SWALI:
Assalaam Alaikum
Jazakum-llahu Kheir, Nimejifunza mengi kuhusu miirathi, naomba lau maelezo ya urithi kutajwa kwa ujumla kama ilivyo kuja kwenye Quran. Jawabu la miirath ya urith wa mama na mtoto wa kike na mamake bwana lilikua makhsus. Shukran, Wassalaam alaikum!
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mirathi. Kawaida sisi huwa tunajibu swali kama tulivyoulizwa na muulizaji. Hilo swali ambalo umelitaja ni mfano wa maswali kuhusu urithi ambalo tumeulizwa na mmoja wa ndugu zetu. Ama maelezo ya kijumla kuhusu mirathi kama yafuatayo:
Soma Aayah katika Suratun Nisaa Namba : 7, 11, 12-13 176- zenye maelezo yote kuhusu Mirathi
Na Allaah Anajua zaidi
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/34
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F3276&title=Maelezo%20Kuhusu%20Hukmu%20Za%20Mirathi%20Kwa%20Ujumla