Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب آداب النَوم والاضْطِجَاع وَالقعُود والمَجلِس وَالجليس وَالرّؤيَا
01-Mlango Wa Adabu za Kulala na Kujilaza na Kukaa na Kikao na Waliomo katika Kikao na Ndoto
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن البَراءِ بن عازِبٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا أوَى إِلَى فِرَاشِهِ نَامَ عَلَى شِقِّهِ الأَيْمَن ، ثُمَّ قَالَ : (( اللَّهُمَّ أسْلَمْتُ نفسي إلَيْكَ ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إلَيْكَ ، وَفَوَّضْتُ أمْرِي إلَيْكَ ، وَألْجَأتُ ظَهْرِي إلَيْك ، رَغْبَةً وَرَهْبَةً إلَيْكَ ، لاَ مَلْجَأ وَلاَ مَنْجا مِنْكَ إِلاَّ إلَيكَ ، آمَنْتُ بكِتَابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ ، وَنَبِيِّكَ الَّذِي أرْسَلْتَ )) رواه البخاري بهذا اللفظ في كتاب الأدب من صحيحه .
Amesema Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Alikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapoyaendea malazi yake akilala kwa ubavu wake wa kulia, kisha akisema:
للَّهُمَّ أسْلَمْتُ نفسي إلَيْكَ ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إلَيْكَ ، وَفَوَّضْتُ أمْرِي إلَيْكَ ، وَألْجَأتُ ظَهْرِي إلَيْك ، رَغْبَةً وَرَهْبَةً إلَيْكَ ، لاَ مَلْجَأ وَلاَ مَنْجا مِنْكَ إِلاَّ إلَيكَ ، آمَنْتُ بكِتَابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ ، وَنَبِيِّكَ الَّذِي أرْسَلْتَ
"Allaahumma Aslamtu nafsiy Ilayka wawajahtu Wajhiy Ilayka wa Fawwadhtu Amriy Ilayka wa Alja'tu Dhahri Ilayka Raghbatan wa Rahbatan Ilayka laa Malja' wala Manjaa illaa Ilayka Aamantu Bikitaabikal Ladhiy Anzalta wa Bikitaabikal Ladhiy Anzalta wa Nabiyyikal Ladhiy Arsalta - Ee Rabb wangu! Hakika nimeikabidhi nafsi yangu Kwako na nikauelekeza uso wangu Kwako. Na jambo langu nimeliegemeza Kwako. Hali ya kupenda na kuhofu Kwako. Hakuna pa kukimbilia wala pa kusalimika na Wewe isipokuwa Kwako. Nimekiamini Kitabu Chako ambacho Umekiteremsha na Nabiy Wako ambaye Umemtuma." [Al-Bukhaariy kwa tamshi hili]
Hadiyth – 2
وعن البَراءِ بن عازِبٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أتَيْتَ مَضْجَعَكَ فَتَوَضَّأ وُضُوءكَ لِلْصَّلاَةِ ، ثُمَّ اضْطَجِعْ عَلَى شِقِّكَ الأَيْمَن ، وَقُلْ ...)) وذَكَرَ نَحْوَهُ ، وفيه : (( وَاجْعَلْهُنَّ آخِرَ مَا تَقُولُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhwiya Allaah 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Utakapoyaendea malazi yako tawadha kama unavyotawadha kwa ajili ya Swalaah. Kisha jilaze juu ya ubavu wako wa kulia, na sema:
للَّهُمَّ أسْلَمْتُ نفسي إلَيْكَ ، وَوَجَّهْتُ وَجْهِي إلَيْكَ ، وَفَوَّضْتُ أمْرِي إلَيْكَ ، وَألْجَأتُ ظَهْرِي إلَيْك ، رَغْبَةً وَرَهْبَةً إلَيْكَ ، لاَ مَلْجَأ وَلاَ مَنْجا مِنْكَ إِلاَّ إلَيكَ ، آمَنْتُ بكِتَابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ ، وَنَبِيِّكَ الَّذِي أرْسَلْتَ
