنْ يَدَعَ طَعَامَهُ وَشَرَابَهُ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ، وَأَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Iwapo mtu hatoacha uongo[18] na matendo yake na ujinga, Allaah Hana haja mtu huyo aache chakula chake na kinywaji chake.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy, na Abuu Daawuwd, na tamshi hili ni lake]
539.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يُقَبِّلُ وَهُوَ صَائِمٌ، وَيُبَاشِرُ وَهُوَ صَائِمٌ، وَلَكِنَّهُ أَمْلَكُكُمْ لِإِرْبِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
وَزَادَ فِي رِوَايَةٍ: {فِي رَمَضَانَ}
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa anabusu[19] na kukumbatia huku akiwa katika Swawm, lakini yeye anamiliki zaidi matamanio yake kuliko nyinyi.”[20] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim inasema: “Katika Ramadhwaan”
540.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم اِحْتَجَمَ وَهُوَ مُحْرِمٌ، وَاحْتَجَمَ وَهُوَ صَائِمٌ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliumikwa wakati amevaa Ihraam (wakati wa Hajj au ‘Umrah), na aliumikwa akiwa na Swawm.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
541.
وَعَنْ شَدَّادِ بْنِ أَوْسٍ رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَتَى عَلَى رَجُلٍ بِالْبَقِيعِ وَهُوَ يَحْتَجِمُ فِي رَمَضَانَ. فَقَالَ: " أَفْطَرَ اَلْحَاجِمُ وَالْمَحْجُومُ "} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ، وَصَحَّحَهُ أَحْمَدُ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Shaddaad bin Aws[21] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikutana na mtu Al-Baqiy’ aliyekuwa anaumikwa ndani ya mwezi wa Ramadhwaan, akasema: “Amefungua Swawm aliyeumika na aliyeumikwa wote wamebatilisha Swawm zao.”[22] [Imetolewa na Al-Khamsah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa At-Tirmidhiy, na wakaisahihisha Ahmad, Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]
542.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رضى الله عنه قَالَ: {أَوَّلُ مَا كُرِهَتِ اَلْحِجَامَةُ لِلصَّائِمِ ، أَنَّ جَعْفَرَ بْنَ أَبِي طَالِبٍ اِحْتَجَمَ وَهُوَ صَائِمٌ، فَمَرَّ بِهِ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: " أَفْطَرَ هَذَانِ "، ثُمَّ رَخَّصَ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم بَعْدُ فِي اَلْحِجَامَةِ لِلصَّائِمِ، وَكَانَ أَنَسٌ يَحْتَجِمُ وَهُوَ صَائِمٌ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَقَوَّاهُ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mwanzo kukatazwa kuumika kwa mwenye Swawm ilikuwa hivi: Ja’far bin Abiy Twaalib alikwenda kuumikwa wakati akiwa ana Swawm, na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipomuona akasema: “Wote wawili hawa wamebatilisha Swawm zawo.” Baadaye Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaruhusu mtu aweza kuumikwa wakati ana Swawm. Anas alikuwa akienda kuumikwa wakati ana Swawm.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy na akaipa nguvu]
543.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم اِكْتَحَلَ فِي رَمَضَانَ، وَهُوَ صَائِمٌ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
قَالَ اَلتِّرْمِذِيُّ: لَا يَصِحُّ فِيهِ شَيْءٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alitia Kuhl[23] ndani ya Ramadhwaan akiwa ana Swawm.” [Imetolewa na Ibn Maajah kwa Isnaad dhaifu]
Na amesema At-Tirmidhiy: “Hakuna lolote katika maudhui haya lililo Swahiyh.”
544.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَنْ نَسِيَ وَهُوَ صَائِمٌ، فَأَكَلَ أَوْ شَرِبَ، فَلْيُتِمَّ صَوْمَهُ، فَإِنَّمَا أَطْعَمَهُ اَللَّهُ وَسَقَاهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِلْحَاكِمِ: {مَنْ أَفْطَرَ فِي رَمَضَانَ نَاسِيًا فَلَا قَضَاءَ عَلَيْهِ وَلَا كَفَّارَةَ} وَهُوَ صَحِيحٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtu yeyote anayesahau wakati yumo katika Swawm, akala au akanywa kitu, basi akamilishe Swawm yake, kwani Allaah Amemlisha na Kumnywesha yeye.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na Al-Haakim amesema: “Mtu yeyote anayefungua Swawm yake kwa kusahau, hana haja ya kulipa Swawm hiyo wala kafara.”[24] [Usimulizi huo ni Swahiyh]
545.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَنْ ذَرَعَهُ اَلْقَيْءُ فَلَا قَضَاءَ عَلَيْهِ، وَمَنْ اسْتَقَاءَ فَعَلَيْهِ اَلْقَضَاءُ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ وَأَعَلَّهُ أَحْمَدُ وَقَوَّاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Endapo mtu atajiwa ghafla na kutapika huku yumo ndani ya Swawm, hana haja ya kulipa, na mwenye kujitapisha atalazimika kulipa.”[25] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na Ahmad aliiona ina dosari, na Ad-Daaraqutwniyy aliipa nguvu]
546.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ عَامَ اَلْفَتْحِ إِلَى مَكَّةَ فِي رَمَضَانَ، فَصَامَ حَتَّى بَلَغَ كُرَاعَ الْغَمِيمِ، فَصَامَ اَلنَّاسُ، ثُمَّ دَعَا بِقَدَحٍ مِنْ مَاءٍ فَرَفَعَهُ، حَتَّى نَظَرَ اَلنَّاسُ إِلَيْهِ، ثُمَّ شَرِبَ، فَقِيلَ لَهُ بَعْدَ ذَلِكَ: إِنَّ بَعْضَ اَلنَّاسِ قَدْ صَامَ. قَالَ: "أُولَئِكَ اَلْعُصَاةُ، أُولَئِكَ اَلْعُصَاةُ"}
وَفِي لَفْظٍ: {فَقِيلَ لَهُ: إِنَّ اَلنَّاسَ قَدْ شَقَّ عَلَيْهِمُ اَلصِّيَامُ، وَإِنَّمَا يَنْظُرُونَ فِيمَا فَعَلْتَ، فَدَعَا بِقَدَحٍ مِنْ مَاءٍ بَعْدَ اَلْعَصْرِ، فَشَرِبَ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdullaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Aliondoka kuenda Makkah wakati wa Ramadhwaan mwaka wa kuiteka Makkah, na yeye na watu walifunga hadi alipofika Kuraa’ Al-Ghamiym. Kisha akaomba kikombe cha maji akakiinua juu mpaka watu wakakitazama ndipo akanywa.[26] Aliambiwa baadaye kuwa watu waliendelea kufunga akasema: “Hao ni waasi, hao ni waasi.”[27]
Tafsiri nyingine inasema: “Watu wanaona ugumu kufunga na wanangojea utakalofanya wewe.” Hapo akaitisha kikombe cha maji, baada ya Swalaah ya alasiri, akanywa. [Imetolewa na Muslim]
547.
