Skip navigation.
Home kabah

Nasiha Ya Ijumaa

Njia 10 Za Kuukaribisha Vizuri Mwezi Mtukufu Wa Ramadhaan

Inatupasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kutupa umri tukiwa katika Uislamu na Iymaan hadi kutufikisha tena kukaribia Mwezi Mtukufu wa Ramadhaan. Na hii ni fursa nyingine Anayotupa Allaah Ta’ala katika maisha yetu kushuhudia mwezi huu na kupata fadhila zake.  

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

 

 

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ))  (( أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ...

 

 

((Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa Swawm, kama waliyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah)) (([Mfunge] siku maalumu za kuhisabika….  [Al-Baqarah: 183-184]

 

Mpya - Maswali

OMBI JIPYA KUHUSU MASWALI YENU

KWANZA: Tunawaomba muwe na subira baada ya kutuma Maswali yenu, kwani maswali mengi mno yanamiminika humu na wengine wanatuma maswali yao zaidi ya mara tatu kukumbusha. Tunaomba mtambue kwamba maswali yanajibiwa kwa zamu ili kufanya haki katika kuyajibu. 
PILI:  Wanaotuma Maswali ya Mirathi, tunawaomba waweke maelezo kamili kuhusu warithi waliobakia. Watajwe wote wanaohusika kupata urithi  ili maswali yaweze kujibiwa ipasavyo bila ya kukurudishieni barua kukuulizeni.   TATU:  Maswali yawekwe maudhui iliyo wazi ili iwe wepesi kufuatilia na kila swali litumwe katika barua ya pekee.
Tunatumai kupata ushirikiano wenu mwema ili mtufanyie wepesi hizi kazi  ambazo ni nyingi sana  khaswa  za Maswali  na watendaji ni wachache sana.
 
Jazaakum Allaahu Khayra.