Malaika
Alhidaaya.com [1]
60: Nafasi Ya Malaika Kwa Waumini
(08)– Malaika Wanasajili Maneno Mema Wanayotamka Waja
Imepokelewa toka kwa Rifa’ah bin Raafi Az-Zuraqiy (Radhwiya Allaah ‘anhu):
قَالَ كُنَّا يَوْمًا نُصَلِّي وَرَاءَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا رَفَعَ رَأْسَهُ مِنَ الرَّكْعَةِ قَالَ " سَمِعَ اللَّهُ لِمَنْ حَمِدَهُ ". قَالَ رَجُلٌ وَرَاءَهُ رَبَّنَا وَلَكَ الْحَمْدُ، حَمْدًا كَثِيرًا طَيِّبًا مُبَارَكًا فِيهِ، فَلَمَّا انْصَرَفَ قَالَ " مَنِ الْمُتَكَلِّمُ ". قَالَ أَنَا. قَالَ " رَأَيْتُ بِضْعَةً وَثَلاَثِينَ مَلَكًا يَبْتَدِرُونَهَا، أَيُّهُمْ يَكْتُبُهَا أَوَّلُ "
“Tulikuwa siku moja tunaswali nyuma ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na aliponyanyua kichwa chake toka kwenye rukuu alisema: Sami’a Allaah liman hamidah (Allaah Amemsikia aliyemhimidi). Mtu mmoja nyuma yake akasema: Rabbanaa walakal hamdu, hamdan kathiyran mubaarakan fiyh (Ee Mola wetu, ni Yako himdi, himdi nyingi njema iliyo na baraka ndani yake). Alipomaliza swalah akauliza: Nani aliyetamka? Nikasema: Ni mimi. Akasema: Nimewaona Malaika thelathini na kidogo hivi wakilishindania, nani awe wa mwanzo kuliandika kabla ya mwenziye”. [Swahiyhul Bukhaariy (799)]
Hadiyth hii inatufunza fadhla kubwa ya kumhimidi Allaah na kumdhukuru, na pia uhalali kwa maamuma kusoma dhikri kwa sauti kidogo nyuma ya imamu bila kumbughudhi aliye karibu yake.
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11796&title=60-Malaika%3A%20%20%20Nafasi%20Ya%20Malaika%20Kwa%20Waumini%3A%20%20%20%20%2808%29%E2%80%93%20Malaika%20Wanasajili%20Maneno%20Mema%20Wanayotamka%20Waja