وَعَنْ حَمْزَةَ بْنِ عَمْرٍو الْأَسْلَمِيِّ رِضَى اَللَّهُ عَنْهُ ، أَنَّهُ قَالَ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَجِدُ بِي قُوَّةً عَلَى اَلصِّيَامِ فِي اَلسَّفَرِ، فَهَلْ عَلَيَّ جُنَاحٌ ؟ فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم " هِيَ رُخْصَةٌ مِنَ اَللَّهِ، فَمَنْ أَخَذَ بِهَا فَحَسَنٌ، وَمَنْ أَحَبَّ أَنْ يَصُومَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِ "} رَوَاهُ مُسْلِمٌ وَأَصْلُهُ فِي " اَلْمُتَّفَقِ " مِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ ، {أَنَّ حَمْزَةَ بْنَ عَمْرٍو سَأَلَ}
Kutoka kwa Hamzah bin ‘Amr Al-Aslamiyy[28] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Aliuliza Ee Rasuli wa Allaah! Mimi najiona nina nguvu za kutosha za Swiyaam nikiwa safarini, je nitapata dhambi? Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hiyo ni ruhsa toka kwa Allaah, na kila atakayeitekeleza atakuwa kafanya vizuri, lakini iwapo mtu yeyote atapenda kufunga, hana dhambi.” [Imetolewa na Muslim na chanzo chake kimo katika Al-Bukhaariy na Muslim kutoka katika ripoti ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) ambayo Hamzah bin ‘Amr aliiulizia]
548.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {رُخِّصَ لِلشَّيْخِ اَلْكَبِيرِ أَنْ يُفْطِرَ، وَيُطْعِمَ عَنْ كُلِّ يَوْمٍ مِسْكِينًا، وَلَا قَضَاءَ عَلَيْهِ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَالْحَاكِمُ، وَصَحَّحَاهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Mzee anaruhusiwa kula katika mwezi wa Ramadhwaan na kulisha maskini kila siku, na hailipi.”[29] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy na Al-Haakim ambao pia waliithibitisha]
549.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: {جَاءَ رَجُلٌ إِلَى اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: هَلَكْتُ يَا رَسُولَ اَللَّهِ. قَالَ: " وَمَا أَهْلَكَكَ ؟ " قَالَ: وَقَعْتُ عَلَى اِمْرَأَتِي فِي رَمَضَانَ، فَقَالَ: " هَلْ تَجِدُ مَا تَعْتِقُ رَقَبَةً ؟ " قَالَ: لَا. قَالَ: " فَهَلْ تَسْتَطِيعُ أَنْ تَصُومَ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ ؟ " قَالَ: لَا. قَالَ: " فَهَلْ تَجِدُ مَا تُطْعِمُ سِتِّينَ مِسْكِينًا ؟ " قَالَ: لَا، ثُمَّ جَلَسَ، فَأُتِي اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم بِعَرَقٍ فِيهِ تَمْرٌ. فَقَالَ: " تَصَدَّقْ بِهَذَا "، فَقَالَ: أَعَلَى أَفْقَرَ مِنَّا ؟ فَمَا بَيْنَ لَابَتَيْهَا أَهْلُ بَيْتٍ أَحْوَجُ إِلَيْهِ مِنَّا، فَضَحِكَ اَلنَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم حَتَّى بَدَتْ أَنْيَابُهُ، ثُمَّ قَالَ: "اذْهَبْ فَأَطْعِمْهُ أَهْلَكَ "} رَوَاهُ اَلسَّبْعَةُ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mtu mmoja[30] alikuja kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “ Ee Rasuli wa Allaah! Nimeangamia.” Akasema: “Kitu gani kilichokuangamiza?” Akasema: “Nimemuingilia mke wangu ndani ya Swawm ya Ramadhwaan.” Akasema: “Je unaweza kupata mtumwa wa kumuacha huru?” Akasema: “Hapana.” Akasema tena: “Unaweza kufunga miezi miwili mfululizo?” Akasema: “Hapana.” Akasema tena: “Je unaweza kuwapa chakula maskini sitini?” Akasema: “Hapana.” Kisha akakaa chini. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaletewa ‘Araq[31] moja lenye tende. Akasema: “Litoe hili Swadaqah.” Akasema: “Je kuna maskini kuliko sisi? Hakuna familia iliyo masikini kuliko yangu kati ya milima hii miwili ya Al-Madiynah.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akacheka hadi magego yake yakaonekana, na akasema: “Nenda ukailishe familia yako[32] kwa hizo.”[33] [Imetolewa na As-Sab’ah (Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) na tamshi hili ni la Muslim]
550.
وَعَنْ عَائِشَةَ وَأُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصْبِحُ جُنُبًا مِنْ جِمَاعٍ، ثُمَّ يَغْتَسِلُ وَيَصُومُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
زَادَ مُسْلِمٌ فِي حَدِيثِ أُمِّ سَلَمَةَ: وَ لَا يَقْضِي
Kutoka kwa ‘Aaishah na Ummu Salamah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akiamka alfajiri[34] akiwa katika hali ya janaba, kisha alikuwa akifanya ghuslu (kuoga josho) na kufunga.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na akaongezea Muslim katika usimulizi wa Ummu Salamah kuwa: “wala halipi.”
551.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ مَاتَ وَعَلَيْهِ صِيَامٌ صَامَ عَنْهُ وَلِيُّهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Endapo atakayefariki na deni la Swawm, Waliy wake amfungie.”[35] [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Maana ye neno Swiyaam na Swawm ni “kusitisha” na “kujizuia”. Kwa mujibu wa Istilaahi za Shariy’ah, inamaanisha kujizuia kula, kunywa, na ngono, kuanzia alfajiri hadi machweo ya jua, huku ukiwa na niyyah thabiti ya kutekeleza amri ya Allaah (سبحانه وتعالى). Swawm ni moja ya nguzo tano za Uislaam. Ukiikataa nguzo hii, wewe siyo Muislam, na ukiikwepa, wewe ni muasi. Swawm iliamrishwa kuwa ni lazima mnamo mwaka wa 2 A.H.
