Tafsiyr Ya Imaam As-Sa'dy:
Kufaridhishwa Swawm
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾
Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa. [Al-Baqarah: 183]
Allaah Anajulisha katika Aliyoyafadhilisha kwa waja Wake kwamba Amewajibisha Swawm kama Alivyowajibisha ummah zilizopita kwa sababu ni shariy’ah (hukmu) na amri zinazomnufaisha bin Aadam katika kila zama.
Nayo ni changamoto ya kumhuisha mtu nafsi yake kwani inapasa kushindana na wengine katika mambo ya khayr ili mkamilishe 'amali zenu na mkimbilie (kuchuma) sifa njema na hakika hayo si katika mambo mazito mliyohusishwa nayo.
Kisha Allaah Anataja hikma Yake kuhusu Shariy’ah ya Swawm, Anasema:
لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ
mpate kuwa na taqwa
kwamba Swawm ni sababu kuu ya taqwa (kumcha Allaah) kwa kuwa ni kutekeleza amri za Allaah na kujiepusha na yaliyokatazwa.
Kwa hiyo katika Swawm yanapatikana yafuatayo:
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/7
[2] http://www.alhidaaya.com
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F6701&title=Tafsiyr%20Ya%20Imaam%20As-Sa%27dy%3A%20Kufaridhiswa%20Swawm