كِتابُ الْحَجّ وَالْعُمْرَة
Kitabu Cha Hajj Na 'Umrah
Abu Maalik Kamaal Bin As-Sayyid Saalim
Imetarjumiwa na 'Abdullaah Mu'aawiyah (Abu Baasim)
Alhidaaya.com
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
01-Taarifu Ya Hajj
Alhidaaya.com [3]
Asili ya maana ya Al-Hajji (الحجُّ) katika lugha, ni kukusudia. Ni kwa kufatahisha “Haa”, na inajuzu kwa kasrah “Al-Hijju”, nayo ni nadra sana. Inasemekana kuwa inatokana na neno lako: (حججتُه) unapomwendea mtu mara kwa mara. Na inasemekana kuwa kinyume na hilo, na la kwanza ndilo mashuhuri. [Taaj Al-‘Aruws na Al-Majmuw’u (7/7)]
Ama katika istilahi ya kisharia, ni kuikusudia Nyumba Tukufu ya Allaah na Maeneo Maalum ya Kutekelezea amali na ‘ibaadah maalum za Hajji katika wakati maalum, na kwa namna maalum.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
02-Hukmu Ya Hajj
Alhidaaya.com [3]
Hajj ni Fardhi ‘Ayn kwa kila aliyebaleghe na mwenye uwezo mara moja katika umri wote. Ni nguzo katika nguzo za Kiislamu, na ufaradhi wake umethibiti katika Qur-aan, Sunnah na Ijma’a.
(a) Katika Qur-aan
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anasema:
((وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ))
((Na kwa ajili ya Allaah imewajibika watu watekeleze Hajj katika Nyumba hiyo kwa mwenye uwezo. Na atakayekufuru, basi hakika Allaah ni Mkwasi kwa walimwengu)). [Aal-‘Imraan (3:97)]
(b) Katika Sunnah
Kuna Hadiyth nyingi sana zilizosimuliwa – zilizofikia mpaka wa Tawaatur - zinazoelezea uyakini na elimu isiyo na shaka yoyote kuhusu kuthibiti Faradhi hii. [Angalia: At-Targhiyb na At-Tarhiyb (2/211)]
Kati ya Hadiyth hizo ni:
1- Ya Ibn ‘Umar kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((بُني الإسلام على خمس: شهادة أن لا إله إلا الله وأن محمدًا رسول الله، وإقام الصلاة، وإيتاء الزكاة، والحج، وصوم رمضان))
((Uislamu umejengwa juu ya (nguzo) tano: Kushahadia kwamba hapana mungu isipokuwa Allaah, na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah, kusimamisha Swalaah, kutoa Zakaah, Hajj na kufunga Ramadhwaan)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (8), Muslim (16) na wengineo]
2- Ya Abu Hurayrah aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitukhutubia akasema:
((يا أيها الناس، قد فرض الله عليكم الحج فحجوا)) ، فقال رجل: أكل عام يا رسول الله؟ فسكت حتى قالها ثلاثا، فقال رسول الله: ((لو قلت نعم لوجبت، ولما استطعتم...))
((Enyi watu! Hakika Allaah Amewafaradhishieni Hajj, basi hijini)). Mtu mmoja akasema: Je, ni kila mwaka ee Rasuli wa Allaah! Akanyamaza mpaka akaliuliza mara tatu. Rasuli wa Allaah akasema: ((Ningelisema na’am basi ingekuwa lazima, na msingeliweza…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1337)]
(c) Katika Ijma’a
Umma wote umekubaliana kuwa Hajj ni waajib – kwa mwenye kuweza - mara moja tu katika umri wote. [Hii ikiwa hakuweka nadhiri ya kwamba atahiji, na kama ataweka nadhiri hiyo, basi ni waajib vile vile]
Na Hajj ni katika mambo yanayojulikana kwa ulazima katika Diyn, anakufuru mwenye kupinga. [Al-Mughniy (3/217) na Al-Majmuw’u (7/13)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
03-Je, Ni Waajib Kuharakia Kuhiji Au Mtu Anaweza Kuchelewesha?
Alhidaaya.com [3]
Jumhuri ya ‘Ulamaa; Abu Haniyfah – katika riwaya mbili swahiyh zaidi -, Abu Yuwsuf, Maalik na Ahmad wanasema kuwa mwenye kutamalaki masharti ya wajibu wa Hajji – ambayo yatakuja kufafanuliwa - na faradhi ya Hajji ikamtimilia, basi huyo ni lazima ahiji bila kukawia, na kama atachelewesha basi atapata madhambi. [Al-Mughniy 3/241), Al-Majmuw’u (7/85) na Al-Furuw’u (3/242)]
Wamelitolea dalili hilo kwa:
1- Kauli Yake Ta’aalaa:
((وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا ۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ))
((Na kwa ajili ya Allaah imewajibika watu watekeleze Hajj katika Nyumba hiyo kwa mwenye uwezo. Na atakayekufuru, basi hakika Allaah ni Mkwasi kwa walimwengu)). [Aal-‘Imraan (3:97]
2- Kauli yake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((أيها الناس إن الله كتب عليكم الحج فحجوا))
((Enyi watu! Hakika Allaah Amewafaradhishieni Hajji, basi hijini)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma]
Asili ya jambo lolote ni kulifanya haraka madhali halikutokea la kulizuia. [Kwa sababu ya hili, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikasirika –katika Vita vya Al-Hudaybiyyah - wakati alipowaamuru Swahaba kuvunja Ihraam, nao wakajivuta vuta kama ilivyo elezwa na Al-Bukhaariy (2731)]
3- Neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((من أراد الحج فليتعجل))
((Anayekusudia kuhiji, basi afanye haraka)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Ahmad (1737), Ibn Maajah (2883), At-Twabaraaniy (18/287-296), Al-Bayhaqiy (4/340) na wengineo kupitia kwa Abiy Israaiyl Al-Mullaaiy toka kwa Fudhwayl bin ‘Amri toka kwa Ibn Jubayr toka kwa Ibn ‘Abbaas toka kwa Al-Fadhwl. Abu Israaiyl ana udhaifu na ana makosa mengi. Maharaan Abu Swafwaan amemfuatilia -mfuatilio pungufu- toka kwa Ibn ‘Abbaas. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1732), Ibn Abiy Shaybah (3/227), Ahmad (1871), Al-Daaramiy (1984), Al-Bayhaqiy (4/339) na wengineo. Lakini Mahraan hajulikani, ufuatiliaji wake hauna faida. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi]
4- Hadiyth Marfuw’u isemayo:
((من ملك زادا وراحلة تبلغ إلى بيت الله ولم يحج فلا عليه أن يموت يهوديا أو نصرانيا))
((Mwenye kumiliki masurufu (fedha) na mnyama (kipando) atakayemfikisha kwenye Nyumba ya Allaah, naye asihiji, basi hana budi afe akiwa Myahudi au Mnaswara)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (812)]
Lakini kwa upande mwingine, Ash-Shaafi’iy, Muhammad bin Al-Hasan, na baadhi ya Masalaf, wanasema hapati madhambi kwa kuchelewesha Hajji –pamoja na uwezo wa kuhiji- lakini kwa sharti aweke niya ya kweli ya kutekeleza nguzo hiyo siku zijazo.
Wametoa dalili wakisema kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliikomboa Makkah mwaka wa nane, na hakuhiji isipokuwa mwaka wa kumi. [Na Hajji ilifaradhishwa katika mwaka wa sita, au wa saba, au wa nane, au wa tisa, au wa kumi wa Hijrah kwa mujibu wa makhitalifiano kati ya ‘Ulamaa. Angalia Al-Majmuw’u (7/87) na Zaad Al-Ma’aad (1/175)]
Na kama ingekuwa ni waajib kuharakiziwa, basi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) asingelichelewa kulifanya alilofaradhishiwa na hususan haukuwepo udhuru wowote wa dhahiri kama vita au ugonjwa! [Al-Ummu (2/118) na Al-Majmuw’u (7/87)]
Na pia kwa vile, akiiahirisha, kisha akaifanya baada ya hapo, hahesabiwi kama anailipa, na hii inadulisha kuwa inafaa kuichelewesha.
Kuhusu Aayah Tukufu, wamejibu wakisema kuwa agizo la kuhiji ndani ya Aayah hii halijawekewa mpaka wala kuainishiwa wakati maalum. Hivyo basi, inaswihi kuifanya wakati wowote ule, na ulazima wa kuifanya haraka hauko, kwa kuwa Aayah itawekewa mpaka bila dalili. Aidha, wamesema Hadiyth zote zenye kuamuru kufanya haraka ni Dhwa’iyf.
Ninasema: “Kiini cha mvutano hapa ni je, asili ya amri ni kufanya haraka au kuchelewesha? Muhimu baada ya yote, lililo bora zaidi ni kuharakisha badala ya kuchelewesha –pamoja na uwezo wa kuhiji- kiakiba tu, kwa kuwa mtu hajui kama umri utakuwepo mpaka aje ahiji. Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
04-Miongoni Mwa Fadhila Za Hajj
Alhidaaya.com [3]
1- Hajj inafuta madhambi ya miaka iliyopita
(a) Toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((من حج فلم يرفث ولم يفسق رجع كيوم ولدته أمه))
((Aliyehiji na hakuzungumza maneno yasiyolaiki na hakufanya mabaya wala maasia, hurejea kama siku mama yake aliyomzaa)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1521) na Muslim (1350)]
(b) ‘Amru bin Al-‘Aaswiy alipotaka kumpa bay-’a Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ya kuingia katika Uislamu (kusilimu), alishurutisha asamehewe madhambi yake. Rasuli akamwambia:
((أما علمت أن الاسلام يهدم ما قبله، وأن الهجرة تهدم ما قبلها، وأن الحج يهدم ما قبله؟))
((Hivi hujui kuwa kusilimu kunapomosha na kufuta madhambi ya nyuma yake, na kwamba Hijra inapomosha na kufuta madhambi ya kabla yake, na kwamba Hajj inapomosha na kufuta madhambi ya kabla yake?)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (121)]
2- Hajj ni sababu ya kuachwa mtu huru na moto
Toka kwa ‘Aaishah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((ما من يوم أكثر أن يعتق الله فيه عبدا من النار من يوم عرفة، وإنه ليدنو ثم يباهي بهم الملائكة))
((Hakuna siku iliyo na wingi zaidi wa Allaah kuwaacha huru waja na moto kuliko Siku ya Arafah, na hakika Yeye Hukurubia kisha Hujifaharisha nao kwa Malaika)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1348)]
3- Hajj malipo yake ni Pepo
Toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((العمرة إلى العمرة كفارة لما بينهما، والحج المبرور ليس له جزاء إلا الجنة))
((‘Umrah hadi ‘Umrah ni kafara kati yao, na Hajj salama iliyotakasika na chochote cha kuiharibu [Mabruwr], haina malipo mengine isipokuwa Pepo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1773) na Muslim (1349)]
4- Hajj ni katika ‘amali bora kabisa
Toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliulizwa: Ni ‘amali ipi bora zaidi?. Akasema:
((إيمان بالله ورسوله)) قيل: ثم ماذا؟ قال: ((جهاد في سبيل الله))، قيل: ثم ماذا؟ قال: ((حج مبرور))
((Kumwamini Allaah na Rasuli Wake)). Akaulizwa: Kisha ipi? Akasema: ((Jihaad katika Njia ya Allaah)). Akaulizwa: Kisha ipi? Akasema: ((Hajj salama iliyotakasika na chochote cha kuiharibu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (26) na Muslim (83)]
5- Hajj ni Jihaad bora zaidi ya wanawake
Toka kwa ‘Aaishah alisema: Ee Rasuli wa Allaah! Tunaona Jihaad kuwa ‘amali bora zaidi, kwa nini na sisi tusende Jihadini? Akasema:
((لا، ولكنّ أفضل الجهاد: حج مبرور))
((Hapana, nyinyi mna Jihaad bora zaidi; Hajj salama iliyotakasika na chochote cha kuiharibu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1520), An-Nasaaiy (5/114) na Ibn Maajah (290)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
05-Shuruti Za Kuwajibisha Hajj
Alhidaaya.com [3]
Nazo ni sifa ambazo ni lazima mtu awe nazo ili atakiwe kufanya Hajj kwa njia ya waajib. Mwenye kukosa moja ya shuruti hizi, basi Hajj si lazima kwake. Shuruti ni tano: Uislamu, akili, kubaleghe, uungwana na uwezo.
Ibn Qudaamah amesema: “Hatujui katika haya yote mvutano wowote”. [Al-Mughniy (3/218) na Nihaayat Al-Muhtaaj (2/375)]
- Uislamu na akili, haya ni masharti mawili ya kuswihi Hajj pia. Hajj ya kafiri au mwendawazimu haiswihi.
- Ama kubaleghe na uungwana, haya ni masharti mawili ya kutosheleza Hajj pia, lakini si masharti ya kuswihi Hajj. Na lau mtoto mdogo au mtumwa watahiji, basi Hajj yao itaswihi. Ni kwa Hadiyth ya mwanamke aliyemnyanyua mtoto mdogo mbele ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akauliza: Je huyu ana Hajj? Akasema:
((نعم، ولك الأجر))
((Na’am, na wewe una malipo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1336), Abu Daawuwd (1736) na An-Nasaaiy (5/120)]
Lakini kwa mujibu wa kauli yenye nguvu, ufaradhi wa Hajj hauondoki kwa mtoto au mtumwa. Ni kwa Hadiyth isemayo:
((من حج ثم عتق فعليه حجة أخرى، ومن حج وهو صغير ثم بلغ فعليه حجة أخرى))
((Aliyehiji kisha akaachwa huru, basi ni juu yake Hajj nyingine, na aliyehiji udogoni kisha akabaleghe, basi ni juu yake Hajj nyingine)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Khuzaymah (3050), Al-Haakim (1/481) na Al-Bayhaqiy (5/179). Angalia Al-Irwaa (4/59)]
- Ama uwezo, huu unakuwa ni sharti ya uwajibu tu. Lau mtu asiye na uwezo atajilazimisha kwa mbinde na tabu akahiji, basi Hajj yake ni swahiyh inayotosheleza. Ni kama mtu aliyejilazimisha kuswali au kufunga kwa tabu naye hawajibikiwi na Swalaah au Swawm, lakini zitaswihi. [Al-Mughniy (3/214)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
06-Ni Vipi Vigezo Vya Uwezo Wa Kuhiji?
Alhidaaya.com [3]
Uwezo wa kuwajibisha Hajj ni lazima uwe na vigezo vifuatavyo:
1- Afya ya mwili na kusalimika na magonjwa yanayoweza kumzuia asiweze kutekeleza ‘amali za Hajj.
Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas: ((Kwamba mwanamke mmoja toka Khath-’am alisema: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika baba yangu imemkuta Faradhi ya Allaah katika Hajj akiwa mzee kikongwe, hawezi kukaa sawa juu ya mnyama, basi je naweza kumhijia? Akamwambia:
((حجي عنه))
((Mhijie)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1855) na Muslim (1334)]
Basi yeyote atakayetimiza shuruti nyinginezo lakini akawa mgonjwa wa maradhi sugu, au mgonjwa hawezi kusimama, basi si wajibu kutekeleza faradhi ya Hajj yeye mwenyewe binafsi kwa itifaki ya ‘Ulamaa wote. Lakini wamekhitalifiana kama ni lazima atafute mtu wa kumhijia au la. Fuqahaa wa Kishaafi’iy, Kihanbali na Maswahibu wawili wa Abu Haniyfah wamesema ni lazima atafute, kwa hoja kwamba afya ya mwili ni sharti ya mtu kujifanyia mwenyewe na si sharti ya wajibu. Ama Abu Haniyfah na Maalik, wao wanasema haimlazimu. [Nihaayatul Muhtaaj (2/385), Al-Kaafiy (1/214) na Fat-hul Qadiyr (2/125)]
Ninasema: “Lililo bayana zaidi ni kuwa inamlazimu atafute mtu kutokana na udulisho wa Hadiyth iliyotangulia ya Ibn ‘Abbaas. Katika baadhi ya riwaya zake, Hadiyth inasema:
((أرأيت إن كان على أبيك دين، أكنت قاضيته؟)) قالت: نعم، قال: ((فدين الله أحق أن يقضى))
((Nieleze, kama baba yako alikuwa anadaiwa deni, je ungelilipa)). Akasema: Na’am. Akasema: ((Basi deni la Allaah lina haki zaidi ya kulipwa)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5699) na An-Nasaaiy (5/116). Angalia Al-Muhallaa (7/57)]
2- Amiliki chenye kumtosha katika safari yake, ukaazi wake, na kurudi kwake ambacho kimezidi mahitaji yake ya kimsingi katika masarifu ya watoto wake na wote ambao ni jukumu lake kuwakimu, na asiwe na deni. Hii ni kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa kinyume na walivyosema Fuqahaa wa Kimaalik. [Al-Majmuw’u (7/56) na Al-Mawsuw’at Al-Fiqhiyyah (17/31)]
Kwa kuwa masarifu ni haki ya wanadamu, na haki hii inawekwa mbele, na kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((كفى بالمرء إثما أن يضيّع من يقوت))
((Inamtosha mtu kuwa anapata madhambi kwa kutowajali anaowalisha)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1676). Angalia Al-Irwaa (989)]
Inaingia katika hili kumiliki fedha za matumizi na kipando (usafiri). Neno السبيل katika Kauli Yake Ta’aalaa:
((مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلًا))
Kwa mwenye uwezo kuiendea
.. ni kwa maana ya masurufu (fedha za matumizi) na kipando. Tafsiyr hii imesimuliwa kwa njia Marfuw’u, na si swahiyh. [Tafsiyr At-Twabariy (4/15)]
3- Usalama wa njia ya usafiri
Unajumuisha usalama wa roho na mali wakati watu wanaposafiri kwenda (Makkah) kuhiji, kwa kuwa uwezo haupo bila usalama.
Mahram ni sharti kwa mwanamke ili awajibikiwe na Hajj
Ili Hajj iwe waajib kwa mwanamke, ni lazima awe na masharti matano yaliyotangulia. Masharti haya huongezewa jingine juu yake, nalo ni kuandamana na mume wake au mahram yake. Na kama hakumpata, basi Hajj si waajib juu kwake. [Taarifu ya mahram itakuja katika mlango wa ndoa kwenye kitabu hiki In Shaa Allaah]
Toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema:
((لا يخلون رجل بامرأة إلا ومعها ذو محرم، ولا تسافر المرأة إلا مع ذي محرم))، فقام رجل فقال: يا رسول الله، إن امرأتي خرجت حاجة، وإني اكتتبت في غزوة كذا وكذا، فقال: ((انطلق فحج مع امرأتك))
((Asikae kabisa mwanamume faragha na mwanamke isipokuwa awe pamoja naye mahram wake, na asisafiri mwanamke isipokuwa awe pamoja na mahram wake)). Mtu mmoja akasimama akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika mke wangu ametoka kwenda kuhiji, na mimi nimesajiliwa katika Vita kadha wa kadha. Akamwambia: ((Chomoka haraka ukahiji na mkeo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (3006) na Muslim (1341)]
Haya ni madhehebu ya Hanafiy na Hanbal. [Al-Badaai’u (3/1089), Al-Mughniy (3/230), Bidaayatul Mujtahid (1/348), na Al-Majmuw’u (7/68)]
Lakini Maalik na Ash-Shaafi’iy wanasema kuwa mahram si sharti katika Hajj, lakini wameshurutisha usalama wa safari na kuandamana na watu wenye kuaminika. Na hii ni katika Hajj ya faradhi, ama Hajj ya Sunnah, haijuzu kutoka mwanamke ila pamoja na mahram yake kwa itifaki ya ‘Ulamaa wote.
Adh-Dhwaahiriyyah wamejuzisha mwanamke asiye na mume wala mahram au baba mkwe wake, ahiji bila mahram. [Al-Muhallaa (7/47)]
Wote wametoa dalili kwa yaliyosimuliwa kuhusiana na tafsiyr ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuwa uwezo ni masurufu na kipando, na tafsiyr hii ni dhwa’iyf kama ilivyotangulia. Na pia kwa neno lake (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)
((يوشك أن تخرج الظعينة من الحيرة تؤم البيت لا جوار معها، لا تخاف إلا الله))
((Imekurubia mwanamke kusafiri peke yake ndani ya hawdaj toka Hiyrah akiikusudia Nyumba, haogopi chochote isipokuwa Allaah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (3595) na wengineo]
“Hawdaj” ni kibanda kidogo kinachopachikwa juu ya mgongo wa ngamia ambapo msafiri hukaa ndani yake.
Hili linajibiwa kwa kusema hii ni habari kuhusiana na yatakayotokea kwa upande wa amani na usalama, na halina uhusiano na hukmu ya kusafiri mwanamke bila mahram.
Na ikiwa mwanamke atahiji bila mahram, basi Hajj yake ni sahihi lakini atapata madhambi kwa kutoka peke yake.
Mke atamtaka idhini mumewe kwenda Hajj, na mume hana haki ya kumzuia
[Al-Mughniy (3/240), Al-Ummu (2/117), Fat-hul Qadiyr (2/130) na Al-Muhallaa (7/52)]
1- Zikipatikana shuruti zilizotangulia za uwajibu wa Hajj kwa mwanamke –katika Hajj ya faradhi- basi inastahabiwa kwake amwombe ruksa mumewe. Akimruhusu vyema, na kama hakumruhusu basi atatoka bila ruksa, kwa sababu, kwa mujibu wa rai ya Jumhuri ya ‘Ulamaa, mume hana haki ya kumzuia mke kwenda kufanya Hajj ya faradhi, kwa kuwa haki ya mume haitangulizwi juu ya Fardhi ‘Ayn kama kufunga Ramadhwaan na mfano wake.
2- Ikiwa Hajj yake ni Hajj ya nadhiri, na nadhiri aliiweka kwa idhini ya mumewe, au aliiweka kabla ya kuoana kisha akamweleza naye akaikubali, basi mume hana haki ya kumzuia. Ama kama ataiweka kinyume na utashi wa mumewe, basi mume ana haki ya kumzuia. ‘Ulamaa wengine wamesema hana haki ya kumzuia vile vile, kwa kuwa ni waajib kama ilivyo Hajj ya faradhi.
3- Ikiwa Hajj yake ni ya Sunnah, au ya kumhijia mtu, hapo kwa mujibu wa Ijma’a, ni lazima aombe ruksa, na inajuzu mume kumzuia.
Je, mwanamke mwenye eda anaweza kwenda kuhiji?
Mwanamke mwenye eda ya talaka au ya kufiwa na mume ya muda wa kuweza kwenda Hijjah, si waajib kuhiji kwa kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa, kwa kuwa Allaah Amewakataza wanawake wenye eda kutokana na Neno Lake:
((لَا تُخْرِجُوهُنَّ مِن بُيُوتِهِنَّ وَلَا يَخْرُجْنَ))
((Msiwatowe katika nyumba zao, na wala wao wasitoke)). [At-Twalaaq (65:1)]
..na kwa vile pia Hajj inaweza kutekelezwa wakati mwingine. Lakini eda ni lazima iwe katika wakati maalum.
Fuqahaa wa Kihanbali wametofautisha kati ya kutoka kwake kwenda Hijja katika eda ya kuachwa (kutalikiwa), na eda ya kufiwa na mume wake. Wamezuia asiende kuhiji katika eda ya kufiwa na mumewe, kwa sababu kubaki nyumbani katika eda hii ni waajib, na wamejuzisha katika eda ya talaka ya kutorejelewa tena (talaka tatu), kwa sababu si waajib kubakia nyumbani.
Ninasema: “Sioni mantiki yoyote ya utofautishaji huu -kuhusu wajibu wa kubakia nyumbani- kati ya eda ya kufiwa na mume na eda ya kuachwa. Kimsingi, Aayah inahusiana na wanawake waliotalikiwa. Na mwanamke mwenye eda ya kufiwa na mume anafanyiwa qiyaas –kwa moja ya kauli mbili-. Na kauli ya pili inasema kuwa mwenye eda ya kufiwa na mumewe atakalia eda yake popote pale anapotaka. Na hili litakuja kuchambuliwa katika mlango wake. Basi si vyema wakageuza kinyume utofautishaji huu!!”
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
07-Kumhijia Mwingine
Alhidaaya.com [3]
1- Kumhijia aliyeshindwa kwenda
Atakayepata uwezo wa kwenda Hijjah, kisha akashindwa kutokana na uzee au ugonjwa sugu, basi ni lazima atafute mtu wa kumhijia na amlipie gharama zote kwa fedha zake. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas toka kwa Al-Fadhwl bin ‘Abbaas: ((Kwamba mwanamke mmoja toka Khath-’am alisema: Ee Rasuli wa Allaah, Hakika baba yangu imemkuta Faradhi ya Allaah katika Hajj akiwa mzee kikongwe, hawezi kukaa sawa juu ya mnyama, basi je naweza kumhijia? Akamwambia: Na’am)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1855) na Muslim (13334)]
Na katika riwaayah, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) anasema:
((أرأيت لو كان على أبيك دين، أكنت قاضيته؟)) قالت: نعم، قال: ((فدين الله أحق أن يقضى))
((Nieleze, kama baba yako alikuwa anadaiwa deni, je ungelilipa?)). Akasema: Na’am. Akasema: ((Basi deni la Allaah lina haki zaidi ya kulipwa)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (6699) na An-Nasaaiy (5/116)]
Hii ni kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa kinyume na Maalik.
Faida
Akihijiwa mwenye maradhi sugu yasiyotegemewa kupona kisha Allaah Akamponya maradhi yake, basi huyo deni lake la Hajj litakuwa limeshasafika na hatotakwa ahiji mwenyewe baada ya hapo –katika moja ya kauli mbili swahiyh zaidi za ‘Ulamaa- kwa kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ameeleza -katika Hadiyth iliyotangulia- kwamba Deni la Allaah hulipwa kwa mtu kuhijiwa na hufutika asidaiwe tena. Hivyo haijuzu faradhi hiyo imrejelee tena isipokuwa kwa dalili, na hapa dalili ya hilo hakuna. Na kama ingekuwa inamrejelea, basi Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) angelibainisha hilo na hususan ukiwepo uwezekano wa mzee kikongwe kuja kupata uwezo wa kupanda (mnyama au kipando kingine). Hivyo faradhi haijuzu kumrejelea baada ya kuhijiwa kwa usahihi unaotakikana.
Haya ni madhehebu ya Mahanbali, Is-Haaq na Ibn Hazm. Lakini Abu Haniyfah, Ash-Shaafi’iy na Ibn Al-Mundhir wanasema Hajj itamwajibikia tena, na ni lazima, kwa kuwa alipopona, imebainika kuwa ugonjwa wake haukuwa wa kukatiwa tamaa kupona, hivyo asili inamganda.
Rai ya kwanza ndio yenye nguvu zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi. [Al-Mughniy (3/449) na Al-Muhallaa (62)]
2- Kumhijia maiti aliyewajibikiwa na Hajj kwa gharama ya mali yake aliyoacha
Aliyekufa naye ana uwezo wa moja ya picha tulizozielezea, atahijiwa kwa fedha za mali yake kabla ya kulipwa madeni anayodaiwa –kama hakupatikana mtu wa kumhijia kwa kujitolea- ni sawa ameusia hilo au hajausia. Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((مِن بَعْدِ وَصِيَّةٍ يُوصِي بِهَا أَوْ دَيْنٍ))
((baada ya kutoa wasia aliousia (maiti) au kulipa deni)). [An-Nisaa (4:11)]
Hapa Allaah Ameyagusa madeni yote. Na tushaeleza nyuma kidogo kuwa Deni la Allaah lina haki zaidi ya kulipwa. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Ahmad na kundi la Masalaf. [Al-Majmuw’u (7/93) na Al-Muhallaa (62)]
Abu Haniyfah na Maalik wamesema hatohijiwa isipokuwa tu kama ameusia, na inakuwa ni katika theluthi ya mali aliyoacha.
3- Anayemhijia mtu ajihijie mwenyewe kwanza
Imeshurutishwa kwa mtu anayetaka kumhijia mwingine, awe yeye ameshafanya Hajj yake ya faradhi kwanza, ili aweze kuhijia kwa niaba. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Hanbali na ‘Ulamaa wengi. Ni kauli pia ya Ibn ‘Abbaas, na hakuna Swahaba yeyote aliyejulikana kulipinga hilo. [Al-Majmuw’u (7/98), Al-Mughniy (3/245), Al-Furuw’u (3/265) na Fataawaa Ibn Taymiyah]
Dalili yao ni Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ya kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimsikia mtu akisema:
((لبيك عن شبرمة، قال: ((من شبرمة؟)) قال: أخ لي – أو قريب لي- قال: ((حججت عن نفسك؟)) قال: لا، قال: ((حج عن نفسك ثم حج عن شبرمة))
“Labbayka”(Nimekuitikia) kwa niaba ya Shubrumah. Akasema (Rasuli): ((Ni nani Shubrumah?)). Akasema: Ni ndugu yangu –au jamaa yangu- Akasema: ((Ushajihijia mwenyewe?)). Akasema: Hapana. Akasema: ((Jihijie mwenyewe, kisha mhijie Shubrumah)). Imezozaniwa kuhusu Raf-‘u yake, Waqf yake na uswahiyh wake. [Imetiwa doa kwa kuelezewa kuwa ni Mawquwf na Mudhw-twarib. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1811), Ibn Maajah (2903) na wengineo]
Abu Haniyfah na Maalik wamesema Hajj itamtosheleza hata kama hajajihijia mwenyewe. Wametoa dalili kwa Hadiyth isiyoainisha ya mwanamke wa Khath-‘amah iliyotangulia Rasuli alipomwambia: ((Mhijie baba yako)), bila ya kumuuliza kama ameshajihijia mwenyewe au la.
Ninasema: “Lililo bora asimhijie mwingine ila baada ya kujihijia mwenyewe ili kutoka kwenye mvutano. Isitoshe, hiyo ni kauli ya Swahaba, nayo inazingatiwa zaidi kuliko kauli ya mwingine na hususan ikijulikana kuwa hakuna Swahaba yeyote aliyekwenda kinyume na kauli hiyo. Halafu, uangalizi (wa kihulka) unamsukuma mtu ajitangulize mwenyewe kabla ya mwingine kwa ujumuishi wa neno lake (Rasuli) kuhusu matumizi:
((ابدأ بنفسك))
((Jianze mwenyewe)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (997) toka kwa Jaabir]
Na kwa haya, inachukulika kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakumuuliza mwanamke huyo wa Khath-‘amah kwa kuwa alishajua kuwa ameshajihijia mwenyewe kwa kutumia vielelezo kama alivyosema Ibn Al-Hammaam. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
4- Kumhijia mtu Hajj ya Sunnah
Inaruhusika kumhijia mtu Hajj ya Sunnah kwa hali yoyote –hata kama anaweza- kwa kuwa ni Hajj ambayo haimlazimu mwenye uwezo kuifanya mwenyewe. Hivyo inajuzu kumwakilisha mtu mfano wa mwenye ugonjwa sugu. Na kwa vile pia, katika Sunnah anajiachilia asivyoweza kujiachilia katika faradhi. Na kama katika faradhi inajuzu kumwakilisha mtu, basi katika Sunnah inajuzu zaidi. Haya ni madhehebu ya Jumhuri ya ‘Ulamaa ya Abu Haniyfah na Hanbali, pia Maalik pamoja na ukaraha.
5- Mwanamke kumhijia mwanamke mwenzake
(a) Inajuzu mwanamke kumhijia mwanamke mwingine kwa makubaliano ya ‘Ulamaa wote, ni sawa akiwa binti yake au mwanamke mwingine. [Majmuw’u Fataawaa Ibn Taymiyah (26/13)]
Toka kwa Muwsaa bin Salamah kuwa mwanamke mmoja alimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuwa mama yake amekufa na hakuwahi kuhiji, je itamtosheleza yeye kumhijia mama yake?Akasema:
((نعم، لو كان على أمها دين فقضته عنها ألم يكن يجزئ عنها؟ فلتحج عن أمها))
((Na’am, lau angelikuwa mama yake ana deni akamlipia, je isingekuwa inamtosheleza? Basi amhijie mama yake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (5/116) na Ahmad (1/279) kwa Sanad Swahiyh. Na mfano wake kwa Muslim (1149) na At-Tirmidhiy (667) toka kwa Buraydah]
(b) Inajuzu pia kwa mwanamke kumhijia mwanaume kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa wakiwemo Maimamu wanne na wengineo. Ni kwa Hadiyth ya mwanamke wa Khath-‘amah tuliyoitaja mara kadhaa.
