33-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Jukumu La Ushahidi Liko Kwa Yule Anayedai Na Kula Kiapo Kunamuwajibikia Yule Anayekanusha

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 33

 

البَيِّنَةُ على المُدَّعِى والْيَمينُ على من أَنْكَرَ

 

Jukumu La Ushahidi Liko Kwa Yule Anayedai

 

Na Kula Kiapo Kunamuwajibikia Yule Anayekanusha

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عن ابن عَبَّاسٍ رضي اللُه عنهما: أن رسولَ الله صلى الله عليه وسلم قال: ((لَو يُعْطَى النَّاسُ بِدَعْوَاهُمْ لادَّعَى رِجَالٌ أموالَ قَوْمٍ ودِماءَهُمْ لَكِنِ البَيِّنَةُ على المُدَّعِى والْيَمينُ على من أَنْكَرَ))  حَدِيثٌ حَسَنٌ، رَوَاهُ الْبَيْهَقِيّ وَغَيْرُهُ هَكَذَا، وَبَعْضُهُ فِي  الصَّحِيحَيْنِ

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kama watu wangelipewa kwa mujibu  wa madai yao, watu wangelidai mali na damu za wenzao (uhai) lakini jukumu la ushahidi liko kwa yule anayedai na kula kiapo kunawajibika kwa yule anayekanusha (kuwa hakutenda)”  [Al-Bayhaqiy na wengineo. Ni Hadiyth Hasan na baadhi yake imo katika Asw-Swahiyhayni]

 

 

 

Share