كِتابُ النِّكاح
Kitabu Cha Nikaah (Ndoa)
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
824.
عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ لَنَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {يَا مَعْشَرَ اَلشَّبَابِ! مَنِ اسْتَطَاعَ مِنْكُمُ اَلْبَاءَةَ فَلْيَتَزَوَّجْ، فَإِنَّهُ أَغَضُّ لِلْبَصَرِ، وَأَحْصَنُ لِلْفَرْجِ، وَمَنْ لَمْ يَسْتَطِعْ فَعَلَيْهِ بِالصَّوْمِ، فَإِنَّهُ لَهُ وِجَاءٌ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alituambia: “Enyi mkusanyiko wa vijana, anayeweza miongoni mwenu kumudu ndoa na aoe,[1] kwani huko kuoa huinamisha zaidi macho na huhifadhi zaidi tupu. Na asiyeweza basi ajilazimu swawm; kwani huko swawm kwake ndiko kuyavunja matamanio.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
825.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ حَمِدَ اَللَّهَ، وَأَثْنَى عَلَيْهِ ، وَقَالَ: " لَكِنِّي أَنَا أُصَلِّي وَأَنَامُ، وَأَصُومُ وَأُفْطِرُ، وَأَتَزَوَّجُ اَلنِّسَاءَ، فَمَنْ رَغِبَ عَنْ سُنَّتِي فَلَيْسَ مِنِّي} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alimhimidi Allaah na akamsifu, akasema… lakini mimi naswali[2] na nalala, nafunga (swawm) na ninakula na naoa wanawake. Basi atakayechukia mwenendo wangu basi si katika mimi.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
826.
وَعَنْهُ قَالَ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَأْمُرُ بِالْبَاءَةِ، وَيَنْهَى عَنِ التَّبَتُّلِ نَهْيًا شَدِيدًا، وَيَقُولُ :" تَزَوَّجُوا اَلْوَدُودَ اَلْوَلُودَ . إِنِّي مُكَاثِرٌ بِكُمُ اَلْأَنْبِيَاءَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
وَلَهُ شَاهِدٌ: عِنْدَ أَبِي دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيِّ، وَابْنِ حِبَّانَ أَيْضًا مِنْ حَدِيثِ مَعْقِلِ بْنِ يَسَارٍ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alikua akituamrisha kuoa na akitukataza kuacha kuoa[3] makatazo makali na akisema: Oweni wanawake wanaozaaa wanaopendeza (kwa waume zao), kwa hakika mimi nitakuwa mwenye kujifakhiri (mbele ya) Manabiy kwa sababu yenu Siku ya Qiyamah.” [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
Na ina ushahidi kwa Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Hibbaan kutoka katika Hadiyth ya Ma’qil bin Yasaar
827.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ:{ تُنْكَحُ اَلْمَرْأَةُ لِأَرْبَعٍ: لِمَالِهَا، وَلِحَسَبِهَا، وَلِجَمَالِهَا، وَلِدِينِهَا، فَاظْفَرْ بِذَاتِ اَلدِّينِ تَرِبَتْ يَدَاكَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ مَعَ بَقِيَّةِ اَلسَّبْعَةِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke huolewa kwa mambo manne:[4] kwa mali yake, hadhi yake, uzuri wake na Dini yake. Basi oa aliyeshika Dini (vinginevyo) mikono yako itachafuka.”[5] [Al-Bukhaariy, Muslim pamoja na Maimaam saba (Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, Ahmad) waliobakia.
828.
وَعَنْهُ، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ إِذَا رَفَّأَ إِنْسَانًا إِذَا تَزَوَّجَ قَالَ: {بَارَكَ اَللَّهُ لَكَ، وَبَارَكَ عَلَيْكَ، وَجَمَعَ بَيْنَكُمَا فِي خَيْرٍ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alikuwa anapomuombea mtu du’aa njema, akimuombea:[6]
بَارَكَ اَللَّهُ لَكَ، وَبَارَكَ عَلَيْكَ، وَجَمَعَ بَيْنَكُمَا فِي خَيْرٍ
Baaraka Allaahu laka, wa baaraka ‘alayka, wa jama’a baynakumaa fiy khayr (Allaah Akubariki (katika mke wako) na Abariki juu yako (uweze kumudu gharama zake) na Awajumuishe katika kheri).” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah), na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Ibn Khuzaymah na Ibn Hibbaan]
829.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {عَلَّمَنَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلتَّشَهُّدَ فِي اَلْحَاجَةِ: " إِنَّ اَلْحَمْدَ لِلَّهِ، نَحْمَدُهُ، وَنَسْتَعِينُهُ، وَنَسْتَغْفِرُهُ، وَنَعُوذُ بِاَللَّهِ مِنْ شُرُورِ أَنْفُسِنَا، مَنْ يَهْدِهِ اَللَّهُ فَلَا مُضِلَّ لَهُ، وَأَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اَللَّهُ، وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ وَيَقْرَأُ ثَلَاثَ آيَاتٍ"} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alitufundisha kushahadia katika haja (ndoa na jambo lolote):
إِنَّ اَلْحَمْدَ لِلَّهِ، نَحْمَدُهُ، وَنَسْتَعِينُهُ، وَنَسْتَغْفِرُهُ، وَنَعُوذُ بِاَللَّهِ مِنْ شُرُورِ أَنْفُسِنَا، مَنْ يَهْدِهِ اَللَّهُ فَلَا مُضِلَّ لَهُ، وَأَشْهَدُ أَنْ لَا إِلَهَ إِلَّا اَللَّهُ، وَأَشْهَدُ أَنَّ مُحَمَّدًا عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ
Innal-Hamda liLLaah, nahmaduhu, wa nasta’iynuhu, wa nastaghfiruhu, wa na’uwdhu biLLaahi min shuruwri anfusinaa, man yahdihi-LLaahu falaa mudhwilla lah, wa ash-hadu an laa ilaaha illa Allaah, wa ash-hadu anna Muhammadan ‘abduhu wa rasuwluhu
(Hakika Himdi anastahiki Allaah, tunamhimidi, tunamuomba msaada na tunamuomba maghfirah. Tunajikinga kwa Allaah dhidi ya shari za nafsi zetu. Anayeongozwa na Allaah hakuna wa kumpoteza na anayepotezwa Naye hakuna wa kumuongoza. Nashuhudia kuwa hapana mwabudiwa wa haki ila Allaah na nashuhudia kuwa Muhammad ni Mja wake na ni Rasuli wake) baada ya hapo anasoma Aayah tatu.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah), na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
830.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا خَطَبَ أَحَدُكُمُ الْمَرْأَةَ، فَإِنْ اِسْتَطَاعَ أَنْ يَنْظُرَ مِنْهَا مَا يَدْعُوهُ إِلَى نِكَاحِهَا، فَلْيَفْعَلْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
وَلَهُ شَاهِدٌ: عِنْدَ اَلتِّرْمِذِيِّ، وَالنَّسَائِيِّ، عَنِ الْمُغِيرَةِ.
وَعِنْدَ اِبْنِ مَاجَهْ، وَابْنِ حِبَّانَ: مِنْ حَدِيثِ مُحَمَّدِ بْنِ مَسْلَمَةَ
وَلِمُسْلِمٍ: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ لِرَجُلٍ تَزَوَّجَ اِمْرَأَةً: أَنَظَرْتَ إِلَيْهَا ؟ " قَالَ: لَا. قَالَ: " اِذْهَبْ فَانْظُرْ إِلَيْهَا}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Yeyote miongoni mwenu anapomposa mwanamke, iwapo ataweza kumtazama sehemu zinazomvutia ndoa yake[7] basi afanye hivyo.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na wapokezi wake ni madhubuti, na akaisahihisha Al-Haakim]
Hadiyth hii ina ushahidi kwa At-Tirmidhiy na An-Nisaaiy kutoka kwa Al-Mughiyrah.
Ibn Maajah na Ibn Hibbaan wameipokea kutoka katika Hadiyth ya Muhammad bin Maslamah.[8]
Na kutoka katika Riwaayah ya Muslim kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuambia mtu alietaka kuoa, “Je umemuangalia?” akasema: “Hapana” Akasema: “Nenda ukamuangalie.”
831.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَخْطُبْ بَعْضُكُمْ عَلَى خِطْبَةِ أَخِيهِ، حَتَّى يَتْرُكَ اَلْخَاطِبُ قَبْلَهُ، أَوْ يَأْذَنَ لَهُ اَلْخَاطِبُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asipose yeyote miongoni mwenu juu ya posa ya nduguye[9] (Muislamu) mpaka yule mposaji aache kabla yake au amruhusu.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
832.
وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ اَلسَّاعِدِيِّ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {جَاءَتِ امْرَأَةٌ إِلَى رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! جِئْتُ أَهَبُ لَكَ نَفْسِي، فَنَظَرَ إِلَيْهَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَصَعَّدَ اَلنَّظَرَ فِيهَا، وَصَوَّبَهُ، ثُمَّ طَأْطَأَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ رَأْسَهُ، فَلَمَّا رَأَتْ اَلْمَرْأَةُ أَنَّهُ لَمْ يَقْضِ فِيهَا شَيْئًا جَلَسَتْ، فَقَامَ رَجُلٌ مِنْ أَصْحَابِهِ
فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنْ لَمْ يَكُنْ لَكَ بِهَا حَاجَةٌ فَزَوِّجْنِيهَا .
قَالَ: " فَهَلْ عِنْدكَ مِنْ شَيْءٍ ؟ " .
فَقَالَ: لَا، وَاَللَّهِ يَا رَسُولَ اَللَّهِ .
فَقَالَ: " اِذْهَبْ إِلَى أَهْلِكَ، فَانْظُرْ هَلْ تَجِدُ شَيْئًا ؟ " فَذَهَبَ، ثُمَّ رَجَعَ ؟
فَقَالَ: لَا، وَاَللَّهِ يَا رَسُولَ اَللَّهِ، مَا وَجَدْتُ شَيْئًا.
فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " انْظُرْ وَلَوْ خَاتَمًا مِنْ حَدِيدٍ"، فَذَهَبَ، ثُمَّ رَجَعَ
فَقَالَ: لَا وَاَللَّهِ ، يَا رَسُولَ اَللَّهِ ، وَلَا خَاتَمًا مِنْ حَدِيدٍ، وَلَكِنْ هَذَا إِزَارِي قَالَ سَهْلٌ: مَالُهُ رِدَاءٌ فَلَهَا نِصْفُهُ .
فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " مَا تَصْنَعُ بِإِزَارِكَ ؟ إِنْ لَبِسْتَهُ لَمْ يَكُنْ عَلَيْهَا مِنْهُ شَيْءٌ، وَإِنْ لَبِسَتْهُ لَمْ يَكُنْ عَلَيْكَ شَيْءٌ " فَجَلَسَ اَلرَّجُلُ، وَحَتَّى إِذَا طَالَ مَجْلِسُهُ قَامَ، فَرَآهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ مُوَلِّيًا، فَأَمَرَ بِهِ، فَدُعِيَ لَهُ، فَلَمَّا جَاءَ .
قَالَ: "مَاذَا مَعَكَ مِنَ الْقُرْآنِ ؟ " .
قَالَ: مَعِي سُورَةُ كَذَا، وَسُورَةُ كَذَا، عَدَّدَهَا .
فَقَالَ: "تَقْرَؤُهُنَّ عَنْ ظَهْرِ قَلْبِكَ ؟ " .
قَالَ: نَعَمْ، قَالَ : "اِذْهَبْ، فَقَدَ مَلَّكْتُكَهَا بِمَا مَعَكَ مِنَ الْقُرْآنِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ .
وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ: {اِنْطَلِقْ، فَقَدْ زَوَّجْتُكَهَا، فَعَلِّمْهَا مِنَ الْقُرْآنِ}
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ: {أَمْكَنَّاكَهَا بِمَا مَعَكَ مِنَ الْقُرْآنِ}
وَلِأَبِي دَاوُدَ: عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ قَالَ:{مَا تَحْفَظُ ؟ " .قَالَ: سُورَةَ اَلْبَقَرَةِ، وَاَلَّتِي تَلِيهَا . قَالَ: " قُمْ . فَعَلِّمْهَا عِشْرِينَ آيَةً}
Kutoka kwa Sahl bin Sa’d As-Saa’idiyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Alikuja mwanamke hadi kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Nimekuja kukupa nafsi yangu.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamtazama juu mpaka chini kisha akainamisha kichwa chake. Yule mwanamke alipoona kuwa hakumuambia lolote aliketi. Mtu mmoja katika Maswahaba akasema: “Ee Rasuli wa Allaah, ikiwa huna haja naye niozeshe mimi.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Una kitu?” Akasema: “Sina Wa-Allaahi Ee Rasuli wa Allaah!” Akasema: “Nenda kwa jamaa zako utazame kama utapata kitu.” Akaenda kisha akarudi, akasema: “Wa-Allaahi sikupata kitu!” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Tafuta hata kama ni pete ya chuma.” Akaenda kisha akarudi, akasema: “Wa-Allaahi Ee Rasuli wa Allaah! Sikupata hata pete ya chuma! Lakini nina hiki kikoi changu.” Sahli (mpokezi wa Hadiyth) amesema: Alikuwa hana shuka. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Atakifanya nini kikoi chako? Ukikivaa yeye hatakuwa na kitu, naye akikivaa wewe hutakuwa na kitu.” Yule mtu akaketi kwa kitambo kirefu kisha akainuka. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuona akienda zake, akaamrisha aitwe, alipokuja akasema: “Umehifadhi kiasi gani cha Qur-aan?” Akasema: “Nimehifadhi Suwrah kadha wa kadhaa.” akazihesabu Suwrah alizohifadhi, akasema: “Umezihifadhi kwa moyo?” Akasema: “Ndiyo” Akasema: “Nimekuoza kwa ulichohifadhi katika Qur-aan.”[10] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Na katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd aliyoipokea kutoka kwa Abuu Hurayrah: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuuliza umehifadhi nini?” Akasema: “Suwratul-Baqarah na inayofuatia.” Akasema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Nenda ukamfundishe Aayah ishirini.”
833.
وَعَنْ عَامِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ اَلزُّبَيْرِ، عَنْ أَبِيهِ، أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ:{أَعْلِنُوا اَلنِّكَاحَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aamir bin ‘Abdillaah bin Az-Zubayr[11] kutoka kwa baba yake amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Tangazeni ndoa.”[12] [Imetolewa na Ahmad na akaisahihisha Al-Haakim]
834.
وَعَنْ أَبِي بُرْدَةَ بْنِ أَبِي مُوسَى، عَنْ أَبِيهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا نِكَاحَ إِلَّا بِوَلِيٍّ} رَوَاهُ أَحْمَدُ وَالْأَرْبَعَةُ وَصَحَّحَهُ اِبْنُ اَلْمَدِينِيِّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَأُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ
Kutoka kwa Abuu Burdah bin Abiy Muwsaa kutoka kwa baba yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ndoa haiswihi ila kwa walii.”[13] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha Ibn Al-Madiyniyy, At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan, na wengine wameiona na ila kwa kuwa ni Mursal]
835.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَيُّمَا اِمْرَأَةٍ نَكَحَتْ بِغَيْرِ إِذْنِ وَلِيِّهَا، فَنِكَاحُهَا بَاطِلٌ، فَإِنْ دَخَلَ بِهَا فَلَهَا اَلْمَهْرُ بِمَا اِسْتَحَلَّ مِنْ فَرْجِهَا، فَإِنِ اشْتَجَرُوا فَالسُّلْطَانُ وَلِيُّ مَنْ لَا وَلِيَّ لَهُ} أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَصَحَّحَهُ أَبُو عَوَانَةَ، وَابْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke yeyote anayeolewa bila idhini ya walii wake ndoa yake ni batili. (Mume) akimuingilia mwanamke huyo ana haki ya kupata mahari kwa alichohalalishia tupu yake. Wakishindana,[14] basi sultani (mtawala) ni walii wa asiyekuwa na walii.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha Abuw ‘Awaanah, Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
836.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا تُنْكَحُ اَلْأَيِّمُ حَتَّى تُسْتَأْمَرَ، وَلَا تُنْكَحُ اَلْبِكْرُ حَتَّى تُسْـتَأْذَنَ" قَالُوا : يَا رَسُولَ اَللَّهِ، وَكَيْفَ إِذْنُهَا ؟ قَالَ: " أَنْ تَسْكُتَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asiolewe mke mkuu mpaka atakwe amri, wala asiolewe mwanamwali mpaka atakwe idhini.[15] Maswahaba wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Ni vipi idhini yake (huyo mwali)? Akasema: Ni kunyamaza.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
837.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ {اَلثَّيِّبُ أَحَقُّ بِنَفْسِهَا مِنْ وَلِيِّهَا ، وَالْبِكْرُ تُسْتَأْمَرُ ، وَإِذْنُهَا سُكُوتُهَا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
وَفِي لَفْظٍ:{لَيْسَ لِلْوَلِيِّ مَعَ اَلثَّيِّبِ أَمْرٌ، وَالْيَتِيمَةُ تُسْتَأْمَرُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mke mkuu ana haki zaidi kwa nafsi yake kuliko walii wake,[16] na mwanamwali hutakwa idhini, na idhini yake ni kunyamaza.” [Imetolewa na Muslim]
Katika tamshi lingine inasema: “Walii hana amri kwa mke mkuu. Yatima huombwa idhini.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
838.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا تُزَوِّجُ اَلْمَرْأَةُ اَلْمَرْأَةَ، وَلَا تُزَوِّجُ اَلْمَرْأَةُ نَفْسَهَا} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke hamuozeshi mwanamke, wala mwanamke hajiozeshi mwenyewe.”[17] [Imetolewa na Ibn Maajah na Ad-Daaraqutwniy na wapokezi wake ni madhubuti]
839.
وَعَنْ نَافِعٍ ، عَنْ اِبْنِ عُمَرَ قَالَ:{نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنِ الشِّغَارِ، وَالشِّغَارُ: أَنْ يُزَوِّجَ اَلرَّجُلُ اِبْنَتَهُ عَلَى أَنْ يُزَوِّجَهُ اَلْآخَرُ اِبْنَتَهُ، وَلَيْسَ بَيْنَهُمَا صَدَاقٌ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَاتَّفَقَا مِنْ وَجْهٍ آخَرَ عَلَى أَنَّ تَفْسِيرَ اَلشِّغَارِ مِنْ كَلَامِ نَافِعٍ
Kutoka kwa Naafi’ naye kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza ndoa ya Ash-Shighaar. Ash-Shighaar ni mtu kumuoza binti yake ili yule mwingine naye amuoze binti yake bila mahari baina yao.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Wameafikiana (Al-Bukhaariy na Muslim) wa njia nyingine kuwa tafsiri ya Ash-Shighaar iliyoelezwa ni maneno ya Naafi’]
840.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا{أَنَّ جَارِيَةً بِكْرًا أَتَتِ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَذَكَرَتْ: أَنَّ أَبَاهَا زَوَّجَهَا وَهِيَ كَارِهَةٌ، فَخَيَّرَهَا اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَأُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Kuna binti mmoja bikra (mwanamwali) alimuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamueleza kuwa baba yake alimuozesha naye (binti huyo) akiwa amechukia. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamkhiyarisha.”[18] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na Ibn Maajah na imedhoofishwa kwa kuwa ni Mursal]
841.
وَعَنْ اَلْحَسَنِ، عَنْ سَمُرَةَ، عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {أَيُّمَا اِمْرَأَةٍ زَوَّجَهَا وَلِيَّانِ، فَهِيَ لِلْأَوَّلِ مِنْهُمَا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَحَسَّنَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Hasan naye kutoka kwa Samurah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke yeyote aliyeozeshwa na mawalii wawili, basi yeye ni mke wa mume aliyeozeshwa na walii wa kwanza.”[19] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
842.
وَعَنْ جَابِرٍ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَيُّمَا عَبْدٍ تَزَوَّجَ بِغَيْرِ إِذْنِ مَوَالِيهِ أَوْ أَهْلِهِ، فَهُوَ عَاهِرٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ، وَكَذَلِكَ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtumwa yeyote[20] anayeoa bila idhini ya mabwana zake au jamaa zake huyo ni mzinifu.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na ameisahihisha vile vile Ibn Hibbaan]
843.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يُجْمَعُ بَيْنَ اَلْمَرْأَةِ وَعَمَّتِهَا، وَلَا بَيْنَ اَلْمَرْأَةِ وَخَالَتِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asikusanye (asioe) mtu baina ya mwanamke na shangazi yake wala baina ya mwanamke na mama yake mdogo.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
844.
وَعَنْ عُثْمَانَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَنْكِحُ اَلْمُحْرِمُ، وَلَا يُنْكَحُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ . وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ: {وَلَا يَخْطُبُ}
وَزَادَ اِبْنُ حِبَّانَ: {وَلَا يُخْطَبُ عَلَيْهِ}
Kutoka kwa ‘Uthmaan (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kuhirimia[21] haoi wala kuozesha.” [Imetolewa na Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine: “…wala kuposa.”
Na Ibn Hibbaan ameongeza: “…wala haposewi.”
845.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {تَزَوَّجَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ مَيْمُونَةَ وَهُوَ مُحْرِمٌ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ: عَنْ مَيْمُونَةَ نَفْسِهَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ تَزَوَّجَهَا وَهُوَ حَلَالٌ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimoa Maymuwnah hali ya kuwa amehirimia.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim kutoka kwa Maymuwnah mwenyewe amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuoa hali ya kuwa ametoka kuhirimia.”
846.
وَعَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ أَحَقَّ اَلشُّرُوطِ أَنْ يُوَفَّى بِهِ، مَا اِسْتَحْلَلْتُمْ بِهِ اَلْفُرُوجَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika masharti yalio na haki zaidi kutekelezwa[22] ni yale mnayohalalishia tupu.”[23] [Al-Bukhaariy, Muslim]
847.
وَعَنْ سَلَمَةَ بْنِ الْأَكْوَعِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {رَخَّصَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَامَ أَوْطَاسٍ فِي اَلْمُتْعَةِ، ثَلَاثَةَ أَيَّامٍ، ثُمَّ نَهَى عَنْهَا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Salamah bin Al-Akwa’ (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliruhusu mwaka wa Vita vya Awtwaas ndoa ya Mut’ah[24] siku tatu kisha akaikataza.” [Imetolewa na Muslim]
848.
وَعَنْ عَلَيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ اَلْمُتْعَةِ عَامَ خَيْبَرَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza ndoa ya Mut’ah mwaka wa Vita vya Khaybar.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
849.
وَعنْهُ أَنَّ رَسولَ الله صلى الله عليه وسلم {نَهَى عَنْ مُتْعَةِ النِّسَاءِ وَعَنْ أَكْلِ الْحُمُرِ الأَهْلِيَّةِ يَوْمَ خَيْبَرَ} أخْرَجَهُ السَّبْعَةُ إلاَّ أبا داوُد
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza Mut’ah ya wanawake na kula nyama ya punda wa mjini siku ya vita vya Khaybar.” [Imetolewa na As-Sab’ah (Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad) isipokuwa Abuu Daawuwd]
850.
عَنِ الرَّبِيعِ بْنِ سَبْرَةَ، عَنْ أَبِيهِ، رضي الله عنه أنَّ رَسولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قال:
{إنِّي كُنْت أَذِنْت لَكُمْ فِي الاِسْتِمْتَاعِ مِنَ النَّساء، وَإِنَّ اللَّهَ قَدْ حَرَّمَ ذلك إِلَى يَوْمِ الْقِيَامَةِ، فَمَنْ كَانَ عِنْدَهُ مِنْهُنَّ شَىْءٌ فَلْيُخَلِّ سَبِيلَهَا وَلاَ تَأْخُذُوا مِمَّا آتَيْتُمُوهُنَّ شَيْئًا} أخْرَجَهُ مُسْلِمٌ وَأَبُو دَاوُدَ وَالنَّسَائِيُّ و اِبْنِ مَاجَهْ و أَحْمَدُ و اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Ar-Rabiy’ bin Sabrah[25] kutoka kwa baba yake amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Nilikuwa nimewaruhusu ndoa ya Mut’ah ya wanawake, kwa hakika Allaah Ameiharamisha ndoa hiyo mpaka siku ya Qiyaamah. Ambaye ana mke wa mut’ah basi amuache aende zake wala msichukue chochote mlichowapa.” [Imetolewa na Muslim, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad na Ibn Hibbaan]
851.
وَعَنِ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {لَعَنَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلْمُحَلِّلَ وَالْمُحَلَّلَ لَهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالنَّسَائِيُّ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ
وَفِي اَلْبَابِ: عَنْ عَلِيٍّ أَخْرَجَهُ اَلْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amemlaani mwenye kuhalalisha na mwenye kuhalalishwa.”[26] ‘Mwenye kuhalalisha’ ni mtu kumuoa mwanamke aliyeachwa na mume mwingine talaka tatu kwa niyyah ya kumhalalishia yule mume wa kwanza baada ya yeye kumtaliki baada ya kujamiiana naye. [Imetolewa na Ahmad na An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy akaisahihisha]
Katika mlango huu kuna Hadiyth iliyopokewa kutoka kwa ‘Aliy iliyopokewa na Maimaam wane (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy.
852.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَنْكِحُ اَلزَّانِي اَلْمَجْلُودُ إِلَّا مِثْلَهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mzinifu aliyepigwa mijeledi asioe isipokuwa mfano wake.”[27] [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na wapokezi wake ni waaminifu (madhubuti)
853.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، قَالَتْ: {طَلَّقَ رَجُلٌ اِمْرَأَتَهُ ثَلَاثًا، فَتَزَوَّجَهَا رَجُلٌ، ثُمَّ طَلَّقَهَا قَبْلَ أَنْ يَدْخُلَ بِهَا، فَأَرَادَ زَوْجُهَا أَنْ يَتَزَوَّجَهَا، فَسُئِلَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ ذَلِكَ، فَقَالَ: "لَا. حَتَّى يَذُوقَ اَلْآخَرُ مِنْ عُسَيْلَتِهَا مَا ذَاقَ اَلْأَوَّلُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Mtu mmoja alimtaliki mkewe mara tatu, yule mke akaolewa na mwanamme mwingine, kisha akamuacha kabla ya kumuingilia, yule mume wake wa kwanza akataka kumuoa, akamuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu jambo hilo. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hapana mpaka mwingine aonje asali yake ile aliyoionja wa kwanza.” (yaani baada ya kuoa mpaka mujamiiane).[28] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
[1] Hii ina maanisha ikiwa mmoja wenu ana uwezo na nguvu za kuoa (kimwili na kimali) na aoe. Wanazuoni wengine wanaona kuwa ni jambo la lazima na wengine wanaona ni jambo lenye kupendeza tu.