6- Kuhiji kwa mali haramu
[Al-Majmuw’u cha An-Nawawiy (7/51)]
‘Ulamaa wengi wanasema kwamba mtu akihiji kwa mali haramu, au akapanda mnyama wa kupora, basi atapata madhambi lakini Hajj yake ni sahihi na itamtosheleza. Wamesema, kwa kuwa, vitendo vya Hajj ni vitendo maalum, na uharamisho ni wa maana iliyo nje ya vitendo hivyo.
Lakini Imaam Ahmad amekhalifiana nao kwa kusema kuwa haimtoshelezi akitoa dalili kwa Hadiyth isemayo:
((إن الله طيب لا يقبل الا طيبا))
((Hakika Allaah ni Mtakasifu, Hakubali isipokuwa kitakasifu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1015), At-Tirmidhiy (2986) na wengineo]
Na kwa Hadiyth Marfuw’u isemayo:
((Anapotoka mwenye kukusudia Hajj kwa kuhiji kwa fedha halali, akiweka mguu wake juu ya kipandio akanadi: Labbayka Al-Laahumma Labbayka, basi mwenye kunadi humwita toka mbinguni: Labbayka wa sa’addayka [Umeitikiwa na umefurahikiwa], masurufu yako ni ya halali, kipando chako ni cha halali, na Hajj yako ni salama iliyotakasika isiyo na madhambi. Na anapotoka na fedha chafu akaweka mguu wake juu ya kipandio akanadi: Labbayka, mwenye kunadi humwita toka mbinguni: Laa Labbayka, walaa sa’addayka [Huitikiwi wala hufurahiwi]. Masurufu yako ni ya haramu, fedha zako ni za haramu, na Hajj yako ni ya madhambi isiyo salama)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na At-Twabaraaniy katika Al-Awsatw (5228) na Abu Nu’aym katika Al-Hilyah. Angalia Al-‘Ilal Al-Mutanaahiyah]
Ninasema: “Yenye nguvu ni kauli ya Jumhuri kwa yaliyotangulia. Ama Hadiyth ya ((إن الله طيب..)) hakuna ndani yake hujjah. Na Hadiyth ya ((وحجك مأزور غير مأجور)) ni Dhwa’iyf, haifai”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
08-Mawaaqiyt (Nyakati Na Mahala Pa Kuhirimia)
Alhidaaya.com [3]
المواقيت ni wingi (plural) wa ميقات , nayo ni ya wakati na ya mahala.
(a) Mawaaqiyt Za Nyakati
Nazo ni nyakati ambazo haijuzu ‘amali yoyote ya Hajj isipokuwa ndani yake. Allaah Ta’aalaa Amezitaja nyakati hizi katika Kauli Yake:
((الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَّعْلُومَاتٌ ۚ فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ))
((Hajj ni miezi maalumu. Na atakayekusudia kuhiji (akahirimia), basi asifanye tendo la ndoa wala ufasiki wala mabishano katika Hajj)). [Al-Baqarah (2:197)]
Aayah hii inatuhabarisha kuwa Hajj ina nyakati maalum zilizotajwa, hivyo haijuzu kuihirimia isipokuwa katika miezi ya Hajj. Allaah Ta’aalaa Amesema:
((وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ اللَّـهِ فَقَدْ ظَلَمَ نَفْسَهُ))
((Na yeyote atakayevuka Mipaka ya Allaah, basi kwa yakini amedhulumu nafsi yake)). [At-Twalaaq (62:1)]
Ikiwa mtu atahirimia Hajj kabla ya miezi yake, basi haitoswihi. Haya ni madhehebu ya Swahaba (Radhwiya Allaah ‘anhum). [Al-Muhallaa (7/65-66) na Al-Majmuw’u (7/128) na kurasa zinazofuatia].
Imepokewa pia toka kwa Ash-Sha-‘abiyy na ‘Atwaa ya kuwa inaswihi kuhirimia.
Al-Awzaa’iy na Ash-Shaafi’iy wamesema: Inakuwa ni ‘Umrah na hapana budi.
Abu Haniyfah, Maalik na Ahmad wamesema kuwa hilo ni makruhu, na Hajj itamlazimu kama amehirimia kabla ya miezi ya Hajj.
Lililo sahihi ni kuwa Hajj yake haiswihi kutokana na Aayah ilivyoeleza. Ama kusema kuwa itakuwa ni ‘Umrah, hapa ni lazima tuhoji. Vipi tubatilishe ‘amali yake ambayo ameingia kwa kuwa tu amekhalifu la sawa? Kisha vipi tumlazimishe kwa kitendo hicho ‘Umrah ambayo hakuitaka asilani, wala hakuikusudia wala hajainuwia? Bali:
((إنما الاعمال بالنيات وإنما لكل امرئ ما نوى))
((Hakika si jinginelo, ‘amali ni kwa mujibu wa niya, na hakika kila mtu ni kwa lile alilolinuwia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy, Muslim (1907) na wengineo]
Huyu ni kama mtu aliyehirimia Swalaah kabla ya wakati wake, Swalaah hii ni batili, na mwenye kunuwia kufunga kabla ya wakati wake, basi Swawm yake ni batili.
Miezi ya Hajj
Ni Shawwaal (Mfungo Mosi), Dhul-Qa-‘adah (Mfungo Pili) na siku tisa za Dhul-Hijjah (Mfungo Tatu) kwa makubaliano ya ‘Ulamaa wote. Kisha kumetokea mvutano kati yao kuhusu Yawm An-Nahr (Siku ya kuchinja) na baki ya siku za Dhul-Hijjah, na zikawa kauli zao kuhusu miezi ya Hajj ni tatu:
1- Ni Shawwaal, Dhul-Qa-‘adah na siku tisa za Dhul-Hijjah.
Ni madhehebu ya Mahanafiy na Mahanbali, na ni kauli iliyosimuliwa toka kwa Ibn Mas-‘uwd, Ibn ‘Abbaas, Ibn ‘Umar, Ibn Az-Zubayr na kundi la Masalaf. [Sharhu Fat-hil Qadiyr (2/220) na Al-Mughniy (3/275)]
2- Ni Shawwaal, Dhul-Qa-‘adah na siku tisa za Dhul-Hijjah lakini Yawm An-Nahr (tarehe 10) haiingii katika miezi hii ya Hajj.
Ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy. [Al-Majmuw-‘u 7/135) na Nihaayatul Muhtaaj (3/256)]
Hoja yao ni Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجّ))
((Na atakayekusudia kuhiji (akahirimia) katika miezi hiyo)). [Al-Baqarah (2:197)
Hivyo, haiwezekani kuihirimia Hajj baada ya usiku wa An-Nahr.
3- Ni Shawwaal, Dhul-Qa-‘adah na Dhul-Hijjah yote.
Ni madhehebu ya Maalik na Ibn Hazm. Ni kauli iliyosimuliwa pia toka kwa ‘Umar na mwanawe pamoja na Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhum). [Bidaayatul Mujtahid (1/351), Al-Kaafiy Fiy Madh-habi Ahlil Madiynah (1/357) na Al-Muhallaa (7/69)]
Hoja yao wanasema uchache wa wingi (plural) ni tatu, na kwamba Kutupia Mawe (Jamaraat) -nayo ni katika ‘amali za Hajj-, hufanywa tarehe kumi na tatu, na Twawaaf Al-Ifaadhwah –nayo ni nguzo ya Hajj- hufanywa katika Dhul Hijjah yote bila makhitalifiano yoyote.
Ninasema: “Yenye nguvu zaidi ni kauli ya tatu. Hivyo miezi ya Hajj inakuwa ni Shawwaal, Dhul-Qa-‘adah na Dhul-Hijjah yote. Na hii ni kwa maana kwamba ni lazima kisifanyike chochote katika ‘amali za Hajj kabla au baada ya miezi hii, na hailazimu kuwa Hajj inajuzu katika siku zote katika masiku ya miezi hii, bali ni lazima kuchunga hili lifuatalo:
Kwamba aliyepitwa na kisimamo cha ‘Arafah katika sehemu ya Usiku wa An-Nahr, basi kaikosa Hajj. Na hili ndilo ambalo Ash-Shaafi’iy ameling’amua alipoitoa Siku ya An-Nahr (Tarehe kumi ya Dhul-Hijjah) nje ya miezi ya Hajj. Naye anajibiwa akiambiwa kuwa Allaah Ta’aalaa Ameiita Siku ya An-Nahr “Yawmu Al-Hajj Al-Akbar” (Siku ya Hajj Kuu) katika Kauli Yake:
((وَأَذَانٌ مِّنَ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ إِلَى النَّاسِ يَوْمَ الْحَجِّ الْأَكْبَرِ))
((Na ni tangazo kutoka kwa Allaah na Rasuli Wake kwa watu siku ya Hajj Kuu)). [At-Tawbah (9:3)]
(b) Mawaaqiyt Za Mwahala
Nazo ni sehemu ambazo zimeainishwa na kuwekewa mpaka na Shariy’ah ili ahirimie kutoka hapo mwenye kunuwia Hajj au ‘Umrah, na haijuzu kwake kuvuka au kutoka nje ya mipaka bila ya kuhirimia. Mahala hapa panamhusu kila anayepita hapo akikusudia Hajj au ‘Umrah sawasawa akiwa ni mkazi wa maeneo hayo au si mkazi. Maeneo hayo ni:
1- Dhul-Hulayfah: Ni kwa watu wa Madiynah. Kwa sasa panajulikana kama Aabaar ‘Aliy.
2- Al-Juhfah: Ni kwa watu wa Sham, Misri na Morocco. Ni karibu na Raabigh [mkoa magharibi mwa Saudia] ambao kwa sasa umefanywa kuwa Miyqaat.
3- Qarnul Manaazil: Ni kwa watu wa Najd. Kwa sasa inajulikana kama Waad As-Sayl.
4- Yalamlam: Ni kwa watu wa Yemen.
Maeneo haya manne yamekubaliwa na ‘Ulamaa wote kutokana na Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) aliyesema:
((وقَّتَ رسولُ اللهِ صلَّى الله عليه وسَلَّم لأهلِ المدينةِ ذا الحُلَيفة، ولأهل الشَّامِ الجُحْفةَ، ولأهل نَجْدٍ قَرْنَ المنازِلِ، ولأهْلِ اليَمَنِ يَلَمْلَمَ، قال: فهُنَّ لهُنَّ، ولِمَن أتى عليهِنَّ مِن غيرِ أهْلِهِنَّ، لِمَن كان يريد الحَجَّ والعُمْرَةَ، فمن كان دونَهنَّ فمُهَلُّه من أهْلِه، وكذاك أهْلُ مكَّةَ يُهِلُّونَ منها))
((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwawekea watu wa Madiynah Dhul Hulayfah kuwa Miyqaat yao , Al-Juhfah kwa watu wa Sham, Qarn Al-Manaazil kwa watu Najd, na Yalamlam kwa watu wa Yemen akasema: Basi [Miyqaat] hizo ni zao na kwa atakayepita humo katika wasio wakazi ambaye amekusudia Hajj au ‘Umrah. Na atakayekuwa nje ya Miyqaat hizo, basi atahirimia mjini kwake alipo, na pia watu wa Makkah watahirimia kutoka ndani ya Makkah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1526) na Muslim (1181)]
5- Dhaatu ‘Irqi. Ni kwa watu wa Irak na Al-Mashriq. Mahala hapa pako karibu na Al-‘Uqayq. Pamekhitalifiwa kuhusiana na aliyepafanya kuwa Miyqaat. Kuna wanaosema ni ‘Umar kutokana na Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Ilipokombolewa miji hii miwili (Yaani Basrah na Kuwfah) walimwendea ‘Umar wakamwambia: Ee Amiyrul Muuminiyn! Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amewawekea watu wa Najd Qarn [Al-Manaazil] kuwa Miyqaat yao, nayo iko mbali na njia yetu, na sisi tukitaka kwenda Qarn tunapata uzito. Akasema: Basi angalieni iliyo mfano wake katika njia yenu, akawahadidia Dhaatu ‘Irqi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1531) na Al-Bayhaqiy (5/27)]
Wengine wanasema, bali aliyeweka mpaka ni Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa Hadiyth ya Jaabir:
((مهلّ أهل المدينة ذي الحليفة، والطريق الآخر الجحفة، ومهلّ العراق من ذات عرق، ومهلّ أهل نجد من قرن، ومهلّ أهل اليمن يلملم))
((Mahala pa kuhirimia watu wa Madiynah ni Dhul-Hulayfah, na njia nyingine Al-Juhfah. Mahala pa kuhirimia watu wa Irak ni Dhaatu ‘Irqi. Mahala pa kuhirimia watu wa Najd ni Qarn. Mahala pa kuhirimia watu wa Yemen ni Yalamlam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuuwd (1183). Za kutilia nguvu umarfuw’u wake ziko kwenye Al-Irwaa (998)].
Hadiyth hii ina mvutano kuhusu umarfu’u wake. Lakini kuwa kwake Marfuw’u kunatiliwa nguvu na Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) isemayo: ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa sallam) aliwahadidia Miyqaat watu wa Iraki Dhaatu ‘Irqi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1739), An-Nasaaiy (2/6) na wengineo. Angalia Al-Irwaa (999)]
Hili linaoanishwa kwa kusema kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ndiye aliyeainisha mpaka huo lakini ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhu) hakulijua hilo, akajitahidi na akaisadifu Sunnah. Ni mengi sana aliyoyasadifu yakaoana na shariah.
Miyqaat ya mkazi wa Makkah ni nyumba za Makkah, na mwenye kuishi kati ya Makkah na kati ya moja ya Miyqaat hizi, basi Miyqaat yake ni nyumbani kwake.
Na mtu ambaye njia yake haipiti katika Miyqaat yoyote kati ya hizi, akijua kwamba yuko usambamba na iliyo karibu zaidi naye, basi atahirimia hapo. Na atakayekuwa ndani ya ndege, basi atahirimia atakapokuwa sambamba na Miyqaat akiwa angani, na anakuwa ashajiandaa kabla ya kuhirimia kwa kuvaa nguo za kuhirimia kabla ya kuwa sambamba na Miyqaat. Anapokuwa sambamba nayo, atanuwia Ihraam hapo hapo, si aicheleweshe mpaka atue.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
09-Picha Halisi Ya Hijjah ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
Alhidaaya.com [3]
Toka kwa Ja’afar bin Muhammad toka kwa baba yake amesema: ((Tuliingia kwa Jaabir bin ‘Abdillaah nikamwambia: Nielezee kuhusu Hijjah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Akaashiria kwa mkono wake akakunja (hesabu) tisa, akasema: Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikaa miaka tisa hakuhiji. Kisha katika mwaka wa kumi, watu walitangaziwa kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) atakwenda kuhiji. Watu wengi mno wakaja Madiynah, na wote wanataka kumfanya Rasuli wa Allaah kigezo kwa kutenda kama atakavyotenda. Tukatoka pamoja naye mpaka tukafika Dhul-Hulayfah, na Asmaa bint ‘Umays akajifungua Muhammad bin Abiy Bakr. Akatuma mtu kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amuulizie nini afanye? Akasema:
((اغتَسِلي، واستَثْفِري بثوبٍ، وأَحْرِمي))
((Oga, ufunge utupu wako vizuri kwa kitambaa, kisha hirimia )).
Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaswali Msikitini, kisha akampanda Al-Qaswaa (ngamia wake), akaenda naye mpaka ngamia alipokaa naye sawa juu ya Al-Baydaa [alihirimia Hajj]. Niliangalia upeo wa macho yangu mbele yake nikaona watu kati ya waliopanda wanyama na wenye kutembea kwa miguu, na kulia kwake hivyo hivyo, kushoto kwake hivyo hivyo, na nyuma yake hivyo hivyo, na Rasuli wa Allaah yuko baina yetu huku Qur-aan inamteremkia, na yeye anajua taawiyl yake. Na chochote alichokifanya nasi pia tulikifanya. Rasuli akanyanyua sauti kuleta Talbiyah [Tawhiyd] akisema:
لبيك اللهم لبيك، لبيك لا شريك لك لبيك إن الحمد والنعمة لك والملك لا شريك لك
“Nimekuitikia haraka ee Allaah nimekuitikia haraka. Nimekuitikia haraka, Huna mshirika, nimekuitikia haraka. Hakika Himdi na Neema ni Zako pamoja na Ufalme, Huna mshirika”.
Na watu wakaitikia kwa sauti [huku baadhi yao] wakiongeza au wakibadili tamko la Rasuli, na Rasuli wa Allaah hakuwasemesha kitu, bali aliendelea kuleta Talbiyah yake. Jaabir (Radhwiya Allaah ‘anhu) akasema: Hatunuwii isipokuwa Hajj, hatujui ‘Umrah. Tukaenda pamoja naye hadi tukafika kwenye Nyumba (Al-Ka’abah), akaligusa Jiwe Jeusi kwa mkono wake, akaenda mwendo wa haraka mara tatu na akatembea mwendo wa kawaida mara nne [katika Kutufu]. Kisha akapenya watu akaenda Maqaam Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) akasoma
وَاتَّخِذُوا مِن مَّقَامِ إِبْرَاهِيمَ مُصَلًّى
akaiweka Maqaam baina yake na Al-Ka’abah (akaswali katikati). Baba yangu alikuwa anasema na mimi najua kwa yakini kuwa kaliona toka kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam): Alikuwa anasoma katika rakaa mbili
قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ
Na,
قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ
(Suwrah Al-Kaafiruwn na Suwrah Al-Ikhlaasw):
Kisha akarudi tena kwenye Jiwe Jeusi akaligusa kwa mkono wake, halafu alitoka kupitia mlangoni kuelekea As-Swafaa. Alipoikurubia As-Swafaa alisoma:
إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ
na kusema:
"أبدأ بما بدأ الله به"
“Ninaanza kwa Alilolianzia kwalo Allaah”. Akaanzia As-Swafaa, akapanda juu yake mpaka akaweza kuiona Nyumba (Al-Ka’abah), akaelekea Qiblah, akamuwahidisha Allaah na akamkabirisha na kusema:
لا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ، لَا إلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ، أَنْجَزَ وَعْدَهُ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ، وهَزَمَ الأَحْزَابَ وَحْدَهُ
“Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah Mmoja Asiye na mshirika, ni Wake Ufalme na ni Yake Hamdi, na Yeye ni Mweza juu ya kila kitu. Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah Mmoja, Ametekeleza Ahadi Yake, Amemsaidia Mja Wake, na Ameyashinda makundi Peke Yake”.
Kisha akaomba du’aa baina ya maneno hayo, na akasema mfano wake mara tatu. Halafu akateremka kwenda Al-Marwah. Miguu yake ilipojikita barabara chini ya bonde aliharakisha mwendo mpaka tulipoanza kupanda, hapo alitembea mwendo wa kawaida hadi Al-Marwah. Akafanya juu ya Al-Marwah mithili ya aliyoyafanya juu ya As-Swafaa mpaka ulipofika mzunguko wake wa mwisho juu ya Al-Marwah alisema: Lau jambo langu lingenibainikia mapema [kuwa Tamattu’u ni bora zaidi] nisingelifanya Qiraan kwa kuja na mnyama, na ningeliifanya ‘Umrah. Basi yeyote kati yenu asiye na mnyama, basi avue Ihraam na aifanye ‘Umrah. Suraaqah bin Maalik bin Khuth-‘um alisimama na kusema: Ee Rasuli wa Allaah! Je, ni kwa mwaka wetu huu tu au hadi milele? Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaviumanisha vidole vyake kimoja ndani ya kingine akasema: ‘Umrah imeingia ndani ya Hajj –mara mbili- hapana, bali milele milele. ‘Aliy akaja toka Yemen akiwa na ngamia wa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), akamkuta Faatwimah ni mmoja kati ya waliovua Ihraam, amevaa nguo ya rangi na amejitia wanja. Akamshangaa sana kwa kufanya hivyo. Faatwimah akamwambia: Baba yangu ameniamuru kufanya hivi, na ‘Aliy alikuwa akizungumza kwa lahaja ya Kiiraqi. Nikaenda [Jaabir] kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ili kumkwaza Faatwimah kutokana na jambo alilolifanya kwa kumuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuhusu hayo ambayo Faatwimah ameyaeleza kuwa yeye amemwamuru. Nikamweleza kuwa mimi nimemshangaa sana kwa aliyoyafanya. Rasuli akasema: Amesema kweli, amesema kweli. Akaniuliza: Umesema nini ulipohirimia Hajj? Nikasema: Ee Allaah! Mimi ninahirimia kwa alilohirimia kwalo Rasuli Wako. Akasema: Mimi nina wanyama wa kuchinja, basi usivue Ihraam. [Jaabir] anaendelea kusema: Jumla ya wanyama wa kuchinja aliokuja nao ‘Aliy kutoka Yemen na ambao Nabiy alikuja nao ilikuwa mia moja. Watu wote wakavua Ihraam na wakapunguza nywele isipokuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) pamoja na wale waliokuwa na wanyama. Ilipofika Siku ya Tarwiyah, walikwenda Mina na wakahirimia Hajj. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimpanda mnyama wake, akaswali hapo Minaa Adhuhuri, Alasiri, Magharibi, ‘Ishaa na Alfajiri. Kisha alikaa kidogo mpaka jua likachomoza. Akaamuru afungiwe hema la manyoya eneo la Namirah. Rasuli wa Allaah (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaenda huku Maqureshi wakidhani kwamba atasimama kwenye Al-Mash-‘ar Al-Haraam kama walivyokuwa wanafanya wao enzi ya ujahilia. Lakini Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipitiliza mpaka akafika karibu na ‘Arafah. Akakuta hema lake lishafungwa Namirah, na akashukia hapo. Na jua lilipopinduka, aliamuru aletewe Al-Qaswaa [ngamia wake], akatayarishwa, akampanda hadi chini ya bonde, na hapo aliwakhutubia watu. Akasema: Hakika damu zenu na mali zenu ni haramu juu yenu kama haramisho la Siku yenu hii, katika Mwezi wenu huu, na katika mji wenu huu. Jueni kwamba kila kitu katika mambo ya ujahilia nimekiweka chini ya miguu yangu [nimekisamehe, nimekifuta], na mauaji ya ujahilia yamesamehewa. Na mauaji ya kwanza ninayoyasamehe katika watu wetu waliouawa ni damu ya Ibn Rabiy-‘ah bin Al-Haarith, alikuwa anatafutiwa mama wa kumnyonyesha katika Baniy Sa’ad, Hudhayl wakamuua. Na riba ya ujahili imesamehewa, na riba ya kwanza ninayoisamehe ni riba yetu; riba ya ‘Abbaas bin ‘Abdil Muttwalib, riba yote hiyo imesamehewa na kufutwa. Basi mcheni Allaah katika wake zenu, kwani nyinyi mmewachukua kwa dhamana ya Allaah, na mmehalalishiwa tupu zao kwa Neno la Allaah. Na haki zao kwenu ni kuwa wasimwingize nyumbani kwenu yeyote msiyetaka aingie, na wakifanya hivyo, basi wapigeni pigo hafifu, na nyinyi mna wajibu kwao wa kuwakimu kwa chakula na nguo kwa mujibu wa ada na desturi. Na ka hakika mimi nimekuachieni kitu ambacho hamtopotea baada yake kama mtashikamana nacho; Kitabu cha Allaah, na nyinyi mtaulizwa kuhusu mimi [kama nimefikisha Ujumbe au la], basi je mtajibu nini? Wakasema: Tunashuhudia kwamba wewe umefikisha, umetekeleza na umenasihi. Akasema huku amekinyanyua kidole chake cha shahada mbinguni na kukizungusha kwa watu: Ee Allaah Shuhudia, ee Allaah Shuhudia (mara tatu). Kisha akaadhini halafu akaqimu, akaswali Adhuhuri, halafu akaqimu akaswali Alasiri, na hakuswali baina ya Swalaah hizi Swalaah yoyote ya Sunnah. Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimpanda ngamia wake akaenda naye mpaka sehemu ya kisimamo, akamwelekeza upande wa miamba ya mawe, na njia ya watembeao kwa miguu ikawa mbele yake. Akaelekea Qiblah, na aliendelea kusimama mpaka jua likachwa, unjano wake ukapotea kidogo na mduara wake ukatoweka. Kisha akampandisha Usaamah nyuma ya ngamia wake, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaanza kuondoka akiwa ameikaza barabara kamba ya ngamia wake [kumdhibiti asiende mbio] mpaka kichwa chake kikawa kinagusana na vishikio vya kupumzishia miguu ya mpandaji. Akawa anawaashiria watu kwa mkono wake wa kulia akiwaambia: Enyi watu! Nendeni taratibu. Nendeni kwa upole. Na kila anapofika kwenye kifusi cha mchanga, aliilegeza kamba ya ngamia kidogo ili aweze kupanda kwa usahali. Alikwenda hadi akafika Muzdalifah, akaswali hapo Magharibi na ‘Ishaa kwa adhana moja na iqaamah mbili, na hakuswali Sunnah yoyote kati ya Swalaah hizo mbili. Halafu Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akalala kwa ubavu mpaka Alfajiri ilipochomoza. Akaswali Swalaatul Fajr wakati As-Subh ilipowadia kwa adhana moja na iqaamah moja. Halafu akampanda Al-Qaswaa mpaka akafika Al-Mash-‘ar Al-Haraam [eneo la Mlima wa Qazah uliopo Muzdalifah], akaelekea Qiblah, akamwomba Allaah, akamkabirisha, akamhalilisha na akamuwahidisha. Aliendelea kusimama katika hali hiyo mpaka anga likawa la kinjano sana, kisha akaondoka kabla jua halijapanda. Rasuli akambeba Al-Fadwl bin ‘Abbaas nyuma ya ngamia wake. Al-Fadwl alikuwa na nywele nzuri, mweupe wa rangi, na mjamala wa sura. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipoanza kuondoka, walipita mbele yake wanawake wenye kwenda haraka. Al-Fadhwl akaanza kuwaangalia na Rasuli wa Allaah (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akauweka mkono wake kwenye uso wa Al-Fadhwl [kumzuia]. Al-Fadhwl akaugeuza uso upande mwingine apate kuangalia. Wakaendelea kwenda mpaka Rasuli akafika eneo la Muhassir, na hapo aliongeza mwendo wa ngamia wake. Kisha akapitia njia ya kati inayotokezea Al-Jamarat Al-Kubraa mpaka akalifikia guzo [Jamarah] lililopo mbele ya mti. Akalitupia vijiwe saba huku akileta Takbiyrah kwa kila kijiwe. Ukubwa wa kila kijiwe ni sawa na kijiwe cha kurusha kwa manati au kwa kidole. Alitupia toka ndani ya bonde. Kisha aliondoka hadi machinjioni, akachinja ngamia sitini na tatu kwa mkono wake, halafu alimpa ‘Aliy akachinja waliobakia na akamshirikisha katika wanyama wake. Halafu akaamuru kiletwe kipande cha nyama ya kila ngamia, vikatiwa kwenye jungu vikapikwa. Akala nyama hiyo yeye na ‘Aliy na wakanywa supu yake. Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akampanda ngamia wake na kuelekea Al-Ka’abah, akaswali Adhuhuri Makkah. Akawaendea Baniy ‘Abdil Muttwalib wakiwa katika shughuli ya kuteka, kujaza mahodhi na kunywesha watu maji ya Zamzam, akawaambia: Tekeni maji enyi Baniy Al-Muttwalib. Na lau [si mimi kuhofia] watu kuwazidini nguvu na kukamata kazi yenu ya kunywesha watu maji, basi ningeliteka maji pamoja nanyi. Wakampa ndoo ya maji, akanywa nayo maji.
Na ametuhadithia ‘Umar bin Hafsw bin Ghiyaath, ametuhadithia baba yangu, ametuhadithia Ja-‘afar bin Muhammad, amenihadithia baba yangu amesema: ((Nilimwendea Jaabir bin ‘Abdillaah nikamuuliza kuhusu Hijjah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), akanihadithia sawa na alivyohadithia Haatim bin ‘Ismaaiyl, na akaongeza katika Hadiyth yake: “Abu Sayaarah alikuwa akiwapeleka Waarabu akiwa amepanda punda asiye na tandiko [enzi ya ujahilia]. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipopita Al-Mash-ar Al-Haraam akitokea Muzdalifah, Maqureshi walidhani atasimama na kushukia hapo. Rasuli akapita bila hata kusimama mpaka akawasili ‘Arafaat, akashukia hapo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1218), Abu Daawuwd (1905), Ibn Maajah (3074), Ad-Daaramiy (1850) na wengineo]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
10-Muhtasari Wa Vitendo Vya Hajj Ya Mwenye Kufanya Tamattu’u
Alhidaaya.com [3]
[Hajj inajuzu kwa moja ya aina tatu: Ifraad, au Tamattu’u au Qiraan ambazo tutazifafanua mbeleni. Tamattu’u ni bora na nyepesi zaidi, nayo inamfaa zaidi Hujaji toka nchi yetu (Misri)]
Hakuna shaka yoyote kuwa Muislamu ana pupa ya Hajj yake kuwa na sifa sawa na Hijjah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa waalihii wa sallam) ili iwe na uhakika zaidi wa kukubaliwa, na imkurubishe zaidi katika kuzipata fadhla za Hajj zilizotajwa nyuma.
Hivyo basi, ninayaandika hapa kwa muhtasari matendo ya “Hajj ya Tamattu’u” toka katika mjumuiko wa Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), kisha nitafuatishia mfululizo huu kwa kuvichambua vitendo hivyo na vigawanyo vyake kwa upande wa nguzo, waajibaat, mustahabbu na kadhalika. Hivyo nasema:
Kabla Ya Safari
1- Aliyepata uwezo wa kuhiji, na akaweka azima na nia ya mwisho ya kuitekeleza Hajj, basi aharakie kutubia toba safi ya kweli kwa maasia yake, ajitahidi kutoka ndani ya duara la kudhulumu watu kwa kuwarejeshea wenyewe haki zao, ajitahidi kulipa madeni yake kiasi awezavyo, ajitahidi kuwafurahisha wazazi wake na kupata ridhaa yao, awaombe radhi jamaa zake kama kuna kitu kati yake na wao, na awaachie watoto na wote anaowakimu kimaisha cha kuwaendeshea maisha muda wote wa kutokuwepo yeye.
2- Awe na pupa ya kuhakikisha kuwa gharama zake za kuhijia ni za chumo halali. Atahadhari na fedha zenye utata wa uhalali au uharamu, au mali haramu (ya kupora) ili awe karibu zaidi na kukubaliwa Hajj yake.
3- Ajitahidi kuongozana na msafara wa watu wema wenye utashi wa kheri, wenye kuchukia shari na watakaomsaidia. Kama itakuwa wepesi kupata msafara wa ‘Ulamaa wenye kuhangaikia watu, basi itakuwa bora zaidi.
4- Atoke kwenda safari yake akiwajibika na adabu za kisharia katika safari, na hiyo ni katika miezi ya Hajj.
Kuhirimia
5- Anapofika katika Miyqaat, atavua nguo zake, atakoga kama anavyooga janaba, na atajitia manukato mazuri zaidi atakayokuwa nayo. Mwanamke atafanya hivyo hivyo hata kama atakuwa na hedhi au nifasi. Kubakia harufu ya manukato kwenye nguo au mwili baada ya kuhirimia hakuna neno kwao wote wawili (mwanaume na mwanamke).
6- Mwanaume atavaa mavazi ya Ihraam (vipande viwili), na mwanamke atavaa nguo yoyote aipendayo.
7- Ukiingia wakati wa Swalaah yake ya Faradhi ataswali, na kama haukuingia, ataswali rakaa mbili kwa niya ya Sunnah ya wudhuu. Akimaliza, atanuwia kuhirimia ‘Umrah baada ya kupanda kipando chake (gari, meli, ndege, mnyama n.k) na atamhimidi Allaah na kupiga Takbiyr akielekea Qiblah, kisha aseme:
((لبيك اللهم عمرة))
8- Atakayekuwa ndani ya ndege, atahirimia atakapokuwa mkabala na Miyqaat, kwa ndege kuwa juu ya eneo hilo. Atakuwa ashajiandaa kabla ya kuhirimia kwa kuoga, kujitia manukato na kuweka tayari mavazi ya Ihraam.