"Allaahumma Aslamtu nafsiy Ilayka wawajahtu Wajhiy Ilayka wa Fawwadhtu Amriy Ilayka wa Alja'tu Dhahri Ilayka Raghbatan wa Rahbatan Ilayka laa Malja' wala Manjaa illaa Ilayka Aamantu Bikitaabikal Ladhiy Anzalta wa Bikitaabikal Ladhiy Anzalta wa Nabiyyikal Ladhiy Arsalta - Ee Rabb wangu! Hakika nimeikabidhi nafsi yangu Kwako na nikauelekeza uso wangu Kwako. Na jambo langu nimeliegemeza Kwako. Hali ya kupenda na kuhofu Kwako. Hakuna pa kukimbilia wala pa kusalimika na Wewe isipokuwa Kwako. Nimekiamini Kitabu Chako ambacho Umekiteremsha na Nabiy Wako ambaye Umemtuma." Na akasema: "Na uyajaaliye haya ni maneno ya mwisho utakayoyasema." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي مِنَ اللَّيْلِ إحْدَى عَشرَةَ رَكْعَةً ، فَإذا طَلَعَ الفَجْرُ صَلَّى رَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ ، ثُمَّ اضْطَجَعَ عَلَى شِقِّهِ الأَيْمَن حَتَّى يَجيءَ الْمُؤَذِّنُ فَيُؤْذِنَهُ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Na amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiswali rakaa kumi na moja za usiku, lakini pindi inapoingia Alfajiri alikuwa akiswali rakaa mbili hafifu (fupi), kisha akijilaza kwa ubavu wake wa kulia mpaka aje muadhini amuarifu ya kwamba watu wamejumuika (kwa ajili ya Swalaah)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن حُذَيْفَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم إِذَا أخَذَ مَضْجَعَهُ مِنَ اللَّيْلِ وَضَعَ يَدَهُ تَحْتَ خَدِّهِ ، ثُمَّ يَقُولُ : (( اللَّهُمَّ بِاسْمِكَ أمُوتُ وَأحْيَا )) وَإِذَا اسْتَيْقَظ قَالَ : (( الْحَمْدُ للهِ الَّذِي أحْيَانَا بَعْدَمَا أمَاتَنَا وَإِلَيْهِ النُشُورُ )) رواه البخاري .
Na amesema Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapoelekea kwa malazi yake usiku akiweka mkono wake chini ya shavu lake, kisha akisema: "Allaahumma Biismika Amuutu wa Ahyaa - Ee Rabb wangu! Kwa jina Lako nina kufa na kupata uhai." Na anapoamka alikuwa akisema: "Alhamdu Lillaahi ladhiy Ahyaana Ba'damaa Amaatana wa Ilayhi Nushuwr - Sifa njema ni za Allaah ambaye ametupa uhai baada ya kutufisha, ni Kwake tu ufufuo (marudio)." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن يَعيشَ بن طِخْفَةَ الغِفَارِيِّ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ أَبي : بينما أَنَا مُضْطَجِعٌ في الْمَسْجِدِ عَلَى بَطْنِي إِذَا رَجُلٌ يُحَرِّكُنِي برجلِهِ ، فَقَالَ : (( إنَّ هذِهِ ضجْعَةٌ يُبْغِضُهَا اللهُ )) ، قَالَ : فَنظَرْتُ ، فَإذَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم . رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Ya'iysh bin Twikhfah Al-Ghifariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba aliniambia baba yangu: Nilipokuwa nimejilaza katika Msikiti juu ya tumbo langu mara nikahisi mtu ananitingisha kwa mguu wake, akisema: "Hakika ulalaji huu Allaah haupendi." Akasema: "Nikamuangalia na kumuona kuwa ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 6
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَعَدَ مَقْعَدَاً لَمْ يَذْكُرِ الله تَعَالَى فِيهِ ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللهِ تَعَالَى تِرَةٌ ، وَمَنِ اضْطَجَعَ مَضجَعاً لاَ يَذْكُرُ اللهَ تَعَالَى فِيهِ ، كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللهِ تِرَةٌ )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ حسن .
Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote anayekaa kikao bila ya kumtaja Allaah Ta'aalaa ndani yake, atakuwa na upungufu mbele ya Allaah. Na yeyote anayejilaza katika malazi yake bila ya kumtaja Allaah Ta'aalaa ndani yake, atakuwa na upungufu mbele ya Allaah Ta'aalaa." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب جواز الاستلقاء عَلَى القفا ووضع إحدى الرِّجلين عَلَى الأخرى إِذَا لم يخف انكشاف العورة وجواز القعود متربعاً ومحتبياً
02-Mlango Wa Kujuzu Kulala kwa Maungo na Kuweka Mguu Mmoja juu ya Mwengine Ikiwa Hapana Hofu ya Kuonekana Utupu na Kujuzu Kukaa kwa Kukunja Mguu na Kufunga Kitambara Kiunini na Miguuni
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عبدِ اللهِ بن زيد رضي الله عنهما : أنَّه رأى رسولَ الله صلى الله عليه وسلم مُسْتَلْقِياً في الْمَسْجِدِ ، وَاضِعاً إحْدَى رِجْلَيْهِ عَلَى الأُخْرَى . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Zayd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa amelala kwa mgongo wake Msikitini na kuweka mguu wake mmoja juu ya mwengine." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن جابر بن سَمُرَة رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم إِذَا صَلَّى الفَجْرَ تَرَبَّعَ في مَجْلِسِهِ حَتَّى تَطْلُعَ الشَّمْسُ حَسْنَاء . حديث صحيح ، رواه أَبُو داود وغيره بأسانيد صحيحة .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa baada ya kuswali Alfajiri akikaa kitako kwa kukunja miguu yake mpaka jua lichomoze kwa kuonekana mng'aro wake." [Hadiyth Swahiyh: Abu Daawuwd na wengineo kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : رأيتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم بفناءِ الكَعْبَةِ مُحْتَبِياً بِيَدَيْهِ هكَذا ، وَوَصَفَ بِيَدَيْهِ الاحْتِبَاءَ ، وَهُوَ القُرْفُصَاءُ . رواه البخاري .
Na amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Nilimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiwa amekaa katika ukumbi wa Ka'bah na mikono yake imefunikwa hivi. Na akaonyesha kwa mikono yake jinsi alivyokaa kwa mikono yake kushika miguu iliyonyanyuliwa." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن قَيْلَةَ بنْتِ مَخْرَمَةَ رضي الله عنها ، قالت : رأيتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم وَهُوَ قَاعِدٌ القُرْفُصَاءَ ، فَلَمَّا رَأَيْتُ رسولَ الله المُتَخَشِّعَ في الجِلْسَةِ أُرْعِدْتُ مِنَ الفَرَقِ . رواه أَبُو داود والترمذي .
Na amesema Qaylah bint Makhramah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nilimuona Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)akiwa amekaa na mikono yake ikishika miundi yake na mapaja juu amenyanyua. Na nilipomuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hali ya kikao cha unyenyekevu nilitetemeka kwa hofu." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 5
وعن الشَّريدِ بن سُوَيْدٍ رضي الله عنه ، قَالَ : مَرَّ بي رسولُ الله صلى الله عليه وسلم وَأَنَا جَالِسٌ هكَذَا ، وَقَدْ وَضَعْتُ يَدِيَ اليُسْرَى خَلْفَ ظَهْرِي ، وَاتَّكَأتُ عَلَى أَليَةِ يَدي ، فَقَالَ : (( أَتَقْعُدُ قِعْدَةَ المَغْضُوبِ عَلَيْهِمْ ؟! )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيح .
