Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل قراءة القرآن
01-Mlango Wa Ubora wa Kusoma Qur-aan
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي أُمَامَةَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( اقْرَؤُوا القُرْآنَ ؛ فَإنَّهُ يَأتِي يَوْمَ القِيَامَةِ شَفِيعاً لأَصْحَابِهِ )) رواه مسلم .
Abu Umamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Amesema kwamba amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Isomeni Qur-aan kwani hakika itakuja Siku ya Qiyaamah kumuombea sahibu yake (aliyeisoma)." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن النَّوَّاسِ بنِ سَمْعَانَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( يُؤْتَى يَوْمَ القِيَامَةِ بِالقُرْآنِ وَأهْلِهِ الذينَ كَانُوا يَعْمَلُونَ بِهِ في الدُّنْيَا تَقْدُمُه سورَةُ البَقَرَةِ وَآلِ عِمْرَانَ ، تُحَاجَّانِ عَنْ صَاحِبِهِمَا )) رواه مسلم .
An-Nawwaas bin Sam'aan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Siku ya Qiyaamah italetwa Qur-aan pamoja na wale waliokuwa wakiitumia duniani. Itamtangulia Suratul Baqarah na Aal 'Imraan zikimtetea sahibu yake (wale waliokuwa wakizisoma katika maisha yao)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( خَيْرُكُمْ مَنْ تَعَلَّمَ الْقُرْآنَ وَعَلَّمَهُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mbora wenu ni yule aliyejifunza Qur-aan na akaifundisha." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( الَّذِي يَقْرَأُ القُرْآنَ وَهُوَ مَاهِرٌ بِهِ مَعَ السَّفَرَةِ الكِرَامِ البَرَرَةِ ، وَالَّذِي يَقْرَأُ الْقُرْآنَ وَيَتَتَعْتَعُ فِيهِ وَهُوَ عَلَيْهِ شَاقٌّ لَهُ أجْرَانِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yule ambaye anasoma Qur-aan naye ni mahiri katika hilo, atakuwa pamoja na Malaaikah na Mitume watukufu wenye kutii na yule ambaye anasoma Qur-aan na huku anaona ugumu na anapata shida, atapata malipo mawili." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na Ibn Maajah]
Hadiyth – 5
وعن أَبي موسى الأشعري رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَثَلُ الْمُؤْمِنِ الَّذِي يَقْرَأُ القُرْآنَ مَثَلُ الأُتْرُجَّةِ : رِيحُهَا طَيِّبٌ وَطَعْمُهَا طَيِّبٌ ، وَمَثَلُ الْمُؤْمِنِ الَّذِي لاَ يَقْرَأُ القُرْآنَ كَمَثَلِ التَّمْرَةِ : لاَ رِيحَ لَهَا وَطَعْمُهَا حُلْوٌ ، وَمَثلُ المُنَافِقِ الَّذِي يقرأ القرآنَ كَمَثلِ الرَّيحانَةِ : ريحُهَا طَيِّبٌ وَطَعْمُهَا مُرٌّ ، وَمَثَلُ المُنَافِقِ الَّذِي لاَ يَقْرَأُ القُرْآنَ كَمَثلِ الحَنْظَلَةِ : لَيْسَ لَهَا رِيحٌ وَطَعْمُهَا مُرٌّ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-'Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mfano wa Muumini ambaye anasoma Qur-aan ni kama mfano wa mbalungi, harufu yake ni nzuri na ladha yake ni nzuri, na mfano wa Muumini ambaye hasomi Qur-aan mfano wake ni kama tende, haina harufu na ladha ni tamu. Na mfano wa mnafiki ambaye anasoma Qur-aan ni kama mfano wa mrehani, harufu yake ni nzuri na ladha yake ni chungu; na mfano wa mnafiki ambaye hasomi Qur-aan ni kama mfano wa handhala, hauna harufu na ladha yake ni chungu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawud, at-Tirmidhiy na An-Nasaai]
Hadiyth – 6
وعن عمر بن الخطاب رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ اللهَ يَرْفَعُ بِهَذَا الكِتَابِ أقْوَاماً وَيَضَعُ بِهِ آخرِينَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah atawanyanyua watu kwa Kitabu hichi na kuwatwaza kwacho wengine." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن ابن عمر رضي اللهُ عنهما ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ حَسَدَ إِلاَّ في اثْنَتَيْنِ : رَجُلٌ آتَاهُ اللهُ القُرْآنَ ، فَهُوَ يَقُومُ بِهِ آنَاء اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ ، وَرَجُلٌ آتَاهُ اللهُ مَالاً ، فَهُوَ يُنْفِقُهُ آنَاءَ اللَّيْلِ وَآنَاءَ النَّهَارِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna husudu isipokuwa katika mambo mawili: Mtu amepewa na Allaah Qur-aan, akawa anaisoma nyakati za usiku na nyakati za mchana; na mtu amepewa mali na Allaah, naye anaitoa wakati wa usiku na wakati wa mchana." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 8
وعن البراءِ بن عازِبٍ رضي اللهُ عنهما ، قَالَ : كَانَ رَجُلٌ يَقْرَأُ سُورَةَ الْكَهْفِ ، وَعِنْدَهُ فَرَسٌ مَرْبُوطٌ بِشَطَنَيْنِ ، فَتَغَشَّتْهُ سَحَابَةٌ فَجَعَلَتْ تَدْنُو ، وَجَعَلَ فَرَسُه يَنْفِرُ مِنْهَا ، فَلَمَّا أصْبَحَ أتَى النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَذَكَرَ ذَلِكَ لَهُ ، فَقَالَ : (( تِلْكَ السَّكِينَةُ تَنَزَّلَتْ لِلقُرْآنِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Mtu mmoja alikuwa anasoma Suwrah Al-kahf, na mbele yake kuna farasi amefungwa kwa kamba mbili, ukungu ukamfunika yeye (wingu) na farasi wake akawa anaogopa huku anaruka ruka na kuukimbia. Kulipopambazuka alikwenda kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumweleza kisa hicho. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Hiyo ni As-Sakiynah (utulivu) unaoteremka kwa ajili ya Qur-aan." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 9
وعن ابن مسعودٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ قَرَأ حَرْفاً مِنْ كِتَابِ اللهِ فَلَهُ حَسَنَةٌ ، وَالحَسَنَةُ بِعَشْرِ أمْثَالِهَا ، لاَ أقول : ألم حَرفٌ ، وَلكِنْ : ألِفٌ حَرْفٌ ، وَلاَمٌ حَرْفٌ ، وَمِيمٌ حَرْفٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Na imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusoma herufi moja kutoka kwa katika Kitabu cha Allaah atapata ujira mmoja, na ujira huu ni sawa na kumi mfano wake. Wala sisemi kuwa Alif Lam Miim ni herufi moja lakini Alif ni herufi na Lam ni herufi na Miim ni herufi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 10
وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الَّذِي لَيْسَ في جَوْفِهِ شَيْءٌ مِنَ القُرْآنِ كَالبَيْتِ الخَرِبِ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika yule ambaye kwamba hana moyoni mwake (yaani hakuhifadhi) chochote kaika Qur-aan ni kama nyumba iliyohamwa." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 11
وعن عبد اللهِ بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يُقَالُ لِصَاحِبِ الْقُرْآنِ : اقْرَأْ وَارْتَقِ وَرَتِّلْ كَمَا كُنْتَ تُرَتِّلُ في الدُّنْيَا ، فَإنَّ مَنْزِلَتَكَ عِنْدَ آخِرِ آية تَقْرَؤُهَا )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aasw (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ataambiwa Mwenye (msomi) Qur-aan Siku ya Qiyaamah: "Soma Qur-aan, Upande daraja, Soma kama ulivyokuwa ukisoma duniani, kwani daraja yako iko mwisho wa ayah utakayosoma." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الأمر بتعهد القرآن والتحذير عن تعريضه للنسيان
02-Mlango Wa Kuchunga Qur-aan na Kutahadharishwa Kupelekea Kwenye Kuisahau
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي موسى رضي اللهُ عنه، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تعاهدوا هَذَا القُرْآنَ ، فَوَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَهُوَ أشَدُّ تَفَلُّتاً مِنَ الإبلِ فِي عُقُلِهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ichungeni hii Qur-aan naapa kwa ambaye nafsi ya Muhammad iko mikononi mwake hakika hii Qur-aan inaponyoka haraka mno kuliko ngamia kutoka kwenye kamba yake aliyefungiwa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّمَا مَثَلُ صَاحبِ الْقُرْآنِ كَمَثَلِ الإِبِلِ المُعَقَّلَةِ ، إنْ عَاهَدَ عَلَيْهَا أمْسَكَهَا ، وَإنْ أطْلَقَهَا ذَهَبَتْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mfano wa mwenye kuhifadhi Qur-aan ni sawa na mwenye ngamia waliofungwa kama ataendelea kuwafunga atakuwa nao na kama atawaachilia wataondoka na kukimbia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب تحسين الصوت بالقرآن
وطلب القراءة من حسن الصوت والاستماع لها
03-Mlango Wa Kupendekezwa Kusoma Qur-aan kwa Sauti Nzuri na Kutaka Isomwe na Mtu Mwenye Sauti Nzuri na Kumsikiliza
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَا أَذِنَ اللهُ لِشَيءٍ مَا أَذِنَ لِنَبِيٍّ حَسَنِ الصَّوْتِ يَتَغَنَّى بِالقُرْآنِ يَجْهَرُ بِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Allaah hakuruhusu kitu kizuri zaidi kama alivyomruhusu Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuitumia sauti nzuri kughania Qur-aan na kuisoma kwa sauti." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Hadiyth – 2
وعن أَبي موسى الأَشعري رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ لَهُ :(( لَقدْ أُوتِيتَ مِزْمَاراً مِنْ مَزَامِيرِ آلِ دَاوُدَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية لمسلمٍ : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ لَهُ : (( لَوْ رَأيْتَنِي وَأنَا أسْتَمِعُ لِقِراءتِكَ الْبَارِحَةَ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia: "Kwa hakika umepewa kinanda miongoni mwa vinanda vya watu wa Daawuwd mwenyewe." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia yeye: "Lau kama ungeniona mimi jana nikisikiliza kisomo chako kizuri cha Qur-aan."
Hadiyth – 3
وعن البَراءِ بنِ عازِبٍ رضي اللهُ عنهما ، قَالَ : سَمِعْتُ النبيَّ صلى الله عليه وسلم قَرَأَ فِي الْعِشَاءِ بالتِّينِ وَالزَّيْتُونِ ، فَمَا سَمِعْتُ أحَداً أحْسَنَ صَوْتاً مِنْهُ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa alimsikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisoma katika Swalaah ya 'Ishaa Suwrah At-Tiyn. Hakika ni kuwa sijawahi kumsikia yeyote mwenye sauti nzuri kuliko yeye." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي لُبَابَةَ بشير بن عبد المنذر رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ لَمْ يَتَغَنَّ بِالقُرْآنِ فَلَيْسَ مِنَّا )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ جيدٍ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Lubaabah Bashiyr bin 'Abdil Mundhir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote asiyeghani (yaani kusoma Qur-aan kwa sauti nzuri) katika kuisoma Qur-aan si katika sisi." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Jayd]
Hadiyth – 5
وعن ابن مسعودٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ لِي النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( اقْرَأْ عَلَيَّ القُرْآنَ )) ، فقلتُ : يَا رسولَ الله ، أَقْرَأُ عَلَيْكَ ، وَعَلَيْكَ أُنْزِلَ ؟! قَالَ : (( إنِّي أُحِبُّ أنْ أسْمَعَهُ مِنْ غَيْرِي )) فَقَرَأْتُ عَلَيْهِ سُورَةَ النِّسَاءِ ، حَتَّى جِئْتُ إِلَى هذِهِ الآية: [ فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِنْ كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ وَجِئْنَا بِكَ عَلَى هَؤُلاَءِ شَهِيداً ] [النِّسَاءِ: ٤١] قَالَ :(( حَسْبُكَ الآنَ )) فَالْتَفَتُّ إِلَيْهِ ، فَإذَا عَيْنَاهُ تَذْرِفَانِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Na Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Aliniambia: "Nisome Qur-aan." Nikamwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Nikusomee wewe na imeteremshwa kwako?", Akasema: "Mimi napenda kuisika kwa mwengine." Ibn Mas'uwd akasema: "Nikamsomea Suwrah An-Nisaa' hadi nikafika ayah hii, "Basi itakuwaje Tutakapoleta kutoka kila Ummah shahidi, na Tukakuleta (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuwa shahidi juu ya hawa?" [An-Nisaa: 41]. Akasema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Inatosha sasa." Nikamgeukia nikaona macho yake yanabubujika machozi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الحث عَلَى سور وآيات مخصوصة
04-Mlango Wa Kuhimiza Kusoma Suwrah na Ayah Maalumu
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي سَعِيدٍ رَافِعِ بن الْمُعَلَّى رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ لي رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أَلاَ أُعَلِّمُكَ أَعْظَمَ سُورَةٍ في القُرْآن قَبْلَ أنْ تَخْرُجَ مِنَ الْمَسْجِدِ ؟ )) فَأخَذَ بِيَدِي ، فَلَمَّا أرَدْنَا أنْ نَخْرُجَ ، قُلْتُ : يَا رَسُولَ اللهِ ، إنَّكَ قُلْتَ : لأُعَلِّمَنَّكَ أعْظَمَ سُورَةٍ في القُرْآنِ ؟ قَالَ : (( الحَمْدُ للهِ رَبِّ العَالَمِينَ ، هِيَ السَّبْعُ المَثَانِي وَالقُرْآنُ العَظِيمُ الَّذِي أُوتِيتُهُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Raafi' bin Al-Mu'allaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: "Je, nisikufundishe Suwrah tukufu katika Qur-aan kabla hujatoka Msikitini?" Akashika mkono wangu, tulipotaka kutoka nilimwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Uliniambia utanifundisha Suwrah tukufu katika Qur-aan." Akasema: "الحَمْدُ للهِ رَبِّ العَالَمِينَ", hiyo ni Suwrah yenye Ayah saba zinazokaririwa, na Qur-aan Tukufu ambayo nimepewa." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ في : ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) : (( وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ إنَّهَا لَتَعْدِلُ ثُلُثَ القُرْآنِ )) .
وفي روايةٍ : أن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ لأَصْحَابِهِ : (( أَيَعْجِزُ أحَدُكُمْ أنْ يَقْرَأَ بِثُلُثِ القُرْآنِ فِي لَيْلَةٍ )) فَشَقَّ ذَلِكَ عَلَيْهِمْ ، وَقَالُوا : أيُّنَا يُطِيقُ ذَلِكَ يَا رسولَ الله ؟ فَقَالَ : (( ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ اللهُ الصَّمَدُ ) : ثُلُثُ الْقُرْآنِ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa; Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema kuhusu ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) : "Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, hakika hiyo ni sawa na thuluthi ya Qur-aan."
Na katika riwaayah nyingine: "Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia Swahaaba wake: 'Je, anashindwa mmoja wenu kusoma thuluthi ya Qur-aan kwa usiku mmoja?" Jambo hilo likawa gumu kwao, na wakasema: "Nani anayeweza kufanya hivyo, Ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ اللهُ الصَّمَدُ ) , ni thuluthi ya Qur-aan." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه : أنَّ رَجُلاً سَمِعَ رَجُلاً يَقْرَأُ : (( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ )) يُرَدِّدُهَا فَلَمَّا أصْبَحَ جَاءَ إِلَى رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم فَذَكَرَ ذَلِكَ لَهُ وَكَانَ الرَّجُلُ يَتَقَالُّهَا ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، إنَّهَا لَتَعْدِلُ ثُلُثَ القُرْآنِ )) رواه البخاري .
Na kutoka kwake Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu); "Mtu alimsikia mtu mwingine anasoma: ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) , anairudiarudia, kulipopambazuka akaja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamueleza hilo, na huyu mtu alikuwa analiona dogo sana. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, hakika Suwrah hiyo ni sawa na thuluthi ya Qur-aan." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هُرَيْرَةَ رضي اللهُ عنه : أَنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ في : (قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) (( إنَّهَا تَعْدِلُ ثُلُثَ الْقُرْآنِ )) رواه مسلم
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema kuhusu ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) : Hakika hiyo ni sawa na thuluthi ya Qur-aan." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أنس رضي اللهُ عنه : أنَّ رَجُلاً قَالَ : يَا رَسُولَ اللهِ ، إني أُحِبُّ هذِهِ السُّورَةَ : ( قُلْ هُوَ اللهُ أحَدٌ ) قَالَ : (( إنَّ حُبَّهَا أدْخَلَكَ الجَنَّةَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) . ورواه البخاري في صَحِيحِهِ تعليقاً .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): kuwa Mtu mmoja aliuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mimi naipenda Suwrah hii: ( قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ) . Akasema: "Hakika kuipenda hiyo (Suwrah) kutakuingiza Peponi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan na ameipokea Al-Bukhaariy katika Swahiyh yake]
Hadiyth – 6
وعن عقبة بن عامِر رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( ألَمْ تَرَ آيَاتٍ أُنْزِلَتْ هذِهِ اللَّيْلَةَ لَمْ يُرَ مِثْلُهُنَّ قَطُّ ؟ ( قُلْ أَعْوذُ بِرَبِّ الفَلَقِ ) وَ( قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ) )) رواه مسلم
Imepokewa kutoka kwa 'Uqbah bin 'Aamir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwani hukuona aya zilizoteremshwa usiku huu ambazo hazijaonekana mfano wake kabisa? ( قُلْ أَعْوذُ بِرَبِّ الفَلَقِ ) na ( قُلْ أَعُوذُ بِرَبِّ النَّاسِ ) ." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن أَبي سَعِيدٍ الخُدريِّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَتَعَوَّذُ مِنَ الجَانِّ ، وَعَيْنِ الإنْسَانِ ، حَتَّى نَزَلَتْ المُعَوِّذَتَانِ ، فَلَمَّا نَزَلَتَا ، أخَذَ بِهِمَا وَتَرَكَ مَا سِوَاهُمَا . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Na Abu Sa'iyd al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akitaka hifadhi kwa Allaah kutokana na majini na macho mabaya ya wanadamu mpaka alipoteremka al-Mu'wwidhatayn (Suwrah mbili za kujikinga kwa Allaah yaani suwratul Falaq na An-Naas). Zilipoteremka alizichukua na akawa anazisoma na kuacha vyengine vyote." [At-Trmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].
Hadiyth – 8
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مِنَ القُرْآنِ سُورَةٌ ثَلاثُونَ آيَةً شَفَعَتْ لِرَجُلٍ حَتَّى غُفِرَ لَهُ ، وَهِيَ : ( تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ المُلْكُ ) )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
وفي رواية أَبي داود : (( تَشْفَعُ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ndani ya Qur-aan ipo Suwrah yenye ayah thelethini ambayo itamuombea mtu mpaka asamehewe na Allaah; nayo ni ( تَبَارَكَ الَّذِي بِيَدِهِ المُلْكُ ) (Suwratul Mulk-Suwrah ya:67) [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 9
وعن أَبي مسعودٍ البَدْرِيِّ رضي اللهُ عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَرَأَ بِالآيَتَيْنِ مِنْ آخر سُورَةِ البَقَرَةِ في لَيْلَةٍ كَفَتَاهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Mas'uud Al-Badriy (Radhwiya Allaahu 'anhu): kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusoma ayah mbili za mwisho wa Suwratul Baqarah usiku zitamtosha." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 10
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ تَجْعَلُوا بُيُوتَكُمْ مَقَابِرَ ، إنَّ الشَّيْطَانَ يَنْفِرُ مِنَ البَيْتِ الَّذِي تُقْرَأُ فِيهِ سُورَةُ البَقرَةِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msifanye nyumba zenu kuwa makaburi, kwa hakika shetani anakimbia kutoka kwa nyumba ambayo husomwa ndani yake Suwratul Baqarah." [Muslim]
Hadiyth – 11
وعن أُبَيِّ بنِ كَعبٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا أَبَا الْمُنْذِرِ ، أَتَدْري أيُّ آيَةٍ مِنْ كِتَابِ الله مَعَكَ أعْظَمُ ؟ )) قُلْتُ : ( اللهُ لاَ إلَهَ إِلاَّ هُوَ الحَيُّ القَيُّومُ ) فَضَرَبَ فِي صَدْرِي ، وقال : (( لِيَهْنِكَ العِلْمُ أَبَا الْمُنْذِرِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ubayy bin Ka'ab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliniuliza: "Ee Abul Mundhir! je, unajua ni ayah gani kwako ndio tukufu kabisa katika Kitabu cha Allaah?" Nikasema: "( اللهُ لاَ إلَهَ إِلاَّ هُوَ الحَيُّ القَيُّومُ ) Al-Baqarah: 255). Alinishika kifua changu, akasema: "Hongera kwa ilimu yako (ya Qur-aan), ee Abul Mundhir." [Muslim]
Hadiyth – 12
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : وَكَّلَنِي رسولُ الله صلى الله عليه وسلم بِحِفْظِ زَكَاةِ رَمَضَانَ، فَأتَانِي آتٍ فَجَعَلَ يَحْثُو مِنَ الطَّعَام، فَأخَذْتُهُ فقُلتُ: لأَرْفَعَنَّكَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : إنِّي مُحْتَاجٌ ، وَعَليَّ عِيَالٌ ، وَبِي حَاجَةٌ شَدِيدَةٌ ، فَخَلَّيْتُ عَنْهُ ، فَأصْبَحْتُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا أَبَا هُريرة ، مَا فَعَلَ أَسِيرُكَ البَارِحَةَ ؟ )) قُلْتُ : يَا رسول الله ، شَكَا حَاجَةً وَعِيَالاً ، فَرحِمْتُهُ فَخَلَّيْتُ سَبيلَهُ . فَقَالَ : (( أمَا إنَّهُ قَدْ كَذَبَكَ وَسَيَعُودُ )) فَعَرَفْتُ أنَّهُ سَيَعُودُ ، لقولِ رسول الله صلى الله عليه وسلم فَرَصَدْتُهُ ، فَجاء يَحْثُو مِنَ الطَّعَامِ ، فَقُلتُ : لأَرْفَعَنَّكَ إِلَى رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : دَعْنِي فَإنِّي مُحْتَاجٌ ، وَعَلَيَّ عِيَالٌ لاَ أعُودُ ، فَرحِمْتُهُ فَخَلَّيْتُ سَبيلَهُ ، فَأصْبَحْتُ فَقَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا أَبَا هُريرة ، مَا فَعَلَ أَسِيرُكَ البَارِحَةَ ؟ )) قُلْتُ : يَا رسول الله ، شَكَا حَاجَةً وَعِيَالاً ، فَرحِمْتُهُ فَخَلَّيْتُ سَبيلَهُ . فَقَالَ : (( إنَّهُ قَدْ كَذَبَكَ وَسَيَعُودُ )) فَرَصَدْتُهُ الثَّالثَة ، فَجاء يَحْثُو مِنَ الطَّعَامِ فَأخَذْتُهُ ، فَقُلتُ : لأَرْفَعَنَّكَ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، وهذا آخِرُ ثلاثِ مَرَّاتٍ أنَّكَ تَزْعُمُ أنَّكَ لاَ تَعُودُ ! فَقَالَ : دَعْنِي فَإنِّي أُعَلِّمُكَ كَلِمَاتٍ يَنْفَعُكَ اللهُ بِهَا ، قُلْتُ : مَا هُنَّ ؟ قَالَ : إِذَا أَوَيْتَ إِلَى فِرَاشِكَ فَاقْرَأْ آيَةَ الكُرْسِيِّ ، فَإنَّهُ لَنْ يَزَالَ عَلَيْكَ مِنَ الله حَافِظٌ ، وَلاَ يَقْرَبُكَ شَيْطَانٌ حَتَّى تُصْبِحَ ، فَخَلَّيْتُ سَبِيلَهُ ، فَأصْبَحْتُ ، فَقَالَ لي رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا فَعَلَ أسِيرُكَ البَارِحَةَ ؟ )) قُلْتُ : يَا رسول الله ، زَعَمَ أنَّهُ يُعَلِّمُنِي كَلِمَاتٍ يَنْفَعُنِي اللهُ بِهَا ، فَخَلَّيْتُ سَبيلَهُ ، قَالَ : (( مَا هِيَ ؟ )) قُلْتُ : قَالَ لي : إِذَا أَوَيْتَ إِلَى فِرَاشِكَ فَاقْرَأْ آيَة الكُرْسِيِّ مِنْ أوَّلِهَا حَتَّى تَخْتِمَ الآية : ( اللهُ لاَ إلَهَ إِلاَّ هُوَ الحَيُّ القَيُّومُ ) وقال لِي : لاَ يَزَالُ عَلَيْكَ مِنَ اللهِ حَافِظٌ ، وَلَنْ يَقْرَبَكَ شَيْطَانٌ حَتَّى تُصْبِحَ . فَقَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( أمَا إنَّهُ قَدْ صَدَقَكَ وَهُوَ كَذُوبٌ ، تَعْلَمُ مَنْ تُخَاطِبُ مُنْذُ ثَلاَثٍ يَا أَبَا هُرَيْرَةَ ؟ )) قُلْتُ : لاَ . قَالَ : (( ذَاكَ شَيْطَانٌ )) رواه البخاري .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alinichagua kuhifadhi Zakaah ya Ramadhwaan, - Zakatul Fitr - Akaja mwenye kuja, akawa anachukua chakula, Nikamshika nikamwambia: "Nitakupeleka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi sallam)." Akasema: "Mimi ni muhitaji, nina familia, nina haja nyingi." Nikamuachia. Nilipoamka; Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Ee Abu Huraiyrah! Alifanya nini mateka wako jana?" Nikasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Alinilalamikia haja na familia, Nilimhurumia nikamuacha." Akasema: "Ama hakika, amekudanganya na atarudi tena." Nilijua kwa hakika atarudi kwa kauli ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), hivyo nilimvizia. Alikuja na kuchukua chakula. Nilimkamata nikamwambia: "Nitampeleka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." Akasema: "Niache kwani mimi ni mhitaji na nina familia wala sitarudi." Nilimhurumia na kumuacha njia yake. Nikaamka, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Ee Abu Huraiyrah! mateka wako jana?" Nilimwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Alinilalamikia kuwa ana haja kubwa na familia, hivyo nilimhurumia na kumuachia aende." Akasema: "Hakika amekudanganya na atarudi." Nilimvizia mara ya tatu, Alikuja na kuchukua chakula, nikamshika. Nikamwambia: "Nitakupeleka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na hii ni mara ya tatu ya mwisho ambayo unadai hutarudi, kisha unarudi." Akasema: "Niachie, hakika mimi nitakufundisha maneno Allaah atakunufaisha nayo." Nikasema: "Ni yapi hayo?" Akasema: "Unapokwenda kitandani kwako soma Ayatul Kursiy (2:255) hadi umalizie ayah, kwani mlinzi wa Allaah hataacha kuwa juu yako, (akuhifadhi) wala hatakukaribia shetani mpaka unapambazuka, Nilimuachia njia yake." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Ee Abu Huraiyrah! Alifanya nini mateka wako jana?" Nilimwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! Alidai kuwa atanifundisha maneno ambayo Allaah ataninufaisha nayo, hivyo nikamwachia." Akasema: "Ni yapi hayo?" Nikasema: "Aliniambia: Unapokwenda kitandani kwako soma Ayatul Kursiy, kuanzia mwanzo mpaka umalize ayah ( اللهُ لاَ إلَهَ إِلاَّ هُوَ الحَيُّ القَيُّومُ ) (Al-Baqarah: 255). Na akaniambia: "Mlinzi wa Allaah hataacha kuwa juu yako, wala hatakukaribia shetani mpaka asubuhi." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)akasema: "Kwa hakika yeye amekuambia kweli na yeye ni muongo. Unajua unazungumza na nani muda wa siku tatu, ee Abu Huraiyrah?" Nikasema: "La." Akasema: "Huyo alikuwa ni shetani." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 13
وعن أَبي الدرداءِ رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ حَفِظَ عَشْرَ آيَاتٍ مِنْ أَوَّلِ سُورَةِ الكَهْفِ ، عُصِمَ مِنَ الدَّجَّالِ )) .
وفي رواية : (( مِنْ آخِرِ سُورَةِ الكَهْفِ )) رواهما مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dardaa' (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuhifadhi ayah kumi mwanzo wa Suwrah Al-Kahf (Suwrah: 18) ataepushwa na Dajjal.
Na katika riwaayah nyengine: "Mwisho wa Suwrah Al-Kahf. [Muslim]. Riwaayah ya kwanza ndiyo iliyohifadhiwa.
Hadiyth – 14
وعن ابنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما : بَيْنَمَا جِبْريلُ (عَلَيْهِ السَّلام) قَاعِدٌ عِنْدَ النبي صلى الله عليه وسلم سَمِعَ نَقيضاً مِنْ فَوقِهِ ، فَرَفَعَ رَأسَهُ ، فَقَالَ : هَذَا بَابٌ مِنَ السَّمَاءِ فُتِحَ اليَوْمَ وَلَمْ يُفْتَحْ قَطٌّ إِلاَّ اليَوْمَ ، فنَزلَ منهُ مَلكٌ ، فقالَ : هذا مَلكٌ نَزلَ إلى الأرضِ لم ينْزلْ قطّ إلاّ اليومَ فَسَلَّمَ وقال : أبْشِرْ بِنُورَيْنِ أُوتِيتَهُمَا لَمْ يُؤتَهُمَا نَبيٌّ قَبْلَكَ : فَاتِحَةُ الكِتَابِ ، وَخَواتِيمُ سُورَةِ البَقَرَةِ ، لَنْ تَقْرَأَ بِحَرْفٍ مِنْهَا إِلاَّ أُعْطِيتَه . رواه مسلم .
Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Jibriyl ('Alayhis Salaam) akiwa amekaa na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), alisikia sauti kutoka juu, akainua kichwa chake, akasema: "Huu ni mlango mbinguni umefunguliwa leo haujafunguliwa kabisa ila leo." Humo akateremka Malaaikah, Jibriyl akasema: "Huyu ni Malaaikah ameteremka ardhini, hajateremka kabisa ila leo." Akamsalimia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)na akasema: "Pata bishara ya nuru mbili ulizopewa, hajapewa Nabiy yoyote kabla yako. Ufunguzi wa Kitabu (Suwrah Al-Faatihah), na mwisho wa Suwrah Al-Baqarah. Hatasoma yoyote herufi moja miongoni mwa hizo ila utapewa ujira." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب الاجتماع عَلَى القراءة
05-Mlango Wa Kupendeza Kukusanyika kwa Ajili ya Kusoma
Alhidaaya.com [4]
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( وَمَا اجْتَمَعَ قَوْمٌ فِي بَيْتٍ مِنْ بُيُوتِ اللهِ يَتلُونَ كِتَابَ اللهِ ، وَيَتَدَارَسُونَهُ بينهم ، إِلاَّ نَزَلَتْ عَلَيْهِمُ السَّكِينَةُ وَغَشِيتْهُمُ الرَّحْمَةُ ، وَحَفَّتْهُمُ المَلاَئِكَةُ ، وَذَكَرَهُمُ اللهُ فِيمَنْ عِنْدَهُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah, kusoma Kitabu cha Allaah na kusomeshana baina yao, ila huteremkiwa na utulivu, wakafunikwa na rehma, na wakazungukwa na malaaikah, na Allaah akawataja kwa walioko naye." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل الوضوء
06-Mlango Wa Ubora wa Wudhuu
Alhidaaya.com [4]
قَالَ الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ وَإِن كُنتُمْ جُنُبًا فَاطَّهَّرُوا ۚ وَإِن كُنتُم مَّرْضَىٰ أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ أَوْ جَاءَ أَحَدٌ مِّنكُم مِّنَ الْغَائِطِ أَوْ لَامَسْتُمُ النِّسَاءَ فَلَمْ تَجِدُوا مَاءً فَتَيَمَّمُوا صَعِيدًا طَيِّبًا فَامْسَحُوا بِوُجُوهِكُمْ وَأَيْدِيكُم مِّنْهُ ۚ مَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيَجْعَلَ عَلَيْكُم مِّنْ حَرَجٍ وَلَـٰكِن يُرِيدُ لِيُطَهِّرَكُمْ وَلِيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكُمْ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٦﴾
Enyi walioamini! Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah; osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visugudi, na panguseni (kwa kupaka maji) vichwa vyenu na (osheni) miguu yenu hadi vifundoni. Na mkiwa na janaba basi jitwaharisheni. Na mkiwa wagonjwa au mko safarini au mmoja wenu akitoka msalani, au mmewagusa wanawake, kisha hamkupata maji; basi tayammamuni (ikusudieni) ardhi kwa juu panguseni kwayo nyuso zenu na mikono yenu. Allaah Hataki kukufanyieni magumu, lakini Anataka kukutwaharisheni na Akutimizieni neema Yake juu yenu ili mpate kushukuru. [Al-Maaidah: 6]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ أُمَّتِي يُدْعَوْنَ يَوْمَ القِيَامَةِ غُرَّاً مُحَجَّلينَ مِنْ آثَارِ الوُضُوءِ ، فَمَنِ اسْتَطَاعَ مِنْكُمْ أنْ يُطِيلَ غُرَّتَهُ فَلْيَفْعَلْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika Ummah wangu utaitwa Siku ya Qiyaamah Ghurran Muhajjaliyn (Ghurrah ni kuosha kwa kuzidisha ile sehemu ya faradhi katika pambizoni mwa paji la uso, masikio na baadhi ya shingo na hivyo kulifanya paji la uso na sehemu hizo kuwa na weupe Siku ya Qiyaamah. Muhajjaliyn ni kurefusha kuosha miguu na mikono katika zile sehemu za faradhi, hivyo kuzifanya ziwe nyeupe Siku ya Qiyaamah). Kutokana na athari ya wudhuu; kwa atakayeweza miongoni mwenu kurefusha Ghurra yake na afanye." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ خليلي صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( تَبْلُغُ الحِلْيَةُ مِنَ المُؤمِنِ حَيْثُ يَبْلُغُ الوُضُوءُ )) رواه مسلم .