9- Anapohirimia ‘Umrah kwa sauti atalabbi:
((لبيك اللهم لبيك، لبيك لا شريك لك لبيك، إن الحمد والنعمة لك والملك، لا شريك لك))
Mwanaume atanyanyua sauti yake akiitikia Talbiyah, na mwanamke atanyanyua kwa kiasi tu cha mwanamke aliye pembeni yake kumsikia.
10– Aliyehirimia anatakiwa akithirishe Talbiyah na hususan zinapobadilika hali na nyakati kama anapopanda kwenye mnyanyuko au anaposhuka kwenye mteremko, au usiku unapoingia au mchana. Mwanamke ataleta Talbiyah hata kama ana hedhi, na Talbiyah haikatishwi isipokuwa pale anapoanza Twawaaf. [Kwa kuwa yuko kwenye ‘Umrah. Ama mwenye kufanya “Ifraad”, au mwenye kufanya “Qiraan”, hawa hawakatishi Talbiyah mpaka pale wanapoanza kutupia Jamarat Al-‘Aqabah]
Kuingia Makkah Na Kutufu
11- Anapofika Makkah, aharakie kwenda Al-Masjid Al-Haraam, atangulie kuliendea Jiwe Jeusi, aliguse kwa mkono wake wa kulia na alibusu – kama itakuwa wepesi - na kama haikuwezekana ataligusa na ataubusu mkono wake. Kama hakuweza kuligusa, ataashiria kwa mkono wake, atapiga Takbiyr na hatoubusu mkono wake. Ni vizuri asiwasonge watu akawaudhi, na yeye akapata adha yao.
12- Kisha atatufu – Al Ka-’abah ikiwa kushotoni kwake -, na anapofika katika Nguzo ya Al-Yamaaniy (Ar-Ruknu Al-Yamaaniy), ataigusa bila kuibusu kama itakuwa wepesi. Anapokuwa kati ya Nguzo ya Al-Yamaaniy na Jiwe Jeusi atasema:
((رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ))
Anapolifikia Jiwe Jeusi, anakuwa ametimiza mzunguko mmoja, na atafanya kando yake aliyoyafanya mwanzoni, kisha ataendelea na Twawaaf mpaka akamilishe mizunguko saba.
13- Mwanamume – si mwanamke - anatakikana apitishe sehemu ya nguo yake ya juu (ridaa) chini ya kwapa lake la kulia na ncha zake mbili azitupie juu ya bega lake la kushoto kuanzia mwanzo wa Twawaaf hadi mwisho wake. Ataharakiza mwendo katika mizunguko mitatu ya kwanza tu, na iliyobaki minne atazunguka kwa mwendo wa kawaida.
14- Akimaliza Twawaaf ataswali rakaa mbili nyuma ya Maqaam Ibraahiym. Atasoma katika rakaa mbili Suwrat Al-Kaafiruwn na Suwrat Al-Ikhlaas.
15- Kisha atakwenda kunywa maji ya Zamzam na atajimwagia kichwani.
16- Halafu atarudi tena kwenye Jiwe Jeusi na ataligusa ikiwa itakuwa wepesi kwake.
Kusai (kwenda) Kati Ya Swafaa Na Marwah
17- Kisha atatoka kwenda sehemu ya Kusai. Anapokaribia Swafaa atasoma:
إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ
na atasema:
"أبدأ بما بدأ الله به"
((Ninaanza kwa Aliloanza nalo Allaah)).
18- Atapanda juu ya Swafaa mpaka aione Al-Ka-‘abah na aielekee na aseme:
((لا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَديرٌ، لَا إلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ، أَنْجَزَ وَعْدَهُ، وَنَصَرَ عَبْدَهُ، وهَزَمَ الأَحْزَابَ وَحْدَهُ))
Ataomba atakacho, na atafanya hivyo mara tatu.
19- Kisha atateremka toka Swafaa kwenda Marwah akitembea. Kati ya alama (taa) mbili za kijani, mwanamume atakwenda matiti (mchakamchaka) na si mwanamke.
20- Anapofika Marwah, atafanya kama alivyofanya juu ya Swafaa. Na hii itakuwa ni raundi moja ya kwanza. Kisha atateremka kwenda Swafaa, na ataendelea hivyo hivyo mpaka akamilishe raundi saba (kwenda ni raundi na kurudi ni raundi).
Kujivua Na Ihraam
21- Anapomaliza Kusai, atanyoa nywele zake au atazipunguza. Kupunguza hapa ni bora zaidi na hasa hasa ikiwa wakati wa Hajj umekurubia. Mwanamke hanyoi bali hupunguza.
Kisha atavaa nguo zake za kawaida, na kila lililokuwa marufuku kwake baada ya kuhirimia kama kujimai, linakuwa halali mpaka utakapowadia wakati wa kuanza Hajj. [Hadi hapo ‘ibaadah ya ‘Umrah itakuwa imemalizika]
Siku Ya Tarwiyah
22- Inapofika tarehe nane ya Dhul-Hijjah (Siku ya Tarwiyah), atajiandaa kuhirimia kama ilivyotangulia – toka nyumbani kwake Makkah - kisha atahirimia Hajj kwa kusema:
لبيك اللهم بحجة
na ataleta Talbiyah.
Akihofia jambo fulani linaweza kumzuia asiweze kuitimiza Hajj yake, basi anaweza kuweka sharuti kwa kusema:
وإن حبسني حابس فمحلي حيث حبستني
Na kama kitanizuia kizuizi, basi pangu pa kuvua Ihraam ni pale Utakaponizuia”.
23- Kisha atatoka kwenda Minaa wakati wa Dhuhaa (jua linapopanda) na atalala huko Minaa. Ataswali huko Adhuhuri, Alasiri, Magharibi, ‘Ishaa na Alfajiri kwa kupunguza bila kukusanya.
Siku ya ‘Arafah
24- Jua linapochomoza – tarehe tisa (‘Arafah) - atatembea toka Minaa hadi ‘Arafah. Atashukia Namirah, na atakaa hapo mpaka jua litakapopinduka (Adhuhuri) kama itakuwa ni wepesi.
25- Jua linapopinduka, atakusanya Adhuhuri na Alasiri kwa pamoja kwa kupunguza (rakaa mbili mbili) kwa Adhana moja na Iqaamah mbili – pamoja na imam - bila Sunnah. (Zitaswaliwa zote katika wakati wa Swalaah ya Adhuhuri).
26- Kisha baada ya kuswali, ataacha mengine yote akae kuleta adhkaar, kuomba du’aa, na kunyenyekea kwa Allaah Ta’aalaa katika eneo hilo la ‘Arafah huku akinyanyua mikono yake, akiwa ameelekea Qiblah – na si kuelekea Kilima- na atasimama hivi mpaka jua lizame.
27- Jua linapozama, atateremka kwa taratibu na upole.
Kutoka ‘Arafah Kwenda Muzdalifah Na Kulala Huko
28- Kisha atatembea hadi Muzdalifah. Akifika huko, atakusanya Magharibi na ‘Ishaa kwa pamoja kwa Adhana moja na Iqaamah mbili bila Sunnah. (Zitaswaliwa zote katika wakati wa Swalaah ya ‘Ishaa)
29- Atalala Muzdalifah mpaka Alfajiri, na hatoswali Sunnah za usiku.
30- Ataswali Alfajiri mwanzoni mwa wakati kwa Adhana moja na Iqaamah moja. Kisha atasimama juu ya Al-Mash-‘ar Al-Haraam (Mlima mashuhuri Muzdalifah) ataelekea Qiblah, ataomba, ataleta Takbiyrah, na ataleta Tahliyl (Laa ilaaha illa Allaah) mpaka unjano wa asubuhi ukomae.
31- Wanawake madhaifu na wengineo, wanaruhusika kuondoka Muzdalifah baada ya usiku wa manane mwezi unapotoweka.
Siku Ya Kuchinja (Yawm An-Nahr) Na Kwenda Minaa Na Kutupia (vijiwe) Jamarah
32- Kisha ataondoka toka Muzdalifah kwenda Minaa asubuhi inapovaa unjano kabla jua halijachomoza. Ataharakisha mwendo zaidi akifika Bonde la Muhassar.
33- Akifika Minaa, ataikata Talbiyah wakati anapoanza kutupia Jamaratul Aqabah – nayo ni ya mwisho kuelekea Makkah - kwa vijiwe saba mfululizo kimoja baada ya kingine. Atapiga Takbiyr kwa kila kijiwe, na kutupia kunakuwa baada ya jua kuchomoza.
34- Anapomaliza kutupia Jamaratul Aqabah, ataruhusiwa kuyafanya yote yaliyokuwa marufuku isipokuwa kujimai. [Hii inaitwa Tahallul ya kwanza. Atavaa nguo aitakayo, atakata kucha na atajitia manukato]
35- Kisha atachinja mnyama wake Minaa au Makkah, na anaruhusiwa kuchinja siku yoyote katika Masiku Matatu ya Tashriyq. Kama hana fedha ya kununulia mnyama, atafunga siku tatu katika Hajj na nyingine saba baada ya kurudi kwao.
36- Halafu atanyoa kichwa chake, na mwanamke atapunguza nywele zake hata kwa kiasi cha pingili ya kidole.
Kurudi Makkah Na Twawaaf Ya Ifaadhwah
37- Halafu atarudi Makkah, atatufu mara saba, na atasai kati ya Swafaa na Marwah. [Kwa kuwa anafanya Tamattu’u, ama mwenye kufanya Qiraan, huyo hatufu isipokuwa Twawaaf moja tu].
Anaweza kuahirisha Twawaaf siku ya mwisho ya Tashriyq. Akitufu, kila kitu kitakuwa halali hata kujimai pia. [Hii ndio Tahallul kubwa]
38- Mwanamke akiwa na hedhi – wakati wa kufanya ‘amali za Hajj -, atafanya mambo yote isipokuwa Twawaaf, ataiakhirisha mpaka atwaharike kama ataweza.
39- Ikiwa atapata uzito na tabu kama atasubiri atwaharike – kama ashakuwa amebuku tarehe ya safari ya kurudi au akahofia madhara kama atabakia - basi atatufu akiwa na hedhi yake kwa mujibu wa kauli sahihi zaidi ya ‘Ulamaa, kwa kuwa huo ndio upeo wa mwisho wa uwezo wake.
Kwenda Minaa
40- Kisha baada ya Kutufu na Kusai, atarudi tena Minaa ili kulala huko Masiku ya Tashriyq (Usiku wa tarehe 11, 12, na 13).
Masiku Ya Tashriyq Na Kutupia Jamaraat Tatu Siku Za Tarehe Kumi Na Moja Na Kumi na Mbili
41- Kisha atatupia Jamaraat tatu tarehe kumi na moja – baada ya Adhuhuri hata mpaka usiku - kila nguzo ataitupia vijiwe saba huku akipiga Takbiyr kwa kila kijiwe. Ataanzia Jamarat ndogo, kisha ya katikati. Atasogea mbele baada ya kila Jamarah, ataelekea Qiblah na aombe du’aa ndefu – ikiwa itakuwa wepesi - kisha ataliendea Jamarah la Aqabah atalitupia vijiwe saba, na hatosimama kuomba du’aa baada yake. Kijiwe ambacho hakitagonga Jamarah au kuingia shimoni, basi hakihesabiwi.
42- Kisha tarehe kumi na mbili atafanya vile vile alivyofanya siku iliyopita ya tarehe kumi na moja.
Akimaliza kutupia vijiwe – tarehe kumi na mbili - akitaka ataharakisha kuondoka, na atashuka toka Minaa, na akitaka atachelewesha kuondoka na atalala Minaa usiku wa tarehe kumi na tatu, na kuchelewesha ni bora zaidi.
Kutupia Tarehe Kumi Na Tatu (Siku Ya Mwisho Ya Tashriyq)
43- Akiamua kulala usiku wa tarehe kumi na tatu, au jua likazama siku ya tarehe kumi na mbili na yeye bado yuko Minaa, basi ni lazima alale Minaa ili kutupia vijiwe Jamaraat tatu tarehe kumi na tatu kama alivyofanya siku mbili zilizotangulia baada ya Adhuhuri.
Twawaaf Ya Kuaga Kabla Ya Safari
44- Mwenye kuhiji akitaka kusafiri kurudi nchini kwake, asitoke mpaka atufu Twawaaf ya kuaga. Ataifanya ni ahadi yake ya mwisho na Makkah. Ama mwenye hedhi na nifasi, hao wanaruhusiwa wasifanye Twawaaf ya kuaga.
45- Imestahabiwa kwa Hujaji azuru Al-Masjid An-Nabawiy huko Al-Madiynah, na kuuzuru si katika ‘amali za Hajj kama wanavyodhani watu wengi.
46- Halafu atarejea nchini kwake. Akifika, atawachinjia watu wake, mafukara na masikini ng’ombe au ngamia kama itakuwa wepesi. Kama hakuweza hilo, basi si lazima. Allaah Ta’aalaa Ndiye Ajuaye Zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
11-Nguzo Za Hajj:
Nguzo Ya Kwanza Ya Hajj: Kuhirimia (Al-Ihraam)
Alhidaaya.com [3]
Matendo yaliyotangulia yanagawanyika katika nguzo, yaliyo wajibu (waajibaat) na yaliyosuniwa (mustahabbaat).
Nguzo za Hajj kwa mujibu wa Jumhuri ya ‘Ulamaa ni nne: Kuhirimia, Kusimama ‘Arafah, Twawaaf ya Ifaadhwah na Kusai kati ya Swafaa na Marwah. [Kwa Ash-Shaafi’iy nguzo hizi ni sita. Ni hizi nne pamoja na kunyoa au kupunguza, na kupangilia kati ya nguzo. Ama kwa Hanafiy ni nguzo mbili: Kusimama ‘Arafah na Twawaaf ya Ifaadhwah]
Nguzo Ya Kwanza Ya Hajj: Kuhirimia (Al-Ihraam)
Kuhirimia ni kutia niya ya Hajj au ‘Umrah toka kwenye Miyqaat inayotambulika kisharia. Ni nguzo kati ya nguzo za Hajj kwa mujibu wa Jumhuri ya ‘Ulamaa, na ni sharti ya kuswihi Hajj kwa Mahanafiy. Allaah Ta’aalaa Amesema:
((وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ))
((Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki)). [Al-Bayyinah (98:5)]
Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((إنما الأعمال بالنيات))
((Hakika si jinginelo, ‘amali ni kwa niya)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa mara nyingi nyuma)).
Aina Za Ihraam (Kuhirimia)
Hajj hufanywa kwa miundo mitatu:
1- Ifraad: Ni Hujaji kunuwia Hajj tu wakati anapohirimia kwa kusema:
لبيك اللهم بحج
kisha atafanya ‘amali za Hajj tu.
2- Qiraan: Ni Hujaji kunuwia Hajj na ‘Umrah kwa pamoja kwa kusema:
لبيك حجا وعمرة
na atazifanya zote mbili hizo (Hajj na ‘Umrah) katika ‘amali (nusuk) moja, au aingize Hajj ndani ya ‘Umrah kabla ya Twawaaf.
Jumhuri wamesema: Viwili vinaingiliana. Atatufu Twawaaf moja na atasai Sai moja, na hilo litamtosheleza kwa Hajj na ‘Umrah.
‘Ulamaa wa Kihanafiy wanasema atatufu Twawaaf mbili na atasai Sai mbili, na mwenye kufanya Qiraan ni lazima achinje mnyama kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa kama itakavyokuja mbeleni.
3- Tamattu’u: Ni kunuwia mwenye kuhji ‘Umrah tu katika miezi ya Hajj kwa kusema:
لبيك عمرة
na atakwenda Makkah, atafanya ‘amali za ‘Umrah na atajivua Ihraam. Atakaa Makkah akiwa hana Ihraam, kisha atahirimia Hajj na atafanya Manaasiki za Hajj, na hiyo ni katika mwaka huo huo.
Mwenye kufanya Tamattu’u ni lazima pia achinje mnyama kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa.
Dalili za uhalali wa ‘amali hizi tatu
1- Hakuna khilafu yoyote kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipoanza Hajj, Hajj ilikuwa inajuzu kwa aina zake hizi tatu tulizozitaja. Na ndivyo hivi hivi walivyofanya Swahaba zake ambao wako waliofanya Tamattu’u, waliofanya Qiraan, na waliofanya Ifraad. Kwa kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwachaguza katika hilo kama ilivyokuja katika Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) anayesema: Tulitoka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akasema:
((من أراد منكم أن يهل بحج وعمرة فليفعل، ومن أراد أن يهل بحج فليهل، ومن أراد أن يهل بعمرة فليهل..))
((Anayetaka miongoni mwenu kunuwia Hajj na ‘Umrah, basi afanye, na anayetaka kunuwia Hajj, basi anuwie, na anayetaka kunuwia ‘Umrah, basi anuwie…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1211)]
2- Kisha Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwahamisha – baada ya chaguzi hizi - kwenda kwenye Tamattu’u bila kuwakazia hilo [kuwashadidia]. ‘Aaishah anasema:..Tukateremka Sarif [Sehemu karibu na At-Tan-’iym], akawatokea Swahaba wake akasema:
((من لم يكن منكم أهدى، فأحب أن يجعلها عمرة فليفعل، ومن كان معه هدي فلا))
((Ambaye miongoni mwenu hakuja na mnyama wa kudhwahi na akataka kuifanya ‘Umrah, basi afanye, na yule mwenye mnyama asifanye)). Akasema (‘Aaishah): “Basi kuna waliolitekeleza hilo na kuna walioliacha katika Swahaba Wake [ambao hawakuwa na wanyama]”. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1560) na Muslim (1211), na ziada ni yake]
Na katika Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipowasili Dhiy Tuwaa – sehemu karibu na Makkah - na akalala hapo, alipopambaukiwa asubuhi aliwaambia:
((من شاء أن يجعلها عمرة فليجعلها عمرة))
((Anayetaka kuifanya [Hajj yake] ‘Umrah basi aifanye ‘Umrah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1564) na Muslim (1240)]
3- Kisha akawaamuru – kwa ambaye hakuswaga mnyama kati yao - waivunje Hajj na kuifanya ‘Umrah na wavue Ihraam. Toka kwa ‘Aaishah amesema: Tulitoka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na hatuoni [ndani ya akili zetu] isipokuwa tunahiji tu. Tulipofika Makkah, tulitufu Nyumba. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akamwamuru kila ambaye hajaswaga mnyama avue Ihraam. Akasema: Akavua Ihraam kila ambaye hakuswaga mnyama, na wakeze hawakuswaga mnyama, wakavua Ihraam…. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1561) na Muslim (1211)]
Na katika riwaya ya Ibn ‘Abbaas: …Akawaamuru waifanye (Hajj) ‘Umrah. Hilo likawapa ukakasi mkubwa sana, wakasema: Ee Rasuli wa Allaah, ni vuo lipi la Ihraam [Tahallul ipi? Ya kuruhusiwa baadhi ya yaliyokatazwa tu]? Akasema: ((Vuo la yote [Tahallul ya kuruhusiwa kufanya marufuku zote])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1564) na Muslim (1240)]
Ninasema: “Kwa ajili ya awamu hizi tatu zilizotangulia, ‘Ulamaa wamekhitalifiana kuhusiana na usharia wa ‘amali hizi tatu:
Jumhuri ya Salaf na Makhalaf wanasema kuwa ‘amali hizi tatu; Ifraad, Qiraan na Tamattu’u, zote zinajuzu, na kwamba uwanja ni mpana, hata baadhi yao wamenukulu Ijma’a kuhusu hilo. [Angalia Al-Majmuw’u (7/144), Al-Mughniy (3/276), na Ma’aalimu As-Sunan cha Al-Khattwaabiy (2/301). An-Nawawiy amesema baada ya kueleza khilafu za baadhi ya Swahaba katika suala hili katika Sharhu Muslim: “Ijma’a imepatikana baada ya hili juu ya kujuzu Ifraad, Tamattu’u na Qiraan bila ya ukaraha” ]
Kisha wakakhitalifiana hawa – baada ya kukubaliana juu ya uhalali na usharia wake - ni ipi ‘amali bora zaidi kati ya hizi tatu? Hili litakuja kugusiwa mbeleni.
Lakini baadhi ya ‘Ulamaa wengine wanaona kuwa ni waajib kufanya Tamattu’u kwa ambaye hakuswaga mnyama, na kwamba akitufu na akasai, basi atavua Ihraam kwa lazima. Na haya ni madhehebu ya Ibn ‘Abbaas na Abu Muwsaa Al-Ash-‘Ariy. Pia ni kauli ya Ahlu Adh-Dhwaahir, na imeungwa mkono na Ibn Hazm, kisha Ibn Al-Qayyim kwa tafiti mbili muhimu. [Rejea Al-Muhallaa (7/99 na zinazofuatia) na Zaad Al-Ma’aadiy (2/77) na zinazofuatia]
Wamelitolea dalili hilo kwa amri aliyoitoa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa Swahaba zake ya kuvunja Hajj kwenda kwenye ‘Umrah na kulifanya hilo ni waajib wa lazima kwao. Hilo lilikuwa na ukakasi mkubwa kwao, jambo linaloonyesha kuwa walifahamu kuwa amri hiyo ni ya waajib, na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akakasirika walipojivuta vuta na kumuuliza tena kama inavyoeleza Hadiyth ya ‘Aaishah: ‘Aliyy akaingia naye amekasirika mno. Nikasema: Nani amekukasirisha ee Rasuli wa Allaah, Allaah Amwingize motoni?. Akasema:
((أو ما شعرت أني أمرت الناس بأمر فإذا هم يترددون..))
((Hivi hujui kwamba nimewaamuru watu amri, na ghafla wao wanasitasita..)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1210) na Ahmad (6/175)]
Wametolea dalili pia kwa kauli yake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalhii wa sallam) walipomuuliza kuhusu agizo la kuvunja Hajj alilowapa: “Je ni kwa mwaka wetu huu tu au milele abadan?” Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi akaingiza vidole vyake ndani ya vingine akasema:
((دخلت العمرة في الحج إلى يوم القيامة، لا بل لأبد أبد، لا بل لأبد أبد))
((‘Umrah imeingia ndani ya Hajj hadi Siku ya Qiyaamah, hapana bali milele na milele, hapana bali milele na milele)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1218)]
Ibn ‘Abbaas alikuwa akijadiliana na watu kitaaluma suala hili mpaka kufikia kusema: Ninawaambieni: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema, na nyinyi mnasema: Amesema Abu Bakr na ‘Umar. Mawe yamekurubia kuwashukieni toka mbinguni.. [Musnad Ahmad (1/337)/ Al-Faqiyhu Al-Mutafaqqih (1/145), na Jaami’u Bayaan Al-‘Ilm (2/239)]
Kwa kuwa Abu Bakr na ‘Umar walikuwa wanaona kuwa Ifraad ni bora zaidi kuliko Tamattu’u kama tutakavyozungumzia hili mbeleni.
Na kiini cha dhana ya madhehebu haya ni kuwa, anayetaka kuhiji na akafika Miyqaat, kama hana mnyama wa kuchinja, basi ni waajib kwake ahirimie ‘Umrah pekee na hapana budi [yaani awe mwenye kufanya Tamattu’u]. Na kama atahirimia Hajj, au Qiraan ya Hajj na ‘Umrah, ni wajibu kwake avunje Ihraam yake kuwa ‘Umrah na avue Ihraam anapoimaliza, kisha aanze kunuwia Hajj kwa Ifraad toka Makkah.
Na kama amemswaga mnyama, basi atafanya Qiraan akinuwia:
((لبيك بعمرة وحج معا))
[Angalia Al-Muhallaa (7/99)]
Ni Ipi Bora Zaidi Kati Ya ‘Amali Hizi Tatu?
Na kwa msingi wa kujuzisha Jumhuri ‘amali hizi tatu, wamekhitalifiana kwa kauli mbalimbali kuhusu ni ipi iliyo bora zaidi. Na sababu ya kukhitilafiana huku, ni mvutano kuhusu Hajj ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam): Je, alifanya Ifraad, au Qiraan, au Tamattu’u?
[1] Kauli ya kwanza: Ifraad ni bora zaidi
Ni madhehebu ya Maalik, Dhwaahir na Ash-Shaafi’iy, nayo imesimuliwa toka kwa ‘Umar, ‘Uthmaan, Ibn ‘Umar, Jaabir na ‘Aaishah. [Al-Mudawwanah (1/360), Al-Ummu (2/143) na Al-Majmuw’u (7/145 na zinazofuatia)]
Hoja zao ni:
1- Yaliyothibiti toka kwa Jaabir, Ibn ‘Umar, Ibn ‘Abbaas na ‘Aaishah kuwa: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alinuwia Hajj. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1562) na Muslim (1211) toka kwa ‘Aaishah]
Na katika riwaya: “Alinuwia Hajj kwa Ifraad.”
2- Makhalifa Waongofu (Radhwiya Allaah ‘anhum) walifanya Ifraad ya Hajj baada ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na wakaendelea kufanya hivyo. Na ndivyo alivyofanya Abu Bakr, ‘Umar na ‘Uthmaan. Wamekhitalifiana alivyofanya ‘Aliyy.
3- Kwamba ‘Umar amesema: Ipambanueni Hajj yenu na ‘Umrah yenu, kwani hiyo ni ukamilifu zaidi wa Hajj yenu na ukamilifu zaidi wa ‘Umrah yenu. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1217), na Maalik (778)]
4- ‘Uthmaan (Radhwiya Allaah ‘anhu) alipotajiwa Tamattu’u ya ‘Umrah kisha Hajj alisema: ((Tamattu’u ni utimilisho zaidi kwa Hajj na ‘Umrah, visifanyike viwili katika mwezi wa Hajj [‘Umrah ifanyike peke yake nje ya mwezi wa Hajj]. Na lau mtaichelewesha ‘Umrah hii ili muizuru Nyumba hii mara mbili, basi ingekuwa bora zaidi, kwani Allaah Ta’alaa Ametanua wigo katika kheri)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Ahmad (1/92) na Ibn Jariyj (2/207) kwa Sanad Swahiyh]
5- Ni kwamba Ifraad haipasi ndani yake kuchinja kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa na hiyo ni kutokana na kukamilika kwake kinyume na Tamattu’u na Qiraan.
6- Ni kwamba umma wote umekubaliana – hivi ndivyo walivyosema wao - kuwa inajuzu Ifraad bila ya umakuruhu kinyume na Tamattu’u na Qiraan, hivyo Ifraad imekuwa ni bora zaidi.
[2] Kauli ya pili: Qiraan ni bora zaidi
Haya ni madhehebu ya Hanafiy na Ath-Thawriy, na riwaya toka kwa Ahmad –kwa aliyeswaga mnyama -, na hoja zao ni:
1- Imethibiti kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa sallam) alinuwia Hajj na ‘Umrah. Kama Hadiyth ya Anas aliposema: Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema:
لبّيك عمرةً وحجّاً
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (4354) na Muslim (1222).
2- Ni neno la ‘Aliyy bin Abiy Twaalib kumwambia ‘Uthmaan wakati alipokataza Qiraan: Hutaki jingine lolote isipokuwa kukataza jambo ambalo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alilifanya? ‘Uthmaan akamwambia: Tuache sisi na jambo letu. Akasema: Hakika mimi siwezi kukuacha. ‘Aliy alipoona mambo hivyo, alinuwia yote mawili. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1569) na Muslim (1222)]
3- Mwenye kufanya Qiraan ni lazima achinje, na chinjo hilo si la kufidia au kuunga kosa, bali ni chinjo la ‘ibaadah, na ‘ibaadah inayofungamana na kiwiliwili na mali ni bora zaidi kuliko inayohusiana na kiwiliwili tu.
4- Mwenye kufanya Qiraan anachakarikia ‘ibaadah, na hilo ni bora zaidi kuliko kuichelewesha.
5- Qiraan inawezesha kufanyika ‘Umrah katika wakati wa Hajj, na hilo ni utukuko zaidi.
[3] Kauli ya tatu: Tamattu’u ni bora zaidi
Ni madhehebu ya Ahmad bin Hanbal, Ahlu Adh-Dhwaahir na Ibn Al-Qayyim, na moja kati ya kauli mbili za Ash-Shaafi’iy. Imesimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar, Ibn ‘Abbaas, Ibn Az-Zubayr, ‘Aaishah na kundi la Salaf [Al-Mughniy (3/260), Al-Majmuw’u (7/150-152), Al-Muhallaa (7/99) na Zaad Al-Ma’aadiy (2/177)]
Hoja zao ni:
1- Hadiyth ya ‘Aaishah: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifanya Tamattu’u kwa (kuanza) ‘Umrah kisha (kumalizia) Hajj, na watu wakafanya Tamattu’u pamoja naye.
Az-Zuhriy amesema: Ni kama vile alivyonielezea Saalim toka kwa Ibn ‘Umar toka kwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1692) na Muslim (1237). Inavyoonekana ni kuwa Tamattu’u inayokusudiwa kwayo hapa ni Qiraan kama alivyosema Sheikh wa Uislamu]
2- Toka kwa ‘Imraan bin Huswayn amesema: Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifanya Tamattu’u, nasi tukafanya Tamattu’u pamoja naye. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy kwa maana yake (1572) na Muslim (1226) na tamko ni lake].
3- Toka kwa Abu Jamrah amesema: Nilifanya Tamattu’u na watu wakanikataza nisifanye hilo. Nikamuuliza Ibn ‘Abbaas, naye akaniamuru kufanya. Nikaona usingizini kana kwamba mtu ananiambia: Hajj Mabruwr na ‘Umrah Mutaqabbalah. Nikamweleza Ibn ‘Abbaas naye akasema: “Sunnah ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam.). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1567) na Muslim (1243)]
4- Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwaamuru Swahaba wake wakati walipotufu Nyumba wavue Ihraam, na waifanye ‘Umrah – kama ilivyotangulia -. Akawahamisha toka kwenye Ifraad na Qiraan na kuwapeleka kwenye Tamattu’u, na yeye hakuwahamisha isipokuwa kwenye zuri zaidi.
5- Hadiyth ya Jaabir aliyesema: Tulihiji pamoja na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) siku alipomswaga ngamia pamoja naye. Watu walishatia niya ya Hajj kwa Ifraad. Akawaambia:
((حلوا من إحرامكم بطواف البيت، وبين الصفا والمروة، ثم أقيموا حلالا حتى إذا كان يوم التروية فأهلوا بالحج، واجعلوا التي قدمتم بها متعة)). قالوا: كيف نجعلها متعة وقد سمينا الحج؟ قال: ((افعلوا ما أمرتكم به، فلولا أني سقت الهدي لفعلت مثل الذي أمرتكم به))
((Vueni Ihraam baada ya Kutufu Nyumba, na [baada ya Kusai] baina ya Swafaa na Marwah, kisha kaeni bila Ihraam mpaka inapofika Siku ya Tarwiyah nuwieni Hajj, na yafanyeni mliyoyatenda kabla kuwa ni Mut-‘ah (Qiraan))). Wakasema: Vipi tutayafanya Mut-‘ah na sisi tumeiita Hajj?”Akasema: ((Fanyeni niliyokuamrisheni, na lau si mimi kumswaga mnyama, ningefanya mfano wa niliyokuamrisheni)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1568) na Muslim (1216)]
5- Tamattu’u imetajwa kiuainisho katika Kitabu cha Allaah Ta’aalaa:
((فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((basi mwenye kufanya Tamattu’u kwa kutekeleza ‘Umrah kwanza kisha Hajj, achinje mnyama aliye mwepesi)). [Al-Baqarah (2:196)]
Lakini ‘amali zingine mbili hazikutajwa.
7- Mwenye kufanya Tamattu’u, zinamkusanyikia kwa pamoja Hajj na ‘Umrah katika miezi ya Hajj zikiwa kamili na zikiwa nyepesi.
8- Kauli yake (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hutangulizwa kabla ya kitendo chake kukitokea ukinzani.