[2] Hadiyth hii inatufundisha kuwa kule kufunga siku moja kabla ya kuja kwa Ramadhwaan, kama wanavyofanya baadhi ya watu wasiojua, imekatazwa
[3] Endapo mtu ana desturi ya kufunga siku fulani maalumu, na siku hiyo ikaangukia kuwa siku moja kabla ya Ramadhwaan, anaruhusiwa mtu huyo kufunga siku hiyo.
[4] Endapo mwezi wa Ramadhwaan haukuonekana mnamo tarehe 29 ya Sha’baan kwa sababu anga ilikuwa na vumbi au mawingu, ubora mtu akamilishe siku thelathini za Sha’baan ndipo aanze Swiyaam. Kuanza Swiyaam kwa kudhani tu mwezi wa Ramadhwaan unaweza kuwa ulionekana mnamo tarehe 29 ya Sha’baan, kumekatazwa.
[5] Hii inatufunza kwamba usianze kufunga hadi baada ya kuuona mwandamo wa mwezi.
[6] Hii inatufunza kuwa hata shahidi mmoja tu anatosha kutangazwa mwanzo wa mfungo, lakini kuutangaza mwandamo wa mwezi wa ‘Iyd (mfungo mosi) wanahitajika mashahidi wawili, kanuni hii imeafikwa kwa pamoja.
[7] Hafswah alikuwa binti wa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) na akaolewa na Khunays bin Hudhaafah As-Sahmi aliyehama naye kwenda Al-Madiynah. Alipokufa baada ya Badr, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuoa mnamo mwaka wa 3 A.H. Alifariki mnamo mwezi Sha’baan mwaka wa 45 A.H akiwa na umri wa miaka 60.
[8] Moja ya masharti ya Swawm ni niyyah. Kwa hivyo kila mtu sharti aweke niyyah ya Swawm kabla ya alfajiri.
[9] Kila mtu ni lazima aweke niyyah ya kufunga kabla ya alfajiri, hasa akiwa anafunga Swawm ya faradhi (ya lazima). Lakini akiwa anafunga Swawm ya Nafl (ya khiari), inatosha kuweka niyyah hata kabla ya saa sita mchana.
[10] Hadiyth hii inatufunza kuwa, niyyah ya kufunga Swawm ya khiari si lazima iwekwe kabla ya Alfajiri, bali niyyah inaweza kuwekwa hata mchana.
[11] Hays ni mchanganyiko wa tende na samli.
[12] Hadiyth hii inatufunza kwamba, Swawm ya khiari inaweza kusitishwa bila sababu yoyote.
[13] Mtu akiwa na hakika kabisa juu ya machweo ya jua, lazima asikawie kufuturu, kwani kuchelewa kufuturu ni desturi ya Mayahudi na Manaswara.
[14] Mayahudi na Wakristo hawana desturi hii ya kula sahuwr (daku). Muslim ameipokea kuwa: “Kula sahuwr ndio tofauti kati yetu na Ahl-al-Kitaab (watu wa kitabu).” Hii inasahilisha Swawm na pia inaleta thawabu zaidi.
[15] Salmaan bin ‘Aamir Adhw-Dhwabbiyy ndiye Ibn Aws bin Hujr bin ‘Amr bin Al-Haarith Adhw-Dhwabbiyy, alikuwa ni Swahaba aliyelowea Basra, na alikuwa mtu mzee wakati wa uhai wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), aliishi hadi kwenye ukhalifa wa Mu’aawiyah, na inasemekana kuwa aliuliwa katika vita vya Al-Jamaal akiwa na umri wa miaka 100. Pia inasemekana kuwa hakuna Swahaba mwingine yoyote kutoka Adhw-Dwabbi isipokuwa yeye.
[16] Kitu kizuri kuliko vyote vya kufungulia Swawm ni tende mbichi, tende kavu, kisha maji, chumvi.
[17] Neno la kiarabu Wiswaal hutumika kwa mtu ambaye hafungui Swawm yake jioni bali anaendelea kufunga mfululizo hadi siku ya pili bila kula wala kunywa katikati. Aina hii ya kufunga Swawm imekatazwa.
[18] Madhumuni ya kufunga Swawm ni kwamba, mtu ajifunze kujidhibiti mwenyewe. Lengo na azma ya kufunga Swawm linapoteza maana iwapo mtu anashindwa kujifunza hilo.
[19] Haijakatazwa kumbusu mkeo au kumkumbatia wakati wa kufunga Swawm, kwani tendo hilo tu halibatilishi Swawm.
[20] ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) anapendekeza kuwa watu wajiepushe kufanya hayo (kubusu na kukumbatia wake/waume), asije mtu akateleza na kubatilisha Swawm yake.
[21] Shaddaad bin Aws ndiye Abuu Ya’laa Al-Answaariy An-Najaariy Al-Madaniy, mpwa wa Hassan bin Thaabit. Alikuwa msomi na mwenye subira sana. Alifia Sham mnamo mwaka 58 A.H. akiwa na umri wa miaka 75.
[22] Hadiyth iliyopita (540) imeruhusu kuumikwa (kunyonywa damu kitabibu) hata kama ni ndani ya Ramadhwaan wakati mtu ana Swawm. Inaelekea kuwa kuna kutofautiana hapa, lakini hakuna. Hadiyth hii iliyosimuliwa na Shaddaad bin Aws imefutwa kwa sababu Shaddaad aliwasili Makkah baada ya mwaka wa kutekwa Makkah. Lakini ‘Abdullaah bin ‘Abbaas alisimulia kuwa hayo hayo yalitokea mnamo mwaka wa Hajjatul-Wadaa’ (Hijjah ya mwisho aliyoitekeleza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kabla hajafariki). Ama kuhusu uhalali wake, kuumika hakubatilishi Swawm kwa mujibu wa ‘Ulamaa walio wengi; lakini kuumika hakupendezi kwa kuwa kuumikwa kunaweza kusababisha udhoofu ambao nao unaweza kupelekea mtu kuvunja Swawm yake. Lakini iwapo mtu ana nguvu za kutosha kuhimili ulegevu au kusinzia kunakoweza kusababishwa na kuumikwa, basi hiyo nasaha ya kuumikwa kutopendeza haiwi na maana.
[23] Kuhl ni chombo kinachotumiwa kwenye nyusi na kope kwa madhumuni ya kujiremba au kitabibu.