Na Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimsikia kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Uzuri wa Muumini Peponi utafika umbali wa maji aliyotumia kuchukua nayo wudhuu. [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( من تَوَضَّأ فَأَحْسَنَ الوُضُوءَ ، خَرَجَتْ خَطَايَاهُ مِنْ جَسَدِهِ حَتَّى تَخْرُج مِنْ تَحْتِ أَظْفَارِهِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kutawadha vizuri, madhambi yake hutoka katika mwili wake mpaka yatatoka kutoka chini ya kucha zake." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : رَأيتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم تَوَضَّأَ مِثْلَ وُضُوئِي هَذَا ، ثُمَّ قَالَ : (( مَنْ تَوَضَّأ هكَذَا ، غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ ، وَكَانَتْ صَلاَتُهُ وَمَشْيُهُ إِلَى المَسْجدِ نَافِلَةً )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba amesema: Nilimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akitawadha mfano wa Wudhuu wangu huu, kisha akasema: "Yeyote atakaye tawadha hivi, anasamehewa madhambi yake yaliyotangulia na Swalaah yake inakuwa na kutembea kwake Msikitini ni nyongeza (ya mizani yake ya mambo mema). [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا تَوَضَّأ العَبْدُ المُسْلِمُ - أَو المُؤْمِنُ - فَغَسَلَ وَجْهَهُ ، خَرَجَ مِنْ وَجْهِهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ نَظَرَ إِلَيْهَا بِعَيْنَيْهِ مَعَ المَاءِ ، أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ ، فَإذَا غَسَلَ يَدَيْهِ ، خَرَجَ مِنْ يَدَيْهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ كَانَ بَطَشَتْهَا يَدَاهُ مَعَ المَاءِ ، أَو مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ ، فَإذَا غَسَلَ رِجْلَيْهِ ، خَرَجَتْ كُلُّ خَطِيئَةٍ مَشَتْهَا رِجْلاَهُ مَعَ المَاءِ ، أَو مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ ، حَتَّى يَخْرُجَ نَقِيَّاً مِنَ الذُّنُوبِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mja , Muumini au Muislamu atakapotawadha kila kosa ambalo ameangalia kwa macho yako pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji, na akikosha mikono yake huondoka kila dhambi ambayo ameifanya kwa mikono yake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji. Anapokosha miguu yake, huondoka kila dhambi ambayo ameifanya kwa miguu yake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji, mpaka anatoka akiwa amesafika na dhambi." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أتى المقبرة ، فَقَالَ : (( السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ دَارَ قَومٍ مُؤْمِنِينَ ، وَإنَّا إنْ شَاءَ اللهُ بِكُمْ لاَحِقُونَ ، وَدِدْتُ أنَّا قَدْ رَأَيْنَا إخْوانَنَا )) قالوا : أوَلَسْنَا إخْوَانَكَ يَا رسول الله ؟ قَالَ : (( أنْتُمْ أصْحَابِي ، وَإخْوَانُنَا الَّذِينَ لَمْ يَأتُوا بَعْدُ )) قالوا : كَيْفَ تَعْرِفُ مَنْ لَمْ يَأتِ بَعْدُ مِنْ أُمَّتِكَ يَا رَسولَ الله ؟ فَقَالَ : (( أرَأيْتَ لَوْ أنَّ رَجُلاً لَهُ خَيلٌ غُرٌّ مُحَجَّلَةٌ بَيْنَ ظَهْرَيْ خَيْلٍ دُهْمٍ بُهْمٍ ، ألا يَعْرِفُ خَيْلَهُ ؟ )) قالوا : بَلَى يَا رسول الله ، قَالَ : (( فإنَّهُمْ يَأتُونَ غُرّاً مُحَجَّلينَ مِنَ الوُضُوءِ ، وأنَا فَرَطُهُمْ عَلَى الحَوْضِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alitembelea makaburi ya Baqii' akasema: As-Salaamu 'alaykum daara Qawmi Mu'miniyna wa Innaa In shaa Allaah bikum laahiquwn (Amani iwashukiewatu wa nyumba ya Waumini, na sisi akitaka Allaah tutakutana nanyi). Ilikuwa ni hamu yangu kubwa kukutana na ndugu zangu." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Sisi si ndugu zako?" Akasema: "Nyinyi ni Swahaaba zangu, na ndugu zetu ni ambao hawajaja bado (Duniani)." Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Umejua vipi ambao hawajaja bado katika uma wako?" Akasema: "Mnaonaje lau mtu ana farasi weupe kwenye nyuso zao na weupe katika kwato zao na wakachanganyika na farasi weusi hatawatambua farasi wake?" Wakasema: "Atawatambua ee Rasuli wa Allaah." Akasema: "Hakika wao watakuja Ghurran Muhajjaaliin kwa sababu ya wudhuu, nami nitawatangulia kwenye Hawdh (birika)." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( ألاَ أَدُّلُكُمْ عَلَى مَا يَمْحُو اللهُ بِهِ الخَطَايَا ، وَيَرْفَعُ بِهِ الدَّرَجَاتِ ؟ )) قالوا : بَلَى يَا رسول الله ، قَالَ : (( إسْبَاغُ الوُضُوءِ عَلَى المَكَارِهِ ، وَكَثْرَةُ الخُطَا إِلَى المَسَاجِدِ ، وَانْتِظَارُ الصَّلاَةِ بَعْدَ الصَّلاَةِ ؛ فَذلِكُمُ الرِّبَاطُ ؛ فَذَلِكُمُ الرِّبَاطُ )) رواه مسلم .
Kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Huvi niwafahamishe juu ya kile ambacho anafuta nacho Allaah makosa na ananyanyua nacho daraja?" Wakasema: "Kwa nini ee Rasuli wa Allaah, tufahamishe." Akasema: "Ni kujieneza wudhuu pamoja na machukivu (mfano baridi, hali ya hewa nzito, kuumwa) na uwingi wa nyayo kwenda Msikitini na kungojea Swalaah baada ya Swalaah, huo ndio ulingaji, huo ndio ulindaji." [Muslim]
Hadiyth – 8
وعن أَبي مالك الأشعري رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( الطُّهُورُ شَطْرُ الإيمَانِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Maalik Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kujitwahirisha ni nusu ya Imani." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن عمر بن الخطاب رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَا مِنْكُمْ مِنْ أحَدٍ يَتَوَضَّأُ فَيُبْلغُ – أَوْ فَيُسْبِغُ – الوُضُوءَ ، ثُمَّ يقول : أشهَدُ أنْ لا إلهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ ، وَأشْهَدُ أنَّ مُحَمَّداً عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ ؛ إِلاَّ فُتِحَتْ لَهُ أَبْوَابُ الجَنَّةِ الثَّمَانِيَةُ يَدْخُلُ مِنْ أَيِّهَا شَاءَ )) رواه مسلم .
وزاد الترمذي : (( اللَّهُمَّ اجْعَلْنِي مِنَ التَّوَّابِينَ ، وَاجْعَلْنِي مِنَ المُتَطَهِّرِينَ )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna yeyote mingoni mwenu anatawadha vizuri au akaeneza wudhuu, kisha akasema: "Nashuhudia kuwa hapana Mola isipokuwa Allaah, Peke Yake hana mshirika. Na nashuhudia kuwa Muhammad ni mja na Rasuli Wake." Isipokuwa itafunguliwa milango minane ya Pepo ataingia katika mlango wowote autakao." [Muslim]
Akaongeza At-Tirmidhiy: "Ee Mola wa haki nifanye mimi ni katika miongoni mwa wenye kutubia na nifanye mimi ni katika wenye kujitakasa."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل الأذان
07-Mlango Wa Ubora wa Adhaan
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا في النِّدَاءِ والصَّفِ الأَوَّلِ ، ثُمَّ لَمْ يَجِدُوا إِلاَّ أنْ يَسْتَهِمُوا عَلَيْهِ لاسْتَهَمُوا عَلَيْهِ ، ولو يَعْلَمُونَ مَا فِي التَّهْجِيرِ لاسْتَبَقُوا إِلَيْهِ ، وَلَوْ يَعْلَمُونَ مَا فِي العَتَمَةِ وَالصُّبْحِ لأَتَوْهُمَا وَلَوْ حَبْواً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau kama watu wangeelewa fadhila za adhana (kuitikia) na kusimama katika safu ya kwanza, kisha wakawa hawakupata njia ya kudiriki isipokuwa kwa kupiga kura basi wangalipiga kura; na kama wangelielewa (fadhila za) kuwahi Swalaah wangalihimiza na kushindana katika kuiendea mapema; na kama wangelielewa (fadhila za) kuswali Swalaah ya Isha na Asubuhi kwa jamaa, wangeziendea Swalaah hizo japokuwa kwa kutambaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن معاوية رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( المُؤَذِّنُونَ أطْوَلُ النَّاسِ أعْناقاً يَوْمَ القِيَامَةِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Mu'awiyah Amesema: 'Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Anasema': "Waadhini watakuwa na shingo ndefu Siku ya Qiyaamah." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عبدِ الله بن عبدِ الرَّحْمانِ بن أَبي صَعصعة : أنَّ أَبَا سَعيد الخدريَّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ لَهُ : (( إنِّي أرَاكَ تُحبُّ الغَنَمَ وَالبَادِيَةَ فَإذَا كُنْتَ في غَنَمِك - أَوْ بَادِيتِكَ - فَأذَّنْتَ للصَّلاَةِ ، فَارْفَعْ صَوْتَكَ بِالنِّدَاءِ ، فَإنَّهُ لا يَسْمَعُ مدى صَوْتِ المُؤذِّنِ جِنٌّ ، وَلاَ إنْسٌ ، وَلاَ شَيْءٌ ، إِلاَّ شَهِدَ لَهُ يَومَ القِيَامَةِ )) قَالَ أَبُو سَعيدٍ : سمعتُهُ مِنْ رَسولِ الله صلى الله عليه وسلم . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Abdir-Rahmaan bin Abu Swa'swa'ah; Abu Sa'iyd alimwambia: "Mimi nakuona wapenda sana kondoo na kuwa katika kijiji, hivyo ukiwa machungioni au katika kijiji chako na ukaadhini kwa ajili ya Swalaah basi nyanyua sauti yako kwa kuita watu katika Swalaah, kwani hatasikia upeo wa sauti ya muadhini huyo jini wala Bin Aadam wala kitu chochote ila atakuwa shahidi yake Siku ya Qiyaamah." Akasema Abu Sa'iyd: "Nimesikia hayo kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا نُودِيَ بالصَّلاَةِ ، أدْبَرَ الشَّيْطَانُ ، وَلَهُ ضُرَاطٌ حَتَّى لاَ يَسْمَعَ التَّأذِينَ ، فَإذَا قُضِيَ النِّدَاءُ أقْبَلَ ، حَتَّى إِذَا ثُوِّبَ للصَّلاةِ أدْبَرَ ، حَتَّى إِذَا قُضِيَ التَّثْوِيبُ أقْبَلَ ، حَتَّى يَخْطِرَ بَيْنَ المَرْءِ وَنَفْسِهِ ، يَقُولُ : اذْكُرْ كَذَا واذكر كَذَا – لِمَا لَمْ يَذْكُر مِنْ قَبْلُ – حَتَّى يَظَلَّ الرَّجُلُ مَا يَدْرِي كَمْ صَلَّى )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inaponadiwa Swalaah, shetani hukimbia na kutoa mashuzi ili asisikie adhana. Ikisha adhana hurudi; na tena anageuza mgongo na kukimbia pale Swalaah inapokimiwa; ikisha kimiwa hurudi tena, mpaka aingize wasi wasi kati ya mtu na nafsi yake (kwa lengo la kumtoa katika Swalaah), anamwambia: 'Kumbuka kadha, kumbuka kadha kwa yale ambayo kabla alikuwa hakumbuki', mpaka anamfanya hajui ameswali ngapi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن عبدِ الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنّه سمع رسول الله صلى الله عليه وسلم، يقول: (( إِذَا سَمِعْتُمُ النداء فَقُولُوا مِثْلَ مَا يَقُولُ ، ثُمَّ صَلُّوا عَلَيَّ ؛ فَإنَّه مَنْ صَلَّى عَلَيَّ صَلاَةً صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ بِهَا عَشْراً ، ثُمَّ سَلُوا اللهَ لِيَ الوَسِيلَةَ ؛ فَإنَّهَا مَنْزِلَةٌ في الجَنَّةِ لاَ تَنْبَغِي إِلاَّ لِعَبْدٍ مِنْ عِبَادِ اللهِ وَأرْجُو أنْ أكونَ أنَا هُوَ ، فَمَنْ سَألَ لِيَ الوَسِيلَةَ حَلَّتْ لَهُ الشَّفَاعَةُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amri bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mtakapomsikia muadhini basi semeni kama anvyosema muadhini kisha nitakieni rehema, kwani anayenitakia rehema mara moja Allaah atamrehemu mara kumi, kisha nitakeni kwa Allaah wasila kwani hiyo ni daraja katika Pepo haipati isipokuwa mja mwema, na ninataraji niwe mimi, yule atakayeniombea wasila atafikiwa na shufaa yangu." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا سَمِعْتُمُ النِّدَاءَ ، فَقُولُوا كَمَا يَقُولُ المُؤذِّنُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mkisikia adhana basi semeni kama anavyosema muadhini." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 7
وعن جابر رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَالَ حِيْنَ يَسْمَعُ النِّدَاءَ : اللَّهُمَّ رَبَّ هذِهِ الدَّعْوَةِ التَّامَّةِ ، وَالصَّلاَةِ القَائِمَةِ ، آتِ مُحَمَّداً الوَسِيلَةَ ، وَالفَضِيلَةَ ، وَابْعَثْهُ مَقَامَاً مَحْمُوداً الَّذِي وَعَدْتَهُ ، حَلَّتْ لَهُ شَفَاعَتي يَوْمَ القِيَامَةِ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusema pindi anaposikia mwito (adhaan): "Allaahumma Rabba Hadhihid Da'watit Taammati was-Swalaatil Qaa'imati Aaati Muhammadanil Wasiilah wal Fadhiilah wab'athhu maqaaman mahmuudani Ladhii wa'adtah" "Ee Rabb Mola wa ulingano huu mkamilifu. Na Mola wa Swalaah hii yenye kusimama, mpe Muhammad cheo (Wasila) na Fadhila. Na umfufue katika cheo chenye kuhimidiwa" Basi shufaa yangu itakuwa halali kwake Siku ya Qiyaamah." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 8
وعن سعدِ بن أَبي وقَّاصٍ رضي اللهُ عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنَّه قَالَ : (( مَنْ قَالَ حِيْنَ يَسْمَعُ المُؤَذِّنَ : أشْهَدُ أنْ لاَ إلَه إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لاَ شَرِيكَ لَهُ ، وَأنَّ مُحَمَّداً عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ ، رَضِيتُ بِاللهِ رَبّاً ، وَبِمُحَمَّدٍ رَسُولاً ، وَبِالإسْلامِ دِيناً ، غُفِرَ لَهُ ذَنْبُهُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Sa'd bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusema pindi anapomsikia muadhini: "Nashuhudia kwamba hapana Mola ila Allaah, hana mshirika. Na nashuhudia kuwa Muhammad ni mja na Rasuli Wake. Nimeridhia Allaah kuwa Rabb wangu, na Muhammad kuwa Rasuli, na Uislamu kuwa Dini", Anasamehemewa dhambi yake." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن أنس رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( الدُّعَاءُ لاَ يُرَدُّ بَيْنَ الأَذَانِ وَالإقَامَةِ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Dua baina ya adhana na iqamah hairudishwi (yaani hukubaliwa na Allaah)." [Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل الصلوات
08-Mlango Wa Fadhila Za Swalaah
Alhidaaya.com [4]
قَالَ الله تَعَالَى :
إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ۗ وَلَذِكْرُ اللَّـهِ أَكْبَرُ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا تَصْنَعُونَ ﴿٤٥﴾
Hakika Swalaah inazuia machafu na munkari. Na bila shaka kumdhukuru Allaah ni kubwa zaidi. Na Allaah Anajua yale mnayoyatenda. [Al-'Ankabuwt: 45]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول :
(( أرَأيْتُمْ لَوْ أنَّ نَهْرَاً بِبَابِ أَحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَوْمٍ خَمْسَ مَرَّاتٍ ، هَلْ يَبْقَى مِنْ دَرنهِ شَيْءٌ ؟ )) قالوا : لا يَبْقَى مِنْ دَرنهِ شَيْءٌ ، قَالَ : (( فَذلِكَ مَثَلُ الصَّلَوَاتِ الخَمْسِ يَمْحُو اللهُ بِهِنَّ الخَطَايَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mnaonaje kama kutakuwa na mto mlangoni kwa mmoja wenu, kila siku anaoga humo mara tano. Je, atabakia na uchafu wowote?" Wakasema: "Hatabakia na uchafu." Akasema: "Basi huo ndio mfano wa Swalaah tano, Allaah anfuta makosa." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن جابرٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَثَلُ الصَّلَواتِ الخَمْسِ كَمَثَلِ نَهْرٍ جَارٍ غَمْرٍ عَلَى بَابِ أحَدِكُمْ يَغْتَسِلُ مِنْهُ كُلَّ يَومٍ خَمْسَ مَرَّاتٍ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mfano wa Swalaah tano ni kama mfano wa mto ulio jirani wenye maji matamu na mengi ulio katika mlango wa mmoja wenu, anaoga humo kila siku mara tano." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن ابن مسعود رضي اللهُ عنه : أنَّ رَجُلاً أصَابَ مِن امْرَأَةٍ قُبْلَةً ، فَأتَى النبيَّ صلى الله عليه وسلم فَأخْبَرَهُ فَأنْزَلَ اللهُ تَعَالَى : ( أَقِمِ الصَّلاَةَ طَرَفَيِ النَّهَارِ وَزُلَفاً مِنَ اللَّيْلِ ، إنَّ الحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ) [ هود : 114 ] فَقَالَ الرَّجُلُ أَلِيَ هَذَا ؟ قَالَ : (( لِجَمِيعِ أُمَّتِي كُلِّهِمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Mtu mmoja alimbusu mwanamke ajnabi (anayeweza kumuoa), akaja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumuelezea hilo. Allaah Ta'aalaa Akateremsha: "Na simamisha Swalaah katika ncha mbili za mchana na sehemu ya kwanza ya usiku, hakika mema yanaondosha maovu. Haya ni ukumbusho kwa wanaokumbuka." [Huwd: 114]. Akasema yule mtu: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, hili ni langu tu?" Akasema: "Hili ni kwa Ummah wangu wote." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الصَّلَوَاتُ الخَمْسُ ، وَالجُمُعَةُ إِلَى الجُمُعَةِ ، كَفَّارَةٌ لِمَا بَيْنَهُنَّ ، مَا لَمْ تُغشَ الكَبَائِرُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah tano, na Ijumaa hadi Ijumaa na Ramadhwaan hadi Ramadhwaan ni zenye kufuta madhambi yaliyo kati yake kama yakiepukwa madhambi makubwa." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَا مِنْ امْرِئٍ مُسْلِمٍ تَحْضُرُهُ صَلاَةٌ مَكْتُوبَةٌ فَيُحْسِنُ وُضُوءها ؛ وَخُشُوعَهَا، وَرُكُوعَهَا ، إِلاَّ كَانَتْ كَفَّارَةً لِمَا قَبْلَهَا مِنَ الذُّنُوب مَا لَمْ تُؤتَ كَبِيرةٌ ، وَذلِكَ الدَّهْرَ كُلَّهُ )) رواه مسلم .
'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hapana mtu yeyote Muislamu ambaye inamuhudhurikia Swalaah iliyofaradhiwa akautengeneza vizuri wudhuu wake na unyenyekevu wake, na rukuu zake ila itakuwa ni kafara la yaliyo kabla yake miongoni mwa madhambi, muda wa kuwa halijatendwa kosa kubwa na utaratibu huo unaendelea maisha yote." [Muslim[.
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل صلاة الصبح والعصر
09-Mlango Wa Fadhila Ya Swalaah Ya Asubuhi Na Alasiri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي موسى رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ صَلَّى البَرْدَيْنِ دَخَلَ الجَنَّةَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakayeswali (katika nyakati za) baridi mbili (Alfajiri na Alasiri) ataingia Peponi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي زهير عُمارة بن رُؤَيْبَةَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ: سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لَنْ يَلِجَ النَّارَ أحَدٌ صَلَّى قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا )) يعني : الفَجْرَ والعَصْرَ . رواه مسلم .
Abuu Zuhayr 'Ummaarah bin Ruwaybah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hataingia Motoni yeyote anayeswali kabla ya kuchomoza kwa jua na kabla kuchwa jua (yaani Alfajiri na Alasiri)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جُنْدُبِ بن سفيان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ صَلَّى الصُّبْحَ فَهُوَ في ذِمَّةِ اللهِ ، فَانْظُرْ يَا ابْنَ آدَمَ ، لاَ يَطْلُبَنَّكَ اللهُ مِنْ ذِمَّتِهِ بِشَيءٍ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jundub bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote mwenye kuswali Swalaah ya Asubuhi yupo katika himaya ya Allaah (katika usalama na chini ya dhamana yake). Hivyo ee Bin Aadam usivunje dhamana ya Allaah kwa chochote." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَتَعَاقَبُونَ فِيكُمْ مَلاَئِكَةٌ بِاللَّيْلِ ، وَمَلاَئِكَةٌ بِالنَّهَارِ ، وَيجْتَمِعُونَ في صَلاَةِ الصُّبْحِ وَصَلاَةِ العَصْرِ ، ثُمَّ يَعْرُجُ الَّذِينَ بَاتُوا فِيكُمْ ، فَيَسْأَلُهُمُ اللهُ - وَهُوَ أعْلَمُ بِهِمْ - كَيْفَ تَرَكْتُمْ عِبَادي ؟ فَيقُولُونَ : تَرَكْنَاهُمْ وَهُمْ يُصَلُّونَ ، وَأتَيْنَاهُمْ وَهُمْ يُصَلُّونَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kwake Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wanapishana kati yenu Malaaikah wakati wa usiku na Malaaikah wakati wa mchana na wanajikusanya pamoja katika Swalaah ya Alfajiri na Swalaah ya Alasiri. Kisha wale Malaaikah waliokuwa usiku pamoja nanyi wanapanda juu na Allaah anawauliza: 'Mumewaachaje waja wangu?' Nao watajibu: 'Tumewaacha wakiwa wanaswali, na tumekwenda kwao tena na tumewakuta wanaswali.' " [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن جرير بن عبد الله البَجَليِّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كُنَّا عِنْدَ النبيِّ صلى الله عليه وسلم فَنَظَرَ إِلَى القَمَرِ لَيْلَةَ البَدْرِ ، فَقَالَ : (( إنَّكُمْ سَتَرَونَ رَبَّكُمْ كَمَا تَرَوْنَ هَذَا القَمَرَ ، لاَ تُضَامُونَ في رُؤْيَتهِ ، فَإنِ اسْتَطَعْتُمْ أنْ لاَ تُغْلَبُوا عَلَى صَلاَةٍ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا ، فَافْعَلُوا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية : (( فَنَظَرَ إِلَى القَمَرِ لَيْلَةَ أرْبَعَ عَشْرَةَ )) .
Na Jariyr bin 'Abdillaah Al-Bajaliy (Radhwiya Allaah 'anhu) amesema: Tulikuwa na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku, akauangalia mwezi uliokamilika mduara wake, akasema: "Hakika mtamuona Rabb wenu kama mnavyouona mwezi huu wala hamtasumbuliwa (au kudhulimiwa) katika kumuona na kama mtaweza kuwa mnaswali (daima) Swalaah ya kabla ya kuchomoza jua na Swalaah ya kabla ya kuzama jua fanyeni." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Na katika riwaayah nyingine: "Akauangalia mwezi usiku wa tarehe kumi na nne (14)."
Hadiyth – 6
وعن بُرَيْدَة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ تَرَكَ صَلاَةَ العَصْرِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuacha Swalaah ya Alasiri basi imeharibika amali yake." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل المشي إلى المساجد
10-Mlango Wa Fadhila Ya Kwenda Msikitini
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ غَدَا إلى المَسْجِدِ أَوْ رَاحَ ، أعَدَّ اللَّهُ لَهُ فِي الجَنَّةِ نُزُلاً كُلَّمَا غَدَا أوْ رَاحَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakayetoks mapema kwenda Msikitini na akarudi Allaah atamuandalia makazi Peponi kila anapoenda au anaporudi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
عن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ تَطَهَّرَ في بَيْتِهِ ، ثُمَّ مَضَى إلى بَيْتٍ مِنْ بُيُوتِ اللَّهِ ، لِيَقْضِي فَرِيضَةً مِنْ فَرَائِضِ اللَّهِ ، كَانَتْ خُطُواتُهُ ، إحْدَاهَا تَحُطُّ خَطِيئَةً ، وَالأُخْرَى تَرْفَعُ دَرَجَةً )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwake Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kujitwahirisha (kutawadha) nyumbani kwake kisha akaelekea kwenye nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah ili atekeleze faradhi miongoni mwa faradhi za Allaah basi hatua yake moja inafuta dhambi na nyingine inanyanyua daraja yake." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أُبيّ بن كعبٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رَجُلٌ مِنَ الأنْصَارِ لاَ أَعْلمُ أَحَداً أبْعَدَ مِنَ المَسْجِدِ مِنْهُ ، وَكَانَتْ لا تُخْطِئُهُ صَلاَةٌ ، فَقيلَ لَهُ : لَوْ اشْتَرَيْتَ حِمَاراً لِتَرْكَبَهُ في الظَّلْمَاءِ وَفِي الرَّمْضَاءِ ، قَالَ : مَا يَسُرُّنِي أنَّ مَنْزِلِي إلى جَنْبِ المَسْجِدِ ، إنِّي أُرِيدُ أنْ يُكْتَبَ لِي مَمْشَايَ إلى المَسْجِدِ ، وَرُجُوعِي إذَا رَجَعْتُ إلى أهْلِي . فَقَالَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( قَدْ جَمَعَ اللَّهُ لكَ ذَلِكَ كُلَّه )) رواه مُسلِم .
Imepokewa kutoka kwake Ubayy bin Ka'ab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Kulikuwa na mtu katika Answaar wala simjui mtu yeyote aliyekuwa mbali na msikiti kama yeye. Na alikuwa hakosi Swalaah hata moja, hivyo akaambiwa: 'Lau kama ungenunua punda ili kumpanda wakati wa giza na wakati wa joto kali.' Akasema: 'Sipendelei kabisa nyumba yangu kuwa karibu na msikiti. Nami napenda niandikiwe kutembea kwangu kuelekea Msikitini na kurudi kwangu ninaporudi kwa familia yangu.' Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): 'Hakika Allaah amekuandikia yote hayo katika hesabu yako'." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن جابر رضي اللهُ عنه ، قَالَ : خَلَت البِقاعُ حولَ المَسْجِدِ ، فَأَرَادَ بَنُو سَلمَةَ أنْ يَنْتَقِلُوا قُرْبَ المَسْجِدِ ، فَبَلَغَ ذَلِكَ النبي صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ لَهُمْ : (( بَلَغَنِي أنَّكُم تُريدُونَ أنْ تَنْتَقِلُوا قُرْبَ المَسْجِدِ ؟ )) قالوا : نعم ، يا رَسُول اللَّهِ ، قَدْ أرَدْنَا ذَلِكَ . فَقَالَ : (( بَنِي سَلِمَةَ دِيَارَكُم تُكْتَبْ آثارُكُمْ ، دِيَارَكُمْ تُكْتَبْ آثارُكُمْ )) فقالوا : مَا يَسُرُّنَا أنَّا كُنَّا تَحَوَّلْنَا . رواه مسلم ، وروى البخاري معناه من رواية أنس .
Imepokewa kutoka kwake Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Ardhi kando ya msikiti ilikuwa tupu "Wakataka Banu (ukoo wa) Salamah kuhamia karibu na Msikiti. Habari hiyo ilimfikia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), ambaye aliwaambia: 'Hakika imenifikia mimi kuwa nyinyi mnataka kuhamia karibu na Msikiti?' Wakasema: 'Ndio, ee Rasuli wa Allaah, hakika sisi tumetaka kufanya hivyo.' Akasema: 'Bani Salamah, kaeni katika nyumba zenu kwani nyayo zenu zinaandikwa. Bani Salamah, kaeni katika nyumba zenu kwani nyao zenu zinaandikwa." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أبي موسى رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قال رَسُول اللَّهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ أَعْظَمَ النَّاسِ أجْراً في الصَّلاةِ أبْعَدُهُمْ إلَيْهَا مَمْشىً ، فَأَبْعَدُهُمْ ، وَالَّذِي يَنْتَظِرُ الصَّلاَةَ حَتَّى يُصَلِّيَهَا مَعَ الإمَامِ أعظَمُ أجْراً مِنَ الَّذِي يُصَلِّيهَا ثُمَّ يَنَامُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mtu anayepata malipo zaidi katika Swalaah, ni yule anayekaa mbali zaidi na anyetembea mbali zaidi. Na pia yule anayesubiri Swalaah mpaka anaswali pamoja na Imamu malipo yake ni makubwa zaidi kuliko yule anayeswali kisha akalala." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن بُريدَة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بَشِّرُوا المَشَّائِينَ في الظُّلَمِ إلى المَسَاجِدِ بِالنُّورِ التَّامِّ يَوْمَ القِيَامَةِ )) رواه أبُو دَاوُدَ وَالتِّرمِذِيُّ .
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Wapeni bishara njema wenye kutembea kuelekea Misikitini katika giza kuwa watapata nuru timilifu (kamili) Siku ya Qiyaamah." [Abuu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 7
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( ألا أدُلُّكُمْ عَلَى مَا يَمْحُو اللهُ بِهِ الخَطَايَا ، وَيَرْفَعُ بِهِ الدَّرَجَاتِ ؟ )) قَالُوا : بَلَى يا رَسُول اللهِ ؟ قَالَ : (( إسْبَاغُ الوُضُوءِ عَلَى المَكَارِهِ ، وَكَثْرَةُ الخُطَا إلَى المَسَاجِدِ ، وَانْتِظَارُ الصَّلاَةِ بَعْدَ الصَّلاَةِ ، فَذَلِكُمُ الرِّبَاطُ ، فذَلِكُمُ الرِّبَاطُ )) رواه مسلِم .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hivi niwafahamishe juu ya kile ambacho Allaah anafutia nacho makosa na ananyanyua nacho daraja?" Wakasema: "Kwa nini ee Rasuli wa Allaah, tufahamishe." Akasema: "Kujieneza wudhuu pamoja na machukivu ( kiviosha viungo pamoja na kutunza adabu na ukamilifu wake mbali na kuwa na taabu mfano wa ubaridi, hali ya hewa mbaya, kuumwa, n.k.) na wingi wa kupiga hatua kwenda Msikitini na kuingoja Swalaah baada ya Swalaah, huo ndio ulindaji." [Muslim]
Hadiyth – 8
وعن أبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إذا رَأَيْتُمُ الرَّجُلَ يَعْتَادُ المَسَاجِدَ فَاشْهَدُوا لَهُ بالإيمَانِ ، قال اللهُ عزوجل : ( إِنَّمَا يَعْمُرُ مَسَاجِدَ اللهِ مَنْ آمَنَ بِاللهِ وَالْيَوْمِ الآخِرِ ) الآية )) رواه الترمذي، وقال: (( حديث حسن )).