[4] Kauli ya nne: Uchanganuzi
Ni chaguo la Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah (Rahimahu-Allaah) na muhtasari wa maneno yake: [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/85-91)]
(a) Ikiwa atafanya Ifraad ya Hajj peke yake kwa safari moja, na ‘Umrah kwa safari nyingine, basi inakuwa ni bora zaidi kuliko kufanya Qiraan na Tamattu’u katika safari moja mahususi, na hii inakuwa kama alifanya ‘Umrah kabla ya miezi ya Hajj. Na hii ndio Ifraad aliyoifanya Abu Bakr na ‘Umar, na alikuwa anawachagulizia watu kuifanya, na pia ‘Aliyy.
(b) Ama akitaka kukusanya ‘amali mbili (Hajj na ‘Umrah) kwa safari moja, na akafika Makkah katika miezi ya Hajj ilhali hakuswaga mnyama, basi Tamattu’u ni bora zaidi kwake.
(c) Na akitaka kukusanya ‘amali mbili kwa safari moja na akaswaga mnyama, basi Qiraan ni bora zaidi kwa kufuata alivyofanya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ambapo alifanya Qiraan na akaswaga mnyama.
Kisha ni lipi bora kati ya viwili: Aswage mnyama na afanye Qiraan, au afanye Tamattu’u bila kuswaga mnyama na avue Ihraam?
Amesema: “Hapa ni mahala pa ijtihaad kutokana na kukinzana Alilomchagulia Allaah Ta’aalaa Nabiy Wake na lile ambalo Nabiy Wake aliwachagulia Swahaba Zake”. Na yeye Rahimahu-Allaah amelipendelea zaidi la kwanza.
Ninasema: “Uchanganuzi huu unakubalika sana. Ndanimwe, Ibn Taymiyah ameitumia kila nassi katika nususi zilizopokelewa katika mahala pake mwafaka. Kisha akaijaalia aina bora zaidi kwa mujibu wa ugumu wake na uzito wake. Ni kama Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alivyomwambia ‘Aaishah wakati aliposema:
يَا رَسُولَ الله، يَصْدُرُ النَّاسُ بِنُسُكَيْنِ وَأصْدُرُ بِنُسُكٍ؟ فَقال: َإِذَا طَهُرْتِ فَاخْرُجِي إِلَى التَّنْعِيمِ فَأهِلِّي، ثُمَّ ائْتِينَا بِمَكَانِ كَذَا، وَلَكِنَّهَا عَلَى قَدْرِ نَفَقَتِكِ أوْ نَصَبِكِ"
Ee Rasuli wa Allaah, watu watarudi wamefanya Nusuk mbili [Hajj na ‘Umrah] na mimi nitarudi nimefanya Nusuk moja tu [Hajj]. Akamwambia: “Ukitwaharika, basi toka uende At-Tan-‘iym unuwie, halafu njoo mahala fulani utatukuta, lakini malipo ni kwa kadiri ya pesa unayotumia au tabu unayopata” [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1787) na Muslim (1211)]
Kadhalika, ameziweka aina bora zaidi kwa mujibu wa kuswaga mnyama, na yote hayo yametajwa katika Sunnah. Na kwa ajili hiyo, Ibn Taymiyah hakuingia kwenye wimbi la machafuko kama walivyoingia Fuqahaa wengi kutokana na kuona kwao kuwa kilicho bora ndicho hicho hicho na hakuna kingine zaidi yake.
Pamoja na hayo yote, sidharau nguvu ya kauli ya waliosema kuwa Tamattu’u ndio bora zaidi bali ni waajib pia. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Wakazi Wa Haram Hawana Isipokuwa Ifraad
Allaah Ta’aalaa Amesema:
((فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ ۚ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ ۗ تِلْكَ عَشَرَةٌ كَامِلَةٌ ۗ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ))
((Basi mwenye kufanya Tamattu’u kwa kutekeleza ‘Umrah kwanza kisha Hajj, achinje mnyama aliye mwepesi. Na asiyepata basi afunge Swiyaam siku tatu katika Hajj na saba mtakaporejea. Hizo ni kumi kamili. Hayo ni kwa ajili ya yule ambaye watu wake hawaishi karibu na Al-Masjidil-Haraam)). [Al-Baqarah (2:196)]
Hapa Allaah Mtukufu Ameruhusu kufanya Tamattu’u kwa mtu ambaye hana watu karibu na Al-Masjid Al-Haraam, yaani, mtu ambaye makazi yake hayako Makkah au Al-Haram – kwa mujibu wa kauli sahihi zaidi - kwa kuwa Tamattu’u imewekwa kwa ajili yake kwa vile hana watu, na mkazi wa Makkah ana watu wake, hivyo yeye hana hilo la kufanya Tamattu’u. Haya ni madhehebu ya Ibn ‘Abbaas na Abu Haniyfah, na yanatiliwa nguvu na Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ambayo inaeleza:
ثُمَّ أَمَرَنَا عَشِيَّةَ التَّرْوِيَةِ أَنْ نُهِلَّ بِالْحَجِّ، فَإِذَا فَرَغْنَا مِنَ الْمَنَاسِكِ جِئْنَا فَطُفْنَا بِالْبَيْتِ وَبِالصَّفَا وَالْمَرْوَةِ فَقَدْ تَمَّ حَجُّنَا، وَعَلَيْنَا الْهَدْىُ كَمَا قَالَ اللَّهُ تَعَالَى {فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ} [البقرة: 196] إِلَى أَمْصَارِكُمْ. الشَّاةُ تَجْزِى، فَجَمَعُوا نُسُكَيْنِ فِى عَامٍ بَيْنَ الْحَجِّ وَالْعُمْرَةِ، فَإِنَّ اللَّهَ تَعَالَى أَنْزَلَهُ فِى كِتَابِهِ وَسَنَّهُ نَبِيُّهُ - صلى الله عليه وسلم - وَأَبَاحَهُ لِلنَّاسِ غَيْرَ أَهْلِ مَكَّةَ، قَالَ اللَّهُ {ذَلِكَ لِمَنْ لَمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ))
((Kisha akatuamuru jioni ya [Siku ya] Tarwiyah tuhirimie Hajj. Tulipomaliza Manaasik, tulikuja tukatufu Nyumba, na [tukasai] Swafaa na Marwah, Hajj yetu ikatimia na tukawajibikiwa kuchinja kama Alivyosema Allaah Ta’aalaa:
((فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ ۚ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ))
((achinje mnyama aliye mwepesi. Na asiyepata basi afunge Swiyaam siku tatu katika Hajj na saba mtakaporejea)).. kwenye miji yenu. Kondoo anatosha. Wakakusanya Nusuki (‘amali) mbili katika mwaka mmoja kati ya Hajj na ‘Umrah, kwani Allaah Mtukufu Ameiteremsha katika Kitabu Chake na Nabiy Wake (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaiwekea sharia, na Akawaruhusu watu ambao si wakazi wa Makkah kuifanya. Allaah Amesema:
((ذَٰلِكَ لِمَن لَّمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ))
((Hayo ni kwa ajili ya yule ambaye watu wake hawaishi karibu na Al-Masjidil-Haraam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1572)]
Ninasema: “Msingi wa madhehebu haya ni kuwa kiwakilishi kionyeshi (demonstrative pronoun) katika Kauli Yake Ta’aalaa katika Aayah (ذَٰلِكَ)
“Hayo”na katika neno la Ibn ‘Abbaas katika Hadiyth
(أَنْزَلَهُ فِى كِتَابِهِ وَسَنَّهُ نَبِيُّهُ)
“Ameiteremsha”, kinarudi kwa Tamattu’u, nalo liko bayana”.
Na inafaa pia kirudi kwa mnyama, na maana ya Aayah inakuwa: Mwenye kufanya Tamattu’u, basi ni lazima achinje kama si katika wakazi wa Makkah, na kama ni mkazi, basi si wajibu kuchinja. Na haya ndiyo yaliyosemwa na Maalik, Ash-Shaafi’iy na Ahmad, na Ibn Hazm ameunga mkono.
Je, inajuzu kuingiza Hajj ndani ya ‘Umrah?
[Al-Majmuw’u (7/168) na Ash-Sharhu Al-Mumti’u]
Mtu akihirimia ‘Umrah peke yake katika miezi ya Hajj, kisha akaona vyema achanganye na Hajj afanye Qiraan, basi anaweza kufanya hilo kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri (kinyume na Hanafiy) kwa sharti iwe kabla ya kuanza kutufu, na kama ameanza kutufu ijapokuwa kwa hatua moja, basi haijuzu kuingiza Hajj ndani ya ‘Umrah.
Dalili ya hilo ni kuwa ‘Aaishah alipopata hedhi huko Sarif baada ya kuhirimia ‘Umrah, Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwamuru anuwie Hajj akimwambia:
((طوافك بالبيت وبالصفا والمروة، يسعك لعمرتك وحجك))
((Kutufu kwako Nyumba, na Swafaa na Marwah, kunakutosheleza wewe ‘Umrah yako na Hajj yako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1211)]
Na hii ni dalili ya kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kumwamuru ‘Aaishah kunuwia Hajj, hakukuwa ni kuibatilisha ‘Umrah yake.
Lakini, mtu anaweza kusema: Dalili imetokea katika hali inayofanana na dharura kwa kuwa ‘Aaishah hakuweza kukamilisha ‘Umrah yake akiwa na hedhi. Hivyo dalili hapa inakuwa mahsusi zaidi kuliko tukio lenyewe. Hapa kidogo kuna kijiukakasi. Na hili linatiliwa nguvu na Rasuli kumwamuru mtu aliyehirimia Hajj na hana mnyama wa kuchinja aifanye Hajj yake kuwa ‘Umrah. Hivyo vipi tuifanye ‘Umrah kuwa Hajj nako ni kinyume na aliloamuru?
Je, Inajuzu Kuingiza ‘Umrah Ndani Ya Hajj?
[Al-Majmuw’u (7/170), Al-Mughniy (3/512), Al-Mabsuwtw (4/180) na Majmuw’u Al-Fataawaa (26/88)]
- Ama akihirimia Hajj, kisha akaingiza ndani yake ‘Umrah, haitoswihi na hawi ni mwenye kufanya Qiraan. Ni kauli ya Maalik, Ash-Shaafi’iy katika kauli yake mpya na Ahmad. Imekhitariwa na Sheikh wa Uislamu.
- Lakini Abu Haniyfah amejuzisha kwa kujengea juu ya asili yake. Anasema: “Kazi ya mwenye kufanya Qiraan ni zaidi ya mwenye kufanya Ifraad. Akihirimia Hajj na akaingiza ndani yake ‘Umrah, anakuwa ni mwenye kufanya Qiraan na lazima atufu mara mbili na asai mara mbili”.
Ninasema: “Na mimi napondokea kwenye kauli ya Abu Haniyfah – si kutokana na hoja aliyoitoa - bali kwa Hadiyth ya ‘Aaishah isemayo:
أهل رسول الله صلى الله عليه وسلم بالحج)
Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alihirimia Hajj [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1562) na Muslim (1211).
Pamoja na Hadiyth Marfuu ya Ibn ‘Umar isemayo:
((أتاني آت من ربي، فقال: صل في هذا الوادي المبارك وقل: عمرة في حجة))
((Alinijia mwenye kunijia [Jibriyl] toka kwa Mola wangu akasema: Swali katika bonde hili [la Al-‘Aqiyq] lililobarikiwa na sema: ‘Umrah ndani ya Hajj). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1534), Abu Daawuwd (1783) na Ibn Maajah (2976)]
Imekhitariwa na Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah).
Je, Inaswihi Niya Ya Kuhirimia Bila Kuainisha?
Mwenye kuhirimia bila kutaja aina yoyote kati ya ‘amali hizi tatu (Ifraad, Qiraan au Tamattu’u) kwa kutokujua, au akahirimia mithili ya Ihraam ya mtu anayejua, basi hilo linajuzu, na Ihraam yake ni sahihi kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa kinyume na Maalik. Ni kwa Hadiyth ya Abu Muwsaa: Kwamba ‘Aliyy alimwendea Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na Rasuli alimuuliza: Umesema nini ulipohirimia?. ‘Aliyy akasema: Nimesema:
لبيك بإهلال كإهلال النبي صلى الله عليه وسلم
((Labbayka kwa niya kama niya ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa sallam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1734) na Muslim (1221)]
Haijuzu Kuvuka Miyqaat Bila Kuhirimia
[Angalia Al-Majmuw’u (7/212-215)]
Aliyepita Miyqaat – ilhali amekusudia kuhiji au kufanya ‘Umrah - basi haijuzu kwake kuivuka bila kuhirimia. Ni Ijma’a ya ‘ Ulamaa wote. Kama ataivuka kisha akahirimia baada yake basi atapata dhambi kwa kufanya hivyo, na dhambi haiondoki mpaka arudi kwenye Miyqaat ahirimie tena kisha akamilishe ‘ibaadah yake. Si lazima achinje mnyama kama alirudi kwenye Miyqaat kabla hajaanza kufanya ‘amali yoyote ni sawa ikiwa Nguzo kama Kusimama ‘Arafah au Kusai, au Sunnah kama Twawaaf ya Quduwm. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Ath-Thawriy, Abu Yuwsuf, Muhammad na Abu Thawr.
Maalik, Ibn Al-Mubaarak na Ahmad wamesema kuchinja hakutenguki (hakuondoki) kwa kurudi kwake.
Abu Haniyfah kasema kama atarudi huku akipiga Talbiyah basi hatochinja, na akirudi kimya kimya basi lazima achinje.
Na Ibn Al-Mundhir amesimulia toka kwa Hasan na An-Nakh-‘iy kuwa aliyevuka Miyqaat halazimiki kuchinja chochote. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Na kama hakurudi kwenye Miyqaat, basi ‘ibaadah yake ni sahihi, na lazima achinje kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri.
Kuhirimia Kabla Ya Kufika Miyqaat
[Al-Majmuw’u (7/205) kwa mabadilisho kidogo]
Salaf katika Swahaba na waliowafuatia wenye kutambulika vyema kwa misimamo imara ya dini, wamekubaliana wote kwa sauti moja kuwa inajuzu kuhirimia kwenye Miyqaat na kabla ya Miyqaat.
Lakini Daawuwd amesema haijuzu kuhirimia kabla yake na Ihraam haitoswihi (akifanya mtu hivyo). Kauli hii inamrudi yeye mwenyewe kwa kuwepo Ijma’a hiyo. Na pamoja na hivyo, ni makruhu kuhirimia kabla ya Miyqaat kwa mujibu wa kauli sahihi zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Mwenye Kupita Miyqaat Mbili
Raia wa nchi za Sham au raia wa Misri akipita Miyqaat ya watu wa Madiynah kabla hajafika Al-Juhfah (Miyqaat yake ya asili), basi haijuzu kwake kuchelewesha Ihraam, bali inampasa ahirimie toka Dhul Hulayfah (ambayo ni ya watu wa Madiynah) kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri. Ni kwa ujumuishi wa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((ولمن أتى عليهنَّ من غير أهلهنَّ))
((Na kwa yule atakayeingia humo katika wasio wakazi wake)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo kwenye mlango wa Miyqaat]
Abu Haniyfah na Maalik wanaona kuwa si waajib kwake, bali inajuzu akawize kuhirimia hadi afike Miyqaat yake kwa kuwa ndiyo ya asili. Hili pia limekhitariwa na Sheikh wa Uislamu. Lakini la kwanza (la kuhirimia hapo hapo) ni la akiba zaidi (kuliko kukawiza hadi afike Miyqaat yake).
Mwenye Kuhirimia Kuweka Shuruti Ya Kuvua Ihraam Kutokana Na Udhuru Wa Kumzuia Kukamilisha Hajj
Inajuzu kwa aliyehirimia aweke shuruti – wakati anapohirimia - la kuvunja Ihraam yake wakati wowote likimzuia jambo kukamilisha ‘amali yake ya Hajj kama ugonjwa au mfano wake kwa kusema:
((اللهم محلي حيث حبستني))
((Ee Allaah, pangu pa kuvua Ihraam ni pale Utakaponizuia)).
Ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliingia kwa Dhwubaa’ah binti Az-Zubayr akamwambia: (([Huenda] ulitaka kuhiji)). Akasema: Wa-Allaahi, najihisi kuumwa sana. Akamwambia: ((Hiji, na ushurutishe, na sema:
اللهم محلي حيث حبستني
((Ee Allaah, pangu pa kuvua Ihraam ni pale Utakaponizuia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5089) na Muslim (1207)]
Akishurutisha, basi itajuzu ajivue na Ihraam yake likitokea la kumzuia asiendelee, na hatochinja mnyama. Na kama hakushurutisha na likatokea la kumzuia asiendelee, basi ni lazima achinje kutokana na Neno Lake Ta’aalaa:
((فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((Na kama mkizuilika, basi chinjeni wanyama walio wepesi kupatikana)). [Al-Baqarah (2:196)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
12-Sunnah Za Kuhirimia
Alhidaaya.com [3]
1- Kuoga kabla ya kuhirimia
Ni kwa Hadiyth ya Zayd bin Thaabit kwamba ((Yeye alimwona Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amevua nguo kwa ajili ya kuhirimia na akaoga)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (831)]
Mwanamke ataoga hata kama ana hedhi au nifasi. Katika Hadiyth ya Jaabir: ((Mpaka tukafika Dhul Hulayfah, na Asmaa bint ‘Umays akamzaa Muhammad bin Abiy Bakr. Akatuma mtu kwenda kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amuulizie nini afanye? Akasema (Rasuli):
((اغتسلي واستثفري بثوب وأحرمي))
((Oga, na funga vizuri kwa kitambaa sehemu ya damu [utupu], kisha hirimia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim]
2- Kujitia manukato mwilini kabla ya kuhirimia
Ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Nilikuwa nikimtia manukato Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa ajili ya kuhirimia kwake wakati anapohirimia, na kwa ajili ya kuvua kwake Ihraam kabla hajatufu Nyumba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1539) na Muslim (1189)]
Kadhalika, mwanamke hujitia manukato. Ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Tulikuwa tunatoka pamoja na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hadi Makkah, kisha tunavipaka vipaji vyetu vya uso kwa uturi wenye harufu nzuri wakati wa kuhirimia. Na mmoja wetu anapotokwa jasho ulikuwa unavuja juu ya uso wake na Rasuli anauona, na wala hatukatazi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1839) na Al-Bayhaqiy (5/48)]
Ninasema: “Ama baada ya kuhirimia, haitojuzu kutumia manukato yoyote kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa kama alivyonukulu An-Nawawiy katika Al-Majmuw’u (7/270)”.
3- Mwanaume ahirimie kwa vipande viwili vyeupe vya nguo cha chini na cha juu (izari na ridaa)
Toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliondoka Madiynah baada ya kuzichana vizuri nywele zake na kujitia mafuta, na akavaa kipande chake cha chini cha nguo (izaar) na cha juu (ridaa) yeye pamoja na Swahaba wake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1545)]
Na toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((البسوا من ثيابكم البياض، فإنها من خير ثيابكم، وكفنوا بها موتاكم))
((Vaeni katika nguo zenu nyeupe, kwani hizo ni katika nguo zenu bora zaidi, na wakafinieni kwazo maiti zenu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (999) na Abu Daawuwd (3860)]
Ama mwanamke, yeye atavaa nguo yoyote aipendayo, lakini hatovaa niqabu wala glovu kama itakavyokuja mbeleni katika mambo yaliyokatazwa. Nguo yake haihusishwi na rangi maalum kama nyeupe na kadhalika kama wanavyoitakidi akina mama wengi na hususan Wamisri. ((‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) alikuwa anavaa nguo ya rangi nyekundu, akiwa amehirimia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Ibn Hajar katika Al-Fat-h (3/405) ameiegemeza kwa Sa’iyd bin Mansuwr na akasema: “Isnaad yake ni Swahiyh”]
4- Kuswali katika Bonde la Al-‘Aqiyq kwa mwenye kupita hapo
Hili ni bonde lililo karibu na Al-Baqiy’u, na kuna umbali wa maili nne kati yake na Madiynah. [Fat-hul Baariy (3/359)]
‘Umar amesema: ((Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema wakati yuko Bonde la Al-‘Aqiyq:
((أتاني الليلة آت من ربي، فقال: صل في هذا الوادي المبارك وقل: عمرة في حجة))
((Alinijia usiku mwenye kunijia [Jibriyl] toka kwa Mola wangu akasema: Swali katika bonde hili [la Al-‘Aqiyq] lililobarikiwa na sema: ‘Umrah ndani ya Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1534) na wengineo. Tumeitaja nyuma]
5- Kuswali katika Msikiti wa Dhul Hulayfah kwa mwenye kupita hapo
Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anaswali rakaa mbili hapo Dhul Hulayfah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1184)]
Na Hadiyth ya Jaabir inasema: ((Alipofika Dhul-Hulayfah aliswali, kisha aliendelea kubaki kimya mpaka akafika Al-Baydaa)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (2756)]
Angalizo:
Jumhuri wamechukulia toka Hadiyth ya Ibn ‘Umar kuwa ni mustahabu kuswali rakaa mbili kwa ajili ya kuhirimia. An-Nawawiy amesema katika kuisherehesha: “Katika yanayopatiwa faida ndani yake ni kuwa imestahabiwa kuswali rakaa mbili wakati mtu anapotaka kuhirimia, na ataziswali kabla ya kuhirimia, na zitakuwa ni Sunnah. Haya ndiyo madhehebu yetu na madhehebu ya ‘Ulamaa wote isipokuwa yale aliyoyasimulia Al-Qaadhwiy na wengineo toka kwa Al-Hasan Al-Baswriy kuwa imestahabiwa iwe baada ya Swalaah ya Faradhi. Amesema: “Kwa kuwa yeye amesimulia kwamba rakaa hizi mbili zilikuwa ni Swalaat As-Subhi. Lakini la sawa ni kauli ya Jumhuri, navyo ndivyo Hadiyth inavyoonyesha”.
Ninasema: “Bali Hadiyth inavyoonyesha ni kwamba Swalaah imestahabiwa kwa ajili ya Masjid na si kwa ajili ya kuhirimia. Haya yanatiliwa nguvu na Hadiyth ya Ibn As-Samatw: ((Kwamba yeye alitoka pamoja na ‘Umar hadi Dhul-Hulayfah. Akaswali rakaa mbili, nami nikamuuliza kuhusu hilo akasema: Hakika mimi nafanya kama nilivyomwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Ahmad]
Hapa kuhirimia hakukutajwa, bali faida zinazoweza kupatikana kutokana na Hadiyth hiyo ni yale yanayokuja baada yake:
6- Kutia niya ya kuhirimia baada ya Swalaah ya Faradhi au ya Sunnah
Lililo bora ni kuhirimia baada ya mtu kuswali Swalaah ya Faradhi au ya Sunnah kutokana na Hadiyth zilizotangulia. Hili linatiliwa nguvu pia na Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas: ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliswali Adhuhuri Dhul-Hulayfah kisha akaitisha ngamia. Alipokaa juu yake na kutulia naye sawa juu ya mwinuko wa Al-Baydaa alihirimia Hajj)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Ad-Daaramiy (1912), Abu Daawuwd (1752) na Ahmad (2982)]
Ninasema: “Linaloonekana ni kuwa Swalaah aliyoiswali Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kabla hajahirimia ilikuwa ni Swalaah ya Adhuhuri. Inajulikana kwamba Nabiy alikuwa akipunguza Swalaah hapo Dhul-Hulayfah –kama tulivyoeleza katika Swalaah ya Msafiri- hivyo aliswali rakaa mbili”.
Tumeshaitaja Hadiyth ya Rasuli isemayo:
((أتاني آت من ربي، فقال: صل في هذا الوادي المبارك وقل: عمرة في حجة))
((Alinijia mwenye kunijia [Jibriyl] toka kwa Mola wangu akasema: Swali katika bonde hili [la Al-‘Aqiyq] lililobarikiwa na sema: ‘Umrah ndani ya Hajj((. [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma]
Na Swalaah hii aliyoamuriwa inawezekana ikawa ya Faradhi au ya Sunnah. Na kwa ajili hiyo, Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah amesema: “Kama anaswali Faradhi, atahirimia baada yake, na kama haswali basi kuhirimia hakuna Swalaah yake maalumu, na hili ndilo lenye nguvu”. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/108) na mfano wake katika Al-Muhallaa cha Ibn Hazm (7/90)]
7- Kuleta tahmiyd, tasbiyh na takbiyr –juu ya mnyama- kabla ya kuhirimia
Ni kwa yaliyomo kwenye Hadiyth ya Anas: ((…kisha akapanda mpaka ngamia akatulia naye sawa juu ya mwinuko wa Al-Baydaa, hapo alimhimidi Allaah, akasabbih na akakabbir, kisha akahirimia Hajj na ‘Umrah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy na Abu Daawuwd (1779)].
8- Kuelekea Qiblah wakati wa kuhirimia
Toka kwa Naafi’i amesema: ((Ibn ‘Umar alipokuwa anaswali asubuhi Dhul-Hulayfah, alikuwa anaagiza aletewe mnyama wake kisha humpanda. Anapotulia naye sawa, huelekea Qiblah na kuleta Talbiyah, na husema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa sallam) alifanya hivyo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1553)]
9- Kunyanyua sauti wakati wa kuitikia Talbiyah
Ni kwa Hadiyth ya As-Saaib bin Khallaad aliyesema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((جاءني جبريل فقال: يا محمد، مر أصحابك أن يرفعوا أصواتهم بالتلبية))
((Jibriyl alinijia na kuniambia: Ee Muhammad! Waamuru Swahaba wako wanyanyue sauti zao kuitikia Talbiyah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (830), Abu Daawwd (1197), An-Nasaaiy (5/162) na Ibn Maajah (2922)]
Jumhuri wanasema agizo hili ni la Sunnah, na Adh-Dhwaahiriyyah wanasema ni la Wajibu. [Haashiyat As-Sanadiy (5/162)]
Toka kwa Jaabir na Abu Sa’iyd wamesema: ((Tulikuja pamoja na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na sisi tunapaza sauti ya nguvu kuitikia Talbiyah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1148)]
Je, mwanamke atanyanyua sauti yake kuitikia Talbiyah?
‘Ulamaa wote kwa sauti moja wanasema kuwa mwanamke hafanyiwi Talbiyah na mwingine kwa niaba, bali ni lazima ailete yeye mwenyewe. [At-Tirmidhiy ameyanukulu haya katika Al-Jaami’u (849). Ama Hadiyth ya Jaaabir isemayo: ((Tulikuwa tunaleta Talbiyah kwa niaba ya wanawake, na tunatupia viguzo kwa niaba ya watoto)) Hadiyth hii ni Dhwa’iyf, haifai]
Lakini je, mwanamke atanyanyua sauti yake kuleta Talbiyah?
Wengi wamesema hatonyanyua sauti yake kwa Talbiyah. [Hata Ibn ‘Abdul Barri amenukuu Ijma’a juu ya hili. Lakini hili limetenguliwa na kauli ya ‘Aaishah na wengineo kama tutakavyo kuja kuona]
Wametoa hoja kwa haya yafuatayo:
1- Mwanamke ameamuriwa kujisitiri, hivyo ni makruhu kwake kunyanyua sauti kuhofia watu kufitinika naye.
2- Ni kauli yake Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((التسبيح للرجال والتصفيق للنساء))
((Tasbiyh ni kwa wanaume na kupiga vikofi kwa wanawake)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa katika mlango wa Swalaah]
Hivyo basi, Hadiyth inadulisha kuwa hatonyanyua sauti yake kwa kuleta Talbiyah kwa kulinganisha na hali yake katika Swalaah.
3- Yanayosimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar kuwa amesema: ((Mwanamke hapandi juu ya Swafaa na Marwah, na hanyanyui sauti yake katika kuleta Talbiyah)). Hadiyth hii ni Dhwa’iyf. [Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy katika Sunan zake (5/46)]
Lakini wengineo wakiongozwa na ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) wanasema mwanamke hunyanyua sauti yake kwa dalili zifuatazo:
1- Kwa ujumuishi wa kauli ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((جاءني جبريل فقال: يا محمد، مر أصحابك أن يرفعوا أصواتهم بالتلبية))
((Jibriyl alinijia na kuniambia: Ee Muhammad! Waamuru Swahaba wako wanyanyue sauti zao kuitikia Talbiyah)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
Na hilo limejumuishwa kwa wote wanawake na wanaume, na ndilo alilolifahamu ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa).
2- Toka kwa ‘Abdur Rahmaan bin Al-Qaasim toka kwa baba yake amesema: ((Mu’aawiyah alitoka usiku wa An-Nafar [tarehe 12], akasikia sauti ya Talbiyah na kuuliza: Nani huyu? Wakamjibu: Ni ‘Aaishah, amenuwia ‘Umrah toka At-Tan-’iym. ‘Aaishah akaelezwa hilo naye akasema: Lau angeniuliza ningemweleza)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah katika Al-Muswannaf (1/4/389)]
Ibn Hazm amesema kwenye Al-Muhallaa (7/93): “Watu walikuwa wakiyasikia maneno ya Wamama wa Waumini na hakukuwa na ukakasi wowote kwa hilo. Watu wamesimulia kutoka kwao na wao wakiwa katika umri wa miaka 20 na zaidi ya hapo, na hakuna yeyote aliyekhalifu kujuzu hilo na kustahabiwa kwake”.
Kisha akaandika athar zinazogusia hilo.
Ninasema: “Kauli nyoofu zaidi kuhusu hili ni ya Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah (26/115) isemayo: “Na mwanamke atanyanyua sauti yake kiasi cha kusikia swahiba wake pembeni”.
Mwenye Hedhi Na Mwenye Nifasi Huhirimia Na Huleta Talbiyah
Tumeshaeleza nyuma kuwa mwenye hedhi na mwenye nifasi hawazuiliwi kuhirimia Hajj, na kuwa imesuniwa kwao kuoga. Aidha, wawili hao hunuwia Hajj baada ya kuoga. Toka kwa ‘Aaishah amesema: ((Asmaa bint ‘Umays alipata nifasi kwa kumzaa Muhammad bin Abiy Bakr huko Ash-Shajarah, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akamwamuru aoge na atie niya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1209), Abu Daawuwd (1744) na Ibn Maajah (2911)]
Na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia ‘Aaishah -alipopata hedhi-:
((افعلي ما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت))
((Fanya (yote) ayafanyayo mwenye kuhiji isipokuwa tu usitufu Nyumba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (294) na Muslim (1211)]
Ash-Shaafi’iy amesema katika Al-Ummu (2/134): Pamoja na Talbiyah katika ayafanyayo Hujaji.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
13-Tamko La Talbiyah
Alhidaaya.com [3]
Maana ya Talbiyah (التلبية) ni kuitikia Wito wa Allaah Ta’aalaa Alioutoa kwa Viumbe Vyake wakati Alipowaita kwenda kuhiji katika Nyumba Yake kupitia ulimi wa Kipenzi Chake Ibraahiym Alayhis Salaam. Na mwitikiaji (الملبي) [Hujaji] ni mwenye kujisalimisha na kuwa mtiifu kwa mwingine kama anavyoburuzwa aliyekunjwa shati kooni. Na maana: Mimi ni mwenye kukujibu Wito Wako, mwenye kujisalimisha kwenye Hukmu Yako, mwenye kutii Amri Yako, mara baada ya nyingine, na nitaendelea kuwa juu ya hayo.
Kayaeleza haya Sheikh wa Uislamu (Rahimahu-Allaah) akiizungumzia Hijjah ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam (uk. 550).