Na amesema Shariyd bin Suwayd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alinipita wakati mmoja Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) nikiwa nimekaa hivi, nikiwa nimeuweka mkono wangu wa kushoto nyuma ya mgongo wangu na nikakaa chini juu ya matumbo ya vidole vyangu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliponiona nimekaa hivi akasema: "Je, unakaa kama kikao cha walioghadhibikiwa (waliokasirikiwa)?" [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب في آداب المجلس والجليس
03-Mlango Wa Adabu za Kikao na Wenye Kukaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لا يُقِيمَنَّ أحَدُكُمْ رَجُلاً مِنْ مَجْلِسِهِ ثُمَّ يَجْلِسُ فِيهِ ، وَلكِنْ تَوَسَّعُوا وَتَفَسَّحُوا )) وكَانَ ابْنُ عُمَرَ إِذَا قَامَ لَهُ رَجُلٌ مِنْ مَجْلِسِهِ لَمْ يَجْلِسْ فِيهِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asimpishe mmoja wenu mtu mwengine katika kikao chake kisha akakaa hapo, lakini toweni wasaa na toweni nafsi." Na alikuwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) anapompisha mtu katika kikazi chake, hakai tena hapo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا قَامَ أَحَدُكُمْ مِنْ مَجْلِسٍ ، ثُمَّ رَجَعَ إِلَيْهِ ، فَهُوَ أَحَقُّ بِهِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Akisimama mmoja wenu kutoka katika kikao chake kisha akakirudia huyo ana haki zaidi ya kikao hicho (kuliko mwengine yeyote)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جابر بن سَمُرَة رضي الله عنهما ، قَالَ : كُنَّا إِذَا أَتَيْنَا النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، جلَسَ أحَدُنَا حَيْثُ يَنْتَهِي . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Na amesema Jaabir bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Tulikuwa tunapomwendea Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hukaa mmoja wetu mahali ambapo litamuweka kwake baraza." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 4
وعن أَبي عبد الله سَلْمَان الفارسي رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم :(( لاَ يَغْتَسِلُ رَجُلٌ يَوْمَ الْجُمُعَةِ، وَيَتَطهَّرُ مَا اسْتَطَاعَ مِنْ طُهْرٍ ، وَيَدَّهِنُ مِنْ دُهْنِهِ، أَوْ يَمَسُّ مِنْ طِيب بَيْتِهِ ، ثُمَّ يَخْرُجُ فَلاَ يُفَرِّقُ بَيْنَ اثْنَينِ ، ثُمَّ يُصَلِّي مَا كُتِبَ لَهُ ، ثُمَّ يُنْصِتُ إِذَا تَكَلَّمَ الإمَامُ ، إِلاَّ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الجُمُعَةِ الأُخْرَى )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu 'Abdillaah Salmaan Al-Faarisiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haogi mmoja wenu siku ya Ijumaa na akajitwahirisha kadri ya uwezo wake na akajitia nyumbani kwake manukato kisha akaenda Msikitini na akawa hapasuwi safu kati ya watu wawili, kisha akaswali kiasi chake, kisha akakaa kimya akamsikia Imamu wakati akizungumza (akitoa Khutbah) isipokuwa atasamehewa kuanzia Ijumaa ile mpaka nyingine." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن عمرو بن شُعَيْب، عن أبيهِ، عن جَدِّهِ رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَحِلُّ لِرَجُلٍ أنْ يُفَرِّقَ بَيْنَ اثْنَيْنِ إِلاَّ بإذْنِهِمَا )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال: (( حديث حسن ))
وفي رواية لأبي داود : (( لاَ يُجْلسُ بَيْنَ رَجُلَيْنِ إِلاَّ بِإذْنِهِمَا ))
Imepokewa kutoka kwa 'Amru bin Shu'ayb kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu yake (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Si halali kwa mtu yeyote kuwatenganisha kati ya watu wawili ila kwa idhini yao." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Na katika riwaayah ya Abu Daawuwd: "Hakika mtu baina ya watu wawili ila kwa idhini yao."
Hadiyth – 6
وعن حذيفة بن اليمان رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم لَعَنَ مَنْ جَلَسَ وَسَطَ الحَلْقَةِ . رواه أَبُو داود بإسنادٍ حسن .