[2] Hii ina maana kuzidisha sana katika ‘Ibaadah hakutakiwi. Jambo hilo linamfanya mtu kuchoka na kumfanya asiweze kutekeleza Swalaah za faradhi. Mtu anaweza kutoka katika Uislamu anapofikiria kuwa Swalaah zake anazoswali (na kuzidisha sana) ni bora kuliko Swalaah alizoswali Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ).
[3] At-Tabattul ina maana ya kutokuoa, mtu kudhani kuwa kuacha kwake kuoa ni aina ya ‘Ibaadah na kudhani kuwa kuoa kwake ni zuio la kufanya kwake ‘Ibaadah. Tabattul kwa Wanazuoni wote ni jambo lisilofaa na ni tendo lililoharamishwa. Hata hivyo, kutokuoa kwa sababu zisizozuilika ni jambo lingine kabisa.
[4] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuwa kuna mambo manne yanayomfanya na kumshawishi mtu kuoa. Katika mambo haya manne Muislamu anatakiwa achague mwanamke mwenye Dini. Ikiwa mwanamke ataolewa kwa sifa nyinginezo, kuna uwezekano wa mtu kupotoka na kuacha Dini. Sababu nyingine ya kuchagua Dini ni kuwa mwanamke huyo ndie mwalimu wa mwanzo kwa watoto, hivyo kwa Dini yake atawaongoza watoto katika njia iliyonyooka.
[5] Maana ya neno hili: “Mikono yako itachafuka” Waarabu hulisema kwa njia ya kulaumu, wala siyo kwa kupendelea maana yake halisi ya kumtakia mtu shari. Maana ya Hadiyth hii ni kuwa: kwa kawaida watu huoa mwanamke mwenye sifa hizi nne, basi wewe fanya hima umuoe aliyeshika Dini.
[6] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa na tabia ya kuwaombea waliofunga ndoa kwa du’aa nzuri nzuri katika umoja wao, mapenzi na kuwaombea Baraka katika maisha yao.
[7] Hizi ni zile sehemu zenye kuonekana kwa nje, kama vile; urefu, uso, mikono na mfano wa hayo.
[8] Alikuwa miongoni mwa Maswahaba wa Answaar, ukoo wa Haarith. Alihudhuria vita vyote isipokuwa vita vya Tabuwk. Alisilimu kupitia kwa Musw’ab bin ‘Umayr. Alikufa akiwa na umri wa miaka 77 katika mwaka wa 43 Hijriyyah.
[9] Katazo hili limewekwa ili ile posa ya kwanza ya nduguye ithibiti. Ikiwa msichana alishaposwa na mtu mwingine, mtu wa pili asipeleke posa. Hata hivyo ikiwa posa ya kwanza imekataliwa au kuvunjika, basi ni ruhusa posa nyingine iende.
[10] Hadiyth hii inaweka wazi mambo mengi: Miongoni mwa hayo ni kufundisha Qur-aan kunaweza kuwa ndio mahari ya mtu. Kingine kilichowekwa wazi hapa ni kuwa kiwango cha mahari hakijawekwa. Watu wengine wanatoa dalili ya Hadiyth kuwa kiwango cha chini cha mahari ni Dirham kumi. Hili si sahihi na Hadiyth hiyo haina msingi huo.
[11] Huyu ni ‘Aamir bin ‘Abdillaah bin Az-Zubayr bin Al-‘Awwaam Al-Asadi Al-Qurayshi Al-Madaniy. Alikuwa ni Taabi’ na alisikia Hadiyth kutoka kwa baba yake na wengineo. Alikuwa madhubuti na Mwenye taqwa alifariki mwaka wa 124 Hijriyyah.
[12] Sherehe za harusi ni bora zitangazwe ili kuondoa fedheha ya aina yoyote na kadhalika kwa sababu zinginezo. Kuna njia nyingi za matangazo aina hii. Mashahidi katika tukio la ndoa ni matangazo vile. Kutangaza katika kadamnasi ya watu ni aina nyingine ya matangazo.
[13] Hadiyth hii imetajwa na takriban Maswahaba thelathini wa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Baadhi ya wapokezi wake ni thiqah (madhubuti). Walii (msimamizi) wa kwanza wa familia ni baba na babu, kisha kaka zake, baada ya hapo baba zake wadogo. Kama kuna rai tofauti kwa mawalii, yeyote aliye karibu zaidi, rai yake itafuatwa zaidi, ikiwa mawalii hao wanalingana kama vile makaka na baba wadogo, kinachofanyika ni mtawala aliyopo ndiye atakayekuwa msimamizi. Vile vile ikiwa kuna wasimamizi wawili wameozesha mwanamke mmoja sehemu mbili tofauti, ndoa ya kwanza iliyofungwa itakuwa ni sahihi na ya pili itakuwa si sahihi. Ikiwa mwanamke aliyeozwa anakubaliana na msimamizi mmoja na kutofautiana na mwingine, rai ya mwanamke itatangulizwa.
[14] Yaani wale mawalii (wasimamizi wa mke) watakaposhindana wakamzuia mwanamke asiolewe, basi uwalii atakuwa nao sultani/mtawala.
[15] Ridhaa ya mwanamke ni jambo la msingi katika ndoa. Ikiwa walii au hata baba anamuozesha binti yake bila ya ridhaa yake, binti ana haki ya kubatilisha ile ndoa na kukataa. Ayyim katika lugha ya kiarabu ni mwanamke aliyekwishawahi kuingiliwa, anaweza kuwa mjane au aliyeachwa. Mzinifu mwanamke ambaye hajaolewa ni Ayyim, lakini kulingana na Shariy’ah siyo Ayyim. Ayyim ni lazima athibitishe ndoa yake kwa kutamka, vinginevyo ndoa haitosihi. Ama bikra ambaye hajabaleghe, ridhaa yake siyo muhimu bali ni ruhusa ya walii wake.
[16] Hii ina maana ya kuwa Ayyim hawezi kuozwa bila ya ridhaa yake, lakini haina maana kuwa anaweza kuolewa bila ya walii. Ikiwa kuna rai tofauti kati ya Ayyim na walii kuhusu mchumba wake na uchaguzi wa mwanamke ukawa ni kutoka katika jamaa zake wa karibu na hakuwa na uhusiano wowote nae mbaya, wakati huo walii atalazimishwa kukubaliana na Ayyim, kama walii hatokubali hilo mwanamke anaweza kuomba msaada wa mtawala wa kumuozesha. Dhul Arhaam (ndugu upande wa mama) hawezi kuwa walii.
[17] Kuhusu ndoa mwanamke hawezi kuwa msimamizi au walii, hawezi kujioza wala hawezi kuozesha mwanamke mwingine.
[18] Ina maana bila ridhaa ya mwanamke, awe bikra au mkuu (Ayyim), hawezi kuozwa, akiolewa bila ya ridhaa yake, ana haki ya kukataa na kuvunja, hata ikiwa ni baba yake au kaka yake ndiye msimamizi wa ndoa ile.
[19] Ikiwa mawalii wawili wamemuozesha mwanamke kwa waume wawili basi ndoa itakayopita ni ya yule mume aliyoozeshwa na walii wa kwanza na ndoa ya pili itakuwa sio sahihi. Ama kama ndoa hizo zitakuwa zimefungwa kwa wakati mmoja, zote zitakuwa ni batili. Kuna rai mbalimbali katika hili.
[20] Kwa ndoa ya mtumwa ni wajibu kupatikana radhi za bwana wake, bila ya ruhusa yake, ndoa haitafungwa. Ikiwa mtumwa hajui ukweli huu kuwa ruhusa ya bwana inatakiwa ni muhimu na akamuingilia mkewe, hatoadhibiwa kwa hilo, lakini kama alikuwa anajua basi ataadhibiwa.
[21] Mtu akiwa katika hali ya Ihraam, kuoa au kuozesha hairuhusiwi. Hii ni kulingana na Wanazuoni takribani wote. Ama kuhusu Hadiyth iliyopokewa na Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) sanad yake ni sahihi, lakini alikosea kusema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuoa Maymuwnah alipokuwa katika Ihraam. Maymuwnah mwenyewe amethibitisha hili katika Hadiyth iliyofuatia.
[22] Ina maana suala la mahari ni la msingi katika ndoa.
[23] Maana ya Hadiyth hii ni kuwa masharti yaliyo na haki zaidi kutekelezwa ni masharti ya ndoa, bora yasipite mipaka, Al-Khatwaab amesema: ‘Masharti katika ndoa, yako tofauti, muna masharti yanayopasa kutimizwa kwa itifaki ya ‘Ulamaa, nayo ni Aliyoamrisha Allaah ya kushikamana kwa wema au kwa kuachana kwa ihsani, na kwa maana hii Ulamaa wengine wameisherehesha Hadiyth hii. Kuna na masharti yasiyofaa kutekelezwa aslan kama vile mwanamke kuweka sharti mke mwenza atalikiwe. Kuna masharti yaliyo na khitilafu miongoni mwa ‘Ulamaa, kama vile kushaurisha asimuolee mke mwingine’
[24] Mut’ah ni ndoa ya muda maalumu. Aina hii ya ndoa ilikuwepo katika zama za Jaahiliyyah. Kuna wakati Uislamu ulikataza na wakati uliruhusu kwa masharti maalumu, mwishowe ndoa hii iliharamishwa katika Hijjatul-Wada’ (Hijjah ya mwisho ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ))
[25] Ar-Rabiy’ bin Sabrah bin Ma’bad Al-Juhani Al-Madaniy alikuwa ni mtu madhubuti kulingana na An-Nasaaiy na Al-‘Ajli.
[26] Al-Muhallil “mwenye kuhalalisha” ni mtu kumuoa mwanamke aliyeachwa na mume mwingine talaka tatu kwa niyyah ya kumhalalishia yule mume wa kwanza baada na yeye kumtaliki baada ya kujamiana naye. Ndoa iliyosimama kwa malengo haya ni haramu, iwe ni kwa muda uliotajwa au isiwe hivyo.
[27] Hii ina maana mwenye taqwa asimuoe mwanamke ambaye ameshatuhumiwa na kuthibitishwa kuwa ni mzinifu na vivyo hivyo mwanamke mwenye taqwa asiolewe na mwanamme mzinifu.
[28] Ina maana mwanamke aliyeachwa talaka tatu akiolewa na mtu mwingine na akawa keshaingiliwa na mume yule kisha mume akamuacha au akafariki hapo ndipo anaweza tena kuolewa na yule mume wake wa mwanzo. Kama hajakutana naye kimwili na mume wake wa pili hawezi kuolewa na yule mume wake wa mwanzo.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ عِشْرَةِ اَلنِّسَاءِ
02-Mlango Wa Kutangamana Na Wake
865.
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {مَلْعُونٌ مَنْ أَتَى اِمْرَأَةً فِي دُبُرِهَا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، وَلَكِنْ أُعِلَّ بِالْإِرْسَالِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Amelaaniwa mwenye kumjamii mkewe katika duburi yake.”[1] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy, matini ya Hadiyth ni yake. Wapokezi wake ni madhubuti lakini imedhoofishwa kwa kuwa ni Mursal]
866.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَنْظُرُ اَللَّهُ إِلَى رَجُلٍ أَتَى رَجُلاً أَوْ اِمْرَأَةً فِي دُبُرِهَا} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَأُعِلَّ بِالْوَقْفِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah Hamtazami mwanamume aliyemjamii mwanamume au mwanamke katika uchi wake wa nyuma.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na Ibn Hibbaan na imedhoofishwa kwa kuwa ni Mawquwf]
867.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ اَلْآخِرِ فَلَا يُؤْذِي جَارَهُ، وَاسْتَوْصُوا بِالنِّسَاءِ خَيْرًا، فَإِنَّهُنَّ خُلِقْنَ مِنْ ضِلَعٍ، وَإِنَّ أَعْوَجَ شَيْءٍ فِي اَلضِّلَعِ أَعْلَاهُ، فَإِنْ ذَهَبْتَ تُقِيمَهُ كَسَرْتَهُ، وَإِنْ تَرَكْتَهُ لَمْ يَزَلْ أَعْوَجَ، فَاسْتَوْصُوا بِالنِّسَاءِ خَيْرًا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
وَلِمُسْلِمٍ: {فَإِنْ اِسْتَمْتَعْتَ بِهَا اِسْتَمْتَعْتَ وَبِهَا عِوَجٌ، وَإِنْ ذَهَبْتَ تُقِيمُهَا كَسَرْتَهَا، وَكَسْرُهَا طَلَاقُهَا}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anayemuamini Allaah na siku ya mwisho, asimuudhi jirani yake.[2] Wafanyieni kheri wanawake, hakika wao wameumbwa kwa ubavu, na hakika kitu kilichopotoka zaidi katika ubavu ni ule wa juu, ukitaka kuunyosha utauvunja[3] na ukiuwacha utaendelea kupotoka, kwa hivyo wafanyieni wema wanawake.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
Na katika Riwaayah ya Muslim: “Ukistarehe naye utastarehe naye akiwa na upotofu. Na ukitaka kumnyoosha utamvunja na kumvunja kwake ni kumtaliki.”
868.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {كُنَّا مَعَ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي غَزَاةٍ، فَلَمَّا قَدِمْنَا اَلْمَدِينَةَ، ذَهَبْنَا لِنَدْخُلَ. فَقَالَ: " أَمْهِلُوا حَتَّى تَدْخُلُوا لَيْلًا يَعْنِي: عِشَاءً لِكَيْ تَمْتَشِطَ اَلشَّعِثَةُ، وَتَسْتَحِدَّ اَلْمَغِيبَةُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِلْبُخَارِيِّ:{إِذَا أَطَالَ أَحَدُكُمُ الْغَيْبَةَ، فَلَا يَطْرُقْ أَهْلَهُ لَيْلاً}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) katika vita, tuliporudi Madiynah tulitaka kuingia (majumbani mwetu) Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akatuambia: Subirini,[4] ili muingie usiku yaani wakati wa ‘Ishaa ili (mke) mwenye nywele timtim apate kujichana, na yule aliyempoteza mumewe apate kujinyoa.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Katika Riwaayah ya Bukhaariy imesema: “Mmoja wenu atakapokuwa safarini muda mrefu basi asiwagongee katu watu wake wakati wa usiku.”
869.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِنَّ شَرَّ اَلنَّاسِ مَنْزِلَةً عِنْدَ اَللَّهِ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ، اَلرَّجُلُ يُفْضِي إِلَى اِمْرَأَتِهِ وَتُفْضِي إِلَيْهِ، ثُمَّ يَنْشُرُ سِرَّهَا} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakika uovu wa watu kwa daraja kubwa mbele ya Allaah siku ya Qiyamah ni mwanamume anamjamii mkewe kisha akaeneza siri yake, na mwanamke anamjamii mme wake kisha anaeneza siri yake.”[5] [Imetolewa na Muslim]
870.
وَعَنْ حَكِيمِ بْنِ مُعَاوِيَةَ، عَنْ أَبِيهِ قَالَ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! مَا حَقُّ زَوْجِ أَحَدِنَا عَلَيْهِ ؟ قَالَ: " تُطْعِمُهَا إِذَا أَكَلْتَ، وَتَكْسُوهَا إِذَا اِكْتَسَيْتَ، وَلَا تَضْرِبِ الْوَجْهَ، وَلَا تُقَبِّحْ، وَلَا تَهْجُرْ إِلَّا فِي اَلْبَيْتِ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَعَلَّقَ اَلْبُخَارِيُّ بَعْضَهُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Hakiym bin Mu’aawiyah kutoka kwa baba yake amesema: “Niliuliza: Ee Rasuli wa Allaah! Ni nini wajibu wa mke kwa mumewe? Akasema: Ni umlishe unapokula, umvishe unapovaa, wala usimpige uso, wala usimkaripie wala usimgure ila nyumbani tu.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah. Al-Bukhaariy ameifanya ni Mu’alaqqah baadhi yake. Akaisahihisha Ibn Hibbaan na Al-Haakim]
871.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {كَانَتِ الْيَهُودُ تَقُولُ: إِذَا أَتَى اَلرَّجُلُ اِمْرَأَتَهُ مِنْ دُبُرِهَا فِي قُبُلِهَا، كَانَ اَلْوَلَدُ أَحْوَلَ. فَنَزَلَتْ: "نِسَاؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوْا حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ" [اَلْبَقَرَة : 223]} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Mayahudi walikuwa wakisema: Mwanamume akimjamii mkewe kinyume nyume kwa uchi wa mbele mtoto akizaliwa atakuwa makengeza. Ikateremka Aayah hii: “Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo” [Al-Baqarah: 223] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
872.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَوْ أَنَّ أَحَدَكُمْ إِذَا أَرَادَ أَنْ يَأْتِيَ أَهْلَهُ قَالَ: بِسْمِ اَللَّهِ. اَللَّهُمَّ جَنِّبْنَا اَلشَّيْطَانَ وَجَنِّبِ الشَّيْطَانَ مَا رَزَقْتَنَا، فَإِنَّهُ إِنْ يُقَدَّرْ بَيْنَهُمَا وَلَدٌ فِي ذَلِكَ، لَمْ يَضُرَّهُ اَلشَّيْطَانُ أَبَدًا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Lau mmoja wenu anapomuendea mkewe (amjamii) aseme:
اَللَّهُمَّ جَنِّبْنَا اَلشَّيْطَانَ وَجَنِّبِ الشَّيْطَانَ مَا رَزَقْتَنَا
BismiLlaah, Allaahumma jannibnaa ash-shaytwaana wa jannibi ash-shaytwaana maa razaqtanaa (Kwa jina la Allaah, Ee Allaah Tuepushe na shaytwaan, na umuepushe shaytwaan katika Utakachoturuzuku). Kisha wakajaaliwa kupata mtoto, shaytwaan hawezi kumdhuru (mtoto huyo) milele.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
873.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا دَعَا اَلرَّجُلُ اِمْرَأَتَهُ إِلَى فِرَاشِهِ فَأَبَتْ أَنْ تَجِيءَ، لَعَنَتْهَا اَلْمَلَائِكَةُ حَتَّى تُصْبِحَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
وَلِمُسْلِمٍ: {كَانَ اَلَّذِي فِي اَلسَّمَاءِ سَاخِطًا عَلَيْهَا حَتَّى يَرْضَى عَنْهَا}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamume atakapomuita mkewe kitandani akakataa kumuendea, akalala, Malaika wanamlaani (mke huyo) mpaka apambazukiwe.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Bukhaariy]
Na katika Riwaayah ya Muslim imesema: “…Aliye mbinguni Atamkasirikia (mke huyo) mpaka mumewe amridhie.”
874.
وَعَنِ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَعَنَ اَلْوَاصِلَةَ وَالْمُسْتَوْصِلَةَ، وَالْوَاشِمَةَ وَالْمُسْتَوْشِمَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Amemlaani mwanamke[6] mwenye kuunga na mwenye kuungwa nywele na mwenye kuchanja na mwenye kuchanjwa.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
875.
وَعَنْ جُذَامَةَ بِنْتِ وَهْبٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ:{حَضَرْتُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي أُنَاسٍ، وَهُوَ يَقُولُ: لَقَدْ هَمَمْتُ أَنْ أَنْهَى عَنِ الْغِيلَةِ، فَنَظَرْتُ فِي اَلرُّومِ وَفَارِسَ، فَإِذَا هُمْ يُغِيلُونَ أَوْلَادَهُمْ فَلَا يَضُرُّ ذَلِكَ أَوْلَادَهُمْ شَيْئًا" . ثُمَّ سَأَلُوهُ عَنِ الْعَزْلِ ؟ فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "ذَلِكَ اَلْوَأْدُ اَلْخَفِيُّ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Judhaamah bint Wahb[7] (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nilikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipowaambia watu: Nilitamani kukataza Ghiylah,[8] Nikatazama Warumi na Wafursi nikawakuta wanawafanyia Ghiylah watoto wao wala hilo halidhuru chochote watoto wao. Kisha Maswahaba wakamuuliza kuhusu ‘Azli’[9] Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akawaambia Huko ndiko kuua kwa siri.” [Imetolewa na Muslim]
876.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ اَلْخُدْرِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَجُلاً قَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ لِي جَارِيَةً، وَأَنَا أَعْزِلُ عَنْهَا، وَأَنَا أَكْرَهُ أَنْ تَحْمِلَ، وَأَنَا أُرِيدُ مَا يُرِيدُ اَلرِّجَالُ، وَإِنَّ اَلْيَهُودَ تُحَدِّثُ: أَنَّ اَلْعَزْلَ المَوْؤُدَةُ اَلصُّغْرَى. قَالَ: " كَذَبَتْ يَهُودُ، لَوْ أَرَادَ اَللَّهُ أَنْ يَخْلُقَهُ مَا اِسْتَطَعْتَ أَنْ تَصْرِفَهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَالنَّسَائِيُّ، وَاَلطَّحَاوِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa “Mtu mmoja alimjia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Mimi nina mjakazi, nami namfanyia ‘azli nachukia kubeba kwake mimba, nami nataka wanayotaka wanaume (kujimai) na Mayahudi huwa wanasema kuwa kufanya ‘azli ni mauaji madogo. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Wayahudi wamedanganya, lau Allaah Angalitaka kumuumba mtoto wewe usingaliweza kumzuia.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Atw-Twahaawiyy, na wapokezi wake ni madhubuti]
877.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {كُنَّا نَعْزِلُ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَالْقُرْآنُ يَنْزِلُ، وَلَوْ كَانَ شَيْئًا يُنْهَى عَنْهُ لَنَهَانَا عَنْهُ اَلْقُرْآنُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ:{فَبَلَغَ ذَلِكَ نَبِيَّ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَلَمْ يَنْهَنَا}
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Tulikuwa tukifanya ‘Azl katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na Qur-aan inateremka. Lau kama (‘azl) ingekuwa ni jambo analokataza basi Qur-aan ingelitukataza.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim inasema: “...habari hiyo ikamfikia Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wala hakutukataza.”
878.
وَعَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ يَطُوفُ عَلَى نِسَائِهِ بِغُسْلٍ وَاحِدٍ} أَخْرَجَاهُ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alikuwa akiwazungukia wakeze kwa josho moja.”[10] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
[1] Wanazuoni wote wamekubaliana kuwa kumuingilia mwanamke nyuma ni haraam.
[2] Kumkera na kumuudhi Muislamu ni jambo lisilotakiwa, ama kumuudhi jirani ni katika madhambi makubwa.
[3] Hadiyth hii inatufundisha kuwa wanawake waamiliwe kwa wema. Tabia ya mwanamke ni tofauti na ya mwanamume. Kuna sababu nyingi za matatizo anayoyapata mwanamke. Mwanamke ni kama ubavu, ambao ukiunyoosha utauvunja. Tabia ya maumbile aliyoumbwa nayo mwanamke haiwezi kubadilika.
[4] Hii ina maana ikiwa mtu ametoka safari ya mbali, si vizuri kuenda nyumbani kwake moja kwa moja. Ni vizuri kutuma taarifa ya kufika kwako kwanza. Kuna sababu nyingi kuhusu jambo hili. Mume anapoondoka, mwanamke hajiangalii kwa kujiremba na kujiweka vizuri kama kunyoa sehemu zake na usafi mzima wa mwili wake. Suala hili linaweza kuonekana dogo lakini linaweza kumfanya mume akapunguza mapenzi kwa mke wake.
[5] Ina maana ya kuelezea lile tendo kwa watu wengine, kwa hakika kufanya jambo hili kunapelekea katika kufanya jambo la haraam.
[6] Katika Hadiyth hii wamelaaniwa wanawake aina nne: 1-Wenye kuunga nywele, 2-Wenye kuungwa nywele, 3-Wenye kuchanja (tattoo), 4- Wenye kuchanjwa (tattoo) katika miili yao.
[7] Judhaamah bint Wahb ni dada yake ‘Ukaashah bin Mihdhan kwa mama, jina lake lingine ni Jundal Al-Asadiyyah. Alikuwa ni Swahaba miongoni mwa Waislamu wa mwanzo. Alihajiri Madiynah. Alikuwa ni mke wa Anis bin Qataadah.
[8] Ghiylah ni mwanamume amjamii mkewe naye ananyonyesha au akiwa ni mjamzito.
[9] ‘Azl ni kumjamii mkewe na ukifika wakati wa kushusha manii akayamwaga nje kwa ajili ya kupanga kizazi. Suala la uhalaal na uharaam wa ‘Azl ni kuwa kuna Hadiyth kuhusiana na suala hili. Ikiwa imeamuliwa kuwa ‘Azl ni halaal na kwa wakati huo huo Shariy’ah haipendekezi. Kwa kadhia ya mwanamke ambaye afya yake ni mbaya hapa ‘Azl itakuwa lina lengo la kuokoa maisha.
[10] Lengo la Hadiyth hii kuwa ugawaji wa muda haukuwa wajibu kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Ingalikuwa ni wajibu kwake kama kwa watu wengine asingelazimika kuwazunguka wote kwa usiku mmoja.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلصَّدَاقِ
03-Mlango Wa Mahari
879.
عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ، عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَنَّهُ أَعْتَقَ صَفِيَّةَ، وَجَعَلَ عِتْقَهَا صَدَاقَهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “alimuacha huru Swafiyyah[1] na akafanya kumuacha huru kwake ndio mahari yake.”[2] [Al-Bukhaariy, Muslim]
880.