Toka kwa Naafi’i toka kwa Ibn ‘Umar kwamba Talbiyah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ilikuwa:
((لبيك اللهم لبيك، لبيك لا شريك لك لبيك، إن الحمد والنعمة لك والملك، لا شريك لك))
Amesema: Na ‘Abdullaah bin ‘Umar alikuwa akiongezea tamko hilo kwa kusema:
((لَبَّيْكَ وَسَعْدَيْكَ، وَالْخَيْرُ فِي يَدَيْكَ، والعمل))
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1549) na Muslim (1184) na ziada ni yake]
Na katika Hadiyth ndefu ya Jaabir: ((..na Rasuli akanyanyua sauti akitamka Tawhiyd akisema:
((لبيك اللهم لبيك، لبيك لا شريك لك لبيك، إن الحمد والنعمة لك والملك، لا شريك لك،))
Na watu wakaitikia kwa sauti kwa hili ambalo wanaliitikia (kivingine na tamko la Rasuli). Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakuwajibu kitu, bali aliendelea na Talbiyah yake..)). Hadiyth [Swahiyh. Imetajwa nyuma kamili]
Na katika riwaya: ((Na watu wakaitikia kwa sauti kwa hili ambalo wanaliitikia kwa sauti [kinyume na matamshi ya Rasuli]:
((لبيك ذا المعارج، لبيك ذا الفواضل))
Na Rasuli hakujibu….)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1812) na Ahmad (13918)]
Na pia imepokelewa toka kwa Abu Hurayrah kwa njia swahiyh kwamba: ((Ilikuwa ni katika Talbiyah yake –‘Alayhis Swalaat Was Salaam-:
((لبيك إله الحق))
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (2752) na Ibn Maajah (2920)]
Ninasema: “Tunapata faida mambo mawili kutokana na Hadiyth hizi:
1- Inajuzu kuongezea juu ya Talbiyah aliyoileta Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa kuwa aliwakubalia Swahaba wake kuongeza kwa yaliyothibiti toka kwa Ibn ‘Umar na wengineo.
2- Kutosheka na Talbiyah ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ni bora zaidi kwa kuwa yeye alishikamana nayo. Ash-Shaafi’iy (Rahimahu-Allaah) amesema: “Kama ataongeza chochote katika Talbiyah cha kumtukuza Allaah, basi hakuna ubaya. Nami napenda mtu atosheke na Talbiyah ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) tu”.
Na ameungana na madhehebu ya Jumhuri kama ilivyo katika Al Fat-h (3/480).
Mwahala Pa Kuleta Talbiyah
Imesuniwa kukithirisha kuleta Talbiyah tokea mtu anapohirimia na baada ya hapo wakati wote akiwa juu ya kipando, anatembea, anapanda, anashuka na katika hali zote mpaka atakapotupia Jamarat Al-‘Aqabah –kwa kauli ya Jumhuri- kinyume na Maalik.
Katika yanayoonyesha hilo ni kuwa uhalali wa Talbiyah umethibiti katika mwahala pafuatapo:
1- Wakati wa kupanda na kushuka njiani
Toka kwa Ibn ‘Abbaas ikiwa Marfuu: -katika Hadiyth ya Dajjaal- :
((أما موسى كأني أنظر إليه إذا انحدر في الوادي يلبي))
((Ama Muwsaa, kana kwamba mimi ninamwangalia naye anashuka kwenye bonde akipiga Talbiyah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukaariy (1555) na Muslim (166)]
Al-Haafidh kasema: “Hadiyth inatuhabarisha kuwa Talbiyah katika vitovu vya mabonde ni katika mwenendo wa Mitume, na inakokotezeka zaidi wakati wa kuteremka na wakati wa kupanda”. [Fat-hul Baariy (3/485)]
2- Wakati wa kwenda ‘Arafaat
Toka kwa Anas bin Maalik kuwa aliulizwa –naye anatoka asubuhi mapema toka Minaa kwenda ‘Arafaat -kuhusu Talbiyah: Vipi mlikuwa mnafanya na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa wasallam)? Akasema: ((Mwenye kulabbiy alikuwa analeta Talbiyah na hakatazwi, na mwenye kuleta Takbiyr alikuwa analeta Takbiyr na hakatazwi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1659) na Muslim (1284)]
3- Wakati wanapoondoka toka Kisimamo cha ‘Arafah mpaka watakapotupia vijiwe
Toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba Usaamah alikaa nyuma ya Nabiy (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) [juu ya ngamia wa Nabiy] toka ‘Arafah hadi Muzdalifah, kisha Al- Fadhwl alikaa nyuma ya Nabiy toka Muzdalifah hadi Minaa. Akasema: Wote wawili wamesema: Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakuacha kupiga Talbiyah mpaka alipotupia vijiwe Jamaratul Aqabah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1544) na Muslim]
An-Nawawiy kasema: “Na hii ni dalili kuwa ataendelea kuleta Talbiyah mpaka pale atakapoanza kutupia Jamaratul Aqabah asubuhi ya tarehe kumi (Yawm An-Nahr)”. [Yaani, riwaya ya Muslim isemayo: Hakuacha kuleta Talbiyah mpaka alipofika Al Jamarah]
Na haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Sufyaan, Ath-Thawriy, Abu Haniyfah, Abu Thawr, Jumhuri ya ‘Ulamaa katika Swahaba, Taabi’iyna, Fuqahaaul Amswaar na waliokuja baada yao.
Ahmad, Is-Haaq na baadhi ya Salaf wamesema: Ataleta Talbiyah mpaka amalize kutupia vijiwe Jamaratul Al-Aqabah. Lakini Jumhuri wamewajibu wakiwaambia kuwa muradi wake ni mpaka atakapoanza kutupia ili riwaya mbili zioanishwe.
Toka kwa Ibn Mas’uwd amesema: ((Nasi tukiwa Muzdalifah, nilimsikia yule ambaye ameteremshiwa Suwrat Al-Baqarah akisema katika sehemu hii tuliposimama:
"لبيك اللهم لبيك"
[Imekharijiwa na Muslim (1383) na An-Nasaaiy (5/265)]
Angalizo:
Maalik anasema kuwa ataikata Talbiyah wakati wa kuingia Makkah, atatufu na atasai, kisha ataanza tena kuleta Talbiyah hadi Adhuhuri ya Siku ya ‘Arafah. Dalili yao ni Hadiyth ya Naafi’u aliyesema: ((Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alikuwa anapoingia mwanzoni mwa Al-Haram huacha Talbiyah, kisha hulala Dhuw Tuwaa, halafu huswali huko Asubuhi na huoga, na hueleza kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anafanya hivyo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1573) na wengineo].
Al-Haafidh kasema: “Neno lake: ((alikuwa anafanya hivyo)), linachukulika kuwa linaashiria kitendo chake cha mwisho ambacho ni kuoga. Pia linachukulika kwa vyote, nalo ndilo lenye nguvu zaidi”. [Fat-hul Baariy (3/509)]
Lakini yeye amesema (Rahimahu-Allaah): “Inavyoonekana ni kuwa amekusudia kuwa atajizuia kuleta Talbiyah ndani ya Msikiti ambao ameutaja kama Al-Haram, na muradi wa kujizuia na Talbiyah ni kujishughulisha na kutufu na ‘ibaadah nyinginezo, na si kuiacha kabisa.
Pia inaonekana kuwa muradi wa kujizuia ni kuacha kuikariri Talbiyah, au kuendelea nayo mfululizo, au kunyanyua sauti katika kuileta, mambo ambayo hufanyika mwanzoni mwa kuhirimia, na si kuiacha kabisa. Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi”.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
14-Marufuku Za Ihraam
Alhidaaya.com [3]
Ni mambo ambayo Allaah Amemkataza aliyehirimia kuyafanya, na Akamharamishia madhali yuko kwenye Ihraam. Marufuku hizi ziko vigawanyo viwili.
(a) Marufuku Inayoharibu Hajj
Ni kujimai kabla ya tahalluli ya kwanza (kabla ya kutupia Jamaratul Aqabah kwa mujibu wa kauli yenye nguvu zaidi). Hii ni marufuku yenye madhambi makubwa zaidi na yenye athari mbaya zaidi kwa ‘amali ya Hajj. Allaah Amesema:
((فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ))
((Na atakayekusudia kuhiji (akahirimia), basi asifanye tendo la ndoa wala ufasiki wala mabishano katika Hajj)). [Al-Baqarah (2:197)]
Imepokewa kauli swahiyh toka kwa Ibn ‘Abbaas, Ibn ‘Umar na Qataadah kuwa maana ya الرفث katika Aayah hii ni kujimai. [Angalia athari hizi katika Tafsiyr At-Twabariy (4/125-126) kwa Asaaniyd Swahiyhah]
Wengine wamesema الرفث ni kumzungumzisha mwanamke maneno yasiyolaiki kuhusiana na jimai na mfano wake. Ibn Jariyr amekhitari kuwa neno ni jumuishi na linakusanya maana hizo zote.
Ibn Qudaamah amesema: “Ama kufisidika Hajj kwa kujimai kwenye utupu, hili halina mvutano”. [Al-Mughniy (3/334), na Al-Ijma’a cha Ibn Al-Mundhir (uk. 1444)]
Ibn Al-Mundhir kasema: “ ’Ulamaa wote wamekubaliana kuwa Hajj haifisidiki kwa kufanya jambo lolote baada ya kuhirimia isipokuwa jimai tu”.
Ninasema: “Hapa kuna mambo kadhaa:
La kwanza:
Ama kutolea dalili Aayah hii Tukufu kwa kusema kwamba maana ya الرفث hapo ni jimai, sisi tunaona kuwa shabaha kuu inayolengwa hapo ni kuzuia jimai isifanywe, na sio kwamba jimai inafisidi Hajj. Na kama si hivyo, basi ingelazimu kusema kuwa mabishano pia yanafisidi Hajj, na hakuna aliyesema hilo [isipokuwa Ibn Hazm]. [Ar-Rawdhwat An-Nadiyyah (1/254)]
La pili:
Hakuna katika suala hili Hadiyth yoyote Swahiyh Marfuw’u toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam).
La tatu:
Ijma’a iliyonukuliwa na Ibn Al-Mundhir na wengineo, je inatenguka kwa aliyoyanukuu Ash-Shawkaaniy katika kitabu chake cha Nayl Al-Awtwaar toka kwa Daawuwd Adh-Dhwaahiriy? Kwa msingi kwamba Ijma’a hii haijajikita kwa nguvu moja kwenye jambo lenyewe mbali na khitilafu ambazo zinaweza kupatikana katika mchanganuo wake.
Ibn ‘Abbaas na Abu Haniyfah wamesema: “Hajj haitenguki kwa kujimai baada ya [Kusimama] ‘Arafah”.
Na Maalik amesema: “Akijimai Yawm An-Nahr (tarehe kumi) kabla ya kutupia Jamarah, Hajj yake itabatilika, na kama atajimai Yawm An-Nahr baada ya kutupia Jamarah, basi Hajj yake haibatiliki. Na kama atajimai baada ya Yawm An-Nahr kabla ya kutupia Jamarah, basi Hajj yake haibatiliki?”
Ash-Shaafi’iy kasema: “Akijimai katika kipindi cha baina ya Kuhirimia na Kutupia Jamaratul Aqabah, basi Hajj yake itaharibika. Na kama atajimai baada ya Kutupia, basi Hajj yake ni kamili”.
Kisha wamekhitalifiana makhitalifiano mengi kuhusiana na linalompasa kufanya mtu aliyejimai kama itakavyokuja mbeleni. [Angalia Al-Muhallaa (7/189)]
La nne: Ni ipi adhabu ya mwenye kujimai? Nini afanye?
Mtu akimwingilia mkewe kabla ya tahalluli ya kwanza, atapata madhambi na Hajj yake itabatilika kwa mujibu wa kauli ya ‘Ulamaa wengi. Atapaswa kuikamilisha Hajj yake –pamoja na kuharibika kwake- kutokana na Kauli Yake Ta’aalaa:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
((Na timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah)).
Na wote wawili (mke na mume) ni lazima wahiji mwaka ujao pamoja na kuchinja (ngamia).
Hivi ndivyo walivyofutu Ibn ‘Umar, Ibn ‘Amri na Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhum). Toka kwa ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa baba yake amesema: ((Mtu mmoja alimwendea Ibn ‘Umar akamuuliza kuhusu mtu aliyehirimia akamwingilia mkewe. [Ibn ‘Umar] akamwelekeza aende kwa ‘Abdillaah bin ‘Amri, naye akamwambia kuwa Hajj yake imebatilika. Akauliza: Je, akae asihiji tena? Akasema hapana, bali atoke pamoja na watu na afanye kama wanavyofanya. Na kama mwaka ujao utamkuta, basi ahiji na achinje. Wakarudi wote wawili kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar wakamweleza. Tukatuma mtu kwenda kwa Ibn ‘Abbaas amuulize. Naye akamwambia yale yale aliyoyasema Ibn ‘Umar. Akarudi kwake akamweleza, na mtu yule akamuuliza: Na wewe unasemaje? Akasema: Kama walivyosema)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (1/4/142) na Al-Bayhaqiy (5/167)]
Lakini Adh-Dhwaahiriyyah wanaona kuwa jimai huharibu ‘amali za Hajj na huzibatilisha, na mfanyaji ataondoka na hatoendelea na Hajj yake, kwa kuwa ‘amali yenyewe ishaharibika. Wamesema: “Imepokelewa Hadiyth Swahiyh toka kwa Rasuli wa Allaah (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuwa Hajj ni mara moja tu. Hivyo basi, mwenye kumlazimisha aendelee na Hajj hiyo mbovu, kisha amlazimishe tena afanye Hajj nyingine (mwakani), basi anakuwa amemlazimisha Hajj mbili, na hii ni kinyume na agizo la Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)”. [Al-Muhallaa (7/189) na zinazofuatia)]
Baadhi ya Taabi’iyna wamesema kuwa atafanya tahalluli kwa kufanya ‘Umrah na atalipa. Wanaifanya kuwa ngazi ya mtu ambaye amepitwa na Kisimamo cha ‘Arafah. Hivyo atatahallal kwa ‘Umrah na kuvua Ihraam.
Ninasema: “Hakuna shaka kuwa lililo na nguvu zaidi ni kauli sahihi waliyosema ‘Ulamaa watatu Swahaba na kutekelezwa na Wanachuoni wengi ya kuwa Hajj ya mwenye kujimai huharibika na anawajibika kuendelea na Hajj yake. [Imehadithiwa pia kuharibika Hajj kutokana na kujimai toka kwa ‘Umar, ‘Aliyy na Abu Hurayrah kwa Asaaniyd Dhwa’iyf].
Na kuwafuata Swahaba katika hili ni bora zaidi kutokana na ukina wa ufahamu wao na usahihi wa rai zao, na hususan pakizingatiwa kuwa hilo ni la akiba zaidi katika dini. Allaah Ndiye Mjuzi zaidi”.
Faida kadhaa:
1- Ikiwa mwanamke atalazimishwa kufanya jimai, basi Hajj yake ni sahihi na hakuna fidia juu yake kinyume na mume wake kwa mujibu wa kauli mbili sahihi za ‘Ulamaa. [Angalia Al-Majmuw’u (7/404)]
2- Akijimai baada ya tahalluli ya kwanza na kabla hajatufu na kusai, basi Hajj yake haiharibiki lakini atapata dhambi. Ni lazima atoke kwenye Ihraam na ahirimie tena upya –akiwa amevaa nguo zake za Ihraam (izaar na ridaa)- ili atufu Twawaafu ya Ifaadhwah akiwa amehirimia, kwa kuwa aliharibu sehemu iliyobaki ya Ihraam yake. Hivyo ni lazima aanze upya na atoe fidia. [Ash-Sharh Al-Mumti’u cha Ibn ‘Uthaymiyn (7/184)]
3- Akijimai kabla ya tahalluli ya kwanza kwa kusahau kuwa ameshahirimia [Al-Muhallaa (7/186) na Al-Majmuw’u (7/364)]
Akijimai aliyehirimia kabla ya kutahaluli na ‘Umrah, au kabla ya tahalluli ya kwanza ya Hajj hali ya kuwa amesahau kuwa ameshahirimia, basi kauli sahihi inasema kuwa Hajj yake haiharibiki, na hatotoa kafara yoyote wala kingine chochote. Na hii ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُم بِهِ وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ))
((Na wala hakuna dhambi juu yenu katika yale mliyoyakosea, lakini isipokuwa katika yale yaliyoyakusudia nyoyo zenu)). [Al-Ahzaab (33:5)]
(b) Marufuku Zenye Kufisidi Hajj
1- Mwanaume kuvaa nguo iliyoshonwa
Ni haramu kwa mwanaume kuvaa nguo iliyoshonwa au inayofanana nayo kwa kiasi cha kiungo cha mwili. [Al-Majmuw’u (7/269) na Al-Muhallaa (7/80). Nguo iliyoshonwa haikusudiwi yenye uzi, kwani Sunnah ni kuvaa kipande cha chini na cha juu [izari na ridaa] hata kama vimeshonwa kwa makubaliano ya Maimamu]
Asivae shati, suruali, kilemba, kofia, juba, khufu mbili, soksi mbili, glovu mbili na mfano wake. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar kwamba mtu mmoja alisema: Ee Rasuli wa Allaah! Ni nguo zipi anavaa mwenye kuhirimia? Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akasema:
((لا يلبسُ القمص، ولا العَمَائِمَ ، وَلاَ السَّرَاوِيلاَتِ، ولا البَرنس، ولا الخِفَافَ، إلا أحدٌ لا يجِدُ نَعْلَيْنِ، فَلْيَلْبَسْ خُفَّيْنِ، وَلْيَقْطَعْهُمَا أسفلَ من الكعبين، وَلا يَلْبَسْ من الثياب شيئا مَسَّهُ زَعْفَران أوْ وَرْسٌ))
((Asivae nguo yenye mikono [kama kanzu au shati], wala vilemba, wala suruali, wala barnas [vazi linalofunika mwili hadi kichwa], wala khufu isipokuwa mtu ambaye hana viatu, huyo atavaa khufu mbili, na azikate chini ya visigino viwili. Na wala asivae nguo yoyote yenye harufu ya zafarani au wars [aina ya mmea wenye harufu nzuri])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1542) na Muslim (1177)]
Faida
Kivazi hiki kilichoharamishwa kwa mwanaume kinachukulika kwa namna ilivyozoeleka katika kila kivazi. Ikiwa atajizungushia kanzu, au akajitanda juu au akajitanda chini kwa suruali jambo ambalo si la kawaida, basi hakuna tatizo kwa hili, kwa kuwa hapo suruali inakuwa ni kama kipande cha juu na cha chini cha Ihraam (izaar na ridaa). [Al-Majmuw’u (7/270) na Majmuw’u Fataawaa Sheikh Al-Islaam (26/109)]
Asiyepata isipokuwa suruali na khufu mbili
Ambaye hakupata kipande cha juu na cha chini cha Ihraam lakini akapata suruali na khufu mbili –na akazihitajia kutembelea- basi inajuzu kwake kuvaa anachokipata. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas aliyesema: ((Nabiy (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitukhutubia ‘Arafaat akisema:
((من لم يجد الإزار فليلبس السراويل، ومن لم يجد النعلين فليلبس الخفين))
((Asiyepata kipande cha chini (izaar), basi avae suruali, na asiyepata viatu basi avae khufu mbili)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1843) na Muslim (1178)]
Hadiyth hii inadulisha kuwa inajuzu kuvaa suruali kama ilivyo –kama hakupata kipande cha chini- na halazimishwi aipasue ili ajitande nayo chini –kama wanavyosema Fuqahaa wa Kihanafiy- na wala hatodaiwa chochote; si fidia wala kingine chochote. Kwa kuwa, lau fidia ingelikuwa wajibu, basi Nabiy angesema hilo. Na haya ni madhehebu ya Jumhuri kinyume na Mahanafiy.
Kama hakupata viatu, atavaa khufu mbili. Lakini je, atazikata –kama ilivyokuja kwenye Hadiyth ya Ibn ‘Umar? au hatozikata kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas?
Ahmad amesema si lazima azikate, na kauli hii imekhitariwa na Ibn Taymiyah ambaye amesema: “Ni bora ahirimie na viatu viwili ikiwa ni wepesi.. na kama hakupata viatu viwili, basi atavaa khufu mbili, na si lazima azikate chini ya visigino viwili. Kwani Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliamuru kukata mwanzoni, kisha akaruhusu baada ya hapo kuzivaa kama zilivyo huko ‘Arafaat. Kwanza aliruhusu zilizokatwa, kwa kuwa zinakuwa kama viatu kwa kukatwa”.
Wengine wamesema: Kukata khufu mbili ni uharibifu wa mali, nao umekatazwa.
Lakini Jumhuri wamesema ni lazima kukata sehemu iliyo chini ya vifundo viwili vya miguu kwa kuipa nguvu Hadiyth ya Ibn ‘Umar ambayo imegusia kukata chini ya vifundo viwili badala ya Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ambayo haijagusia hilo bali imeacha mlango wazi.
Ninasema: “Na hili ni bora zaidi kuliko la kwanza. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
2- Mwanaume kufunika kichwa chake kwa chenye kushika kichwa
Mwanamume asivae kofia (kibaragashia) wala kilemba na mfano wake. Ni kwa kauli yake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) katika Hadiyth iliyotangulia nyuma kidogo ya Ibn ‘Umar isemayo:
((لا يلبس القمص ولا العمائم))
((Asivae nguo yenye mikono [kama kanzu au shati], wala vilemba)).
Asifunike kichwa chake kwa khimari (ghutrah na mfano wake) kutokana na ujumuishi wa neno lake (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuhusiana na Swahaba aliyeangushwa na ngamia wake ‘Arafah akavunjika shingo na kufa:
((ولا تخمروا رأسه))
((Na wala msifunike kichwa chake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1851) na Muslim (1206)]
Na hii ni jumla ya kila kifunikacho. Haisemwi kuwa inahusishwa tu na vilemba pasina vingine vyenye kufunika kichwa, kwani cha jumla hakihusishwi na kimoja katika vipengele vyake isipokuwa katika hali ya kukinzana –kama inavyoelezwa katika taaluma ya Usuwl- na hapa hakuna mkinzano. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Na kama atakaa kwenye kivuli cha kitu kisichogusana naye kama mwavuli, au gari, au mti na mfano wake, basi hakuna ubaya kwa hilo kama tutakavyokuja kuzungumzia hilo mbeleni.
3- Mwanamke kuvaa niqabu, burqui na glovu mbili
Ni kwa ziada ya yaliyokuja kwenye Hadiyth ya Ibn ‘Umar iliyotangulia katika kauli yake:
((ولا تنتقب المحرمة، ولا تلبس القفازين))
((Na mwanamke aliyehirimia havai niqabu, wala havai glovu mbili)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1838), Abu Daawuwd (1825), At-Tirmidhiy (833) na An-Nasaaiy (5/133)]
Matamshi haya yana mvutano: Je yamesemwa na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)? Au yapo katika orodha ya semi za Ibn ‘Umar?
Al-Haafidh katika Al Fat-h katilia nguvu la mwisho. [Angalia: Fat-hul Baariy (4/64). Imetiliwa nguvu na Sheikh wetu –Allaah Amhifadhi- katika Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/483)]
‘Ulamaa wamekhitalifiana suala la mwanamke kuvaa niqabu. Jumhuri wamezuia lakini Mahanafiy wamejuzisha. Ni kwa riwaya iliyoko kwa Fuqahaa wa Kishaafi’iy na Kimaalik. [Fat-hul Baariy (4/65)]
Ninasema: “Kwa msingi wa kauli inayokataza mwanamke aliyehirimia kuvaa niqabu, inajuzu kwake kuuteremsha ushungi wake toka kichwani hadi usoni wanapopita wanaume wasio maharimu wake sawasawa ukigusa uso wake au usiguse, kwa kuwa mwanamke kakatazwa niqabu, na kushusha ushungi hakuzingatiwi kama niqabu. Dalili ya hili zitakuja mbeleni, si mbali”.
4- Mwanaume au mwanamke aliyehirimia kutumia manukato mwilini au kwenye nguo
Ni kwa kauli ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) katika Hadiyth ya Ibn ‘Umar:
((ولا تلبسوا من الثياب شيئا مسّه زعفران أو ورس))
((Na wala msivae nguo yoyote yenye harufu ya zafarani au wars [aina ya mmea wenye harufu nzuri])). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
Na kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa mhirimiaji aliyevunjwa shingo na ngamia wake:
((لا تحنّطوه، ولا تخمروا رأسه، فإنه يبعث يوم القيامة ملبيا))
((Msimtie manukato, na wala msifunike kichwa chake, kwani hakika yeye atafufuliwa Siku ya Qiyaamah huku akileta Talbiyah)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
5- Kunyoa nywele za kichwa
Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((وَلَا تَحْلِقُوا رُءُوسَكُمْ حَتَّىٰ يَبْلُغَ الْهَدْيُ مَحِلَّهُ))
((Na wala msinyoe vichwa vyenu mpaka mnyama afikie machinjoni pake)). [Al-Baqarah (2:196)]
‘Ulamaa wote wanasema ni haramu kunyoa kichwa sawasawa mwanaume au mwanamke, na kama atanyoa, basi atalipa fidia. [Al-Majmuw’u cha An-Nawawiy (7/262)]
Lakini kama nywele zitamsababishia adha, itajuzu kuzinyoa lakini atatoa fidia. Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ بِهِ أَذًى مِّن رَّأْسِهِ فَفِدْيَةٌ مِّن صِيَامٍ أَوْ صَدَقَةٍ أَوْ نُسُكٍ))
((Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au ana vya kumuudhi kichwani mwake (ikambidi anyoe); basi atoe fidia kwa kufunga Swiyaam au kutoa swadaqah au kuchinja mnyama)). [Al-Baqarah: (2:196)]
Aayah hii ilishuka kwa sababu ya Ka-’ab bin ‘Ajarah wakati Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipompitia –akiwa amehirimia- huku chawa wakipukutika usoni kwake. Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akamuuliza: ((Je, vijidudu hivi vinakusumbua?)). Akasema: Na’am. Akamwambia:
((احلق رأسك، وصم ثلاثة أيام، أو أطعم ستة مساكين، أو أنسك بشاة))
((Nyoa kichwa chako, na funga siku tatu, au lisha masikini sita, au chinja mbuzi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1814), Muslim (1201) na wengineo.
Je, inakatazwa kukata nywele tu au kunyoa sehemu nyingine isiyo kichwa?
An-Nawawiy amesema: [Al-Majmuw’u (7/262)]: “Maswahibu zetu wamesema: Haramisho halihusiani na kunyoa kichwa tu, bali huharamishwa kuondosha nywele kabla ya wakati wa tahallul. Na kwa kuziondosha, ni lazima kutoa fidia ni sawa nywele za kichwa, ndevu, sharubu, kwapa, kinena na sehemu nyingine za mwili. Na ni sawa akiziondosha kwa kunyoa, au kupunguza, au kuzinyofoa, au kuzichoma na mfano wa hivyo. Na hakuna khilafu katika haya yote kwetu sisi”.
Ninasema: “Hakuna shaka kuwa dalili ni mahsusi zaidi kuliko hukmu. Hivyo haiswihi hukmu kutolewa dalili isipokuwa kama itasemwa: “Dalili hapa ni Qiyaas”. Kwa hiyo tunasema: Asli na tanzu ni lazima ziwe sawa katika sababu. Mwenye kuifanya sababu ya katazo la kunyoa kichwa kuwa ni kuzuia burudiko la mwili (nao ni usemi wa walio wengi), basi huyo atazuia kunyoa nywele nyingine za mwili. Na mwenye kuifanya sababu kuwa Muhrim akinyoa kichwa chake, basi anapomosha kwa kunyoa huko nusuk halali ambayo ni kunyoa au kupunguza, basi huyo hatozuia isipokuwa kunyoa kichwa tu. Wameliunga hili mkono kwa kusema kuwa asili ni halali katika kinachoondoshwa katika nywele, na hilo halizuiliwi isipokuwa kwa dalili”. [Amelieleza hili Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu-Allaah) katika Al-Mumti’u (7/131-133)]
Ninasema tena: “Pamoja na yote hayo, la akiba zaidi ni kuifuata kauli ya Jumhuri katika suala hili inayokataza kunyoa nywele za kichwa chake, sharubu zake, kwapa zake na kinena chake. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.”
Faida
Hakuna ubaya kwa Muhrim kukuna kichwa chake hata kama zitadondoka nywele bila kukusudia kuzidondosha.
6- Kukata kucha
Ibn Al-Mundhir amenukuu Ijma’a isemayo ni haramu kwa Muhrim kukata kucha. Ibn Qudaamah amesema: “ ‘Ulamaa wamekubaliana wote kuwa ni marufuku kwa Muhrim kukata kucha zake. Wengi wao akiwemo Hammaad, Maalik, Ash-
Shaafi’iy, Abu Thawr na Asw-haab Ar-Ra-ay wanasema ni lazima alipe fidia akizikata”.
Na ‘Atwaa amesema: “Si lazima atoe fidia, kwa kuwa sharia haikugusia hilo”. [Al-Ijma’a cha Ibn Al-Mundhir (57) na Al-Mughniy (5/388)]
Ninasema: “Ikiwa mwono wa Ijma’a ni sahihi, basi utakuwa ni hujja wajibishi. Na kama si sahihi, basi utafiti ufanyike kujua undani kama ilivyo katika suala lililopita la kunyoa nywele za sehemu nyingine za mwili”.
Lakini Daawuwd Adh-Dhwaahiriy amelikhalifu hili kwa kujuzisha kukata kucha zote na bila fidia yoyote. [Al-Majmuw’u (7/263)]
An-Nawawiy kasema: “Ibn Al-Mundhir na wengineo wamenukuu Ijma’a ya Waislamu ya kuharamisha kukata kucha katika Ihraam, na huenda wao hawakumzingatia Daawuwd, na kumzingatia ndani ya Ijma’a ni kutegua uwiano..”.
Ninasema: “Ibn Hazm vile vile amelikhalifu hili kwenye Kitabu chake cha Al-Muhallaa (7/246). Amejuzisha kukata kucha”.
Faida
Ash-Shanqiytwiy (Rahimahu-Allaah) katika Kitabu chake cha Adhwaaul Bayaan (5/404) ametoa dalili ya kuharamisha kukata kucha kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
ثُمَّ لْيَقْضُوا تَفَثَهُم
kwa mujibu wa Tafsiyr ya baadhi ya Swahaba na Taabi’iyna waliosema kuwa قضاء النفث maana yake ni kunyoa kichwa, kukata kucha, na kunyofoa nywele za kikwapa. Akasema (Rahimahu-Allaah) “Na kwa msingi wa tafsiyr tajwa, Aayah inadulisha kuwa kucha ni kama nywele kwa aliyehirimia, na hususan kuchinja mnyama kukiwa “kumeatwifiwa”na ثُمَّ. Hivyo imedulisha kuwa kunyoa, kukata kucha na mengineyo, yanatakikana yafanywe baada ya kuchinja”.
Faida
Kucha yake ikivunjika, basi aikate, na hapana kitu juu yake.
7- Vishawishi vya jimai
An-Nawawiy kasema: “Ni haramu kujikabilisha na yenye kusisimua matamanio ya kimwili kama kumweka mke mapajani, kumpiga kisi na kumgusa kwa mkono kwa matamanio kabla ya tahalluli mbili. Ikiwa ameshaingia kwenye Ihraam halafu akafanya kusudi kujikabilisha na matamanio hayo, basi ni lazima fidia, nayo ni mbuzi au badali yake ya kulisha masikini au kufunga. Halazimiwi fidia ya ngamia ni sawa akimwaga au asimwage manii, bali fidia ya ngamia itamlazimu kama atajimai, na hakuna makhitalifiano kati ya Fuqahaa kuhusu hili. Kujikabilisha kwa matamanio hakuharibu ‘amali yake ya Hajj ni sawa akimwaga au asimwage. Na haya yote kama atafanya hivyo huku anajua yuko kwenye Ihraam, lakini kama amesahau, basi hana fidia, na hakuna makhitalifiano kuhusu hili”.
Ninasema: “Dalili ya kuharamisha hilo inaingia ndani ya ujumuishi wa Kauli Yake Ta’aalaa فلا رفث kama ilivyoelezwa nyuma.
Lakini mimi sijaipata dalili yoyote kutoka kwenye Qur-aan au Sunnah inayowajibisha kuchinja mnyama kwa aliyejikabilisha kwa matamanio bila kujimai. Labda tu niichukue toka kwenye qaaidah ya Fuqahaa isemayo: “Kufanya lililoharamishwa ndani ya Ihraam kunawajibisha kafara”, lakini pamoja na hivyo, qaaidah hii haina muamana.
