Tarehe Ya Hijriy

Kibainisho Muhimu

Ukumbusho Wa Swiyyaam (Funga) Za Ayyaamul-Biydhw Tarehe 13, 14, 15

 

Swiyaam (Funga) Za Siku Tatu Kila Mwezi Thawabu Zake

Ni Sawa Na Thawabu Za Swiyaam Za Milele!

Alhidaaya.com

 

 

Swiyaam (funga) za Ayyaamul-Biydhw (Masiku Meupe) ni tarehe 13, 14, 15 katika kila mwezi wa Kiislamu (Hijriyyah).  

 

 

Tanbihi: Isipowezekana kufunga Swiyaam za Ayyaamul-Biydhw, basi inajuzu kufunga siku tatu zozote nyengine katika mwezi ili kupata thawabu za Milele, na si lazima zifungwe mfululizo.

 

 

عَنْ أَبي ذَرٍّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيهِ وَسَلَّمَ:((مَنْ صَامَ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ثَلاثَةَ أَيَّامٍ فَذَلِكَ صِيَامُ الدَّهْرِ)) فَأَنْزَلَ اللهُ تُصْدِيقَ ذَلِكَ في كِتَابِهِ الْكَرِيمِ: ((مَنْ جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا))، الْيَوْمُ بِعَشَرَةِ أَيّامٍ. أخرجه أحمد والترمذي وقال حديث حسن ، والنسائي وابن ماجه وابن خزيمة

Imepokelew a kutoka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Yeyote atakayefunga (Swawm) kila mwezi siku tatu, ni sawa na Swawm ya milele)) Kisha Allaah Akateremsha Aayah ithibitishayo hayo: “Atakayekuja kwa 'amali nzuri basi atapata (thawabu) kumi mfano wa hiyo.” Siku moja kwa malipo ya siku kumi. [Imepokewa na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Hasan, An Nasaaiy na Ibn Maajah, Ibn Khuzaymah na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Al-Irwaa (4/102)]. Aayah: Suwrat Al-An’aam (160)]

 

Maana Ya Al-Biydhw:  Masiku hayo yameitwa ‘Al-Biydhw’ (meupe) sababu usiku wa siku hizo hung'aa kutokana na mwanga wa mwezi. Ayyaam Al-Biydhw (Masiku Meupe) tarehe zake ni 13, 14 na 15 katika kila mwezi wa kalenda ya Kiislamu. Dalili ni Hadiyth zifuatazo:

 

Bonyeza Upate fadhila za Ayyaamul-Biydhw, fadhila za Swawm ya Jumatatu na Alkhamiys na fadhila za Swawm kwa ujumla.

 

 

Share

Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

'Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

 

Alhidaaya.com

 

 

AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Kutuendeleza uhai katika mwezi mwengine mtukufu.  Ni fursa nyingine ya kutenda mema tuchume thawabu nyingi. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla haijafika siku ya kuaga kwetu dunia.

 

Utukufu wa miezi hiyo mitukufu imetajwa katika Qur-aan na Sunnah: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾

Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo, (iko miezi) minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu (kwa kufanya maasi), na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]

 

Na miezi hiyo minne mitukufu imetajwa katika Hadiyth ifuatayo:

 

عن أبي بَكْرَةَ رضي الله عنه عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أنه قَالَ:  ((إن الزَّمَانَ قَدْ اسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْمَ خَلَقَ اللَّهُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ السَّنَةُ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ثَلاثٌ مُتَوَالِيَاتٌ ذُو الْقَعْدَةِ وَذُو الْحِجَّةِ وَالْمُحَرَّمُ وَرَجَبُ مُضَرَ الَّذِي بَيْنَ جُمَادَى وَشَعْبَانَ))

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika mgawano wa zama umerudi katika hali yake ya asili siku Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Mwaka una miezi kumi na mbili; minne miongoni ya hiyo ni mitukufu, mitatu inafuatana pamoja; Dhul-Qa'adah, Dhul-Hijjah na Muharram, mwengine ni Rajab wa (kabila la) Mudhwarr ambao uko baina ya Jumaadaa na Sha'baan))  [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Imaam Atw-Twabariy amesema:

 

 

Share

11-Dhul-Qa'dah: Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

11-Dhul-Qa'dah

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri: Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

 

 

 

'Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

 

'Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

 

Alhidaaya.com

 

Ni fursa nyingine ya Waumini kutilia juhudi kubwa ya kutenda mema, ili kujichumia thawabu tele katika Miezi Mitukufu. Utukufu wa miezi hiyo imetajwa katika Qur-aan na Sunnah: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):

 

 إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾

Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo, (iko miezi) minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu (kwa kufanya maasi), na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa. [At-Tawbah: 36]

 

Na miezi hiyo minne mitukufu imetajwa katika Hadiyth ifuatayo:

 

Endelea....

 

Umuhimu Wa Kukimbilia Kutekeleza Nguzo Ya Hajj

 

 

 

Sababu Za Kuwa Na Miezi Mitukufu -- Maswali: Taqwa - Tazkiyyah

 

Tofauti Ya Miezi Ya Kiislamu (Hijriyyah) Na Ya Miladi Zipi Sifa Zake?

 

 

Share