وَعَنْ أَبِي سَلَمَةَ بْنِ عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ، رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّهُ قَالَ: {سَأَلْتُ عَائِشَةَ زَوْجَ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَمْ كَانَ صَدَاقُ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَتْ: كَانَ صَدَاقُهُ لِأَزْوَاجِهِ ثِنْتَيْ عَشْرَةَ أُوقِيَّةً وَنَشًّا. قَالَتْ: أَتَدْرِي مَا اَلنَّشُّ ؟ قَالَ: قُلْتُ: لَا. قَالَتْ: نِصْفُ أُوقِيَّةٍ. فَتِلْكَ خَمْسُمِائَةِ دِرْهَمٍ، فَهَذَا صَدَاقُ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لِأَزْوَاجِهِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Salamah bin ‘Abdir-Rahmaan[3] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nilimuuliza ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) mahari ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ilikuwa kiasi gani?[4] Akasema: Mahari ya wakeze yalikuwa ni wakia kumi na mbili na An-Nash. Akasema: Unajua ni nini An-Nash? Akasema Hapana. Akasema: ni nusu wakia. Kwa hivyo hizo ni dirhamu mia tano (500) haya ndiyo mahari ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kwa wakeze.” [Imetolewa na Muslim]
881.
وَعَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ : {لَمَّا تَزَوَّجَ عَلِيٌّ فَاطِمَةَ عَلَيْهِمَا اَلسَّلَامُ . قَالَ لَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " أَعْطِهَا شَيْئًا " ، قَالَ: مَا عِنْدِي شَيْءٌ . قَالَ:" فَأَيْنَ دِرْعُكَ الحُطَمِيَّةُ ؟} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “’Aliy alipomuoa Faatwimah عَلَيْهِمَا اَلسَّلَامُ, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuambia: Mpe kitu (kama mahari yake), ‘Aliy akasema: Sina kitu, Rasuli wa Allaah akasema: Iko wapi ile deraya yako ya Al-Hutwamiyyah?.”[5] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na akaisahihisha Al-Haakim]
882.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَيُّمَا اِمْرَأَةٍ نَكَحَتْ عَلَى صَدَاقٍ، أَوْ حِبَاءٍ، أَوْ عِدَةٍ، قَبْلَ عِصْمَةِ اَلنِّكَاحِ، فَهُوَ لَهَا، وَمَا كَانَ بَعْدَ عِصْمَةِ اَلنِّكَاحِ، فَهُوَ لِمَنْ أُعْطِيَهُ، وَأَحَقُّ مَا أُكْرِمَ اَلرَّجُلُ عَلَيْهِ اِبْنَتُهُ، أَوْ أُخْتُهُ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke yeyote anayeolewa kwa mahari, zawadi au kwa ahadi ya kupewa zawadi kabla ya kifungo cha ndoa, basi kitu hicho ni chake.[6] Na kinachotolewa baada ya kifungo cha ndoa hicho ni cha aliyepewa. Na kilicho haki zaidi mtu kukirimiwa kwa sababu yake ni binti yake au dada yake.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy.
883.
وَعَنْ عَلْقَمَةَ، عَنِ ابْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ { أَنَّهُ سُئِلَ عَنْ رَجُلٍ تَزَوَّجَ اِمْرَأَةً، وَلَمْ يَفْرِضْ لَهَا صَدَاقًا، وَلَمْ يَدْخُلْ بِهَا حَتَّى مَاتَ، فَقَالَ اِبْنُ مَسْعُودٍ: لَهَا مِثْلُ صَدَاقِ نِسَائِهَا، لَا وَكْسَ، وَلَا شَطَطَ، وَعَلَيْهَا اَلْعِدَّةُ، وَلَهَا اَلْمِيرَاثُ، فَقَامَ مَعْقِلُ بْنُ سِنَانٍ الْأَشْجَعِيُّ فَقَالَ: قَضَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي بِرْوَعَ بِنْتِ وَاشِقٍ اِمْرَأَةٍ مِنَّا مِثْلَ مَا قَضَيْتَ، فَفَرِحَ بِهَا اِبْنُ مَسْعُودٍ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَالْجَمَاعَةُ
Kutoka kwa ‘Alqamah[7] naye kutoka kwa Ibn Mas ‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) aliulizwa: “kuhusu mtu aliyeoa mke, hakumkadiria mahari, wala hakumuingilia hadi akafa. Ibn Mas‘uwd akasema: ana mfano wa mahari ya wanawake wake, hakuna kupunguza wala kuzidisha, naye (mwanamke) itamlazimu akae eda na pia anastahiki kupata mirathi. Ma’qil bin Sinaan Al-Ashja’iyy akasimama na akasema: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihukumu kwa Birwa’[8] bint Waashiq ni mwanamke miongoni mwetu kama hivyo ulivyo hukumu wewe. Ibn Mas-‘uwd akafurahi kwa ushahidi huu.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy na ‘Ulamaa
884.
وَعَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: { مَنْ أَعْطَى فِي صَدَاقِ اِمْرَأَةٍ سَوِيقًا، أَوْ تَمْرًا، فَقَدْ اِسْتَحَلَّ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَأَشَارَ إِلَى تَرْجِيحِ وَقْفِهِ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye kutoa Sawiyq[9] au tende katika mahari ya mwanamke basi amekuwa halaal kwake mwanamke huyo.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd]
885.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَامِرِ بْنِ رَبِيعَةَرَضِيَ اللهُ عَنْهُ ، عَنْ أَبِيهِ {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَجَازَ نِكَاحَ اِمْرَأَةٍ عَلَى نَعْلَيْنِ} أَخْرَجَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ، وَخُولِفَ فِي ذَلِكَ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Aamir bin Rabiy’ah[10] kutoka kwa baba yake (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) Ameruhusu mwanamke kuolewa kwa (mahari ya) viatu.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha na amekhalifiwa katika hilo (la kufanya Hadiyth kuwa ni sahihi)
886.
وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ قَالَ: {زَوَّجَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ رَجُلاً اِمْرَأَةً بِخَاتَمٍ مِنْ حَدِيدٍ} أَخْرَجَهُ اَلْحَاكِمُ.
وَهُوَ طَرَفٌ مِنَ الْحَدِيثِ اَلطَّوِيلِ اَلْمُتَقَدِّمِ فِي أَوَائِلِ اَلنِّكَاحِ
Kutoka kwa Sahl bin Sa’d (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuoza mtu mwanamke kwa (mahari ya) pete ya chuma.” [Imetolewa na Al-Haakim nayo ni sehemu katika Hadiyth ndefu iliyotangulia mwanzo wa Mlango wa Ndoa][11]
887.
وَعَنْ عَلَيٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {لَا يَكُونُ اَلْمَهْرُ أَقَلَّ مِنْ عَشَرَةِ دَرَاهِمَ} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ مَوْقُوفًا، وَفِي سَنَدِهِ مَقَالٌ
Kutoka kwa ‘Aliy (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mahari haiwi chini ya dirhamu kumi.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy ikiwa ni Mawquwf na katika Isnaad yake kuna maelezo]
888.
وَعَنْ عُقْبَةَ بْنِ عَامِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {خَيْرُ اَلصَّدَاقِ أَيْسَرُهُ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Uqbah bin ‘Aamir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mahari yalio na kheri ni yalio mepesi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Al-Haakim]
889.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ عَمْرَةَ بِنْتَ اَلْجَوْنِ تَعَوَّذَتْ مِنْ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ حِينَ أُدْخِلَتْ عَلَيْهِ تَعْنِي: لَمَّا تَزَوَّجَهَا فَقَالَ: "لَقَدْ عُذْتِ بِمَعَاذٍ"، فَطَلَّقَهَا، وَأَمَرَ أُسَامَةَ فَمَتَّعَهَا بِثَلَاثَةِ أَثْوَابٍ} أَخْرَجَهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَفِي إِسْنَادِهِ رَاوٍ مَتْرُوكٌ
وَأَصْلُ اَلْقِصَّةِ فِي "اَلصَّحِيحِ" مِنْ حَدِيثِ أَبِي أُسَيْدٍ اَلسَّاعِدِيِّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “’Amrah bint Al-Jawn alijilinda dhidi ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wakati alipoingia kwake (siku aliyomuoa). Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Kwa hakika umejilinda kwa kinga. Akamtaliki na akamuamrisha Usaamah ampe (mwanamke yule) nguo tatu.” [Imetolewa na Ibn Maajah na katika Isnaad yake kuna mpokezi anayeachwa. Asili ya kisa chenyewe kimo katika Swahiyh Al-Bukhaariy kutoka katika Hadiyth ya Abuu Usayd As-Saa’idiy]
[1] Huyu ni Mama wa Waumini Swafiyyah bint Huyai bin Al-Akhtwab, ni kutoka katika kizazi cha Nabiy Haaruwn. Mwanzoni alikuwa ameolewa na Kinaanah bin Abdil-Huqaiq ambaye aliuwawa katika vita vya Khaybar. Swafiyyah alitekwa, kisha Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimchagua kuwa mke wake na akasilimu. Aliachwa huru na uhuru wake ndiyo iliyokuwa mahari yake. Alifariki mwaka 50 Hijriyyah na alizikwa katika makaburi ya Baqi’
[2] Hii ina maana mahari inaweza kuwa kitu kisichokuwa fedha.
[3] Huyu ni Abuu Salamah bin ‘Abdir-Rahmaan bin ‘Awf Az-Zuhri Al-Qurayshiy. Huyu ni mmoja katika Mafuqahaa saba wakubwa katika mji wa Madiynah na ni miongoni mwa Taabii’ wakubwa. Ni madhubuti na amepokea Hadiyth nyingi ambazo alizisikia kutoka katika makundi mbalimbali ya Maswahaba na kutoka kwa waliopokea kutoka kwake. Alifariki mwaka 94 au 104 katika mapokezi mengine akiwa na umri wa miaka 70.
[4] Hakuna kiwango maalumu cha mahari katika Shariy’ah, hata hivyo kuifanya ndogo zaidi kunapendeza, ili kuifanya ndoa kuwa ni nyepesi kwa watu wengi.
[5] Ni deraya iliyotengenezwa na watu wa kabila la Al-Hutwamah, walikuwa mahodari wa kutengeneza maderaya ya kivita. Hadiyth hii ni dalili kuwa bwana arusi anatakiwa ampe mkewe kitu kabla ya kumuingilia.
[6] Hii ina maana kila kilichoamuliwa kabla ya ndoa ni mahari, na yote yanakuwa ni ya muolewa. Ikiwa zawadi hiyo ni ya fedha, dhahabu, nguo, ardhi, nyumba au kitu kingine chochote, yeye ndiye mmiliki kamili wa kitu hicho. Ikiwa kuna kitu chochote watakachopewa jamaa za binti baada ya kuolewa kwake, hilo halitazingatiwa kuwa ni mahari, na si milki ya binti. Ni zawadi aliyopewa mtu tu.
[7] Huyu ni ‘Alqamah bin Qays Abu Shibl bin Maalik katika kabila la Banu Bakr bin An-Nakha, amepokea Hadiyth nyingi kutoka kwa ‘Umar na Ibn Mas-‘uwd. Alikuwa ni Taabi’ mkubwa, alikuwa maarufu kwa Hadiyth ya Abdullaah bin Mas‘uwd na kuwa na usuluba naye, alikuwa ni mjomba wa Al-Aswad bin An-Nakahi alifariki mwaka 61 Hijriyyah.
[8] Jina hili la Birwa’ lina ikhtilafu kwa Wanazuoni wa lugha ambao wao humuita Barwa’ na Wanazuoni wa Hadiyth humuita Birwa’
[9] Sawiyq ni unga wa mtama au wa mahindi au wa shayiri uliokaangwa.
[10] Huyu ni Abuu ‘Imraan ‘Abdillaah bin ‘Aamir bin Rabiy’ah Al-Anzi. Alikuwa ni mwenye umri wa miaka minne au mitano pindi Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipofariki. Alifariki mwaka wa 85 Hijriyyah.
[11] Tazama Hadiyth ya 832.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْوَلِيمَةِ
04-Mlango Wa Waliymah (Karamu Ya Harusi)
890.
عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ رَأَى عَلَى عَبْدِ اَلرَّحْمَنِ بْنِ عَوْفٍ أَثَرَ صُفْرَةٍ، قَالَ: {" مَا هَذَا؟ "، قَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنِّي تَزَوَّجْتُ اِمْرَأَةً عَلَى وَزْنِ نَوَاةٍ مِنْ ذَهَبٍ. فَقَالَ: " فَبَارَكَ اَللَّهُ لَكَ، أَوْلِمْ وَلَوْ بِشَاةٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِمُسْلِمٍ
Kutoka kwa Anas bin Maalik (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ): “Alimuona ‘Abdir-Rahmaan bin ‘Awf ana athari ya manukato ya zafarani, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Una jambo gani? Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nimeoa mwanamke (fulani) kwa uzito wa kokwa ya dhahabu.[1] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Allaah Akubarikie. Fanya waliymah (karamu) japo mbuzi.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
891.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا دُعِيَ أَحَدُكُمْ إِلَى اَلْوَلِيمَةِ فَلْيَأْتِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِمُسْلِمٍ:{إِذَا دَعَا أَحَدُكُمْ أَخَاهُ، فَلْيُجِبْ، عُرْسًا كَانَ أَوْ نَحْوَهُ}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapoalikwa mmoja wenu katika waliymah (karamu) aende.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah ya Muslim inasema: “Mmoja wenu anapomualika nduguye ajibu (aende) iwe ni harusi au mfano wake.”[2]
892.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {شَرُّ اَلطَّعَامِ طَعَامُ اَلْوَلِيمَةِ: يُمْنَعُهَا مَنْ يَأْتِيهَا، وَيُدْعَى إِلَيْهَا مَنْ يَأْبَاهَا، وَمَنْ لَمْ يُجِبِ اَلدَّعْوَةَ فَقَدْ عَصَى اَللَّهَ وَرَسُولَهُ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Chakula kibaya ni chakula cha waliymah (karamu ya harusi) kinanyimwa anayekiendea na hualikwa anayekikataa. Na asiyejibu mualiko atakuwa amemuasi Allaah na Rasuli wake.” [Imetolewa na Muslim]
893.
وَعَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا دُعِيَ أَحَدُكُمْ فَلْيُجِبْ، فَإِنْ كَانَ صَائِمًا فَلْيُصَلِّ، وَإِنْ كَانَ مُفْطِرًا فَلْيُطْعَمْ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ أَيْضًا
وَلَهُ مِنْ حَدِيثِ جَابِرٍ نَحْوُهُ. وَقَالَ:{فَإِنْ شَاءَ طَعِمَ وَإِنْ شَاءَ تَرَكَ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Anapoalikwa mmoja wenu aitike, akiwa ana swawm aombe du’aa na akiwa hana swawm basi ale.” [Imetolewa na Muslim]
Vile vile Muslim amepokea kutoka katika Hadiyth ya Jaabir kama hiyo na akasema: “Akipenda atakula na akipenda ataacha”
894.
وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {طَعَامُ الْوَلِيمَةِ أَوَّلَ يَوْمٍ حَقٌّ، وَطَعَامُ يَوْمِ اَلثَّانِي سُنَّةٌ، وَطَعَامُ يَوْمِ اَلثَّالِثِ سُمْعَةٌ، وِمَنْ سَمَّعَ سَمَّعَ اللهُ بِهِ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ وَاسْتَغْرَبَهُ، وَرِجَالُهُ رِجَالُ اَلصَّحِيحِ
وَلَهُ شَاهِدٌ: عَنْ أَنَسٍ عِنْدَ اِبْنِ مَاجَهْ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Chakula cha waliymah (karamu) siku ya kwanza ni haki, chakula cha siku ya pili ni Sunnah, na chakula cha siku ya tatu ni riyaa. Mwenye kuidhihirisha amali yake kwa riyaa Allaah Atamfedhehesha Siku ya Qiyaamah.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy]
895.
وَعَنْ صَفِيَّةَ بِنْتِ شَيْبَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ:{أَوْلَمَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَلَى بَعْضِ نِسَائِهِ بِمُدَّيْنِ مِنْ شَعِيرٍ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Swafiyyah bint Shaybah[3] (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alifanya waliymah (karamu) alipomuowa mmoja katika wakeze kwa pishi mbili za shayiri.”[4] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
896.
وَعَنْ أَنَسٍ قَالَ: {أَقَامَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ بَيْنَ خَيْبَرَ وَالْمَدِينَةِ ثَلَاثَ لَيَالٍ، يُبْنَى عَلَيْهِ بِصَفِيَّةَ، فَدَعَوْتُ اَلْمُسْلِمِينَ إِلَى وَلِيمَتِهِ، فَمَا كَانَ فِيهَا مِنْ خُبْزٍ وَلَا لَحْمٍ، وَمَا كَانَ فِيهَا إِلَّا أَنْ أَمَرَ بِالْأَنْطَاعِ، فَبُسِطَتْ، فَأُلْقِيَ عَلَيْهَا اَلتَّمْرُ، وَالْأَقِطُ، وَالسَّمْنُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Anas amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikaa siku tatu baina ya Khaybar na Madiynah akimkamilishia Swafiyyah ndoa yake. Nikawaalika Waislamu katika waliymah (karamu) yake, hakukuwa na mkate wala nyama. Akaamrisha iletwe busati la ngozi likatandikwa ikawekwa juu yake tende, aqitw[5] na samli.” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
897.
وَعَنْ رَجُلٍ مِنْ أَصْحَابِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ:{إِذَا اِجْتَمَعَ دَاعِيَانِ، فَأَجِبْ أَقْرَبَهُمَا بَابًا، فَإِنْ سَبَقَ أَحَدُهُمَا فَأَجِبِ اَلَّذِي سَبَقَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَسَنَدُهُ ضَعِيفٌ
Kutoka kwa mtu mmoja katika Maswahaba amehadithia kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Wanapojumuika waalikaji wawili nenda kwa yule ambaye mlango wake uko karibu zaidi (nawe), mmoja kati yao atakapotangulia (kukualika) nenda kwa yule aliyetangulia.”[6] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Isnaad yake ni dhaifu]
898.
وَعَنْ أَبِي جُحَيْفَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا آكُلُ مُتَّكِئًا} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Abuu Juhayfah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mimi sili nikiwa nimeegemea.”[7] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
899.
وَعَنْ عُمَرَ بْنِ أَبِي سَلَمَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {يَا غُلَامُ! سَمِّ اَللَّهَ، وَكُلْ بِيَمِينِكَ، وَكُلْ مِمَّا يَلِيكَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Umar bin Abuu Salamah[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Ee kijana! Mtaje Allaah, na kula kwa mkono wako wa kuume, na kula kinachokuelekea.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
900.
وَعَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أُتِيَ بِقَصْعَةٍ مِنْ ثَرِيدٍ، فَقَالَ: "كُلُوا مِنْ جَوَانِبِهَا، وَلَا تَأْكُلُوا مِنْ وَسَطِهَا، فَإِنَّ اَلْبَرَكَةَ تَنْزِلُ فِي وَسَطِهَا} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَهَذَا لَفْظُ النَّسَائِيِّ، وَسَنَدُهُ صَحِيحٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliletewa sahani ya thariyd[9] akasema: kuleni kando yake wala msile katikati yake, kwa hakika Baraka huteremka kati kati yake“ [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na tamshi hili ni la An-Nisaaiy na Isnaad yake ni Swahiyh]
901.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {مَا عَابَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ طَعَامًا قَطُّ، كَانَ إِذَا اِشْتَهَى شَيْئًا أَكَلَهُ، وَإِنْ كَرِهَهُ تَرَكَهُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hajapatapo kamwe hakukiaibisha chakula, alikuwa akitamani kitu hula na asipokipenda hukiacha.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
902.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ، عَنْ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا تَأْكُلُوا بِالشِّمَالِ، فَإِنَّ اَلشَّيْطَانَ يَأْكُلُ بِالشِّمَالِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Msile kwa kushoto, hakika shaytwaan hula kwa kushoto.” [Imetolewa na Muslim]
903.
وَعَنْ أَبِي قَتَادَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِذَا شَرِبَ أَحَدُكُمْ، فَلَا يَتَنَفَّسْ فِي اَلْإِنَاءِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَلِأَبِي دَاوُدَ: عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ نَحْوُهُ، وَزَادَ: {أَوْ يَنْفُخْ فِيهِ} وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Abuu Qataadah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Yeyote kati yenu anapokunywa asipumue ndani ya chombo.”[10] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na Abuu Daawuwd amepokea Riwaayah kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas Hadiyth kama hii na akaongezea: “…wala asipumulie humo.” [Na ameisahihisha At-Tirmidhiy]
[1] Nawaah ya dhahabu ni takribani gramu 18.4 za dhahabu
[2] Kujibu mwito wa sherehe ya harusi au jambo lingine ni wajibu, isipokuwa kuwe kuna yenye kuchukiza, hapo haifai kwenda. Na iwapo atenda na akaona chukizo hilo anawajibika kuukanya, wasipokatazika wanapaswa waondoke.
[3] Huyu ni Swafiyyah bint Shaybah bin ‘Uthmaan bin Abiy Twalhah Al-‘Abadariy wa ukoo wa Banuu ‘Abdid-Daar. Inasemekana kuwa alimuona Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wakati wengine wanakataa hilo. Ibn Sa’d anakiri kuwa alikuwa Taabi’iy
[4] Shayiri nafaka inayofanana na ngano inayotumika kuwa chakula
[5] Aqitw ni maziwa yaliyogandishwa kwa moto
[6] Hadiyth hii ni dalili kuwa mtu anapoalikwa na watu wawili kwa pamoja basi aliye na haki ya kujibiwa ni yule aliyetangulia, wakilingana katika hilo atatangulizwa jirani. Na majirani wako kwa daraja, mwenye haki zaidi ni yule ambaye mlango wake uko karibu zaidi na mlango wako, wakilingana kwa hilo itapigwa kura.
[7] Al-Khatwabi amesema: “Makusudio ya ‘kuegemea’ katika Hadiyth hii ni kuketi juu ya tandiko laini kama yule aliyekusudia kula sana bali alikuwa akiketi bila kujituliza (ili asile sana) na huwa akila kidogo.” Wengine wamesema kuwa ‘kuegemea’ ni mtu kula kwa kuegemea kwa ubavu wake.
[8] ‘Umar bin Abiy Salamah ‘Abdillaah bin ‘Abdil-Asad bin Hilaal Al-Makhzuwm, alikuwa ni mtoto wa Ummul-Muuminiyna Ummu Salamah. Alizaliwa katika nchi ya Uhabeshi (Ethiopia) baina ya Hijrah ya Uhabeshi na ile ya Madiynah. Alifariki katika mji wa Madiynah mwaka 83 Hijriyyah.
[9] ‘Thariyd’, ni mikate mepesi mikavu inayopikwa kwa unga wa shayiri (talbiynah/barley) na inakatwakatwa na kuchanganywa na supu ya nyama au mchuzi. Inasemekana ni chakula tokea zama za Nabiy Ibraahiym ('Alayhis-Salaam) mpaka zama za Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Ni chakula waliokuwa wakikaribishwa Hujaji wa Makkah kabla ya Uislamu.
[10] Hii ina maana ni pale anapokunywa mtu asipumulie kwenye chombo, kwani ni sababu ya kueneza magonjwa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْقَسْمِ
05-Mlango Wa Kugawa (Zamu)
904.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقْسِمُ، فَيَعْدِلُ، وَيَقُولُ: "اَللَّهُمَّ هَذَا قَسْمِي فِيمَا أَمْلِكُ، فَلَا تَلُمْنِي فِيمَا تَمْلِكُ وَلَا أَمْلِكُ} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ، وَلَكِنْ رَجَّحَ اَلتِّرْمِذِيُّ إِرْسَالَه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akigawa muda baina ya wakeze, na akifanya uadilifu na anasema: Ee Allaah! Huu ni mgao wangu[1] katika ninachokimiliki, usinilaumu kwa kile unachomiliki nami sikimiliki.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisa Ibn Hibbaan na Al-Haakim, lakini At-Tirmidhiy ametilia nguvu kuwa ni Mursal]
905.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ كَانَتْ لَهُ اِمْرَأَتَانِ، فَمَالَ إِلَى إِحْدَاهُمَا، جَاءَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ وَشِقُّهُ مَائِلٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَسَنَدُهُ صَحِيح
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye wake wawili, na akaegemea zaidi kwa mmojawapo,[2] Siku ya Qiyaamah atakuja ilhali ubavu wake mmoja umeinama.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na Isnaad yake ni sahihi]
906.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ:{مِنَ اَلسُّنَّةِ إِذَا تَزَوَّجَ اَلرَّجُلُ اَلْبِكْرَ عَلَى اَلثَّيِّبِ أَقَامَ عِنْدَهَا سَبْعًا، ثُمَّ قَسَمَ، وَإِذَا تَزَوَّجَ اَلثَّيِّبَ أَقَامَ عِنْدَهَا ثَلَاثًا، ثُمَّ قَسَمَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Katika Sunnah (mtu) anapooa mwanamwali juu ya mke mkuu akalale kwake siku saba kisha agawanye (siku). Na anapooa mke mkuu akae kwake siku tatu kisha agawanye (siku).” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
907.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لَمَّا تَزَوَّجَهَا أَقَامَ عِنْدَهَا ثَلَاثًا، وَقَالَ: "إِنَّهُ لَيْسَ بِكِ عَلَى أَهْلِكِ هَوَانٌ، إِنْ شِئْتِ سَبَّعْتُ لَكِ، وَإِنْ سَبَّعْتُ لَكِ سَبَّعْتُ لِنِسَائِي} رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipomuoa alikaa kwake siku tatu na akamuambia: Hutapata udhalilifu kwangu, nikipenda nitakukamilishia siku saba na iwapo nitakukamilishia siku saba vile vile nitawakamilishia wake zangu wote siku saba.” [Imetolewa na Muslim]
908.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ سَوْدَةَ بِنْتَ زَمْعَةَ وَهَبَتْ يَوْمَهَا لِعَائِشَةَ، وَكَانَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقْسِمُ لِعَائِشَةَ يَوْمَهَا وَيَوْمَ سَوْدَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Sawdah bint Zam’ah aliitoa siku yake[3] kumpa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akimgawia ‘Aaishah siku yake na siku ya Sawdah.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
909.