Imepokewa kutoka kwa Abuu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mnapomuona mtu anazoea Msikitini mshuhudie kuwa ana Imani. Amesema Allaah Ta'aalaa: 'Hakika wanaoamirisha Misikiti ya Allaah ni wale wanaomwamini Allaah na Siku ya Mwisho, na wakasimamisha Swalaah na wakatoa Zakaah na hawamkhofu (yeyote) isipokuwa Allaah. Basi asaa hao wakawa miongoni mwa walioongoka'. [At-Tawbah: 18]." [At-Tirmidhiy, na akasema Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل انتظار الصلاة
11-Mlango Wa Ubora Wa kungojea Swalaah
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لا يَزَالُ أحَدُكُمْ في صَلاَةٍ مَا دَامَتِ الصَّلاَةُ تَحْبِسُهُ ، لا يَمنَعُهُ أنْ يَنقَلِبَ إلى أهلِهِ إلاَّ الصَّلاةُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hatoacha mmoja wenu kuwa anahesabiwa yuko katika Swalaah madamu Swalaah ndiyo inayomzuia, hakuna kinachomzuia kurudi kwa familia yake isipokuwa Swalaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الْمَلائِكَةُ تُصَلِّي عَلَى أَحَدِكُمْ مَا دَامَ فِي مُصَلاَّهُ الَّذِي صَلَّى فِيهِ، مَا لَمْ يُحْدِثْ، تَقُولُ : اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ ، اللَّهُمَّ ارْحَمْهُ )) رواه البُخَارِيُّ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Malaaikah wanamuombea msamaha na rehema mmoja wenu madamu amebaki kwenye msala alioswalia juu yake muda wa kuwa hajahuduthi hapo (hajatokwa na wudhuu), wakisema: "Ee Mola wetu msamehe, ee Mola wetu mrehemu." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم أَخَّرَ لَيْلَةً صَلاَةَ العِشَاءِ إِلَى شَطْرِ اللَّيْلِ ثُمَّ أقْبَلَ عَلَيْنَا بِوَجْهِهِ بَعْدَمَا صَلَّى ، فَقَالَ : (( صَلَّى النَّاسُ وَرَقَدُوا ، وَلَمْ تَزَالُوا في صَلاَةٍ مُنْذُ انْتَظَرْتُمُوهَا )) رواه البُخَارِيُّ .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) anasimulia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliakhirisha usiku mmoja Swalaah ya Isha mpaka nusu ya usiku. Baada ya Swalaah alitukabili na kusema: "Baadhi ya watu waliswali na kwenda kulala lakini waliosubiri (ili kupata Swalaah ya jamaa) walikuwa katika Swalaah kuanzia walipoanza kuingojea." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل صلاة الجماعة
12-Mlango Wa Fadhila ya Swalah ya Jamaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلاَةُ الْجَمَاعَة أفْضَلُ مِنْ صَلاَةِ الْفَذِّ بِسَبْعٍ وَعِشْرِينَ دَرَجَةً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah ya jamaa inazidi Swalaah ya mtu peke yake kwa daraja ishirini na saba (27)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قال رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( صَلاةُ الرَّجُلِ في جَمَاعةٍ تُضَعَّفُ عَلَى صَلاتِهِ فِي بَيْتهِ وفي سُوقِهِ خَمْساً وَعِشْرِينَ ضِعْفَاً ، وَذلِكَ أَنَّهُ إذَا تَوَضَّأ فَأحْسَنَ الوُضُوءَ ، ثُمَّ خَرَجَ إلى المَسْجِدِ ، لا يُخرِجُهُ إلاَّ الصَّلاةُ ، لَمْ يَخْطُ خَطْوَةً إلاَّ رُفِعَتْ لَهُ بِهَا دَرَجَةٌ ، وَحُطَّتْ عَنهُ بِهَا خَطِيئَةٌ ، فَإذَا صَلَّى لَمْ تَزَلِ المَلائِكَةُ تُصَلِّي عَلَيْهِ مَا دَامَ في مُصَلاَّهُ ، مَا لَمْ يُحْدِث ، تقولُ : اللَّهُمَّ صَلِّ عَلَيهِ ، اللَّهُمَّ ارْحَمْهُ ، وَلاَ يَزَالُ في صَلاةٍ مَا انْتَظَرَ الصَّلاَةَ )) متفقٌ عَلَيهِ ، وهذا لفظ البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah ya jamaa inazidi Swalaah ya mtu nyumbani kwake, na Swalaah yake sokoni kwake kwa daraja ishirini na tano (25). Hakika mmoja wenu atakapotawadha na akafanya uzuri wudhuu wake na akaja Msikitini hakusudii jingine ila Swalaah, basi hapigi hatua moja ila Allaah atamnyanyua kwa kila hatua daraja na utamuondoshea kwa kila hatua kosa mpaka aingie Msikitini na anpoingia Msikitini atakuwa katika Swalaah muda wa kuwa Swalaah ndiyo inamzuia, na Malaaikah wanamtakia rehema madamu yupo katika kikao chake anachoswalia. Wakisema: 'Ee Mola wetu msamehe, ee Mola wetu mrehemu.' Na anaendelea kuwa katika Swalaah madamu anaingojea Swalaah." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : أَتَى النبيَّ صلى الله عليه وسلم رَجُلٌ أعْمَى ، فقَالَ : يا رَسُولَ اللهِ ، لَيسَ لِي قَائِدٌ يَقُودُنِي إلى الْمَسْجِدِ ، فَسَأَلَ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ يُرَخِّصَ لَهُ فَيُصَلِّي فِي بَيْتِهِ ، فَرَخَّصَ لَهُ ، فَلَّمَا وَلَّى دَعَاهُ ، فَقَالَ لَهُ : (( هَلْ تَسْمَعُ النِّدَاءَ بِالصَّلاَةِ ؟ )) قَالَ : نَعَمْ . قَالَ : (( فَأجِبْ )) رواه مُسلِم .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba alikuja mtu kipofu alimwambia: "Ee Rasuli wa Allaah! mimi sina wa kuniongoza kwenda Msikitini", hivyo akamtaka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amruhusu kuswali nyumbani kwake. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimruhusu na alipoondoka akamwita na kumuuliza: "Je, unasikia adhana?" Akasema: "Ndio." Akasema: "Basi itikia wito." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن عبدِ الله – وقيل : عَمْرو بن قَيسٍ - المعروف بابن أُمّ مكتوم المؤذن رضي الله عنه أنَّه قَالَ: يا رَسُول اللهِ ، إنَّ المَدينَةَ كَثيرةُ الهَوَامِّ وَالسِّبَاعِ . فَقَالَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( تَسْمَعُ حَيَّ عَلَى الصَّلاةِ حَيَّ عَلَى الفَلاحِ ، فَحَيَّهلاً )) رَوَاهُ أبُو دَاوُدَ بإسناد حسن .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah, na kulisemwa 'Amru bin Qays (Radhwiya Allaahu 'anhu) maarufu kwa jina la Ibn Umma Maktuum muadhini wa Nabiy kuwa yeye amesema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mji wa Madiynah una wadudu wengi na wanyama wabaya." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Unasikia Hayya 'alasw Swalaah, Hayya 'alai Falaah (Njooni kwenye Swalaah, njooni kwenye kheri yaani adhana), hivyo njoo Msikitini." [Abuu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Hadiyth – 5
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( وَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لَقَدْ هَمَمْتُ أنْ آمُرَ بحَطَبٍ فَيُحْتَطَبَ ، ثُمَّ آمُرَ بِالصَّلاَةِ فَيُؤذَّنَ لهَا ، ثُمَّ آمُرَ رَجُلاً فَيَؤُمَّ النَّاسَ ، ثُمَّ أُخَالِفَ إلى رِجَالٍ فَأُحَرِّقَ عَلَيْهِمْ بُيُوتَهمْ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Naapa kwa Allaah ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake hakika nilitaka kuamrisha ziletwe kuni na ziwashwe, kisha niamrishe Swalaah iadhiniwe, kisha niamrisha mtu awaswalishe watu. Kisha niwaendee watu ambao hawakuhudhura Swalaah ya jamaa nizichome nyumba zao." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : مَنْ سَرَّهُ أنْ يَلْقَى اللهَ تَعَالَى غداً مُسْلِماً ، فَلْيُحَافِظْ عَلَى هؤُلاَءِ الصَّلَوَاتِ حَيْثُ يُنَادَى بِهِنَّ ، فَإنَّ اللهَ شَرَعَ لِنَبِيِّكم صلى الله عليه وسلم سُنَنَ الهُدَى ، وَإنَّهُنَّ مِنْ سُنَنِ الهُدَى ، وَلَوْ أنَّكُمْ صَلَّيْتُمْ في بُيُوتِكم كَمَا يُصَلِّي هذا المُتَخَلِّفُ فِي بَيْتِهِ لَتَرَكْتُمْ سُنَّةَ نَبِيِّكُمْ ، وَلَوْ تَرَكْتُمْ سُنَّة نَبِيِّكُم لَضَلَلْتُمْ ، وَلَقَدْ رَأيْتُنَا وَمَا يَتَخَلَّفُ عَنْهَا إلاَّ مُنَافِقٌ مَعْلُومُ النِّفَاقِ ، وَلَقَدْ كَانَ الرَّجُلُ يُؤتَى بهِ ، يُهَادَى بَيْنَ الرَّجُلَيْنِ حَتَّى يُقَامَ في الصَّفِّ . رَوَاهُ مُسلِم .
وفي رواية لَهُ قَالَ : إنّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم عَلَّمَنَا سُنَنَ الهُدَى ؛ وإنَّ مِنْ سُنَنِ الهُدَى الصَّلاَةَ في المَسْجِدِ الَّذِي يُؤَذَّنُ فِيهِ .
Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Mwenye kupenda kukutana na Allaah Ta'aalaa kesho akiwa Muislamu basi azihifadhi hizi Swalaah tano anapoitwa kwazo. Hakika Allaah ameweka kwa Nabiy wenu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Sunnah za uwongofu na kwa hakika hizo (Swalaah) ni sunnah za uwongofu. Na lau nyinyi mtaswali majumbani mwenu kama anavyoswali huyu anayebaki nyuma katika nyumba yake mtakuwa mumeacha sunnah ya Nabiy wenu. Na lau mtaacha Sunnah ya Nabiy wenu basi mutapotea. Ungetuona ilikuwa mtu hawezi kuacha Swalaah ya jamaa isipokuwa mnafiki anayejulikana unafiki wake, na ilikuwa mtu huletwa hali ya kuwa amebebwa na watu wawili na anawekwa kwenye safu katika hali hiyo." [Mulim]
Na katika riwaayah yake nyengine amesema: "Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametufundisha Sunnah za uwongofu na hakika miongoni mwa Sunnah za uwongofu ni kuswali kwenye Msikiti unaoadhiniwa ndani yake."
Hadiyth – 7
وعن أبي الدرداء رضي الله عنه ، قال : سمعت رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَا مِنْ ثَلاثَةٍ فِي قَرْيةٍ ، وَلاَ بَدْوٍ ، لا تُقَامُ فِيهِمُ الصَّلاَةُ إلاَّ قَد اسْتَحْوَذَ عَلَيْهِم الشَّيْطَانُ . فَعَلَيْكُمْ بِالجَمَاعَةِ ، فَإنَّمَا يَأْكُلُ الذِّئْبُ مِنَ الغَنَمِ القَاصِيَة )) رَوَاهُ أبُو دَاوُدَ بإسناد حسن .
Abuu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna watu watatu katika kijiji au kitongoji ambako haisimamishwi hapo Swalaah ya jamaa isipokuwa watakuwa wamepotezwa na shetani, basi jilazimisheni kusimamisha jamaa kwani mbwa mwitu humla kondoo aliyejitenga." [Abuu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الحث عَلَى حضور الجماعة في الصبح والعشاء
13-Mlango Wa Kuhimiza Kuhudhuria Jamaa Katika Swalah ya Asubuhi na Ishaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَنْ صَلَّى العِشَاءَ فِي جَمَاعَةٍ ، فَكَأنَّمَا قَامَ نِصْفَ اللَّيْلِ ، وَمَنْ صَلَّى الصُّبْحَ في جَمَاعَةٍ ، فَكَأنَّمَا صَلَّى اللَّيْلَ كُلَّهُ )) رواه مُسلِم .
وفي رواية الترمذي عن عثمان بن عفان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ شَهِدَ العِشَاءَ فِي جَمَاعَةٍ كَانَ لَهُ قِيَامُ نِصْفَ لَيلَةٍ ، وَمَنْ صَلَّى العِشَاءَ وَالفَجْرَ فِي جَمَاعَةٍ ، كَانَ لَهُ كَقِيَامِ لَيْلَةٍ )) قَالَ الترمذي : (( حديث حسن صحيح )) .
'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) Amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Mwenye kuswali Swalaah ya Ishaa kwa jamaa ni kama ameswali nusu ya usiku na mwenye kuswali Asubuhi kwa jamaa ni kama kwamba ameswali usiku kucha (usiku wote)." [Muslim]
Na katika riwaayah ya At-Tirmidhiy kutoka kwa 'Uthmaan bin 'Affaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kushuhudia Swalaah ya Ishaa kwa jamaa ni kama aliyesimama kuswali nusu ya usiku. Na mwenye kuswali Ishaa na Alfajiri kwa jamaa ni kama kwamba ameswali usiku mzima." [Amesema At-Tirmidhiy kuwa hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( وَلَوْ يَعْلَمُونَ مَا في العَتَمَةِ وَالصُّبْحِ لأَتَوْهُمَا وَلَوْ حَبْوَاً )) متفقٌ عَلَيهِ . وقد سبق بِطولِهِ .
Imepokewa kutoka kwaAbuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Na lau kama wanafiki wangejua fadhila za Swalaah ya Ishaa na Asubuhi basi wangekuja hata kwa kutambaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لَيْسَ صَلاَةٌ أثْقَلَ عَلَى المُنَافِقِينَ مِنْ صَلاَةِ الفَجْرِ وَالعِشَاءِ ، وَلَوْ يَعْلَمُونَ مَا فِيهِمَا لأَتَوْهُمَا وَلَوْ حَبْواً )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna Swalaah nzito kwa wanafiki kuliko Swalaah ya Alfajiri na Ishaa, na lau wangejua ubora wa Swalaah hizi mbili wangezijia hata kwa kutambaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الأمر بالمحافظة عَلَى الصلوات المكتوبات
والنهي الأكيد والوعيد الشديد في تركهنّ
14-Mlango Wa Amri ya Kuhifadhi Swalah za Faradhi na Onyo Kali kwa Kuziacha
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
حَافِظُوا عَلَى الصَّلَوَاتِ وَالصَّلَاةِ الْوُسْطَىٰ وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ﴿٢٣٨﴾
Shikamaneni na Swalaah na khaswa Swalaah ya katikati (Alasiri), na simameni mbele ya Allaah katika hali ya utiifu. [Al-Baqarah: 238]
فَإِن تَابُوا وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَآتَوُا الزَّكَاةَ فَخَلُّوا سَبِيلَهُمْ ۚ ﴿٥﴾
Lakini wakitubu, na wakasimamisha Swalaah na wakatoa Zakaah, basi iacheni njia yao (huru). [At-Tawbah: 5]
Hadiyth – 1
وعن ابن مسعود رضي اللهُ عنه ، قال : سألت رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم أيُّ الأعْمَالِ أفْضَلُ ؟ قَالَ : (( الصَّلاَةُ عَلَى وَقْتِهَا )) قلتُ : ثُمَّ أيٌّ ؟ قَالَ : (( بِرُّ الوَالِدَيْنِ )) قلتُ : ثُمَّ أيٌّ ؟ قَالَ : (( الجِهَادُ في سَبِيلِ اللهِ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Nilimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ni amali gani inampendeza Allaah zaidi ?" Akasema: "Ni Swalaah kwa wakati wake." Nikasema: "Kisha ni ipi?" Akasema: "Kuwatendea wema wazazi wawili." Nikasema: "Kisha ipi?" Akasema: "Jihadi katika Njia ya Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( بُنِيَ الإسْلامُ عَلَى خَمْسٍ : شَهَادَةِ أنْ لاَ إلهَ إلاَّ اللهُ ، وَأنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللهِ ، وَإِقَامِ الصَّلاَةِ ، وَإِيتَاءِ الزَّكَاةِ ، وَحَجِّ البَيْتِ ، وَصَوْمِ رَمَضَانَ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Uislamu Umejengwa juu ya nguzo tano: Kukiri kwa moyo na kubaini kwa ulimi kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Allaah, na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, na kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah, na kuhiji na kufunga mwezi wa Ramadhwaan." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaai].
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أُمِرْتُ أنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى يَشْهَدُوا أنْ لاَ إلهَ إلاَّ اللهُ ، وأنَّ مُحَمَّداً رَسُولُ اللهِ ، وَيُقِيمُوا الصَّلاَةَ ، وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَ ، فَإذَا فَعَلُوا ذَلِكَ ، عَصَمُوا مِنِّي دِمَاءهُمْ وَأَمْوَالَهُمْ ، إلاَّ بِحَقِّ الإسْلاَمِ ، وَحِسَابُهُمْ عَلَى اللهِ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nimeamrishwa nipigane na watu mpaka wakubali kuwa hakuna Mola wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, na kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah. Wakifanya hivyo zitahifadhika kwangu damu zao na mali yao isipokuwa kwa haki ya Uislaamu, na hesabu yao iko kwa Allaah Ta'aalaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن معاذٍ رضي الله عنه ، قَالَ : بَعثنِي رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم إلى اليَمَنِ ، فَقَالَ : (( إنَّكَ تَأْتِي قَوْماً مِنْ أَهْل الكِتَابِ ، فَادْعُهُمْ إلى شَهَادَةِ أنْ لاَ إلهَ إلاَّ اللهُ ، وأنِّي رَسُولُ اللهِ ، فَإنْ هُمْ أطاعُوا لِذلِكَ ، فَأعْلِمْهُمْ أنَّ اللهَ تَعَالَى افْتَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صلَوَاتٍ فِي كُلِّ يَومٍ وَلَيلَةٍ ، فَإنْ هُمْ أطَاعُوا لِذَلِكَ ، فَأعْلِمْهُمْ أنَّ اللهَ تَعَالَى افْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤخَذُ مِنْ أغْنِيَائِهِمْ فَتُرَدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ ، فَإنْ هُمْ أطَاعُوا لِذلِكَ ، فَإيَّاكَ وَكَرَائِمَ أمْوَالهِمْ ، واتَّقِ دَعْوَةَ المَظْلُومِ ، فَإنَّهُ لَيْسَ بَينَهَا وبَيْنَ اللهِ حِجَابٌ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Mu'aadh (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinituma: "Hakika wewe unaenda kwa watu waliopewa Kitabu, hivyo waite katika Uislaamu na washuhudie ya kwamba hapana mungu anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na kwamba mimi ni Rasuli Wake. Wakikutii katika hilo, wafahamishe kuwa Allaah amewafaradhishia juu yao Swalaah tano kwa kila mchana na usiku. Wakikutii katika hilo, wafahamishe kuwa Allaah amewafaradhishia juu yao kutoa Swadaqah, inayochukuliwa kutoka kwa matajiri wao na kupatiwa mafakiri miongoni mwao. Ikiwa wao watakutii katika hilo, tahadhari sana na vilivyo bora ya mali zao. Naogopa sana dua ya mwenye kudhulumiwa kwa sababu hakuna kizuizi baina yake na Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن جابرٍ رضي الله عنه ، قال : سمعت رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ بَيْنَ الرَّجُلِ وَبَيْنَ الشِّرْكِ والكفر ، تَرْكَ الصَّلاَةِ )) رواه مُسلِم .
Na Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Kizuizi kilichoko baina ya mtu na shirki na ukafiri ni kuacha Swalaah." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن بُرَيْدَة رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( العَهْدُ الَّذِي بَيْنَنَا وَبَيْنَهُمْ الصَّلاَةُ ، فَمَنْ تَرَكَهَا فَقَدْ كَفَرَ )) رواه التِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ صحيح ))
Imepokewa kutoka kwa Buraydah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tofauti iliyopo baina yetu na wao (yaani wanafiki) ni Swalaah, mwenye kuiacha hakika amekufuru." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن شقِيق بن عبدِ الله التَّابِعيِّ المتفق عَلَى جَلاَلَتِهِ رَحِمهُ اللهُ ، قَالَ : كَانَ أصْحَابُ محَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم لا يَرَوْنَ شَيْئاً مِنَ الأعْمَالِ تَرْكُهُ كُفْرٌ غَيْرَ الصَّلاَةِ . رَوَاهُ التِّرمِذِيُّ في كِتابِ الإيمان بإسنادٍ صحيحٍ .
Na kutoka kwa Shaqiyq bin 'Abdillaah, Tabi'iy (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye utukufu kumeafikiwa na ubora wake amesema kwamba: Swahaaba wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Walikuwa hawaoni ni chochote katika amali ambazo kuziacha ni ukafiri isipokuwa Swalaah." [At-Tirmidhiy katika Kitabu cha Iymaan kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 8
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ أوَّلَ مَا يُحَاسَبُ بِهِ العَبْدُ يَوْمَ القِيَامَةِ مِنْ عَمَلِهِ صَلاَتُهُ ، فَإنْ صَلَحَتْ ، فَقَدْ أفْلَحَ وأَنْجَحَ ، وَإنْ فَسَدَتْ ، فَقَدْ خَابَ وَخَسِرَ ، فَإنْ انْتَقَصَ مِنْ فَرِيضَتِهِ شَيْءٌ ، قَالَ الرَّبُ عزوجل : انْظُرُوا هَلْ لِعَبدي من تطوّعٍ ، فَيُكَمَّلُ مِنْهَا مَا انْتَقَصَ مِنَ الفَرِيضَةِ ؟ ثُمَّ تَكُونُ سَائِرُ أعْمَالِهِ عَلَى هَذَا )) رواه التِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )) .
Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Faradhi ya kwanza atakayoulizwa Muislamu Siku ya Qiyaamah kuwa kaitekeleza - na kaitekeleza vilivyo ni Swalaah. Ikiwa aliitekeleza vilivyo basi amefaulu na kuokoka. Na kama faradhi yake imepungua chochote Rabb atasema angalieni Swalaah za Sunnah, na alizileta vilivyo? Ikiwa alifanya hivyo ataungiwaungiwa katika hizo faradhi alizoziharibu kidogo. Kisha amali nyengine zitahesabiwa hivyo hivyo." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل الصف الأول
والأمر بإتمام الصفوف الأُوَل وتسويتها والتراصّ فِيهَا
15-Mlango Wa Fadhila za Safu ya Kwanza na Amri ya Kutimiza Safu ya Kwanza na Kuzinyoosha
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن جابر بن سَمُرَة رضي الله عنهما ، قَالَ : خَرَجَ عَلَيْنَا رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ: (( ألاَ تَصُفُّونَ كَمَا تَصُفُّ المَلائِكَةُ عِندَ رَبِّهَا ؟ )) فَقُلنَا : يَا رَسُول اللهِ ، وَكَيفَ تُصَفُّ المَلائِكَةُ عِندَ رَبِّهَا ؟ قَالَ : (( يُتِمُّونَ الصُّفُوفَ الأُوَلَ ، وَيَتَرَاصُّونَ في الصَّفِّ )) رواه مُسلِم
Imepokewa kutoka kwa Jaabir bin Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuja kutuswalisha naye akauliza: "Kwa nini hamnyooshi safu kama wanyoshavyo Malaaikah mbele ya Rabb wao?" Tukamwuliza: "Malaaikah wananyoshaje safu mbele ya Rabb wao?" Akajibu: "Wanakamilisha safu ya mwanzo, nao hujipanga katika safu zilizonyooka sambamba." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْ يَعْلَمُ النَّاسُ مَا فِي النِّدَاءِ وَالصَّفِّ الأَوَّلِ ، ثُمَّ لَمْ يَجِدُوا إلاَّ أنْ يَسْتَهِمُوا عَلَيْهِ لاسْتَهَمُوا )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Lau kama watu wangejua fadhila za adhana (kuitikia) na kusimama katika safu ya kwanza, kisha wakawa hawakupata njia ya kudiriki isipokuwa kwa kupiga kura basi wangalipiga kura." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( خيْرُ صُفُوفِ الرِّجَالِ أوَّلُهَا ، وَشَرُّهَا آخِرُهَا ، وَخَيْرُ صُفُوفِ النِّسَاءِ آخِرُهَا ، وَشَرُّهَا أوَّلُهَا )) رواه مُسلِم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Safu bora ya wanaume ni ile ya mbele na safu yenye shari ni ile ya mwisho na bora ya safu kwa wanawake ni ile ya mwisho na safu yenye shari kwao ni ile ya mwanzo." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أبي سعيد الخدرِيِّ رضي الله عنه : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم رأى في أصْحَابِهِ تَأَخُّراً ، فَقَالَ لَهُمْ : (( تَقَدَّمُوا فَأتَمُّوا بِي ، وَلْيَأتَمَّ بِكُمْ مَنْ بَعْدَكُمْ ، لاَ يَزَالُ قَوْمٌ يَتَأَخَّرُونَ حَتَّى يُؤَخِّرَهُمُ الله )) رواه مُسلِم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaona baadhi ya Swahaaba zake wanachelewa nyuma (wakati wa Swalaah ya jamaa) akawaambia: "Njooni mbele nyuma yangu na wanaofuatia wasimame nyuma yenu. Na hawataacha watu kuendelea kujiweka nyuma mpaka Allaah awaweke nyuma." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أبي مسعود رضي الله عنه ، قال : كَانَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يَمْسَحُ مَنَاكِبَنَا في الصَّلاَةِ ، وَيَقُولُ : (( اسْتَووا ولاَ تَخْتَلِفُوا فَتَخْتَلِفَ قُلُوبُكُمْ ، لِيَلِيَنِي مِنْكُمْ أُولُو الأحْلاَمِ وَالنُّهَى ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ ، ثُمَّ الَّذِينَ يَلُونَهُمْ )) رَوَاهُ مُسلِم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiyagusa mabega yetu wakati wa Swalaah, na akisema: "Nyookeni na wala msipinde pinde kwani msiponyooka, Allaah Atatia khitilafu nyoyoni mwenu mkhitilafiane. Wasimame nyuma yangu wale waliobaleghe na wenye akili na ilimu, kisha wale wanaowafuata." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قال رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( سَوُّوا صُفُوفَكُمْ ؛ فَإنَّ تَسْوِيَةَ الصَّفِّ مِنْ تَمَامِ الصَّلاَةِ )) متفقٌ عَلَيهِ .
وفي رواية للبخاري : (( فَإنَّ تَسْوِيَةَ الصُّفُوفِ مِنْ إقَامَةِ الصَّلاَةِ )) .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nyoosheni safu zenu kwani kunyoosha safu ni katika kukamilisha safu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: "Hakika kunyoosha safu ni katika kusimamisha Swalaah."
Hadiyth – 7
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : أُقِيمَتِ الصَّلاَةُ فَأقْبَلَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم بِوَجْهِهِ ، فَقَالَ : (( أقِيمُوا صُفُوفَكُمْ وَتَرَاصُّوا ؛ فَإنِّي أرَاكُمْ مِنْ وَرَاءِ ظَهْرِي )) رواه البُخَارِيُّ بلفظه ، ومسلم بمعناه .
وفي رواية للبخاري: وَكَانَ أَحَدُنَا يُلْزِقُ مَنْكِبَهُ بِمَنْكِبِ صَاحِبِهِ وَقَدَمَهُ بِقَدَمِهِ.
Na kutoka kwake Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: "Siku moja palikuwa pamekimiwa, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akageuka akatukabili, akasema: "Nyoosheni safu zenu, najipangeni kwani ninawaona nyuma ya mgongo wangu." [Al-Bukhaariy kwa lafdhi hiyo na Muslim kwa maana yake.
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: "Kila moja wetu alikuwa akiambatanisha bega la mwenziwe aliye karibu naye, na hivyo hivyo mguu wake na wa mwenziwe katika safu."
Hadiyth – 8
وعن النعمان بن بشير رضي الله عنهما ، قَالَ : سمعت رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( لَتُسَوُّنَّ صُفُوفَكُمْ ، أوْ لَيُخَالِفَنَّ اللَّهُ بَيْنَ وُجُوهِكُمْ )) متفقٌ عَلَيهِ .
وفي رواية لمسلم : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُسَوِّي صُفُوفَنَا ، حَتَّى كَأنَّمَا يُسَوِّي بِهَا القِدَاحَ حَتَّى رَأى أنَّا قَدْ عَقَلْنَا عَنْهُ ، ثُمَّ خَرَجَ يَوماً فَقَامَ حَتَّى كَادَ يُكَبِّرُ ، فَرَأى رَجُلاً بَادِياً صَدْرُهُ مِنَ الصَّفِّ ، فَقَالَ : (( عِبَادَ اللهِ ، لتُسَوُّنَّ صُفُوفَكُمْ ، أو لَيُخَالِفَنَّ اللهُ بَيْنَ وُجُوهِكُمْ )) .
An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Pangeni safu zenu, au sivyo Allaah Atabadilisha nyuso zenu (yaani kuwaingisha baina yenu uadui, bughudha na khitilafu ya mioyo yenu) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akipanga safu zetu kama kwamba anapanga mishale katika ala, mpaka akatuona tumemfahamu. Akatoka siku moja na kusimama mpaka akakaribia kupiga takbira ya kwanza ya Swalaah, hapo akamuona mtu ametoa kifua chake nje ya safu, akasema: 'Enyi waja wa Allaah! WaLlaahi zipangeni safu zenu sawa, au kama sivyo Allaah Atazibadilisha nyuso zenu (kuwa za wanyama)."
Hadiyth – 9
وعن البراءِ بن عازِبٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم يَتَخَلَّلُ الصَّفَّ مِنْ نَاحِيَةٍ إلى نَاحِيَةٍ ، يَمْسَحُ صُدُورَنَا وَمَنَاكِبَنَا ، وَيَقُولُ : (( لا تَخْتَلِفُوا فَتَخْتَلِفَ قُلُوبُكُمْ )) وكانَ يَقُولُ : (( إنَّ اللهَ وَمَلائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى الصُّفُوفِ الأُوَلِ )) رواه أبُو دَاوُدَ بإسناد حسن .
