Tarehe Ya Hijriy

Kibainisho Muhimu

Taqabbala Allaahu Minnaa Wa Minkum – Iydul-Adhw-haa Al-Mubaarak

 

Taqabbala Allaahu Minnaa Wa Minkum – Iydul-Adhw-haa Al-Mubaarak

 

 

Kwa Munaasabah huu wa furaha wa siku tukufu ya ‘Iyd Al-Adhw-haa tunapenda kuwawasilishia salaam zetu na du'aa njema kwenu wote, tukimuomba Allaah (Subhaanahu Wa Ta'alaa) Atughufurie dhambi zetu na Atuwache huru kutokana na Moto na Atutaqabalie 'amali zetu na zenu ‘TAQABBALA ALLAAHU MINNAA WA MINKUM’ (Hivi ndivyo Maswahaba watukufu walivyokuwa wakiambiana pindi wanapokutana katika siku ya 'Iyd).

 

Kadhaalika, tunamuomba Yeye Allaah ('Azza wa Jalla) kwa Majina Yake mazuri, na Sifa Zake tukufu, Awataqabalie Hujaji Hijjah yao na Atujaalie sote furaha, amani, mapenzi, siha na iymaan pamoja na thabaat katika masiku yote ya uhai wetu, na Atutakabalie du'aa zetu.

 

Msisahau kuendeleza Takbira mpaka tarehe 13 Dhul-Hijjah Kwa maelezo zaida tafadhali bonyeza viungo vifuatavyo:

 

Katazo La Swiyaam (Funga) Ayyaamut-Tashriyq: 11, 12, 13 Dhul-Hijjah Na Amali Za Kutenda

 

Ukumbusho Wa Takbiyr Katika Masiku Kumi Na Tatu Ya Dhul-Hijjah: Tarehe 1–13 Dhul-Hijjah

 

Bonyeza bango upate Takbira:

 

 

 

 

 

Share

Katazo La Swiyaam (Funga) Ayyaamut-Tashriyq: 11, 12, 13 Dhul-Hijjah Na Amali Za Kutenda

 

 

Katazo La Swiyaam (Funga) Ayyaamut-Tashriyq:

Tarehe 11, 12, 13 Dhul-Hijjah  Na Amali Za Kutenda

 

 Alhidaaya.com

 

 

Walio na ada ya kufunga Swawm za Sunnah za Jumatatu na Alkhamiys, au Ayyaamul-Biydhw haitoruhusiwa kufunga tarehe hizo kwani ni katika masiku yaliyokatazwa kufungwa.

  

Ayyaamut-Tashriyq ni masiku ya kula na kunywa; yanayoanzia siku ya pili baada ya ‘Iydul-Adhwhaa ambayo ni tarehe 11, 12 na 13 Dhul-Hijjah. Masiku haya yameitwa At-Tashriyq kwa sababu Hujaji walikuwa wakikata nyama vipande vipande na kuanikwa juani. Na pia imeitwa At-Tashriyq kwa sababu Swalaah ya 'Iyd huswaliwa baada ya kuchomoza jua, na ndio masiku matatu yaliyofuatia yakajulikana kwa jina hilo. Na pi siku hizi hujulikana kwa: ‘Siku za Minaa'

 

Katazo La Swawm Na 'Amali Za Kutenda:

 

 

a) Haifai Swawm (kufunga) katika Ayyamut-Tashriyq: 

 

Haifai kufunga masiku haya ya Tashriyq hata kama mtu alikuwa na mazowea ya Swawm za Sunnah kama vile Jumatatu, Alkhamiys au Ayyaamul-Biydhw. Dalili ya makatazo ni katika Hadiyth ifuatayo:   

 

عن أبي هريرة  أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بَعَثَ عَبْدَ اللَّهِ بْنَ حُذَافَةَ يَطُوفُ فِي مِنًى أَنْ: ((لَا تَصُومُوا هَذِهِ الْأَيَّامَ فَإِنَّهَا أَيَّامُ أَكْلٍ وَشُرْبٍ وَذِكْرِ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amehadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtuma 'Abdullaah bin Hudhaafah azunguke Minaa na atangaze: "Msifunge siku hizi, kwani hizi ni siku za kula na kunywa na kumdhukuru Allaah ‘Azza wa Jalla.” [At-Twabariy 4: 211]