وَعَنْ عُرْوَةَ قَالَ: {قَالَتْ عَائِشَةُ: يَا اِبْنَ أُخْتِي! كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لَا يُفَضِّلُ بَعْضَنَا عَلَى بَعْضٍ فِي اَلْقَسْمِ مِنْ مُكْثِهِ عِنْدَنَا، وَكَانَ قَلَّ يَوْمٌ إِلَّا وَهُوَ يَطُوفُ عَلَيْنَا جَمِيعًا، فَيَدْنُو مِنْ كُلِّ اِمْرَأَةٍ مِنْ غَيْرِ مَسِيسٍ، حَتَّى يَبْلُغَ اَلَّتِي هُوَ يَوْمُهَا، فَيَبِيتَ عِنْدَهَا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
وَلِمُسْلِمٍ: عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ إِذَا صَلَّى اَلْعَصْرَ دَارَ عَلَى نِسَائِهِ، ثُمَّ يَدْنُو مِنْهُنَّ} اَلْحَدِيث
Kutoka kwa ‘Urwah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “’Aaishah aliniambia: Ee mpwa wangu! Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa hamfadhilishi yeyote miongoni mwetu katika mgawo wa kukaa kwake kwetu. Alikuwa akitutembelea sisi sote, akimkaribia kila mke bila ya kufanya jimai mpaka afike kwa yule ambaye ni siku yake[4] akalala kwake.” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na matini ya Hadiyth ni yake, na akaisahihisha Al-Haakim]
Na katika Riwaayah ya Muslim kutoka kwa ‘Aaishah inasema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) anapomaliza kuswali alasiri akiwazungukia wakeze na akiwakaribia (kwa kuwabusu na kuwakumbatia)...” Mpaka mwisho wa Hadiyth
910.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ يَسْأَلُ فِي مَرَضِهِ اَلَّذِي مَاتَ فِيهِ: " أَيْنَ أَنَا غَدًا ؟ "، يُرِيدُ: يَوْمَ عَائِشَةَ، فَأَذِنَ لَهُ أَزْوَاجُهُ يَكُونُ حَيْثُ شَاءَ، فَكَانَ فِي بَيْتِ عَائِشَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa katika maradhi yake aliyofia alikuwa akiuliza: “Kesho nitakuwa wapi?”[5] akikusudia siku ya ‘Aaishah. Wakeze wakamruhusu abaki pale anapopapenda. Akakaa katika nyumba ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
911.
وَعَنْهَا قَالَتْ:{كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ إِذَا أَرَادَ سَفَرًا أَقْرَعَ بَيْنَ نِسَائِهِ، فَأَيَّتُهُنَّ خَرَجَ سَهْمُهَا، خَرَجَ بِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa anataka kusafiri hupiga kura baina ya wakeze, yoyote atakayepata kura husafiri pamoja naye.”[6] [Al-Bukhaariy, Muslim]
912.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ زَمْعَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَجْلِدُ أَحَدُكُمْ اِمْرَأَتَهُ جَلْدَ اَلْعَبْدِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيّ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Zam’ah[7] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu asimpige mkewe kipigo cha mtumwa.”[8] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
[1] Haikuwa muhimu kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuenda kwa wake zake kwa zamu, pamoja na kuwa alikuwa na mapenzi zaidi kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا), lakini aliendelea kufanya uadilifu kwa wake zake wengine. Kila mara alimuomba Allaah Amsamehe.
[2] Katika hali hii uadilifu hapa unakusudiwa ni ule wa vitu na kuwahudumia kwa usawa katika mahitaji mengine na kutoa zamu. Yote haya mtu ana uwezo wa kuyafanya au kutoyafanya, na haya ndio ataulizwa kama ameyafanyia uadilifu. Kumpenda mtu na moyo kutekwa na mtu huyo si dhambi, maadamu halimzuii kufanya uadilifu.
[3] Hadiyth hii ina maana kwamba ikiwa mwanamke atakubaliwa mwenyewe kupunguziwa fedha zake za matumizi au zamu ya mumewe kwake, ni jambo linaloruhusiwa na mwanamme katika jambo hili si wa kulaumiwa, hata hivyo, ana haki ya kudai kurejeshewa haki yake wakati wowote.
[4] Hapa zamu inakusudiwa kulala kwake. Vinginevyo, mmoja anaweza kuruhusiwa kuongea na wengine na kuenda katika nyumba zao.
[5] Hii ina maana wakati wa ugonjwa wake, kuwepo kwa niyyah tu ya kubaki kwa mmoja sio tatizo. Hii ina maana ya ruhusa ya wake wengine, mtu anaweza kukaa kwa mmoja wao. Ugonjwa huu wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ulianzia kwa Maymwunah.
[6] Jina linalotokeza katika kura basi ndie wa kufuatana na Nabiy katika safari zake. Siku zote za safari hazihesabiwi katika zamu. Hata hivyo wake wanaweza kukubaliana wenyewe bila ya kuwepo kwa kura.
[7] Huyu ni ‘Abdullaah bin Zam’ah bin Al-Aswad bin ‘Abdil-Mutwalib bin Asad bin ‘Abdil-‘Uzza Al-Asadi, ni kaka wa Ummul Muuminiyna Sawdah bint Zam’ah. Alikuwa ni Swahaba mkubwa katika wakazi wa Madiynah. Aliuawa katika siku ya Ad-Daar.
[8] Ni haraam kumpiga mwanamke katika hali zozote isipokuwa moja tu la kufanya uzinifu. Haifai kumpiga usoni au kumpiga kiasi cha kumvunja, katika hali kama hiyo mume ataadhibiwa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْقَسْمِ
05-Mlango Wa Kugawa (Zamu)
904.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقْسِمُ، فَيَعْدِلُ، وَيَقُولُ: "اَللَّهُمَّ هَذَا قَسْمِي فِيمَا أَمْلِكُ، فَلَا تَلُمْنِي فِيمَا تَمْلِكُ وَلَا أَمْلِكُ} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ وَالْحَاكِمُ، وَلَكِنْ رَجَّحَ اَلتِّرْمِذِيُّ إِرْسَالَه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akigawa muda baina ya wakeze, na akifanya uadilifu na anasema: Ee Allaah! Huu ni mgao wangu[1] katika ninachokimiliki, usinilaumu kwa kile unachomiliki nami sikimiliki.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisa Ibn Hibbaan na Al-Haakim, lakini At-Tirmidhiy ametilia nguvu kuwa ni Mursal]
905.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {مَنْ كَانَتْ لَهُ اِمْرَأَتَانِ، فَمَالَ إِلَى إِحْدَاهُمَا، جَاءَ يَوْمَ اَلْقِيَامَةِ وَشِقُّهُ مَائِلٌ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَسَنَدُهُ صَحِيح
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwenye wake wawili, na akaegemea zaidi kwa mmojawapo,[2] Siku ya Qiyaamah atakuja ilhali ubavu wake mmoja umeinama.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na Isnaad yake ni sahihi]
906.
وَعَنْ أَنَسٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ:{مِنَ اَلسُّنَّةِ إِذَا تَزَوَّجَ اَلرَّجُلُ اَلْبِكْرَ عَلَى اَلثَّيِّبِ أَقَامَ عِنْدَهَا سَبْعًا، ثُمَّ قَسَمَ، وَإِذَا تَزَوَّجَ اَلثَّيِّبَ أَقَامَ عِنْدَهَا ثَلَاثًا، ثُمَّ قَسَمَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Katika Sunnah (mtu) anapooa mwanamwali juu ya mke mkuu akalale kwake siku saba kisha agawanye (siku). Na anapooa mke mkuu akae kwake siku tatu kisha agawanye (siku).” [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Al-Bukhaariy]
907.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لَمَّا تَزَوَّجَهَا أَقَامَ عِنْدَهَا ثَلَاثًا، وَقَالَ: "إِنَّهُ لَيْسَ بِكِ عَلَى أَهْلِكِ هَوَانٌ، إِنْ شِئْتِ سَبَّعْتُ لَكِ، وَإِنْ سَبَّعْتُ لَكِ سَبَّعْتُ لِنِسَائِي} رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipomuoa alikaa kwake siku tatu na akamuambia: Hutapata udhalilifu kwangu, nikipenda nitakukamilishia siku saba na iwapo nitakukamilishia siku saba vile vile nitawakamilishia wake zangu wote siku saba.” [Imetolewa na Muslim]
908.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ سَوْدَةَ بِنْتَ زَمْعَةَ وَهَبَتْ يَوْمَهَا لِعَائِشَةَ، وَكَانَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقْسِمُ لِعَائِشَةَ يَوْمَهَا وَيَوْمَ سَوْدَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Sawdah bint Zam’ah aliitoa siku yake[3] kumpa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa akimgawia ‘Aaishah siku yake na siku ya Sawdah.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
909.
وَعَنْ عُرْوَةَ قَالَ: {قَالَتْ عَائِشَةُ: يَا اِبْنَ أُخْتِي! كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لَا يُفَضِّلُ بَعْضَنَا عَلَى بَعْضٍ فِي اَلْقَسْمِ مِنْ مُكْثِهِ عِنْدَنَا، وَكَانَ قَلَّ يَوْمٌ إِلَّا وَهُوَ يَطُوفُ عَلَيْنَا جَمِيعًا، فَيَدْنُو مِنْ كُلِّ اِمْرَأَةٍ مِنْ غَيْرِ مَسِيسٍ، حَتَّى يَبْلُغَ اَلَّتِي هُوَ يَوْمُهَا، فَيَبِيتَ عِنْدَهَا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
وَلِمُسْلِمٍ: عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ إِذَا صَلَّى اَلْعَصْرَ دَارَ عَلَى نِسَائِهِ، ثُمَّ يَدْنُو مِنْهُنَّ} اَلْحَدِيث
Kutoka kwa ‘Urwah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “’Aaishah aliniambia: Ee mpwa wangu! Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alikuwa hamfadhilishi yeyote miongoni mwetu katika mgawo wa kukaa kwake kwetu. Alikuwa akitutembelea sisi sote, akimkaribia kila mke bila ya kufanya jimai mpaka afike kwa yule ambaye ni siku yake[4] akalala kwake.” [Imetolewa na Ahmad na Abuu Daawuwd na matini ya Hadiyth ni yake, na akaisahihisha Al-Haakim]
Na katika Riwaayah ya Muslim kutoka kwa ‘Aaishah inasema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) anapomaliza kuswali alasiri akiwazungukia wakeze na akiwakaribia (kwa kuwabusu na kuwakumbatia)...” Mpaka mwisho wa Hadiyth
910.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كَانَ يَسْأَلُ فِي مَرَضِهِ اَلَّذِي مَاتَ فِيهِ: " أَيْنَ أَنَا غَدًا ؟ "، يُرِيدُ: يَوْمَ عَائِشَةَ، فَأَذِنَ لَهُ أَزْوَاجُهُ يَكُونُ حَيْثُ شَاءَ، فَكَانَ فِي بَيْتِ عَائِشَةَ} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa katika maradhi yake aliyofia alikuwa akiuliza: “Kesho nitakuwa wapi?”[5] akikusudia siku ya ‘Aaishah. Wakeze wakamruhusu abaki pale anapopapenda. Akakaa katika nyumba ya ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
911.
وَعَنْهَا قَالَتْ:{كَانَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ إِذَا أَرَادَ سَفَرًا أَقْرَعَ بَيْنَ نِسَائِهِ، فَأَيَّتُهُنَّ خَرَجَ سَهْمُهَا، خَرَجَ بِهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuwa anataka kusafiri hupiga kura baina ya wakeze, yoyote atakayepata kura husafiri pamoja naye.”[6] [Al-Bukhaariy, Muslim]
912.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ زَمْعَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَجْلِدُ أَحَدُكُمْ اِمْرَأَتَهُ جَلْدَ اَلْعَبْدِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيّ
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Zam’ah[7] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu asimpige mkewe kipigo cha mtumwa.”[8] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
[1] Haikuwa muhimu kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuenda kwa wake zake kwa zamu, pamoja na kuwa alikuwa na mapenzi zaidi kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا), lakini aliendelea kufanya uadilifu kwa wake zake wengine. Kila mara alimuomba Allaah Amsamehe.
[2] Katika hali hii uadilifu hapa unakusudiwa ni ule wa vitu na kuwahudumia kwa usawa katika mahitaji mengine na kutoa zamu. Yote haya mtu ana uwezo wa kuyafanya au kutoyafanya, na haya ndio ataulizwa kama ameyafanyia uadilifu. Kumpenda mtu na moyo kutekwa na mtu huyo si dhambi, maadamu halimzuii kufanya uadilifu.
[3] Hadiyth hii ina maana kwamba ikiwa mwanamke atakubaliwa mwenyewe kupunguziwa fedha zake za matumizi au zamu ya mumewe kwake, ni jambo linaloruhusiwa na mwanamme katika jambo hili si wa kulaumiwa, hata hivyo, ana haki ya kudai kurejeshewa haki yake wakati wowote.
[4] Hapa zamu inakusudiwa kulala kwake. Vinginevyo, mmoja anaweza kuruhusiwa kuongea na wengine na kuenda katika nyumba zao.
[5] Hii ina maana wakati wa ugonjwa wake, kuwepo kwa niyyah tu ya kubaki kwa mmoja sio tatizo. Hii ina maana ya ruhusa ya wake wengine, mtu anaweza kukaa kwa mmoja wao. Ugonjwa huu wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ulianzia kwa Maymwunah.
[6] Jina linalotokeza katika kura basi ndie wa kufuatana na Nabiy katika safari zake. Siku zote za safari hazihesabiwi katika zamu. Hata hivyo wake wanaweza kukubaliana wenyewe bila ya kuwepo kwa kura.
[7] Huyu ni ‘Abdullaah bin Zam’ah bin Al-Aswad bin ‘Abdil-Mutwalib bin Asad bin ‘Abdil-‘Uzza Al-Asadi, ni kaka wa Ummul Muuminiyna Sawdah bint Zam’ah. Alikuwa ni Swahaba mkubwa katika wakazi wa Madiynah. Aliuawa katika siku ya Ad-Daar.
[8] Ni haraam kumpiga mwanamke katika hali zozote isipokuwa moja tu la kufanya uzinifu. Haifai kumpiga usoni au kumpiga kiasi cha kumvunja, katika hali kama hiyo mume ataadhibiwa.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْخُلْعِ
Mlango Wa Khul’[1]
913.
عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ اِمْرَأَةَ ثَابِتِ بْنِ قَيْسٍ أَتَتْ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! ثَابِتُ بْنُ قَيْسٍ مَا أَعِيبُ عَلَيْهِ فِي خُلُقٍ وَلَا دِينٍ، وَلَكِنِّي أَكْرَهُ اَلْكُفْرَ فِي اَلْإِسْلَامِ، قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " أَتَرُدِّينَ عَلَيْهِ حَدِيقَتَهُ؟ "، قَالَتْ: نَعَمْ. قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " اِقْبَلِ اَلْحَدِيقَةَ، وَطَلِّقْهَا تَطْلِيقَةً} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ .
وَفِي رِوَايَةٍ لَهُ: {وَأَمَرَهُ بِطَلَاقِهَا}
وَلِأَبِي دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيِّ وَحَسَّنَهُ:{أَنَّ اِمْرَأَةَ ثَابِتِ بْنِ قَيْسٍ اِخْتَلَعَتْ مِنْهُ، فَجَعَلَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عِدَّتَهَا حَيْضَةً}
وَفِي رِوَايَةِ عَمْرِوِ بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ عِنْدَ اِبْنِ مَاجَهْ: {أَنَّ ثَابِتَ بْنَ قَيْسٍ كَانَ دَمِيمًا وَأَنَّ اِمْرَأَتَهُ قَالَتْ: لَوْلَا مَخَافَةُ اَللَّهِ إِذَا دَخَلَ عَلَيَّ لَبَسَقْتُ فِي وَجْهِهِ}
وَلِأَحْمَدَ: مِنْ حَدِيثِ سَهْلِ بْنِ أَبِي حَثْمَةَ: {وَكَانَ ذَلِكَ أَوَّلَ خُلْعٍ فِي اَلْإِسْلَامِ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Mke wa Thaabit bin Qays[2] alimuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Thaabit bin Qays simtii kasoro katika tabia wala Dini lakini nachukia kukufuru nikiwa Muislamu. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Utamrudishia shamba lake?” Akasema: Ndio. Rasuli wa Allaah akasema: (kumwambia Thaabit): “Kubali shamba lako na umuache talaka moja.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Katika Riwaayah yake nyingine imesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuamrisha ampe talaka.”
Katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy ambayo imesema ni Hasan: “Mke wa Thaabit bin Qays alipewa talaka kwa kurudisha shamba, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaamuru Eda yake iwe ni kipindi kimoja cha hedhi.”
Katika Riwaayah iliyo kwa Ibn Maajah kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb amepokea kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake amesema: “Thaabit bin Qays alikuwa na sura mbaya, mkewe akasema: “Lau si kwa sababu ya kumuogopa Allaah, ningalimtemea mate usoni mwakwe wakati anapoingia!”
Ahmad amepokea kutoka Hadiyth ya Sahl bin Hathmah: “Hiyo ndiyo ilikuwa Khulu’ ya kwanza katika Uislamu.”
[1] Khulu’ maana yake kilugha ni kuvua nguo. Kulingana na Shariy’ah khulu’ ina maana ya haki aliyonayo mwanamke kuvunja ndoa. Ana haki ya kuvunja ndoa baada ya kurudisha mahari. Mtu anaweza kutoa talaka akiwa na sababu za msingi. Vivyo hivyo, mwanamke naye ana haki ya kujivua (khulu’) baada ya kurejesha mahari kama ana haki ya msingi. Kulingana na ‘Ulamaa wengine, Khulu’ ni talaka, wakati wengine wakiichukulia kuwa ni kuvunja ndoa. Kuna rai tofauti kuhusu kurudisha mahari na haswa ile ya awali. Hivyo kimsingi mwanamme hawezi kudai mahari makubwa kurejeshewa zaidi ya mahari ile aliyotoa ya asili.
[2] Thaabit bin Qays Al-Ansaar Al-Khazraj alikuwa mmoja wa Maswahaba wakubwa na alikuwa ni msemaji mkuu wa Answaar na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alishuhudia vita vya Uhud na vita vingine vilivyofuatia baada yake. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimthibitishia Jannah na aliuwawa katika vita vya Al-Yamaamah.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلطَّلَاقِ
07-Mlango Wa Talaka
914.
عَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {أَبْغَضُ اَلْحَلَالِ عِنْدَ اَللَّهِ اَلطَّلَاقُ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَرَجَّحَ أَبُو حَاتِمٍ إِرْسَالَهُ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Halali ichukizayo kwa Allaah ni talaka.”[1] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Ibn Maajah, na akaisahihisha Al-Haakim na Abuu Haatim anaiona kuwa ni Mursal]
915.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّهُ طَلَّقَ اِمْرَأَتَهُ وَهِيَ حَائِضٌ فِي عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَسَأَلَ عُمَرُ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ ذَلِكَ؟ فَقَالَ: " مُرْهُ فَلْيُرَاجِعْهَا ، ثُمَّ لْيُمْسِكْهَا حَتَّى تَطْهُرَ، ثُمَّ تَحِيضَ، ثُمَّ تَطْهُرَ، ثُمَّ إِنْ شَاءَ أَمْسَكَ بَعْدُ، وَإِنْ شَاءَ طَلَّقَ بَعْدَ أَنْ يَمَسَّ، فَتِلْكَ اَلْعِدَّةُ اَلَّتِي أَمَرَ اَللَّهُ أَنْ تُطَلَّقَ لَهَا اَلنِّسَاءُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: {مُرْهُ فَلْيُرَاجِعْهَا، ثُمَّ لْيُطَلِّقْهَا طَاهِرًا أَوْ حَامِلًا}
وَفِي رِوَايَةٍ أُخْرَى لِلْبُخَارِيِّ: {وَحُسِبَتْ عَلَيْهِ تَطْلِيقَةً}
وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ: قَالَ اِبْنُ عُمَرَ: {أَمَّا أَنْتَ طَلَّقْتَهَا وَاحِدَةً أَوْ اِثْنَتَيْنِ، فَإِنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَمَرَنِي أَنْ أُرَاجِعَهَا، ثُمَّ أُمْهِلَهَا حَتَّى تَحِيضَ حَيْضَةً أُخْرَى، وَأَمَّا أَنْتَ طَلَّقْتَهَا ثَلَاثًا، فَقَدْ عَصَيْتَ رَبَّكَ فِيمَا أَمَرَكَ مِنْ طَلَاقِ اِمْرَأَتِكَ}
وَفِي رِوَايَةٍ أُخْرَى: قَالَ عَبْدُ اَللَّهِ بْنُ عُمَرَ:{فَرَدَّهَا عَلَيَّ، وَلَمْ يَرَهَا شَيْئًا، وَقَالَ: " إِذَا طَهُرَتْ فَلْيُطَلِّقْ أَوْ لِيُمْسِكْ}
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Alimtaliki mkewe akiwa katika hedhi zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), ‘Umar akamuuliza Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) jambo hili. Akasema: “Muamrishe amrejee kisha akae naye mpaka atwaharike, halafu akipenda atakuwa naye, na kumuingilia. Hiyo ndiyo Eda aliyoiamrisha Allaah, wanawake waachwe namna hiyo.”[2] [Al-Bukhaariy, Muslim]
Katika Riwaayah nyengine ya Muslim inasema: “Muamrishe amrejee kisha amtaliki akiwa ni twahara au ana mimba.”
Katika Riwaayah nyengine ya Bukhaariy imesema: “…na itahesabiwa kuwa ni talaka moja.”
Katika Riwaayah nyengine ya Muslim kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (alimuambia muulizaji): “Ama wewe umemtaliki talaka moja au mbili, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliniamrisha nimrejee kisha niishi naye mpaka apate hedhi nyengine, kisha nimpe muda ili atwahirike, kisha nimtaliki kabla ya kumgusa (kumuingilia). Ama wewe umemuacha talaka tatu umemuasi Rabb wako katika Alivyokuamrisha kumtaliki mkeo.”
Katika Riwaayah nyengine imesema: “’Abdullaah Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) alisema: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamrudisha kwangu wala hakuihisabu hiyo kuwa ni talaka. Akasema: “Atakapotwahirika umtaliki au ubaki naye (akiwa ni mkewe).”
916.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {كَانَ اَلطَّلَاقُ عَلَى عَهْدِ رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَأَبِي بَكْرٍ، وَسَنَتَيْنِ مِنْ خِلَافَةِ عُمَرَ، طَلَاقُ اَلثَّلَاثِ وَاحِدَةٌ، فَقَالَ عُمَرُ بْنُ اَلْخَطَّابِ: إِنَّ اَلنَّاسَ قَدْ اِسْتَعْجَلُوا فِي أَمْرٍ كَانَتْ لَهُمْ فِيهِ أَنَاةٌ، فَلَوْ أَمْضَيْنَاهُ عَلَيْهِمْ؟ فَأَمْضَاهُ عَلَيْهِمْ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Katika zama za Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), Abuu Bakar na miaka miwili ya mwanzo wa Ukhalifa wa ‘Umar, talaka tatu zilikuwa ni moja.[3] ‘Umar akasema: “Hakika watu wanalifanyia haraka jambo ambalo ndani yake linatakiwa upole. Itakuwa bora tukiwapitishia.” Akawapitishia. [Imetolewa na Muslim]
917.
وَعَنْ مَحْمُودِ بْنِ لَبِيدٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ:{أُخْبِرَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ عَنْ رَجُلٍ طَلَّقَ اِمْرَأَتَهُ ثَلَاثَ تَطْلِيقَاتٍ جَمِيعًا، فَقَامَ غَضْبَانَ ثُمَّ قَالَ: "أَيُلْعَبُ بِكِتَابِ اَللَّهِ تَعَالَى، وَأَنَا بَيْنَ أَظْهُرِكُمْ" حَتَّى قَامَ رَجُلٌ، فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَلَا أَقْتُلُهُ؟} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ وَرُوَاتُهُ مُوَثَّقُونَ
Kutoka kwa Mahmuwd bin Labiyd[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliambiwa kuhusu mtu aliyemtaliki mkewe talaka tatu pamoja, akasimama kwa hasira akasema: “Kitabu cha Allaah kinachezewa nami niko miongoni mwenu?” Mtu mmoja akasimama na akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Waonaje nikamuua?” [Imetolewa na An-Nasaaiy na wapokezi wake ni madhubuti]
918.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {طَلَّقَ أَبُو رُكَانَةَ أُمَّ رُكَانَةَ . فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " رَاجِعِ امْرَأَتَكَ"، فَقَالَ: إِنِّي طَلَّقْتُهَا ثَلَاثًا. قَالَ: " قَدْ عَلِمْتُ، رَاجِعْهَا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ
وَفِي لَفْظٍ لِأَحْمَدَ: {طَلَّقَ أَبُو رُكَانَةَ اِمْرَأَتَهُ فِي مَجْلِسٍ وَاحِدٍ ثَلَاثًا، فَحَزِنَ عَلَيْهَا، فَقَالَ لَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ " فَإِنَّهَا وَاحِدَةٌ} وَفِي سَنَدِهَا اِبْنُ إِسْحَاقَ، وَفِيهِ مَقَالٌ
وَقَدْ رَوَى أَبُو دَاوُدَ مِنْ وَجْهٍ آخَرَ أَحْسَنَ مِنْهُ:{أَنَّ رُكَانَةَ طَلَّقَ اِمْرَأَتَهُ سُهَيْمَةَ اَلْبَتَّةَ، فَقَالَ: "وَاَللَّهِ مَا أَرَدْتُ بِهَا إِلَّا وَاحِدَةً، فَرَدَّهَا إِلَيْهِ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اَللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Abuu Rukaanah alimtaliki Ummu Rukaanah. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Mrudie mkeo”. Abuu Rukaanah akamuambia: “Nimemtaliki talaka tatu.” Akamuambia: “Najua mrejee (mkeo).” [Imetolewa na Abuu Daawuwd]
Katika tamshi lingine la Ahmad imesema: “Abuu Rukaanah alimtaliki mkewe talaka tatu katika kikao kimoja, halafu akahuzunika kule kumtaliki mkewe. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Hiyo ni talaka moja.” Katika Isnaad zake kuna Ibn Ishaaqa[5] ambaye ndani yake kuna maelezo.