Na kutoka kwa Al-Baraa' bin 'Aazib (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akipita kati ya safu toka mwanzo mpaka mwisho kuzinyoosha huku akisema: "Msizipindishe safu zenu ili Allaah Asizipindishe nyoyo zenu mkawa mmoja dhidi ya mwengine." Na alikuwa akisema: "Hakika Allaah na Malaaika Wake wanamimina baraka Zao juu ya safu ya mwanzo." [Abuu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Hadiyth – 10
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أقيمُوا الصُّفُوفَ ، وَحَاذُوا بَيْنَ المَنَاكِبِ ، وَسُدُّوا الخَلَلَ ، وَلِينوا بِأيْدِي إخْوانِكُمْ ، ولاَ تَذَرُوا فُرُجَاتٍ للشَّيْطَانِ ، وَمَنْ وَصَلَ صَفّاً وَصَلَهُ اللهُ ، وَمَنْ قَطَعَ صَفّاً قَطَعَهُ اللهُ )) رواه أبُو دَاوُدَ بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nyoosheni safu zenu na mlinganishe mabega yenu na jazeni mapengo (nafasi) katika safu zenu na kuweni wapole na wema kwa ndugu zenu na wala msiache mapengo kwa shetani. Na Allaah humkamilishia yake anayekamilisha safu na asiyekamilisha safu Allaah Hamkamilishii yake." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh]
Hadiyth – 11
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عَنهُ : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( رُصُّوا صُفُوفَكُمْ ، وَقَارِبُوا بَيْنَهَا ، وَحَاذُوا بِالأعْنَاقِ ؛ فَوَالَّذِي نَفْسِي بِيَدِهِ إنِّي لأَرَى الشَّيْطَانَ يَدْخُلُ مِنْ خَلَلِ الصَّفِّ ، كَأَنَّهَا الحَذَفُ )) حديث صحيح رَوَاهُ أبُو دَاوُدَ بإسنادٍ عَلَى شرط مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nyoosheni safu zenu, na karibianeni baina yake, na linganisheni shingo zenu. Naapa kwa ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake kwani mimi namuona shetani anajipenyeza penyeza kwenye safu kama kwamba ni vitoto vya kondoo." [Hadiyth Swahiyh iliyopokewa na Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyoafikiana na sharti zilizowekwa na Muslim]
Hadiyth – 12
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عَنهُ : أنَّ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أتِمُّوا الصَّفَّ المُقَدَّمَ ، ثُمَّ الَّذِي يَلِيهِ ، فَمَا كَانَ مِنْ نَقْصٍ فَلْيَكُنْ في الصَّفِّ المُؤَخَّرِ )) رواه أبُو دَاوُدَ بإسناد حسن .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kamilisheni safu ya mwanzo kisha inayofuata na kama kuna upungufu basi uwe tu katika safu ya mwisho." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Hadiyth – 13
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ اللهَ وَمَلاَئِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى مَيَامِنِ الصُّفُوفِ )) رواه أبُو دَاوُدَ بإسنادٍ عَلَى شرط مسلم ، وفيه رجل مُخْتَلَفٌ في تَوثِيقِهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Allaah na Malaaika Zake wanawarehemu watu wanaoswali kuliani mwa safu." [Abu Daawuwd kwa Isnaad na sharti ya Muslim, na katika wapokezi yupo mtu ambaye wametafautiana wanazuoni juu ya uaminifu wake].
Hadiyth – 14
وعن البراء رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : كُنَّا إذَا صَلَّيْنَا خَلْفَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم أحْبَبْنَا أنْ نَكُونَ عَنْ يَمِينهِ ، يُقْبِلُ عَلَيْنَا بِوَجْهِهِ ، فَسَمِعْتُهُ يَقُولُ : (( رَبِّ قِني عَذَابَكَ يَوْمَ تَبْعَثُ - أو تَجْمَعُ - عِبَادَكَ )) رواه مُسلِمٌ .
Na Al-Baraa (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa tunaswali nyuma ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tunapenda kuwa upande wake wa kulia, anatuelekea kwa uso wake, anasema: "Rabb wangu niepushe adhabu Yako siku utakayofufua au Utakayokusanya waja Wako." [Muslim]
Hadiyth – 15
وعن أبي هريرة رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ: قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( وَسِّطُوا الإمَامَ ، وَسُدُّوا الخَلَلَ )) رواه أبُو دَاوُد .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mfanyeni Imamu awe katikati na jazeni mapengo." [Abuu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل السنن الراتبة مع الفرائض
وبيان أقلها وأكملها وما بينهما
16-Mlango Wa Fadhila za Swalaah za Sunnah Rawatib Pamoja na Faradhi na Kubainisha Uchache na Utimilifu Wake na Zilizo Baina Yake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أُمِّ المُؤْمِنِينَ أُمِّ حَبِيبَةَ رملة بِنْتِ أبي سُفْيَانَ رَضِيَ اللهُ عَنهما ، قالت : سمعت رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( مَا مِنْ عَبْدٍ مُسْلِمٍ يُصَلِّي للهِ تَعَالى كُلَّ يَوْمٍ ثِنْتَيْ عَشرَةَ رَكْعَةً تَطَوُّعاً غَيرَ الفَرِيضَةِ ، إلاَّ بَنَى الله لَهُ بَيْتاً في الجَنَّةِ ، أو إلاَّ بُنِيَ لَهُ بَيْتٌ فِي الجَنَّةِ )) رواه مُسلِمٌ .
Imepokewa kutoka kwa Mama wa Waumini, Ummu Habibah Ramlah bint Abu Sufyaan (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakuna mja Muislamu ataswali kwa ajili ya Allaah Ta'aalaa kila siku Rakaa kumi na mbili za nyongeza (kwa hiyari yake) zisizokuwa za faradhi isipokuwa Allaah Humjengea nyumba Peponi au ila hujengewa yeye nyumba Peponi." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ، وَرَكْعَتْينِ بَعْدَهَا، وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَ الجُمُعَةِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ المَغْرِبِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ العِشَاءِ . متفقٌ عَلَيهِ
Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Adhuhuri, na Rak'ah mbili baada yake, Rak'ah mbili baada ya Ijumaa, na Rak'ah mbili baada ya Maghrib na Rak'ah mbili baada ya Isha." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 3
وعن عبد الله بن مُغَفَّلٍ رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كل أذانين صلاة )) قال في الثَّالِثةِ : (( لِمَنْ شَاءَ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mughaffal kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah (makusudio ya adhana mbili ni baina ya adhana na iqamah), baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah, baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah." Akasema katika mara ya tatu: "Kwa mwenye kupenda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تأكيد ركعتي سنّةِ الصبح
17-Mlango Wa Kuhimiza Rak'ah Mbili za Sunnah ya Asubuhi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لا يَدَعُ أرْبَعاً قَبْلَ الظُّهْرِ ، وَرَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الغَدَاةِ . رَوَاهُ البُخَارِيُّ .
Amehadithia 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa haachi Rakaa nne kabla ya Adhuhuri na Rak'ah mbili kabla ya Asubuhi." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : لَمْ يَكُنِ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَى شَيْءٍ مِنَ النَّوَافِلِ أشَدَّ تَعَاهُدَاً مِنهُ عَلَى رَكْعَتَي الفَجْرِ . متفقٌ عَلَيهِ .
Na amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakuwa mwenye kuchunga Swalaah za Nawaafil na kuhimiza sana kuichunga, kuliko Rak'ah mbili za Sunnah ya Swalatul Fajr." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( رَكْعَتَا الفَجْرِ خَيْرٌ مِنَ الدنْيَا وَمَا فِيهَا )) رواه مُسلِمٌ . وفي رواية : (( لَهُمَا أحَبُّ إليَّ مِنَ الدنْيَا جَمِيعاً )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Rakaa mbili za Alfajiri ni bora kuliko dunia na vilivyomo ndani yake." [Muslim]
Na katika riwaayah nyingine: "Rakaa mbili hizo zinapendeza zaidi kwangu kuliko dunia yote."
Hadiyth – 4
وعن أبي عبد الله بلالِ بن رَبَاح رَضِيَ اللهُ عَنه ، مُؤَذِّن رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم : أنَّهُ أتَى رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، لِيُؤْذِنَه بِصَلاةِ الغَدَاةِ ، فَشَغَلَتْ عَائِشَةُ بِلالاً بِأَمْرٍ سَأَلَتْهُ عَنْهُ ، حَتَّى أصْبَحَ جِدّاً، فَقَامَ بِلالٌ فَآذَنَهُ بِالصَّلاَةِ، وَتَابَعَ أذَانَهُ ، فَلَمْ يَخْرُجْ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، فَلَمَّا خَرَجَ صَلَّى بِالنَّاسِ ، فَأخْبَرَهُ أنَّ عَائِشَةَ شَغَلَتْهُ بِأمْرٍ سَأَلَتْهُ عَنْهُ حَتَّى أصْبَحَ جِدّاً ، وَأنَّهُ أبْطَأَ عَلَيْهِ بِالخُرُوجِ ، فَقَالَ - يَعْنِي النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم - : (( إنِّي كُنْتُ رَكَعْتُ رَكْعْتَي الفَجْرِ )) فقالَ : يَا رَسُولَ اللهِ ، إنَّكَ أصْبَحْتَ جِدّاً ؟ فقَالَ : (( لَوْ أصْبَحْتُ أكْثَرَ مِمَّا أصْبَحْتُ ، لَرَكَعْتُهُمَا ، وَأحْسَنْتُهُمَا وَأجْمَلْتُهُمَا )) رواه أبُو دَاوُدَ بإسناد حسن .
Abu 'Abdillaah Bilaal bin Rabaah (Radhwiya Allaahu 'anhu), amesema kuwa siku moja muadhini wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ili kumfahamisha kuwa Swalaah ya Asubuhi imefika lakini 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa), alimshughulisha Bilaal kwa jambo alilomuuliza mpaka ikawa asubuhi sana. Ulipoanza kutoka mwangaza Bilaal aliinuka na kumjulisha Rasuli wa Allaah kuwa jamaa iko tayari na kumkumbusha lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakutoka. Alipotoka aliwaswalisha watu. Kisha Bilaal alimuuliza ilikuwaje mpaka akashughulishwa na swali kutoka kwa 'Aaishah jambo ambalo lilimfanya kuchelewa kumuarifu kuhusu kufika kwa wakati Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka kukawa asubuhi sana pamoja na kutokea kwa mwangaza, naye (Nabiy Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akachukua muda kutoka nje (ya chumba chake). Akasema (yaani) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) : "Hakika nilikuwa nikiswali Rak'ah mbili za Alfajiri." Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hakika umepambazukiwa sana." Akasema: "Lau kungepambazuka zaidi ya hivi ningeswali Rak'ah hizo mbili vyema na vizuri zaidi." [Abuu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تخفيف ركعتي الفجر
وبيان مَا يقرأ فيهما وبيان وقتهما
18-Mlango Wa Kufanya Nyepesi Rak'ah Mbili za Alfajiri na Kubainisha Kinachosomwa na Wakati Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصَلّي رَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ بَيْنَ النِّدَاءِ وَالإقَامَةِ مِنْ صَلاَةِ الصُّبْحِ . متفقٌ عَلَيهِ .
وفي روايَةٍ لَهُمَا : يُصَلِّي رَكْعَتَي الفَجْرِ ، فَيُخَفِّفُهُمَا حَتَّى أقُولَ : هَلْ قَرَأَ فِيهما بِأُمِّ القُرْآنِ .
وفي رواية لمسلم : كَانَ يُصلِّي رَكْعَتَي الفَجْرِ إذَا سَمِعَ الأذَانَ وَيُخَفِّفُهُمَا .
وفي رواية : إذَا طَلَعَ الفَجْرُ .
Kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anaswali Rak'ah mbili nyepesi kati ya adhana na Iqamah ya Swallaah ya Asubuhi." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Na katika riwaayah nyingine: "Alikuwa akiswali Rakaa mbili za Alfajiri anaposikia adhana kwa kuzifanya nyepesi mpaka nikawa ninasema: "Je, amesoma katika hizo Rak'ah mbili Suwratil Faatihah."
Katika riwaayah ya Muslim: "Alikuwa akiswali Rakaa mbili za Alfajiri anaposikia adhana na kuzifanya nyepesi."
Na katika riwaayah nyingine: "Alfajiri inapochomoza."
Hadiyth – 2
وعن حفصة رَضِيَ اللهُ عَنها : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ إذَا أذَّنَ المُؤَذِّنُ لِلْصُّبْحِ وَبَدَا الصُّبْحُ ، صَلَّى رَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ . متفقٌ عَلَيهِ .
وفي رواية لمسلم : كَانَ رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم ، إذَا طَلَعَ الفَجْرُ لا يُصَلِّي إلاَّ رَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ .
Imepokewa kutoka kwake Hafswah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa wakati muadhini anapokuwa tayari ameadhini adhana ya Swalaah ya Asubuhi, na Asubuhi ikabainika, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Rak'ah mbili nyepesi kabla Swalaah haijaqimiwa." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]
Na katika riwaayah ya Muslim: "Rasuli wa Allaah Alikuwa unapotokea mwangaza akiswali Rak'ah mbili za Sunnah nyepesi wala haswali nyingine."
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي مِنَ اللَّيْلِ مَثْنَى مَثْنَى ، وَيُوتِرُ بِرَكْعَةٍ مِنْ آخِرِ اللَّيْلِ ، وَيُصَلِّي الرَّكْعَتَيْنِ قَبْلَ صلاةِ الغَدَاةِ ، وَكَأنَّ الأَذَانَ بِأُذُنَيْهِ . متفقٌ عَلَيهِ .
Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Swalaah za usiku Rakaa mbili mbili na Rak'ah moja ya witri mwisho wa usiku. Na alikuwa akiswali Rakaa mbili kabla ya Swalaah ya Asubuhi na kama kwamba Iqamah iko katika masikio yake (kwa ukaribu wa Swalaah yake na Iqamah). [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai].
Hadiyth – 4
وعن ابن عباسٍ رضي الله عنهما : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَقْرَأُ في رَكْعَتَي الفَجْرِ في الأُولَى مِنْهُمَا : [ قُولُوا آمَنَّا بِاللهِ وَمَا أُنْزِلَ إِلَيْنَا ] الآية الَّتي في البقرة ، وفي الآخِرَةِ مِنْهُمَا : [ آمَنَّا بِاللهِ وَاشْهَدْ بِأنَّا مُسْلِمُونَ ] .
وفي رواية : وفي الآخِرَةِ الَّتي في آل عِمْران : [ تَعَالَوْا إلَى كَلِمَةٍ سَوَاءٍ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمْ ] رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisoma katika Rak'ah mbili za Alfajiri, ya kwanza: "Semeni: Tumemwamini Allaah na yaliyoteremshwa kwetu" [Al-Baqarah: 136], na katika ya mwisho (yaani Rak'ah): "Tumemwamini Allaah, na shuhudia kwamba sisi ni Waislamu (wenye kujisalimisha Kwake). [Aal-'Imraan: 52].
Na katika riwaayah ya Muslim: "Katika Rak'ah ya mwisho alikuwa akisoma aya ambayo iko katika Aal-'Imraan: 'Njooni katika neno lililo sawa baina yetu na baina yenu,'" [Muslim].
Hadiyth – 5
وعن أبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم قرأ في رَكْعَتَي الفَجْرِ: [ قُلْ يَا أَيُّهَا الكَافِرُونَ ] وَ[ قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ] رَوَاهُ مُسلِمٌ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisoma katika Rak'ah mbili za Sunnah ya Alfajiri: "Sema: Enyi makafiri!" [Al-Kaafiruwn] na "Sema: Yeye Allaah Ni Mmoja Pekee. [Al-Ikhlaasw]." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : رَمَقْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، شَهْراً فَكَانَ يَقْرَأُ في الرَّكْعَتَيْنِ قَبْلَ الفَجْرِ : [ قُلْ يَا أيُّهَا الْكَافِرُونَ ] وَ[ قُلْ هُوَ اللهُ أَحَدٌ ] رَوَاهُ التِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )) .
Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nilimchunguza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mwezi mzima alikuwa anasoma katika Rak'ah mbili kabla ya Alfajiri: "Sema: Enyi makafiri!" [Al-Kaafiruwn] na "Sema: Yeye Allaah Ni Mmoja Pekee. [Al-Ikhlaasw]." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب الاضطجاع بعد ركعتي الفجرعَلَى جنبه الأيمن والحث عليه
سواءٌ كَانَ تَهَجَّدَ بِاللَّيْلِ أمْ لا
19-Mlango Wa Kupendeza Kujilaza Baada ya Rak'ah Mbili za Alfajiri kwa Ubavu Wake wa Kulia na Kuhimizwa Sawa Ikiwa ni Tahajjud Au La
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم إذَا صَلَّى ركعتي الفجر ، اضْطَجَعَ عَلَى شِقِّهِ الأَيْمَن . رَوَاهُ البُخَارِي .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapomaliza kuswali Rakaa mbili za Alfajiri akijilaza kwa ubavu wake wa kulia." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي فِيمَا بَيْنَ أنْ يَفْرُغَ مِنْ صَلاَةِ العِشَاءِ إلَى الفَجْرِ إحْدَى عَشرَةَ رَكْعَةً ، يُسَلِّمُ بَيْنَ كُلِّ رَكْعَتَيْنِ ، وَيُوتِرُ بِوَاحِدَةٍ ، فَإذَا سَكَتَ المُؤَذِّنُ مِنْ صَلاَةِ الفَجْرِ ، وَتَبَيَّنَ لَهُ الفَجْرُ ، وَجَاءهُ المُؤَذِّنُ ، قَامَ فَرَكَعَ رَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَينِ ، ثُمَّ اضْطَجَعَ عَلَى شِقِّهِ الأَيْمَنِ ، هكَذَا حَتَّى يأْتِيَهُ المُؤَذِّنُ لِلإِقَامَةِ . رَوَاهُ مُسلِم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Rakaa kumi na moja baina ya Swalaah ya Isha na Swalaah ya Alfajiri akitoa salamu baada ya kila Rakaa mbili, na anaswali rakaa moja witri. Muadhini anapomaliza kuadhini adhana ya Swalaah ya Alfajiri, na mwangaza kutokeza, muadhini anakuja. Anasimama kuswali Rakaa mbili hafifu, kisha akijilaza kwa ubavu wake wa kulia, hivi hadi muadhini anapomjia kukimu." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أبي هريرة رَضِيَ اللهُ عَنه ، قَالَ : قال رَسُول اللَّهِ صلى الله عليه وسلم : (( إذا صَلَّى أحَدُكُمْ رَكْعَتَي الفَجْرِ ، فَلْيَضْطَجِعْ عَلَى يَمِينِهِ )) رواه أبُو دَاوُدَ وَالتِّرمِذِيُّ بأسانيد صحيحة ، قال الترمذي : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anaposwali mmoja wenu Rak'ah mbili za Sunnah ya Alfajiri ajilaze kwa ubavu wake wa kulia." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy kwa Isnaad zilizo Swahiyh. Na akasema At-Tirmidhiy kuwa hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب سنة الظهر
20-Mlango Wa Sunnah ya Adhuhuri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَهَا . متفقٌ عَلَيهِ .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Swalaah ya Adhuhuri na Rak'ah mbili baada yake." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لا يَدَعُ أرْبَعاً قَبْلَ الظُّهْرِ . رَوَاهُ البُخَارِيُّ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa haachi rakaa nne kabla ya Adhuhuri." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : كَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي في بَيْتِي قَبْلَ الظُّهْرِ أرْبَعاً ، ثُمَّ يَخْرُجُ ، فَيُصَلِّي بِالنَّاسِ ، ثُمَّ يَدْخُلُ فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ . وَكَانَ يُصَلِّي بِالنَّاسِ المَغْرِبَ ، ثُمَّ يَدْخُلُ فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ ، وَيُصَلِّي بِالنَّاسِ العِشَاءِ ، وَيَدْخُلُ بَيتِي فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ . رَوَاهُ مُسلِم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiswali nyumbani kwangu Rak'ah nne kabla ya Adhuhuri, kisha anatoka kuwaswalisha watu kisha anarudi na kuswali Rak'ah mbili. Na alikuwa akiwaswalisha watu Swalaah ya Magharib, kisha anaingia (nyumbani kwangu) na kuswali Rakaa mbili. Na alikuwa anawaswalisha watu Swalaah ya Ishaa na anaingia nyumbani kwangu na kuswali Rakaa mbili." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أُمّ حَبِيبَةَ رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : قال رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ حَافَظَ عَلَى أرْبَعِ رَكَعَاتٍ قَبْلَ الظُّهْرِ ، وَأرْبَعٍ بَعْدَهَا ، حَرَّمَهُ اللَّهُ عَلَى النَّارِ )) رواه أبُو دَاوُدَ وَالتِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Ummu Habibah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuzihifadhi (kuzichunga kwa kuswali) Rak'ah nne kabla ya Adhuhuri na nne baada yake, Allaah atamharamisha Moto." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 5
وعن عبد الله بن السائب رَضِيَ اللهُ عَنه : أنَّ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصَلِّي أرْبَعاً بَعْدَ أنْ تَزُولَ الشَّمْسُ قَبْلَ الظُّهْرِ ، وقَالَ : (( إنَّهَا سَاعَةٌ تُفْتَحُ فِيها أبْوَابُ السَّمَاءِ ، فَأُحِبُّ أنْ يَصْعَدَ لِي فيهَا عَمَلٌ صَالِحٌ )) رواه التِّرمِذِيُّ، وَقَالَ: (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin As-Saa'ib (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Rak'ah nne baada ya jua kuzama na kabla ya Adhuhuri na akasema: "Hakika huo ni wakati ambao milango ya mbinguni hufunguliwa, hivyo napenda amali yangu njema iwe inapanda (mbinguni) wakati huo." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 6
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إذا لَمْ يُصَلِّ أربَعاً قَبلَ الظُّهْرِ ، صَلاَّهُنَّ بَعْدَهَا . رَوَاهُ التِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah(Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapokosa kuswali Rak'ah nne kabla ya Adhuhuri ya alikuwa akiswali baada yake (yaani baada ya Swalaah ya Adhuhuri) ." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب سنة العصر
21-Mlango Wa Sunnah za Alasiri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن علي بن أبي طالب رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي قَبْلَ العَصْرِ أرْبَعَ رَكَعَاتٍ ، يَفْصلُ بَيْنَهُنَّ بِالتَّسْلِيمِ عَلَى المَلائِكَةِ المُقَرَّبِينَ ، وَمَنْ تَبِعَهُمْ مِنَ المُسْلِمِينَ وَالمُؤْمِنِينَ . رَوَاهُ التِّرمِذِيُّ ، وَقَالَ : (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )) .
Kutoka kwake Ali bin Abu Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali kabla ya Alasiri Rak'ah nne anazipambanua baina yake kwa salamu kwa Malaaika walio karibu naye na wale waliomfuata miongoni mwa Waislamu na Waumini." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
عن ابن عمر رَضِيَ اللَّهُ عَنهُما ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( رَحِمَ اللَّهُ امْرءاً صَلَّى قَبْلَ العَصْرِ أرْبَعاً )) رواه أبُو دَاوُدَ وَالتِّرمِذِيُّ، وَقَالَ: (( حَدِيثٌ حَسَنٌ )).
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah humrehemu mtu aliyeswali Rak'ah nne kabla ya Alasiri." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 3
وعن علي بن أبي طالب رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصَلِّي قَبلَ العَصْرِ رَكْعَتَيْنِ . رَوَاهُ أبُو دَاوُدَ بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa 'Ali bin Abu Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Rak'ah mbili kabla ya Alasiri." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Swahiyh].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب سنة المغرب بعدها وقبلها
22-Mlango Wa Swalaah ya Sunnah Kabla na Baada ya Maghrib
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ، وَرَكْعَتْينِ بَعْدَهَا، وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَ الجُمُعَةِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ المَغْرِبِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ العِشَاءِ . متفقٌ عَلَيهِ
Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Adhuhuri, na Rak'ah mbili baada yake, Rak'ah mbili baada ya Ijumaa, na Rak'ah mbili baada ya Maghrib na Rak'ah mbili baada ya Isha." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عَنها ، قالت : كَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي في بَيْتِي قَبْلَ الظُّهْرِ أرْبَعاً ، ثُمَّ يَخْرُجُ ، فَيُصَلِّي بِالنَّاسِ ، ثُمَّ يَدْخُلُ فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ . وَكَانَ يُصَلِّي بِالنَّاسِ المَغْرِبَ ، ثُمَّ يَدْخُلُ فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ ، وَيُصَلِّي بِالنَّاسِ العِشَاءِ ، وَيَدْخُلُ بَيتِي فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ . رَوَاهُ مُسلِم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Alikuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akiswali nyumbani kwangu Rak'ah nne kabla ya Adhuhuri, kisha anatoka kuwaswalisha watu kisha anarudi na kuswali Rak'ah mbili. Na alikuwa akiwaswalisha watu Swalaah ya Magharib, kisha anaingia (nyumbani kwangu) na kuswali Rakaa mbili. Na alikuwa anawaswalisha watu Swalaah ya Ishaa na anaingia nyumbani kwangu na kuswali Rakaa mbili." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عبد الله بن مُغَفَّل رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلُّوا قَبْلَ المَغْرِبِ )) قال في الثَّالِثَةِ : (( لِمَنْ شَاءَ )) رواه البُخَارِيُّ .
'Abdillaah bin Mughaffal amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalini kabla ya Swalaah ya Maghrib." Akasema kwa mara ya tatu: "Kwa anayetaka." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 4
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : لَقَدْ رَأيْتُ كِبَارَ أصْحَابِ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يَبْتَدِرُونَ السَّوَارِيَ عِندَ المَغْرِبِ . رَوَاهُ البُخَارِيُّ .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimewaona wakongwe miongoni mwa Swahaaba wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakikimbilia kwenye nguzo za Msikiti wakati wa Maghrib." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : كُنَّا نصلِّي عَلَى عهدِ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم رَكْعَتَيْنِ بَعْدَ غُرُوبِ الشَّمْسِ قَبْلَ المَغْرِبِ ، فَقِيلَ : أكَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم صَلاَّهما ؟ قَالَ : كَانَ يَرَانَا نُصَلِّيهِمَا فَلَمْ يَأمُرْنَا وَلَمْ يَنْهَنَا . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa tukiswali Rak'ah mbili baada ya kuzama kwa jua kabla ya Maghribi. Akaulizwa: "Je, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliziswali?" Akasema: "Alikuwa akituona tukiziswali naye hakutuamuru wala kutukataza." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أنس رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : كُنَّا بِالمَدِينَةِ فَإذَا أذَّنَ المُؤَذِّنُ لِصَلاَةِ المَغْرِبِ ، ابْتَدَرُوا السَّوَارِيَ ، فَرَكَعُوا رَكْعَتَيْنِ ، حَتَّى إنَّ الرَّجُلَ الغَريبَ لَيَدْخُلُ المَسْجِدَ فَيَحْسَبُ أنَّ الصَّلاَةَ قَدْ صُلِّيَتْ مِنْ كَثْرَةِ مَنْ يُصَلِّيهِمَا . رواه مسلم .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa Madiynah wakati muadhini alipoadhini kwa ajili ya Swalaah ya Maghribi tulikuwa tunafanya haraka kuwahi kwenye nguzo za Msikiti na kuswali Rakaa mbili kiasi ya kwamba mtu mgeni anayeingia Msikitini anadhani Swalaah imemalizika kwa sababu ya watu wengi waliokuwa wakiiswali." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب سنة العشاء بعدها وقبلها
23-Mlango Wa Sunnah Kabla na Baada ya Swalaah ya Ishaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ، وَرَكْعَتْينِ بَعْدَهَا، وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَ الجُمُعَةِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ المَغْرِبِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ العِشَاءِ . متفقٌ عَلَيهِ
Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Adhuhuri, na Rak'ah mbili baada yake, Rak'ah mbili baada ya Ijumaa, na Rak'ah mbili baada ya Maghrib na Rak'ah mbili baada ya Isha." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن عبد الله بن مُغَفَّلٍ رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كل أذانين صلاة )) قال في الثَّالِثةِ : (( لِمَنْ شَاءَ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mughaffal kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah (makusudio ya adhana mbili ni baina ya adhana na iqamah), baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah, baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah." Akasema katika mara ya tatu: "Kwa mwenye kupenda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب سنة الجمعة
24-Mlango Wa Sunnah ya Ijumaa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رَضِيَ اللهُ عَنهُما ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ الظُّهْرِ، وَرَكْعَتْينِ بَعْدَهَا، وَرَكْعَتَيْنِ بَعْدَ الجُمُعَةِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ المَغْرِبِ ، وَرَكْعَتَينِ بَعدَ العِشَاءِ . متفقٌ عَلَيهِ
Na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Niliswali pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Rak'ah mbili kabla ya Adhuhuri, na Rak'ah mbili baada yake, Rak'ah mbili baada ya Ijumaa, na Rak'ah mbili baada ya Maghrib na Rak'ah mbili baada ya Isha." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن عبد الله بن مُغَفَّلٍ رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قال رَسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كُلِّ أذَانَيْنِ صَلاَةٌ ، بَيْنَ كل أذانين صلاة )) قال في الثَّالِثةِ : (( لِمَنْ شَاءَ )) متفقٌ عَلَيهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Mughaffal kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah (makusudio ya adhana mbili ni baina ya adhana na iqamah), baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah, baina ya kila adhana mbili kuna Swalaah." Akasema katika mara ya tatu: "Kwa mwenye kupenda." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai].
Hadiyth – 3
عن أَبي هريرة رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا صَلَّى أَحَدُكُم الجُمُعَةَ ، فَلْيُصَلِّ بَعْدَهَا أرْبعاً )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Pindi anaposwali mmoja wenu Swalaah ya Ijumaa, aswali baada yake Rakaa nne." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ لاَ يُصَلِّي بَعْدَ الجُمُعَةِ حَتَّى يَنْصَرِفَ ، فَيُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ في بَيْتِهِ . رواه مسلم .
Amesema Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Hakika Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa haswali baada ya Swalaah ya Ijumaa mpaka aondoke, hivyo huswali Rakaa mbili nyumbani kwake." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب جعل النوافل في البيت
سواء الراتبة وغيرها والأمر بالتحول للنافلة من موضع
الفريضة أَو الفصل بينهما بكلام
25-Mlango Wa Kupendeza Kuswali Sunnah Nyumbani Sawa ni Zile Zilizohimizwa au Nyinginezo na Maagizo ya Kubadilisha Sehemu Uliyoswali Swalaah ya Faradhi au Kupambanua Baina yao kwa Mazungumzo
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن زيد بن ثابت رَضِيَ اللهُ عَنهُ : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلُّوا أَيُّهَا النَّاسُ فِي بُيُوتِكُمْ ، فَإنَّ أفْضَلَ الصَّلاَةِ صَلاَةُ المَرْءِ في بَيْتِهِ إِلاَّ المَكْتُوبَةَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Zayd bin Thaabit (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Enyi watu swalini majumbani mwenu. Hakika Swalaah bora ni ile mtu anayoswali nyumbani kwake isipokuwa Swalaah za faradhi (ndio anayowajibika kuswali Msikitini)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اجْعَلُوا مِنْ صَلاَتِكُمْ فِي بُيُوتِكُمْ ، وَلاَ تَتَّخِذُوهَا قُبُوراً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalini Swalaah zenu majumbani na wala msifanye nyumba zenu kuwa kama makaburi." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن جابر رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا قَضَى أحَدُكُمْ صَلاَتَهُ في مَسْجِدِهِ فَلْيَجْعَلْ لِبَيْتِهِ نَصِيباً مِنْ صَلاَتِهِ ؛ فَإنَّ اللهَ جَاعِلٌ في بَيْتِهِ مِنْ صَلاَتِهِ خَيْراً )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapomaliza mmoja wenu Swalaah yake ya faradhi katika Msikiti, ajaalie nyumbani kwake sehemu ya Swalaah zake (za Sunnah), kwani Allaah atampatia kheri kwenye nyumba kwa sababu hiyo." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن عمر بن عطاءٍ : أنَّ نَافِعَ بْنَ جُبَيْرٍ أرْسَلَهُ إِلَى السَّائِبِ ابن أُخْتِ نَمِرٍ يَسأَلُهُ عَنْ شَيْءٍ رَآهُ مِنْهُ مُعَاوِيَةُ في الصَّلاَةِ ، فَقَالَ : نَعَمْ ، صَلَّيْتُ مَعَهُ الجُمُعَةَ في المَقْصُورَةِ ، فَلَمَّا سَلَّمَ الإمَامُ ، قُمْتُ في مَقَامِي ، فَصَلَّيْتُ ، فَلَمَّا دَخَلَ أَرْسَلَ إلَيَّ ، فَقَالَ: لاَ تَعُدْ لِمَا فَعَلْتَ. إِذَا صَلَّيْتَ الجُمُعَةَ فَلاَ تَصِلْهَا بِصَلاةٍ حَتَّى تَتَكَلَّمَ أَوْ تَخْرُجَ ؛ فَإنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم أمَرَنَا بِذلِكَ ، أن لاَ نُوصِلَ صَلاَةً بِصَلاَةٍ حَتَّى نَتَكَلَّمَ أَوْ نَخْرُجَ . رواه مسلم .