 

Lakini anaweza mtu kufunga tarehe 14, 15 na 16 kukamilisha siku tatu ili apate fadhila za kufunga siku tatu kila mwezi. [Fataawaa ibn Baaz]

 

 

b) Kumdhukuru Allaah ('Azza wa Jalla) kwa Wingi:

 

Katika siku hizi inampasa Muislamu azidishe kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama Anavyosema:

((وَاذْكُرُواْ اللّهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ)

((Na mdhukuruni Allaah katika siku za kuhesabika.)) [Al-Baqarah: 203]

 

Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Siku za kuhesabika ni siku za tashriyq (11, 12, 13 Dhul-Hijjah) na siku maalumu ni siku za kumi za mwanzo za Dhul-Hijjah. [Al-Qurtwubiy: 3.3]

 

Pia kutamka Tabkiyr Al-Muqayyad (Takbiyr za kuthibitika mahali maalumu na nyakati maalumu za kukadirika) imekusudiwa kila baada ya Swalaah ya fardhi. Rejea kiungo kifutacho kupata maelezo na faida:

 

Amali Za Kutenda Ayyaamut-Tashriyq: Tarehe 11, 12, 13 Dhul-Hijjah Na Katazo La Swiyaam

 

 

Ukumbusho Wa Takbiyr Katika Masiku Kumi Na Tatu Ya Dhul-Hijjah: Tarehe 1–13 Dhul-Hijjah

 

 

Siku Kumi Bora Kabisa Za Allaah - 01 - 10 Dhul-Hijjah

 

 

Mdhukuru Allaah Kwa Wingi Na Omba Maghfirah Baada Ya Kutenda Mema Katika Siku Kumi Bora Kabisa Za Allaah

 

12-Dhul-Hijjah: Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

 

Fataawaa:

 

 

 

 

Wa biLlaahi At-Tawfiyq

 

 

 

Share

Ukumbusho Wa Takbiyr Katika Masiku Kumi Na Tatu Ya Dhul-Hijjah: Tarehe 1–13 Dhul-Hijjah

 

Ukumbusho Wa Takbiyr Katika Masiku Kumi Na Tatu Ya Dhul-Hijjah:

Tarehe 1 – 13 Dhul-Hijjah

 

Alhidaaya.com

 

 

Ndugu Waumini! Tukumbushane kuifufua Sunnah ya kuleta Takbiyr kuanzia unapoandama mwezi wa Dhul-Hijjah mpaka mwisho wa Ayyaamut-Tashriyq (Yaani kuanzia tarehe 1 Dhul-Hijjah mpaka 13 Dhul-Hijjah) baada ya Swalaatul-'Asr ndio kumalizika kwake kutokana na dalili zifuatazo:

 

Allaah ('Azza wa Jalla) Anaamrisha:

 

لِّيَشْهَدُوا مَنَافِعَ لَهُمْ وَيَذْكُرُوا اسْمَ اللَّـهِ فِي أَيَّامٍ مَّعْلُومَاتٍ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّن بَهِيمَةِ الْأَنْعَامِ ۖ

((Ili washuhudie manufaa yao; na walitaje Jina la Allaah katika siku maalumu kwa yale Aliyowaruzuku kati ya wanyama wenye miguu minne wa mifugo.    [Al-Hajj  28]

 

Na pia:

 

كَانَ إبْن عَمَر وَأبُو هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّه عَنْهُما يَخْرُجَانِ إِلَى السُّوقِ فِي أَيَّامِ العَشْرِ يُكَبِّرَانِ، وَيُكَبِّرُ النَّاسُ بِتَكْبِيرِهِمَا .