Abuu Daawuwd amepokea kwa njia nyengine bora zaidi kuliko hiyo ikisema: “Abuu Rukaanah alimtaliki mkewe anayeitwa Suhaymah talaka isiyorudiwa akasema: “Wallaahi nimekusudia talaka moja tu.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamrudishia mkewe.
919.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {ثَلَاثٌ جِدُّهنَّ جِدٌّ، وَهَزْلُهُنَّ جِدٌّ: اَلنِّكَاحُ، وَالطَّلَاقُ، وَالرَّجْعَةُ} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
وَفِي رِوَايَةٍ لِابْنِ عَدِيٍّ مِنْ وَجْهٍ آخَرَ ضَعِيفٍ:{اَلطَّلَاقُ، وَالْعِتَاقُ، وَالنِّكَاحُ}
وَلِلْحَارِثِ اِبْنِ أَبِي أُسَامَةَ: مِنْ حَدِيثِ عُبَادَةَ بْنِ اَلصَّامِتِ رَفَعَهُ:{لَا يَجُوزُ اَللَّعِبُ فِي ثَلَاثٍ: اَلطَّلَاقُ، وَالنِّكَاحُ، وَالْعِتَاقُ، فَمَنْ قَالَهُنَّ فَقَدَ وَجَبْنَ} وَسَنَدُهُ ضَعِيفٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mambo matatu kweli yake ni kweli na mzaha wake ni kweli:[6] nikaah, talaka na kumrejea mke.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha Al-Haakim]
Na katika Riwaayah nyengine ya Ibn ‘Adiyy imepokewa kwa njia nyengine dhaifu: “…talaka, kuacha huru na ndoa.”
Al-Haarith Ibn Abuu Usaamah amepokea kutoka katika Hadiyth ya ‘Ubaadah bin Asw-Swaamit ambayo ni Marfuw’: “Haifai kufanya mchezo katika mambo matatu: talaka, ndoa na kuacha huru, atakayesema maneno hayo itakuwa imepasa.” Isnaad yake ni dhaifu.
920.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِنَّ اَللَّهَ تَجَاوَزَ عَنْ أُمَّتِي مَا حَدَّثَتْ بِهِ أَنْفُسَهَا، مَا لَمْ تَعْمَلْ أَوْ تَكَلَّمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Allaah Amesamehe Ummah wangu wanayoyazungumza nafsini mwao maadamu hawajatenda au kuyazungumza.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
921.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {إِنَّ اَللَّهَ تَعَالَى وَضَعَ عَنْ أُمَّتِي اَلْخَطَأَ، وَالنِّسْيَانَ، وَمَا اسْتُكْرِهُوا عَلَيْهِ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَالْحَاكِمُ، وَقَالَ أَبُو حَاتِمٍ: لَا يَثْبُتُ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kwa hakika Allaah Amewasamehe umati wangu kukosea, kusahau na walilolazimishwa.”[7] [Imetolewa na Ibn Maajah na Al-Haakim. Na akasamea Abuu Haatim kuwa ‘Haikuthibitu’
922.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {إِذَا حَرَّمَ اِمْرَأَتَهُ لَيْسَ بِشَيْءٍ} وَقَالَ : لَقَدْ كَانَ لَكُمْ فِي رَسُولِ اَللَّهِ أُسْوَةٌ حَسَنَةٌ رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
وَلِمُسْلِمٍ:{إِذَا حَرَّمَ اَلرَّجُلُ عَلَيْهِ اِمْرَأَتَهُ ، فَهِيَ يَمِينٌ يُكَفِّرُهَا}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Mtu anapojiharamishia mkewe[8] hakuna kitu.” Na akasema: “Kwa hakika mna mfano mzuri kwa Rasuli wa Allaah.”[9] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Na katika Riwaayah ya Muslim inasema: “Mtu anapojiharamishia mkewe hiyo ni yamini na ataitolea kafara.”
923.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا {أَنَّ اِبْنَةَ اَلْجَوْنِ لَمَّا أُدْخِلَتْ عَلَى رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَدَنَا مِنْهَا. قَالَتْ: أَعُوذُ بِاَللَّهِ مِنْكَ، قَالَ: "لَقَدْ عُذْتِ بِعَظِيمٍ، اِلْحَقِي بِأَهْلِكِ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: “Bint Al-Jawn alipoingizwa kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na akamkaribia (Amrah) alisema: “Najilinda kwa Allaah kwa sababu yako.” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Kwa hakika umejilinda kwa Mtukufu. Nenda kwa jamaa zako.”[10] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
924.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا طَلَاقَ إِلَّا بَعْدَ نِكَاحٍ، وَلَا عِتْقَ إِلَّا بَعْدَ مِلْكٍ} رَوَاهُ أَبُو يَعْلَى، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَهُوَ مَعْلُولٌ
وَأَخْرَجَ اِبْنُ مَاجَهْ: عَنِ اَلْمِسْوَرِ بْنِ مَخْرَمَةَ مِثْلَهُ، وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ، لَكِنَّهُ مَعْلُولٌ أَيْضًا
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna talaka ila baada ya ndoa, wala hakuna kuacha huru ila baada ya kumiliki.”[11] [Imetolewa na Abuu Ya’laa, na akaisahihisha Al-Haakim nayo ni Ma’luwl
Ibn Maajah amepokea Hadiyth kama hii kutoka kwa Al-Miswar bin Makhramah, sanad yake ni hasan lakini bado inabaki kuwa ni Ma’luwl (yenye ‘illah iliyojificha)
925.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ شُعَيْبٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ لَا نَذْرَ لِابْنِ آدَمَ فِيمَا لَا يَمْلِكُ، وَلَا عِتْقِ لَهُ فِيمَا لَا يَمْلِكُ، وَلَا طَلَاقَ لَهُ فِيمَا لَا يَمْلِكُ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَصَحَّحَهُ، وَنُقِلَ عَنْ اَلْبُخَارِيِّ أَنَّهُ أَصَحُّ مَا وَرَدَ فِيهِ
Kutoka kwa ‘Amr bin Shu’ayb kutoka kwa baba yake naye kutoka kwa babu yake amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna nadhiri kwa mwana Aadam katika asichomiliki, wala kuacha huru (mtumwa) katika asiyemmiliki, wala kutoa talaka asiyoimiliki.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy na wakaisahihisha.
Imenakiliwa kutoka kwa Bukhaariy kuwa Hadiyth hii ndio sahihi zaidi iliyopokewa katika mas-ala haya.
926.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {رُفِعَ اَلْقَلَمُ عَنْ ثَلَاثَةٍ: عَنِ اَلنَّائِمِ حَتَّى يَسْتَيْقِظَ، وَعَنِ اَلصَّغِيرِ حَتَّى يَكْبُرَ، وَعَنِ اَلْمَجْنُونِ حَتَّى يَعْقِلَ، أَوْ يَفِيقَ} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا اَلتِّرْمِذِيَّ وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kalamu zimeinuliwa kwa watu watatu:[12] aliyelala mpaka atakapoamka, mtoto mdogo mpaka atakapobaleghe na mwenda wazimu mpaka akili itakapomrudia.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Al-Haakim
[1] Hadiyth hii ina mafundisho mengi (kama ingethibitishwa kuwa ni Swahiyh). Kuwa siyo vitu vyote vilivyokuwa halaal vinapendezesha kwa Allaah, kwa mfano talaka ni jambo la halaal lakini siyo kila mara huwa ni jambo zuri. Ni halaal kwa kuwa katika mazingira mengine jambo linakuwa gumu na mtu kulazimishwa kuacha. Katika hali kama hizo, jambo hilo linakubaliwa, kama hakuna njia nyingine. Talaka ni kitu kisichokuwa kizuri, ni jambo linalopelekea uadui na ni furaha ya shaytwaan. Maana ya talaka ni kukiacha kitu huru kishariy’ah, na kumtoa mwanamke katika kifungo cha ndoa.
[2] Hadiyth hii nayo ina mafundisho kadhaa ndani yake: 1. Ni haraam kumuacha mwanamke akiwa katika hedhi, 2. Bila ushauri wa mwanamke, mtu anaweza kubadilisha uamuzi wake, 3. Ni Bid’ah kumuacha mwanamke katika hali ya Twuhr (ni pale mwanamke anapomaliza hedhi yake) ambapo ni ruhusa kufanya tendo la ndoa, ambapo ni sawa na wakati ule wa kumuacha akiwa na hedhi. Kuna aina nne za talaka, mbili katika hizo ni halaal na mbili zingine siyo halaal. Kumuacha wakati akiwa na mimba akiwa katika hali ya Twuhr ambapo kumuingilia hakuruhusiwi ni halaal, wakati kumuacha akiwa katika hedhi katika hali ya Twuhr ambapo huruhusiwa kumuingilia talaka ni haraam. Kwa upande mwingine kuna aina tatu za talaka: (i) Ahsan (ii) Hasan (iii) Bid’ah. Ahsan ni kumuacha tu pindi anapokuwa mjamzito au wakati wa Twuhr na kuacha eda ipite (eda ni muda uliopangwa wa kusubiri baada ya mwanamke kuachwa ambapo hawezi kuolewa, inatofautiana katika hali mbali mbali). Hasan ni kuacha mara tatu, katika ya tatu, katika nyakati tatu tofauti za Twuhr. Hadi talaka mbili au tohara mbili, mtu anaweza kuvunja talaka na kuoa tena. Akishatamka talaka ya tatu hawezi kuvunja talaka wala hawezi kumuoa tena mke wake aliyemuacha kabla ya kuolewa na mtu mwingine, ambaye inabidi amuingilie na ikija kutokea akaja kumuacha baadae ndipo anaweza kumuoa au afiwe na mumewe wa pili. Bid’ah ni talaka mbili au tatu kwa mara moja, ‘Ulamaa wengi wana rai kuwa talaka inayotolewa wakati wa hedhi huhesabiwa.
[3] Ni nini hukumu ya talaka tatu zinazotolewa mara moja? Kuna rai mbali mbali za ‘Ulamaa kuhusu suala hili. 1. Talaka tatu zinazotolewa mara moja na hazina nguvu zozote kishariy’ah. 2. Talaka tatu za mara moja zinahesabiwa na mwanamke anaachika. 3. Rai ya tatu ni kuwa talaka tatu zinazotolewa wakati mmoja zinazingatiwa kuwa ni talaka moja. 4. Rai ya nne ni kuwa ikiwa mwanamke alishaingiliwa, talaka zitahesabiwa, na kama hakuingiliwa, itakuwa ni moja tu. Miongoni mwa rai hizi rai ya tatu ndiyo yenye nguvu zaidi na inayoingia akilini zaidi. Hukumu hii ndiyo iliyokuwa wakati wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), hivyo basi Abuu Rukaanah aliamrishwa kumrudia mkewe baada ya kutoa talaka tatu kwa mara moja. Ingekuwa zile talaka tatu zingehesabiwa, basi Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) asingemuamrisha kumrudia mkewe. Aina hii ya talaka inaingia katika mantiki ya watu. Kwa talaka tatu, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) ameweka muda wa miezi mitatu.
[4] Mahmuwd bin Labiyd bin Abuu Rafi Al-Answaaar Al-Ash-hal. Alizaliwa katika zama za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ), ni Swahaba. Abuu Haatim amesema kuwa uswahaba wake haujulikani. Ama Imaam Muslim anamuona kuwa ni miongoni mwa Taabi’iyna. Alikuwa ni miongoni mwa ‘Ulamaa, alifariki mwaka wa 96 Hijriyyah.
[5] Huyu ni Abuu ‘Abdillaah Muhammad bin Ishaaq bin Yassar Al-Mutwalibi, muachwa huru wa Qayd bin Makhrama Al-Madani ambaye alikuwa ni mtaalamu katika historia na medani ya vita wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na Maswahaba zake. Alikufa mwaka 51 Hijriyyah.
[6] Kuwa vitu hivi vinne kwa namna vilivyo havifanyiwi mzaha navyo ni: 1. Ndoa, 2. Talaka, 3. Kutengua talaka, 4. Kumuacha huru mtumwa.
[7] Hii ina maana kufikiria tu talaka bila ya kutenda hakuhesabiwi. Hii ina maana vile vile talaka inayotolewa kwa kulazimishwa sio talaka. Vivyo hivyo, ndoa ya kulazimishwa nayo si ndoa.
[8] Ikiwa mtu atamuambia mke wake kuwa hataendelea na uhusiano naye na kujiharamishia mke wake haizingatiwi kuwa ni talaka bali ni kiapo ambacho kinabidi kilipiwe fidia.
[9] Mfano wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hapa ni pindi alipowagomea wake zake kwa muda fulani.
[10] Aina nyingine ya talaka imewekwa wazi katika Hadiyth hii, ambayo ni 1. Ushahidi na talaka ya wazi: katika hali hii hakuna haja ya nia kulingana na maneno kuwa wazi. Ni maneno pekee yanakamilisha talaka. 2. Iwe ni moja kwa moja au kwa kuashiria: katika hali hii maneno yanakuwa kwa mafumbo, na yanaweza kuwa hayana maana ya talaka. Kwa mfano: “uko huru” au “Nenda kwa wazazi wako” n.k. maneno kama haya yanapotolewa niyyah zao zitazingatiwa lakini siyo maneno yao. Ikiwa mzungumzaji ana maana ya talaka, basi itathibiti, na ikiwa hana niyyah hiyo basi haitothibitu.
[11] Hii ina maana kuwa mtu anaweza kumuacha mwanamke aliyemuoa tu.
[12] Hii ina maana ikiwa kuna aliyetoa talaka akiwa na usingizi talaka haiswihi. Kadhalika kichaa hatoi talaka, haitozingatiwa kuwa ni talaka.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلرَّجْعَةِ
08-Mlango Wa (Talaka Ya) Rejea
927.
عَنْ عِمْرَانَ بْنِ حُصَيْنٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُ، {أَنَّهُ سُئِلَ عَنْ اَلرَّجُلِ يُطَلِّقُ، ثُمَّ يُرَاجِعُ، وَلَا يُشْهِدُ؟ فَقَالَ: أَشْهِدْ عَلَى طَلَاقِهَا، وَعَلَى رَجْعَتِهَا} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ هَكَذَا مَوْقُوفًا، وَسَنَدُهُ صَحِيحٌ
Kutoka kwa ‘Imraan bin Huswayn (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Aliulizwa kuhusu mtu aliyemtaliki mkewe kisha akamrejea wala hakushuhudisha mtu. Akasema: “Shuhudisha talaka yake na kumrejea kwake.”[1] [Imetolewa na Abuu Daawuwd na ikiwa ni Mawquwf na Isnaad yake ni swahiyh]
928.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا، {أَنَّهُ لَمَّا طَلَّقَ اِمْرَأَتَهُ، قَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ ، لِعُمَرَ: "مُرْهُ فَلْيُرَاجِعْهَا} مُتَّفَقٌ عَلَيْه
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Alipomtaliki mkewe, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuambia: “Muamrishe amrejee.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
[1] Ina maana talaka na kumrejea mashahidi wawili ni lazima wawepo. Kama hakuna mashahidi, mwanaume au mwanamke anaweza kufanya kitu kwa kudanganya na ikasababisha matatizo zaidi. Kuita mashahidi ni lazima na ni jambo lenye kupendeza. Rai ya ‘Ulamaa wengi ni kuwa ni jambo linalopendeza kulifanya, lakini kwa ukweli haswa ni jambo la lazima.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْإِيلَاءِ وَالظِّهَارِ وَالْكَفَّارَةِ
09-Mlango Wa Al-Iylaa,[1] Dhwihaar[2], Kafaara[3]
929.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {آلَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ مِنْ نِسَائِهِ وَحَرَّمَ، فَجَعَلَ اَلْحَرَامَ حَلَالًا، وَجَعَلَ لِلْيَمِينِ كَفَّارَةً} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَرُوَاتُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliapa (kuwa hatawaingilia) wakeze kwa muda. Hivyo akajiharamishia (baadhi ya vitu) akafanya haraam kuwa halaal, na akafanya kafara kwa ajili ya kiapo.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na wapokezi wake ni madhubuti]
930.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ:{إِذَا مَضَتْ أَرْبَعَةُ أَشْهُرٍ وَقَفَ اَلْمُؤْلِي حَتَّى يُطَلِّقَ، وَلَا يَقَعُ عَلَيْهِ اَلطَّلَاقُ حَتَّى يُطَلِّقَ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيّ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Inapopita miezi minne muapaji atasimama ili atoe talaka, na talaka haipiti mpaka mume atoe talaka.”[4] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
931.
وَعَنْ سُلَيْمَانَ بْنِ يَسَارٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {أَدْرَكْتُ بِضْعَةَ عَشَرَ مِنْ أَصْحَابِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ كُلُّهُمْ يَقِفُونَ اَلْمُؤْلِي} رَوَاهُ اَلشَّافِعِيّ
Kutoka kwa Sulaymaan bin Yasaar[5] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nimewakuta zaidi ya Maswahaba kumi wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wote wakimsimamisha aliyeapa.” [Imetolewa na Ash-Shafi’iyy]
932.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {كَانَ إِيلَاءُ اَلْجَاهِلِيَّةِ اَلسَّنَةَ وَالسَّنَتَيْنِ، فَوَقَّتَ اَللَّهُ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ، فَإِنْ كَانَ أَقَلَّ مِنْ أَرْبَعَةِ أَشْهُرٍ، فَلَيْسَ بِإِيلَاءٍ} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Ilikuwa kiapo cha Jahiliyyah[6] ni mwaka mmoja au miaka miwili, Allaah Akaweka muda wa miezi minne, inapokuwa ni uchache wa miezi minne hicho si kiapo.”[7] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy]
933.
وَعَنْهُ رَضِيَ اَللَّهُ تَعَالَى عَنْهُمَا، {أَنَّ رَجُلًا ظَاهَرَ مِنِ اِمْرَأَتِهِ، ثُمَّ وَقَعَ عَلَيْهَا، فَأَتَى اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: إِنِّي وَقَعْتُ عَلَيْهَا قَبْلَ أَنْ أُكَفِّرَ، قَالَ: "فَلَا تَقْرَبْهَا حَتَّى تَفْعَلَ مَا أَمَرَكَ اَللَّهُ"} رَوَاهُ اَلْأَرْبَعَةُ وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَرَجَّحَ النَّسَائِيُّ إِرْسَالَهُ
وَرَوَاهُ اَلْبَزَّارُ: مِنْ وَجْهٍ آخَرَ، عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ وَزَادَ فِيهِ:{كَفِّرْ وَلَا تَعُدْ}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Mtu mmoja alimfanyia Dhwihaar mkewe kisha akamjamii, akamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Mimi nimemjamii kabla ya kutoa kafara.” Akamuambia: “Usimkaribie mpaka utende Alilokuamrisha Allaah.” [Imetolewa na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy amesema ni Mursal]
Al-Bazzaar ameipokea kwa njia nyingine kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) na akaongezea: “…toa kafara wala usirudie.”
934.
وَعَنْ سَلَمَةَ بْنِ صَخْرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {دَخَلَ رَمَضَانُ، فَخِفْتُ أَنْ أُصِيبَ اِمْرَأَتِي، فَظَاهَرْتُ مِنْهَا، فَانْكَشَفَ لِي مِنْهَا شَيْءٌ لَيْلَةً، فَوَقَعَتْ عَلَيْهَا، فَقَالَ لِي رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "حَرِّرْ رَقَبَةً" قُلْتُ: مَا أَمْلِكُ إِلَّا رَقَبَتِي. قَالَ: "فَصُمْ شَهْرَيْنِ مُتَتَابِعَيْنِ"، قُلْتُ: وَهَلْ أَصَبْتُ اَلَّذِي أَصَبْتُ إِلَّا مِنْ اَلصِّيَامِ ؟ قَالَ: "أَطْعِمْ عِرْقًا مِنْ تَمْرٍ بَيْنَ سِتِّينَ مِسْكِينًا"} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ إِلَّا النَّسَائِيَّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ خُزَيْمَةَ، وَابْنُ اَلْجَارُود
Kutoka kwa Salamah bin Swakhr[8] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Uliingia mwezi wa Ramadhwaan, nikahofia kumjamii mke wangu nikamfanyia Dhwihaar, usiku mmoja kitu kikanifunikia mwilini mwake, nikamjamii. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaniambia: “Acha mtumwa huru.” Nikamuambia: “Similiki ila shingo yangu”. Akaniambia: “Funga (Swiyaam) miezi miwili mfululizo.” Nikamuambia: “Yale yaliyonifikia ni kwa sababu ya Swiyaam.” Akaniambia: “Lisha maskini tende (vikapu) sitini.”[9] [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) isipokuwa An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Khuzaymah na Ibn Al-Jaaruwd]
[1] Al-Iylaa ni kiapo anachoapa mtu kuwa hatomuingilia mke wake; au kumuambia mke wake moja kwa moja kwa kuapa kwa Allaah kuwa hatomuingilia tena. Allaah Ameweka muda wa miezi mine ya kurudisha uhusiano baina ya mume na mke. Ni vizuri kurudisha uhusiano, kwa kutoa kafaara kwa kiapo kwa muda uliopangwa. Vinginevyo talaka itakuwa imeshatoka; au kulingana na ‘Ulamaa wengine, mtu atalazimishwa kumuacha mkewe au kurudisha uhusiano kama mwanzoni.
[2] Dhwihaar imetokana na neno Dhwahr kwa maana ya mgongo au nyuma, ni kumfananisha mke wa mtu na mgongo wa mama yake. Aina hii ya mazungumzo katika lugha ya kiarabu ina maana ya kuwa: “Wewe ni kama mama yangu na ni haraam kwa ndoa yangu au kukuoa au kukuingilia”. Kulingana na Istwilahi za kishariy’ah Adhw-Dhwihaar ni kumfananisha mke wa mtu na mama wa mtu na hivyo kumfanya kuwa ni haraam kwake. Jambo hili kishariy’ah halizingatiwi kuwa ni talaka lakini ni lazima mtu atoe kafaara kabla ya kumrudia mke wake. Kafaara yake ni kumuacha huru mtu mtumwa au kufunga Swiyaam siku sitini kwa mfululizo au kuwalisha maskini sitini. Ni wajibu kutekeleza moja ya adhabu hii.
[3] Kaffaarah ina maana ya kutubia kwa madhambi hayo mawili yaliyotajwa hapo juu.
[4] Katika hali ya kuapa mtu huulizwa aache au aendelee na mahusiano, nayo hufanyika baada ya miezi minne. Kama hataki kufanya hivyo, anaweza kutengua ndoa yake kwa msaada wa mtawala, na baada ya kumalizia eda yake ataruhusiwa kuolewa tena.
[5] Huyu ni Abuu Ayuwb Sulaymaan bin Yasaar, muachwa huru wa Ummul-Mu’miniyn Maymuwnah. Alikuwa ni mmoja wa ‘Ulamaa saba wakubwa wa Fiqhi na ni Taabi’ mkubwa katika mji wa Madiynah. Ni mtu madhubuti, mwenye taqwa na Mwanazuoni. Alifariki mwaka 107H akiwa na umri wa miaka 73.
[6] Wakati wa Ujahiliyah, mwanamke alionewa sana. Wakati mwingine kwa miaka, hajulikani yuko wapi si muolewa wala si aliyeachwa, yupo katikati. Vile vile haruhusiwi kuolewa baada ya kwisha Eda yake. Mwanamke alikuwa akionewa katika hili na kuachwa kwa muda wa miaka, nayo ilikuwa aina ya kumkomoa, ndipo Allaah Alipoweka miezi minne.
[7] Hadiyth hii inaweka wazi kuwa kama mahusiano yatarudi kabla ya miezi minne, basi itakuwa siyo Iylaa na hakutokuwepo na adhabu.
[8] Huyu ni Salamah bin Swakhr bin Sulaymaan Bin As-Samma Al-Bayadi anatokana na kizazi cha Banu Bayaad, ukoo wa Al-Khazraj, mmoja katika Al-Bukauwn miongoni mwa Swahaba.
[9] Araq moja ni pishi 15 (mfuko mmoja wa tende)
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَللِّعَانِ
10-Mlango Wa Kulaaniana[1]
935.
عَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {سَأَلَ فُلَانٌ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! أَرَأَيْتَ أَنْ لَوْ وَجَدَ أَحَدُنَا اِمْرَأَتَهُ عَلَى فَاحِشَةٍ، كَيْفَ يَصْنَعُ ؟ إِنْ تَكَلَّمَ تَكَلَّمَ بِأَمْرٍ عَظِيمٍ، وَإِنْ سَكَتَ سَكَتَ عَلَى مِثْلِ ذَلِكَ! فَلَمْ يُجِبْهُ، فَلَمَّا كَانَ بَعْدَ ذَلِكَ أَتَاهُ، فَقَالَ: إِنَّ اَلَّذِي سَأَلْتُكَ عَنْهُ قَدِ ابْتُلِيتُ بِهِ، فَأَنْزَلَ اَللَّهُ اَلْآيَاتِ فِي سُورَةِ اَلنُّورِ، فَتَلَاهُنَّ عَلَيْهِ وَوَعَظَهُ وَذَكَّرَهُ، وَأَخْبَرَهُ أَنَّ عَذَابَ اَلدُّنْيَا أَهْوَنُ مِنْ عَذَابِ اَلْآخِرَةِ. قَالَ: لَا، وَاَلَّذِي بَعَثَكَ بِالْحَقِّ مَا كَذَبْتُ عَلَيْهَا، ثُمَّ دَعَاهَا اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَوَعَظَهَا كَذَلِكَ، قَالَتْ: لَا، وَاَلَّذِي بَعَثَكَ بِالْحَقِّ إِنَّهُ لَكَاذِبٌ، فَبَدَأَ بِالرَّجُلِ، فَشَهِدَ أَرْبَعَ شَهَادَاتٍ، ثُمَّ ثَنَّى بِالْمَرْأَةِ، ثُمَّ فَرَّقَ بَيْنَهُمَا} رَوَاهُ مُسْلِم
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Fulani aliuliza: “Ee Rasuli wa Allaah! Nieleze lau mmoja wetu atamkuta mkewe katika machafu (zinaa) afanye nini? Ikiwa atazungumza basi atasema jambo kubwa, na ikiwa atanyamaza, atanyamazia kitu kibaya.” Wala hakumjibu. Baada ya hapo akamuendea tena, akasema: “Lile swali nililokuuliza mimi nimejaribiwa nalo.” Allaah akateremsha Aayah katika Suwrah An-Nuwr, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamsomea Aayah hizo akamnasihi akamkumbusha na akamueleza kuwa adhabu ya duniani ni sahali kuliko adhabu ya Aakhirah. Akasema: “Hapana, naapa kwa aliyekutuma kwa haki sikumzulia uongo!” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuita (mwanamke) akamnasihi vile vile. Mwanamke akasema: “Hapana naapa kwa Aliyekutuma kwa haki yeye ni muongo!” Akaanza kwa mwanamume, akashuhudilia mara nne kwa kiapo cha Allaah. Halafu akamgeukia yule mwanamke (akashuhudia kama yule mume), kisha akawaachanisha.” [Imetolewa na Muslim]
936.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا أَيْضًا {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ لِلْمُتَلَاعِنَيْنِ: "حِسَابُكُمَا عَلَى اَللَّهِ تَعَالَى، أَحَدُكُمَا كَاذِبٌ، لَا سَبِيلَ لَكَ عَلَيْهَا" قَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! مَالِي ؟ قَالَ: "إِنْ كُنْتَ صَدَقْتَ عَلَيْهَا، فَهُوَ بِمَا اِسْتَحْلَلْتَ مِنْ فَرْجِهَا، وَإِنْ كُنْتَ كَذَبْتَ عَلَيْهَا، فَذَاكَ أَبْعَدُ لَكَ مِنْهَا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) alisema tena kuwa: “Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaambia wale waliolaaniana: “Hisabu yenu iko kwa Allaah.[2] Mmoja wenu ni muongo, wewe (mume) huna njia ya kumrudia mkeo.” Yule mume akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Mali yangu?” Akasema: “Ikiwa ulisema kweli kumhusu yeye (mwanamke) basi mali hiyo ni kwa uchi wake uliojihalalishia.[3] Na ikiwa umemzulia uongo basi mali hiyo iko mbali nawe zaidi kuliko huyo (mwanamke).” [Al-Bukaariy, Muslim]
937.
وَعَنِ أَنَسٍرَضِيَ اللهُ عَنْهُ، أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {أَبْصِرُوهَا، فَإِنْ جَاءَتْ بِهِ أَبْيَضَ سَبِطًا فَهُوَ لِزَوْجِهَا، وَإِنْ جَاءَتْ بِهِ أَكْحَلَ جَعْدًا، فَهُوَ اَلَّذِي رَمَاهَا بِهِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Anas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtizameni, ikiwa aliyezaliwa ni mweupe maumbile yake yamekamilika basi ni wa mume wake, na akiwa macho yake ni kama yaliyopaka wanja na nywele koto basi huyo ni wa aliyemsingizia uzinifu (uzinzi).”[4] [Al-Bukhaariy, Muslim]
938.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَمَرَ رَجُلاً أَنْ يَضَعَ يَدَهُ عِنْدَ اَلْخَامِسَةِ عَلَى فِيهِ، وَقَالَ: "إِنَّهَا مُوجِبَةٌ"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimuamrisha mtu aweke mkono wake mdomoni[5] mwake katika ile mara ya tano na akasema: “Itawajibisha.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nisaaiy na wapokezi wake ni Madhubuti]
939.
وَعَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍرَضِيَ اللهُ عَنْهُ فِي قِصَّةِ اَلْمُتَلَاعِنَيْنِ قَالَ: {فَلَمَّا فَرَغَا مِنْ تَلَاعُنِهِمَا قَالَ: كَذَبْتُ عَلَيْهَا يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنْ أَمْسَكْتُهَا، فَطَلَّقَهَا ثَلَاثًا قَبْلَ أَنْ يَأْمُرَهُ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Sahl bin Sa’d (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kisa cha wale waliolaaniana: “Walipomaliza kulaaniana kwao mume alisema: “Nitakuwa nimemsingizia Ee Rasuli wa Allaah! Kama nitakuwa naye.” Akamtaliki talaka tatu[6] kabla ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kumuamrisha kufanya hivyo.” [Al-Bukhaariy, Muslim
940.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ رَجُلاً جَاءَ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: إِنَّ اِمْرَأَتِي لَا تَرُدُّ يَدَ لَامِسٍ. قَالَ: "غَرِّبْهَا". قَالَ: أَخَافُ أَنْ تَتْبَعَهَا نَفْسِي. قَالَ: "فَاسْتَمْتِعْ بِهَا"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالْبَزَّارُ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ.
وَأَخْرَجَهُ النَّسَائِيُّ مِنْ وَجْهٍ آخَرَ: عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ بِلَفْظٍ{قَالَ: طَلِّقْهَا. قَالَ: لَا أَصْبِرُ عَنْهَا. قَالَ: "فَأَمْسِكْهَا}
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Mtu mmoja alimuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Mke wangu harudishi mkono wa mwenye kugusa.”[7] Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Mhamishe.” Akasema: “Nahofia kumfuata.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Basi starehe naye.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na Al-Bazzaar, na wapokezi wake ni waaminifu (madhubuti)]
Na An-Nasaaiy ameipokea kwa njia nyingine kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kwa lafdhi: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Mtaliki.” Yule mtu akasema: “Siwezi kuwa mbali naye.” Akamuambia: “Basi baki naye.”
941.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّهُ سَمِعَ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ يَقُولُ حِينَ نَزَلَتْ آيَةُ اَلْمُتَلَاعِنَيْنِ: "أَيُّمَا اِمْرَأَةٍ أَدْخَلَتْ عَلَى قَوْمٍ مَنْ لَيْسَ مِنْهُمْ، فَلَيْسَتْ مِنْ اَللَّهِ فِي شَيْءٍ، وَلَنْ يُدْخِلَهَا اَللَّهُ جَنَّتَهُ، وَأَيُّمَا رَجُلٍ جَحَدَ وَلَدَهُ وَهُوَ يَنْظُرُ إِلَيْهِ اِحْتَجَبَ اَللَّهُ عَنْهُ، وَفَضَحَهُ اَللَّهُ عَلَى رُءُوسِ اَلْخَلَائِقِ اَلْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Alimsikia Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akisema iliposhuka Aayah[8] ya wanaolaaniana: “Mwanamke yeyote amemuingiza katika watu asiye miongoni mwao[9] basi mwanamke huyo hana kitu kwa Allaah na Allaah Hatamuingiza katika Jannah Yake, na mwanaume yeyote anayekana mtoto wake naye anamuangalia, Allaah Atajitenga naye na Atamfedhehesha mbele ya watu wa mwanzo na wa mwisho.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Ibn Maajah, na akaisahihisha Ibn Hibbaan]
942.
وَعَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ:{مَنْ أَقَرَّ بِوَلَدٍ طَرْفَةَ عَيْنٍ، فَلَيْسَ لَهُ أَنْ يَنْفِيَهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ، وَهُوَ حَسَنٌ مَوْقُوف
Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Mwenye kumkiri mtoto wake japo kwa kupepesa jicho hana haki ya kumkana.”[10] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy, na Hadiyth hii ni Hasan na Mawquwf]
943.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّ رَجُلًا قَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ اِمْرَأَتِي وَلَدَتْ غُلَامًا أَسْوَدَ ؟ قَالَ: "هَلْ لَكَ مِنْ إِبِلٍ ؟" قَالَ: نَعَمْ. قَالَ: "فَمَا أَلْوَانُهَا ؟" قَالَ: حُمْرٌ. قَالَ: "هَلْ فِيهَا مَنْ أَوْرَقَ ؟"، قَالَ: نَعَمْ. قَالَ: "فَأَنَّى ذَلِكَ ؟"، قَالَ: لَعَلَّهُ نَزَعَهُ عِرْقٌ. قَالَ: "فَلَعَلَّ اِبْنَكَ هَذَا نَزَعَهُ عِرْقٌ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
وَفِي رِوَايَةٍ لِمُسْلِمٍ:{وَهُوَ يُعَرِّضُ بِأَنْ يَنْفِيَهُ}، وَقَالَ فِي آخِرِهِ:{وَلَمْ يُرَخِّصْ لَهُ فِي اَلِانْتِفَاءِ مِنْهُ}
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Mtu mmoja alimuendea Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Mke wangu amejifungua mtoto mweusi.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Je, una ngamia?” Akasema: “Ndio.” Akasema: “Ni rangi gani?” Akasema: “Ni wekundu.” Akasema: “Je kuna mwenye rangi nyeusi miongoni mwao?” akasema: “Ndio.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Imekuwaje hilo?” Akasema: “Pengine amerithi hilo.” Akasema: “Na huyu (pia) yawezekana katika baba (na babu) zake yuko aliyekuwa na rangi hiyo na pia ikampata.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
Na katika Riwaayah nyingine ya Muslim inasema: “Naye anazungumza kwa mafumbo ili amkane mtoto wake.” Amesema mwisho wake: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hakumkubalia kumkana mtoto wake.”
[1] Al-Li’aan inamaanisha kumtuhumu mmoja wa wanandoa kuwa amezini, bila ya kuwepo kwa ushahidi madhubuti. Ikiwa mwanamke anakana tuhuma, mwanamme analazimika kuapa viapo vine akirejea tuhuma katika kila kiapo, cha tano atasema: “Ghadhabu ya Allaah inishukie ikiwa nimesema uongo.” Ikiwa mwanamke atakaa kimya ataadhibiwa. Hata hivyo akikana hutuma, atawajibika kuapa viapo vinne akikana tuhuma ile katika kila kiapo na katika kiapo cha tano atasema: “Ikiwa anasema kweli basi laana ya Allaah iniangukie.” Laana hii inayokusudiwa hapa inarejea katika Li’aan. Li’aan maana yake ni kuwajibisha kutengana, hakuna njia nyingine ya hawa wawili kuoana tena.
[2] Katika Hadiyth hii umuhimu umewekwa katika kufanya toba ya dhambi aliyokuwa nayo mtu.
[3] Hii ina maana kwamba mahari ya mwanamke haiwezi kurejeshwa tena kwa mume.
[4] Hadiyth hii inahusu mambo matatu: Kwanza, kuhusu mas-ala ambayo hayajawekwa wazi na wahyi, mambo hayo huwa yanatolewa ufafanuzi na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Pili: Ikiwa dalili za msingi ya maamuzi ya jambo hayapo, kuamua kwa kudhania kunakubaliwa. Tatu: kuhusu suala la Li’aan, hata ikiwa kudhania kumesibu, mwanamke hawezi kuadhibiwa kwa uzinifu.
[5] Kuweka mkono mdomoni ni dalili ya kumzindua mtu kwa kiapo cha mwisho; baada ya kiapo hiki majukumu yanarudi kwao katika maisha haya na ya kesho Aakhirah. Ikiwa mwanamme atanyamaza kwenye kiapo cha tano ataadhibiwa kwa kumsingizia na kumkashifu. mwanamke ana haki ya kufanya Li'aan akitaka.
[6] Baada ya Li’aan hakuna haja tena ya kutoa talaka, wakati huo talaka inakuwa imeshatoka. Baada ya Li’aan mwanamke hana haki ya kupokea masrufu yoyote.
[7] Ina maana nyingi: Kwanza, ni hajali anapokutana na ajnabi. Pili: ni mzinifu. Tatu: si muangalizi mzuri wa mali ya mume wake. Maana ya kwanza ndio inayoelekea kuwa sahihi zaidi. Ingekuwa maana ya pili ni sahihi basi mwenye kutuhumu inabidi aje na mashahidi, na hapo basi Li’aan itabidi ifanyike, au mwanamke angeadhibiwa. Hata hivyo yote haya hayakufanyika. Kinyume chake Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alimtaka avumilie. Lau maana ya pili ingekuwa sahihi, basi Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) angekuwa ameruhusu yule bwana kuwa Dayyuwth (mtu asiyejali tabia mbaya aliyouwa nayo mwanamke ambaye yumo katika himaya yake)
[8] Angalia Suwrah An-Nuwr aayah ya 6 (24:6)
[9] Hii ina maana ya kuzaa mtoto ambaye si halaal kisha kuonesha kuwa ni halaal. Suala hili linaleta matatizo mengi katika mirathi, mambo ya kishariy’ah na mas-ala ya ndoa, n.k.
[10] Hatakiwi mtu kumkana mtoto wake, muda wa kuwa uzazi umeshakubalika, ikiwa hali imejitokeza hivyo, kwa upande mmoja, atakuwa ni mtoto wa kitendo cha haraam, na kwa upande wa pili mama yake atakuwa ametuhumiwa uzinifu na mtoto atatengwa na mirathi.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْعِدَّةِ وَالْإِحْدَادِ
11-Mlango Wa Al-‘Iddah (Kukaa Eda)[1] Na Al-Ihdaad (Matanga)[2]
944.
عَنْ اَلْمِسْوَرِ بْنِ مَخْرَمَةَ{ أَنَّ سُبَيْعَةَ الْأَسْلَمِيَّةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا نُفِسَتْ بَعْدَ وَفَاةِ زَوْجِهَا بِلَيَالٍ، فَجَاءَتْ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَاسْتَأْذَنَتْهُ أَنْ تَنْكِحَ، فَأَذِنَ لَهَا، فَنَكَحَتْ} رَوَاهُ اَلْبُخَارِيُّ وَأَصْلُهُ فِي " اَلصَّحِيحَيْنِ "
وَفِي لَفْظٍ: {أَنَّهَا وَضَعَتْ بَعْدَ وَفَاةِ زَوْجِهَا بِأَرْبَعِينَ لَيْلَةً}
وَفِي لَفْظٍ لِمُسْلِمٍ، قَالَ اَلزُّهْرِيُّ: {وَلَا أَرَى بَأْسًا أَنْ تَزَوَّجَ وَهِيَ فِي دَمِهَا، غَيْرَ أَنَّهُ لَا يَقْرَبُهَا زَوْجُهَا حتَّى تَطْهُرَ}
Kutoka kwa Al-Mis-war bin Makhramah amesema kuwa Subay’a Al-Aslamiyyah[3] (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) alijifungua baada tu ya kufariki mumewe kwa siku chache, akamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akimuomba idhini aolewe, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamruhusu akaolewa.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy na asili ya Hadiyth hii imo katika Swahiyh Al-Bukhaariy na Swahiyh Muslim]
Katika tamshi lingine: “…alijifungua baada ya mumewe kufariki kwa siku arubaini.”
Katika tamshi lingine la Muslim inasema: Az-Zuhriy[4] amesema: “Sioni kama pana ubaya akiolewa baada ya kujifungua hata kama yuko damuni (Nifaas), isipokuwa tu mumewe hawezi kumkaribia (kumjamii) mpaka atwahirike.”
945.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {أُمِرَتْ بَرِيرَةُ أَنْ تَعْتَدَّ بِثَلَاثِ حِيَضٍ} رَوَاهُ اِبْنُ مَاجَهْ، وَرُوَاتُهُ ثِقَاتٌ، لَكِنَّهُ مَعْلُولٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Bariyrah aliamrishwa akae eda hedhi tatu.”[5] [Imetolewa na Ibn Maajah, Wapokezi wake ni madhubuti lakini ina ‘illah]
946.
وَعَنْ اَلشَّعْبِيِّ، عَنْ فَاطِمَةَ بِنْتِ قَيْسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {عَنِ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي اَلْمُطَلَّقَةِ ثَلَاثًا: "لَيْسَ لَهَا سُكْنَى وَلَا نَفَقَةٌ"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Ash-Sha’biyy[6] kutoka kwa Faatwimah bint Qays (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kuhusu mwanamke aliyeachwa talaka tatu: “Hana maskani wala chakula.”[7] [Imetolewa na Muslim]
947.
وَعَنْ أُمِّ عَطِيَّةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا أَنَّ رَسُولَ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ:{لَا تَحِدَّ اِمْرَأَةٌ عَلَى مَيِّتٍ فَوْقَ ثَلَاثٍ إِلَّا عَلَى زَوْجٍ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا، وَلَا تَلْبَسْ ثَوْبًا مَصْبُوغًا، إِلَّا ثَوْبَ عَصْبٍ، وَلَا تَكْتَحِلْ، وَلَا تَمَسَّ طِيبًا، إِلَّا إِذَا طَهُرَتْ نُبْذَةً مِنْ قُسْطٍ أَوْ أَظْفَارٍ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَهَذَا لَفْظُ مُسْلِمٍ وَلِأَبِي دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيِّ مِنْ اَلزِّيَادَةِ:{ وَلَا تَخْتَضِبْ}
وَلِلنَّسَائِيِّ: "وَلَا تَمْتَشِطْ"
Kutoka kwa Ummi ‘Atwiyyah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke haombolezi maiti zaidi ya siku tatu, isipokuwa juu ya mumewe miezi minne na siku kumi.[8] Wala asivae nguo ya rangi isipokuwa nguo ya ‘aswbi,[9] wala asijipake wanja, wala asiguse manukato isipokuwa atakapotwahirika (atajipaka) kiasi kidogo tu cha Qustwi au adhwfaari.”[10] [Al-Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Muslim]
Katika Riwaayah ya Abuu Daawuwd na An-Nisaaiy amezidisha: “…wala asipake hina.”
Na kwa An-Nasaaiy: “…wala asijichane.”
948.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {جَعَلْتُ عَلَى عَيْنِي صَبْرًا، بَعْدَ أَنْ تُوُفِّيَ أَبُو سَلَمَةَ، فَقَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "إِنَّهُ يَشِبُ اَلْوَجْهَ، فَلَا تَجْعَلِيهِ إِلَّا بِاللَّيْلِ، وَانْزِعِيهِ بِالنَّهَارِ، وَلَا تَمْتَشِطِي بِالطِّيبِ، وَلَا بِالْحِنَّاءِ، فَإِنَّهُ خِضَابٌ". قُلْتُ: بِأَيِّ شَيْءٍ أَمْتَشِطُ ؟ قَالَ: "بِالسِّدْرِ"} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ
Kutoka kwa Ummi Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: Nilipaka swabira (aina ya dawa) machoni mwangu baada ya Abuu Salamah kufariki. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaniambia: “Hiyo hurembesha uso kwa hiyo jipake usiku, na mchana iondoe. Wala usijichane kwa manukato wala kwa hina,[11] kwani hiyo ni rangi.” Nikasema: “Nijichane kwa nini?” Akasema: “Kwa majani ya mkunazi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na An-Nasaaiy na Isnaad yake ni hasan]
949.
وَعَنْهَا رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا، {أَنَّ اِمْرَأَةً قَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ اِبْنَتِي مَاتَ عَنْهَا زَوْجُهَا، وَقَدْ اِشْتَكَتْ عَيْنَهَا، أَفَنَكْحُلُهَا ؟ قَالَ: "لَا"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ummu Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema kuwa: Mwanamke mmoja alisema Ee Rasuli wa Allaah! Binti yangu amefiwa na mumewe na jicho lake linauma, je tumpake wanja? Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: “Hapana.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
950.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {طُلِّقَتْ خَالَتِي، فَأَرَادَتْ أَنْ تَجُدَّ نَخْلَهَا فَزَجَرَهَا رَجُلٌ أَنْ تَخْرُجَ، فَأَتَتْ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: بَلْ جُدِّي نَخْلَكِ، فَإِنَّكَ عَسَى أَنْ تَصَدَّقِي، أَوْ تَفْعَلِي مَعْرُوفًا} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Khaalat wangu (Mama mdogo/mkubwa) alitalikiwa, akataka kuenda kukata mitende yake, mtu mmoja akamkanya asitoke.[12] Akamuendea Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Akasema: “Nenda ukakate mitende yako kwani pengine ukatoa Swadaqah au ukafanya wema.”[13] [Imetolewa na Muslim]
951.
وَعَنْ فُرَيْعَةَ بِنْتِ مَالِكٍ، {أَنَّ زَوْجَهَا خَرَجَ فِي طَلَبِ أَعْبُدٍ لَهُ فَقَتَلُوهُ. قَالَتْ: فَسَأَلْتُ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ أَرْجِعَ إِلَى أَهْلِي; فَإِنَّ زَوْجِي لَمْ يَتْرُكْ لِي مَسْكَنًا يَمْلِكُهُ وَلَا نَفَقَةً، فَقَالَ: "نَعَمْ". فَلَمَّا كُنْتُ فِي اَلْحُجْرَةِ نَادَانِي، فَقَالَ: " اُمْكُثِي فِي بَيْتِكَ حَتَّى يَبْلُغَ اَلْكِتَابُ أَجَلَهُ". قَالَتْ: فَاعْتَدَدْتُ فِيهِ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا، قَالَتْ: فَقَضَى بِهِ بَعْدَ ذَلِكَ عُثْمَانُ} أَخْرَجَهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، والذُّهْلِيُّ، وَابْنُ حِبَّانَ، وَالْحَاكِمُ وَغَيْرُهُمْ
Kutoka kwa Furay’ah bint Maalik[14] amesema: Mumewe alitoka kuenda kuwatafuta watumwa wake, wakamuua. Akaeleza: Nikamuuliza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuhusu kurudi kwa jamaa zangu kwani mume wangu hakuniachia maskani anayomiliki wala matumizi. Nabiy akaniambia: “Sawa.” Nilipokuwa chumbani aliniita akaniambia: “Kaa nyumbani mwako mpaka eda imalizike.”[15] Nikakaa Eda humo miezi minne na siku kumi. (Furay’ah) akasema: “Baada ya hapo ‘Uthmaan akahukumu kwa hukumu hiyo.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy, Adh-Dhuhliyy, Ibn Hibbaan , Al-Haakim na wengineo]
952.
وَعَنْ فَاطِمَةَ بِنْتِ قَيْسٍ قَالَتْ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ زَوْجِي طَلَّقَنِي ثَلَاثًا، وَأَخَافُ أَنْ يُقْتَحَمَ عَلَيَّ، قَالَ: فَأَمَرَهَا، فَتَحَوَّلَتْ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Faatwimah bint Qays amesema: “Ee Rasuli wa Allaah! Mume wangu ameniacha talaka tatu nami nachelea kushambuliwa.” Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuamrisha ahame. [Imetolewa na Muslim]
953.
وَعَنْ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {لَا تُلْبِسُوا عَلَيْنَا سُنَّةَ نَبِيِّنَا، عِدَّةُ أُمِّ اَلْوَلَدِ إِذَا تُوُفِّيَ عَنْهَا سَيِّدُهَا أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَابْنُ مَاجَهْ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَأَعَلَّهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ بِالِانْقِطَاعِ
Kutoka kwa ‘Amr bin Al-‘Aasw (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Msituchanganye na Sunnah ya Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) wetu. Eda ya mjakazi (aliyezalishwa na bwana wake) bwana wake akifa ni miezi minne na siku kumi.”[16] [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na Ibn Maajah, na akaisahihisha Al-Haakim, na akaidhoofisha kwa kuwa Munqatw Ad-Daaraqutwniy]
954.
وَعَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {إِنَّمَا اَلْأَقْرَاءُ، اَلْأَطْهَارُ} أَخْرَجَهُ مَالِكٌ فِي قِصَّةٍ بِسَنَدٍ صَحِيحٍ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Quruwu tatu ni twahara.”[17] [Imetolewa na Maalik kwa Isnaad sahihi katika kisa fulani]
955.
وَعَنِ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {طَلَاقُ اَلْأَمَةِ تَطْلِيقَتَانِ، وَعِدَّتُهَا حَيْضَتَانِ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَأَخْرَجَهُ مَرْفُوعًا وَضَعَّفَهُ
وَأَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَابْنُ مَاجَهْ: مِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ، وَخَالَفُوهُ، فَاتَّفَقُوا عَلَى ضَعْفِهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Talaka ya mjakazi ni talaka mbili, na Eda yake ni hedhi mbili.”[18] [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniyy ikiwa Marfuw’ na ameidhoofisha]
Na wameipokea Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah kutoka katika Hadiyth ya ‘Aaishah, na akaisahihisha Al-Haakim. (Wanazuoni wa Hadiyth) wametofautiana nae, wameafikiana kuwa ni dhaifu.
956.
وَعَنْ رُوَيْفِعِ بْنِ ثَابِتٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَحِلُّ لِامْرِئٍ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ اَلْآخِرِ أَنْ يَسْقِيَ مَاءَهُ زَرْعَ غَيْرِهِ} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَحَسَّنَهُ اَلْبَزَّارُ
Kutoka kwa Ruwyfi’ bin Thaabit[19] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Si halaal kwa mtu anayemuamini Allaah na siku ya mwisho kunyosheleza maji yake katika mmea wa mtu mwingine.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan, na Al-Bazzaar akasema ni Hasan]
957.
وَعَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {فِي اِمْرَأَةِ اَلْمَفْقُودِ تَرَبَّصُ أَرْبَعَ سِنِينَ، ثُمَّ تَعْتَدُّ أَرْبَعَةَ أَشْهُرٍ وَعَشْرًا} أَخْرَجَهُ مَالِكٌ، وَالشَّافِعِيُّ
Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: Kuhusu mwanamke ambaye mumewe ametoweka (hajulikani aliko): “Asubiri kwa miaka minne kisha ataketi eda miezi minne na siku kumi.”[20] [Imetolewa na Maalik na Ash-Shaafi’yy]
958.
وَعَنْ اَلْمُغِيرَةِ بْنِ شُعْبَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اِمْرَأَةُ اَلْمَفْقُودِ اِمْرَأَتُهُ حَتَّى يَأْتِيَهَا اَلْبَيَانُ} أَخْرَجَهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ بِإِسْنَادٍ ضَعِيفٍ
Kutoka kwa Al-Mughiyrah bin Shu’bah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mke wa mume aliyetoweka (asiyejulikana aliko) anabaki kuwa ni mkewe mpaka ajiwe na ubainifu.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy kwa isnaad dhaifu]
959.