'Umar bin 'Atwaa' Amesema: Naafi' bin Jubayr alimtuma kwa Saa'ib mtoto wa dada wa Namir alichoona kwake katika Swalaah. Akasema: "Ndio niliswali pamoja nye Ijumaa katika sehemu ya Msikiti iliyofungwa. Alipotoa salamu imamu nilisimama katika sehemu niliyoswali, (Sunnah). Alipotoka Msikitini alinitumia mtu, akasema: 'Usirudie tena ulichofanya, unaposwali Ijumaa, usiswali Swalaah nyingine mpaka uzungumze au utoke. Kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuamuru hilo, tusiunganishe Swalaah kwa Swalaah mpaka tuzungumze au tutoke." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الحث عَلَى صلاة الوتر وبيان أنه سنة مؤكدة وبيان وقته
26-Mlango Wa Kuhimiza Kuswali Witri na Kubainisha Kuwa Hiyo ni Sunnah Muakkadah na Kubainisha Wakati Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن عليٍّ رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : الوِتْرُ لَيْسَ بِحَتْمٍ كَصَلاَةِ المَكْتُوبَةِ ، وَلَكِنْ سَنَّ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ اللهَ وِتْرٌ يُحِبُّ الوِتْرَ ، فَأَوْتِرُوا يَا أهْلَ القُرْآنِ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
'Ali (Radhwiya Allaahu 'anhu) Amesema: Witri si lazima kama ilivyo Swalaah ya faradhi lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliiweka Sunnah hii, kwa kusema: "Hakika Allaah ni Witri (yaani mmoja pekee), na Anapenda Witri, basi Swalini Witri enyi watu wa Qur-aan." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مِنْ كُلِّ اللَّيْلِ قَدْ أَوْتَرَ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، مِنْ أَوَّلِ اللَّيْلِ، وَمِنْ أوْسَطِهِ، وَمِنْ آخِرِهِ، وَانْتَهَى وِتْرُهُ إِلَى السَّحَرِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali witri muda wote wa usiku: mwanzo wake, katika ya usiku na mwisho wake ambapo witri yake alikuwa akiimaliza inapofika Alfajiri." [Al-Bukaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( اجْعَلُوا آخِرَ صَلاَتِكُمْ بِاللَّيْلِ وِتْراً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ifanyeni Swalaah yenu ya mwisho katika usiku kuwa ni witri." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Hadiyth – 4
وعن أَبي سعيد الخدري رَضِيَ اللهُ عَنهُ : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أوْتِرُوا قَبْلَ أنْ تُصْبِحُوا )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalini witri kabla ya asubuhi." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن عائشة رضي الله عنها: أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصَلِّي صَلاَتَهُ باللَّيْلِ ، وَهِيَ مُعْتَرِضَةٌ بَيْنَ يَدَيْهِ ، فَإذَا بَقِيَ الوِتْرُ ، أيْقَظَهَا فَأوْتَرتْ . رواه مسلم .
وفي روايةٍ لَهُ : فَإذَا بَقِيَ الوِتْرُ ، قَالَ : (( قُومِي فَأوتِري يَا عائِشَةُ )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Swalaah zake za usiku akiwa yeye amelala mbele yake (karibu naye). Inapobakia witri alikuwa anamuamsha, nami naswali witri." [Muslim]
Na katika riwaayah yake: Inapobakia witri alisema: "Amka uswali witri, ee 'Aaishah."
Hadiyth – 6
وعن ابن عمرَ رضي الله عنهما : أنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بَادِرُوا الصُّبْحَ بِالوِتْرِ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Shindaneni kuswali witri asubuhi." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن جابر رَضِيَ اللهُ عَنهُ ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ خَافَ أنْ لاَ يَقُومَ مِنْ آخِرِ اللَّيْلِ ، فَلْيُوتِرْ أوَّلَهُ ، وَمَنْ طَمِعَ أنْ يَقُومَ آخِرَهُ فَلْيُوتِرْ آخِرَ اللَّيلِ ، فَإنَّ صَلاَةَ آخِرِ اللَّيْلِ مَشْهُودَةٌ ، وذَلِكَ أفْضَلُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuhofia kuwa hataamka mwisho wa usiku, aswali waitri mwanzoni. Na mwenye tamaa ya kuswali Swalaah ya usiku basi aswali mwisho, kwani Swalaah ya mwishoni mwa mwisho wa usiku inashuhudiwa (na Malaaika) na hiyo ni bora zaidi." [Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل صلاة الضحى
وبيان أقلها وأكثرها وأوسطها ، والحث عَلَى المحافظة عَلَيْهَا
27-Mlango Wa Ubora wa Swalaah ya Dhuwhaa na Kubainisha Uchache, Wingi, Wastani Wake na Kuhimizwa katika Kuihifadhi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أوْصَانِي خَلِيلي صلى الله عليه وسلم بِصِيَامِ ثَلاَثَةِ أيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ، وَرَكْعَتَي الضُّحَى ، وَأنْ أُوتِرَ قَبْلَ أنْ أرْقُدَ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Mpenzi wangu Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameniusia vitu vitatu, nisiviache mpaka ninakufa: "Kufunga siku tatu kila mwezi, kuswali Swalaah ya Dhuwhaa na kulala baada ya witri." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai]. Witri kabla ya kulala inapendeza kwa yule mwenye shaka ya kuamka mwisho wa usiku. Akiwa ana imani kuwa ataamka basi kuiswali mwisho wa usiku ni bora.
Hadiyth – 2
وعن أَبي ذَرٍّ رضي اللهُ عنه ، عن النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يُصْبحُ عَلَى كُلِّ سُلاَمَى مِنْ أَحَدكُمْ صَدَقَةٌ : فَكُلُّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقَةٌ ، وَكُلُّ تَحْمِيدَةٍ صَدَقَةٌ ، وَكُلُّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةٌ ، وَكُلُّ تَكْبِيرَةٍ صَدَقَةٌ ، وَأَمْرٌ بِالمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ ، وَنَهْيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقَةٌ ، وَيُجْزِىء مِنْ ذَلِكَ رَكْعَتَانِ يَرْكَعُهُمَا مِن الضُّحَى )) رواه مسلم .
Kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) ya kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kila kiungo cha mmoja wenu kinapambazukiwa kwa kufanya swadaqah (jambo jema). Hivyo kila tasbiyh (ni kusema Subhaana Allaah, yaani Allaah ameepukana na kila aina ya upungufu) ni swadaqah, na kila tahmiyd (ni kusema AlhamduliLLaah, yaani kila jinsi ya sifa njema ni za Allaah) ni swadaqah, na kila takbiyr (ni kusema Allaahu Akbar, yaani Allaah ni Mkubwa kuliko wote) ni swadaqah na kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza mabaya ni swadaqah. Na rakaa mbili za Swalaah ya Dhuwhaa unazoswali zatosheleza (kama swadaqah ya yote haya)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي الضُّحَى أرْبَعاً ، وَيَزِيدُ مَا شَاءَ الله . رواه مسلم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Rak'ah nne za Dhuwhaa na akizidisha kama anavyopenda Allaah." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أُمِّ هَانِىءٍ فاختة بنت أَبي طالب رضي الله عنها ، قالت : ذَهَبْتُ إِلَى رَسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، عَامَ الفَتْحِ فَوَجَدْتُهُ يَغْتَسِلُ ، فَلَمَّا فَرَغَ مِنْ غُسْلِهِ ، صَلَّى ثَمَانِيَ رَكَعَاتٍ، وَذَلِكَ ضُحىً. متفقٌ عَلَيْهِ . وهذا مختصرُ لفظِ إحدى روايات مسلم.
Kutoka kwa Ummu Haani bint Abu Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nilikwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mwaka wa Fathi (siku mji wa Makkah ulipotekwa) nikamkuta anakoga. Alipomaliza kukoga aliswali Rak'ah nane na hiyo ilikuwa ni Dhuwhaa." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تجويز صلاة الضحى من ارتفاع
الشمس إِلَى زوالها والأفضل أن تُصلَّى عِنْدَ
اشتداد الحر وارتفاع الضحى
28-Mlango Wa Kufaa Swalaah ya Dhuwhaa Kuanzia Linaponyanyuka Jua Mpaka Kupinduka (Zawaal), na Bora ni Kuiswali Wakati Jua Linapokuwa Kali
Alhidaaya.com [4]
عن زيد بن أَرْقَم رضي اللهُ عنه : أنَّهُ رَأَى قَوْماً يُصَلُّونَ مِنَ الضُّحَى ، فَقَالَ : أمَا لَقَدْ عَلِمُوا أنَّ الصَّلاَةَ في غَيْرِ هذِهِ السَّاعَةِ أفْضَلُ ، إنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلاَةُ الأَوَّابِينَ حِيْنَ تَرْمَضُ الفِصَالُ )) رواه مسلم .
Zayd bin Arqam (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Aliona watu wanaswali Dhuwhaa, akasema: Ama kwa hakika hawajajua kwamba Swalaah katika wakati mwingine usiokuwa huu ni bora zaidi kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah ya Awwaabiyn (wanaorudi kutoka kwa kughafika wakaja kuhudhuria na kutoka katika dhambi kuelekea kwa tauba na msamaha) ni wakati wa jua kali ambapo watoto wa ngamia hukusanywa." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الحث عَلَى صلاة تحية المسجد بركعتين
وكراهة الجلوس قبل أن يصلي ركعتين في أي وقت دخل
وسواء صلَّى ركعتين بنية التَّحِيَّةِ أَوْ صلاة فريضة أَوْ سنة راتبة أَوْ غيرها
29-Mlango Wa Kuhimizwa Swalaah ya Tahiyyatul Masjid kwa Rak'ah Mbili na Ukaraha wa Kukaa Kabla ya Kuziswali katika Wakati Wowote Anapoingia
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا دَخَلَ أحَدُكُمُ المَسْجِدَ ، فَلاَ يَجْلِسْ حَتَّى يُصَلِّي رَكْعَتَيْنِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qaatadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoingia mmoja wenu Msikitini na aswali Rak'ah mbili kabla hajakaa." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن جابرٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أَتَيْتُ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم وَهُوَ في المَسْجِدِ ، فَقَالَ : (( صَلِّ رَكْعَتَيْنِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) naye alikuwa Msikitini. Akaniambia: "Swali Rakaa mbili." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب ركعتين بعد الوضوء
30-Mlango Wa Kupendeza Kuswali Rak'ah Mbili Baada Wudhuu
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ لِبِلاَلٍ : (( يَا بِلاَلُ ، حَدِّثْنِي بِأَرْجَى عَمَلٍ عَمِلْتَهُ فِي الإسْلاَمِ ، فَإنِّي سَمِعْتُ دَفَّ نَعْلَيْكَ بَيْنَ يَدَيَّ في الجَنَّةِ )) قَالَ : مَا عَمِلْتُ عَمَلاً أرْجَى عِنْدي مِنْ أَنِّي لَمْ أتَطَهَّرْ طُهُوراً فِي سَاعَةٍ مِنْ لَيْلٍ أَوْ نَهَارٍ إِلاَّ صَلَّيْتُ بِذَلِكَ الطُّهُورِ مَا كُتِبَ لِي أنْ أُصَلِّي . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimuuliza Bilaal (Radhwiya Allaahu 'anhu): "Ee Bilaal! Niambie amali uliyoifanya katika Uislamu, kwani mimi nimesikia sauti ya viatu vyako ukiwa mbele yangu Peponi." Akasema: "Sijafanya amali yoyote ambayo kwayo natarajia hayo isipokuwa ninapojitwahirisha katika wakati wowote wa usiku au mchana ila huswali kwa tohara hiyo zile Alizoniandikia Allaah kuziswali." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل يوم الجمعة ووجوبها والاغتسال لَهَا
والطّيب والتبكير إِلَيْهَا والدعاء يوم الجمعة والصلاة
عَلَى النبي صلى الله عليه وسلم وفِيهِ بيان ساعة الإجابة
واستحباب إكثار ذكر الله تعالى بعد الجمعة
31-Mlango Wa Ubora wa Siku ya Ijumaa na Wajibu wa Kuoga Kwayo na Kujipaka Manukato, Kwenda Mapema, Kuomba Dua Siku ya Ijumaa, Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Kubainisha Wakati wa Kujibiwa Dua, Kupendeza Kukithirisha Kumtaja Allaah Baada ya Ijumaa
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
فَإِذَا قُضِيَتِ الصَّلَاةُ فَانتَشِرُوا فِي الْأَرْضِ وَابْتَغُوا مِن فَضْلِ اللَّـهِ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا لَّعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ﴿١٠﴾
Na inapomalizika Swalaah, basi tawanyikeni katika ardhi, na tafuteni Fadhila za Allaah, na mdhukuruni Allaah kwa wingi ili mpate kufaulu. [Al-Jumua'ah: 10]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( خَيْرُ يَومٍ طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ يَوْمُ الجُمُعَةِ : فِيهِ خُلِقَ آدَمُ ، وَفِيهِ أُدْخِلَ الجَنَّةَ ، وَفِيهِ أُخْرِجَ مِنْهَا )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Siku bora ya zilizochomozewa na jua ni siku ya Ijumaa, ndani yake aliumbwa Aadam na ndani yake aliingizwa Peponi na ndani yake alitolewa humo." [Muslim].
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ تَوَضَّأ فَأَحْسَنَ الوُضُوءَ ثُمَّ أتَى الجُمُعَةَ ، فَاسْتَمَعَ وأنْصَتَ ، غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الجُمُعَةِ وَزِيادَةُ ثَلاَثَةِ أيَّامٍ ، وَمَنْ مَسَّ الحَصَى ، فَقَدْ لَغَا )) رواه مسلم .
Na imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote atakayetawadha vizuri, kisha akaja Msikitini kwa ajili ya Swalaah ya Ijumaa. Akasikiliza na akanyamaza (katika kufanya hivyo), atasamehewa madhambi yake kuanzia Ijumaa iliyopita na Ijumaa hii na ziada ya siku tatu. Na yeyote atakayegusa vijiwe na kucheza navyo amefanya upuuzi." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الصَّلَوَاتُ الخَمْسُ ، وَالجُمُعَةُ إِلَى الجُمُعَةِ ، وَرَمَضَانُ إِلَى رَمَضَانَ ، مُكَفِّراتٌ مَا بَيْنَهُنَّ إِذَا اجْتُنِبَتِ الكَبَائِرُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah tano (za faradhi) na Ijumaa mpaka Ijumaa na Ramadhwaan mpaka Ramadhwaan inafuta madhambi yaliyo madogo baina yake ikiwa dhambi kubwa zitaepukwa." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أَبي هريرة ، وعن ابن عمر رضي الله عنهم : أنهما سَمعَا رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقولُ عَلَى أعْوَادِ مِنْبَرِهِ : (( لَيَنْتَهِيَنَّ أقْوَامٌ عَنْ وَدْعِهِمُ الجُمُعَاتِ أَوْ لَيَخْتِمَنَّ اللهُ عَلَى قُلُوبِهِمْ ثُمَّ لَيَكُونَنَّ مِنَ الغَافِلِينَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah na Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhum) kuwa walimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema akiwa juu ya mimbar yake ya mbao: "Watu watakoma kuacha kwao Ijumaa, au Allaah atapiga muhuri mioyo yao, kisha watakuwa miongoni mwa walioghafilika." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا جَاءَ أَحَدُكُمُ الجُمُعَةَ فَلْيَغْتَسِلْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mmoja wenu anapokwenda kwenye Swalaah ya Ijumaa na akoge." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( غُسْلُ يَوْمِ الجُمُعَةِ وَاجِبٌ عَلَى كُلِّ مُحْتَلِمٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ
Abuu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allahu 'anhu) amesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kuoga siku ya Ijumaa ni wajibu kwa kila baleghe." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Hadiyth – 7
وعن سَمُرَةَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ تَوَضَّأَ يَوْمَ الجُمُعَةِ فبِها وَنِعْمَتْ وَمَن اغْتَسَلَ فَالغُسْلُ أفْضَلُ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن ))
Imepokewa kutoka kwa Samurah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kutawadha siku ya Ijumaa, hiyo ni neema (nzuri), na mwenye kuoga ni bora zaidi." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 8
وعن سَلمَان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( لاَ يَغْتَسِلُ رَجُلٌ يَومَ الجُمُعَةِ ، وَيَتَطَهَّرُ مَا اسْتَطَاعَ مِن طُهْرٍ ، وَيَدَّهِنُ مِنْ دُهْنِهِ ، أَوْ يَمَسُّ مِنْ طِيبِ بَيْتِهِ ، ثُمَّ يَخْرُجُ فَلاَ يُفَرِّقُ بَيْنَ اثنَيْنِ ، ثُمَّ يُصَلِّي مَا كُتِبَ لَهُ ، ثُمَّ يُنْصِتُ إِذَا تَكَلَّمَ الإمَامُ ، إِلاَّ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الجُمُعَةِ الأُخْرَى )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Salmaan Al-Faarisiy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Haogi mmoja wenu siku ya Ijumaa na akajitwahirisha kadiri ya uwezo wake na akajitia manukato nyumbani kwake kisha akaenda Msikitini na akawa hapasuwi safu kati ya watu wawili, kisha akaswali kiasi chake, kisha akakaa kimya akimsikiliza Imamu wakati akizungumza (akitoa Khutbah) isipokuwa atasamehewa kuanzia Ijumaa ile mpaka nyingine." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 9
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَن اغْتَسَلَ يَومَ الجُمُعَةِ غُسْلَ الجَنَابَةِ ، ثُمَّ رَاحَ في الساعة الأولى فَكَأنَّمَا قَرَّبَ بَدَنَةً ، وَمَنْ رَاحَ في السَّاعَةِ الثَّانِيَةِ ، فَكَأَنَّمَا قَرَّبَ بَقَرَةً ، وَمَنْ رَاحَ في الساعة الثَّالِثَةِ ، فَكَأنَّمَا قَرَّبَ كَبْشاً أقْرَنَ ، وَمَنْ رَاحَ في السَّاعَةِ الرَّابِعَةِ ، فَكَأنَّمَا قَرَّبَ دَجَاجَةً ، وَمَنْ رَاحَ في السَّاعَةِ الخَامِسَةِ ، فَكَأنَّمَا قَرَّبَ بَيْضَةً ، فَإذَا خَرَجَ الإمَامُ ، حَضَرَتِ المَلاَئِكَةُ يَسْتَمِعُونَ الذِّكْرَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuoga siku ya Ijumaa kama anavyooga janaba kisha akaondoka (kuelekea kwenye Swalaah ya Ijumaa katika saa za mwanzo) basi atakuwa ni kama ametoa ngamia swadaqah. Na atakayekwenda katika saa ya pili basi atakuwa ni kama aliyetoa ng'ombe swadaqah, na atakayeondoka wakati wa saa ya tatu kama ametoa kondoo mwenye pembe swadaqah, na mwenye kuondoka wakati wa saa ya nne kama ametoa kuku swadaqah; na mwenye kuondoka wakati wa saa ya tano kama ametoa yai swadaqah. Na Imamu anapojitokeza kutoa khutbah basi wakati huo Malaaika wanafika kusikiliza khutbah." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 10
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ذَكَرَ يَوْمَ الجُمُعَةِ ، فَقَالَ : (( فِيهَا سَاعَةٌ لا يُوافِقُهَا عَبْدٌ مُسْلِمٌ ، وَهُوَ قَائِمٌ يُصَلِّي يَسْألُ اللهَ شَيْئاً ، إِلاَّ أعْطَاهُ إيّاهُ )) وَأشَارَ بيَدِهِ يُقَلِّلُهَا . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alieleza kuhusu siku ya Ijumaa akasema: "Ndani yake mna saa haafikiani nayo mja Muislamu akiwa anaswali na akimuomba kitu chochote Allaah isipokuwa atatimiziwa haja yake." Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliashiria uchache au ufupi wa muda huo kwa mkono wake. [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 11
وعن أَبي بُرْدَةَ بن أَبي موسى الأشعريِّ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ عبد الله بن عمر رضي الله عنهما : أسَمِعْتَ أبَاكَ يُحَدِّثُ عَنْ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، في شأنِ سَاعَةِ الجُمُعَةِ ؟ قَالَ : قُلْتُ : نَعَمْ ، سَمِعْتُهُ يَقُولُ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( هِيَ مَا بَيْنَ أنْ يَجْلِسَ الإمَامُ إِلَى أنْ تُقْضَى الصَّلاةُ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Burdah bin Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa 'Abdullaah bin 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) alimuuliza: "Je, umemsikia babako akihadithia kutoka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu wakati ambao dua hukubaliwa?" Akasema: Nikasema: "Ndio, nimemsikia akisema: 'Ni wakati baina ya Imamu kukaa kwenye mimbari na kumalizika kwa Swalaah." [Muslim].
Hadiyth – 12
وعن أوس بن أوسٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ مِنْ أفْضَلِ أيَّامِكُمْ يَوْمَ الجُمُعَةِ ، فَأكْثِرُوا عَلَيَّ مِنَ الصَّلاَةِ فِيهِ ؛ فَإنَّ صَلاَتَكُمْ مَعْرُوضَةٌ عَلَيَّ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Aws bin Aws (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika miongoni mwa siku zenu, Ijumaa ndio siku bora, hivyo kithirisheni (ongezeni) kuniswalia ndani yake, kwani ninaonyeshwa Swalaah zenu hizo." [Abu Daawuwd, na Isnaad yake ni Swahiyh].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب سجود الشكر
عِنْدَ حصول نعمة ظاهرة أَو اندفاع بلية ظاهرة
32-Mlango Wa Kupendeza Kusujudu Sijda ya Kushukuru (Sijdatus-Shukr) Unapopata Neema ya Wazi au Kuondokewa na Balaa
Alhidaaya.com [4]
عن سعد بن أَبي وقاص رضي اللهُ عنه ، قَالَ : خَرَجْنَا مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ مَكّةَ نُريدُ المَدِينَةَ ، فَلَمَّا كُنَّا قَرِيباً مِنْ عَزْوَرَاءَ نَزَلَ ثُمَّ رَفَعَ يَدَيْهِ فَدَعَا الله سَاعَةً ، ثُمَّ خَرَّ سَاجِداً ، فَمَكَثَ طَويلاً ، ثُمَّ قَامَ فَرَفَعَ يَدَيْهِ سَاعَةً ، ثُمَّ خَرَّ سَاجِداً - فَعَلَهُ ثَلاثَاً - وقال : (( إنِّي سَألتُ رَبِّي ، وَشَفَعْتُ لأُمَّتِي ، فَأعْطَانِي ثُلُثَ أُمَّتِي ، فَخَرَرْتُ سَاجِداً لِرَبِّي شُكْراً ، ثُمَّ رَفَعْتُ رَأسِي ، فَسَألْتُ رَبِّي لأُمَّتِي ، فَأعْطَانِي ثُلُثَ أُمَّتِي، فَخَرَرْتُ سَاجِداً لِرَبِّي شُكْراً ، ثُمَّ رَفَعْتُ رَأسِي ، فَسَألْتُ رَبِّي لأُمَّتِي ، فَأعْطَانِي الثُّلثَ الآخَرَ ، فَخَرَرْتُ سَاجِداً لِرَبِّي )) رواه أَبُو داود .
Amesema Sa'ad bin Abu Waqqaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) : Tulitoka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Makkah kwenda Madiynah. Tulipokuwa karibu na 'Azwaraa', alishuka, kisha akainua mikono yake, akamuomba Allaah kwa muda, kisha akasujudu muda mrefu kisha akasimama akainua mikono yake kwa muda, kisha akasujudu - akaifanya mara tatu-akasema: "Hakika nimeomba Rabb wangu, na nimeombea shafaa Ummah wangu. Amenipa thuluthi ya Ummah wangu, Nikasujudu kumshukuru Rabb wangu, kisha nikainua kichwa changu, nikamuomba Rabb wangu kwa ajili ya Ummah wangu. Akanipa thuluthi ya Ummah wangu, nikasujudu kumshukuru Rabb wangu, Kisha nikainua kichwa changu, nikamuomba Rabb wangu kwa ajili ya Ummah wangu, Akanipa thuluthi ya mwisho, Nikamsujudia Rabb wangu." [Abuu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل قيام الليل
33-Mlango Wa Ubora wa Kisimamo cha Usiku
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَمِنَ اللَّيْلِ فَتَهَجَّدْ بِهِ نَافِلَةً لَّكَ عَسَىٰ أَن يَبْعَثَكَ رَبُّكَ مَقَامًا مَّحْمُودًا ﴿٧٩﴾
Na katika usiku, amka uswali (tahajjud) kwa kuisoma (Qur-aan) ikiwa ni ziada kwako. Asaa Rabb wako Akakuinua cheo cha kuhimidiwa (kusifika). [Al-Israa: 79]
تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا ﴿١٦﴾
Mbavu zao zinatengana na vitanda, wanamuomba Rabb wao kwa khofu na matumaini. [As-Sajdah: 16]
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ﴿١٧﴾
Walikuwa kidogo tu katika usiku wakilala kwa raha. [Adh-Dhaariyaat: 17]
Hadiyth – 1
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم يَقومُ مِنَ اللَّيْلِ حَتَّى تَتَفطَّرَ قَدَمَاهُ ، فَقُلْتُ لَهُ : لِمَ تَصْنَعُ هَذَا ، يَا رَسُولَ الله ، وَقَدْ غُفِرَ لَكَ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأخَّرَ ؟ قَالَ : (( أفَلاَ أكُونُ عَبْداً شَكُوراً! )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وَعَن المُغِيرَةِ بن شُعبة نَحْوهُ متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali Swalaah ya usiku mpaka miguu yake ikivimba. Nikamwambia: "Kwa nini unafanya hivi ee Rasuli wa Allaah na haliyakuwa Allaah amekusamehe madhambi yako yaliyopita na ya baadaye?" Akasema: "Je, basi nisiwe mja mwenye kushukuru?" [Al-Bukhaariy na Muslim] Na mfano wake katika Swahiyh mbili katika riwaayah ya Mughiyrah bin Shu'bah.
Hadiyth – 2
وعن علي رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم طَرَقَهُ وَفَاطِمَةَ لَيْلاً ، فَقَالَ : (( أَلاَ تُصَلِّيَانِ ؟ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda kwake usiku akiwa na mkewe Faatwimah na akauliza: "Mbona hamuswali (Tahajjud)?" [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]
Hadiyth – 3
وعن سالم بن عبدِ الله بن عمر بن الخطاب رضي الله عنهما ، عن أبيِهِ : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( نِعْمَ الرَّجُلُ عَبْدُ اللهِ ، لَوْ كَانَ يُصَلِّي مِنَ اللَّيلِ )) قَالَ سالِم : فَكَانَ عَبدُ اللهِ بَعْدَ ذَلِكَ لاَ يَنامُ مِنَ اللَّيلِ إِلاَّ قَلِيلاً . متفقٌ عَلَيْهِ .
Saalim bin 'Abdullaah bin 'Umar bin Al-Khatwaab kutoka kwa babake (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "'Abdullaah ni mtu mzuri na bora sana lau angekua anaswali Swalaah ya usiku." Amesema Saalim: "Baada ya hapo 'Abdullaah hakuwa akilala usiku isipokuwa kidogo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن عبد الله بن عَمرو بن العاصِ رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا عَبدَ اللهِ ، لاَ تَكُنْ مِثْلَ فُلانٍ ؛ كَانَ يَقُومُ اللَّيلَ فَتَرَكَ قِيَامَ اللَّيلِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
'Abdillaah bin 'Amru bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ya kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ee 'Abdillaah usiwe mfano wa fulani ambaye alikuwa akiswali Swalaah ya usiku kisha akaacha kisimamo hicho cha usiku." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن ابن مسعودٍ رضي الله عنه ، قَالَ : ذُكِرَ عِنْدَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم رَجُلٌ نَامَ لَيْلَةً حَتَّى أصْبَحَ ، قَالَ : (( ذَاكَ رَجُلٌ بَالَ الشَّيطَانُ في أُذُنَيْهِ - أَوْ قَالَ : في أُذُنِهِ - )) متفقٌ عَلَيْهِ
Na Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Kuna mtu mmoja alitajwa mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa amelala usiku wote mpaka ikafika asubuhi, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Huyo ni mtu ambaye shetani amemkojolea, masikioni mwake" au alisema: "Katika sikio lake." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaai]
Hadiyth – 6
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( يَعْقِدُ الشَّيطَانُ عَلَى قَافِيَةِ رَأسِ أحَدِكُمْ ، إِذَا هُوَ نَامَ ، ثَلاَثَ عُقَدٍ ، يَضْرِبُ عَلَى كُلِّ عُقْدَةٍ : عَلَيْكَ لَيْلٌ طَويلٌ فَارْقُدْ، فَإن اسْتَيقَظَ ، فَذَكَرَ اللهَ تَعَالَى انحَلَّتْ عُقْدَةٌ ، فَإنْ تَوَضّأ ، انْحَلّتْ عُقدَةٌ ، فَإنْ صَلَّى ، انْحَلَّتْ عُقَدُهُ كُلُّهَا ، فَأصْبَحَ نَشِيطاً طَيِّبَ النَّفْسِ ، وَإلاَّ أصْبحَ خَبيثَ النَّفْسِ كَسْلاَنَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Shetani anafunga kwenye kichogo cha mmoja wenu anapolala fundo tatu anapiga juu ya kila fundo 'lala usiku mrefu' na anapoamka mja na akamtaja Allaah linafunguka fundo na akitawadha linafunguka fundo la pili na akiswali linafunguka fundo la mwisho na atafika asubuhi akiwa mwenye nguvu mchangamfu mwenye nafsi nzuri na kama si hivyo atafika asubuhi akiwa na nafsi mbaya mvivu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Hadiyth – 7
وعن عبد الله بن سلام رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أيُّهَا النَّاسُ : أفْشُوا السَّلامَ ، وَأطْعِمُوا الطَّعَامَ ، وَصَلُّوا بِاللَّيْلِ وَالنَّاسُ نِيَامٌ ، تَدْخُلُوا الجَنَّةَ بِسَلاَمٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin Salaam (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Enyi watu! Enezeni ujumbe (salamu) wa Kiislamu, na walisheni masikini na Swalini Swalaah ya usiku wakati watu wengine wamelala, mtaingia Peponi kwa amani." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 8
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( أفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ : شَهْرُ اللهِ المُحَرَّمُ ، وَأفْضَلُ الصَّلاَةِ بَعْدَ الفَرِيضَةِ : صَلاَةُ اللَّيْلِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Funga bora baada ya Ramadhwaan ni mwezi wa Allaah Muharram. Na Swalaah bora baada ya faradhi ni Swalaah ya usiku." [Muslim]
Hadiyth – 9
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( صَلاةُ اللَّيْلِ مَثْنَى مَثْنَى ، فَإذَا خِفْتَ الصُّبْحَ فَأوْتِرْ بِوَاحِدَةٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah ya usiku ni rakaa mbili mbili na unapoogopea kuingia kwa asubuhi swali witri rak'ah moja." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 10
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يُصَلِّي مِنَ اللَّيْلِ مَثْنَى مَثْنَى ، وَيُوتِرُ بِرَكْعَةٍ .متفقٌ عَلَيْهِ .
Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akiswali Swalaah ya usiku rak'ah mbili mbili na akimalizia na rak'ah moja ya witri." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 11
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يُفْطِرُ مِنَ الشَّهْرِ حَتَّى نَظُنَّ أنْ لاَ يَصُومَ مِنْهُ ، وَيَصُومُ حَتَّى نَظُنَّ أنْ لاَ يُفْطِرَ مِنْهُ شَيْئاً ، وَكَانَ لاَ تَشَاءُ أنْ تَرَاهُ مِنَ اللَّيلِ مُصَلِّياً إِلاَّ رَأيْتَهُ ، وَلاَ نَائِماً إِلاَّ رَأيْتَهُ . رواه البخاري .
Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akila katika mwezi mpaka tukidhani hatafunga katika mwezi huo, na akifunga mpaka tukidhani hatofungua katika mwezi huo. Na ukitaka kumuona akiswali usiku utaona hilo na ukitaka kumuona akiwa amelala usiku utamuona pia." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 12
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يُصَلِّي إحْدَى عَشْرَةَ رَكْعَةً – تَعْنِي في اللَّيلِ – يَسْجُدُ السَّجْدَةَ مِنْ ذَلِكَ قَدْرَ مَا يَقْرَأُ أحَدُكُمْ خَمْسِينَ آيَةً قَبْلَ أنْ يَرْفَعَ رَأسَهُ ، وَيَرْكَعُ رَكْعَتَيْنِ قَبْلَ صَلاَةِ الفَجْرِ ، ثُمَّ يَضْطَجِعُ عَلَى شِقِّهِ الأيْمَنِ حَتَّى يَأتِيَهُ المُنَادِي للصَلاَةِ . رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali rak'ah kumi na moja yaani usiku, anasujudu katika hizo rak'ah sawa na kisomo cha ayah hamsini kabla ya kunyanyua kichwa chake. Na alikuwa akiswali rak'ah mbili kabla ya Swalaah ya Alfajiri, kisha alikuwa akijilaza kwa ubavu wake wa kulia mpaka anapokuja muadhini kumuita kwa ajili ya Swalaah." [Al-Bukhaariy].