Maalik naye anasema kuwa ikiwa atamzongazonga mkewe, au akampiga kisi, au akamgusa na akamwaga manii, basi Hajj yake itaharibika, na atawajibika kuhiji tena mwaka ujao. Na kama atapiga busu, au akamvaa, au akajisugua sugua kwa raha bila kumwaga wala kuingiza dhakari, basi ni lazima atoe kafara. [Al-Mudawwanah (1/327)]
Ama Ibn Hazm, yeye amehalalisha yote yaliyo chini ya jimai kwa msingi kwamba الرفث maana yake ni jimai tu na si vinginevyo”.
8, 9- Kuposa na kufunga ndoa
Ni kwa Hadiyth ya ‘Uthmaan bin ‘Affaan aliyesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((لَا يَنْكِحُ اَلْمُحْرِمُ, وَلَا يُنْكِحُ, وَلَا يَخْطُبُ))
((Muhrim haoi, wala haozeshi, wala haposi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na
Muslim (1409), At-Tirmidhiy (840), Abu Daawuwd (1841) An-Nasaaiy (5/292) na Ibn Maajah (1966)]
An-Nawawiy kasema: “Agizo la Hadiyth hii linafuatwa na baadhi ya Swahaba wa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam”.
Pia ni kauli ya Maalik, Ash-Shaafi’iy, Ahmad na Is-haaq. Wanaona Muhrim hafai kufunga ndoa, na akifunga basi ndoa yake ni baatwil.
Hadiyth hii ya ‘Uthmaan imepingwa na Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) aliyesema: ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwoa Maymuwnah akiwa Muhrim)). [Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1837) na Muslim (1410)]
Abu Haniyfah na Ath-Thawriy wamesema hivi hivi, wakajuzisha Muhrim kuoa.
Lakini hili la kujuzisha Muhrim kuoa limejibiwa na Jumhuri kwa majibu kadhaa yaliyopita kwenye mkondo wa nguvu. [Angalia Al-Muhallaa (7/200), Al-Mughniy (3/158), Fat-hul Baariy (4/62), Zaadul Ma’aadiy (3/372) na Sharhul ‘Umdah cha Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah (2/194)]
Kati ya majibu hayo ni:
1- Ni kuwa kauli hii ya Ibn ‘Abbaas imeshtukiwa na kuchukuliwa kama ni mazigazi na mawazo yake tu. Sa’iyd Ibn Al-Musayyib amesema: “Ni mazigazi ya Ibn ‘Abbaas –hata kama ni khalati yake-, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakumwoa ila baada ya kufanya tahalluli”.
Ahmad kasema: “Hadiyth hii ni makosa”.
2- Ibn ‘Abbaas wakati huo alikuwa mtoto wa miaka kumi. Mtoto kama huyu anaweza asijue mambo mengi yaliyojiri katika zama zake.
3- Maymuwnah mwenyewe pamoja na Abu Raafi’i ambaye alikuwa mshenga wa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) katika ndoa hiyo, wamethibitisha kuwa Rasuli alimwoa baada ya tahalluli.
Toka kwa Yaziyd bin Al-Aswamm amesema: ((Maymuwnah bint Al-Haarith amenihadithia akisema: Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwoa akiwa ameshavua Ihraam)). Amesema: ((Alikuwa ni khalati yangu na khalati ya Ibn ‘Abbaas)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1411), Abu Daawuwd (1843), At-Tirmidhiy (845), Ibn Maajah (1963) na wengineo]
Na toka kwa Abu Raafi’u amesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwoa Maymuwnah akiwa amevua Ihraam, akamtengenezea kichumba cha kulala naye, na mimi nilikuwa mshenga kati yao)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (841) kwa Sanad Dhwa’iyf, lakini inatiwa nguvu na Hadiyth iliyoitangulia. At-Tirmidhiy ameitia ila kwa Irsaal. Na mimi sioni Irsaal kuwa ni tatizo kwa kuwa Yaziyd ameichukua moja kwa moja toka kwa Maymuwnah]
4- Ni kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwoa katika ‘Umrat Al-Qadhwaa "عمرة القضاء" na Makkah wakati huo ni eneo la vita. Rasuli akapatana nao kusimamisha vita kwa muda ili aweze kuingia na kufanya ‘Umrah kwa muda wa siku tatu tu kisha atoke. Akaja kutoka Madiynah akiwa amehirimia ‘Umrah. Na hakuna shaka kuwa alimwoa baada ya kutimiza ‘Umrah yake, kisha akarudi pamoja naye toka Makkah. Naye alikuwa anahirimia toka Dhul-Hulayfah, na hivyo hali inabainisha kuwa alimwoa akiwa Muhrim. Ama aliyehadithia kuwa alimwoa akiwa amevua Ihraam, basi atakuwa ameuona ukweli wa mambo na akauelezea.
5- Tukichukulia kwamba Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ni Swahiyh, tutaona kuwa kitendo kimepishana na kauli –katika Hadiyth ya ‘Uthmaan-, hivyo ni lazima kutanguliza kauli, kwa kuwa kitendo kinaendana na uhalali asili, nao ni kuwa ndoa ni halali katika hali zote, wakati kauli inanukuu toka kwenye asili. Hivyo basi, kwa hali hii, Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas inakuwa imenasikhiwa. Na hapa haijuzu kutanguliza kitendo kwa kuwa kutalazimu kubadili hukmu mara mbili, na hii ni kinyume na qaaidah ya ahkaam. [Al-Haafidh ameashiria katika Al-Fat-h (9/166) kuwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ni Swahiyh toka kwa Abu Hurayrah na ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa)].
Ninasema: “Bali kuna maneno kwa wote wawili. Na huenda kutokana na hilo, Ibn ‘Abdul Barri amesema katika At-Tamhiyd (3/153): Simjui Swahaba yeyote aliyesimulia toka kwake kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwoa Maymuwnah akiwa Muhrim isipokuwa Ibn ‘Abbaas”.
Ninasema: “Haya ni majibu ya nguvu kwa kuwa yanaendana na Usuwl. Yanatiliwa nguvu vile vile na kuthibiti Makhalifa Waongofu kuharamisha ndoa ya Muhrim kwa Makhalifa Waongofu. Toka kwa Ghatwafaan toka kwa baba yake: ((Kwamba ‘Umar alifarikisha baina yao, yaani mwanaume aliyeoa naye ni Muhrim)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Maalik katika Al-Muwattwaa (869), na toka kwake Al-Bayhaqiy (5/66). Angalia Al-Irwaa (1038)]
‘Aliyy amesema: ((Muhrim haoi, akioa ndoa yake hurejeshwa)). [Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy]
Kuna baadhi ya ‘Ulamaa waliolichukulia jambo hili kama linamhusu Rasuli tu na hususan suala hili la kuoa ambalo yeye ana umahususi wake pekee unaojulikana. Lakini nguvu ya majibu yaliyotangulia iko juu kwa kuwa umahususi unaodaiwa hapa umekosa dalili. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
10,11- Kufanya maasia, kuzozana na kulumbana
Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ))
((Na atakayekusudia kuhiji (akahirimia) katika miezi hiyo, basi asifanye tendo la ndoa wala ufasiki wala mabishano katika Hajj)). [Al-Baqarah (2:197)]
12- Kuwinda wanyama wa nchi kavu
Ni sawa kwa kuua, au kuchinja, au kuashiria, au kuonyesha. Ni kwa Neno Lake Ta’aalaa:
((وَحُرِّمَ عَلَيْكُمْ صَيْدُ الْبَرِّ مَا دُمْتُمْ حُرُمًا))
((Na mmeharamishiwa mawindo ya nchi kavu madamu mtakuwa katika Ihraam)). [Al-Maaidah (5:96)]
Na Neno Lake Subhaanah:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ))
((Enyi walioamini! Msiue mawindo na hali mko katika Ihraam)). [Al-Maaidah (5:95)]
Na kwa Hadiyth ya Ibn Qataadah ambayo sehemu yake inasema: ((Walipoondoka, wote walihirimia isipokuwa Abu Qataadah, yeye hakuhirimia. Na walipokuwa wanakwenda, ghafla wakaona punda milia. Abu Qataadah akawashambulia na akamuua jike kati yao. Wakashuka wakala nyama yake. Wakasema: Hivi tunakula nyama ya mnyama aliyewindwa na sisi tuko katika Ihraam? Tukabeba nyama iliyobakia ya punda jike. Walipofika kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) walisema: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika sisi tulikuwa tumehirimia, na Abu Qataadah hakuwa amehirimia. Tukaona punda milia, Abu Qataadah akawashambulia na akaua punda jike. Tukashuka tukala nyama yake. Kisha tukasema: Hivi tunakula nyama ya kiwindwa na sisi tuko kwenye Ihraam? Tukabeba nyama iliyobakia. Akasema (Rasuli): ((Je kuna yeyote kati yenu aliyemwamuru kuwashambulia au kumwashiria?)). Wakasema hapana. Akasema: ((Basi kuleni nyama yake iliyobakia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1824) na Muslim (1196).
Adhabu ya mwenye kuua mnyama
Allaah Ta’aalaa Amesema:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَقْتُلُوا الصَّيْدَ وَأَنتُمْ حُرُمٌ ۚ وَمَن قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ يَحْكُمُ بِهِ ذَوَا عَدْلٍ مِّنكُمْ هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ أَوْ كَفَّارَةٌ طَعَامُ مَسَاكِينَ أَوْ عَدْلُ ذَٰلِكَ صِيَامًا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمْرِهِ ۗ عَفَا اللَّـهُ عَمَّا سَلَفَ ۚ وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللَّـهُ مِنْهُ ۗ وَاللَّـهُ عَزِيزٌ ذُو انتِقَامٍ))
((Enyi walioamini! Msiue mawindo na hali mko katika Ihraam. Na atakayemuua (mnyama) miongoni mwenu kwa kusudi, basi malipo yake itakuwa ni kilicho sawa na alichokiua katika wanyama wa mifugo. Kama wanavyohukumu wawili wenye uadilifu miongoni mwenu. Mnyama huyo afikishwe Ka’bah, au kafara ya kulisha maskini, au badala ya hayo, kufunga swiyaam ili aonje matokeo maovu ya jambo lake. Allaah Ameshasamehe yaliyopita; na yeyote atakayerudia tena, basi Allaah Atamlipiza (kumuadhibu). Na Allaah ni Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kulipiza)). [Al-Maaidah (5:95)]
Aayah hii Tukufu inadulisha kuwa muuaji mnyama anachaguzishwa adhabu moja kati ya tatu. Ataitolea kafara yoyote aitakayo, ni sawa awe anajiweza kimali au hajiwezi. Adhabu hizo ni:
Ya kwanza: Achinje mfano wa mnyama aliyemuua kama atapata mfano wake katika wanyama wa kufugwa. Atagawa swadaqah nyama yake kwa masikini wa Al-Haram. Anaweza kumchinja wakati wowote anaotaka, na si lazima achinje siku maalum za kuchinja.
Muradi wa mfano ni yule anayefanana naye kwa sura na umbo na si kwa thamani. Atamchinja aliyefanana zaidi kwa sura na umbo na mnyama aliyemwinda. Akiwinda fisi atachinja kondoo, akiwinda paa atachinja mbuzi, na akiwinda mbuni atachinja ngamia jike na mfano wa hivi.
Toka kwa Jaabir amesema: ((Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuhusu fisi. Akasema:
((هو صيد، ويجعل فيه كبش، إذا صاده المحرم))
((Ni mnyama wa kuwindwa, na hulipiwa fidia kondoo Muhrim akimwinda)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (3801) na wengineo. Imeelezwa kuwa Swahiyh katika Al-Irwaa (1050)]
Toka kwa Jaabir: ((Kwamba ‘Umar bin Al-Khattwaab alilipa kondoo kwa fisi, na mbuzi kwa paa, na kichanga cha mbuzi kwa sungura, na mbuzi wa miezi minne kwa jerboa [mnyama kama panya])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Maalik (947), na toka kwake Ash-Shaafi’iy (987), na toka kwake Al-Bayhaqiy (2/183). Angalia Al-Irwaa (1051)].
Salaf katika Swahaba na Taabi’iyna walilipa ngamia jike kwa kuwinda mbuni. [Ibn Qudaamah amenukuu katika Al-Mughniy (5/204,404), na Sheikh wa Uislamu katika Sharhul ‘Umdah (2/283), Ijma’a ya Swahaba juu ya hilo na kwa yaliyotangulia toka kwa ‘Umar. Angalia Muswannaf wa ‘Abdul Razzaaq (8213) na Al-Muhallaa (7226)].
Na hii ni kauli ya Maalik na Ash-Shaafi’iy. Ibn Hazm amesema hakuna katika ngamia jike anayefanana na mbuni kwa upande wa urefu wa shingo, wala umbo wala sura.
Ama akiwinda punda milia, ngamia na nyati, basi atatoa ng’ombe.
‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhu) alihukumu atolewe mbuzi kwa kuwindwa njiwa. [Al-Haafidh kasema ni Hasan. Imekharijiwa na Ash-Shaafi’iy katika Al-Umm (2/214) na Al-Bayhaqiy (5/502). Ibn Hajar katika At-Talkhiysw (2/285) amesema kuwa Isnaad yake ni Hasan]
Pia, Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alihukumu hivyo hivyo. [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/205). Angalia Al-Irwaa (1056)]
Ama kiwindwa ambacho Swahaba hawakukitolea hukmu -katika vilivyotangulia na vinginevyo- katika hali hiyo, itabidi tuwalete mahakimu wawili waadilifu na wajuzi wa kutoa hukmu ya ufananisho. Na kama hawakupata mshabaha wa mnyama wa kufugwa, basi ni lazima kutoa thamani yake, na haijuzu kutoa fedha taslimu, bali thamani ya fedha hiyo itanunuliwa chakula, kisha atachaguzwa kati ya mambo mengine mawili kati ya matatu.
Ya pili: Amtie thamani mnyama mfananishwa kwa dirham. Thamani hiyo atanunulia chakula kisha atakigawa swadaqah kwa masikini, kila masikini kibaba. Haitotosheleza kutoa fedha. [Angalia Al-Majmuw’u (7/423)]
Ya tatu: Afunge badala ya kuchinja mnyama mfananishwa na kulisha kibaba kimoja kila siku kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri.
Kulisha na kufunga hufanywa sehemu yoyote aitakayo mtu, kwa kuwa Allaah Mtukufu Hakuyawekea mpaka mambo hayo mawili. [Al-Muhallaa (7/235)]
Ikiwa kundi la watu litashiriki pamoja kuua mnyama
Watu hawa hawatakuwa isipokuwa na adhabu moja tu. Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَجَزَاءٌ مِّثْلُ مَا قَتَلَ مِنَ النَّعَمِ))
((basi malipo yake itakuwa ni kilicho sawa na alichokiua katika wanyama wa mifugo)). [Al-Maaidah (5:95)]
Hakuna katika kiwindwa isipokuwa mfano wake na si mifano yake. Toka kwa ‘Imaad bin Abiy ‘Ammaar: ((Kwamba waachwa huru wa Ibn Az-Zubayr walimuua fisi wakiwa kwenye Ihraam, wakamuuliza Ibn ‘Umar (kuhusu kitendo hicho). Akasema: Chinjeni kondoo. Wakauliza: Kwa kila mmoja wetu? Akasema: Bali kondoo mmoja kwenu nyote)). [Isnaad yake ni Hasan. Imekharijiwa na Ad-Daaraqutwniy (2/250) na Ibn Hazm (7/237)]
Hakuna Swahaba yeyote aliyejulikana kwenda kinyume na Ibn ‘Umar. Haya pia ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na kundi la Salaf.
Hivyo, wauaji watashirikiana katika adhabu moja na kulisha kumoja. Lakini wakichagua kufunga, basi kila mmoja ni lazima afunge siku zote, kwa kuwa Swiyaam haishirikiwi na hilo haliwezekaniki kinyume na fedha.
Mwenye kuua mnyama kisha akaua mwingine
Ni lazima atoe fidia kwa kila mnyama. Na Kauli Yake Ta’aalaa:
وَمَنْ عَادَ فَيَنتَقِمُ اللَّـهُ مِنْهُ
si yenye kumwondoshea adhabu, kwani Allaah Hakusema kwamba hakuna malipo juu yake, bali Amewajibisha malipo kwa mwenye kumuua mnyama kwa kukusudia. Hivyo malipo ni kwa kila mwenye kuua pamoja na adhabu (ya mnyama mwingine) kwa mwenye kurudia kuua. [Al-Muhallaa (7/238) na Al-Majmuw’u (7/437)]
Mwenye kuua kwa kusahau
Jumhuri ya ‘Ulamaa; Abu Haniyfah, Maalik na Ash-Shaafi’iy wanaona kwamba mwenye kukusudia na mwenye kusahau, wote wawili ni lazima watoe malipo. Dalili zao ni:
1- Wamesema: “Allaah Amewajibisha kafara kwa mtu aliyemuua Muumini kwa makosa, hivyo tumelichukulia hilo Qiyaas kwa aliyeua mnyama kwa makosa.
2- Wamesema: “Ilivyokuwa kwamba mwenye kuharibu mali za watu kwa kukusudia au kwa makosa ni lazima azilipe, na mnyama ni Mali ya Allaah, basi ni lazima alipe kwa kuua kwa kukusudia au kwa bahati mbaya”.
3- Baadhi wengine wamesema: “Mwenye kukusudia ametajwa ili ijulikane kuwa hukmu ya mwenye kukosea pia ni hiyo hiyo”.
Lakini Ibn Hazm anasema kuwa mwenye kusahau kuwa yuko kwenye Ihraam na bila kukusudia, hana malipo na hana madhambi kutokana na Neno Lake Ta’aalaa:
((وَمَن قَتَلَهُ مِنكُم مُّتَعَمِّدًا))
((Na atakayemuua (mnyama) miongoni mwenu kwa kusudi)).
Amesema kwa kuwa Allaah kuonjesha adhabu kutokana na matokeo mabaya ya kosa hilo, na makamio makali ya kumlipizia, Waislamu wawili hawatofautiani kuwa hayo yote hayamhusu kabisa aliyekosea wala asiyekusudia maasia au kuyanuilia. Allaah Anasema:
((وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُم بِهِ وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ))
((Na wala hakuna dhambi juu yenu katika yale mliyoyakosea, lakini isipokuwa katika yale yaliyokusudiwa na nyoyo zenu)). [Al-Ahzaab (33:5)]
Madhehebu haya yamenukuliwa toka kwa ‘Umar bin Al-Khattwaab, ‘Abdur Rahmaan bin ‘Awf, Ibn ‘Abbaas, Sa’iyd bin Jubayr, Ibn Al-Musayyib, Twaawuws, Al-Qaasim bin Muhammad Saalim bin ‘Abdullaah, ‘Atwaa na Mujaahid.
Kisha Ibn Hazm amezijibu hoja za Jumhuri kwa maneno murua na mantiki ya upeo wa juu. Ukipenda waweza kuzirejea. Allaah Ndiye Mwezeshaji wa mambo yote.
Wanyama ambao si haramu kuwaua au kuwawinda kwa Muhrim
1- Wanyama ambao kiasili ni wa kufugwa
Tumetangulia kusema kuwa ni haramu kuua au kuwinda wanyama wa nchi kavu. Ama wanyama wa kufugwa kama ngamia, ng’ombe, mbuzi, kondoo na kuku, hao hawaharamishwi kama hawakugeuka na kuwa wanyama wakali. Ikiwa ngamia atamtoroka mmiliki wake Muhrim kisha akampata na akamuua kwa kumlenga (kwa mshale, risasi n.k), basi ni halali hata kama ngamia huyu akigeuka na kuwa mkali wa kudhuru, kwa kuwa asili yake ni wa kufugwa.
2- Kiwindwa cha baharini
Ni kwa Neno Lake Ta’aalaa:
((أُحِلَّ لَكُمْ صَيْدُ الْبَحْرِ وَطَعَامُهُ مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِلسَّيَّارَةِ ۖ وَحُرِّمَ عَلَيْكُمْ صَيْدُ الْبَرِّ مَا دُمْتُمْ حُرُمًا ۗ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ))
((Mmehalalishiwa mawindo ya bahari na chakula chake ni manufaa kwenu na kwa wasafiri. Na mmeharamishiwa mawindo ya nchi kavu madamu mtakuwa katika Ihraam. Na mcheni Allaah Ambaye Kwake mtakusanywa)). [Al-Maaidah (5:96)]
[Ash-Sharhul Mumti’u ‘Alaa Zaadil Mustanqa’i (7/167) kwa mabadilisho kidogo].
3- Mnyama ambaye ni haramu kuliwa
Ni kama wanyama wakali na wenye meno na kucha, kwa kuwa hawana thamani na wala si wa kuwindwa. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na kauli ya Mahanbali kinyume na Jumhuri ambao wamewajibisha fidia kwa kumuua mnyama mkali. [Al-Muhallaa (7238). Angalia Tafsiyr Ibn Kathiyr (2/98)]
4- Wanyama tulioamuriwa tuwaue na wenye madhara
Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amewataja watano ambao huuawa watu wakiwa kwenye Ihraam na wakiwa kwenye tahallul.
Toka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((خمس من الدواب كلهن فواسق، يُقتلن في الحل والحرم: الغراب، والحدأة، والعقرب، والفأرة والكلب العقور))
((Watano katika wanyama, wote ni wadhurifu, huuawa katika tahallul na katika Ihraam: Kunguru, mwewe (kite), nge, panya na mbwa anayeng’ata watu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1829) na Muslim (1198)]
Sheikh wa Uislamu amesema: “Na vyote vyenye kuwadhuru watu au kuharibu mali zao, basi inaruhusiwa kuviua, ni sawa madhara yake yawe ya uhakika kama mnyama mkali anayeweza kumshambulia Muhrim, au mnyama ambaye madhara yake hayana mwamana kama nyoka, nge, panya na mbwa anayeng’ata watu. Wanyama hawa na mfano wao, huingia kinyemela kwa watu bila kuhisiwa na madhara yao yanakuwa makubwa yasiyotabirika”. [Sharhul ‘Umdah (1/136)]
Maswahibu wetu wamesema: “Kuwaua kumesuniwa”.
Pia hapana ubaya kuua mbu, nzi, viroboto na chawa kama wanasababisha kero, na Muhrim hadaiwi chochote. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/118) na Al-Muhallaa (7/245)]
5- Kumuua mwanadamu mshambuliaji
Mtu anahitajika kujiepushia madhara yoyote yatokanayo na wanadamu wenzake au wanyama hata kama mtu atamshambulia na haikuwezekana kumwondosha isipokuwa kwa kupigana naye, basi apambane naye. Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((من قتل دون ماله فهو شهيد))
((Anayeuawa akipigania mali yake basi huyo ni shahidi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (2480) na Muslim (141)]
13- Kula kilichowindwa kwa ajili yake, au kwa ishara yake au kwa msaada wake
Ni kwa yaliyotangulia katika Hadiyth ya Abu Qataadah Rasuli aliposema:
((أمنكم أحد أمره أن يحمل عليها، أو أشار إليها؟ قالوا: لا، قال: فكلوا))
((Je kuna yeyote kati yenu aliyemwamuru kuwashambulia au kuwaonyeshea?)). Wakasema hapana. Akasema: ((Basi kuleni)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
Aliyevua Ihraam akiwinda mnyama kisha akamlisha Muhrim, basi inajuzu ale nyama lakini kama hajawindwa kwa ajili yake. Toka kwa ‘Abdur Rahmaan bin ‘Uthmaan At-Tamiymiy amesema: ((Tulitoka pamoja na Twalha bin ‘Ubaydillaah –tukiwa tumehirimia- na yeye akapewa zawadi ndege. Twalha akiwa amelala, baadhi yetu walimla, na wengine walisita kula. Twalha alipoamka, aliwaunga waliokula na kusema: Tulimla pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1197) na wengineo]
Hadiyth hii inachukulika kuwa ndege huyo hakuwa amewindwa kwa ajili yake.
Na kama amemwinda kwa ajili ya kumlisha Muhrim, basi haitojuzu kumla. Na hili linafahamika kutokana na Hadiyth ya Asw-Swa’ab bin Jath-thaamah kwamba alimpa zawadi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) punda mlia na Rasuli akamrudishia. Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipoona huzni katika uso wake alimwambia:
((إنَّا لم نرُدَّه عليك إلَّا أنَّا حُرُمٌ))
((Sisi hatukukurudishia isipokuwa sisi hakika tuko kwenye Ihraam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1825) na Muslim (1193)
Hivyo inachukulika kuwa alimwinda kwa ajili ya kumpa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akiwa Muhrim, na yeye hakukubali.
Na haya ni madhehebu ya Jumhuri ya ‘Ulamaa, na Ibn Al-Qayyim ameyatilia nguvu akisema kuwa athari zote za Swahaba kuhusiana na hili zinaonyesha ufafanuzi huu. [Angalia Zaadul Ma’aad (1/164), Tahdhiyb As-Sunan (5/215)].
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
15-Mambo Ambayo Muhrim Anaruhusiwa Kuyafanya Bila Tatizo
Alhidaaya.com [3]
Baadhi ya Mahujaji huhisi vibaya kuyafanya mambo haya, nayo hayana ubaya wowote.
1- Kuoga bila kuota, na kubadilisha nguo zake za Ihraam (izari na ridai)
Toka kwa ‘Abdullaah bin Hunayn toka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas na Al-Miswar bin Makhramah kwamba walikhitalifiana hapo Al-Abwaa. Ibn ‘Abbaas akasema: Muhrim huosha kichwa chake, na Al-Miswar akasema Muhrim haoshi kichwa chake. Ibn ‘Abbaas akanituma niende kwa Abu Ayyuwb Al-Answaariy nimuulize kuhusu hilo. Nikamkuta anaoga baina ya nguzo mbili za kisima huku akijistiri na nguo, nami nikamsalimia. Akauliza: Nani huyu? Nikasema: “Mimi ni ‘Abdullaah bin Hunayn. ‘Abdullaah bin ‘Abbaas amenituma kwako nikuulize ni vipi Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anaosha kichwa chake akiwa Muhrim? Abu Ayyuwb akaweka mkono wake juu ya nguo akaiteremsha kidogo mpaka nikakiona kichwa chake. Kisha akamwamuru mtu ammwagie maji, akamwagia juu ya kichwa chake, akakisogeza kichwa chake kwa mikono yake miwili, akaipeleka mbele na nyuma, kisha akasema: Hivi ndivyo nilivyomwona Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akifanya. [Al-Miswar akamwambia Ibn ‘Abbaas: Sitolumbana nawe milele]. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1840) na Muslim (1205) na nyongeza ni yake]
Hadiyth hii ni dalili juu ya kujuzu kuoga kwa Muhrim.
Toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Huenda ‘Umar bin Al-Khattwaab aliniambia: ((Njoo nishindane nawe kuzamia ndani ya maji tuone nani ana pumzi ndefu zaidi, na sisi tumehirimia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy]
2- Kuchana nywele
Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwamuru ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) akimwambia:”
((انقضي رأسك وامتشطي))
((Fumua nywele zako na uzichane)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (316) na Muslim (1211)
Hilo linajuzu kama kuna usalama wa kutoanguka nywele yoyote. Kama hakuna usalama, basi hilo ni mahala pa mvutano na ijtihaad. Na lenye nguvu ni kujuzu hilo, kwa kuwa hakuna dalili ya kulizuia.
3- Kukuna mwili na kichwa
Toka kwa ‘Aaishah kuwa aliulizwa kuhusu Muhrim kukuna mwili wake akasema: ((Na’am, aukune na aivute ngozi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Maalik katika Al-Muwattwa (803)]
Hili linadulishwa na Hadiyth ya Abu Ayyuwb iliyotangulia. Na kwa ajili hiyo, Sheikh wa Uislamu amesema: “Anaweza kukuna mwili wake ukimwasha, na vile vile akioga na zikaanguka baadhi ya nywele zake, hilo halitomharibia kitu”. [Al-Majmuw’at Al-Kubraa (2/368) mlango wa Hijjah ya Nabiy uk. 27]
An-Nawawiy kasema: “Ama Muhrim kukuna kichwa chake, mimi siujui mvutano wowote kuhusu uhalalisho wake…lakini wamesema kuwa ajikune kwa ulaini ili nywele zisidonoke”. [Al-Majmuw’u (7/263)]
4- Kuumika hata kwa kunyoa nywele sehemu ya kuumika
Ni kwa Hadiyth ya Ibn Buhaynah (Radhwiya Allaah ‘anhu) amesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliumikwa katikati ya kichwa chake akiwa Muhrim huko Lihaa Jamal –eneo katika barabara kuelekea Makkah-)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1836) na Muslim (1203)]
Sheikh wa Uislamu amesema: “Anaweza kujikuna mwili wake ukimwasha, na kuumikwa kichwani kwake na sehemu nyingine, na kama atahitajia kunyoa nywele za dhakari yake, basi anaweza kunyoa. Kwani imethibiti katika Swahiyh (kisha akaileta Hadiyth iliyotangulia na kusema): Na hilo haliwezekani isipokuwa pamoja na kunyoa baadhi ya nywele…”.
Jumhuri wanasema kuwa inajuzu kuumika kwa sharti nywele zisikatwe, na kama akikata, basi ni lazima fidia. Ibn Hazm amewajibu katika Al-Muhallaa (7/257) akiwaambia baada ya Hadiyth iliyotangulia: “Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakueleza kwamba kuna faini katika hilo wala fidia. Na kama ingekuwa lazima, basi asingeacha kusema. Na yeye Rasuli alikuwa ana nywele nyingi ndefu. Na bila shaka tumekatazwa kunyoa nywele katika Ihraam, na shingo ya nyuma (nape) si kichwa, wala si sehemu ya kichwa”.
Faida
Inaingia katika yaliyotangulia kun’goa gego na kutumbua jipu, hayo hayana ubaya.
5- Kunusa maua yanukiayo uzuri na mafuta marashi kwa haja na si kwa kujiburudisha
Toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: ((Muhrim anaingia msalani, anang’oa jino lake, ananusa maua mazuri, na ukucha wake ukikatika anautupa)).
Na amesema tena: ((Jiondosheeni vinavyowasumbueni, kwani Allaah ‘Azza wa Jalla Hafanyi lolote kwa vinavyowasumbueni)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/62-63)]
Kunusa manukato kuna hali tatu:
[Angalia Ash-Sharhul Mumti’u (7/158-159)]
1- Mtu kuyanusa bila kukusudia. Hili halina ubaya wowote.
2- Akusudie kuyanusa, si kwa ajili ya kupata mwonjo au kujiburudisha, bali kujua ubora wake na mfano wa hilo. Hili pia halina ubaya.
3- Akusudie kupata mwonjo na kuburudika nayo. Hili linakatazwa kwa mujibu wa kauli mbili za karibu zaidi za ‘Ulamaa. Lakini mtu anaweza kusema: Hilo halina ubaya, kwa kuwa si kuyatumia, na wala kunusa hakuna athari yoyote kwa nguo wala kwa mwili.
6- Kuitupa kucha ikikatika
Dalili ya hili ni athar ya Ibn ‘Abbaas iliyotangulia. Sa’iyd bin Al-Musayyib aliulizwa kuhusu kucha ikikatika na yeye ni Muhrim, akajibu: “Ninaikata”. [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Maalik katika Al-Muwattwa (805)]
7- Mwanaume kufunika uso
Hakuna ubaya mwanaume kufunika uso wake kwa kutumia alichojitandia au kwa kinginecho kwa ajili ya kujikinga na jua, au vumbi au mfano wa hilo akiwa Muhrim. Hili limesimuliwa toka kwa ‘Uthmaan bin ‘Affaan, Zayd bin Thaabit, Ibn Az-Zubayr, Jaabir, Ibn ‘Abbaas na Jumhuri ya Taabi’iyna. Pia ni madhehebu ya Ath-Thawriy na Ash-Shaafi’iy. [Angalia athar zilizonukuliwa toka kwao katika Al-Muhallaa (7/91), na angalia Al-Majmuw’u (7/280)]
Ni moja pia ya kauli mbili katika madhehebu ya Ahmad. [Al-Mubdi’u]
Lakini Abu Haniyfah, Maswahibu zake na Maalik, wao wanaona kwamba Muhrim hafuniki uso wake. Na hili limesimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar, na hutolea dalili kwalo kwa ziada iliyopo kwenye Hadiyth ya Muhrim ambaye ngamia wake alimvunja shingo akafa, na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akasema:
ولا تخمروا رأسه
((Na wala msifunike uso wake)). Na katika riwaya nyingine:
ولا تغطوا وجهه
((Wala msifumike uso wake))
badala ya
ولا تخمروا رأسه
Na ziada hii imekhitalifiwa kwa upande wa usahihi wake. [Hadiyth hii kama ilivyotangulia nyuma, ni Muttafaqun ‘Alayhi, na ziada iko kwa Muslim. Angalia Al-Fat-h (4/47) na Al-Irwaa (4/200)]
Waliyeiona kuwa ni Dhwa’iyf, watasema hakuna ubaya kufunika uso. Ama wanayoiona kuwa ni Swahiyh, kuna baadhi yao waliozuia mwanaume Muhrim kufunika uso wake, na kuna wengine waliohusisha marufuku kwa maiti ya Muhrim na si kwa aliye hai wakichukulia mwonekano wa tamshi. Na hili ni kwa madhehebu ya Ibn Hazm.