[24] Hii inatujulisha kuwa, kula au kunywa kwa kusahau, hakubatilishi Swawm. Na mtu hana haja ya kuilipa Swawm hiyo wala kuilipia fidia.
[25] Kuna tofauti ya maoni juu ya kama kutapika kunabatilisha Swawm au laa. Rai inayoelekea kuwa sahihi na ina mantiki ni kuwa, iwapo kutapika huko kumetokea kwenyewe, Swawm ni halali, lakini ikiwa ni kwa maksudi Swawm hubatilika.
[26] Inaruhusiwa Swawm wakati wa safari, lakini ni bora zaidi kutofunga. Endapo mtu atahisi kachoka sana wakati wa safari, anaruhusiwa kufungua. Anaweza kulipa kwa kufunga baadaye, lakini halazimiki kufidia au kutubu.
[27] Kwa kawaida inaruhusiwa Swawm kwa mtu akiwa safarini. Wale watu waliokuwa hawakufungua alipofungua Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) waliitwa hawana utii kwa sababu kuwa, kwa vile Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alifungua Swawm yake, wao ni nani waendelee na Swawm? Utii unahitaji utekelezaji wa kikamilifu kabisa wa amri za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Maswahaba zake walidhani kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaamrisha kwa kufungua Swawm yake kwa sababu aliwaonea huruma wao Maswahaba, vinginevyo Maswahaba zake wasingesita kamwe kufuata atakavyo.
[28] Hamzah bin ‘Amr Al-Aslamiyy alikuwa Swahaba aliyehesabika kutoka Al-Hijaaz. Aliitwa jina la utani Abuu Muhammad au Abuu Swaalih. Mwanawe Muhammad na ‘Aaishah, Mama wa Waumini walipokea Hadiyth hii kutoka kwake. Alikufa mnamo mwaka wa 61 A.H. akiwa na umri wa miaka 80.
[29] Mzee ambaye hawezi Swawm anaweza kulipia upungufu huu kwa kutoa fidia. Halikadhalika mtu mgonjwa asiyejiweza ambaye haelekei kupona karibuni, anaweza kutoa fidia. Fidia ni kutolewa chakula mara mbili kwa maskini. Pia fidia ya kukosa kufunga Swawm kwa siku moja ni hiyo hiyo.
[30] Huyo aliyemuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ni Salama bin Sakhr.
[31] ‘Araq ni kapu lenye pishi moja ya tende.
[32] Hii inatufahamisha kwamba, endapo mtu ni maskini sana, anaweza kuilisha familia yake yeye mwenyewe kwa kafara yake mwenyewe. Wanazuoni wengu hawaiafiki Hadiyth hii na wanadai kuwa siyo kweli. Wengine wanaihesabu Hadiyth hii kuwa ni agizo maalumu alilopewa bwana huyo mahususi. Lakini maoni yote hayo hayana ushahidi.
[33] Hadiyth hii inatufahamisha kwamba, mwanamke hastahili kutozwa kafara (kafara au fidia ya kosa). Wengi wa Wanazuoni hawaafiki. Kanuni itumikayo ya kuwa, iwapo mme na mke wote walikubaliana kukutana kimwili, basi wote wawili wanastahili kulipa kafara. Lakini ikiwa mme ndiye aliyemlazimisha mke kukutana naye kimwili, basi mme ndiye anayestahili kafara siyo mke.
[34] Iwapo mme atakutana kimwili na mkewe usiku wa Ramadhwaan, lazima aoge asubuhi akiwa ana wasaa wa kutosha na kisha afunge.
[35] Endapo mtu atakufa kabla hajatimiza wajibu wake wa Swiyaam, warithi wake lazima wafunge siku hizo kwa niaba ya aliyefariki ndipo aliyefariki atasamehewa deni lake la Swiyaam.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلصِّيَامِ
Kitabu Cha Swawm
بَابُ صَوْمُ اَلتَّطَوُّعِ وَمَا نُهِيَ عَنْ صَوْمِهِ
02-Mlango Wa Swawm Za Sunnah, Na Siku Zilizokatazwa Swawm
552.
عَنْ أَبِي قَتَادَةَ اَلْأَنْصَارِيِّ رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم سُئِلَ عَنْ صَوْمِ يَوْمِ عَرَفَةَ. قَالَ: " يُكَفِّرُ اَلسَّنَةَ اَلْمَاضِيَةَ وَالْبَاقِيَةَ "، وَسُئِلَ عَنْ صِيَامِ يَوْمِ عَاشُورَاءَ. قَالَ: " يُكَفِّرُ اَلسَّنَةَ اَلْمَاضِيَةَ " وَسُئِلَ عَنْ صَوْمِ يَوْمِ اَلِاثْنَيْنِ، قَالَ: " ذَاكَ يَوْمٌ وُلِدْتُ فِيهِ، وَبُعِثْتُ فِيهِ، أَوْ أُنْزِلَ عَلَيَّ فِيهِ "} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Qataadah Al-Answaariy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliulizwa kuhusu Swawm ya siku ya ‘Arafah akasema: “Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na unaobakia.” Akaulizwa kuhusu Swawm ya siku ya ‘Aashuwraa akasema: “Inafuta madhambi ya mwaka uliopita.” Akaulizwa kuhusu Swawm ya siku za Jumatatu, akasema: “Hiyo ni siku niliyozaliwa na siku niliyopewa Unabiy na ni siku niliyoteremshiwa Qur-aan.”[1] [Imetolewa na Muslim]
553.
وَعَنْ أَبِي أَيُّوبَ اَلْأَنْصَارِيِّ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ صَامَ رَمَضَانَ، ثُمَّ أَتْبَعَهُ سِتًّا مِنْ شَوَّالٍ كَانَ كَصِيَامِ اَلدَّهْرِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Ayyuwb Al-Answaariyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kufunga Ramadhwaan, kisha akafuatishia siku sita za mwezi Shawwaal,[2] huwa kama Swiyaam ya mwaka mzima.” [Imetolewa na Muslim]
554.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {مَا مِنْ عَبْدٍ يَصُومُ يَوْمًا فِي سَبِيلِ اَللَّهِ إِلَّا بَاعَدَ اَللَّهُ بِذَلِكَ اَلْيَوْمِ عَنْ وَجْهِهِ اَلنَّارَ سَبْعِينَ خَرِيفًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna mja yoyote anayefunga siku moja katika njia ya Allaah isipokuwa Allaah Atamuweka mbali na moto miaka sabini elfu kwa sababu ya siku hiyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim][3]
555.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَصُومُ حَتَّى نَقُولَ لَا يُفْطِرُ، وَيُفْطِرُ حَتَّى نَقُولَ لَا يَصُومُ، وَمَا رَأَيْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم اِسْتَكْمَلَ صِيَامَ شَهْرٍ قَطُّ إِلَّا رَمَضَانَ، وَمَا رَأَيْتُهُ فِي شَهْرٍ أَكْثَرَ مِنْهُ صِيَامًا فِي شَعْبَانَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akifunga hadi tunasema kuwa hatofungua; na anakula hadi tunasema hatofunga. Sikuwahi kumuona Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) anafunga mwezi mzima bila kufungua isipokuwa mwezi wa Ramadhwaan tu, na sikumuona anafunga sana katika mwezi wowote zaidi ya Sha’baan.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
556.
