Skip navigation.
Home kabah

Faidika Na Chuma Katika Ramadhaan

 


 

Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,

Ndugu wapenzi,

Tunawaombea kheri nyingi na Ramadhaan njema itakayokuwa  Maqbuul  na dhambi za kughufuriwa  Inshaa-Allaah.

Kadhaalika tunapenda kuwajulisha kuwa tumewakusanyia mambo mengi mbalimbali ya kusoma na kusikiliza yanayohusu mwezi mtukufu wa Ramadhaan, tukitumai kwamba mtafaidika nayo; muweze kubakia katika hali ya Iymaan na Ucha Mungu daima. Pia mnufaike nayo na muweze kuchuma thawabu nyingi kwa kuyafanyia kazi yale yote mnayojifunza na mtoke katika mwezi huu mtukufu zikiwa Swawm zenu zimekubaliwa na madhambi kughufuriwa pamoja na sisi sote. Tunawomba msitutasahau kwa du'aa zenu.

Nasiha Ya Ijumaa

Laylatul-Qadr- Vipi Uweze Kuupata Usiku Huu?

Tunaingia   kumi la mwisho, kumi ambalo ndani yake kuna siku tukufu, siku ya Laylatul-Qadr, ambayo ibada yake ni bora kuliko ibada ya miezi elfu. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):  

﴿ بِسْمِ اللّهِ الرَّحْمَنِ الرَّحِيمِ ﴾ (( إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ)) (( وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ)) (( لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ))  ((تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ)) ((   سَلَامٌ هِيَ حَتَّى مَطْلَعِ الْفَجْرِ))

KWA JINA LA ALLAAH MWINGI WA REHMA MWENYE KUREHEMU. ((Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatul Qadr. (Usiku wa Makadirio[Majaaliwa])) ((Na nini kitachokujuulisha nini Laylatul Qadr?)) ((Laylatul-Qadr ni bora kuliko miezi elfu)) ((Huteremka Malaika na Roho [Jibriyl) katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo)) ((Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri))  [Al-Qadr: 1-5)

 

Mpya - Maswali

KUSIMAMISHA KUPOKEA MASWALI KWA MUDA

 

Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh, Ndugu wapenzi,

 

Tunasikitika kuwajulisha kuwa tunasimamisha kupokea maswali yote mapya hadi tutakapowajulisha tena.  Tuna maswali mengi sana ambayo yanasubiri kujibiwa na wenye kuuliza wanasubiri majibu yao kwa muda mrefu, jambo ambalo halipendezi ingawa lipo nje ya uwezo wetu.

 

Maswali yanayotufikia kwa siku yamekithiri kuliko matarajio yetu na uwezo wetu. Kadhalika wengi huuliza maswali ambayo tayari majibu yake yapo ndani ya tovuti na kupoteza muda wao kusubiri majibu wakati ambapo wangeweza kutafuta kwanza kupitia sehemu ya 'Tafuta ndani ya Alhidaaya' ambako unapoandika neno linalohusiana na swali lako yatakutokezea majibu yake.

 

Insha Allaah tutakapofanikiwa kumaliza viporo tulivyonavyo, tutawatangazia tena kupokea maswali yenu.Tunawaomba radhi kwa usumbufu huu na tunaomba du'aa zenu kwa kazi hizi nzito.

 

Jazaakum Allaahu khayra