Na kuna wengine waliosema kuwa amekatazwa kufunika uso kwa ajili ya kukilinda kichwa chake na hakukusudiwi kufunua uso wake, kwa kuwa, ikiwa watafunika uso wake, hawatoweza kufunika kichwa. Hivyo ni lazima kufanya taawiyl, kwa kuwa Maalik na Abu Haniyfah wanasema: Hakukatazwi kufunika kichwa cha maiti na uso wake. Na Jumhuri wanasema: Inaruhusiwa kufunika uso bila kichwa. Hivyo ni lazima Hadiyth iawiliwe. Amesema katika Al-Majmuw’u (7/281).
8- Mwanamke kushusha ushungi wake usoni toka kichwani
[Majmuw’u Al-Fataawiy (26/112), Al-Muhallaa (7/91) na Al-Mughniy (3/325)]
Tumeshasema nyuma kuwa haijuzu kwa mwanamke kuvaa niqabu na kinachofanana na niqabu kama burqu na mfano wake, na kwamba inajuzu kwake kuteremsha mtandio wake toka kichwani hadi usoni wakati wanapopita wanaume ajanibu, ni sawa mtandio ukigusa uso wake au usiguse. Na hii ni kauli sahihi zaidi kati ya mbili, kwa kuwa kuteremsha hakuitwi niqabu. Toka kwa Asmaa bint Abiy Bakr amesema: ((Tulikuwa tunafunika nyuso zetu wanaume wasituone, na tulikuwa tunazichana nywele zetu kabla ya hapo katika Ihraam)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Haakim katika Al-Mustadrak (1/454)]
‘Aaishah amesema: ((Wapandaji walikuwa wakipita karibu yetu na sisi tuko pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) tukiwa tumehirimia. Wakituelekea, mmoja wetu huteremsha jilbabu yake usoni mwake toka kichwani kwake, na wanapotupita, tunazifunua)). [Hadiyth Hasan Lighayrih. Imekharijiwa na Ahmad (6/30) na Abu Daawuwd (1833) kwa Sanad Dhwa’iyf. Ina Hadiyth wenza zinazoifanya kuwa Hasan]
9- Mwanamke kuvaa nguo yoyote aipendayo ya rangi yoyote
Toka kwa Al-Qaasim bin Muhammad amesema: ((‘Aaishah alikuwa anavaa nguo ya kinjano na yeye amehirimia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Al-Haafidh katika Al Fat-h (2/405) ameinasibisha kwa Sa’iyd bin Mansuwr, na Isnaad yake amesema ni Swahiyh]
Na toka kwa Asmaa bint Abiy Bakr: ((Ni kwamba alikuwa anavaa nguo za kinjano iliyokoza na yeye amehirimia, hakuna za zafarani)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Maalik (719) na Ash-Shaafi’iy katika Al-Umm (2/126)]
Na toka kwa Yaziyd Al-Faqiyr amesema: ((Nilisafiri pamoja na Ummu Salamah –mke wa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)-, na baadhi ya nguo zake zilikuwa ni za kinjano)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abi Shaybah katika Al-Muswannaf]
Na toka kwa ‘Atwaa –kuhusiana na kisa cha ‘Aaishah kutufu pamoja na wanaume- ((Na nikamwona amejitanda abaya la rangi ya waridi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1618) na ‘Abdur Razzaaq (5/67)]
Kivazi cha mwanamke Muhrimah hakihusishwi na rangi nyeupe tu kama wanavyoamini wanawake wengi –na hususan Wamisri- bali anavaa rangi yoyote aipendayo madhali nguo imekidhi shuruti za vazi la kisharia.
10- Mwanamke kuvaa suruali na khufu mbili
Inajuzu kwa mwanamke kuvaa suruali au kingine chochote akipendacho. Hazuiwi kuvaa nguo iliyoshonwa kama anavyozuiwa mwanaume. Lakini anazuiwa kuvaa niqabu na glovu mbili kama ilivyotangulia. Pia ana haki ya kuvaa khufu mbili, na haikatwi sehemu ya juu ya vifundo viwili. [Angalia Al-Ummu (2/126), Al-Mughniy (3/328), Majmuw’u Al-Fataawaa (26/112), Fat-hul Baariy (3/406) na Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/490)]
Toka kwa Ibn ‘Umar amesema: ((Hakuna ubaya kwa Muhrimah kuvaa khufu mbili na suruali)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (4/92)]
Na toka kwa Saalim toka kwa baba yake: ((Ni kwamba alikuwa akiwafutu wanawake wanapohirimia kuwa wazikate khufu mbili mpaka Swafiyyah alipomjuvya toka kwa ‘Aaishah kuwa alikuwa akiwafutu wanawake wasikate, na yeye akaacha hilo)). [Isnaad yake Ni Swahiyh Marfuw’u. Imekharijiwa na Ash-Shaafi’iy. Imekuja Marfuw’u kwa Abu Daawuwd (1831), Al-Bayhaqiy (5/52)]
11- Mwanamke kuvaa vipambo akipenda
Toka kwa Swafiyyah bint Shaybah kwamba mwanamke mmoja alimwambia ‘Aaishah: ((Ee Mama wa Waumini! Hakika binti yangu fulani ameapa hatovaa kipambo chake katika msimu (Na katika riwaya: katika Ihraam yake). ‘Aaishah akamwambia: Mweleze kwamba Mama wa Waumini anakulalamikia vikali kama hukuvaa vipambo vyako vyote)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ash-Shaafi’iy, na kupitia kwake Al-Bayhaqiy (5/52) na Ibn Abiy Shaybah (1/4/219)]
Toka kwa Naafi’u kwamba: ((Wake wa ‘Abdallah bin ‘Umar na mabinti zake, walikuwa wakivaa vipambo vyao wakiwa wamehirimia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (1/4/320)]
Na toka kwa Maalik bin Mighwal amesema: ((Nilimuuliza Ibn Al-Aswad: Je, mwanamke aliyehirimia anavaa vipambo vyake?)). Akajibu: ((Alivyokuwa anavivaa kabla ya kuhirimia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (1/4/320)]
Imepokelewa kwa njia swahiyh kuwa ‘Atwaa alikuwa anachukia vipambo vya umashuhuri, yaani ambavyo kwavyo mwanamke anaonekana ni yeye tu baina ya wanawake wenzake. [Angalia Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/495) cha Sheikh wetu]
12- Kujipaka mwanamke hina na mfano wake akipenda
Mwanamke anaweza kujipaka hina na kinginecho kwa kuwa hakuna katazo lolote toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), kama ambavyo hina si manukato. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy na Mahanbali, isipokuwa baadhi yao wamelikirihisha hilo kwa kuwa ni katika mapambo. [Angalia Al-Majmuw’u (7/219) na Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/497)]
‘Ulamaa wa Kihanafi na Kimaalik wamesema: Haijuzu kwa aliyehirimia kujipaka sawasawa ni mwanaume au mwanamke.
Ninasema: “Linaloonekana wazi ni kuwa hakuna dalili ya kuzuia hilo si kwa mwanaume au kwa mwanamke. Na kwa maneno haya, ikiwa mwanamke atavingirisha kitambaa pamoja na hina kwenye mikono yake miwili, basi hakuna ubaya wala hatolipa fidia kwa mujibu wa kauli ya karibu zaidi ya ‘Ulamaa”.
Lakini je, hili linachafua kauli ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((وطيب النساء ما ظهر لونه وخفي ريحه))
((Manukato ya mwanamke ni yale yenye kuonekana rangi yake na yenye kufichika harufu yake?)). [Hadiyth Hasan. Itakharijiwa katika mahala pake, In Shaa Allaah]
Na je, kwa Hadiyth hii, hina inakuwa ni manukato?
Ninasema: “Linaloonekana wazi ni kuwa haiharibu kuwa hina ni katika manukato. Kwa kuwa chenye kukatazwa ni chenye harufu kama ilivyotangulia. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
13- Kujitia wanja kwa dharura
Hakuna ubaya kwa Muhrim kujitia wanja kama ana maumivu machoni. ‘Ulamaa kama alivyonukuu An-Nawawiy wamekubaliana wote kwamba Muhrim anaweza kujitia wanja usionukia kama atadharurika, na hana fidia kwa hilo. [Sharhu Muslim (3/292). Na haya ni madhehebu ya Maalik kama ilivyo katika Al-Mudawwanah (1/342) na Ash-Shaafi’ iy katika Al-Ummu (2/129)]
Toka kwa Shumaysah amesema: “Nilisumbuliwa na jicho langu nikiwa nimehirimia. Nikamuuliza Mama wa Waumini ‘Aaishah kuhusu wanja, akasema: ((Jitie wanja wa aina yoyote isipokuwa wanja manga. Wanja huu si haramu lakini ni pambo, na sisi tunaukirihisha)). Akasema: (Ukipenda, nitakutia wanja wa subiri, nikakataa)). [Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/63). Shumaysah huyu hajathibitishwa, isipokuwa ndiye mwenye kisa]
Na toka kwa Ibn ‘Umar amesema: ((Muhrim hujipaka wanja wowote autakao madhali si wa kunukia)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (1/4/424)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
16-Kuingia Makkah
Alhidaaya.com [3]
Sunnah Za Kuingia Makkah
1,2,3- Kulala Dhiy Tuwaa, kuoga kwa ajili ya kuingia hapo, na kuingia mchana
Ni kwa Hadiyth ya Naafi’u aliyesema: ((Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alikuwa anapoingia karibu na Al-Haram, huacha Talbiyah, kisha hulala Dhiy Tuwaa, halafu huswali huko Asubuhi na huoga. Na hueleza kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anafanya hivyo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1573) na Muslim (1259)]
4- Kuingia Makkah kutokea njia ya juu ya mlimani [Ath-Thaniyyat Al-‘Ulyaa]
Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anaingia kutokea Ath-Thaniyyat Al-‘Ulyaa, na hutokea Ath-Thaniyyat As-Suflaa [Sehemu ya chini ya Makkah])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1575) na Muslim (1257)]
5- Kutanguliza mguu wa kulia wakati wa kuingia Al-Masjid Al-Haraam na kuomba kwa kusema:
"يسم الله، اللهم صل على محمد وسلم، اللهم افنح لي أبواب رحمتك"
“Bismil Laah. Ee Allaah! Mpe Rahmah na Amani Muhammad. Ee Allaah! Nifungulie milango ya Rahmah Zako”.
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (713), At-Tirmidhiy (314), na An-Nasaaiy (729) bila kumswalia Nabiy. Ipo kwa Abu Daawuwd (465)]
6- Kunyanyua mikono na kuomba du’aa wakati mtu anapoiona Al-Ka’abah
Limethibiti hili toka kwa Ibn ‘Abbaas. [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (3/96). Angalia Manaasikul Hajj cha Al-Albaaniy (20)]
Kisha ataomba du’aa nyepesi. Na akisema:
"اللهم أنت السلام، ومنك السلام، فحينا ربنا بالسلام"
“Ee Allaah! Wewe ni As Salaam (Amani), na Amani inatoka Kwako, basi tuhuishe ee Mola wetu kwa Amani”.
..basi ni vyema zaidi kwa vile imethibiti toka kwa Ibn ‘Umar. [Isnaad yake ni Hasan. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/72). Angalia Manaasikul Hajj (20)]
7- Atufu Twawaaf ya Kuwasili (Twawaaful Quduwm)
Itakuja kuelezewa mbeleni.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
17-Nguzo Ya Pili Ya Hajj: Twawaaf “Kutufu” (Twawaaful Ifaadhwah)
Alhidaaya.com [3]
Twawaaf ni nini?
Kilugha, Twawaaf ni kukizunguka kitu kwa pembeni. Ama kisharia, ni kuizunguka Nyumba Tukufu [Al-Ka’abah] kwa namna itakavyoelezewa baadaye.
Aina za Twawaaf
Twawaaf za kisharia katika Hajj ni tatu:
1- Twawaaf Al-Quduwm:
Inaitwa pia Twawaaf Al-Wuruwd (ya kuja) na Twawaaf At-Tahiyyah (maamkizi), kwa kuwa imewekwa kwa mjaji asiye mkazi wa Makkah ili kuisalimia Nyumba. Imesuniwa kwa mjaji anayetoka nje ya mipaka ya Makkah kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa –kinyume na Fuqahaa wa Kimaalik ambao wamewajibisha
Twawaaf Al-Quduwm na kusema: Mwenye kuiacha ni lazima achinje kwa ajili ya kuisalimia Nyumba Kongwe.
Na asili ya hili ni kitendo chake Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Katika Hadiyth ya Jaabir: ((Mpaka tulipoifikia Nyumba pamoja naye, aliigusa nguzo kwa mkono [kama anaisalimia], akaenda kasi kidogo mara tatu (mizunguko mitatu ya kwanza) na akatembea kawaida mara nne [mizunguko minne ya mwisho])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1218)]
Na toka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa): ((Jambo la kwanza aliloanza nalo Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) wakati alipowasili Makkah ni kutawadha, kisha alitufu…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1615) na Muslim (1245)]
‘Ulamaa wa Kimaalik wametolea dalili ulazima wa hilo kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((خذوا عني مناسككم))
((Jifunzeni kutoka kwangu matendo yenu ya Hajj)). [Imekharijiwa na Muslim (1297), An-Nasaaiy (3062) na Abu Daawuwd (1970]
Jumhuri wamesema: “Kiashirio kimethibiti kuwa si waajib, kwa kuwa makusudio ni kusalimia. Ni sawa na Swalaah ya Maamkizi ya Msikiti ambayo ni Sunnah”.
Kauli hii ni imara zaidi. Allaah Ndiye Mjuzi wa yote.
Faida
Aliyekwenda moja kwa moja Minaa au ‘Arafaat akitokea Miyqaat na hakuwahi kuingia Makkah kabla ya hapo, basi si vizuri kwake –wala kwa mwenye kufanya Tamattu’u- kutufu Twawaaf Al-Quduwm baada ya kusimama ‘Arafah, kwa kuwa Twawaaf Al-Quduwm inapotea kwa kusimama ‘Arafah.
2- Twawaaf Al-Ifaadhwah (Twawaaf Ar-Ruknu)
Inaitwa pia Twawaaf ya Ziara. Nayo ni nguzo kati ya nguzo za Hajj kwa makubaliano ya Fuqahaa wote. Na Hujaji hawezi kufanya tahalluli kubwa bila ya kuifanya Twawaaf hii, na hakuna kabisa chochote cha badali yake. Qur-aan, Sunnah na Ijma’a zimethibitisha kuwa ni nguzo ya Hajj. [Al-Mughniy (3/440), Al-Badaai’u (1/128) na At-Tamhiyd (6/133- Fat-hul Maalik]
Allaah Amesema:
((ثُمَّ لْيَقْضُوا تَفَثَهُمْ وَلْيُوفُوا نُذُورَهُمْ وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ الْعَتِيقِ))
((Kisha wamalize ‘ibaadah zao; wajisafishe taka zao na watimize nadhiri zao, na watufu kwenye Nyumba ya Kale (Al-Ka’bah)). [Al-Hajj (22:29)]
‘Ulamaa wameafikiana wote kuwa Aayah hii inahusu Twawaaf Al-Ifaadhwah.
Na katika Hadiyth ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) ni kuwa Swafiyyah bint Huyayy (Radhwiya Allaah ‘anhaa) alihiji pamoja na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na akapata hedhi. Rasuli akasema: ((Je, yeye katuzuia?)). Wakasema: Yeye ameshatufu Twawaaf Al-Ifaadhwah”. Akasema: ((Basi kama hivyo, hawezi kutuzuia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1733) na Muslim (1211)]
Hivyo, haya yanadulisha kuwa Twawaaf Al-Ifaadhwah ni faradhi ya lazima. Na kama isingekuwa faradhi, basi asingelizuiliwa kusafiri ambaye hakuifanya.
Wakati wa Twawaaf Al-Ifaadhwah
(a) Wakati wake wa mwanzo:
Twawaaf hii haiswihi kabla ya wakati wake ainishwa wa kisharia. Ni wakati mpana unaoanzia tokea jua linapochomoza Siku ya Kuchinja [Yawm An-Nahr tarehe 10]. Hii ni kwa mujibu wa Maalik na Hanafiy.
Ama Ash-Shaafi’iy na Hanbal, wao wanasema wakati wake unaanzia baada ya usiku wa manane wa kuamkia Siku ya Kuchinja kwa aliyesimama ‘Arafah kabla yake.
(b) Wakati wa mwisho wake:
Mahanafi wanasema mwisho wa wakati wake ni Siku ya Mwisho ya Tashriyq. Na Fuqahaa wa Kimaalik wanasema wakati wake ni Mwezi wa Dhul Hijjah, na kama atachelewesha ukapita, basi ni lazima achinje mnyama fidia.
Ama Fuqahaa wa Kishaafiíy, Kihanbali na Maswahibu wawili wa Abu Haniyfah, wao wanasema: Asili ni kutoweka wakati maalum wa hilo, na hakuna linalowajibisha kufanyika Twawaaf hii katika Masiku ya Kuchinja, na wala mtu halazimikiwi kutoa fidia kama ataichelewesha baada ya Masiku ya Kuchinja au baada ya Mwezi wa Dhul Hijjah. Na Twawaaf hii haisameheki kwa mtu milele, na hata fidia pia haiwezi kuziba kitu, kwa kuwa ni nguzo, na mtu ataendelea kuzuiwa asijimai mpaka arudi aifanye.
Ninasema: “Kauli inayosema kuwa haijuzu kuichelewesha Twawaaf hii baada ya Mwezi wa Dhul Hijjah ni elekevu zaidi, kwa kuwa katika Mwezi huu, ndimo ‘amali za Hijjah hufanywa ingawa kiakiba zaidi ni Hujaji asiicheleweshe mpaka baada ya Masiku ya Kuchinja ili atoke ndani ya mvutano. Na kwa ajili hiyo, Sheikh wa Uislamu amesema katika Kitabu chake cha Mansak: “Ataingia Makkah na atatufu Twawaaf Al-Ifaadhwah –kama ataweza hilo Siku ya Kuchinja (tarehe 10)- na kama hakuweza, basi ataifanya baada ya hapo, lakini inatakikana iwe katika Masiku ya At-Tashriyq, kwa kuwa kuichelewesha baada ya Masiku hayo, kuna mgogoro”. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/138). Ibn Hazm (7/172) anasema akiichelewesha baada ya Mwezi wa Dhul Hijjah, basi Hajj yake inabatilika.
(c) Wakati wake bora zaidi
Imesuniwa Twawaafu hii ifanywe Siku ya Kuchinja (Siku ya ‘Iyd) kwa kuwa Rasuli alifanya siku hiyo kwa mujibu wa Hadiyth ndefu ya Jaabir na nyinginezo.
Imeshurutishwa katika Twawaaf hii mahsusi itanguliwe na Kisimamo cha ‘Arafah. Kama atatufu kabla ya Kusimama ‘Arafah, basi faradhi hiyo ya Twawaaf haimwondokei kwa mujibu wa Ijma’a ya ‘Ulamaa.
Mwanamke akipata hedhi kabla ya Twawaaf Al-Ifaadhwah
Kama ataweza –ikiwa hakuna uzito- kusubiri hadi atwaharike kisha atufu, basi itamlazimu afanye hivyo. Ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kumwambia ‘Aaishah alipopata hedhi:
((افعَلي ما يفعَلُ الحاجُّ، غير ألَّا تطوفي بالبيتِ حتى تطهُرِي))
((Fanya anayoyafanya Hujaji, ila usitufu Nyumba mpaka utwaharike)). [Hadiyth Swahiyh. Takhriyj yake imetajwa nyuma]
Sheikh wa Uislamu amesema: “Ama ambalo silijui lenye mzozo ni kuwa haifai mwanamke kutufu akiwa na hedhi kama anaweza kutufu pamoja na utwahara. Simjui mpingaji yeyote asemaye kuwa hilo ni haramu kwake na anapata madhambi kwa kulifanya. Na wao wamevutana kwa upande wa kutoshelezwa na hilo. Madhehebu ya Abu Haniyfah yanasema hilo linamtosheleza, nayo ni kauli katika madhehebu ya Ahmad..” [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/205-206)]
Lakini, ikiwa mwanamke huyo hawezi kusubiri mpaka atwaharike ili atufu kwa sababu ameshaweka tarehe ya safari ya kurudi au mfano wa hilo –na hii ndio hali halisi katika nyakati zetu za sasa- basi hatokosa moja kati ya vigawanyo vinane:
[Muhtasari wa utafiti murua wa Al-‘Allaamah Ibn Al-Qayyim katika I-‘ilaam Al-Muwaqqi’iyna (3/19) na zinazofuatia].
1- Aambiwe: Bakia Makkah mpaka utwaharike na utufu hata kama wanaume watasafiri na kuondoka.
Katika hili kuna ufisadi kwa kumwacha abaki peke yake ugenini ambapo anaweza kupata madhara mengi.
2- Aambiwe: Twawaaf Al-Ifaadhwah inapomoka kwa kushindikana sharti yake.
Hili hakuna wa kulisema, kwa kuwa Twawaaf hii ni nguzo kuu ya Hajj, nayo ndio makusudio yake hasa. Kusimama ‘Arafah na yanayofuatia ni utangulizi wa nguzo hii.
3- Aambiwe: Ukihofia hedhi kukujia wakati wa kutufu, basi inajuzu kuifanya kabla ya wakati wake. Na hili hakuna aliyelisema. Ni kama kutanguliza kusimama ‘Arafah kabla ya Siku yake.
4- Isemwe: Ikiwa anajua kwa mazoea kuwa siku zake zinamjia katika masiku ya Hajj, basi atasameheka na faradhi ya Hajj mpaka afikie umri wa kutotokwa na damu ya hedhi na ikatike kabisa.
Hili litalazimisha kuondosha ufaradhi wa Hajj kwa wanawake wengi, nalo ni batili.
5- Isemwe: Arudi kwenye Ihraam yake kwa kujizuia jimai na nikaah mpaka arudi kwenye Al-Ka’abah, atufu akiwa twahara hata baada ya miaka. Na hili ndilo ambalo linarejeshwa na Usuwl ya sharia na yaliyomo ndani yake kati ya rahmah, hikmah na maslaha. Na bila shaka uzito ulioko ndani ya hili haufichiki.
6- Isemwe: Atavua Ihraam mpaka atwaharike kama anavyovua Ihraam aliyezuilika asiweze kufanya Hajj pamoja na kusalia Hajj katika dhima yake. Na wakati wowote atakapokuwa na uwezo, basi itamlazimu, na atatufu akiwa twahara. Na hili ni dhaifu kwa kuwa kuzuilika mtu asiweze kufanya Hajj ni jambo linalotokea bila kutarajiwa ambalo linamzuilia Hujaji kufika Makkah katika wakati wa Hajj. Lakini mwanamke huyu ashafika kwenye Al-Ka’abah, kisha udhuru wake haupomoshi faradhi yake ya Hajj. Hivyo kutokewa ghafla na hali hiyo hakumuwajibishii kuvua Ihraam kama inavyofanyika kwa jambo lenye kumzuia asiweze kufika Makkah.
7- Isemwe: Ni lazima amtafute mtu wa kumhijia mfano wa mwenye kuugua maradhi sugu yasiyopona na asiyeweza kuhiji. Hili hakuna mwenye kulisema. Halafu, mwenye maradhi sugu, hana tena matumaini ya udhuru wake huo kuondoka, lakini mwanamke huyo hakati tamaa ya kuondoka udhuru wake kwa kuwezekana kukatika kabisa damu yake katika umri wa kufunga damu ya hedhi au kabla yake. Yeye si kama mgonjwa wa maradhi sugu.
Makadirio haya yote saba hayafai, ni batili. Hivyo imebidi lipatikane la nane ambalo ni:
8- Isemwe: Atatufu Al-Ka’abah –akiwa na hedhi- kwa dharura. Na hili linaendana na roho samehevu ya sharia, na kwa ajili ya kuondosha uzito kwa umma.
Ama yaliyosemwa na ‘Ulamaa na Fatwa walizotoa kuhusu kushurutisha mwanamke awe twahara kutokana na hadathi kubwa wakati wa kutufu, haya bila shaka ni katika hali ya kuwa na uwezo na wasaa na si katika hali ya dharura na kushindwa. Kufutu hivi hakupingani na sharia wala kauli za ‘Ulamaa.
Na hili ni chaguo la Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah –Allaah Amrehemu- ambaye amesema katika kaditama ya utafiti wake: “Hili ndilo lenye mwelekeo zaidi kwa upande wangu katika suala hili, na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa toka kwa Allaah Al-‘Aliyyu Al-‘Adhiwym. Na lau si kudharurika watu na kulihitajia hilo kivitendo na kielimu, basi nisingejitaabisha kuzungumzia hili pale ambapo sikukuta ndani yake maneno ya mtu mwingine zaidi yangu, kwa kuwa ijtihaad wakati wa dharura ni jambo ambalo Allaah Ametuamuru”. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/176-241). Sheikh wetu ameitilia nguvu katika Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/572) na zinazofuatia]
Ninasema: “Mwanamke akiweza kutumia dawa ya kuzuia hedhi wakati wa Hajj, basi anaweza kutumia –kama haitomfanyia matatizo- ili kuondokana na mvutano. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
3- Twawaaful Widaa (Ya Kuaga)
Inajulikana pia kama Twawaaf As-Swadr na Twawaaf Aakhir Al-‘Ahd. Twawaaf hii ni wajibu kati ya nyujubu za Hajj kwa mujibu wa Jumhuri ya ‘Ulamaa –kinyume na Fuqahaa wa Kimaalik ambao wanasema ni Sunnah-. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) aliyesema: ((Watu wameamuriwa iwe ahadi yao ya mwisho na Nyumba, isipokuwa imesamehewa kwa mwanamke mwenye hedhi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1755) na Muslim (1327)]
Na katika tamko: ((Watu walikuwa [baada ya kumaliza Hajj yao] wakitawanyika huku na kule, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akasema:
((لا بنفرن أحد حتى يكون آخر عهده بالبيت))
((Asiondoke mtu [Makkah] mpaka ahadi yake ya mwisho iwe [Kutufu] Nyumba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1327)]
Hadiyth hii ni dalili juu ya wajibu wa Twawaafu ya Kuaga, na kwamba mwanamke kama atapata hedhi baada ya Twawaaful Ifaadhwah, itamlazimu abakie mpaka atwaharike, na kisha atufu Twawaafu ya Kuaga. Lakini anaruhusiwa kuacha Twawaafu ya Kuaga na kusafiri kurudi kwao na si wajibu kwake kuchinja. Dalili ya hili ni yaliyotangulia nyuma kidogo kuwa Swafiyyah alipopata hedhi, Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa sallam) alisema:
((أحابستنا هي؟))
((Je, yeye katuzuia?)).
Wakasema: Yeye ameshatufu Twawaaf Al-Ifaadhwah”. Akasema:
((فلتنفر إذن))
((Basi kama hivyo, aondoke)). [Al-Ummu cha Ash-Shaafi’iy (2/154)]
Angalizo
Ikiwa mwanamke atatwaharika kabla hajasafiri, basi ni lazima atufu Twawaaf ya Kuaga kama bado hajatoka nje ya majumba ya Makkah. Kama atatwaharika naye bado yuko ndani ya Makkah, basi ni lazima atufu Twawaaf hii. [Al-Ummu cha Ash-Shaafi’iy (2/154)]
Mkazi wa Makkah hana Twawaaf ya Kuaga
Twawaaf ya Kuaga si wajibu isipokuwa kwa Hujaji toka nje ya Makkah. Ama mkazi wa Makkah, huyo hana Twawaaf kwa mujibu wa Fuqahaa wa Kihanafiy na Kihanbali, na Mahanafiy wanamuhesabu kuwa mkazi wa Makkah mtu ambaye nyumba yake iko ndani ya mipaka ya Miyqaat, kwa kuwa Twawaaf ni wajibu kwa ajili ya kuaga Nyumba, na wakazi wa Makkah hawana hali hii, kwa kuwa wako mjini kwao.
Ama kwa upande wa Maalik na Ash-Shaafiíy, Twawaaf ya Kuaga inatakiwa ifanywe na kila aliyekusudia kusafiri toka Makkah hata kama ni mkazi wa Makkah ikiwa atakusudia safari ya umbali wa kumruhusu kupunguza Swalaah kutokana na ujumuishi wa amri ya kuwa agano la mwisho liwe kwa Nyumba (Al-Ka’abah). [Al-Mawsuw’at Al-Fiqhiyyah (17/58)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
18-Hukmu Kiujumla Kuhusu Twawaaf
Alhidaaya.com [3]
Shuruti Za Kutufu
1- Je, mwenye kutufu ni lazima awe twahara?
Jumhuri ya ‘Ulamaa –kinyume na Mahanafiy, riwaya toka kwa Ahmad na Ibn Hazm- wanasema kutwaharika na hadathi na najisi ni sharti ya kuswihi Twawaaf. Ikiwa atatufu bila twahara na vitu hivyo, basi Twawaaf yake ni batili, haihesabiwi.
Hoja yao ni Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas toka kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliyesema:
((الطواف بالبيت صلاة إلا أن الله أباح فيه الكلام))
((Kutufu Nyumba ni Swalaah isipokuwa Allaah Ameruhusu ndani yake maneno)). [Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (960), An-Nasaaiy (2922), Al-Haakim (1/630) na wengineo. Haifai kuwa Marfuw’u, na sawa ni kuifanya Mawquwf kama alivyoielezea Sheikh wetu katika Kitabu cha Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/515-521), kinyume na Al-‘Allaamah Al-Albaaniy ambaye amesema ni sahihi kuwa Marfuw’u katika Al-Irwaa (1/156)]
Hoja hii inapingwa kwa hoja kadhaa:
(a) Hadiyth hii haifai kuwa Marfuw’u, na la sawa ni Hadiyth Mawquwf kutokana na maneno ya Ibn ‘Abbaas. Haya yametiliwa nguvu na At-Tirmidhiy, Al-Bayhaqiy, Ibn Taymiyah, Ibn Hajar na Sheikh wetu Mustwafaa Al-‘Adawiy.
(b) Hata tukisema ni Swahiyh, lakini hata hivyo, hailazimu kutokana nayo kuwa Twawaaf ifanane na Swalaah katika kila kitu mpaka ishurutishiwe yanayoshurutishwa kwa Swalaah. [Angalia njia za kupambanua kati ya Swalaah na Twawaaf katika Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/522)]
(c) Idadi kubwa ya Waislamu ambao idadi yao hakuna aijuaye isipokuwa Allaah ‘Azza wa Jalla, walikuwa wanatufu enzi ya Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na halikunukuliwa lolote kuwa aliwahi kumwamuru yeyote kati yao atawadhe kwa ajili ya Twawaaf yake, pamoja na kuwepo uwezekano wa wengi wao kuwa walitengukwa na wudhuu, na wengi wao pia kuingia kwenye Twawaaf bila ya wudhuu, na hususan sambamba na msongamano mkubwa katika Twawaaf ya Quduwm na Ifaadhwah. [Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/515) kwa mabadilisho madogo. Angalia Majmuw’u Al-Fataawaa (21/273)]
Na kwa ajili hiyo, Sheikh wa Uislamu amesema katika Al-Fataawaa (6/198): “Imebainika kuwa twahara ya hadathi haishurutishwi katika Twawaaf na si wajibu kwayo bila shaka, lakini imesuniwa kuwa na twahara ndogo (wudhuu), kwa kuwa dalili za kisharia zinadulisha kuwa si wajibu kwa Twawaaf, na hakuna katika sharia linalodulisha ulazima wa kuwa na wudhuu”.