وروى الترمذي عن أبي مِجْلَزٍ : أنَّ رَجُلاً قَعَدَ وَسَطَ حَلْقَةٍ ، فَقَالَ حُذَيْفَةُ : مَلْعُونٌ عَلَى لِسَانِ مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم - أَوْ لَعَنَ اللهُ عَلَى لِسَانِ مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم - مَنْ جَلَسَ وَسَطَ الحَلْقَةِ . قَالَ الترمذي : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Hudhayfah bin Al-Yamaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimlaani mtu mwenye kukaa katikati ya duara ya watu." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy kwa Isnaad Hasan]
Amepokea At-Tirmidhiy kutoka kwa Abu Mijlaz kwamba kulikuwa na mtu aliyekaa katikati ya duara, Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) akasema: "Amelaaniwa katika ulimi wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) au Allaah amemlaani kutoka kwa ulimi wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), mwenye kukaa katikati ya duara." [Amesema At-Tirmidhiy kuwa hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن أَبي سعيدٍ الخدريِّ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( خَيْرُ المَجَالِسِ أوْسَعُهَا )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيح عَلَى شرط البخاري .
Na amesema Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Bora ya vikao ni vyenye wasaa." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh kulingana na sharti ya Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 8
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ جَلَسَ في مَجْلِسٍ ، فَكَثُرَ فِيهِ لَغَطُهُ فَقَالَ قَبْلَ أنْ يَقُومَ مِنْ مَجْلِسِهِ ذَلِكَ : سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ وَبِحَمْدِكَ ، أشْهَدُ أنْ لا إلهَ إِلاَّ أنْتَ ، أسْتَغْفِرُكَ وَأَتُوبُ إلَيْكَ ، إِلاَّ غُفِرَ لَهُ مَا كَانَ في مَجْلِسِهِ ذَلِكَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote anayekaa katika baraza na mazungumzo yakawa mengi (yasiyo mfaidisha Aakhera yake), akawa ni mwenye kusema kabla ya kuondoka kwenye kikazi hicho: 'Subhaanaka Allaahumma wa Bihamdika Ashhadu an Laa Illaaha illa Anta Astaghfiruka wa Atuubu Ilayka - Kutakasika na maovu ni Kwako Ee Rabb wangu wa haki pamoja na sifa Zako nzuri nakiri kwa moyo na kubaini kwa ulimi kwamba hapana Rabb mwenye haki ya kuabudiwa ila Wewe nakuomba msamaha na ninarudi Kwako,' isipokuwa husamehewa yale yaliokuwa katika kikao hicho." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 9
وعن أَبي بَرْزَة رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يقولُ بأَخَرَةٍ إِذَا أرَادَ أنْ يَقُومَ مِنَ الْمَجْلِسِ : (( سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ وبِحَمْدِكَ ، أشْهَدُ أنْ لا إلهَ إِلاَّ أنتَ أسْتَغْفِرُكَ وَأَتُوبُ إليكَ )) فَقَالَ رَجُلٌ : يَا رسولَ الله ، إنَّكَ لَتَقُولُ قَوْلاً مَا كُنْتَ تَقُولُهُ فِيمَا مَضَى ؟ قَالَ : (( ذَلِكَ كَفَّارَةٌ لِمَا يَكُونُ في المَجْلِسِ )) رواه أَبُو داود ، ورواه الحاكم أَبُو عبد الله في " المستدرك " من رواية عائشة رضي الله عنها وقال : (( صحيح الإسناد )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Barzah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alikuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema mwisho wa umri wake dua ifuatayo pindi alipokuwa anasimama kuondoka katika baraza: "Subhaanaka Allaahumma wa Bihamdika Ashhadu an Laa Illaah illa Anta Astaghfiruka wa Atuubu Ilayka." "Kutakasika na maovu ni Kwako Ee Rabb wangu wa haki pamoja na sifa Zako nzuri nakiri kwa moyo na kubaini kwa ulimi kwamba hapana Rabb mwenye haki ya kuabudiwa ila Wewe nakuomba msamaha na ninarudi Kwako." Akasema mtu mmoja: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika wewe unasema maneno ambayo hukuwa ukiyasema kabla." Akasema: "Hiyo ni kafara kwa yanayotendeka katika baraza." [Abu Daawuwd na Al-Haakim Abu 'Abdillaah katika Al-Mustadrak yake kwa riwaayah ya 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) na akasema kuwa Isnaad yake ni Swahiyh].