وَعَنْ أَبِي ذَرٍّ رضى الله عنه قَالَ: {أَمَرَنَا رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَنْ نَصُومَ مِنْ اَلشَّهْرِ ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ: ثَلَاثَ عَشْرَةَ، وَأَرْبَعَ عَشْرَةَ وَخَمْسَ عَشْرَةَ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abuu Dharri (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alituamrisha Swawm siku tatu kila mwezi, siku ya kumi na tatu na kumi na nne na kumi na tano.”[4] [Imetolewa na An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
557.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَا يَحِلُّ لِلْمَرْأَةِ أَنْ تَصُومَ وَزَوْجُهَا شَاهِدٌ إِلَّا بِإِذْنِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ .
وَزَادَ أَبُو دَاوُدَ: {غَيْرَ رَمَضَانَ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halali kwa mwanamke kufunga (Swawm ya khiari wakati) mume wake yupo, bila idhini yake.”[5] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
Na Abuu Daawuwd Akaongezea: “Swawm ambayo si ya Ramadhwaan.”
558.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنْ صِيَامِ يَوْمَيْنِ: يَوْمِ اَلْفِطْرِ وَيَوْمِ اَلنَّحْرِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikataza watu kufunga siku mbili hizi: siku ya ‘Iydul-Fitwr na siku ya ‘Iydul-Adhwhaa.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
559.
وَعَنْ نُبَيْشَةَ اَلْهُذَلِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {أَيَّامُ اَلتَّشْرِيقِ أَيَّامُ أَكْلٍ وَشُرْبٍ، وَذِكْرٍ لِلَّهِ عَزَّ وَجَلَّ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Nubayshah Al-Hudhaliyy[6] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Siku za At-Tashriyq[7] ni siku za kula, kunywa na za kumdhukuru Allaah (عزّ وجلّ).” [Imetolewa na Muslim]
560.
وَعَنْ عَائِشَةَ وَابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمْ قَالَا: {لَمْ يُرَخَّصْ فِي أَيَّامِ اَلتَّشْرِيقِ أَنْ يُصَمْنَ إِلَّا لِمَنْ لَمْ يَجِدِ اَلْهَدْيَ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Aaishah na Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) wamesema: “Hakuna aliyeruhusiwa Swawm siku za At-Tashriyq, isipokuwa yule mtu asiyekuwa na uwezo wa Al-Hadya (mnyama wa kafara).” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
561.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه عَنِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَا تَخْتَصُّوا لَيْلَةَ اَلْجُمُعَةِ بِقِيَامٍ مِنْ بَيْنِ اَللَّيَالِي، وَلَا تَخْتَصُّوا يَوْمَ اَلْجُمُعَةِ بِصِيَامٍ مِنْ بَيْنِ اَلْأَيَّامِ، إِلَّا أَنْ يَكُونَ فِي صَوْمٍ يَصُومُهُ أَحَدُكُمْ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msiufanye usiku wa Ijumaa miongoni mwa nyusiku nyenginezo kuwa makhsusi kwa Qiyaam (kusimama kuswali), na msiifanye siku ya Ijumaa miongoni mwa siku kuwa makhsusi kwa Swiyaam isipokuwa iwe ni Swawm anayofunga mmoja wenu.” [Imetolewa na Muslim]
562.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لَا يَصُومَنَّ أَحَدُكُمْ يَوْمَ اَلْجُمُعَةِ، إِلَّا أَنْ يَصُومَ يَوْمًا قَبْلَهُ، أَوْ يَوْمًا بَعْدَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Yeyote kati yenu asifunge siku ya Ijumaa[8] isipokuwa ikiwa anaifunga pamoja na siku kabla yake au siku baada yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
563.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {إِذَا اِنْتَصَفَ شَعْبَانَ فَلَا تَصُومُوا} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَاسْتَنْكَرَهُ أَحْمَدُ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwezi wa Sha’baan ukifikia nusu, msifunge.”[9] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) Ahmad hakuiafiki]
564.
وَعَنِ اَلصَّمَّاءِ بِنْتِ بُسْرٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَا تَصُومُوا يَوْمَ اَلسَّبْتِ، إِلَّا فِيمَا اِفْتُرِضَ عَلَيْكُمْ، فَإِنْ لَمْ يَجِدْ أَحَدُكُمْ إِلَّا لِحَاءَ عِنَبٍ، أَوْ عُودَ شَجَرَةٍ فَلْيَمْضُغْهَا} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، إِلَّا أَنَّهُ مُضْطَرِبٌ
وَقَدْ أَنْكَرَهُ مَالِكٌ
وَقَالَ أَبُو دَاوُدَ: هُوَ مَنْسُوخٌ
Kutoka kwa Asw-Swammaai bint Busr[10] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msifunge siku ya Jumamosi isipokuwa katika mliofaradhishwa, na iwapo mmoja wenu hakupata isipokuwa punje ya zabibu au kijiti cha mti basi na akitafune.”[11] [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad), wapokezi wake wanaaminika, lakini ni Mudhwtwarib (inababaisha)]
Maalik hakuiafiki
Na Abuu Daawuwd amesema: “Hii ni mansuwkh (imefutwa)”
565.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ أَكْثَرَ مَا يَصُومُ مِنَ اَلْأَيَّامِ يَوْمُ اَلسَّبْتِ، وَيَوْمُ اَلْأَحَدِ، وَكَانَ يَقُولُ: " إِنَّهُمَا يَوْمَا عِيدٍ لِلْمُشْرِكِينَ، وَأَنَا أُرِيدُ أَنْ أُخَالِفَهُمْ "} أَخْرَجَهُ النَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَهَذَا لَفْظُهُ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akifunga zaidi siku ya Jumamosi na Jumapili, na alikuwa akisema: “Hizo ni siku za sikukuu za washirikina, nami nataka kutofautiana nao.” [Imetolewa na An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah, na hii ni tafsiri yake]
566.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم {نَهَى عَنْ صَوْمِ يَوْمِ عَرَفَةَ بِعَرَفَةَ} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ غَيْرَ اَلتِّرْمِذِيِّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَالْحَاكِمُ، وَاسْتَنْكَرَهُ الْعُقَيْلِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikataza Swawm siku ya ‘Arafah ndani ya ‘Arafah.”[12] [Imetolewa na Al-Khamsah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Al-Haakim, na hakuiafiki Al-‘Uqayliyy]
567.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِوٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم {لَا صَامَ مَنْ صَامَ اَلْأَبَدَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ عَنْ أَبِي قَتَادَةَ بِلَفْظِ: {لَا صَامَ وَلَا أَفْطَرَ}
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakufunga Swawm anayefunga milele”[13] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na Muslim ameandika Hadiyth ya Abuu Qataadah ikiwa na tamshi: “Hakufunga Swawm wala hakula.”