Ibn 'Umar na Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) walikuwa wakienda sokoni katika siku kumi (za Dhul-Hijjah) na kutamka Takbiyr kwa sauti na watu wakiwaigiza. [Al-Bukhaariy]

 

Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ ۚ

Na mdhukuruni Allaah katika siku za kuhesabika.  [Al-Baqarah: 203]

 

Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Siku za kuhesabika ni siku za tashriyq (11, 12, 13 Dhul-Hijjah) na siku maalumu ni siku za kumi za mwanzo za Dhul-Hijjah[Al-Qurtwubiy: 3.3]

 

Takbiyr katika masiku haya matukufu ni aina mbili:[1]

 

Takbiyr Al-Mutwlaq: Za Nyakati Zote:

 

Takbiyr wakati wote mchana na usiku, mahali popote ulipo, tokea unapoingia mwezi wa Dhul-Hijjah na inaendelea mpaka siku ya mwisho ya Tashriyq (tarehe 13 Dhul-Hijjah) na kumalizika baada ya kuingia Magharibi.

 

Takbiyr Al-Muqayyad: Za Kuthibitika Mahali Maalumu Na Nyakati Maalumu, Za Kukadirika:

 

Takbiyr baada ya kila Swalaah za fardhi na huanza baada ya Swalaah ya Alfajiri Siku ya 'Arafah mpaka mpaka baada ya Swalaah ya Alasiri siku ya mwisho ya Tashriyq (tarehe 13 Dhul-Hijjah).

 

Inavyopasa kufanya Takbiyr:

 

   اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ،  لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، وَلِلَّهِ الْحَمْد

Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, laa Ilaaha illa Allaah, Allaahu Akbar Allaahu Akbar WaliLLaahil-Hamd

 

Bonyeza bango upate takbiyrah kwa sauti:

 

 

 

[1] Takbiyr hizo za masiku haya matukufu zimetekelezwa na baadhi ya Maswahaba watukufu na ni Mustahabb (imependekezwa) na wengi katika Salaf wa madhehebu ya Hanbaliy, Ash-Shaafi’iyy, Hanafiy na wengineo kama ifuatavyo:  

Imaam An-Nawawiy - Al-Majmuw’ (5/32).

Ibn Rajab - Fat-hul-Baariy (6/125, 130).

Ibn Taymiyyah - Majmuw’ Al-Fataawaa (24/220. 222).

Imaam Ibn Baaz - Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb (13/355).

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn - Ash-Sharh Al-Mumti’ (5/166), Majmuw’ Fataawaa wa Rasaail Al-‘Uthyamiyn (16/262, 265).

 

Share

12-Dhul-Hijjah: Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

12-Dhul-Hijjah

Mafunzo Mbalimbali Ya Hajj

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

 

 

Ukumbusho Wa Mas-ala Ya Hajj

 

 

Ukumbusho Wa Kuzuia Kukata Kucha Na Nywele Kwa Anayenuia Kuchinja

 

 

 

Ukumbusho Wa Takbiyr Katika Masiku Kumi Na Tatu Ya Dhul-Hijjah: Tarehe 1–13 Dhul-Hijjah

 

 

Tunawakumbusha Kutamka Maneno Bora Kabisa Siku Ya ‘Arafah, Kuomba Maghfirah Na Kuepushwa Na Moto!

 

 

Nasaha Na Ukumbusho Wa Swawm Ya ‘Arafah Ili Ufutiwe Madhambi Ya Miaka Miwili!

 

 

 

Katazo La Swiyaam (Funga) Ayyaamut-Tashriyq: 11, 12, 13 Dhul-Hijjah Na Amali Za Kutenda

 

 

 

Nasiha

 

 

Umuhimu Wa Kukimbilia Kutekeleza Nguzo Ya Hajj  

 

 

Siku Kumi Bora Kabisa Za Allaah - 01 - 10 Dhul-Hijjah

 

 

Fadhila Za Siku Ya 'Arafah Na Yawmun-Nahr (Siku Ya Kuchinja) – Hajj

 

 

Kuchinja - Fadhila, Hikmah Na Hukmu Zake

 

Amali Za Kutenda Ayyaamut-Tashriyq: Tarehe 11, 12, 13 Dhul-Hijjah Na Katazo La Swiyaam

 

 

Mdhukuru Allaah Kwa Wingi Na Omba Maghfirah Baada Ya Kutenda Mema Katika Siku Kumi Bora Kabisa Za Allaah

 

 