Hadiyth – 10
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَلَّمَا كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَقُومُ مِنْ مَجْلِسٍ حَتَّى يَدْعُوَ بِهؤلاء الدَّعَواتِ : (( اللَّهُمَّ اقْسِمْ لَنَا مِنْ خَشْيَتِكَ مَا تَحُولُ بِهِ بَيْنَنَا وَبَيْنَ مَعَاصِيكَ ، وَمِنْ طَاعَتِكَ مَا تُبَلِّغُنَا بِهِ جَنَّتَكَ ، وَمِنَ الْيَقِينِ مَا تُهَوِّنُ عَلَيْنَا مَصَائِبَ الدُّنْيَا ، اللَّهُمَّ مَتِّعْنَا بأسْمَاعِنا ، وَأَبْصَارِنَا ، وقُوَّتِنَا مَا أحْيَيْتَنَا ، وَاجْعَلْهُ الوارثَ مِنَّا ، وَاجْعَلْ ثَأرَنَا عَلَى مَنْ ظَلَمَنَا ، وَانْصُرْنَا عَلَى مَنْ عَادَانَا ، وَلاَ تَجْعَلْ مُصيبَتَنَا فِي دِينِنَا ، وَلاَ تَجْعَلِ الدُّنْيَا أَكْبَرَ هَمِّنَا ، وَلاَ مَبْلَغَ عِلْمِنَا ، وَلاَ تُسَلِّطْ عَلَيْنَا مَنْ لاَ يَرْحَمُنَا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba: Ilikuwa nadra sana kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuondoka katika kikao bila kuomba dua ifwatayo: "Allaahummaqsim Lanaa min Khashyatika maa tahuulu bihi baynana wa bayna Ma'aswiyka. Wa min Twaa'atika maa Tubalighunaa bihi Janattaka wa minal yaqiyni maa Tuhawwinu 'alayna maswaa'ibud Dunya. Allaahumma matti'naa biasmaa'inaa wa Abswaarinaa wa quwwatinaa maa ahyaytanaa waj'alhul waaritha minna waj'al tha'ranaa 'alaa man dhalamana wansurnaa 'alaa man 'aadaanaa walaa taj'al muswiibatanaa fii Diyninaa walaa taj'alid Dunya akbara hamminaa walaa mablagha 'ilminaa walaa tusallitw 'alayna man laa yarhamunaa." "Ee Rabb wangu! Tupatie hofu kubwa Kwako ambayo itakuwa ni kikwazo baina yetu na maasia; na kukutii Wewe ambako kutatusaidia kupata Pepo Yako; na Utupatie yakini (na Imaani) ambayo itatusaidia katika masikizi yenu na kuona kwetu na nguvu zetu maadamu Umetupatia uhai na Utujaalie ni warithi (na tufaidike) kwazo; na Ujaalie uchungu kutoka kwetu kwa wenye kutudhulumu, na Utusaidie dhidi ya maadui zetu; wala Usitujaalie kuwa na misiba katika Dini yetu; na Usitufanye dunia kuwa hamu yetu kubwa wala Usiiwinje elimu yetu na Usituchagulie kiongozi juu yetu ambaye hataturehemu." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 11
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ قَوْمٍ يَقُومُونَ مِنْ مَجْلِسٍ لاَ يَذْكُرُونَ الله تَعَالَى فِيهِ ، إِلاَّ قَامُوا عَنْ مِثْل جِيفَةِ حِمَارٍ ، وَكَانَ لَهُمْ حَسْرَةٌ )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna kaumu yeyote itainuka katika kikazi (kikao) ambacho hakimtaji Allaah Ta'aalaa ndani yake isipokuwa wanainuka (kuondoka) mfano wa punda mfu na watakuwa na majuto makuu kwao." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 12
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا جَلَسَ قَوْمٌ مَجْلِساً لَمْ يَذْكُرُوا الله تَعَالَى فِيهِ ، وَلَمْ يُصَلُّوا عَلَى نَبِيِّهِمْ فِيهِ ، إِلاَّ كَانَ عَلَيْهِمْ تِرَةٌ ؛ فَإنْ شَاءَ عَذَّبَهُمْ ، وَإنْ شَاءَ غَفَرَ لَهُمْ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kaumu haitakaa katika kikao ambacho ndani yake hatajwi Allaah Ta'aalaa wala hawamswalii Nabiy wao isipokuwa watakumbwa na upungufu. Akipenda Atawaadhibu na akipenda Atawasamehe." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 13
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَعَدَ مَقْعَداً لَمْ يَذْكُر الله تَعَالَى فِيهِ كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللهِ تِرَةٌ ، وَمَنْ اضْطَجَعَ مَضْجَعَاً لاَ يَذْكُرُ الله تَعَالَى فِيهِ كَانَتْ عَلَيْهِ مِنَ اللهِ تِرَةٌ )) رواه أَبُو داود .
Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anayekaa kikao chochote kile asimdhukuru Allaah katika kikao hicho basi ana dhambi kutoka kwa Allaah, na anayelala sehemu yeyote ile kisha asimdhukuru Allaah wakati wakuinuka sehemu hiyo basi ana dhambi kwa Allaah." [Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الرؤيا وَمَا يتعلق بها
04-Mlango Wa Ndoto na Yanayohusiana Nayo
Alhidaaya.com [4]
قَالَ الله تَعَالَى:
وَمِنْ آيَاتِهِ مَنَامُكُم بِاللَّيْلِ وَالنَّهَارِ ﴿٢٣﴾
Na katika Aayaat (ishara, dalili) Zake ni kulala kwenu usiku na mchana. [Ar-Ruwm: 23]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لَمْ يَبْقَ مِنَ النُّبوَّةِ إِلاَّ المُبَشِّرَاتِ )) قالوا : وَمَا المُبَشِّرَاتُ ؟ قَالَ : (( الرُّؤْيَا الصَّالِحَةُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) aliyesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna ishara ya Unabiy iliyobakia isipokuwa bishara njema (Mubashshiraat)." Wakasema: "Bishara njema ni nini?" Akasema: "Ndoto ya kweli." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا اقْتَرَبَ الزَّمَانُ لَمْ تَكَدْ رُؤيَا المُؤْمِنِ تَكْذِبُ ، وَرُؤْيَا الْمُؤْمِنِ جُزْءٌ مِنْ سِتَّةٍ وَأرْبَعِينَ جُزْءاً مِنَ النُّبُوَّةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية : (( أصْدَقُكُمْ رُؤْيَا ، أصْدَقُكُمْ حَدِيثاً )) .
Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Zama zinapokaribia (za kufufuliwa) ndoto ya Muumini haitaongopa, na ndoto ya Muumini ni sehemu moja ya sehemu arubaini na sita ya Unabiy." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Na katika riwaaya nyingine: "Ndoto za kweli ni kwa wale miongoni mwenu walio wakweli katika mazungumzo."
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ رَآنِي في المَنَامِ فَسَيَرَانِي في اليَقَظَةِ – أَوْ كَأنَّما رَآنِي في اليَقَظَةِ – لاَ يَتَمَثَّلُ الشَّيْطَانُ بِي )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwake Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Aliyeniona usingizini basi ataniona akiwa macho (Aakhera) au kama kwamba ameniona akiwa macho, na shetani hajifananisha na mimi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي سعيدٍ الخدرِيِّ رضي الله عنه : أنَّه سَمِعَ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إِذَا رَأى أحَدُكُمْ رُؤيَا يُحِبُّهَا ، فَإنَّمَا هِيَ مِنَ اللهِ تَعَالَى ، فَلْيَحْمَدِ اللهَ عَلَيْهَا ، وَلْيُحَدِّثْ بِهَا – وفي رواية : فَلاَ يُحَدِّثْ بِهَا إِلاَّ مَنْ يُحِبُّ – وَإِذَا رَأَى غَيْرَ ذَلِكَ مِمَّا يَكْرَهُ ، فإنَّمَا هِيَ مِنَ الشَّيْطَانِ ، فَلْيَسْتَعِذْ مِنْ شَرِّهَا ، وَلاَ يَذْكُرْهَا لأَحَدٍ ؛ فَإنَّهَا لا تَضُرُّهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy kwamba amemsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Anapoona mmoja wenu ndoto nzuri, hakika hiyo ni (baraka) kutoka kwa Allaah Ta'aalaa, hivyo anatakiwa amsifu na amshukuru Allaah na awahadithie wengine.