[1] Hii inamaanisha kuwa dhambi ndogo hufutwa kwa sababu ya Swawm, lakini dhambi kubwa hufutwa kwa kutubu tu. Ama kuhusu haki za watu, madeni na wajibu wa kipesa, kuhusiana na mdaiwa, kusamehewa kunategemea matakwa ya watu wanaomdai. ‘Arafah ni jina la siku ya 9 ya mwezi wa Dhul-Hijjah (Mfungo tatu au mwezi wa kumi na mbili wa Kiislam), na ‘Aashuwraa ni siku ya 10 ya mwezi Muharram (Mfungo nne au mwezi wa kwanza wa Kiislam). Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipenda kufunga siku za Jumatatu, lakini hakuelezea juu ya thawabu zake.
[2] Endapo siku 30 za Ramadhwaan zitaunganishwa na siku 6 za kufunga mwezi wa Shawwaal ambayo inaifanya jumla iwe ni siku 36. Kwa mujibu wa Shariy’ah kila jema linalipwa mara kumi. Kwa hivyo tukizidisha siku 36 kwa mara 10 tutapata 360, namba ambayo ni sawa na siku za mwaka mmoja. Wanazuoni wengine wanasema siku hizo 6 za kufunga katika mwezi wa Shawwaal ni sharti zifungwe mfululizo mara baada ya Ramadhwaan. Wengine wanasema inatosha kuzifunga siku zote 6 ndani ya mwezi Shawwaal kwa mpangilio wowote, ama mfululizo au ukajiwekea siku za kufungua baada ya kufunga siku moja. Rai hii ya pili inachukuliwa kuwa sahihi zaidi. Kadhalika Swawm ya Shawwaal hutekelezwa baada ya kukamilisha funga kamili ya Ramadhwaan na kama kuna siku iliyopita basi ifungwe kulipwa kabla ya kuanza Sita za Shawwaal.
[3] Swawm kwa ajili ya Allaah (سبحانه وتعالى) kunaweza kumaanisha kuwa mtu anafunga huku yumo katika uwanja wa vita vya Jihaad. Inaweza pia kumaanisha mfungo wa khiari (Sunnah).
[4] Siku hizo tatu zinaitwa Ayyaamul-biydhw (Masiku meupe), mwanga wa angani unaangaza (kwa sababu ya mwezi mpevu) usiku kucha.
[5] Mwanamke kakatazwa Swiyaam za Sunnah bila ruhusa ya mumewe. Hata kama atataka kufunga siku za fardhi alizozikosa ni sharti aombe ruhusa.
[6] Nubayshah Al-Hudhaliyy ndiye Abuu Twariyf Nubayshah bin ‘Abdillaah bin ‘Amr bin ‘Itaab Al-Hudhali. Huyu ni Swahaba ambaye ana Hadiyth kumi na moja. Alilowea Basra na aliitwa Nubayshah mkarimu.
[7] Siku za Tashriyq ni siku kumi na moja na kumi na mbili na kumi na tatu ya mwezi wa Dhul-Hijjah. Imekatazwa Swiyaam katika siku hizi. Mtu anayehiji anaweza kufunga katika siku hizo iwapo kashindwa kupata mnyama wa kuchinja kama kafara. Watu wengine hawana ruhusa ya kufunga siku hizo. Pia imekatazwa kufunga siku za ‘Iyd zote mbili (ya Fitwr na Adhwhaa), iwe ni Swawm ya khiari au ya kulipia Swiyaam za fardhi.
[8] Imekatazwa Swawm siku ya Ijumaa peke yake. Katazo hili ni makhususi la kumsudia mtu anayefunga siku ya Ijumaa kwa kuamini kuwa atapata thawabu zaidi kwa kufunga siku hii.
[9] Mtu anaweza kufunga ilimradi awe analipa Swawm ya faradhi, au Swawm zinazohesabika kuwa ni za Waajib (za lazima). Lakini Swiyaam za khiari zimekatazwa asije mtu akachoshwa au akadhoofishwa mno kiasi cha kuifanya Swawm ya Ramadhwaan inayokuja iwe nzito kwake.
[10] Asw-Swammaai bint Busr alikuwa ni Buhaiya au Bahima bint Busr. Alikuwa Swahaba wa kutoka ukoo wa Mazin. Ikisemekana kuwa ni dada wa au shangazi wa ‘Abdullaah bin Busr.
[11] Kwa kuwa Jumamosi ina umuhimu maalumu kwa Mayahudi na wao hufunga katika siku hii, tunatakiwa tuwe tofauti nao, na kwa kuwa Swawm hiyo inavyofanana na ya Mayahudi, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza kuichagua Jumamosi peke yake kwa Swawm. Lakini Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) anasimulia kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akifunga Jumamosi pamoja na Jumapili. Kwa kuwa siku ya Jumamosi ni sikukuu kwa Mayahudi, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alifunga siku hii ili kuharibu kawaida ya Mayahudi na kuongeza thawabu zake, alifunga siku ya Jumapili pia.