وَعَنْ جَابِرٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يَبِيتَنَّ رَجُلٌ عِنْدَ اِمْرَأَةٍ، إِلَّا أَنْ يَكُونَ نَاكِحًا، أَوْ ذَا مَحْرَمٍ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamume yeyote asilale kwa mwanamke[21] isipokuwa awe amemuoa au ni maharimu wake.”[22] [Imetolewa na Muslim]
960.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {لَا يَخْلُوَنَّ رَجُلٌ بِاِمْرَأَةٍ، إِلَّا مَعَ ذِي مَحْرَمٍ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Asikae faragha mwanamume na mwanamke ila awe pamoja naye maharimu.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
961.
وَعَنْ أَبِي سَعِيدٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ فِي سَبَايَا أَوْطَاسٍ: {لَا تُوطَأُ حَامِلٌ حَتَّى تَضَعَ، وَلَا غَيْرُ ذَاتِ حَمْلٍ حَتَّى تَحِيضَ حَيْضَةً} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ وَلَهُ شَاهِدٌ: عَنْ اِبْنِ عَبَّاسٍ فِي اَلدَّارَقُطْنِيِّ
Kutoka kwa Abuu Sa’iyd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema katika mateka wa kabila la Awtwaas: “Mjamzito asijamiiwe mpaka ajifunguwe, na asiyekuwa mjamzito asijamiiwe mpaka apate hedhi moja.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na akaisahihisha Al-Haakim nayo ina ushahidi katika Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Abbaas iliyopokewa na Ad-Daaraqutwniy]
962.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {اَلْوَلَدُ لِلْفِرَاشِ، وَلِلْعَاهِرِ اَلْحَجَرُ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ مِنْ حَدِيثِهِ
وَمِنْ حَدِيثِ عَائِشَةَ فِي قِصَّةٍ وَعَنْ اِبْنِ مَسْعُودٍ، عِنْدَ النَّسَائِيِّ وَعَنْ عُثْمَانَ. عِنْدَ أَبِي دَاوُدَ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtoto ni wa kitanda,[23] mzinifu lake ni jiwe.” [Al-Bukhaariy, Muslim kutoka katika Hadiyth yake (Abuu Hurayrah)]
Na kutoka katika Hadiyth ya ‘Aaishah katika kisa kimoja kimepokewa kwa ‘Abdullaah bin Mas-‘uwd na An-Nasaaiy vile vile kimepokewa ‘Uthmaan kwa Abuu Daawuwd
[1] Eda ni muda wa kusubiri ambapo mwanamke haruhusiwi kuolewa, baada ya kifo cha mumewe au kuachika. Kuna aina tatu za Eda: 1. Eda ya kuzaliwa. 2. Eda ya hedhi, na 3. Eda ya mwezi. Kwa mwanamke mwenye mimba, katika hali yoyote iwe ni kifo cha mumewe au kuachika, eda yake ni baada ya kuzaliwa mtoto. Kwa mfano ameachika au mumewe amefariki leo, na siku inayofuata akajifungua mtoto, eda yake huisha kwa kuzaliwa mtoto. Hapo anaruhusiwa kuolewa wakati wowote, lakini kwa muda wote ambapo atakuwa yupo katika nifaas hatoruhusiwa kuingiliwa na mumewe.
[2] Al-Ihdaad ni ile hali ya kuangalilia msiba, kwa mwanamke aliyefiwa na mumewe.
[3] Huyu ni Subay’a ni binti wa Al-Haarith Al-Aslamiyyah wa Banu Aslam. Alikuwa ni Swahaabiyyah. Ibn Sa’d anamtaja kuwa alikuwa ni miongoni mwa waliohajiri. Aliolewa na Sa’d bin Khawlah ambaye alifariki katika Hajjatul Wadaai’ baada ya hapo akaolewa na kijana katika jamaa zake. Imetajwa katika mapokezi mengine kuwa aliolewa na Abuu Sanaabil.
[4] Huyu ni Muhammad bin Muslim bin ‘Ubaidillaah bin Abdillaah bin Shihaab Al-Quraysh Az-Zuhriy, mmoja katika Maimaamu wakubwa na Mwanazuoni mkubwa katika Hijaaz na Shaam. Alikua ni kiongozi wa kizazi cha nne cha Taabi’iyna uwezo wake ulifahamika na kukubaliwa. Al-Layth anasema hakuwahi kumuona Mwanazuoni aliyekusanya elimu nyingi kama Ibn Shihaab. Maalik anaeleza Ibn Shihaab alikuwa katika watu karimu na hakuwa na mfano wake. Alifariki mwaka 124H.
[5] Mume wake Bariyrah alikuwa ni mtumwa. Baada ya kuachwa huru kutoka utumwani kama mwanamke huru, alipewa khiyari ya kuchagua kuhusu ndoa yake. Bariyrah alichagua kuvunja ndoa yake. Kwa hivyo ilibidi kukaa eda ya hedhi tatu. Hadiyth hii inamaanisha kuwa muda wa eda unaotakiwa ni kwa kuangalia hali ya mke sio ya mume.
[6] Huyu ni Abuu ‘Amr ‘Aamir bin Sharahil bin ‘Abdillaah Ash-Sha’biyy Al-Hamdani Al-Kufi. Ni taabi’ na maarufu na Mwanazuoni mkubwa. Az-Zuhri anamueleza kuwa: “Ulamaa ni wanne: Ibn Al-Musayab wa Madiynah, ASh-Sha’b wa Kufa, Hasan Al-Baswri aliyepo Baswra na Mak-hul wa Shaam”. Ash-Sha’biyy alizaliwa wakati wa Ukhalifa wa ‘Umar na inasemekana kuwa alizaliwa miaka sita kabla ya kuanza kwa Ukhalifa wa ‘Uthmaan.
[7] Hukumu ya kishariy’ah kuhusu talaka ni kuwa ni jukumu la mwanamme kugharamia maskani na chakula hadi muda wa eda wa mwanamke unapomalizika. Lakini mwanamme huyo huyo hana haki ya kumgharamia maskani na chakula pindi anapotoa talaka tatu. (ambayo si talaka rejea)
[8] Muda wa eda kwa mjane (asiyekuwa mjamzito) ni miezi mine na siku kumi. Eda ya mwanamke aliyeachika ni hedhi tatu kamili, maadamu ni bado kijana. Ama ikiwa ni ajuza hedhi yake imeshakatika au ni msichana mdogo eda yake ni miezi mitatu.
[9] ‘Aswbi ni aina ya nguo kutoka Yemen
[10] Qustwi ni aina ya udi au manukato.
[11] Maelekezo yaliyopo wakati wa eda ni kuwa hairuhusiwi kwa mwanamke kutumia manukato, kuvaa nguo za rangi rangi, kupaka wanja na kuingia katika mkataba au mazungumzo yoyote ya posa na mwanamme. Hali hii inahusu wanawake wote walioolewa kwa ujumla.
[12] Furay’ah bint Maalik ni dada yake Abuu Sa’d AL-Khudriyy alishuhudia Bay’ah Ar-Ridhwaan. Amepokea baadhi ya Hadiyth
[13] Wanawake walioachika wanatakiwa wakae eda zao katika nyumba za waume zao, iwe wameachika au ni wajane. Hata hivyo mwanamke aliyeachika talaka tatu haiwi hivyo. Mwanamke aliyeachika talaka tatu hakai katika nyumba ya mume wake.
[14] Jina lake ni Furay’ah bint wa Maalik bin Sinaan Al-Khudriyah, dada wa Swahaba maarufu Sa’d Al-Khudriyy. Alihudhuria Bay’ah Ar-Ridhwaan.
[15] Mjane anatakiwa amalize muda wake wa eda katika nyumba ya mumewe. Hii ndio hukumu iliyotolewa na ‘Ulamaa wengi.
[16] Muda wa Eda wa Ummul Walad (kijakazi aliyejifungua mtoto wa bwana wake), kama ni mjane, baadhi ya ‘Ulamaa wanaona kuwa ni miezi mine na siku kumi, wengine wanaona kuwa ni hedhi moja, ambayo ndiyo hukumu iliyo sahihi.
[17] Kuna maneno kadha ya kiarabu ambayo ina maana ya neno na kinyume chake. Maneno kama hayo yanaitwa Dhawaatul-‘Addad (ni maneno na kinyume chake). Moja katika maneno hayo ni Al-Qar-u ambayo maana yake ni kipindi cha hedi, na wakati huo huo ina maana ya Twuhr na kadhalika.
[18] Hii ina maana kijana wa kiume (mtumwa) anaacha kwa talaka mbili na mwanamke muda wake wa eda ni hedhi mbili.
[19] Ruwyfi’ bin Thaabit Al-Answaar ni wa kabila la Baniy Maalik bin An-Najjar, anahisabiwa ni katika wakazi wa Misri. Alifariki mwaka wa 46 Hijriyyah.
[20] Mwanamke aliyepotewa na mume wake asubiri miaka mine (kabla ya kuolewa tena. Muda huu uliwekwa na ‘Umar bin Al-Khatwaab. Baadaye Maswahaba walikubaliana na hukumu hii na ndio hukumu ambayo inafuatwa na ‘Ulamaa wote.
[21] Hadiyth hii inakataza mwanamme kuwa na mwanamke ajnabi peke yake. Hukumu ya Hadiyth hii kadhalika imetajwa katika Hadiyth nyingine, ushawishi wa shaytwaan unaweza kuingia katikati yao na kufanya jambo lisilotakiwa la uzinifu. Hata kama hawawezi au wasifanye jambo hili lakini kuna uwezekano mkubwa wa kutuhumiwa katika hilo, ni vizuri watu wakawa mbali na tuhuma kama hizi.
[22] Maharimu ni jamaa wa karibu wa mwanamke ambao ndoa baina yao ni haraam, uharaam wa milele.
[23] Hii ina maana mtoto wa mwanamke atanasibishwa kwa mume wake na atakuwa chini ya ulezi wake, ikiwa mtu atadai kuwa alikuwa na uhusiano na mwanamke fulani na ya kuwa mtoto ni wake, katika hali hii bado mtoto atakuwa chini ya ulezi wa mumewe na yule mwanamme aliyethibitisha kuzini, shariy’ah itamhukumu kwa hilo. Hakuna hukumu yoyote itakayochukuliwa dhidi ya mwanamke kwa maneno ya mtu bila ushahidi wa wazi wa watu wane. Vinginevyo hukumu itamuendea aliyemtuhumu na kuadhibiwa yeye.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلرَّضَاعِ
12-Mlango Wa Kunyonya (Mtoto Kunyonyeshwa Na Asiye Mamake)
963.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا تُحَرِّمُ اَلْمَصَّةُ وَالْمَصَّتَانِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Kunyonya mara moja na mbili hakuharamishi.”[1] [Imetolewa na Muslim]
964.
وَعَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اُنْظُرْنَ مَنْ إِخْوَانُكُنَّ، فَإِنَّمَا اَلرَّضَاعَةُ مِنْ اَلْمَجَاعَةِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Angalieni vizuri ndugu zenu ni nani.[2] Hakika kunyonyesha (kunakoleta udugu) ni kutokana na kumaliza njaa (ya mtoto).” [Al-Bukhaariy, Muslim]
965.
وَعَنْهَا قَالَتْ: {جَاءَتْ سَهْلَةُ بِنْتُ سُهَيْلٍ. فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ سَالِمًا مَوْلَى أَبِي حُذَيْفَةَ مَعَنَا فِي بَيْتِنَا، وَقَدْ بَلَغَ مَا يَبْلُغُ اَلرِّجَالُ. قَالَ: "أَرْضِعِيهِ. تَحْرُمِي عَلَيْهِ"} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Sahlah bint Suhayl[3] alikuja kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Saalim[4] muachwa huru wa Abuu Hudhayfah[5] yuko pamoja nasi nyumbani mwetu na amefikia yanayofikiwa na wanaume. Nabiy akasema: “Mnyonyeshe utakuwa haraam kwake.”[6] [Imetolewa na Muslim]
966.
وَعَنْهَا: {أَنْ أَفْلَحَ أَخَا أَبِي الْقُعَيْسِ جَاءَ يَسْتَأْذِنُ عَلَيْهَا بَعْدَ اَلْحِجَابِ. قَالَتْ: فَأَبَيْتُ أَنْ آذَنَ لَهُ، فَلَمَّا جَاءَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَخْبَرْتُهُ بِاَلَّذِي صَنَعْتُ، فَأَمَرَنِي أَنْ آذَنَ لَهُ عَلَيَّ. وَقَالَ: "إِنَّهُ عَمُّكِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Aflah (mjomba aliyenyonya naye) nduguye Abuu Al-Qu’ays,[7] aliomba ruhusa kuingia kwangu baada ya kuteremka Aayah ya hijaab. Nikakataa kumruhusu. Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipokuja nilimueleza nililotenda, akaniamurisha nimruhusu na akaniambia: “Huyo ni ami yako.”[8] [Al-Bukhaariy, Muslim]
967.
وَعَنْهَا قَالَتْ: {كَانَ فِيمَا أُنْزِلُ فِي اَلْقُرْآنِ: عَشْرُ رَضَعَاتٍ مَعْلُومَاتٍ يُحَرِّمْنَ، ثُمَّ نُسِخْنَ بِخَمْسٍ مَعْلُومَاتٍ، فَتُوُفِّيَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ وَهِيَ فِيمَا يُقْرَأُ مِنَ اَلْقُرْآنِ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Miongoni mwa Aayah za Qur-aan zilizoteremka ilikuwa ni Aayah hii: “Manyonyesho kumi yanayojulikana yanafanya mtu kuwa maharimu wa mnyonyeshaji.” Kisha zikafutwa kwa manyonyesho matano yanayojulikana….” [Imetolewa na Muslim]
968.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أُرِيدُ عَلَى اِبْنَةِ حَمْزَةَ. فَقَالَ: "إِنَّهَا لَا تَحِلُّ لِي، إِنَّهَا اِبْنَةُ أَخِي مِنْ اَلرَّضَاعَةِ} وَيَحْرُمُ مِنْ اَلرَّضَاعَةِ مَا يَحْرُمُ مِنْ اَلنَّسَبِ. مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alipewa binti wa Hamzah. Alisema: Yeye si halaal kwangu kumuoa, yeye ni binti ya ndugu yangu wa kunyonya, na yale[9] yanayoharamishwa katika kunyonya yanaharamishwa katika nasaba.” [Al-Bukhaariy, Muslim]
969.
وَعَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا يُحَرِّمُ مِنْ اَلرَّضَاعَةِ إِلَّا مَا فَتَقَ اَلْأَمْعَاءَ، وَكَانَ قَبْلَ اَلْفِطَامِ} رَوَاهُ اَلتِّرْمِذِيُّ، وَصَحَّحَهُ هُوَ وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Ummi Salamah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Haiharamishi katika kunyonya ila kiasi kilichopenya matumboni na ikawa kabla ya kuachishwa kunyonya.” [Imetolewa na At-Tirmidhiy na akaisahihisha At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
970.
وَعَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: {لَا رَضَاعَ إِلَّا فِي اَلْحَوْلَيْنِ} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ وَابْنُ عَدِيٍّ مَرْفُوعًا وَمَوْقُوفًا، وَرَجَّحَا اَلْمَوْقُوفَ
Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: “Hakuna kunyonyesha isipokuwa ile miaka miwili ya mwanzo.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy na Ibn ‘Adiyy ikiwa ni Marfuw’ na Mawquwf, wameitilia nguvu kuwa ni Mawquwf]
971.
وَعَنِ اِبْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لَا رَضَاعَ إِلَّا مَا أَنْشَزَ اَلْعَظْمَ، وَأَنْبَتَ اَللَّحْمَ} رَوَاهُ أَبُو دَاوُدَ
Kutoka kwa Ibn Mas-‘uwd (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hakuna kunyonyesha ila yanayoimarisha mfupa na kuotesha nyama.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd]
972.
وَعَنْ عُقْبَةَ بْنِ اَلْحَارِثِ، {أَنَّهُ تَزَوَّجَ أُمَّ يَحْيَى بِنْتَ أَبِي إِهَابٍ، فَجَاءَتْ اِمْرَأَةٌ. فَقَالَتْ: قَدْ أَرْضَعْتُكُمَا، فَسَأَلَ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: "كَيْفَ وَقَدْ قِيلَ ؟ " فَفَارَقَهَا عُقْبَةُ. وَنَكَحَتْ زَوْجًا غَيْرَهُ} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
Kutoka kwa ‘Uqbah bin Al-Haarith[10] anasema kuwa: Yeye alimuoa Ummi Yahya[11] binti Abuu Ihaab. Akaja mwanamke mmoja akasema: “Nimekunyonyesheni wewe na huyo mkeo.” Akaja akamuuliza Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) jambo hilo. Akasema: “Itakuwaje (unasita) na imeshasemwa (kuwa amewanyonyesha?)”[12] ‘Uqbah akamtaliki yule mke akaolewa na mtu mwingine.[13] [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
973.
وَعَنْ زِيَادِ اَلسَّهْمِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {نَهَى رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ أَنْ تُسْتَرْضَعَ اَلْحَمْقَى} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ وَهُوَ مُرْسَلٌ، وَلَيْسَتْ لِزِيَادٍ صُحْبَةٌ
Kutoka kwa Ziyaad As-Sahmiyy[14] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amekataza watu wasiwape wapumbavu kuwanyonyeshea watoto wao.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd nayo ni mursal na Ziyaad si Swahaba]
[1] Hadiyth hii inatujulisha kuwa kitendo cha kunyonya ziwa la mwanamke mara moja au mbili halithibitisha umaharim. Hadiyth iliyopokewa na ‘Aaishah anaeleza kuwa ili kuthibitisha makatazo hayo mwanamke anatakiwa anyonyeshe kwa uchache mara tano.
[2] Ilitokea wakati fulani mtu alikuwa amekaa karibu na Mama ‘Aaishah. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) hakupenda hali hiyo. ‘Aaishah alimjulisha kuwa yule aliyekaa naye alikuwa ni nduguye kwa kunyonya. Baada ya kusikia hivi Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akalitolea ufafanuzi suala hili la kunyonya kwa watoto pamoja utotoni.
[3] Sahlah binti wa Suhayl bin ‘Amr Al-Qushariyah alikuwa wa kabila la Banuu ‘Aamir bin Lu’ayy. Alisilimu mapema na alihama pamoja na Abuu Hudhayfah kuenda Uhabeshi na akamzalia Muhammad bin Abiy Hudhayfah.
[4] Huyu ni Saalim bin Ma’qil muachwa huru wa Abuu Hudhayfah. Alilelewa na mwanamke wa Ki-answaar akiitwa Layla au Thubayta, binti wa Ya’ar, pindi Abuu Hudhayfah alipomuoa alikuja pamoja na Saalim ambaye Abuu Hudhayfah alimfanya katika watu wake. Saalim alihudhuria Badr na Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) aliwaamurrisha Maswahaba zake wasikilize Qur-aan kutoka kwa watu wane na miongoni mwa hao watu wane Saalim alikuwemo. Alikuwa na mazowea ya kuwaongoza Muhajiruwna, akiwemo ‘Umar, katika Swalaah Msikiti wa Quba kabla ya Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kuwasili Madiynah. Hadiyth hii inamhusu Sahlah bint Suhayl. ‘Ulamaa wote wakiwemo Taabi’iyna na Fuqahaa wana msimamo kuwa mtu mkubwa hanyonyeshwi. Na wana msimamo kuwa Hadiyth hii ni Mansuwkh (Hukumu yake imefutwa)
[5] Inasemekana kuwa jina lake lilikuwa ni Muhaashim au Hishaam bin ‘Utbah bin Rabiy’ah bin ‘Abd Shams. Alikuwa ni Swahaba maarufu aliyehudhuria Badr, Uhud na vita vyote muhimu. Aliuwawa katika vita vya Al-Yamaamah akiwa na umri wa miaka 53.
[6] ‘Ulamaa wengi wamekubaliana na rai kuwa kunyonyesha kunakofanya uharaam wa watu wawili ni ule wa miaka miwili ya mwanzo wa umri wa mtoto. Ama kadhia hii ya Saalim katika Hadiyth hii ni maalum, haitumiki kwa mtu mwingine yeyote.
[7] Jina lake kamili ni Abul-Ja’d Aflah, muachwa huru wa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) au muachwa huru wa Ummu Salamah. Kaka yake Abul-Qu’ays alikuwa akiitwa Al-Ja’d au Wail bin Aflah Al-Ash’ari, hivyo basi jina la kaka yake Aflah ni sawa sawa na jina la baba yake. ‘Aaishah alikuwa na wajomba wawili wa kunyonya, miongoni mwao akiwemo kaka zake Abuu Bakr kwa kunyonya ambao walifariki katika zama za Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) na wa pili alikuwa ni Aflah ambaye ni kwa kaka wa baba yake kwa kunyonya.
[8] Mwanamke ananyonyesha maziwa yake, atakuwa ni mama halisi wa mtoto, kama kwamba yeye ndiye aliyemzaa na baba halikadhalika ataonekana hivyo. Na ichukuliwe hivyo kwa watoto wote watakaonyonya nao pamoja nao katika makatazo ya maharim kuoana.
[9] Yatupasa kufahamu kuwa mtoto anaelekea kwa mama yake aliyemyonyesha. Hata hivyo mama huyo hatokuwa na uhusiano wa ndugu wa damu wa mtoto yule. Uharaam huu utakuwa na wenzake walionyonya.
[10]Alikua akiitwa Sirwa’ta ‘Uqbah bin Al-Haarith bin ‘Aamir bin Nawfal bin ‘Abd Manaaf Al-Makkiy. Alikuwa ni Swahaba miongoni mwa waliosilimu siku ya Fat-h Makkah. Aliishi hadi miaka ya hamsini ya Hijrah.
[11] Jina lake ni Ghaniyah, binti wa Abiy Ihaab bin ‘Uwair At-Tamiymiy. Inasemekana kuwa jina lake lilikuwa Zaynab vile vile.
[12] Hadiyth hii inatufahamisha kuwa tukitaka kuthibitisha uhusiano wa walionyonyeshwa pamoja (ukaka na udada), ushahidi wa mtu mmoja unatosha kuthibitisha. Hili linaonesha vile vile kuwa ushahidi utakaotolewa na mwanamke, katika mas-ala yanayohusiana na mwanamke, ana nguvu zaidi kuliko itakayotolewa na mwanamume.
[13] Imeandikwa katika kitabu At-Taqriyb kuwa alikuwa ni Taabi’ wa kizazi cha tatu na anajulikana kama ni thiqah (madhubuti). Ameripoti Hadiyth ambayo ni Mursal. Na inasemekana kuwa ni muacha huru wa ‘Amr bin Al-‘Aasw. Waandishi wote wa Usudul Al-Ghaba na Al-Isti’aba hakutajwa miongoni mwa Maswahaba.
[14] Hind bin ‘Utbah bint Rabiy’ah bin ‘Abd Shams alisilimu mwaka wa Fat-h Makkah baada ya mume wake kusilimu katika mwaka huo huo wa Fat-h Makkah. Kifo cha baba yake ‘Utbah mjomba wake Shaybah na kaka yake Al-Waliyd huko Badr vilimshtua sana na alifurahi sana pindi Hamza alipouawawa katika vita vya Uhud.
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلنَّفَقَاتِ
13-Mlango Wa Matumizi
974.
عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: {دَخَلَتْ هِنْدُ بِنْتُ عُتْبَةَ اِمْرَأَةُ أَبِي سُفْيَانَ عَلَى رَسُولِ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ . فَقَالَتْ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ أَبَا سُفْيَانَ رَجُلٌ شَحِيحٌ لَا يُعْطِينِي مِنْ اَلنَّفَقَةِ مَا يَكْفِينِي وَيَكْفِي بَنِيَّ، إِلَّا مَا أَخَذْتُ مِنْ مَالِهِ بِغَيْرِ عِلْمِهِ، فَهَلْ عَلِيَّ فِي ذَلِكَ مِنْ جُنَاحٍ ؟ فَقَالَ: "خُذِي مِنْ مَالِهِ بِالْمَعْرُوفِ مَا يَكْفِيكِ، وَيَكْفِي بَنِيكِ"} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa ‘Aaishah (رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا) amesema: “Siku moja Hind bint ‘Utbah[1] mke wa Abuu Sufyaan[2] aliingia kwa Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Kwa hakika Abuu Sufyaan ni mtu bakhili mwenye tamaa, wala hanipi kinachonitosha mimi na wanangu ila ninachokichukua katika mali yake ilhali hajui, je nikifanya hivyo nina dhambi? Akasema: “Chukua kwa wema katika mali yake kinachokutosha wewe na wanao.”[3] [Al-Bukhaariy, Muslim]
975.
وَعَنْ طَارِقِ الْمُحَارِبِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {قَدِمْنَا اَلْمَدِينَةَ، فَإِذَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَائِمٌ يَخْطُبُ وَيَقُولُ: "يَدُ اَلْمُعْطِي اَلْعُلْيَا، وَابْدَأْ بِمَنْ تَعُولُ: أُمَّكَ وَأَبَاكَ، وَأُخْتَكَ وَأَخَاكَ، ثُمَّ أَدْنَاكَ أَدْنَاكَ"} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ، وَصَحَّحَهُ اِبْنُ حِبَّانَ، وَاَلدَّارَقُطْنِيُّ
Kutoka kwa Twaariq Al-Muhaaribiyy[4] (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Tulienda Madiynah tukamkuta Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) yuko juu ya mimbari amesimama anawahutubia watu: “Mkono wa mtoaji ni wa juu,[5] anza kwa unayemlisha: mama yako, baba yako, dada yako na ndugu yako, halafu aliye karibu nawe zaidi.” [Imetolewa na An-Nasaaiy, na akaisahihisha Ibn Hibbaan na Ad-Daaraqutwniy]
976.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {لِلْمَمْلُوكِ طَعَامُهُ وَكِسْوَتُهُ، وَلَا يُكَلَّفُ مِنْ اَلْعَمَلِ إِلَّا مَا يُطِيقُ} رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mtumwa ana haki kwa bwana wake kupata chakula chake na nguo zake[6] wala halazimishwi kufanya kazi ila anayoiweza.” [Imetolewa na Muslim]
977.