Hadiyth – 13
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَزيدُ - في رَمَضَانَ وَلاَ في غَيْرِهِ - عَلَى إحْدَى عَشْرَةَ رَكْعَةً : يُصَلِّي أرْبَعاً فَلاَ تَسْألْ عَنْ حُسْنِهِنَّ وَطُولِهِنَّ ، ثُمَّ يُصَلِّي أرْبَعاً فَلاَ تَسْألْ عَنْ حُسْنِهِنَّ وطُولِهِنَّ، ثُمَّ يُصَلِّي ثَلاثاً. فَقُلتُ: يَا رسولَ اللهِ ، أتَنَامُ قَبْلَ أنْ تُوتِرَ؟ فَقَالَ: (( يَا عَائِشَة، إنَّ عَيْنَيَّ تَنَامَانِ وَلاَ يَنَامُ قَلْبِي)) متفقٌ عَلَيْهِ.
Na amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) : Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa haswali zaidi ya rak'ah kumi na moja katika Ramadhwaan wala katika miezi mingine. Alikuwa akiswali rak'ah nne, wala usiulize kuhusu urefu wake! Kisha alikuwa akiswali rak'ah nne wala usiulize uzuri, ukamilifu na urefu wake! Kisha alikuwa anaswali rak'ah tatu. Nikamuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! je, unalala kabla ya kuswali witri?" Akasema: "Ee 'Aaishah! Hakika macho yangu yanalala lakini moyo wangu haulali." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 14
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَنَامُ أوّلَ اللَّيلِ ، وَيَقُومُ آخِرَهُ فَيُصَلِّي . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa analala mwanzo wa usiku na baadae akiamka mwisho wake (wa usiku) kwa ajili ya kuswali (Swalaah ya usiku)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 15
وعن ابن مسعود رضي الله عنه ، قَالَ : صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم لَيْلَةً ، فَلَمْ يَزَلْ قائِماً حَتَّى هَمَمْتُ بِأَمْر سوءٍ ! قيلَ : مَا هَمَمْتَ ؟ قَالَ : هَمَمْتُ أنْ أجِلْسَ وَأدَعَهُ . متفقٌ عَلَيْهِ
Imepokewa kutoka kwa Ibn Mas'uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: "Niliswali pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku naye akarefusha kisimamo mpaka nikaanza kufikiria jambo baya." Akaulizwa: "Hilo jambo baya ni lipi?" Alisema: "Nilifikiria kukaa na kuacha kumfuata (katika Swalaah)." [Ahmad, Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 16
وعن حذيفة رضي الله عنه ، قَالَ: صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ لَيْلَةٍ فَافْتَتَحَ البَقرَةَ ، فَقُلْتُ : يَرْكَعُ عِنْدَ المئَةِ ، ثُمَّ مَضَى ، فقلتُ : يُصَلِّي بِهَا في رَكْعَةٍ فَمَضَى ، فقلتُ : يَرْكَعُ بِهَا ، ثُمَّ افْتَتَحَ النِّسَاءَ فَقَرَأَهَا ، ثُمَّ افْتَتَحَ آلَ عِمْرَانَ فَقَرَأَهَا ، يَقرَأُ مُتَرَسِّلاً : إِذَا مَرَّ بآيةٍ فِيهَا تَسبيحٌ سَبَّحَ ، وَإذَا مَرَّ بسُؤَالٍ سَأَلَ ، وَإذَا مَرَّ بتَعَوُّذٍ تَعَوَّذَ ، ثُمَّ رَكَعَ ، فَجَعَلَ يَقُولُ : (( سُبْحَانَ رَبِّيَ العَظِيمِ )) فَكَانَ رُكُوعُهُ نَحواً مِنْ قِيَامِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( سَمِعَ اللهُ لِمَنْ حَمِدَهُ ، رَبَّنَا لَكَ الحَمْدُ )) ثُمَّ قَامَ طَويلاً قَريباً مِمَّا رَكَعَ ، ثُمَّ سَجَدَ ، فَقَالَ : (( سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى )) فَكَانَ سجُودُهُ قَريباً مِنْ قِيَامِهِ. رواه مسلم.
Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Niliswali nyuma ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) usiku, Akaanza Suwrah Al-Baqarah. Nikasema atarukuu ayah ya mia, Akapita, Nikasema huenda akamaliza katika rakaa, lakini aliendelea. Nikasema ataiswalia rakaa moja, akapita, Alianza Suwrah An-Nisaa akaisoma, kisha akaanza Aal-'Imraan akaisoma, Akawa anasoma mutarassila (kisomo ambacho alikuwa akibainisha vilivyo kila herufi na kuzipatia haki zake) na anapofika katika ayah ya tasbihi, analeta tasbihi, na anapofika katika maombo huomba, na akifika ayah ya kujilinda anajilinda, Kisha akarukuu akawa anasema: 'Subhaana Rabbiyal 'Adhiym - Ametakasika Mola wangu Mtukufu'. Rukuu yake ilikuwa kama kisimamo chake, kisha akasema: 'Sami'a LLaahu liman hamidahu, Rabbanaa Lwalakal hamdu' - Allaah anamsikia anayemhimidi, Ee Rabb wetu kuhimidiwa ni Kwako'. Kisha akasimama kisimamo kirefu karibu ya alichorukuu. Kisha akasujudu akasema: 'Subhaana Rabbiyal a'alaa' - Ametakasika Rabb wangu Aliye juu.' Sijda yake ikakaribia kisimamo chake." [Muslim]
Hadiyth – 17
وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : سُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم أيُّ الصَّلاَةِ أفْضَلُ ؟ قَالَ : (( طُولُ القُنُوتِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: "Ni Swalaah gani iliyo bora?" Akasema: "Yenye kisimamo kirefu." [Muslim]
Hadiyth – 18
وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أحَبُّ الصَّلاةِ إِلَى اللهِ صَلاةُ دَاوُدَ ، وَأحَبُّ الصِّيَامِ إِلَى اللهِ صِيَامُ دَاوُدَ ، كَانَ يَنَامُ نِصْفَ اللَّيلِ وَيَقُومُ ثُلُثَهُ وَيَنَامُ سُدُسَهُ وَيَصُومُ يَوماً وَيُفْطِرُ يَوْماً )) متفقٌ عَلَيْهِ
Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah bin 'Amri bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swalaah inayopendwa sana na Allaah Ta'aalaa ni Swalaah ya Daawuwd na funga inayopendeza sana mbele ya Allaah Ta'aalaa ni funga ya Daawuwd. Alikuwa akilala nusu ya usiku na kusimama kuswali thuluthi (1/3) yake na akilala sudusi (nusu ya thuluthi - 1/6) na alikuwa akifunga siku moja na akila siku ya pili." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 19
وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّ في اللَّيْلِ لَسَاعَةً، لاَ يُوَافِقُهَا رَجُلٌ مُسْلِمٌ يَسْألُ الله تَعَالَى خَيْراً مِنْ أمْرِ الدُّنْيَا وَالآخِرَةِ، إِلاَّ أعْطَاهُ إيَّاهُ ، وَذَلِكَ كُلَّ لَيْلَةٍ )) رواه مسلم .
Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Hakika upo wakati usiku hatauwahi mtu yeyote Muislamu anayemuomba Allaah Ta'aalaa jambo lolote la kheri la unia na Aakhera ila Atampatia. Na hilo linakuwa kwa kila usiku." [Muslim]
Hadiyth – 20
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا قَامَ أحَدُكُمْ مِنَ اللَّيْلِ فَلْيَفْتَتِحِ الصَّلاَةَ بركْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu ;anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoamka mmoja wenu kwa ajili ya kuswali Swalaah ya usiku aanze kwa rak'ah mbili nyepesi." [Muslim]
Hadiyth – 21
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إِذَا قَامَ مِنَ اللَّيْلِ افْتَتَحَ صَلاَتَهُ بِرَكْعَتَيْنِ خَفِيفَتَيْنِ . رواه مسلم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa anapoamka kwa Swalaah ya usiku akianza kwa rakaa mbili nyepesi." [Muslim]
Hadiyth – 22
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا فَاتَتْهُ الصَّلاةُ مِن اللَّيْلِ مِنْ وَجَعٍ أَوْ غَيْرِهِ ، صَلَّى مِنَ النَّهَارِ ثِنْتَيْ عَشرَةَ ركْعَةً . رواه مسلم .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa inapompita Swalaah ya usiku kwa sababu ya maumivu au sababu nyengine yoyote, anaswali mchana rakaa kumi na mbili (za Sunnah)." [Muslim]
Hadiyth – 23
وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ نَامَ عَنْ حِزْبِهِ ، أَوْ عَنْ شَيْءٍ مِنْهُ ، فَقَرَأَهُ فيما بَيْنَ صَلاَةِ الفَجْرِ وصلاة الظُّهْرِ ، كُتِبَ لَهُ كَأنَّمَا قَرَأهُ مِنَ اللَّيْلِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote anayelala bila kutekeleza Hizb (ni anachojaalia mtu kufanya kwa nafasi yake kwa mfano kusoma Qur-aan au kuswali au kufanya amali nyengine yoyote) yake au sehemu ya hiyo, akawa ni mwenye kusoma baina ya Swalaah ya Alfajiri na Adhuhuri anaandikiwa ni kama amesoma usiku." [Muslim]
Hadiyth – 24
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( رَحِمَ اللهُ رَجُلاً قَامَ مِنَ اللَّيْلِ ، فَصَلَّى وَأيْقَظَ امْرَأَتَهُ ، فَإنْ أبَتْ نَضَحَ في وَجْهِهَا المَاءَ ، رَحِمَ اللهُ امْرَأَةً قَامَتْ مِنَ اللَّيْلِ ، فَصَلَّتْ وَأيْقَظَتْ زَوْجَهَا ، فَإن أبَى نَضَحَتْ فِي وَجْهِهِ المَاءَ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah amrehemu mtu anaamka usiku, akaswali, na akamuamsha mkewe. Akikataa anamnyunyizia maji usoni mwake. Allaah amrehemu mwanamke ambaye ameamka usiku ili kuswali (Swalaah ya usiku) na akamuamsha mumewe akikataa akamnyunyizia maji usoni mwake." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 25
وعن أَبي هريرة وعن أَبي سعيدٍ رضي الله عنهما ، قالا : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أَيْقَظَ الرَّجُلُ أهْلَهُ مِنَ اللَّيْلِ فَصَلَّيَا - أَوْ صَلَّى رَكْعَتَيْنِ جَمِيعاً ، كُتِبَا في الذَّاكِرِينَ وَالذَّاكِرَاتِ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Kutoka kwa Abu Huraiyrah na kwa Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) wamesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mume anapomuamsha Mkewe wakati wa usiku na wakaswali pamoja - au wakaswali rak'ah mbili wote (kwa jamaa), wanaandikiwa kuwa ni miongoni mwa wenye kumdhukuru Allaah, katika wanaume na wanawake." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Hadiyth – 26
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا نَعَسَ أحَدُكُمْ في الصَّلاَةِ ، فَلْيَرْقُدْ حَتَّى يَذْهَبَ عَنْهُ النَّوْمُ ، فَإنَّ أحَدَكُمْ إِذَا صَلَّى وَهُوَ نَاعِسٌ ، لَعَلَّهُ يَذْهَبُ يَسْتَغْفِرُ فَيَسُبَّ نَفْسَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Akisinzia mmoja wenu naye anaswali basi alale mpaka usingizi unapomalizika. Hakika mmoja wenu anaposwali naye anasinzia hatafahamu maneno anayosema, hivyo huenda akawa anaitukana (anajilaani) nafsi yake badala ya kuomba msamaha." [Al-Bukhaariy, Muslim na Ahmad]
Hadiyth – 27
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا قَامَ أحَدُكُمْ مِنَ اللَّيْلِ ، فَاسْتَعْجَمَ القُرْآنَ عَلَى لِسَانِهِ ، فَلَمْ يَدْرِ مَا يَقُولُ ، فَلْيَضْطَجِع )) رواه مسلم
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapoamka mmoja wenu usiku (Tahajjud) na akaona vigumu kutamka ayah za Qur-aan (inavyotakiwa) kwa ulimi wake, na akawa hajui anayosema basi alale." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب قيام رمضان وَهُوَ التراويح
34-Mlango Wa Kupendeza Kuswali Swalaah ya Ramadhwaan Nayo ni Tarawehe
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَامَ رَمَضَانَ إيماناً وَاحْتِسَاباً غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kusimama usiku katika mwezi wa Ramadhwaan kwa 'Ibadah hali ya kuwa na Imaani, na hali ya kutarajia kupata thawabu mtu huyo husamehewa yaliyotangulia katika madhambi yake." [Al-Bukhaariy, Muslim na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يُرَغِّبُ في قِيَامِ رَمَضَانَ مِنْ غَيْرِ أنْ يَأمُرَهُمْ فِيهِ بِعَزِيمَةٍ ، فيقولُ : (( مَنْ قَامَ رَمَضَانَ إيمَاناً وَاحْتِسَاباً غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ )) رواه مسلم .
Na amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) : Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akihimiza kusimamisha usiku wa Ramadhwaan bila kuwaamuru wao kuwa ni lazima akisema: "Mwenye kusimama usiku Ramadhwaan kwa Imaani, na kutarajia thawabu huyo husamehewa madhambi yake yaliyotangulia." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل قيام ليلة القدر وبيان أرجى لياليها
35-Mlango Wa Fadhila za Kisimamo cha Usiku wa Qadr (Cheo Kitukufu) na Kubainisha Usiku Unaotarajiwa
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةِ الْقَدْرِ ﴿١﴾
Hakika Sisi Tumeiteremsha Qur-aan katika Laylatul-Qadr (Usiku wa Qadr).
وَمَا أَدْرَاكَ مَا لَيْلَةُ الْقَدْرِ ﴿٢﴾
Na nini kitakachokujulisha ni nini Laylatul-Qadr?
لَيْلَةُ الْقَدْرِ خَيْرٌ مِّنْ أَلْفِ شَهْرٍ ﴿٣﴾
Laylatul-Qadr ni mbora kuliko miezi elfu.
تَنَزَّلُ الْمَلَائِكَةُ وَالرُّوحُ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمْرٍ ﴿٤﴾
Wanateremka humo Malaika pamoja na Ar-Ruwh (Jibriyl) kwa Idhini ya Rabb wao kwa kila jambo.
سَلَامٌ هِيَ حَتَّىٰ مَطْلَعِ الْفَجْرِ ﴿٥﴾
Usiku huo ni amani mpaka kuchomoza Alfajiri. [Al-Qadr: 1-5]
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ ﴿٣﴾
Hakika Sisi Tumekiteremsha katika usiku uliobarikiwa. [Ad-Dukhaan: 3]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ قَامَ لَيْلَةَ القَدْرِ إيمَاناً وَاحْتِسَاباً غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Mwenye kusimama Laylatul Qadr kwa Imaani, na kutarajia thawabu huyo husamehewa madhambi yakeyaliyotangulia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رِجالاً مِنْ أصْحَابِ النبيِّ صلى الله عليه وسلم أُرُوا لَيْلَةَ القَدْرِ في المَنَامِ في السَّبْعِ الأَوَاخِرِ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أرَى رُؤْيَاكُمْ قَدْ تَوَاطَأتْ في السَّبْعِ الأوَاخِرِ ، فَمَنْ كَانَ مُتَحَرِّيهَا فَلْيَتَحَرَّهَا في السَّبْعِ الأَوَاخِرِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa watu fulani miongoni mwa Swahaaba wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) walionyeshawa Laylatul Qadr ndotoni katika siku saba za mwisho. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Naona ndoto zenu zimeangukia siku saba za mwisho basi mwenye kutafuta na atafute katika siku saba za mwishao." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُجَاوِرُ في العَشْرِ الأَوَاخِرِ مِنْ رَمَضَانَ ، ويقول : (( تَحرَّوا لَيْلَةَ القَدْرِ في العَشْرِ الأواخرِ منْ رَمَضانَ ))متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anakaa itikafu katika kumi la mwisho la Ramadhwaan na anasema: "Itafuteni Laylatul Qadr katika kumi la mwisho la Ramadhwaan." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 4
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تَحَرَّوْا لَيْلَةَ القَدْرِ في الوَتْرِ مِنَ العَشْرِ الأوَاخِرِ مِنْ رَمَضَانَ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Itafuteni Laylatul Qadr katika siku za witr (yaani usiku wa tarehe 21, au 23, au 27, au 29) katika kumi la mwisho la Ramadhwaan." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن عائشة ، رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ العَشْرُ الأَوَاخِرُ مِنْ رَمَضَانَ ، أحْيَا اللَّيْلَ ، وَأيْقَظَ أهْلَهُ ، وَجَدَّ وَشَدَّ المِئزَرَ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) : Zilipokuwa zinaanza siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhwaan Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anaswali usiku kucha na akiwaamsha familia yake na anajipinda na kukaza mkanda wake." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 6
وعن عائشة ، رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَجْتَهِدُ في رَمَضَانَ مَا لاَ يَجْتَهِدُ في غَيْرِهِ ، وَفِي العَشْرِ الأوَاخِرِ مِنْهُ مَا لا يَجْتَهِدُ في غَيْرِهِ . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akijitahidi (kwa kufanya 'Ibadah) katika mwezi wa Ramadhwaan zaidi kuliko miezi mingine. Na katika mwezi huo alikuwa anajitahidi zaidi katika kuni la mwisho kuliko siku nyinginezo katika mwezi huo." [Muslim]
Hadiyth – 7
وعن عائشة ، رضي الله عنها ، قالت : قُلْتُ : يَا رسول الله ، أرَأيْتَ إنْ عَلِمْتُ أيُّ لَيلَةٍ لَيْلَةُ القَدْرِ مَا أقُولُ فِيهَا ؟ قَالَ : (( قُولِي : اللَّهُمَّ إنَّكَ عَفُوٌ تُحِبُّ العَفْوَ فَاعْفُ عَنّي )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Nilimuuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Waonaje nikiweza kuujua usiku wa Laylatul Qadr, niseme nini ndani yake?" Akasema: "Sema: Allaahumma Innaka 'Afuwwun Tuhibbul 'Afwa Fa'fu'anniy - Ee Mola wangu! Hakika Wewe ni Mwingi wa kusamehe na Unapenda kusamehe, hivyo nismehe." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل السواك وخصال الفطرة
36-Mlango Wa Fadhila za Kupiga Mswaki na Mambo ya Kimaumbile
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لَوْلاَ أنْ أشُقَّ عَلَى أُمَّتِي - أَوْ عَلَى النَّاسِ - لأَمَرْتُهُمْ بِالسِّوَاكِ مَعَ كُلِّ صَلاَةٍ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kama sikuhofia kwa Ummah wangu - au watu - ningewaamuru wapige mswaki kabla ya kila Swalaah." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaai]
Hadiyth – 2
وعن حُذَيْفَةَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا قَامَ مِن النَّومِ يَشُوصُ فَاهُ بِالسِّوَاكِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu) : Alipokuwa akiamka usingizini usiku, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisafisha kinywa chake kwa mswaki." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na An-Nasaai]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كُنَّا نُعِدُّ لِرسولِ الله صلى الله عليه وسلم سِوَاكَهُ وَطَهُورَهُ ، فَيَبْعَثُهُ اللهُ مَا شَاءَ أنْ يَبْعَثَهُ مِنَ اللَّيْلِ ، فَيَتَسَوَّكُ ، وَيَتَوضَّأُ وَيُصَلِّي . رواه مسلم .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Tulikuwa tukimtayarisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) mswaki wake na maji yake ya wudhuu, na alikuwa akianza kupiga mswaki na kisha kutawadha na kuswali pindi atakapoamshwa na Allaah usiku." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن أنس رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أكْثَرْتُ عَلَيْكُمْ في السِّوَاكِ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ninawahimizeni sana nyinyi muwe mkitumia mswaki." [Al-Bukhaariy]
Hadiyth – 5
وعن شريح بن هانىءٍ ، قَالَ : قلت لعائشة رضي اللهُ عنها : بأَيِّ شَيْءٍ كَانَ يَبْدَأُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ بَيْتَهُ ؟ قالت : بِالسِّوَاكِ . رواه مسلم .
Amesema Shurayh bin Haani': Nilimuuliza 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) : "Ni kitu gani alikuwa anaanza nacho Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapoingia nyumbani kwake?" Akajibu: "Alikuwa akipiga mswaki." [Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي موسى الأشعري رضي اللهُ عنه ، قَالَ : دَخلتُ عَلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم وَطَرَفُ السِّوَاكِ عَلَى لِسَانِهِ . متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ مسلمٍ .
Amesema Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) : Niliingia kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na ncha ya mswaki ipo mdomoni mwake." [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Muslim]
Hadiyth – 7
وعن عائشة رضي الله عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( السِّوَاكُ مَطْهَرَةٌ لِلْفَمِ مَرْضَاةٌ للرَّبِّ )) رواه النسائي وابنُ خُزَيْمَةَ في صحيحهِ بأسانيدَ صحيحةٍ .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mswaki unasafisha mdomo na unamridhisha Rabb." [An-Nasaai na Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake kwa Isnaad zilizo Swahiyh]
Hadiyth – 8
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( الفِطْرَةُ خَمْسٌ ، أَوْ خَمْسٌ مِنَ الفِطْرَةِ : الخِتَانُ ، وَالاسْتِحْدَادُ ، وَتَقْلِيمُ الأظْفَارِ ، وَنَتْفُ الإبطِ ، وَقَصُّ الشَّارِبِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Fitrah ni mambo matano au mambo matano ni katika Fitrah: Kutahiri, kunyoa nywele za kinena (sehemu za siri), kung'oa nywele za kwapani, kukata kucha na kupunguza sharubu." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 9
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( عَشْرٌ مِنَ الفِطْرَةِ : قَصُّ الشَّارِبِ ، وَإعْفَاءُ اللِّحْيَةِ ، وَالسِّوَاكُ ، وَاسْتِنْشَاقُ المَاءِ ، وَقَصُّ الأظْفَارِ ، وَغَسْلُ البَرَاجِمِ ، وَنَتف الإبْطِ ، وَحَلْقُ العَانَةِ ، وَانْتِقَاصُ المَاءِ )) قَالَ الرَّاوِي : وَنَسِيْتُ العَاشِرَةَ إِلاَّ أنْ تَكُونَ المَضمَضَةُ . قَالَ وَكِيعٌ - وَهُوَ أحَدُ رُواتِهِ - انْتِقَاصُ المَاءِ : يَعْنِي الاسْتِنْجَاءِ . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mambo kumi ni katika Fitrah: Kupunguza sharubu, na kufuga ndevu bila ya kuzipunguza, na kupiga mswaki, na kusafisha pua kwa kupandisha maji puani, na kukata kucha, na kuosha mashina ya vidole, na kung'oa nywele za kwapani, na kunyoa nywele za kinena na kujisafisha kwa maji baada ya kwenda haja." Amesema mpokezi: "Na nimesahau jambo la kumi ila huenda ikawa ni kusukutuwa." Akasema Waki'un mmoja miongoni mwa wapokezi: "Intiqaaswul Maa'ina maana ya kujiosha baada ya haja (ndogo au kubwa)." [Muslim]
Hadiyth – 10
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( أحْفُوا الشَّوَارِبَ وَأعْفُوا اللِّحَى )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Punguzeni sharubu na fugeni ndevu." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تأكيد وجوب الزكاة وبيان فضلها وَمَا يتعلق بِهَا
37-Mlango Wa Kusisitizwa Wajibu wa Zakaah na Kubainisha Fadhila Zake na Mambo Yanayohusiana Nayo
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
وَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ ﴿٤٣﴾
Na simamisheni Swalaah na toeni Zakaah [Al-Baqarah: 43]
وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ ﴿٥﴾
Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah hali ya kuwa ni wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki, na wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah. Na hiyo ndiyo Dini iliyosimama imara. [Al-Bayyinah: 5]
خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ ۖ ﴿١٠٣﴾
Chukua (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) katika mali zao Swadaqah, uwatwaharishe na uwatakase kwazo, na waombee Du’aa (na Maghfirah). [At-Tawbah: 103]
Hadiyth – 1
وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( بُنِيَ الإسْلاَمُ عَلَى خَمْسٍ : شَهَادَةِ أنْ لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ ، وَأنَّ مُحَمَّداً عَبْدُهُ وَرَسُولُهُ ، وَإقَامِ الصَّلاَةِ ، وَإيتَاءِ الزَّكَاةِ ، وَحَجِّ البَيْتِ ، وَصَوْمِ رَمَضَانَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Umejengwa Uislamu juu ya nguzo tano: Kikiri kwa moyo na kubaini kwa ulimi kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah, na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, na kusimamisha Swalaah, na kutoa Zakaah, na kuhiji na kufunga mwezi wa Ramadhwaan." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن طَلْحَةَ بن عبيد الله رضي الله عنه ، قَالَ : جَاءَ رَجُلٌ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم مِنْ أَهْلِ نَجْدٍ ثَائِرُ الرَّأسِ نَسْمَعُ دَوِيَّ صَوْتِهِ ، وَلاَ نَفْقَهُ مَا يَقُولُ ، حَتَّى دَنَا مِنْ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، فَإذا هُوَ يَسألُ عَنِ الإسْلاَم ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( خَمْسُ صَلَواتٍ في اليَوْمِ وَاللَّيْلَةِ )) قَالَ : هَلْ عَلَيَّ غَيْرُهُنَّ ؟ قَالَ : (( لاَ ، إِلاَّ أنْ تَطَّوَّعَ )) فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( وَصِيامُ شَهْرِ رَمَضَانَ )) قَالَ : هَلْ عَلَيَّ غَيْرُهُ ؟ قَالَ : (( لاَ ، إِلاَّ أنْ تَطَّوَّعَ )) قَالَ : وَذَكَرَ لَهُ رسول الله صلى الله عليه وسلم الزَّكَاةَ ، فَقَالَ : هَلْ عَلَيَّ غَيْرُهَا ؟ قَالَ : (( لاَ ، إِلاَّ أنْ تَطَّوَّعَ )) فَأدْبَرَ الرَّجُلُ وَهُوَ يَقُولُ : وَاللهِ لاَ أُزِيدُ عَلَى هَذَا وَلاَ أنْقُصُ مِنْهُ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أفْلَحَ إنْ صَدَقَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Twalhah bin 'Ubaydillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alikuja mtu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka Najd, nywele timtim. Tunasikia mvumo wa sauti yake, wala hatuelewi anachosema, mpaka akamkaribia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tukajua kumbe anauliza kuhusu Uislamu, akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) : "Zipo Swalaah tano mchana na usiku." Akasema: "Je, kuna Swalaah nyingine mbali na hizo?" Akasema: "Hapana, ila za Sunnah." Akasema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Na funga ya mwezi wa Ramadhwaan." Akauliza: "Je, kuna funga nyingine mbali na hiyo?" Akasema: "Hapana ila funga ya khiari." Akasema Twalhah: "Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtajia kuhusu Zakaah." Akauliza yule mtu: "Je, kuna nyingine mbali na hiyo?" Akasema: "Hapana, ila unaweza kutoa swadaqah." Aliondoka yule mtu na huku anasema: "Naapa kwa Allaah sitazidisha juu ya hizi wala sitazipunguza juu ya hizi wala sitazipunguza." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: "Kama amesema kweli, basi amefanikiwa (yaani ataingizwa Peponi)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن ابن عباس رضي الله عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم بعث مُعاذاً رضي الله عنه إِلَى اليَمَنِ ، فَقَالَ : (( ادْعُهُمْ إِلَى شَهَادَةِ أنْ لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ وَأنِّي رسول اللهِ ، فإنْ هُمْ أطَاعُوا لِذلِكَ ، فَأعْلِمْهُمْ أن اللهَ تَعَالَى ، افْتَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسَ صَلَواتٍ في كُلِّ يَوْمٍ وَلَيْلَةٍ ، فَإنْ هُمْ أطَاعُوا لِذلِكَ ، فَأعْلِمْهُمْ أنَّ اللهَ افْتَرَضَ عَلَيْهِمْ صَدَقَةً تُؤخَذُ مِنْ أغْنِيَائِهِمْ ، وتُرَدُّ عَلَى فُقَرَائِهِمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipomtuma Mu'aadh (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwenda Yemen alimwambia: "Waite katika kushuhudia ya kwamba hapana anayepaswa kuabudiwa isipokuwa Allaah na kuwa mimi ni Rasuli wa Allaah. Wanapokutii katika hilo basi wafahamishe kuwa Allaah Ta'aalaa amewafaridhisha Swalaah tano kwa kila mchana na usiku. Ikiwa watakutii katika hilo basi wajulishe kuwa Allaah amefaradhisha juu yao swadaqah inayochukuliwa kutoka kwa matajiri miongoni mwao na inarejeshwa kwa mafukara wao." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 4