[12] Kwa mtu ambaye yumo katika tendo la kuhiji, imekatazwa Swawm siku ya ‘Arafah kwa vile mtu analazimika kukabiliana na taabu na mihangaiko migumu siku hiyo. Kwa hiyo Swawm siku hii atachoka na kudhoofu sana ambako kutapelekea kushindwa kuyafanya uzuri matendo mengine ya Hajj (Hijjah). Watu wengine wote wasiokuwa katika mchakato wa kuhiji siku ile wao hawakatazwi kufunga Swawm siku ile, na kwa yakini Swawm siku ile kwao kuna umuhimu na thawabu nyingi sana.
[13] Watu wengine wasiojua, hung’ang’ania kufunga Swawm mfululizo bila kuacha hata siku moja. Hadiyth hii inadhihirisha kuwa desturi hii imekatazwa. Wengi wa Wanazuoni wanaamini kuwa desturi hii ya kufunga Swawm kila siku milele kwa sababu hii inamdhoofisha mtu kwa hivyo inakuwa kikwazo kwa harakati zake za kidini na kidunia. Hadiyth nyingine inasema mtu anadaiwa au ana deni kwa afya yake na uhai wa mwili wake unahitaji mtu kujipa mapumziko mara kwa mara. Hata Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akifunga siku moja na anafungua siku nyingine.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلصِّيَامِ
Kitabu Cha Swawm
بَابُ اَلِاعْتِكَافِ وَقِيَامِ رَمَضَانَ
03-Mlango Wa Al-I’tikaaf Na Qiyaam: Kisimamo cha Swalaah Za Usiku Wa Ramadhwaan
568.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضى الله عنه أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {مَنْ قَامَ رَمَضَانَ إِيمَانًا وَاحْتِسَابًا، غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kusimama katika mwezi wa Ramadhwaan[1] kwa Iymaan na kutaraji malipo[2] ataghufuriwa dhambi zake zilizotangulia.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
569.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ اَلْعَشْرُ أَيْ: اَلْعَشْرُ اَلْأَخِيرُ مِنْ رَمَضَانَ شَدَّ مِئْزَرَهُ، وَأَحْيَا لَيْلَهُ، وَأَيْقَظَ أَهْلَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Siku kumi za mwisho wa Ramadhwaan zilipoingia, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alijifunga mkanda wake na alikesha usiku wake na aliiamsha familia yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
570.
وَعَنْهَا: {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَعْتَكِفُ اَلْعَشْرَ اَلْأَوَاخِرَ مِنْ رَمَضَانَ، حَتَّى تَوَفَّاهُ اَللَّهُ، ثُمَّ اعْتَكَفَ أَزْوَاجُهُ مِنْ بَعْدِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema tena kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akikaa I’tikaaf siku kumi za mwisho za Ramadhwaan mpaka alipofishwa na Allaah (عزّ وجلّ) kisha wakeze wakakaa I’tikaaf baada yake.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
571.
وَعَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا أَرَادَ أَنْ يَعْتَكِفَ صَلَّى اَلْفَجْرَ، ثُمَّ دَخَلَ مُعْتَكَفَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa anapotaka kukaa I’tikaaf anaswali Alfajiri kisha anaingia I’tikaaf yake.”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
572.
وَعَنْهَا قَالَتْ: {إِنْ كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم لَيُدْخِلُ عَلَيَّ رَأْسَهُ وَهُوَ فِي اَلْمَسْجِدِ فَأُرَجِّلُهُ، وَكَانَ لَا يَدْخُلُ اَلْبَيْتَ إِلَّا لِحَاجَةٍ، إِذَا كَانَ مُعْتَكِفًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akiweka kichwa chake katika chumba changu wakati alipokuwa Msikitini, nami nikawa namchana nywele zake Msikitini, na alikuwa haingii nyumbani isipokuwa kwa haja tu anapokuwa kwenye I’tikaaf.”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
573.
وَعَنْهَا قَالَتْ: {اَلسُّنَّةُ عَلَى اَلْمُعْتَكِفِ أَنْ لَا يَعُودَ مَرِيضًا، وَلَا يَشْهَدَ جِنَازَةً، وَلَا يَمَسَّ امْرَأَةً، وَلَا يُبَاشِرَهَا، وَلَا يَخْرُجَ لِحَاجَةٍ، إِلَّا لِمَا لَا بُدَّ لَهُ مِنْهُ، وَلَا اعْتِكَافَ إِلَّا بِصَوْمٍ وَلَا اعْتِكَافَ إِلَّا فِي مَسْجِدٍ جَامِعٍ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَلَا بَأْسَ بِرِجَالِهِ، إِلَّا أَنَّ اَلرَّاجِحَ وَقْفُ آخِرِهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Ni Sunnah kwa mwenye kukaa I’tikaaf asiende kumzuru mgonjwa, wala kuenda mazikoni, na asimuingilie wala kumkumbatia mwanamke,[5] au kutoka kwa haja yoyote ila asiyo budi nayo, iwe dharura muhimu sana kwake. Hakuna I’tikaaf ila kwa Swawm na hakuna I’tikaaf ila ndani ya Msikiti wa jamaa.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd kwa upokezi sahihi, lakini huhesabika Mawquwd]
574.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: {لَيْسَ عَلَى اَلْمُعْتَكِفِ صِيَامٌ إِلَّا أَنْ يَجْعَلَهُ عَلَى نَفْسِهِ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَالْحَاكِمُ، وَالرَّاجِحُ وَقْفُهُ أَيْضًا
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Swiyaam si lazima[6] kwa mwenye kukaa I’tikaaf Msikitini siku kumi za mwisho wa Ramadhwaan isipokuwa kama yeye mwenyewe anataka.”[7] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy na Al-Haakim, pia ni Mawquwf]
575.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا: {أَنَّ رِجَالاً مِنْ أَصْحَابِ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم أُرُوا لَيْلَةَ اَلْقَدْرِ فِي اَلْمَنَامِ، فِي اَلسَّبْعِ اَلْأَوَاخِرِ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم "أَرَى رُؤْيَاكُمْ قَدْ تَوَاطَأَتْ فِي اَلسَّبْعِ اَلْأَوَاخِرِ، فَمَنْ كَانَ مُتَحَرِّيَهَا فَلْيَتَحَرَّهَا فِي اَلسَّبْعِ اَلْأَوَاخِرِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Baadhi ya Maswahaba wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) waliona katika ndoto Laylatul-Qadr mnamo usiku wa saba wa mwisho wa Ramadhwaan. Kwa hivyo Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Naona ndoto zenu zinaafikiana na usiku wa saba wa mwisho, kwa hivyo mtu anayeitafuta aitafute mnamo siku saba za mwisho.”[8] [Al-Bukhaariy, Muslim]
576.