وَعَنْ حَكِيمِ بْنِ مُعَاوِيَةَ اَلْقُشَيْرِيِّ، عَنْ أَبِيهِ قَالَ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! مَا حَقُّ زَوْجَةِ أَحَدِنَا عَلَيْهِ ؟ قَالَ: "أَنْ تُطْعِمَهَا إِذَا طَعِمْتَ، وَتَكْسُوَهَا إِذَا اِكْتَسَيْتَ، وَلَا تَضْرِبِ اَلْوَجْهَ، وَلَا تُقَبِّحْ…"} اَلْحَدِيثُ. وتَقَدَّمَ فِي عِشْرَةِ اَلنِّسَاءِ.
Kutoka kwa Hakiym bin Mu’aawiyah Al-Qushayriyy amepokea kutoka kwa baba yake amesema: “Nilisema Ee Rasuli wa Allaah! Ni ipi haki ya mke wa mmoja wetu juu ya mumewe? Akasema: ‘Ni kumlisha unapokula na kumvisha unapovaa’.” Hadiyth imetangulia katika mlango wa matengamano ya waume kwa wake zao.
978.
وَعَنْ جَابِر بْنِ عَبْدِ اَللَّهِ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فِي حَدِيثِ اَلْحَجِّ بِطُولِهِ قَالَ فِي ذِكْرِ اَلنِّسَاءِ: {وَلَهُنَّ عَلَيْكُمْ رِزْقُهُنَّ وَكِسْوَتُهُنَّ بِالْمَعْرُوفِ} أَخْرَجَهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdullaah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema kutoka katika Hadiyth ya Hajj iliyotajwa kwa urefu alisema alipowataja wanawake: “Wao (wanawake) wana haki inayowapasa nyinyi chakula chao na nguo zao kwa wema.”[7] [Imetolewa na Muslim]
979.
وَعَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرٍو رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {كَفَى بِالْمَرْءِ إِثْمًا أَنْ يُضَيِّعَ مَنْ يَقُوتُ} رَوَاهُ النَّسَائِيُّ
وَهُوَ عِنْدَ مُسْلِمٍ بِلَفْظِ: "أَنْ يَحْبِسَ عَمَّنْ يَمْلِكُ قُوتَهُ"
Kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Yatosha mtu kuwa ana dhambi kwa kumtelekeza anayemlisha.”[8] [Imetolewa na An-Nasaaiy].
Nayo iko kwa Muslim kwa tamshi: “Kuzuia chakula kwa yule anayekimiliki.”
980.
وَعَنْ جَابِرٍ يَرْفَعُهُ، فِي اَلْحَامِلِ اَلْمُتَوَفَّى عَنْهَا قَالَ: {لَا نَفَقَةَ لَهَا} أَخْرَجَهُ اَلْبَيْهَقِيُّ، وَرِجَالُهُ ثِقَاتٌ، لَكِنْ قَالَ: اَلْمَحْفُوظُ وَقْفُهُ
وَثَبَتَ نَفْيُ اَلنَّفَقَةِ فِي حَدِيثِ فَاطِمَةَ بِنْتِ قَيْسٍ كَمَا تَقَدَّمَ. رَوَاهُ مُسْلِمٌ
Kutoka kwa Jaabir amesema kuhusu mwanamke mjamzito aliyefiwa na mumewe, Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Hana matumizi.”[9] [Imetolewa na Al-Bayhaqiyy na wapokezi wake ni madhubuti lakini amesema: Ilivyohifadhiwa ni kuwa Hadiyth hii ni Mawquwf]
Na imethibiti mwanamke huyo kutopewa matumizi katika Hadiyth ya Faatwimah bint Qays kama iliyotangulia. [Imetolewa na Muslim]
981.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {اَلْيَدِ اَلْعُلْيَا خَيْرٌ مِنْ اَلْيَدِ اَلسُّفْلَى، وَيَبْدَأُ أَحَدُكُمْ بِمَنْ يَعُولُ. تَقُولُ اَلْمَرْأَةُ: أَطْعِمْنِي، أَوْ طَلِّقْنِي} رَوَاهُ اَلدَّارَقُطْنِيُّ، وَإِسْنَادُهُ حَسَنٌ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mkono wa juu ni bora kuliko mkono wa chini, mmoja wenu aanze na anayemlisha. Mwanamke husema[10]: “Nilishe au nipe talaka.” [Imetolewa na Ad-Daaraqutwniy na Isnaad yake ni hasan]
982.
وَعَنْ سَعِيدِ بْنِ اَلْمُسَيَّبِ فِي اَلرَّجُلِ لَا يَجِدُ مَا يُنْفِقُ عَلَى أَهْلِهِ قَالَ: {يُفَرَّقُ بَيْنَهُمَا} أَخْرَجَهُ سَعِيدُ بْنُ مَنْصُورٍ: عَنْ سُفْيَانَ، عَنْ أَبِي اَلزِّنَادِ، عَنْهُ. قَالَ: {فَقُلْتُ لِسَعِيدِ بْنِ اَلْمُسَيَّبِ: سُنَّةٌ ؟ فَقَالَ: سُنَّةٌ} وَهَذَا مُرْسَلٌ قَوِيَ
Kutoka kwa Sa’iyd bin Al-Musayyib amesema kuhusu mtu aliyekuwa hapati matumizi ya mkewe: “Watatenganishwa.” [Imetolewa na Sa’iyd bin Manswuwr kutoka kwa Sufyaan[11] naye kutoka kwa Abuu Az-Zinaad[12]]
Kutoka kwa Sa’iyd bin Al-Musayyib amesema: “Nilisema kumuambia Sa’iyd bin Al-Musayyib je hii ni Sunnah? Akasema: ndiyo ni sunnah.” [Hadiyth hii ni Mursal yenye nguvu]
983.
وَعَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ {أَنَّهُ كَتَبَ إِلَى أُمَرَاءِ اَلْأَجْنَادِ فِي رِجَالٍ غَابُوا عَنْ نِسَائِهِمْ: أَنْ يَأْخُذُوهُمْ بِأَنَّ يُنْفِقُوا أَوْ يُطَلِّقُوا، فَإِنْ طَلَّقُوا بَعَثُوا بِنَفَقَةِ مَا حَبَسُوا} أَخْرَجَهُ اَلشَّافِعِيُّ. ثُمَّ اَلْبَيْهَقِيّ بِإِسْنَادِ حَسَنٌ
Kutoka kwa ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: “Aliwaandikia viongozi wa majeshi kuhusu watu walio mbali na wake zao muda mrefu, kuwa watoe matumizi au wawataliki wake zao, ikiwa watawataliki watume gharama[13] za zile siku walizozuwia kutoa.” [Imetolewa na Ash-Shaafi’iyy na Al-Bayhaqiyy kwa Isnaad hasan]
984.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: {جَاءَ رَجُلٌ إِلَى اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ فَقَالَ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! عِنْدِي دِينَارٌ ؟ قَالَ: "أَنْفِقْهُ عَلَى نَفْسِكَ". قَالَ: عِنْدِي آخَرُ ؟ قَالَ: "أَنْفِقْهُ عَلَى وَلَدِكَ". قَالَ: عِنْدِي آخَرُ ؟ قَالَ: "أَنْفِقْهُ عَلَى أَهْلِكَ". قَالَ: عِنْدِي آخَرُ، قَالَ: "أَنْفِقُهُ عَلَى خَادِمِكَ". قَالَ عِنْدِي آخَرُ، قَالَ: "أَنْتَ أَعْلَمَ"} أَخْرَجَهُ اَلشَّافِعِيُّ وَاللَّفْظُ لَهُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَأَخْرَجَهُ النَّسَائِيُّ وَالْحَاكِمُ بِتَقْدِيمِ اَلزَّوْجَةِ عَلَى اَلْوَلَدِ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema: “Alikuja mtu kwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Nina dinari moja (niifanyeje?) akasema: Jitolee mwenyewe. Akasema: Ninayo nyingine. Akasema: Mpe mwanao. Akasema: Ninayo nyingine. Akasema: Mpe mkeo. Akasema: Ninayo nyingine. Akasema: Mpe mtumishi wako. Akasema: Ninayo nyingine. Akasema: Wewe ndiye unaejua zaidi (cha kuifanyia).” [Imetolewa na Ash-Shaafi’iyy na Abuu Daawuwd. Matini ya Hadiyth ni ya Abuu Daawuwd, vile vile An-Nasaaiy na Al-Haakim wameipokea kwa kumtanguliza mke mbele ya mtoto]
985.
وَعَنْ بَهْزِ بْنِ حَكِيمٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ جَدِّهِ قَالَ: {قُلْتُ: يَا رَسُولَ اَللَّهِ! مَنْ أَبَرُّ ؟ قَالَ: "أُمَّكَ". قُلْتُ: ثُمَّ مِنْ ؟ قَالَ: "أُمَّكَ". قُلْتُ: ثُمَّ مِنْ " ؟ قَالَ: "أُمَّكَ". قُلْتُ: ثُمَّ مِنْ ؟ قَالَ: "أَبَاكَ، ثُمَّ اَلْأَقْرَبَ فَالْأَقْرَبَ"} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَاَلتِّرْمِذِيُّ وَحُسَّنَهُ
Kutoka kwa Bahz bin Hakiym kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake amesema: Nilisema Ee Rasuli wa Allaah! Nimfanyie nani wema? Akasema: “Mama yako.” Nikasema: Kisha nani? Akasema: “Mama yako.” Nikasema kisha nani? Akasema “Mama yako.” Nikasema kisha nani? Akasema: “Baba yako, kisha jamaa wa karibu zaidi.” [Imetolewa na Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy amesema ni sahihi]
[1] Hind bint ‘Utbah bint Rabiy’a bin ‘Abd Shams alisilimu mwaka wa Fat-h Makkah baada ya mume wake kusilimu katika mwaka huo huo wa Fat-h Makkah. Kifo cha baba yake ‘Utbah, mjomba wake Shaiba na kaka yake Al-Waliyd huko Badr vilimshtua sana na alifurahi sana pindi Hamza alipouwawa katika vita vya Uhud.
[2] Jina lake ni Sakhr bin Harb bin Umaiyyah bin ‘Abd Shams ambaye alibeba bendera ya ukafiri na alikuwa kiongozi aliyepigana na Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ). Alisilimu katika Fat-h Makkah pindi Al-‘Abbaas alipomchukuwa kwa Nabiy kabla ya kuingia Makkah. Aliishi akiwa ni Muislamu mzuri.
[3] Lengo la Hadiyth hii kuwekwa hapa ni kuonesha majukumu aliyokuwa nayo mtu katika kusimamia mahitaji ya mkewe au wakeze na watoto wake. Inaonyesha hali kadhalika kuwa ikiwa mtu atakataa kutoa haki anayotakiwa kutoa, basi Shariy’ah itaruhusu haki hiyo itolewe kwa njia nyingine. Kwa maneno mengine, ikiwa mtu amedhulumiwa anaweza kutafuta haki yake kupitia njia nyingine.
[4] Twaariq bin ‘Abdillaah Al-Muhaaribiyy alikuwa ni Swahaba ambaye alipokea baadhi ya Hadiyth. Alikuwa Muhaaribiyy bin Khasfa, katika kabila la Banu Ghatafan.
[5] Mkono unaotoa ni bora kuliko mkono unaopokea. Ni vizuri mtu kutokopa fedha. Hadiyth hii haikutaja mke na watoto kwani wao wameshaingizwa katika matumizi ya familia. Maelezo ya ziada ni kuwa familia ya mtu tajiri inajumuisha jamaa zake wa karibu kama kaka na dada zake walio masikini ili nao waishi maisha mazuri.
[6] Kilichokuwa kizuri katika muamala wa mtu na watumwa au wafanyakazi ni pale anapokula amlishe anachokula na amvishe anachovaa. Kadhalika asizidishiwe kazi ila anachoweza kufanya kama kuna uzito basi asaidiwe.
[7] Lengo la kuwekwa kwa Hadiyth hii ni matumizi yatachukuliwa kulingana na kipato cha mtu. Ikiwa mtu ni tajiri mkewe anaweza kuomba ziada ya matumizi, inayolingana na uwezo wa mumewe. Ikiwa hali yake ni ya umasikini atapata kile kinacholingana na uwezo wa mumewe.
[8] Maelezo ya Hadiyth hii yanasisitiza kuwa ni dhambi kuwatekeleza wale ambao umeamrishwa kuwahudumia. Watu ambao ni lazima kishariy’ah kuwahudumia kwa daraja la mwanzo kabisa ni mke, watoto, wafanyakazi wake na wazazi wake.
[9] Mwanamke asiyekuwa na mimba na aliyeachika talaka tatu, kwa makubaliano ya ‘Ulamaa, hana haki ya kupewa nyumba na gharama zake. Mjamzito, aliyeachika talaka tatu anayo haki ya kupewa chakula lakini siyo nyumba. Mjane asiye na mimba anapewa nyumba lakini siyo chakula. Mjane mwenye mimba ana haki ya nyumba, kuna tofauti ya rai kutokana na ‘Ulamaa ikiwa ana haki ya kupewa chakula na gharama zingine za maisha. Mjadala upo katika huduma za nyumba na maisha kwa mwanamke aliyekuwa katika eda. Pindi eda yake inapomalizilka, hana haki ya chochote katika yaliyotangulia.
[10] Hadiythi hii inatupambanulia kwamba ikiwa mwanamme hawezi gharama za mke wake, wataachanishwa ikiwa mwanamke ametaka hivyo. Hata hivyo, ikiwa mwanamke atapendelea asubiri kwa matamu ya maisha na machungu yake, atakuwa ni mwenye kupata ujira.
[11] Huyu ni Sufyaan bin Sa’iyd bin Masruq Ath-Thawriy Abuu ‘Abdillaah Al-Kufi. Alikuwa ni Imaam maarufu na makini, Hafidhi na mwenye elimu kubwa ya Hadiyth, alikuwa ni mwenye taqwa. Alizaliwa mwaka 77H na alikufa katika mji wa Basra mwaka 161H.
[12] Jina lake halisi ni ‘Abdullaah bin Dhakwaan, ni katika ukoo wa Al-Amawi wa Madiynah. Alikuwa ni miongoni mwa maimaam wakubwa, Ahmad anamuelezea kwa kusema: “Alikuwa ni mtu madhubuti na kamanda wa Waumini.” Al-Bukhaariy naye anamuelezea kwa kusema: “Isnaad iliyokuwa bora zaidi ni kutoka kwa Abuu Az-Zinaad naye kutoka kwa Al-A’raaj kutoka kwa Abuu Hurayrah (ambaye amepokea kutoka kwa Nabiy).” Alifariki mwaka 130 Hijriya au 131.
[13] Katika Hadiyth nyingine inasisitiza kuwa fedha inayotumiwa na mtu kwa ajili ya mke wake na watoto wake ndiyo yenye ujira mkubwa na ni bora kuliko ile inayotumika katika kuwapa maskini wa mbali (wasiokuwa ndugu).
بُلُوغُ الْمَرام
Buluwgh Al-Maraam
كِتَابُ اَلنِّكَاحِ
Kitabu cha Nikaah (Ndoa)
بَابُ اَلْحَضَانَةِ
14-Mlango Wa Al-Hadhwaanah Malezi[1]
986.
عَنْ عَبْدِ اَللَّهِ بْنِ عَمْرِوٍ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ اِمْرَأَةً قَالَتْ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ اِبْنِي هَذَا كَانَ بَطْنِي لَهُ وِعَاءً، وَثَدْيِي لَهُ سِقَاءً، وَحِجْرِي لَهُ حِوَاءً، وَإِنَّ أَبَاهُ طَلَّقَنِي، وَأَرَادَ أَنْ يَنْتَزِعَهُ مِنِّي. فَقَالَ لَهَا رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "أَنْتِ أَحَقُّ بِهِ، مَا لَمْ تَنْكِحِي".} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَأَبُو دَاوُدَ، وَصَحَّحَهُ اَلْحَاكِمُ
Kutoka kwa ‘Abdillaah bin ‘Amr (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema: Mwanamke mmoja alikuja akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Kwa hakika mwanangu huyu tumbo langu lilikuwa ndio mfuko wake, ziwa langu lilikuwa ni kiriba chake cha maji, na paja langu lilikuwa kitanda chake. Baba yake alinitaliki na anataka kunipokonya mtoto huyu!” Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamuambia: “Wewe una haki zaidi kwake maadamu hujaolewa.” [Imetolewa na Ahmad, Abuu Daawuwd na akaisahihisha Al-Haakim]
987.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ اِمْرَأَةً قَالَتْ: {يَا رَسُولَ اَللَّهِ! إِنَّ زَوْجِي يُرِيدُ أَنْ يَذْهَبَ بِابْنِي، وَقَدْ نَفَعَنِي، وَسَقَانِي مِنْ بِئْرِ أَبِي عِنَبَةَ فَجَاءَ زَوْجُهَا، فَقَالَ اَلنَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ "يَا غُلَامُ! هَذَا أَبُوكَ وَهَذِهِ أُمُّكَ، فَخُذْ بِيَدِ أَيُّهُمَا شِئْتَ" فَأَخَذَ بِيَدِ أُمِّهِ، فَانْطَلَقَتْ بِهِ.} رَوَاهُ أَحْمَدُ، وَالْأَرْبَعَةُ، وَصَحَّحَهُ اَلتِّرْمِذِيُّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema kuwa: Mwanamke mmoja alikuja akasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Mume wangu anataka kumchukua mwanangu na ananisaidia kuchotea maji katika kisima cha Abiy ‘Inabah, mumewe akaja, akasema Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) kumuambia yule kijana: “Ee mtoto, huyu ni baba yako na huyu ni mama yako, mshike mkono umtakae.”[2] Yule kijana akashika mkono wa mama yake na akaondoka naye.” [Imetolewa na Ahmad na Al-Arba’ah (At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Abuu Daawuwd, Ibn Maajah) na akaisahihisha At-Tirmidhiy]
988.
وَعَنْ رَافِعِ بْنِ سِنَانٍ، {أَنَّهُ أَسْلَمَ، وَأَبَتِ اِمْرَأَتُهُ أَنْ تُسْلِمَ. فَأَقْعَدَ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ اَلْأُمَّ نَاحِيَةً، وَالْأَبَ نَاحِيَةً، وَأَقْعَدَ اَلصَّبِيَّ بَيْنَهُمَا. فَمَالَ إِلَى أُمِّهِ، فَقَالَ: "اَللَّهُمَّ اِهْدِهِ". فَمَالَ إِلَى أَبِيهِ، فَأَخَذَهُ.} أَخْرَجَهُ أَبُو دَاوُدَ، وَالنَّسَائِيُّ، وَالْحَاكِمُ
Kutoka kwa Raafi’ bin Sinaan[3] amesema kuwa: Yeye alisilimu, na mkewe akakataa kusilimu. Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akamkalisha mama upande mmoja na baba upande mwingine, na akamkalisha mtoto katikati yao, yule mtoto akawa ameegemea upande wa mama yake, Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) akaomba: “Ee Allaah! Muongoze (mtoto huyu).” Yule mtoto akaegemea upande wa baba yake akamchukua.[4] [Imetolewa na Abuu Daawuwd, An-Nasaaiy na Al-Haakim]
989.
وَعَنْ اَلْبَرَاءِ بْنِ عَازِبِ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، {أَنَّ اَلنَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَضَى فِي اِبْنَةِ حَمْزَةَ لِخَالَتِهَا، وَقَالَ: اَلْخَالَةُ بِمَنْزِلَةِ اَلْأُمِّ.} أَخْرَجَهُ اَلْبُخَارِيُّ
وَأَخْرَجَهُ أَحْمَدُ: مِنْ حَدِيثِ عَلَيٍّ فَقَالَ: {وَالْجَارِيَةُ عِنْدَ خَالَتِهَا، فَإِنَّ اَلْخَالَةَ وَالِدَةٌ}
Kutoka kwa Al-Baraai bin ‘Aazib (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa: Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) alihukumu kuhusu binti wa Hamza kwa mama yake mdogo na akasema: “Mama mdogo ni katika daraja yake mama.” [Imetolewa na Al-Bukhaariy]
Na kutoka kwa Ahmad ameipokea hadiyth ya ‘Aliy alisema: “Binti mdogo anafaa kulelewa na mama yake mdogo kwani mama mdogo ni mama.”
990.
وَعَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اَللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ {إِذَا أَتَى أَحَدَكُمْ خَادِمُهُ بِطَعَامِهِ، فَإِنْ لَمْ يُجْلِسْهُ مَعَهُ، فَلْيُنَاوِلْهُ لُقْمَةً أَوْ لُقْمَتَيْنِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ، وَاللَّفْظُ لِلْبُخَارِيِّ
Kutoka kwa Abuu Hurayrah (رَضِيَ اللهُ عَنْهُ) amesema Rasuli wa Allaah (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mmoja wenu atakapoletewa chakula na mtumishi wake iwapo hakumkalisha ale pamoja naye basi ampe tonge moja au matonge mawili.”[5] [Bukhaariy, Muslim na tamshi hili ni la Bukhaariy]
991.
وَعَنْ اِبْنِ عُمَرَ رَضِيَ اَللَّهُ عَنْهُمَا، عَنْ اَلنَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ قَالَ: {عُذِّبَتْ اِمْرَأَةٌ فِي هِرَّةٍ سَجَنَتْهَا حَتَّى مَاتَتْ، فَدَخَلْتِ اَلنَّارَ فِيهَا، لَا هِيَ أَطْعَمَتْهَا وَسَقَتْهَا إِذْ هِيَ حَبَسَتْهَا، وَلَا هِيَ تَرَكَتْهَا، تَأْكُلُ مِنْ خَشَاشِ اَلْأَرْضِ} مُتَّفَقٌ عَلَيْهِ
Kutoka kwa Ibn ‘Umar (رَضِيَ اللهُ عَنْهُمَا) amesema kuwa Nabiy (صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَآلِهِ وَسَلَّمْ) amesema: “Mwanamke kaadhibiwa kwa sababu ya paka, alimfunga hadi akafa, akaingizwa motoni kwa ajili ya paka. Hakumlisha wala hakumpa maji, wala hakumuacha ale vidudu vya ardhini.” [Bukhaariy, Muslim]
[1] Al-Hadhwaanah kwa lugha ya kiarabu ina maana ya kuhifadhi na kulinda. Kulingana na Istilahi ya kishariy’ah ina maana ya malezi na maangalizi anayopewa mtoto. Ikiwa mtu kamuacha mkewe na wote ni Waislamu na wana watoto, katika hali hii mwanamke huwa ana haki zaidi ya malezi ya mtoto. Mwanamme hawezi kuwachukua na kuwaweka mbali na mama yao kwa nguvu. Ikiwa mtoto au watoto wapo katika hatua ya kunyonyeshwa ni haki ya baba kumgharimia mahitaji na matumizi ya yule mtoto kwa muda wote akiwa ni mtoto anayenyonya. Mtoto ataendelea kuhudumiwa na baba yake ikiwa anakaa naye au anakaa na mama yake. Akiwa anakaa na mama yake itaendelea kuwa hivyo maadamu mama yule atakuwa hajaolewa tena hadi atakapofikia baleghe. Ikiwa mama kaolewa ulezi wa mtoto utahamia kwa baba yake. Kulingana na madhehebu ya Hanafi ni kuwa, atakapoolewa na jamaa wa mtoto, malezi na uangalizi wake utabaki kwa mama yake.
[2] Hadiyth iliyotangulia, mama ametangulizwa zaidi kwa ulezi wa mwanawe, wakati katika Hadiyth hii mwana anapewa uhuru wa kuchagua baina ya wazazi wake wawili. Sababu ni kuwa katika Hadiyth hii mtoto ameshakuwa mkubwa na mwenye uwezo zaidi wa kuchagua wapi pa kumfaa zaidi. Kwa hali hii tunajifunza kuwa mtoto anapokuwa ameshakuwa na hana haja ya ulezi na ulinzi wa wazazi wake ana khiyari ya kuchagua pa kuenda kati ya kwa baba na kwa mama.
[3] Huyu ni Abul-Hakam Al-Answaar Al-Madaniy ambaye alikuwa Swahaba, Abul-Qaasim bin Salam amesema katika Al-Answaab kuwa walikuwa ni kizazi cha Al-‘Atbun ambaye ni ‘Aamir bin Tha’alabah.
[4] Hadiyth hii inathibitisha kuwa hata ikiwa mama ni kafiri hakumnyima haki ya mwanawe, ikiwa mtoto keshapambanukiwa, hatoendelea kukaa nae.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/277
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9406&title=08-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%20%20-%20%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D9%8E%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%8E%D9%84%D9%86%D9%91%D9%90%D9%83%D9%8E%D8%A7%D8%AD%D9%90
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9407&title=01-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9529&title=02-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Kutangamana%20Na%20Wake
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9530&title=03-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Mahari
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9531&title=04-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Waliymah%20%28Karamu%20Ya%20Harusi%29
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9532&title=05-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Kugawa%20%28Zamu%29
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9533&title=05-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Kugawa%20%28Zamu%29
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9684&title=06-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20%20Mlango%20Wa%20Khul%E2%80%99%20
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9685&title=07-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Talaka
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9686&title=08-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20%28Talaka%20Ya%29%20Rejea
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9687&title=09-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Al-Iylaa%2C%20Dhwihaar%2C%20Kafaara
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9688&title=10-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Kulaaniana
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9689&title=11-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%3A%20Al-%E2%80%98Iddah%20%28Kukaa%20Eda%29%20Na%20Al-Ihdaad%20%28Matanga%29
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9690&title=12-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Kunyonya%20%28Mtoto%20Kunyonyeshwa%20Na%20Asiye%20Mamake%29%20
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F9969&title=13-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Matumizi
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10010&title=14-Buluwgh%20Al-Maraam%3A%20Kitabu%20Cha%20Nikaah%3A%20Mlango%20Wa%20Al-Hadhwaanah%20Malezi