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( أُمِرْتُ أنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى يَشْهَدُوا أنْ لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ، وَأنَّ مُحَمَّداً رسول الله ، وَيُقِيمُوا الصَّلاةَ ، وَيُؤتُوا الزَّكَاةَ، فَإذَا فَعَلُوا ذَلِكَ عَصَمُوا مِني دِمَاءهُمْ وَأمْوَالَهُمْ ، إِلاَّ بِحَقِّ الإسْلاَمِ ، وَحِسَابُهُم عَلَى الله )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nimeamrishwa niwapige watu vita mpaka wakiri kwa moyo na watamke kwa ulimi kuwa, 'Hakuna Mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allaah na kuwa Muhammad ni Rasuli wa Allaah, na wadumishe Swalaah na watoe Zakaah na kama watafanya hivyo wamesalimisha damu zao na mali zao isipokuwa kwa haki ya Uislamu na hesabu yao iko kwa Allaah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : لَمَّا تُوُفِّيَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم - وَكَانَ أَبُو بَكْرٍ رضي الله عنه - وَكَفَرَ مَنْ كَفَرَ مِنَ العَرَبِ ، فَقال عُمَرُ رضي الله عنه : كَيْفَ تُقَاتِلُ النَّاسَ وَقَدْ قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( أُمِرْتُ أنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى يَقُولوُا لاَ إلهَ إِلاَّ اللهُ ، فَمَنْ قَالَهَا فَقَدْ عَصَمَ مِنِّي مَالَهُ وَنَفْسَهُ إِلاَّ بِحَقِّهِ ، وَحِسَابُهُ عَلَى الله )) فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ : وَاللهِ لأُقَاتِلَنَّ مَنْ فَرَّقَ بين الصَّلاَةِ وَالزَّكَاةِ ، فَإنَّ الزَّكَاةَ حَقُّ المَالِ . وَاللهِ لَوْ مَنَعُونِي عِقَالاً كَانُوا يُؤدُّونَهُ إِلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، لَقَاتَلْتُهُمْ عَلَى مَنْعِهِ . قَالَ عُمَرُ رضي الله عنه : فَوَاللهِ مَا هُوَ إِلاَّ أنْ رَأيْتُ اللهَ قَدْ شَرَحَ صَدْرَ أَبي بَكْرٍ لِلقِتَالِ ، فَعَرَفْتُ أنَّهُ الحَقُّ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipofishwa, na Abu Bakar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa khalifah, na wakakufuru walio kufuru miongoni mwa Waarabu (Abu Bakar aliamua kuwapiga vita). 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) akauliza: "Vipi utawapiga watu vita wakati Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, 'Nimeamrishwa kuwapiga watu vita mpaka waseme kuwa hakuna Mola anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Allaah. Atakayesema hivyo atakuwa amelinda kwangu, mali na nafsi yake, isipokuwa kwa haki yake, na hesabu yake iko kwa Allaah'." Akasema Abu Bakar: "Naapa kwa Allaah! Nitampiga vita aliyetenganisha kati ya Swalaah na Zakaah, hakika Zakaah ni wajibu katika mali. Naapa kwa Allaah! Lau kama wangalininyima mtoto wa mbuzi tu waliyekuwa wanamtoa kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ningewapiga vita." 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) Akasema: "Naapa kwa Allaah! haikuwa isipokuwa Allaah Amekikunjua kifua cha Abu Bakar (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwa ajili ya vita, na nikaelewa kuwa hiyo ndiyo haki." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nassaiy]
Hadiyth – 6
وعن أَبي أيُّوب رضي الله عنه : أنّ رَجُلاً قَالَ للنبيِّ صلى الله عليه وسلم : أخْبِرْنِي بعمل يُدْخِلُنِي الجَنَّة ، قَالَ : (( تَعْبُدُ اللهَ ، وَلاَ تُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً ، وَتُقِيمُ الصَّلاَةَ ، وَتُؤْتِي الزَّكَاةَ ، وَتَصِلُ الرَّحِمَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Ayyub (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa mtu mmoja alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Nieleze amali itakayoniingiza Peponi?" Akasema: "Umuabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, udumishe Swalaah, utoe Zakaah na Uunge undugu." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 7
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه: أنَّ أعْرَابياً أتَى النبيَّ صلى الله عليه وسلم ، فَقَالَ : يَا رسولَ اللهِ، دُلَّنِي عَلَى عَمَلٍ إِذَا عَمِلْتُهُ ، دَخَلْتُ الجَنَّةَ . قَالَ : (( تَعْبُدُ اللهَ لاَ تُشْرِكُ بِهِ شَيْئاً ، وتُقِيمُ الصَّلاَةَ ، وتُؤتِي الزَّكَاةَ المَفْرُوضَةَ ، وَتَصُومُ رَمَضَانَ )) قَالَ : وَالذي نَفْسِي بِيَدِهِ ، لا أزيدُ عَلَى هَذَا ، فَلَمَّا وَلَّى ، قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ سَرَّهُ أنْ يَنْظُرَ إِلَى رَجُلٍ مِنْ أهْلِ الجَنَّةِ فَلْيَنْظُرْ إِلَى هَذَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Mbedui mmoja alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kumwambia: "Nielekeze amali nikifanya nitaingia Peponi." Akamjibu: "Muabudu Allaah usimshirikishe na chochote, na dumisha Swalaah na utoe Zakaah za faradhi na ufunge Ramadhwaan." Akasema: "Ninaapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi Mwake, siongezi zaidi ya hivi." Alipoondoka Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: "Anayefurahishwa kumuangalia mtu miongoni mwa watu wa Peponi amuangalie mtu huyu." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 8
وعن جرير بن عبد الله رضي الله عنه ، قَالَ : بايَعْتُ النبيَ صلى الله عليه وسلم عَلَى إقَامِ الصَّلاَةِ ، وَإيتَاءِ الزَّكَاةِ ، وَالنُّصْحِ لِكُلِّ مُسْلِمٍ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Jariyr bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: "Nilimbai Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) juu ya kusimamisha Swalaah na kutoka Zakaah na kumpa nasaha kila Muislamu." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 9
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ صَاحِبِ ذَهَبٍ ، وَلاَ فِضَّةٍ ، لا يُؤَدِّي مِنْهَا حَقَّهَا إِلاَّ إِذَا كَانَ يَومُ القِيَامَةِ صُفِّحَتْ لَهُ صَفَائِحُ مِنْ نَارٍ، فَأُحْمِيَ عَلَيْهَا في نَارِ جَهَنَّمَ ، فَيُكْوَى بِهَا جَنْبُهُ، وَجَبِينُهُ ، وَظَهْرُهُ، كُلَّمَا بَرَدَتْ أُعِيدَتْ لَهُ في يَومٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ ألْفَ سَنَةٍ ، حَتَّى يُقْضَى بَيْنَ العِبَادِ فَيَرَى سَبيلَهُ ، إمَّا إِلَى الجَنَّةِ ، وَإمَّا إِلَى النَّارِ )) قيل : يَا رسولَ الله ، فالإبلُ ؟ قَالَ : (( وَلاَ صَاحِبِ إبلٍ لا يُؤَدِّي مِنْهَا حَقَّهَا ، وَمِنْ حَقِّهَا حَلْبُهَا يَومَ وِرْدِهَا ، إِلاَّ إِذَا كَانَ يَومُ القِيَامَةِ بُطِحَ لَهَا بِقَاعٍ قَرْقَرٍ أوْفَرَ مَا كَانَتْ ، لاَ يَفْقِدُ مِنْهَا فَصيلاً وَاحِداً ، تَطَؤُهُ بِأخْفَافِهَا ، وَتَعَضُّهُ بِأفْوَاهِهَا ، كُلَّمَا مَرَّ عَلَيْهِ أُولاَهَا ، رُدَّ عَلَيْهِ أُخْرَاهَا ، في يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ ألْفَ سَنَةٍ ، حَتَّى يُقْضى بَيْنَ العِبَادِ ، فَيَرَى سَبِيلَهُ ، إمَّا إِلَى الجَنَّةِ ، وَإمَّا إِلَى النَّارِ )) قِيلَ : يَا رَسولَ اللهِ ، فَالبَقَرُ وَالغَنَمُ ؟ قَالَ : (( وَلاَ صَاحِبِ بَقَرٍ وَلاَ غَنَمٍ لاَ يُؤَدِّي مِنْهَا حَقَّهَا ، إِلاَّ إِذَا كَانَ يَوْمُ القِيَامَةِ ، بُطِحَ لَهَا بقَاعٍ قَرْقَرٍ ، لاَ يَفْقِدُ مِنْهَا شَيْئاً ، لَيْسَ فِيهَا عَقْصَاءُ ، وَلاَ جَلْحَاءُ ، وَلاَ عَضْبَاءُ ، تَنْطَحُهُ بقُرُونها ، وَتَطَؤُهُ بِأظْلاَفِهَا ، كُلَّمَا مرَّ عَلَيْهِ أُولاَهَا ، رُدَّ عَلَيْهِ أُخْرَاهَا ، في يَومٍ كَانَ مِقْدَارُهُ خَمْسِينَ ألْفَ سَنَة حَتَّى يُقْضى بَيْنَ العِبَادِ ، فَيَرى سَبيِلَهُ ، إمَّا إِلَى الجَنَّةِ ، وَإمَّا إِلَى النَّارِ )) قيل : يَا رسول الله فالخَيْلُ ؟ قَالَ : (( الخَيلُ ثَلاَثَةٌ : هِيَ لِرَجُلٍ وِزْرٌ ، وَهِيَ لِرَجُلٍ سِتْرٌ ، وَهِيَ لِرَجُلٍ أجْرٌ . فَأمَّا الَّتي هي لَهُ وِزْرٌ فَرَجُلٌ ربطها رِيَاءً وَفَخْراً وَنِوَاءً عَلَى أهْلِ الإسْلاَمِ ، فَهِيَ لَهُ وِزْرٌ ، وَأمَّا الَّتي هي لَهُ سِتْرٌ ، فَرَجُلٌ رَبَطَهَا في سَبيلِ الله ، ثُمَّ لَمْ يَنْسَ حَقَّ اللهِ في ظُهُورِهَا ، وَلاَ رِقَابِهَا ، فَهِيَ لَهُ سِتْرٌ ، وَأمَّا الَّتي هي لَهُ أجْرٌ ، فَرَجُلٌ رَبَطَهَا في سَبيلِ الله لأهْلِ الإسْلاَمِ في مَرْجٍ ، أَوْ رَوْضَةٍ فَمَا أكَلَتْ مِنْ ذَلِكَ المَرْجِ أَوْ الرَّوْضَةِ مِنْ شَيْءٍ إِلاَّ كُتِبَ لَهُ عَدَدَ مَا أَكَلَتْ حَسَنَات وكُتِبَ لَهُ عَدَدَ أرْوَاثِهَا وَأبْوَالِهَا حَسَنَات ، وَلاَ تَقْطَعُ طِوَلَهَا فَاسْتَنَّتْ شَرَفاً أَوْ شَرَفَيْنِ إِلاَّ كَتَبَ اللهُ لَهُ عَدَدَ آثَارِهَا ، وَأرْوَاثِهَا حَسَنَاتٍ ، وَلاَ مَرَّ بِهَا صَاحِبُهَا عَلَى نَهْرٍ ، فَشَرِبَتْ مِنْهُ ، وَلاَ يُرِيدُ أنْ يَسْقِيهَا إِلاَّ كَتَبَ اللهُ لَهُ عَدَدَ مَا شَرِبَتْ حَسَنَاتٍ )) قِيلَ : يَا رسولَ اللهِ فالحُمُرُ ؟ قَالَ : (( مَا أُنْزِلَ عَلَيَّ في الحُمُرِ شَيْءٌ إِلاَّ هذِهِ الآية الفَاذَّةُ الجَامِعَةُ : [ فَمَنْ يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْراً يَرَهُ وَمَنْ يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ شَرّاً يَرَهُ ] )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ مسلم
Kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna mwenye dhahabu na fedha, na hatoi haki yake, ila Siku ya Qiyaamah ataviringishwa mabamba ya moto. Atachomwa navyo ubavu wake, paji lake la uso na mgongo wake. kila yakipoa yatarudishwa katika siku kiasi chake ni miaka elfu hamsini, mpaka ihukumiwe baina ya waja, Waonyeshwe njia yao ima ya Peponi au ya Motoni. Pakasemwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, ngamia?" , Akasema: "Hata mwenye ngamia hatoi haki yake, na haki yake ni maziwa tangu siku ilipoanza kunywa maji. Vingenevyo atachomwa kwa uso wake Siku ya Qiyaamah katika wangwa mpana kuliko, Nagamia wake watakuwa wengi kama walivyokuwa na wamenona, Hakosekani hata mmoja, watamkanyanga kwa miguu yao na watamng'ata kwa meno yao. Wa mwisho akimaliza wa kwanza anaanza. Katika siku kiasi chake ni miaka hamsini elfu, hadi ihukumiwe baina ya waja, Ataona njia yake, ima ya Peponi au ya Motoni." Pakasemwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, ng'ombe na mbuzi?" Akasema: "Hata mwenye ng'ombe na mbuzi, hatoi haki zake, Siku ya Qiyaamah ni atarushwa kwa uso wake katika wangwa mpana kuliko, hakosekani hata mmoja, hakuna asiye na pembe. Watamrarua kwa pembe zao, kila wakimaliza wa kwanza wa mwisho atarudishwa, katika siku kiasi chake ni miaka elfu hamsini, mpaka ihukumiwe baina ya waja, na akaona njia yake ima ya Peponi au Motoni." Akaulizwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, mwenye farasi?" Akasema: "Farasi anafugwa kwa moja katika mambo matatu: Wao kwa baadhi ya watu ni njia ya kupata dhambi, na kwa wengine ni sitara na kwa wengine ni njia ya malipo. Ama ambaye anapata dhambi ni kwa yule mtu aliyemfunga kwa ajili ya kujionyesha na fakhari na kwa uadui kwa Waislamu, basi ufugaji huo ni dhambi kwake. Na ama ambaye kwake ni kwa sitara ni mtu aliyemfunga kwa ajili ya kupigania Dini ya Allaah, kisha asisahau haki ya Allaah kwa migongo yao na shingo zao, basi kwa ufugaji huo atapata maisha yake. Na ama ambaye atapata malipo (thawabu) ni mtu aliyemfunga farasi wake katika njia ya Allaah kwa sababu ya Waislamu, akafika katika malisho au bustani. Kwa hivyo anachokula katika malisho au bustani chochote ila huandikiwa idadi ya alichokula mema na pia huandikiwa idadi ya kinyesi chake na alama za kwato zake pia ni mema. Na wala hatakata kamba yaek ndefu na akaruka hatua moja au mbili isipokuwa Allaah humuandikia idadi ya hatua zake na kinyesi chake kuwa ni mema. Na wala hatakwenda naye katika mto na akanywa ndani yake na hakutaka kumnywesha basi kwa hilo Allaah humuandikia mema kwa idadi ya alicho kunywa. Akaulizwa: "Ee Rasuli wa Allaah! Je, mwenye punda?" Akasema: "Kuhusu punda sikuteremshiwa isipokuwa ayah hii yenye kukusanya aina yake: 'Basi yule atakayetenda kheri uzito wa chembe ataiona Na yule atakayetenda shari uzito wa chembe ataiona'." [Al-Zalzalah: 7-8] [Al-Bukhaariy na Muslim, na hii ni lafdhi ya Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب وجوب صوم رمضان
وبيان فضل الصيام وَمَا يتعلق بِهِ
38-Mlango Wa Wajibu wa Fungu na Kubainisha Fadhila za Fungu na Mambo Yanayohusiana Nayo
Alhidaaya.com [4]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ ﴿١٨٣﴾
Enyi walioamini! Mmefaridhishwa Swiyaam kama ilivyofaridhishwa kwa walio kabla yenu mpate kuwa na taqwa.
أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ ۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۚ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ ۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ ۚ وَأَن تَصُومُوا خَيْرٌ لَّكُمْ ۖ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٨٤﴾
(Swiyaam ni) Siku za kuhesabika. Lakini atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu, au yuko safarini, basi (inapaswa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo. Na kwa wale wanaoiweza lakini kwa mashaka na kutaabika watoe fidia kulisha masikini. Na atakayefanya kwa khiari yake jema lolote, basi hilo ni bora kwake. Na mkifunga Swiyaam ni bora kwenu mkiwa mnajua.
شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِي أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَىٰ وَالْفُرْقَانِ ۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ ۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَىٰ سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ ۗ ﴿١٨٥﴾
Mwezi wa Ramadhwaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan ili iwe mwongozo kwa watu na hoja bayana za mwongozo na pambanuo (la haki na batili). Basi atakayeshuhudia miongoni mwenu mwezi na afunge. Na atakayekuwa mgonjwa au safarini, basi (inapaswa kulipa) idadi sawa katika masiku mengineyo. [Al-Baqarah: 183-185]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( قَالَ اللهُ عَزَّ وَجَلَّ : كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ لَهُ إِلاَّ الصِّيَام ، فَإنَّهُ لِي وَأنَا أجْزِي بِهِ ، وَالصِّيَامُ جُنَّةٌ ، فَإذَا كَانَ يَومُ صَوْمِ أحَدِكُمْ فَلاَ يَرْفُثْ وَلاَ يَصْخَبْ فإنْ سَابَّهُ أحَدٌ أَوْ قَاتَلَهُ فَلْيَقُلْ: إنِّي صَائِمٌ . وَالذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَخُلُوفُ فَمِ الصَّائِمِ أطْيَبُ عِنْدَ اللهِ مِنْ رِيحِ المِسْكِ . لِلصَّائِمِ فَرْحَتَانِ يَفْرَحُهُمَا : إِذَا أفْطَرَ فَرِحَ بفطره ، وَإذَا لَقِيَ رَبَّهُ فَرِحَ بِصَوْمِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ روايةِ البُخَارِي .
وفي روايةٍ لَهُ : (( يَتْرُكُ طَعَامَهُ ، وَشَرَابَهُ ، وَشَهْوَتَهُ مِنْ أجْلِي ، الصِّيَامُ لي وَأنَا أجْزِي بِهِ ، وَالحَسَنَةُ بِعَشْرِ أمْثَالِهَا )) .
وفي رواية لمسلم : (( كُلُّ عَمَلِ ابْنِ آدَمَ يضاعَفُ ، الحسنةُ بِعَشْرِ أمْثَالِهَا إِلَى سَبْعِمِئَةِ ضِعْفٍ . قَالَ الله تَعَالَى : إِلاَّ الصَّوْمَ فَإنَّهُ لِي وَأنَا أجْزِي بِهِ ؛ يَدَعُ شَهْوَتَهُ وَطَعَامَهُ مِنْ أجْلِي . للصَّائِمِ فَرْحَتَانِ : فَرْحَةٌ عِنْدَ فِطْرِهِ ، وَفَرْحَةٌ عِنْدَ لِقَاءِ رَبِّهِ . وَلَخُلُوفُ فِيهِ أطْيَبُ عِنْدَ اللهِ مِنْ رِيحِ المِسْكِ )) .
Abu Huraiyrah amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Allaah Ta'aalaa amesema: Kila 'Ibadah ya mwanadamu ni yake isipokuwa funga, hiyo ni Yangu na Mimi Nitailipa. Funga ni kinga, na ikiwa mmoja wenu amefunga asiropoke, wala asifanye zogo, yeyote akimtukana au akimpiga, na aseme, 'Mimi nimefunga." Naapa kwa Ambaye nafsi ya Muhammad iko Mikononi Mwake, harufu ya kinywa cha mfungaji ni nzuri zaidi kwa Allaah kuliko harufu ya miski. Mfungaji ana furaha mbili anazofurahia; Anapofuturu anafurahi futari yake, na atakapo kutana na Rabb wake atafurahia funga yake." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy] Na hii ni lafdhi ya riwaayah ya Al-Bukhaariy.
Na katika riwaayah yake: "Anaacha chakula chake, kinywaji chake, na matamanio yake kwa ajili Yangu. Funga ni Yangu na Mimi Nitailipa na jema ni mara kumi mfano wake."
Na katika riwaayah ya Muslim: "Kila amali ya mwanadamu huzidishwa: Jema ni mara kumi hadi nyongeza mia saba. Amesema Allaah Ta'aalaa: 'Isipokuwa funga hiyo ni Yangu Nami nitailipa. Anaacha matamanio yake na chakula chake kwa ajili Yangu.' Mfungaji ana furaha mbili: Furaha anapofuturu na atakapo kutana na Rabb wake. Na harufu ya kinywa cha mfungaji ni nzuri zaidi mbele ya Allaah kuliko harufu ya miski."
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ أنْفَقَ زَوْجَيْنِ في سَبِيلِ اللهِ نُودِيَ مِنْ أبْوَابِ الجَنَّةِ ، يَا عَبْدَ اللهِ هَذَا خَيرٌ ، فَمَنْ كَانَ مِنْ أهْلِ الصَّلاَةِ دُعِيَ مِنْ بَابِ الصَّلاَةِ ، وَمَنْ كَانَ مِنْ أهْلِ الجِهَادِ دُعِيَ مِنْ بَابِ الجِهَادِ ، وَمَنْ كَانَ مِنْ أهْلِ الصِّيَامِ دُعِيَ مِنْ بَابِ الرَّيَّانِ ، وَمَنْ كَانَ مِنْ أهْلِ الصَّدَقَةِ دُعِيَ مِنْ بَابِ الصَّدَقَةِ )) قَالَ أَبُو بَكْرٍ رضي اللهُ عنه : بِأبي أنْتَ وَأُمِّي يَا رسولَ اللهِ ! مَا عَلَى مَنْ دُعِيَ مِنْ تِلْكَ الأَبْوَابِ مِنْ ضَرورةٍ ، فهل يُدْعى أحَدٌ مِنْ تِلْكَ الأبوَابِ كُلِّهَا ؟ فَقَالَ : (( نَعَمْ ، وَأرْجُو أنْ تَكُونَ مِنْهُمْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Atakaye toa vitu viwili katika njia ya Allaah, ataitwa kwenye milango ya Pepo, ee mtumwa wa Allaah, hii ni kheri. Atakayekuwa katika watu wa Swalaah, ataitwa katika mlango wa Swalaah, atakayekuwa katika watu wa Jihadi ataitwa katika mlango wa Jihaad na atakayekuwa katika watu wa funga ataitwa katika mlango wa Rayyan. Na atakayekuwa katika watu wa Swadaqah ataitwa katika mlango wa Swadaqah." Abu Bakar (Radhwiya Allaahu 'anhu) Akasema: "Fidia yako ni baba yangu na mam yangu, ee Rasuli wa Allaah hakuna dhara kwa atakayeitwa kwa milango yote. Je, kuna yeyote atakayeitwa milango hiyo yote?" Akasema: "Ndiyo na nataraji utakuwa miongoni mwa hao." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 3
وعن سهل بن سعد رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إنَّ في الجَنَّةِ بَاباً يُقَالُ لَهُ : الرَّيَّانُ ، يَدْخُلُ مِنْهُ الصَّائِمُونَ يَومَ القِيَامَةِ ، لاَ يَدْخُلُ مِنْهُ أحدٌ غَيْرُهُمْ ، يقال : أيْنَ الصَّائِمُونَ ؟ فَيَقُومُونَ لاَ يَدخُلُ مِنْهُ أَحَدٌ غَيْرُهُمْ ، فَإذَا دَخَلُوا أُغْلِقَ فَلَمْ يَدْخُلْ مِنْهُ أَحَدٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Sahl bin Sa'ad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika Peponi kuna mlango unaitwa Rayyan, wataingia katika mlango huo Siku ya Qiyaamah wafungaji na hataingia yeyote katika mlango huo asiyekuwa katika wao. Patasemwa, 'Wako wapi wafungaji?' Watasimama, na hatoingia katika mlango huo isipokuwa wao tu. Wakisha ingia utafungwa na haingii hapo yeyeote zaidi yao." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 4
وعن أَبي سعيد الخدري رضي اللهُ عنه، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ عَبْدٍ يَصُومُ يَوْماً في سَبِيلِ اللهِ إِلاَّ بَاعَدَ اللهُ بِذَلِكَ اليَوْمِ وَجْهَهُ عَنِ النَّارِ سَبْعِينَ خَرِيفَاً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Sa'iyd Al-Khudry (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna mja yeyote anafunga siku moja katika njia ya Allaah isipokuwa Allaah atauweka mbali uso wake na moto kwa hiyo siku aliyefunga, umbali wa safari ya miaka sabini." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ صَامَ رَمَضَانَ إيمَاناً وَاحْتِسَاباً ، غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kufunga Ramadhwaan hali ya kuwa na Imaani na kutarajia kupata thawabu husamehewa mtu huyo madhambi yaliyotangulia." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 6
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا جَاءَ رَمَضَانُ ، فُتِحَتْ أبْوَاب الجَنَّةِ ، وَغُلِّقَتْ أبْوَابُ النَّارِ ، وَصفِّدَتِ الشَّيَاطِينُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inapoingia Ramadhwaan, inafunguliwa milango ya Pepo na ianfungwa milango ya moto na wanafungwa mashetani minyororo." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 7
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: (( صُومُوا لِرُؤْيَتِهِ، وَأفْطِرُوا لِرُؤيَتِهِ، فَإنْ غَبِيَ عَلَيْكُمْ ، فَأكمِلُوا عِدَّةَ شَعْبَانَ ثَلاَثِينَ )) متفقٌ عَلَيْهِ ، وهذا لفظ البخاري .
وفي رواية لمسلم : (( فَإنْ غُمَّ عَلَيْكُمْ فَصُومُوا ثَلاَثِينَ يَوْماً )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu HUraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Fungeni kwa kuonekana kwake na kuleni kwa kuonekana kwake, na ukizibwa juu yenu na mawingu basi kamilisheni Sha'baan siku thalathini." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Na katika riwaayah ya Muslim: "Ikiwa haukuonekana kwenu basi fungeni siku thelathini."
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب الجود وفعل المعروف والإكثار من الخير
في شهر رمضان والزيادة من ذَلِكَ في العشر الأواخر منه
39-Mlango Wa Ukarimu na Kutenda Mema na Kuzidisha Mambo ya Kheri katika Mwezi wa Ramadhwaan na Kuongeza Hayo katika Kumi la Mwisho
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم أجْوَدَ النَّاسِ ، وَكَانَ أجْوَدَ مَا يَكُونُ في رَمَضَانَ حِيْنَ يَلْقَاهُ جِبْريلُ ، وَكَانَ جِبْريلُ يَلْقَاهُ في كُلِّ لَيْلَةٍ مِنْ رَمَضَانَ فَيُدَارِسُهُ القُرْآنَ ، فَلَرَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم ، حِيْنَ يَلْقَاهُ جِبرِيلُ أجْوَدُ بالخَيْرِ مِن الرِّيحِ المُرْسَلَةِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa mkarimu zaidi kwa watu katika mambo ya kheri na alikuwa mkarimu zaidi katika mwezi wa Ramadhwaan, wakati anapokutana na Jibriyl, Na Jibriyl alikuwa anakutana naye katika kila usiku wa Ramadhwaan na kumsomesha Qur-aan. Hivyo, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pindi alipokuw anakutana na Jibriyl alikuwa mkarimu zaidi katika mambo ya kheri kuliko upepo uliotumwa (pamoja na mvua) [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 2
وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ العَشْر أحْيَا اللَّيْلَ ، وَأيْقَظَ أهْلَهُ ، وَشَدَّ المِئْزَرَ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Zilipokuwa zinaanza siku kumi za mwisho katika mwezi wa Ramadhwaan Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anaswali usiku kucha na akiwaamsha familia yake na kukaza mkanda wake." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن تقدم رمضان بصوم بعد نصف
شعبان إِلاَّ لمن وصله بما قبله أَوْ وافق عادة لَهُ بأن كَانَ
عادته صوم الإثنين والخميس فوافقه
40-Mlango Wa Kukatazwa Kutanguliza Ramadhwaan kwa Kufunga Siku Moja Baada ya Nusu ya Sha'baan Isipokuwa kwa Yule Aliyekuwa na Ada ya Kufunga Jumatatu na Alkhamis
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَتَقَدَّمَنَّ أَحَدُكُم رَمَضَانَ بِصَوْمِ يَوْمٍ أَوْ يَوْمَيْنِ ، إِلاَّ أنْ يَكُونَ رَجُلٌ كَانَ يَصُومُ صَومَهُ ، فَليَصُمْ ذَلِكَ اليَوْمَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Asitangulize mmoja wenu Ramadhwaan kwa funga ya siku moja au siku mbili isipokuwa kama mtu anayo funga yake anayofunga na aifunge siku hiyo." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَصُومُوا قَبْلَ رَمضَانَ ، صُومُوا لِرُؤيَتِهِ ، وَأفْطِرُوا لِرُؤيَتِهِ ، فَإنْ حَالَتْ دُونَهُ غَيَايَةٌ فَأكْمِلُوا ثَلاثِينَ يَوْماً )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسنٌ صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Msifunge kabla ya Ramadhwaan, fungeni kwa kuonekena kwake (mwezi) na kuleni kwa kuonekana kwake. Ikiwa kuna mawingu (hivyo kutoonekana mwezi) basi kamilisheni siku thalathini." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا بَقِيَ نِصْفٌ مِنْ شَعْبَانَ فَلاَ تَصُومُوا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Inapobakia nusu ya Sha'baan basi musifunge." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 4
وعن أَبي اليقظان عمارِ بن يَاسِرٍ رضي الله عنهما ، قَالَ : مَنْ صَامَ اليَوْمَ الَّذِي يُشَكُّ فِيهِ ، فَقَدْ عَصَى أَبَا القَاسِمِ صلى الله عليه وسلم . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Amesema Abu Al-Yaqdhaan 'Ammaar bin Yaasir (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): "Mwenye kufunga siku yenye shaka amemuasi Abal Qaasim (yaani Nabiy Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب مَا يقال عند رؤية الهلال
41-Mlango Wa Kinachosemwa Wakati wa Kuona Mwezi Mwandamo
Alhidaaya.com [4]
عن طلحة بن عبيدِ اللهِ رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا رَأى الهلاَلَ ، قَالَ : (( اللَّهُمَّ أهِلَّهُ عَلَيْنَا بِالأمْنِ وَالإيمانِ ، وَالسَّلاَمَةِ وَالإسْلاَمِ ، رَبِّي وَرَبُّكَ اللهُ ، هِلالُ رُشْدٍ وخَيْرٍ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Kutoka kwake Twalhah bin 'Ubaydullaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anapoona mwezi mwandamo alikuwa akisema: "Allaahumma Ahillahu 'alaynaa Bil-amni wal Iymaan was Salaamati wal Islaam Rabbiy wa Rabbuka Allaah Hilaalu Rushdin wa khayr - Ee Mola wangu! tuandamishe kwa amani na Iymaan, usalama na Uislaamu. Rabb wako na Rabb wangu ni Allaah. Mwezi wa uongofu na kheri." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل السحور وتأخيره
مَا لَمْ يخش طلوع الفجر
42-Mlango Wa Fadhila za Kula Daku na Kuichelewesha Maadamu Hakutahofiwa Kuingia kwa Alfajiri
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أنس رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( تَسَحَّرُوا ؛ فَإنَّ في السُّحُورِ بَرَكَةً )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kuleni daku kwani ndani ya daku mna baraka." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An- Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن زيدِ بن ثابتٍ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : تَسَحَّرْنَا مَعَ رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، ثُمَّ قُمْنَا إِلَى الصَّلاَةِ . قِيلَ : كَمْ كَانَ بينهما ؟ قَالَ : قَدْرُ خَمْسين آيةً . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Zayd bin Thaabit (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikula daku pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kisha tukasimama kuswali. Akauliza: "Ni muda gani kati ya kula na kuswali?" Akasema: "Kiasi cha ayah hamsini." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وعن ابن عمر رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ لرسولِ الله صلى الله عليه وسلم مُؤَذِّنَانِ : بِلاَلٌ وَابْنُ أُمِّ مَكْتُومٍ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنْ بِلالاً يُؤَذِّنُ بِلَيْلٍ ، فَكُلُوا وَاشْرَبُوا حَتَّى يُؤَذِّنَ ابْنُ أُمِّ مَكْتُومٍ )) قَالَ : وَلَمْ يَكُنْ بَيْنَهُمَا إِلاَّ أنْ يَنْزِلَ هَذَا وَيَرْقَى هَذَا . متفقٌ عَلَيْهِ .
Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na waadhini wawili: Bilaal na Ibn Ummi Maktuwm. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akasema: "Hakika Bilaal anaadhini usiku, kwa hivyo kuleni na kunyweni mpaka aadhini Ibn Ummi Maktuwm." Akasema: "Na hakukuwa na tofauti baina yao ila kushuka huyu na kupanda huyu mwingine." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 4
وعن عمرو بن العاص رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( فَصْلُ مَا بَيْنَ صِيَامِنَا وصِيَامِ أهْلِ الكِتَابِ ، أكْلَةُ السَّحَرِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaahu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Tofauti baina ya funga yetu na ya Ahluk Kitaab (Waliopewa Kitabu) ni kula daku." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل تعجيل الفطر
وَمَا يفطر عَلَيْهِ ، وَمَا يقوله بعد الإفطار
43-Mlango Wa Fadhila za Kufuturu Mapema na Unachofuturia Nacho na Anachosema Mfungaji Baada ya Iftari
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن سهل بن سعد رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( لاَ يَزَالُ النَّاسُ بِخَيْرٍ مَا عَجَّلُوا الفِطْرَ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Sahl bin sa'ad (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Watu wataendelea kuwa katika kheri muda wa kuwa wanaharakisha kufuturu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي عطِيَّة ، قَالَ : دَخَلْتُ أنَا وَمَسْرُوقٌ عَلَى عائشة رضي الله عنها ، فَقَالَ لَهَا مَسْرُوق : رَجُلاَنِ مِنْ أصْحَابِ محَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم ، كِلاَهُمَا لا يَألُو عَنِ الخَيْرِ ؛ أحَدُهُمَا يُعَجِّلُ المَغْرِبَ وَالإفْطَارَ ، وَالآخَرُ يُؤَخِّرُ المَغْرِبَ وَالإفْطَارَ ؟ فَقَالَتْ : مَنْ يُعَجِّلُ المَغْرِبَ وَالإفْطَارَ ؟ قَالَ : عَبْدُ اللهِ - يعني : ابن مسعود - فَقَالَتْ : هكَذَا كَانَ رسولُ اللهِ يَصْنَعُ . رواه مسلم .