وَعَنْ مُعَاوِيَةَ بْنَ أَبِي سُفْيَانَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ: { لَيْلَةُ سَبْعٍ وَعِشْرِينَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالرَّاجِحُ وَقْفُهُ .
وَقَدْ اِخْتُلِفَ فِي تَعْيِينِهَا عَلَى أَرْبَعِينَ قَوْلًا أَوْرَدْتُهَا فِي " فَتْحِ اَلْبَارِي "
Kutoka kwa Mu’aawiyah bin Abiy Sufyaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa kuhusu Laylatul Qadr, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ni usiku wa ishirini na saba.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na ni Mawquwf]
577.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {قُلْتُ يَا رَسُولَ اَللَّهِ : أَرَأَيْتَ إِنْ عَلِمْتُ أَيَّ لَيْلَةٍ لَيْلَةُ اَلْقَدْرِ، مَا أَقُولُ فِيهَا ؟ قَالَ: " قُولِي: اَللَّهُمَّ إِنَّكَ عَفُوٌّ تُحِبُّ اَلْعَفْوَ فَاعْفُ عَنِّي "} رَوَاهُ اَلْخَمْسَةُ، غَيْرَ أَبِي دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Mimi nilisema: Ee Rasuli wa Allaah! Unaonaje, nikiwa najua Laylatul-Qadr inaangukia usiku gani,[9] niseme nini?” Akasema: Sema:
اَللَّهُمَّ إِنَّكَ عَفُوٌّ تُحِبُّ اَلْعَفْوَ فَاعْفُ عَنِّي
Allaahumma Innaka ‘Afuwwun Tuhibul-‘Afwa Fa’fu ‘Anniy
Ee Allaah! Hakia Wewe ni Msamehevu na Unapenda kusamehe, kwa hivyo nisamehe mimi.” [Imetolewa na Al-Khamsah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa Abuu Daawuwd, na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
578.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صلى الله عليه وسلم : {لَا تُشَدُّ اَلرِّحَالُ إِلَّا إِلَى ثَلَاثَةِ مَسَاجِدَ: اَلْمَسْجِدِ اَلْحَرَامِ، وَمَسْجِدِي هَذَا، وَالْمَسْجِدِ اَلْأَقْصَى} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msifunge safari isipokuwa ya Misikiti mitatu: Al-Masjid Al-Haraam (Makkah), Msikiti wangu na Al-Masjid Al-Aqswaa.”[10] [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Qiyaam ni kuswali Swalaah za khiari katika usiku. Katika mwezi wa Ramadhwaan, Swalaah inayoswaliwa baada ya ‘Ishaa inajulikana kwa Taraawiyh. Kwa kuswali Swalaah hizi, mtu hughufuriwa dhambi zake zote zilizopita, ilimradi mtu huyo ana Iymaan kamili juu ya ahadi ya Allaah (عزّ وجلّ) kuhusu malipo yake.
[2] Inamaanisha kuwa hayo yasifanywe kwa ajili ya riyaa (kujionyesha). Iwapo mtu hafanyi kwa riyaa, basi ataghufuriwa madhambi yake madogomadogo yote. Wanazuoni wengine wanasema kughufuriwa huko kuna masharti ataghufuriwa mtu ikiwa tu anayo ‘Aqiydah (Iymaan) thabiti.
[3] Kwa mujibu wa Hadiyth hii, wanawake pia wanafaa kukaa I’tikaaf (kujitenga na kukaa faragha Msikitini kuswali na kumdhukuru Allaah (عزّ وجلّ) mnamo siku 10 za mwisho za Ramadhwaan). Lakini wanawake lazima iwe shariy’ah inamruhusu kukaa I’tikaaf.
[4] Hapa “shida (Haja)” inamaanisha kuenda haja ndogo au kubwa.
[5] Hapa kumgusa mwanamke kunamaanisha kukutana naye kimwili, tendo linalobatilisha I’tikaaf. Vinginevyo, kumgusa tu mwanamke hakukatazwi.
[6] Inamaanisha siku zile za kawaida, zisizokuwa za Ramadhwaan.
[7] Mtu anayefanya I’tikaaf siyo lazima afunge Swawm, ila kama yeye kaapa kufunga.
[8] Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Umar kupitia kwa Swahiyhayn yasema mtu aitafute Laylatul-Qadr masiku kumi ya mwisho. Vinginevyo aitafute masiku saba ya mwisho, khususani masiku ya Witr kama ya tarehe ishirini na moja, ishirini na tatu, ishirini na tano, ishirini na saba, na tarehe ishirini na tisa.
[9] Maoni ya wengi kuhusu Laylatul-Qadr ni kwamba, usiku huu huangukia usiku wa 10 wa mwisho ya Ramadhwaan, khususan katika usiku wa Witr, na hubadilika kila Ramadhwaan. Usiku huo huweza kutokea mnamo tarehe 21, 23, 25, n.k. haiwezi kusemwa kwa hakika kabisa, kwa kuwa siku hiyo imegubikwa na siri, ndivyo Hadiyth zinavyoelezea.
[10] Kama ilivyotajwa katika Hadiyth ya hapo nyuma, kuwa I’tikaaf ni sharti iwe Msikitini kutokana na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):
وَلَا تُبَاشِرُوهُنَّ وَأَنتُمْ عَاكِفُونَ فِي الْمَسَاجِدِ ۗ
Na wala msiwaingilie hali ya kuwa nyinyi wenye kukaa i’tikaaf Misikitini. [Al-Baqarah: 186]
Hadiyth hii pia inatuambia kuwa hairuhusiwi kuenda kutembea popote kwa madhumuni ya kupatia thawabu isipokuwa Misikiti hii mitatu ambayo ina fadhila zake. Mtu akienda katika Msikiti wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), basi na apate fadhila za kulizuru kaburi la Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9183&title=05-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Swiyaam%20-%20%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D8%B5%D9%91%D9%90%D9%8A%D9%8E%D8%A7%D9%85%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9184&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Swiyaam%20
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9185&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Swiyaam%3A%20Mlango%20Wa%20Swawm%20Za%20Sunnah%2C%20Na%20Siku%20Zilizokatazwa%20Swawm
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9186&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Swiyaam%3A%20Mlango%20Wa%20Al-I%E2%80%99tikaaf%20Na%20Qiyaam%3A%20Kisimamo%20cha%20Swalaah%20Za%20Usiku%20Wa%20Ramadhwaan