Ratiba Ya ‘Ibaadah Za Kutekeleza Siku Tukufu Ya ‘Arafah

 

 

Vitabu:

 

 

 

 

 

http://www.alhidaaya.com/sw/swahiy_fiqh_as_sunnah

 

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Hajj Na 'Umrah

 

 

 

 

 

 

Fataawaa Za 'Ulamaa:

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Anayetia Niyyah Kuchinja Asikate Au Kunyoa Nywele Au Kukata Kucha

 

 

Al-Lajnah Ad-Daaimah: Nani Wa Kujizuia Kukata Nywele Na Kucha Katika Kuchinja (Udhwhiyah)?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Udhwhiyah (Kuchinja) Ni Sunnah Iliyosisitizwa Kwa Mwenye Uwezo

 

 

Imaam Ibn Baaz - Vipi Kuigawa Nyama Ya Udhw-hiyah

 

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kuigawa Nyama Ya Udhw-hiyah Kama Zawadi Au Swadaqah Iwe Freshi Si Ya Kupikwa

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Masharti Ya Udhwhiyah Ni Yepi?

 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Haijuzu Kumpa Mchinjaji Wa Udhw-hiyah Nyama Kama Ujira Wake

 

 

 

Imaam Ibn Baaz - Hukmu Ya Kuchinja Kwa Kutumia Mkono Wa Kushoto

 

 

 

Al-Lajnah Ad-Daa'imah: Hukmu Ya Kumuita Mtu Aliyetoka Kuhiji Jina La “Haji”

 

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Kujiita Au Kuitwa “Haji Fulani”

 

 

 

Kauli Za Salaf:

 

 

Imaam Ibn Hajar: Sababu Za Utukufu Wa Masiku Kumi Ya Dhul-Hijjah

 

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Chukua Fursa Kutenda Mema Masiku Kumi Dhul-Hijjah

 

 

 

Makala:

 

 

 

 

Mashairi:

 

 

Tufanye Mema Kwa Wingi, Siku Kumi Dhul-Hijjah

 

Hija Yao Taqabali, Tunakuomba Jalali

 

Twamshukuru Manani, Wamehiji Kwa Salama

 

 

 

Zingatio:

 

Zingatio: Rabb Awatakabalie Hijjah Zao Pamoja Na Sisi Kughufuriwa Madhambi Yetu

 

Zingatio: Hijjah Wajibu Wetu

 

Zingatio: Siku Kumi Tukufu Za Dhul-Hijjah

 

 

 

Maswali Na Majibu:

 

 

 

 

Uzushi Wa Unoadaiwa Ni Fadhila Za Siku Kumi Za Dhul-Hijjah

 

 

Kuzuia Kukata Nywele Na Kukata Kucha Ni Kwa Familia Nzima Au Kwa Mtu Mmoja Anayechinja Au Kugharamia Uchinjaji?

 

 

Fadhila Za Siku Ya ‘Arafah, Sababu Zake Na Tofauti Ya Nyakati Baina Ya Nchi

 

 

Dhul-Hijjah: Haifai Kufunga (Swawm) Ayyamut-Tashriyq (Masiku ya 11-13 Dhul-Hijjah)

 

 

Dhul-Hijjah: Inafaa Kufunga (Swawm) Siku Zote 9 Za Dhul-Hijjah?

 

 

Dhul-Hijjah: Inafaa Kulipa Deni La Ramadhwaan Pamoja Na Niyyah Ya Swawm Za Naawafil Kama Dhul-Hijjah?

 

 

Dhul-Hijjah: Kauli Za 'Ulamaa Kuhusu Hadiyth Za Mama Wa Waumini Za Swiyaam Siku 9 Dhul-Hijjah

 

 

Dhul-Hijjah: Nini Sababu Ya Swawm Ya 'Arafah?

 

 

Dhul-Hijjah: Swawm Ya 'Arafah Ipi Sahihi Kuwafuata Hujaji Au Kufuata Nchi Uliyoko?

 

 

Hukmu Ya Swawm Ijumaa Ikiwa Ni Siku Ya 'Arafah Au 'Aashuraa

 

 

 

 

 

 

 

Share