Amesema Abu 'Atiyyah: Tulikwenda mimi na Masruwq kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) Masruwq akamuuliza: "Watu wawili miongoni mwa Swahaaba wa Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), wote hawana kasoro katika kutenda mambo ya kheri. Mmoja wao anafanya haraka kuswali Maghrib na kufuturu na mwingine anachelewesha Maghrib na kufuturu?" Akauliza: "Ni nani anaye fanya haraka kuswali Maghrib na kufuturu?" Akajibu: " 'Abdullaah - yaani Ibn Mas'uwd." Akasema: "Hivyo ndivyo alivyokuwa akufanya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( قَالَ اللهُ عَزَّ وَجَلَّ : أحَبُّ عِبَادِي إلَيَّ أعْجَلُهُمْ فِطْراً )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Amesema Allaah 'Azza wa Jalla: Mja ninayempenda zaidi ni yule mwenye kuharakisha kufuturu." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 4
وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا أقْبَلَ اللَّيْلُ مِنْ هاهُنَا ، وَأدْبَرَ النهارُ مِنْ هَاهُنَا ، وَغَرَبَتِ الشَّمْسُ ، فَقَدْ أفْطَر الصَّائِمُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ukifika usiku kutokea hapa (yaani upande wa Mashariki) na mchana ukaondoka kutokea hapa (yaani upande wa Magharibi), na jua likazama mwenye kufunga amekwisha kufuturu." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 5
وعن أَبي إبراهيم عبدِ الله بنِ أَبي أوفى رضي الله عنهما ، قَالَ : سِرْنَا مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم ، وَهُوَ صَائِمٌ ، فَلَمَّا غَرَبَتِ الشَّمْسُ ، قَالَ لِبَعْضِ القَوْمِ : (( يَا فُلاَنُ انْزِلْ فَاجْدَحْ لَنَا )) ، فَقَالَ : يَا رسول الله ، لَوْ أمْسَيْتَ ؟ قَالَ : (( انْزِلْ فَاجْدَحْ لَنَا )) قَالَ : إنَّ عَلَيْكَ نَهَاراً ، قَالَ : (( انْزِلْ فَاجْدَحْ لَنَا )) قَالَ : فَنَزَلَ فَجَدَحَ لَهُمْ فَشَرِبَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم ، ثُمَّ قَالَ : (( إِذَا رَأَيْتُمُ اللَّيْلَ قَدْ أقْبَلَ مِنْ هاهُنَا ، فَقَدْ أفْطَرَ الصَّائِمُ )) وَأشَارَ بِيَدِهِ قِبَلَ المَشْرِقِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Amesema Abu Ibraahiym 'Abdillaah bin Abi Awfaa (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika safari, naye alikuwa amefunga, jua lilipozama aliwaambia baadhi ya watu: "Ee fulani! Terema utuchanganyie (sawiqa na maji)." Akasema: "Ee Rasuli wa Allaah! Lau kungekuchwa (yaani hakujaingia usiku)?" Akasema: "Teremka utuchanganyie." Akasema: "Hakika bado ni mchana." Akasema: "Teremka utuchanganyie." Akasema: "Akateremka akawachanganyia, akanywa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kisha akasema: "Mkiona usiku umekuja kutokea hapa basi mwenye kufunga amekwisha kufuturu." Akaashiria kwa mkono wake upande wa Mashariki." [Al-Bukhaariy, Muslim na Abu Daawuwd].
Hadiyth – 6
وعن سلمان بن عامر الضَّبِّيِّ الصحابي رضي الله عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا أفْطَرَ أحَدُكُمْ ، فَلْيُفْطِرْ عَلَى تَمْرٍ ، فَإنْ لَمْ يَجِدْ ، فَلْيُفْطِرْ عَلَى مَاءٍ ؛ فإنَّهُ طَهُورٌ )) رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Salmaan bin 'Aamir Adh-Dhibbiy, ambaye ni Swahaaba (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Alllahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Anapofuturu mmoja wenu basi afuturu kwa tende. Ikiwa hakupata tende basi afuturu kwa maji kwani hayo ni tohara." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 7
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُفْطِرُ قَبْلَ أنْ يُصَلِّي عَلَى رُطَبَاتٍ ، فَإنْ لَمْ تَكُنْ رُطَبَاتٌ فَتُمَيْرَاتٌ ، فَإنْ لَمْ تَكُنْ تُمَيْرَاتٌ حَسَا حَسَوَاتٍ مِنْ مَاءٍ . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Amesema Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akifuturu kabla ya kuswali kwa tende zilizo komaa, zikikosekana anafuturia tende zilizo wiva na zikikosekana anachukua maji kidogo." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب أمر الصائم بحفظ لسانه وجوارحه
عن المخالفات والمشاتمة ونحوها
44-Mlango Wa Amri kwa Mfungaji Kuhifadhi Ulimi Wake na Viungo Vyake kwa Kwenda Kinyume na Matusi na Mfano Wake
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا كَانَ يَوْمُ صَوْمِ أَحَدِكُمْ ، فَلاَ يَرْفُثْ وَلاَ يَصْخَبْ ، فَإنْ سَابَّهُ أحَدٌ أَوْ قَاتَلَهُ ، فَلْيَقُلْ : إنِّي صَائِمٌ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ikiwa mmoja wenu amefunga basi asiseme maneno machafu na wala asifanye zogo, kama yeyote (katika watu) ikatokea kumtukana au kupigana naye na aseme, 'Mimi nimefunga'." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ النبيُّ صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ لَمْ يَدَعْ قَوْلَ الزُّورِ وَالعَمَلَ بِهِ فَلَيْسَ للهِ حَاجَةٌ في أنْ يَدَعَ طَعَامَهُ وَشَرَابَهُ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Yeyote ambaye hataacha maneno ya uwongo na matendo machafu, Allaah hana haja kuacha kwake chakula na kinywaji." [Al-Bukhaariy].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب في مسائل من الصوم
45-Mlango Wa Masuala ya Fungu
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( إِذَا نَسِيَ أَحَدُكُمْ ، فَأكَلَ ، أَوْ شَرِبَ ، فَلْيُتِمَّ صَوْمَهُ ، فَإنَّمَا أطْعَمَهُ اللهُ وَسَقَاهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kama atasahau mmoja wenu akala na akanywa, basi na akamilishe funga yake, kwani Allaah Ndiye Aliyemlisha na ndiye Aliyemnywesha." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]
Hadiyth – 2
وعن لَقِيط بن صَبِرَةَ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قُلْتُ : يَا رسول الله ، أخْبِرْني عَنِ الوُضُوءِ ؟ قَالَ : (( أسْبغِ الوُضُوءَ ، وَخَلِّلْ بَيْنَ الأَصَابِعِ ، وَبَالِغْ في الاسْتِنْشَاقِ ، إِلاَّ أنْ تَكُونَ صَائِماً )) رواه أَبُو داود والترمذي، وقال : (( حديث حسن صحيح )).
Laqiytw bin Swabirah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Niliuliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Nielezee kuhusu wudhuu?" Akasema: "Kamilisha wudhuu na safisha mashina ya vidole vyako na zidisha katika kupandisha maji puani ila utakapokuwa umefunga." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 3
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُدْرِكُهُ الفَجْرُ وَهُوَ جُنُبٌ مِنْ أهْلِهِ ، ثُمَّ يَغْتَسِلُ وَيَصُومُ . متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anafikiwa na Alfajiri hali ana janaba baada ya kujamiiana na mkewe, kisha anaoga na anaendelea na funga." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na Abu Daawuwd]
Hadiyth – 4
وعن عائشة وأم سلمة رضي الله عنهما ، قالتا : كَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يُصْبحُ جُنُباً مِنْ غَيْرِ حُلُمٍ ، ثُمَّ يَصُومُ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Wamesema 'Aaishah na Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akipambazukiwa katika hali ya janaba bila ya kuwa ameota (kwa kujamiiana na mkewe), kisha anafunga." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل صوم المحرم وشعبان والأشهر الحرم
46-Mlango Wa Kubainisha Fadhila ya Kufunga ya Mwezi wa Muharram na Sha'baan na Miezi Mitukufu
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( أفْضَلُ الصِّيَامِ بَعْدَ رَمَضَانَ : شَهْرُ الله المُحَرَّمُ ، وَأفْضَلُ الصَّلاَةِ بَعدَ الفَرِيضَةِ : صَلاَةُ اللَّيْلِ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Funga bora baada ya Ramadhwaan ni mwezi wa Allaah Muharram. Na Swalaah bora baada ya faradhi ni Swalaah ya usiku." [Muslim]
Hadiyth – 2
عن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : لَمْ يكن النبي صلى الله عليه وسلم يَصُومُ مِنْ شَهْرٍ أكْثَرَ مِنْ شَعْبَانَ ، فَإنَّهُ كَانَ يَصُومُ شَعْبَانَ كُلَّهُ .
وفي رواية : كَانَ يَصُومُ شَعْبَانَ إِلاَّ قَلِيلاً . متفقٌ عَلَيْهِ .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anha) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema hakuwa anafunga mwezi zaidi kuliko Sha'baan kwani alikuwa anafunga Sha'baan yote.
Na katika riwaayah nyingine: Alikuwa akifunga Sha'baan isipokuwa kwa siku chache. [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 3
وعن مُجِيبَةَ البَاهِليَّةِ ، عن أبيها أَوْ عمها : أنه أتى رسولَ اللهِ رضي اللهُ عنه ، ثُمَّ انطَلَقَ فَأَتَاهُ بَعْدَ سَنَةٍ – وَقَدْ تَغَيَّرَتْ حَالُهُ وَهيئَتُهُ – فَقَالَ : يَا رسولَ الله ، أمَا تَعْرِفُنِي ؟ قَالَ : (( وَمَنْ أنْتَ )) ؟ قَالَ : أَنَا الباهِليُّ الَّذِي جِئْتُك عام الأَوَّلِ . قَالَ : (( فَمَا غَيَّرَكَ ، وَقَدْ كُنْتَ حَسَنَ الهَيْئَةِ ! )) قَالَ : مَا أكَلْتُ طَعَاماً مُنْذُ فَارقتُكَ إِلاَّ بِلَيْلٍ . فَقَالَ رسولُ اللهِ رضي اللهُ عنه : (( عَذَّبْتَ نَفْسَكَ ! )) ثُمَّ قَالَ : (( صُمْ شَهْرَ الصَّبْرِ ، وَيَوماً مِنْ كُلِّ شَهْرٍ )) قَالَ : زِدْنِي ، فَإنَّ بِي قُوَّةً ، قَالَ : (( صُمْ يَوْمَيْن )) قَالَ : زِدْنِي ، قَالَ : (( صُمْ ثَلاثَةَ أيَّامٍ )) قَالَ : زِدْنِي ، قَالَ : (( صُمْ مِنَ الحُرُم وَاتركْ ، صُمْ مِنَ الحُرُمِ وَاتركْ ، صُمْ مِنَ الحُرُمِ وَاتركْ )) وقال بأصابِعه الثَّلاثِ فَضَمَّها ، ثُمَّ أرْسَلَهَا . رواه أَبُو داود .
Kutoka kwa Mujiyban Al-Baahiliyyah na kutoka kwa Babake au ami yake amesema: Alikuja kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), kisha akaondoka, akamjia baada ya mwaka - hali na umbo lake limebadilika. Akasaema: "Ee Rasuli wa Allaah! Hujanitambua?" Akasema (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Na wewe ni nani?" Akasema: "Mimi ni Al-Bukhaariy nilikuja mwaka uliopita." Akasema: "Na ni kitu gani kimekubadilisha na ulikuwa mzuri wa umbo?", Akajibu: "Sijala chakula tangu nilipoachana nawe, isipokuwa usiku tu." Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Akamwambia: "Umeiadhibu nafsi yako!" Kisha akamwambia: "Funga mwezi wa subira, na siku moja kila mwezi." Akasema: "Niongezee" akasema: "Funga siku tatu." Akasema: "Nizidihsie." Akamwambia: "Funga miezi mitukufu na uchache, funga, funga miezi mitukufu na uchache kufunga." Alisema kwa vidole vyake mara tatu, akavikunja, kisha akaviacha." [Abu Daawuwd]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل الصوم وغيره في العشر الأول من ذي الحجة
47-Mlango Wa Fadhila za Funga na Nyenginezo katika Kumi la Kwanza la Mwezi wa Dhul Hijjah
Alhidaaya.com [4]
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَا مِنْ أيَّامٍ ، العَمَلُ الصَّالِحُ فِيهَا أحَبُّ إِلَى اللهِ مِنْ هذِهِ الأَيَّام )) يعني أيام العشر . قالوا : يَا رسولَ اللهِ ، وَلاَ الجِهَادُ في سَبيلِ اللهِ ؟ قَالَ : (( وَلاَ الجِهَادُ فِي سَبِيلِ اللهِ ، إِلاَّ رَجُلٌ خَرَجَ بِنَفْسِهِ وَمَالِهِ ، فَلَمْ يَرْجِعْ مِنْ ذَلِكَ بِشَيءٍ )) رواه البخاري .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakuna siku yeyote ambayo matendo mema humpendezea zaidi Allaah kuliko ndani ya siku hizi", yaani anakusudia siku kumi (za mwanzo za mwezi wa Dhul Hijjah). Wakasema: "Ee Rasuli wa Allaah, wala Jihadi katika njia ya Allaah?" Akasema: "Wala Jihadi katika njia ya Allaah isipokuwa mtu ametoka pamoja na nafsi na mali yake halafu asirudi na chochote." [Al-Bukhaariy]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل صوم يوم عرفة وعاشوراء وتاسوعاء
48-Mlango Wa Fadhila za Funga ya Arafah na 'Aashuuraa' na Ta'suu'aa
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه، قَالَ : سُئِلَ رسول الله صلى الله عليه وسلم عن صَومِ يَوْمِ عَرَفَةَ ، قَالَ : (( يُكَفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيَةَ وَالبَاقِيَةَ )) رواه مسلم .
Amesema Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Aliulizwa kuhusu funga ya siku ya Arafah. Akasema: "Hufuta madhambi ya mwaka uliopita na ujao." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن ابن عباس رضي الله عنهما : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم صَامَ يَومَ عاشوراءَ وَأمَرَ بِصِيامِهِ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifunga siku ya 'Aashuwraa' na akawaamuru watu wafunge (siku hiyo)." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 3
وعن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم سُئِلَ عَنْ صِيامِ يَوْمِ عَاشُوراءَ، فَقَالَ : (( يُكَفِّرُ السَّنَةَ المَاضِيَةَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu funga ya 'Aashuwraa', akasema: "Inafuta madhambi ya mwaka uliopita." [Muslim]
Hadiyth – 4
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لَئِنْ بَقِيتُ إِلَى قَابلٍ لأَصُومَنَّ التَّاسِعَ )) رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Nikibakia mpaka mwaka ujao nitafunga tarehe tisa (yaani katika mwezi wa Muharram, nayo inaitwa Ta'suw'aa)." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب صوم ستة أيام من شوال
49-Mlango Wa Kupendeza Kufunga Siku Sita za Shawwaal
Alhidaaya.com [4]
عن أَبي أيوب رضي اللهُ عنه : أنَّ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ صَامَ رَمَضَانَ ثُمَّ أتْبَعَهُ سِتّاً مِنْ شَوَّالٍ ، كَانَ كَصِيَامِ الدَّهْرِ )) رواه مسلم .
Abu Ayyub (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kufunga mwezi wa Ramadhwaan na akafuatiliza siku sita za Shawwaal (Mfungo Mosi) anakuwa ni kama aliyefunga milele." [Muslim]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب صوم الإثنين والخميس
50-Mlango Wa Kupendeza Kufunga Jumatatu na Alkhamis
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن أَبي قتادة رضي اللهُ عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم سُئِلَ عَنْ صَومِ يَوْمِ الإثْنَيْنِ ، فَقَالَ : (( ذَلِكَ يَومٌ وُلِدْتُ فِيهِ ، وَيَومٌ بُعِثْتُ ، أَوْ أُنْزِلَ عَلَيَّ فِيهِ )) رواه مسلم .
Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa kuhusu funga ya Jumatatu, akasema: "Hiyo ni siku niliyozaliwa na ni siku niliyopewa Utume au niliyoteremshiwa Wahyi nadani yake." [Muslim]
Hadiyth – 2
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( تُعْرَضُ الأَعْمَالُ يَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيسِ ، فَأُحِبُّ أنْ يُعْرَضَ عَمَلِي وَأنَا صَائِمٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) ، ورواه مسلم بغير ذِكر الصوم .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kwa hakika matendo ya waja huonyeshwa siku ya Jumatatu na Alkhamisi, hivyo napenda amali zangu zionyeshwe nami nikiwa nimefunga." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan], Na ameipokea Muslim bila kutaja funga.
Hadiyth – 3
وعن عائشة رَضِيَ اللهُ عنها ، قالت : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَتَحَرَّى صَومَ الإثْنَيْنِ وَالخَمِيس . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ameema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa akifunga sana siku ya Jumatatu na Alkhamisi. [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب استحباب صوم ثلاثة أيام من كل شهر
51-Mlango Wa Kupendeza Kufunga Siku Tatu Kila Mwezi
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
وعن أَبي هريرة رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أوْصاني خَلِيلي صلى الله عليه وسلم بِثَلاثٍ : صِيَامِ ثَلاَثَةِ أيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ، وَرَكْعَتَي الضُّحَى ، وَأنْ أُوتِرَ قَبْلَ أنْ أنَامَ . متفقٌ عَلَيْهِ .
Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameniusia vitu vitatu, nisiviache mpaka ninakufa: "Kufunga siku tatu kila mwezi, kuswali Swalaah ya Dhuwhaa na kulala baada ya kuswali Witri." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy]
Hadiyth – 2
وعن أَبي الدرداءِ رضي اللهُ عنه ، قَالَ : أوصاني حَبِيبـي صلى الله عليه وسلم بِثَلاثٍ لَنْ أدَعَهُنَّ مَا عِشتُ : بِصِيَامِ ثَلاثَةِ أيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ، وَصَلاَةِ الضُّحَى ، وبِأنْ لاَ أنَامَ حَتَّى أُوتِرَ . رواه مسلم .
Amesema Abu Dardaa (Radhwiya Allaahu 'anhu): Amenisusia kipenzi changu (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kushikamana na vitu vitatu nami sitaacha maadamu ni hai: "Kufunga siku tatu kila mwezi, na kuswali Swalaah ya Dhuwhaa na nisilale mpaka niswali Witri." [Muslim]
Hadiyth – 3
وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( صَوْمُ ثَلاَثَةِ أيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ صَوْمُ الدَّهْرِ كُلِّهِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
'Abdillaah bin 'Amruw bin Al-'Aas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Kufunga siku tatu katika kila mwezi ni sawa na funga ya milele." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن مُعاذة العدوية : أنها سألت عائشةَ رَضِيَ اللهُ عنها : أكَانَ رسول الله صلى الله عليه وسلم يَصُومُ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ثَلاَثة أيَّامٍ ؟ قالت : نَعَمْ . فقلتُ : مِنْ أيِّ الشَّهْرِ كَانَ يَصُومُ ؟ قالت : لَمْ يَكُنْ يُبَالِي مِنْ أيِّ الشَّهْرِ يَصُومُ . رواه مسلم .
Mu'aadhah Al-'Adawiyyah alimuuliza 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): "Je, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anafunga siku tatu kila mwezi?" Akasema: "Ndio." Nikamuuliza: "Alikuwa akifunga katika mwezi gani?" Akasema: "Alikuwa hajali ni katika mwezi gani aliokuwa akifunga." [Muslim]
Hadiyth – 5
وعن أَبي ذر رضي اللهُ عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إِذَا صُمْتَ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاَثاً، فَصُمْ ثَلاَثَ عَشْرَةَ، وَأرْبَعَ عَشْرَةَ ، وَخَمْسَ عَشْرَةَ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Unapofunga siku tatu katika kila mwezi basi funga tarehe kumi na tatu (13), na kumi na nne (14) na kumi na tano (15)." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 6
وعن قتادة بن مِلْحَان رضي اللهُ عنه ، قَالَ : كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَأمُرُنَا بِصِيَامِ أيَّامِ البِيضِ : ثَلاثَ عَشْرَةَ ، وَأرْبَعَ عَشْرَةَ ، وَخَمْسَ عَشْرَةَ . رواه أَبُو داود .
Qataadah bin Milhaan (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anatuamuru tufunge siku Nyeupe: Tarehe kumi na tatu (13), na kumi na nne (14) na kumi na tano (15)." [Abu Daawuwd]
Hadiyth – 7
وعن ابن عباس رضي الله عنهما ، قَالَ : كَانَ رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم لاَ يُفْطِرُ أيَّامَ البِيضِ في حَضَرٍ وَلاَ سَفَرٍ . رواه النسائي بإسنادٍ حسن .
Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alikuwa hali katika siku Nyeupe akiwa mjini wala safarini." [An-Nasaaiy kwa Isnaad iliyo Hasan]
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب فضل من فطَّر صائماً وفضل الصائم
الذي يؤكل عنده ودعاء الآكل للمأكول عنده
52-Mlango Wa Fadhila za Mwenye Kumfuturisha Aliye Funga na Fadhila za Mfungaji Ambaye Watu Wanakula Kwake na Duaa ya Mwalikwa kwa Mwalikaji
Alhidaaya.com [4]
Hadiyth – 1
عن زيد بن خالد الجُهَنِيِّ رضي اللهُ عنه ، عن النبي صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( مَنْ فَطَّرَ صَائِماً ، كَانَ لَهُ مِثْلُ أجْرِهِ ، غَيْرَ أنَّهُ لاَ يُنْقَصُ مِنْ أجْرِ الصَّائِمِ شَيْءٌ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Zayd bin Khaalid Al-Juhaniyy amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kumfuturisha mfungaji anapata thawabu mfano wa thawabu zake bila mfungaji kupunguziwa chochote katika thawabu zake." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 2
وعن أُمِّ عُمَارَةَ الأنصارِيَّةِ رَضِيَ اللهُ عنها : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم دَخَلَ عَلَيْهَا ، فَقَدَّمَتْ إِلَيْهِ طَعَاماً ، فَقَالَ : (( كُلِي )) فَقَالَتْ : إنِّي صَائِمَةٌ ، فَقَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إنَّ الصَائِمَ تُصَلِّي عَلَيْهِ المَلاَئِكَةُ إِذَا أُكِلَ عِنْدَهُ حَتَّى يَفْرغُوا )) وَرُبَّمَا قَالَ : (( حَتَّى يَشْبَعُوا )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) .
Imepokewa kwa Ummi 'Umarah Al-Answaariyyah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimtembelea naye akamkaribisha kwa kumuwekea chakula. Akasema: "Kula." Akasema: "Hakika mimi nimefunga." Hapo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: "Hakika Malaaika wanamuombea aliyefunga kinapoliwa chakula mbele yake mpaka mwenye kula aondoke", na huenda alisema: "Mpaka ashibe." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]
Hadiyth – 3
وعن أنسٍ رضي اللهُ عنه : أنَّ النبيَّ صلى الله عليه وسلم جَاءَ إِلَى سعد بن عبادة رضي اللهُ عنه فَجَاءَ بِخُبْزٍ وَزَيْتٍ ، فَأكَلَ ، ثُمَّ قَالَ النبي صلى الله عليه وسلم : (( أفْطَرَ عِنْدَكُمُ الصَّائِمُونَ ؛ وَأكَلَ طَعَامَكُمُ الأَبرَارُ ، وَصَلَّتْ عَلَيْكُمُ المَلاَئِكَةُ )) رواه أَبُو داود بإسناد صحيح .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikwenda kwa Sa'ad bin 'Ubaadah (Radhwiya allahu 'anhu), naye akamletea mkate na mafuta na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akala hicho chakula, kisha akasema: "Aftwara 'indakumus Swaa'imuuna wa akala twa'aamakumul Abraar wa Swallat 'alaykumul Malaaikah - Wamefuturu kwenu walio funga na watu wema wamekula chakula chenu na Malaaika wamewaombea nyinyi maghfira." [Abu Daawuwd kwa Isnaad iliyo Swahiyh]
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/280
[2] http://www.alhidaaya.com/sw/
[3] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10322&title=08-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Kitabu%20Cha%20Fadhila%20Mbalimbali%20-%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%92%D9%81%D9%8E%D8%B6%D8%A7%D8%A6%D9%90%D9%84
[4] http://www.alhidaaya.com/
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11094&title=01-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Kusoma%20Qur-aan
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11096&title=02-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuchunga%20Qur-aan%20na%20Kutahadharishwa%20Kupelekea%20Kwenye%20Kuisahau
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11097&title=03-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendekezwa%20Kusoma%20Qur-aan%20kwa%20Sauti%20Nzuri%20na%20Kutaka%20Isomwe%20na%20Mtu%20Mwenye%20Sauti%20Nzuri%20na%20Kumsikiliza
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11098&title=04-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimiza%20Kusoma%20Suwrah%20na%20Ayah%20Maalumu
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11099&title=05-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kukusanyika%20kwa%20Ajili%20ya%20Kusoma
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11100&title=06-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Wudhuu
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11101&title=07-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Adhaan
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11102&title=08-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20Za%20Swalaah
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11103&title=09-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20Ya%20Swalaah%20Ya%20Asubuhi%20Na%20Alasiri
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11105&title=10-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20Ya%20Kwenda%20Msikitini
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11106&title=11-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20Wa%20kungojea%20Swalaah
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11152&title=12-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20ya%20Swalah%20ya%20Jamaa
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11153&title=13-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimiza%20Kuhudhuria%20Jamaa%20Katika%20Swalah%20ya%20Asubuhi%20na%20Ishaa
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11154&title=14-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Amri%20ya%20Kuhifadhi%20Swalah%20za%20Faradhi%20na%20Onyo%20Kali%20kwa%20Kuziacha
[19] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11195&title=15-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Safu%20ya%20Kwanza%20na%20Amri%20ya%20Kutimiza%20Safu%20ya%20Kwanza%20na%20Kuzinyoosha
[20] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11196&title=16-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Swalaah%20za%20Sunnah%20Rawatib%20Pamoja%20na%20Faradhi%20na%20Kubainisha%20Uchache%20na%20Utimilifu%20Wake%20na%20Zilizo%20Baina%20Yake
[21] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11197&title=17-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimiza%20Rak%27ah%20Mbili%20za%20Sunnah%20ya%20Asubuhi
[22] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11198&title=18-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kufanya%20Nyepesi%20Rak%27ah%20Mbili%20za%20Alfajiri%20na%20Kubainisha%20Kinachosomwa%20na%20Wakati%20Wake
[23] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11199&title=19-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kujilaza%20Baada%20ya%20Rak%27ah%20Mbili%20za%20Alfajiri%20kwa%20Ubavu%20Wake%20wa%20Kulia%20na%20Kuhimizwa%20Sawa%20Ikiwa%20ni%20Tahajjud%20Au%20La
[24] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11200&title=20-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20ya%20Adhuhuri
[25] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11201&title=21-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20za%20Alasiri
[26] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11202&title=22-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Swalaah%20ya%20Sunnah%20Kabla%20na%20Baada%20ya%20Maghrib
[27] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11203&title=23-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20Kabla%20na%20Baada%20ya%20Swalaah%20ya%20Ishaa
[28] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11204&title=24-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Sunnah%20ya%20Ijumaa
[29] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11205&title=25-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kuswali%20Sunnah%20Nyumbani%20Sawa%20ni%20Zile%20Zilizohimizwa%20au%20Nyinginezo%20na%20Maagizo%20ya%20Kubadilisha%20Sehemu%20Uliyoswali%20Swalaah%20ya%20Faradhi%20au%20Kupambanua%20Baina%20yao%20kwa%20Mazungumzo
[30] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11206&title=26-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimiza%20Kuswali%20Witri%20na%20Kubainisha%20Kuwa%20Hiyo%20ni%20Sunnah%20Muakkadah%20na%20Kubainisha%20Wakati%20Wake
[31] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11207&title=27-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Swalaah%20ya%20Dhuwhaa%20na%20Kubainisha%20Uchache%2C%20Wingi%2C%20Wastani%20Wake%20na%20Kuhimizwa%20katika%20Kuihifadhi
[32] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11208&title=28-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kufaa%20Swalaah%20ya%20Dhuwhaa%20Kuanzia%20Linaponyanyuka%20Jua%20Mpaka%20Kupinduka%20%28Zawaal%29%2C%20na%20Bora%20ni%20Kuiswali%20Wakati%20Jua%20Linapokuwa%20Kali
[33] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11209&title=29-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kuhimizwa%20Swalaah%20ya%20Tahiyyatul%20Masjid%20kwa%20Rak%27ah%20Mbili%20na%20Ukaraha%20wa%20Kukaa%20Kabla%20ya%20Kuziswali%20katika%20Wakati%20Wowote%20Anapoingia
[34] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11210&title=30-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kuswali%20Rak%27ah%20Mbili%20Baada%20Wudhuu
[35] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11211&title=31-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Siku%20ya%20Ijumaa%20na%20Wajibu%20wa%20Kuoga%20Kwayo%20na%20Kujipaka%20Manukato%2CKwenda%20Mapema%2CKuomba%20Dua%20Siku%20ya%20Ijumaa%2C%20Kumswalia%20Nabiy%20na%20Kubainisha%20Wakati%20wa%20Kujibiwa%20Dua%2CKupendeza%20Kukithirisha%20Kumtaja%20Allaah%20Baada%20ya%20Ijumaa
[36] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11212&title=32-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kusujudu%20Sijda%20ya%20Kushukuru%20%28Sijdatus-Shukr%29%20Unapopata%20Neema%20ya%20Wazi%20au%20Kuondokewa%20na%20Balaa
[37] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11213&title=33-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ubora%20wa%20Kisimamo%20cha%20Usiku
[38] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11214&title=34-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kuswali%20Swalaah%20ya%20Ramadhwaan%20Nayo%20ni%20Tarawehe
[39] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11215&title=35-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Kisimamo%20cha%20Usiku%20wa%20Qadr%20%28Cheo%20Kitukufu%29%20na%20Kubainisha%20Usiku%20Unaotarajiwa
[40] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11216&title=36-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Kupiga%20Mswaki%20na%20Mambo%20ya%20Kimaumbile
[41] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11217&title=37-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kusisitizwa%20Wajibu%20wa%20Zakaah%20na%20Kubainisha%20Fadhila%20Zake%20na%20Mambo%20Yanayohusiana%20Nayo
[42] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11218&title=38-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Wajibu%20wa%20Fungu%20na%20Kubainisha%20Fadhila%20za%20Fungu%20na%20Mambo%20Yanayohusiana%20Nayo
[43] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11219&title=39-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukarimu%20na%20Kutenda%20Mema%20na%20Kuzidisha%20Mambo%20ya%20Kheri%20katika%20Mwezi%20wa%20Ramadhwaan%20na%20Kuongeza%20Hayo%20katika%20Kumi%20la%20Mwisho
[44] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11220&title=40-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kutanguliza%20Ramadhwaan%20kwa%20Kufunga%20Siku%20Moja%20Baada%20ya%20Nusu%20ya%20Sha%27baan%20Isipokuwa%20kwa%20Yule%20Aliyekuwa%20na%20Ada%20ya%20Kufunga%20Jumatatu%20na%20Alkhamis
[45] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11221&title=41-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kinachosemwa%20Wakati%20wa%20Kuona%20Mwezi%20Mwandamo
[46] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11222&title=42-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Kula%20Daku%20na%20Kuichelewesha%20Maadamu%20Hakutahofiwa%20Kuingia%20kwa%20Alfajiri
[47] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11223&title=43-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Kufuturu%20Mapema%20na%20Unachofuturia%20Nacho%20na%20Anachosema%20Mfungaji%20Baada%20ya%20Iftari
[48] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11224&title=44-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Amri%20kwa%20Mfungaji%20Kuhifadhi%20Ulimi%20Wake%20na%20Viungo%20Vyake%20kwa%20Kwenda%20Kinyume%20na%20Matusi%20na%20Mfano%20Wake
[49] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11225&title=45-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Masuala%20ya%20Fungu
[50] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11226&title=46-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kubainisha%20Fadhila%20ya%20Kufunga%20ya%20Mwezi%20wa%20Muharram%20na%20Sha%27baan%20na%20Miezi%20Mitukufu
[51] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11227&title=47-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Funga%20na%20Nyenginezo%20katika%20Kumi%20la%20Kwanza%20la%20Mwezi%20wa%20Dhul%20Hijjah
[52] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11228&title=48-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Funga%20ya%20Arafah%20na%20%27Aashuuraa%27%20na%20Ta%27suu%27aa
[53] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11229&title=49-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kufunga%20Siku%20Sita%20za%20Shawwaal
[54] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11230&title=50-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kufunga%20Jumatatu%20na%20Alkhamis
[55] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11231&title=51-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kupendeza%20Kufunga%20Siku%20Tatu%20Kila%20Mwezi
[56] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11232&title=52-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Fadhila%20za%20Mwenye%20Kumfuturisha%20Aliye%20Funga%20na%20Fadhila%20za%20Mfungaji%20Ambaye%20Watu%20Wanakula%20Kwake%20na%20Duaa%20ya%20Mwalikwa%20kwa%20Mwalikaji