Na katika riwaayah nyengine: Asiwahadithie isipokuwa wale anaowapenda tu. Na anapoona ndoto kinyume na hivyo (ndoto mabaya), hakika hiyo inatokana na shetani hivyo ajilinde kwa Allaah na shari ya ndito hiyo na wala asimueleze yeyote. Kama atafanya hivyo haita mdhuru." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي قَتَادَة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( الرُّؤْيَا الصَّالِحَةُ – وفي رواية : الرُّؤْيَا الحَسَنَةُ – مِنَ اللهِ ، وَالحُلُمُ مِنَ الشَّيْطَانِ ، فَمَنْ رَأى شَيْئاً يَكْرَهُهُ فَلْيَنْفُثْ عَن شِمَالِهِ ثَلاَثاً ، وَلْيَتَعَوَّذْ مِنَ الشَّيْطَانِ ؛ فإنَّهَا لا تَضُرُّهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ndoto njema -
Na katika riwaayah nyengine: Ndoto nzuri inatoka kwa Allaah, na ndoto mbaya, inatoka kwa shetani, hivyo anapoota mmoja wenu ndoto asiyoipenda basi anapoamka, ateme, kushotoni mwake mara tatu. Na ajilinde kwa Allaah kutokana na shetani, kama atafanya hivyo haita mdhuru." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن جابر رضي الله عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا رَأى أحَدُكُمْ الرُّؤْيَا يَكْرَهُهَا ، فَلْيَبْصُقْ عَنْ يَسَارِهِ ثَلاثَاً ، وَلْيَسْتَعِذْ بِاللهِ مِنَ الشَّيْطَانِ ثَلاَثاً ، وَلْيَتَحَوَّل عَنْ جَنْبِهِ الَّذِي كَانَ عَلَيْهِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: "Anapoona mmoja wenu ndoto anayoichukia, ateme (kwa kupeleka mdomo bila kutokwa na mate) kushotoni mwake mara tatu. Na atake ulinzi kutoka kwa Allaah dhidi ya shetani mara tatu na ageuke upande mwingine katika malazi yake." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن أَبي الأسقع واثِلةَ بن الأسقعِ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ مِنْ أعْظَمِ الفِرَى أنْ يَدَّعِيَ الرَّجُلُ إِلَى غَيرِ أبِيهِ ، أَوْ يُرِي عَيْنَهُ مَا لَمْ تَرَ ، أَوْ يَقُولَ عَلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم مَا لَمْ يَقُلْ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abil Asqa'i Waathilah bin al-Asqa'i (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika miongoni mwa uwongo mkubwa ni mtu kudai kwa baba asiyekuwa wake, au kudai kuwa ameona kitu (katika ndoto) kwa macho yake lakini hajaona, au anamsingizia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa amesema jambo ambalo hakusema." [Al-Bukhaariy]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/280
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10318&title=04-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Kitabu%20Cha%20Nidhamu%20Za%20Kulala%20-%20%D8%A2%D8%AF%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%86%D9%91%D9%8E%D9%88%D9%85
[4] http://www.alhidaaya.com/
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11016&title=01-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Adabu%20za%20Kulala%20na%20Kujilaza%20na%20Kukaa%20na%20Kikao%20na%20Waliomo%20katika%20Kikao%20na%20Ndoto
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11017&title=02-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kujuzu%20Kulala%20kwa%20Maungo%20na%20Kuweka%20Mguu%20Mmoja%20juu%20ya%20Mwengine%20Ikiwa%20Hapana%20Hofu%20ya%20Kuonekana%20Utupu%20na%20Kujuzu%20Kukaa%20kwa%20Kukunja%20Mguu%20na%20Kufunga%20Kitambara%20Kiunini%20na%20Miguuni
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11018&title=03-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Adabu%20za%20Kikao%20na%20Wenye%20Kukaa
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11019&title=04-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ndoto%20na%20Yanayohusiana%20Nayo