Swahiyh Fiqh As-Sunnah
كِتَابُ الزَّوَاجِ
Kitabu Cha Ndoa
الخِطْبَةُ وأَحْكَامُهَا
Posa Na Hukumu Zake
Alhidaaya.com [1]
02: Ni Nani Anayekabidhiwa Posa?
1- Kiasili, posa inapelekwa kwa walii wa mwanamke:
Toka kwa ‘Urwah:
"أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ خَطَبَ عَائِشَةَ إِلَى أَبِي بَكْرٍ، فَقَالَ لَهُ أَبُو بَكْرٍ: إِنَّمَا أَنَا أَخُوكَ، فَقَالَ: أَنْتَ أَخِي فِي دِينِ اللَّهِ وَكِتَابِهِ وَهِىَ لِي حَلاَلٌ"
“Kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimweleza Abu Bakr shauri la kumposa ‘Aaishah. Abu Bakr akamwambia: “Hakika mimi ni nduguyo. Rasuli akamwambia: “Wewe ni ndugu yangu katika Dini ya Allaah na Kitabu Chake, lakini yeye kwangu ni halali”. [Imechakatwa na Al-Bukhaariy (5081)]
2- Mwanamke mkomavu anayejitambua anaweza kupokea posa ya kuchumbiwa yeye mwenyewe au kuikataa:
Ni kwa Hadiyth ya Ummu Salamah:
"لَمَّا مَاتَ أَبُو سَلَمَةَ أَرْسَلَ إِلَىَّ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ حَاطِبَ بْنَ أَبِي بَلْتَعَةَ يَخْطُبُنِي لَهُ فَقُلْتُ: إِنَّ لِي بِنْتًا وَأَنَا غَيُورٌ"
“Alipokufa Abu Salamah, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimtuma Haatwib bin Abu Balta’ah aniletee posa yake ya kunichumbia mimi. Nikamwambia: Mimi nina binti, na mimi nina wivu sana”. [Hadiyth Swahiyh. Muslim na An-Nasaaiy (6/81)]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11864&title=02-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Kitabu%20Cha%20Ndoa%3A%20Posa%20Na%20Hukumu%20Zake%3A%20Ni%20Nani%20Anayekabidhiwa%20Posa%3F%20%20