Na Ibn Hazm (7/179) amesema: “Kutufu Nyumba bila ya twahara kunajuzu”.
Ni chaguo pia la Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn –Allaah Amrehemu- katika Al-Mumti’u (7/300).
Ninasema: “Pamoja na kutilia nguvu kujuzu kutufu bila wudhuu, lakini hakuna shaka kuwa ni vizuri kuwa nao kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Jambo la kwanza aliloanza nalo Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) wakati alipokuja ni kuwa alitawadha, kisha akatufu kisha…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5/16) na Muslim (1235)]
Na pia kwa ujumuishi wa dalili zenye kustahabisha kufanya dhikr mtu akiwa na twahara. Lakini pamoja na hivyo, sisi hatuwezi kumlazimisha aliyetengukwa na wudhuu wakati anatufu, aende kutawadha katikati ya msongamano mkubwa bila kuwepo dalili bayana. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Haya yote ni kuhusu kutwaharika na hadathi ndogo. Ama hadathi kubwa kama hedhi, nifasi na janaba, inavyoonekana ni kuwa ni lazima kujitwaharisha nazo kwa mwenye kutufu kutokana na neno lake Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa ‘Aaishah:
((افعلي ما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت))
((Fanya (yote) ayafanyayo mwenye kuhiji isipokuwa tu usitufu Nyumba)). [Hadiyth Swahiyh. Takhriyj yake imetajwa nyuma]
Hivyo basi, mwenye kutufu naye ana hadathi kubwa –bila ya udhuru- kisha akarejea kwao, basi hukmu yake ni hukmu ya ambaye hakutufu asilani kwa mujibu wa kauli ya Maalik na Ash-Shaafi’iy. Abu Haniyfah amesema: “Atapeleka mnyama [Makkah], na itamtosheleza”. [At-Tamhiyd cha Ibn ‘Abdul Barr (19/262)]
2- Kusitiri uchi:
Haijuzu kwa yeyote kutufu Nyumba akiwa uchi. Akitufu uchi, haitomtosheleza kwa kauli ya Jumhuri. Ni kwa Neno Lake Ta’aalaa:
((يَا بَنِي آدَمَ خُذُوا زِينَتَكُمْ عِندَ كُلِّ مَسْجِدٍ))
((
Enyi wana wa Aadam! Chukueni mapambo yenu (ya mavazi ya sitara na twahara) katika kila mahala pa ‘Ibaadah)). [Al-A’araaf (7:31)]
Na kwa Hadiyth ya Abu Hurayrah: ((Kwamba Abu Bakr As-Swiddiyq (Radhwiya Allaah ‘anhu) alimtuma katika Hajj ambayo Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimpa uongozi kwa kundi la watu kabla ya Hajj ya Kuaga Siku ya Kuchinja awatangazie watu:
((ألا لا يحج بعد العام مشرك، ولا يطوف بالبيت عريان))
((Jueni na tambueni! Asihiji mpagani baada ya mwaka (huu), na asitufu mtu Nyumba akiwa uchi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (369) na Muslim (1347)]
‘Ulamaa wa Kihanafiy wamesema: Kusitiri uchi ni lazima katika Twawaaf na si sharti ya kuswihi. Atakayetufu uchi, basi Twawaaf yake itabatwilika kwa maneno ya Jumhuri.
Ama kwa Mahanafiy, Twawaaf itaswihi lakini ni lazima achinje.
3- Twawaaf iwe nje ya Nyumba (Al-Ka’abah)
Allaah Ta’aalaa Amesema:
((وَلْيَطَّوَّفُوا بِالْبَيْتِ الْعَتِيقِ))
((na watufu kwenye Nyumba ya Kale [Al-Ka’bah])). [Al-Hajj (22:29)]
Na lau atatufu katika “Al-Hijr”, basi Twawaaf yake haiswihi. Na “Al-Hijri” ni sehemu iliyozungushwa nusu duara ukuta pembeni kidogo mwa Al-Ka’abah kwa upande wake wa mashariki. Inaitwa pia “Al-Hatwiym” na “Al-Jadr”. Kutoswihi huku ni kwa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam:
((الحجر من البيت))
((Al-Hijr ni sehemu ya Al-Ka’abah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (876), Abu Daawuwd (2028) na Ibn Maajah (2955). Asili yake ni kutoka Swahiyh Mbili toka kwa ‘Aaishah]
“Al-Hijr” ilikuwa ni sehemu ya Al-Ka’abah na Maqurayshi waliiacha kutokana na ufinyu wa fedha za kukamilishia, hivyo wakatosheka kuzungushia sehemu hiyo ya ukuta. Hivyo basi, ili Twawaaf iswihi, ni lazima iwe nje ya kijikuta hicho, na kama si hivyo, itabatilika kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri.
Ama Mahanafiy, wao wanasema ni lazima atufu upya madhali bado yuko Makkah, na kama amesharejea kwao, basi ni lazima atoe mnyama amtume Makkah.
4,5- Aanze Twawaaf yake tokea kwenye Jiwe Jeusi (Al-Hajar Al-As-wad) na amalizie na kuanzia mizunguko hapo hapo, na Al-Ka’abah iwe kushotoni mwake
Ni kwa Hadiyth ya Jaabir: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipoingia Makkah, aliliendea Jiwe Jeusi akaligusa kwa mkono, kisha akaenda kwa kuliani mwake, akatembea mwendo kasi kidogo mara tatu [mizunguko mitatu ya mwanzo], na mwendo kawaida mara nne [mizunguko minne ya mwisho])). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa kamili nyuma pamoja na takhriyj yake]
Na hili ni sharti la kutufu kwa Jumhuri kutokana na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuendelea kufanya hivyo, na kwa kuwa pia ni ubainisho wa ujumla wa agizo la Qur-aan la kutufu, na likawa katika uhakika wake. Na kwa neno lake Nabiy:
((من عمل عملا ليس عليه أمرنا فهو رد))
((Mwenye kufanya ‘amali yoyote isiyo juu ya amri yetu, basi anarejeshewa mwenyewe)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy katika mlango wa biashara, na Muslim (1718)]
6- Iwe mizunguko saba kamili
Kwa kuwa ndivyo alivyofanya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akibainisha kipimo kinachotakikana cha Twawaaf kwa mujibu wa Agizo Lake (تعالى)
((وَلْيَطَّوَّفُوا))
”Na watufu”,
Hivyo inakuwa ni lazima. Na haya ni madhehebu ya Jumhuri. Na kama ataacha hatua moja [ya kumalizia au akaruka ya kuanzia] katika mzunguko wowote, basi mzunguko huo hauhesabiwi.
Ama Mahanafiy, wao wamekufanya kuzunguka zaidi ya mara saba kuwa ni nguzo, na chini iliyobaki kuwa ni wajibu, na si nguzo. Na hili linakataliwa kwa kuwa vipimo vya matendo ya’ibaadah havijulikani kwa rai za watu wala ijtihaad, bali ni kwa “Tawqiyf”(Uainisho toka kwenye Qur-aan na Sunnah) na vyanzo vya kisharia. Ni kama mtu aliyepunguza rakaa moja katika Swalaah yake, Swalaah hii haijuzu. Na kwa ajili hiyo, Al-Kamaal bin Al-Hammaam –ambaye ni katika Fuqahaa wa Kihanafiy- amelikataa hili akisema: “Tunalolifuata ni kuwa haijuzu chini ya saba, wala baadhi yake haziungwi kwa chochote”. [Nihaayatul Muhtaaj (2/409), Badaai’u As-Swanaai’i (2/132) na Fat-hul Qadiyr (2/247)]
Akifanyia shaka idadi ya mizunguko
Akifanyia shaka ni mizunguko mingapi amezunguka naye bado anatufu, basi atalichukulia la uhakika, nalo ni idadi ndogo [yaani akifanyia shaka kati ya minne au mitano, basi atachukulia ni minne]. Hii ni kauli ya Jamhuiri ya Fuqahaa, na imenukuliwa toka kwa Ibn Al-Mundhir Ijma’a juu ya hilo. [Al-Mughniy (3/378) na Al-Majmuw’u (8/25)]
Ninasema: “Lakini kama uhakika wa idadi kubwa utakuwa na nguvu zaidi kwake, basi ataichukulia hiyo hiyo. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
7- Kuandamisha kati ya mizunguko
Kwa maana ya kutoachanisha mzunguko na mzunguko kwa muda mrefu. Na hili ni sharti la Kutufu kwa ‘Ulamaa wa Kimaalik na Kihanbali. Kuna kauli kwa ‘Ulamaa wa Kishaafi’iy inayosema kuandamisha ni wajibu. Ama kwa ‘Ulamaa wa Kihanafiy na Kishaafi’iy ni Sunnah.
Na mwenye kukata Twawaaf yake kwa udhuru kama kwenda haja au kutawadha –kwa mwenye kuliona hilo ni sharti- au kuswali Swalaah ya Faradhi, au kupumzika kutokana na mchoko, basi atakuja kukamilishia idadi aliyofikia. Lakini kama ataikata Twawaaf kipuuzi bila udhuru, basi itabatwilika. [Angalia Al-Muhallaa cha Ibn Hazm (7/180)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
19-Sunan Za Twawaaf
Alhidaaya.com [3]
1- Kutawadha kabla ya Kutufu
Ni kwa Hadiyth ya Mama ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa): ((Jambo la kwanza aliloanza nalo Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) wakati alipokuja ni kuwa alitawadha, kisha akatufu Nyumba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1615) na Muslim (1235)]
Na hiki ni kitendo tu kinachodulisha kuwa kufanya hivyo ni jambo mustahabu na halifikii kiwango cha uwajibu. Na wudhuu hauingii ndani ya wigo wa ujumuishi wa ‘amali za Hajj mpaka usemwe kuwa ni bainisho la kauli yake Rasuli:
((خذوا عني مناسككم))
((Jifunzeni kutoka kwangu matendo yenu ya Hajj)).
Kisha, inayumkinika alitawadha kwa ajili ya Swalaah baada ya kumaliza Twawaaf.
Kiujumla, Twawaaf ni dhikri, hivyo ni vizuri mtu kuwa twahara wakati anapoifanya kutokana na Hadiyth ya mtu ambaye alimsalimia Nabiy: ((Naye hakumjibu mpaka akaelekea [ukuta, akatayammamu], akapukusa uso wake na mikono yake miwili, halafu akamjibu salaam)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1875) na wengineo]
2- Kupitisha chini ya kikwapa kipande cha juu cha nguo ya Ihraam
Hii ni kwa wanaume tu. Atapitisha sehemu ya kati ya izari yake chini ya kwapa lake la kulia na atazitupia ncha zake mbili juu ya bega lake la kushoto, na bega lake la kulia litabaki wazi. Ni kwa Hadiyth ya Ya-‘alaa bin Umayyah: ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu bega lake la kulia likiwa wazi)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1883), At-Tirmidhiy (859) na Ibn Maajah (2954). Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh]
Kuacha bega la kulia wazi ni Sunnah kwa mujibu wa Jumhuri ya ‘Ulamaa kwa wanaume tu pasina wanawake katika mizunguko yote. Limesuniwa hili kwa kila Twawaaf inayofuatiliwa na Kusai kama Twawaaf Al-Quduwm kwa anayetaka Kusai baada yake, Twawaaf ya ‘Umrah na Twawaaf ya Ziara kwa aliyechelewesha Kusai. Ama Fuqahaa wa Kihanafiy, Kishaafi’iy na Kihanbali, wao wanasema haachi bega wazi isipokuwa katika Twawaaf Al-Quduwm tu. [Al-Mawsuw’at Al-Fiqhiyyah (29/134)]
Angalizo
Kuacha bega wazi kunafanyika wakati wa Twawaaf tu na si kwa ‘amali nyingine za Hajj kama wanavyofanya watu wengi tokea anapohirimia na kuendelea na hali hiyo mpaka anapotahalluli. Huku ni kujingikiwa na Sunnah, na hata utamwona anaswali bega likiwa wazi. Jambo hili limekatazwa kama tulivyoeleza katika mambo yaliyo makruhu katika Swalaah.
Hivyo basi, baada ya kumaliza Twawaaf yake, anatakikana aiweke sawa nguo yake ya juu na alifunike bega lake la kulia, kwa kuwa mahala pa kufunuliwa bega ni wakati wa Kutufu tu.
3- Kwenda mwendo kasi kidogo katika mizunguko mitatu ya kwanza (kwa wanaume tu)
Nako ni kuharakisha mwendo kwa hatua za mkaribiano na kuyatingisha mabega mawili bila kuruka, na hili linafanyika katika mizunguko mitatu tu ya kwanza, minne iliyobakia atatembea mwendo wa kawaida.
Mwendo kasi ni Sunnah katika kila Twawaaf baada ya Kusai. Toka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) amesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuja na Swahaba Zake Makkah huku homa ya Yathrib ikiwa imewadhoofisha. Washirikina wakasema: Kesho watakujieni watu ambao homa imewakondesha, na imewapiga vibaya. Wakakaa karibu na nusu mduara ya ukuta wa Al-Ka’abah [ili kuwaangalia na kuwacheza shere]. Na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akawaamuru [Swahaba] waende mwendo kasi katika mizunguko mitatu ya kwanza, na watembee mwendo wa kawaida kati ya Nguzo Mbili ili washirikina wauone uimara na ukakamavu wao. Washirikina wakasema: Hivi ni hawa mliodai kuwa homa imedhoofisha? Hawa ni wakakamavu kuliko kadha na kadha)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1602) na Muslim (1266)]
Nguzo Mbili zilizokusudiwa katika Hadiyth hii ni Jiwe Jeusi na Nguzo ya Yamaaniy. Walipokuwa kati ya sehemu hizi mbili, washirikina walikuwa hawawezi kuwaona, hivyo walipata nafasi ya kupumzika ili wabakie na nguvu zao.
Hii ilikuwa katika ‘Umrat Al-Qadhwaa mwaka wa saba. Lakini mwendo kasi umebakia ni Sunnah katika mizunguko mitatu kamili ya kwanza. Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliifanya katika Hajj yake –na ilikuwa baada ya kuikomboa Makkah na watu kuingia katika Dini ya Allaah makundi kwa makundi- kama ilivyokuja katika Hadiyth ya Jaabir: ((…akaenda kasi mara tatu, na akatembea kawaida mara nne)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma mara nyingi]
Na katika Hadiyth ya Ibn ‘Umar: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikwenda haraka mizunguko mitatu, na akatembea kawaida minne katika Hajj na ‘Umrah [toka nusu duara ukuta hadi Jiwe Jeusi])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1604), Muslim (1261) na wengineo bila nyongeza, na ziada iko kwa Ibn Maajah (2950)]
Kwenda mwendo kasi katika mizunguko mitatu ya awali ni Sunnah iliyobakia ingawa sababu yake haipo tena ya kuwatia hasira washirikina. Linalotilia nguvu kubakia kwake ni kuwa ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaah ‘anhu) alikuwa amekusudia kuiacha akisema: ((Unatuhusu nini tena mwendo kasi? Hakika tulikuwa tumewaonyesha kwao washirikina, na Allaah Ashawaangamiza”. Kisha akasema: “Jambo ambalo Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amelifanya, basi sisi hatupendi kuliacha)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1605) na Muslim (1270)]
Haifai kisharia kulipia mwendo kasi
Kama hakuweza kwenda mwendo kasi katika mizunguko mitatu ya kwanza kutokana na msongamano na mfano wake, basi hatoilipia kwa minne iliyosalia, kwa kuwa umbile la mizunguko hii minne ni utulivu (kwenda taratibu), hivyo haibadilishwi. [Fat-hul Baariy (3/551)]
Wanawake hawaruhusiwi mwendo kasi
[Al-Ummu (2/150), Al-Mughniy (3/394), Fat-hul Baariy (3/551) na Sharhu Muslim (3/397)]
Wengi katika ‘UIamaa wamelisema hili hata baadhi yao wamenukuu Ijma’a.
‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) amesema: ((Enyi kundi la akina mama! Hampaswi mwendo kasi katika Nyumba. Nyinyi kwetu ni kiigizo)). [Hasan Lighayrih. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/84) na Ibn Abiy Shaybah (1/4/121)]
Mfano wa maneno haya yamenukuliwa toka kwa Ibn ‘Umar kwa njia sahihi. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bayhaqiy (5/84) na Ibn Abiy Shaybah (1/4/121)]
Na pia imesimuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas na Masalaf wengine. [Isnaad yake ni Layyin. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (1/4/122). Katika Sanad yake yuko Muhammad bin ‘Abdur Rahmaan bin Abiy Laylaa]
4,5- Kuligusa Jiwe Jeusi kwa mkono na kulibusu katika kila mzunguko ikiwezekana
Ni Sunnah kutokana na Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipowasili Makkah akiligusa Jiwe Jeusi anapoanza Kutufu, anakwenda kasi mizunguko mitatu kati ya saba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1603) na Musim (1261)]
Toka kwa Naafi’u amesema: ((Nilimwona Ibn ‘Umar akiligusa Jiwe kwa mkono wake, kisha akabusu mkono wake, na akasema: Sikuliacha hili toka nilipomwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalhii wa sallam) akilifanya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1267)]
‘Umar bin Al-Khattwwaab alilibusu Jiwe na kusema: ((Lau si mimi kumwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akikubusu, basi nisingelikubusu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1605) na Muslim (1270)]
Kama hakuweza kulibusu au kuligusa
Imestahabiwa aliguse Jiwe kwa mkono wake na alibusu kama ataweza. Kama ataligusa na ikawa uzito kulibusu, basi ataubusu mkono wake. Ikishindikana kuligusa kwa mkono, anaweza kuligusa kwa fimbo na mfano wake kisha ataibusu. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas aliyesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu katika Hajj ya Kuaga akiwa juu ya ngamia akaligusa Jiwe kwa bakora yake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1607)]
Kama hakuweza kabisa kuligusa, basi ataliashiria kwa mkono wake na atapiga Takbiyr. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas aliyesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu Nyumba juu ya ngamia. Kila alipoijia Nguzo [Jiwe], aliiashiria kwa kitu alichokuwa nacho na akapiga Takbiyr)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1613)]
Na imepokewa kiusahihi toka kwa Ibn ‘Umar: ((Kwamba alikuwa anapoigusa Nguzo husema Bismil Laah Allaahu Akbar)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na ‘Abdur Razzaaq (8894) na Al-Bayhaqiy (5/79). Al-Haafidh kasema ni Swahiyh katika At-Talkhiysw (2/247)]
6- Kusujudu juu ya Jiwe Jeusi
Toka kwa Ibn ‘Umar amesema: ((Nilimwona ‘Umar bin Al-Khattwwaab akilibusu Jiwe na akisujudu juu yake, kisha akarudi akalibusu na akasujudu juu yake, halafu akasema: Hivi ndivyo nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh kama ilivyo katika Al-Irwaa (4/312)]
Na hili limethibiti vile vile toka kwa Ibn ‘Abbaas kutokana na kitendo chake.
Al-Albaaniy (Rahimahul Laah) kasema katika Al-Irwaa (4/312): “Inaonekana kutokana na ujumla wa yaliyotangulia kuwa kusujudu juu ya Jiwe Jeusi kumethibiti kukiwa Marfuw’u na Mawquwf. Na Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
7- Kuigusa kwa mkono Nguzo ya Al-Yamaaniy
Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar aliyesema: ((Sikumwona Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akigusa [kingine chochote] katika Nyumba isipokuwa Nguzo Mbili za Al-Yamaaniy)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1609) na Muslim (1267)]
Mwanamke asisongane na wanaume
Haitakikani mwanamke apigane vikumbo na wanaume kwa ajili ya kuzigusa Nguzo Mbili au kulibusu Jiwe Jeusi wakati wa Twawaaf. Toka kwa ‘Atwaa amesema: ((‘Aaishah alikuwa anatufu sehemu kando na wanaume, hachanganyikani nao. Mwanamke mmoja akamwambia: Kazana tuguse ee Mama wa Waumini! Akasema: Kazana wewe, mimi niache. Akakataa. [‘Atwaa amesema] Wanatoka usiku wakiwa wamejibadilisha na kutufu pamoja na wanaume, lakini wao walikuwa wanapoingia Al-Ka’abah husimama mpaka wanaume watolewe)).
Ummu Salamah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) alipolalamika, Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia:
((طوفي من وراء الناس وأنت راكبة))
((Tufu nyuma ya wanaume ukiwa umepanda [mnyama])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1618) na Abdur Razzaaq (5/67)]
Nguzo Mbili za Kishaam haziguswi
Ni kwa Hadiyth iliyotangulia nyuma kidogo ya Ibn ‘Umar. Kwa kuwa Nguzo ya Kaskazini na Magharibi (mwelekeo wa nusu duara ukuta) haziko ndani ya misingi iliyojengwa na Ibraahiym ‘Alayhis Salaam kama ilivyotangulia.
8- Kuomba du’aa baina ya Nguzo Mbili za Yamaaniy
Toka kwa ‘Abdullaah bin As-Saaib amesema: ((Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema baina ya Nguzo na Jiwe:
رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّار
[Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1892), An-Nasaaiy katika Al-Kubraa (3934), Ahmad (3/411) na wengineo. Hilo limethibiti vile vile kwa kufanywa na ‘Umar na mwanawe kwa yaliyoelezewa na ‘Abdur Razzaaq (8966-8964)]
Sheikh wa Uislamu amesema katika Al-Fataawaa (26/122): “Imestahabiwa kwake wakati wa Kutufu amdhukuru Allaah Ta’aalaa na amwombe kwa du’aa za kisharia. Kama atasoma Qur-aan kwa sauti ya chini, basi si vibaya. Na hakuna adhkaar maalum toka kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), si kwa amri yake, wala kauli yake, wala maelekezo yake, bali mtu ataomba wakati wa Twawaaf du’aa zote zilizothibiti. Na du’aa maalum ambazo baadhi ya watu wanazileta chini ya bomba la mfereji wa maji ya paa la Al-Ka’abah (gutter) na mfano wa hilo, du’aa hizo hazina asili yoyote. Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akitamatisha Twawaaf yake baina ya Nguzo Mbili kwa kusema:
((رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّار))ِ
..kama alivyokuwa anatamatishia du’aa zake nyinginezo.
9- Kumalizia kwenye Maqaamu Ibraahiym –baada ya Twawaaf- na kusoma:
((وَاتَّخِذُوا مِن مَّقَامِ إِبْرَاهِيمَ مُصَلًّى))
10- Kuswali rakaa mbili nyuma ya Maqaamu Ibraahiym baada ya Twawaaf ikiwezekana.
11- Asome katika rakaa hizi mbili:
((قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ)) na ((قُلْ هُوَ اللَّـهُ أَحَدٌ))
Sunani hizi tatu za mwisho zimethibiti katika Hadiyth ndefu ya Jaabir inayozungumzia sifa ya Hajj ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Jumhuri ya ‘Ulamaa wanasema rakaa mbili nyuma ya Maqaam baada ya Twawaaf ni Sunnah kinyume na Mahanafiy wanaosema kuwa kwao wao ni waajib. Nayo ni riwaya toka kwa Ahmad, na kauli toka kwa Mashaafi’iy. Fuqahaa wa Kimaalik wamekubaliana nao katika Twawaaf ya Nguzo tu pasina nyinginezo. [Fat-hul Qadiyr (2/154), Haashiyatu Al-‘Adwaa (1/467), Mughnil Muhtaaj (1/492) na Al-Mughniy (3/394)]
Fuqahaa wa Kishaafi’iy na Kimaalik wanaona kuwa akiswali Swalaah ya Faradhi baada ya Kutufu, itamtosheleza na Rakaa mbili za Twawaaf.
Rakaa mbili za Twawaaf huswaliwa wakati wowote bila ya ukaraha ijapokuwa katika nyakati ambazo Swalaah imekatazwa kuswaliwa. Ni kwa Hadiyth ya Jubayr bin Mutw’im kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alisema:
((يا بني عبد مناف، لا تمنعوا أحدا طاف بهذا البيت، وصلى أية ساعة شاء من ليل أو نهار))
((Enyi Baniy ‘Abdi Man aaf. Msimzuie yeyote aliyeitufu Nyumba hii, na akaswali saa yoyote aitakayo usiku au mchana)). Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (869), An-Nasaaiy (5/223) na Ibn Maajah (1254)]
Haijuzu kupita mbele ya anayeswali katika Al-Haram na kwenye sehemu nyingine
Ama tamshi la Sheikh wa Uislamu (Rahimahul Laah): “Lau mwenye kuswali ataswali ndani ya Msikiti (Al-Masjid Al-Haraam) na watu wanatufu mbele yake, haitokuwa makruhu, ni sawa akipita mbele yake mwanaume au mwanamke. Na hili ni katika mambo mahsusi ya Makkah”. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/122)]
Mimi siijui dalili yoyote kuhusiana na umahususi huu, Na asili ni kutokujuzu kupita mbele ya mwenye kuswali kama ilivyotangulia katika mlango wa Swalaah. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
12- Kunywa Maji ya Zamzam na kuyamimina kichwani baada ya Kutufu na kuswali rakaa mbili
Hadiyth ya Jaabir inasema: ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikwenda mwendo kasi kidogo mizunguko mitatu [ya kwanza] toka kwenye kikuta cha kiduara hadi kwenye Jiwe, akaswali rakaa mbili, kisha akarudi kwenye Jiwe. Halafu akaenda kwenye Zamzam na akanywa toka humo, akajimwagia kichwani mwake, kisha akarejea, na akaigusa Nguzo…..)). [Imekharijiwa na Ahmad (3/394). Katika Muslim (1218) kumetajwa kunywa tu]
13- Je, mtu ataambatisha kifua chake na shavu lake la kulia na ukuta wa Al-Ka’abah kati ya Jiwe Jeusi na Mlango [wa Al-Multazam]?
Imesimuliwa kuwa Nabiy (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alilifanya hilo Siku alipoikomboa Makkah. Toka kwa ‘Abdur Rahmaan bin Abiy Swafwaan amesema: ((Rasuli wa Allaah alipoikomboa Makkah, nilichomoka haraka, nikamwona Rasuli wa Allaah ametoka toka kwenye Al-Ka’abah yeye pamoja na Swahaba Zake, wakiwa wameigusa Nyumba tokea mlangoni hadi kwenye Al-Khatwiym (Kikuta cha nusu duara), na wakaweka mashavu yao juu ya Nyumba, na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) yuko kati yao)). [Isnaad yake ni Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1898)]
Na imesimuliwa toka kwa ‘Amri bin Shu’ayb toka kwa baba yake toka kwa babu yake amesema: ((Nilitufu pamoja na ‘Abdullaah bin ‘Amri, na alipoelekea sambamba nyuma ya Al-Ka’abah nilisema: Hivi huleti isti’aadhah? Akasema: Tunajilinda kwa Allaah na moto. Kisha akaenda mpaka akaligusa Jiwe, akasimama kati ya Nguzo na Mlango, akakiweka kifua chake, uso wake na mikono yake miwili hivi –akaikunjua mpaka mwisho- na akasema: Hivi ndivyo nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akifanya)). [Isnaad yake ni Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1899), Ibn Maajah (2962), Al-Bayh aqiy katika As-Sunan (5/93), na katika Ash-shu’ab (4058) kwa Sanad Dhwa’iyf]
Ninasema: “Hadiyth zote mbili ni Dhwa’iyf. Lakini je, moja yao inapata mwega kwa nyingine? Hili ni la kulitafiti. Kisha hili la kujiambatisha kifua na mashavu linayumkinika liwe wakati wa kuaga, na liwe katika jingine. Lakini Jumhuri wamesema: Imesuniwa asimame kwenye Al-Multazam (kati ya Jiwe Jeusi na Mlango wa Al-Ka’abah) baada ya Twawaaf ya Kuaga na aombe du’aa, kwa kuwa hapo ni katika mwahala ambapo du’aa hujibiwa kama ilivyosimuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”. [Zaadul Ma’aadiy (2/298), Sharhu Ibn ‘Aabidiyna (1/170-187), Rawdhwat At-Twaalibiyna (3/118), na Kash-shaaful Qinaa (2/513)]
Mazungumzo, kuelimisha na kujibu swali katika Twawaaf
Inajuzu kuzungumza wakati wa Twawaaf. Twawaaf haibatiliki wala haibebi umakruhu, lakini ni bora kuacha isipokuwa kama maneno ni ya kheri kama kuamrisha mema, au kukataza munkari, au kumwelekeza asiye jua, au kujibu fatwa na kadhalika.
Toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) –alipokuwa anatufu Al-Ka’abah- alimpitia mtu ambaye alikuwa amefunga mkono wake kwa mtu mwingine kwa kamba au uzi au kitu kingine kisicho hivyo, Nabiy akaikata kwa mkono wake kisha akamwambia: ((Mwongoze kwa [kumkamata] mkono wake)). [Al-Majmuw’u cha An-Nawawiy (8/62-63)]
Kutufu juu ya kipando
Inajuzu Kutufu juu ya kipando –hata kama mtu anaweza kutembea- kutokana na dharura. ((Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu juu ya ngamia na kuigusa Nguzo kwa bakora yake)) ili watu wapate kumuona. Ni kwa Hadiyth ya Jaabir aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu Nyumba katika Hajj ya Kuaga juu ya mnyama wake, na [alisai] kati ya Swafaa na Marwah [juu ya mnyama pia] ili watu wamwone, ili achomoze, na ili wamuulize, kwani watu walimzonga)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1215)]
Hii ni kauli ya Ash-Shaafi’iy, na riwaya toka kwa Ahmad. Wanasema hakuna tatizo lolote kwa aliyepanda hata bila ya udhuru. Lakini Mahanafiy na Mahanbali wanasema ni lazima atembee kwa hali yoyote. Na akina Maalik wanasema ni lazima atembee lakini katika Twawaaf ya Wajibu tu. Na kama atatufu kwa kupanda naye anaweza kutembea, basi ni lazima achinje mnyama. [Al-Badaai’u (2/128), Haashiyatul ‘Adhwaa (1/468), Al-Mughniy (3/397) na Nihaayatul Muhtaaj (3/275)]
Lenye mashiko ni kuwa hawajibikiwi na chochote. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
20-Nguzo Ya Tatu Ya Hajj: Sa’yi Kati Ya As-Swafaa Na Al-Marwah
Alhidaaya.com [3]
Maana ya Sa’yi
Ni kutembea kati ya Swafaa na Marwah kwenda na kurudi kwa niya ya kutaabudia. Ni “ashwaatw” 7 [mwendo wa kwenda na kurudi] kwa kuanzia As-Swafaa na kumalizia Al-Marwah.
Hukmu yake
Kusai kati ya Swafaa na Marwah ni nguzo kati ya nguzo za Hajj kwa mujibu wa kauli sahihi ya ‘Ulamaa. Ni madhehebu ya Maalik, Ash-Shaafi’iy, Ahmad –katika moja ya riwaya mbili-, Is-Haaq, na Abu Thawr. Ni kauli pia ya Ibn ‘Umar, Jaabir na ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa).
Mwenye kusahau Kusai, au akasahau “shawtw” moja, basi ni lazima arudi kuifanya kamili wakati atakapokumbuka hata kama yuko nchini kwake au sehemu nyingine. Asiporudi, basi Hajj yake itabatilika kwa kuiacha, na haiungwi kwa kuchinja wala kwa jingine lolote. [Fat-hul Qadiyr (2/156), Haashiyatul ‘Adwaa (1/470), Al-Majmuw’u (8/71) na Al-Mughniy (3/385)]
Dalili ya hilo ni:
1- Kauli Yake Ta’aalaa:
((إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ ۖ فَمَنْ حَجَّ الْبَيْتَ أَوِ اعْتَمَرَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِ أَن يَطَّوَّفَ بِهِمَا))
((Hakika Asw-Swafaa na Al-Marwah ni katika Alama za Allaah. Basi yeyote anayehiji kwenye Nyumba hiyo au akatekeleza ‘Umrah basi hakuna lawama kwake Kutufu (vilima) viwili hivyo.)). [Al-Baqarah (2: 158)]
‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) amebainisha maana ya kuteremka Aayah hii na dhana yake. Ameweka wazi kwa ufasaha na usahihi hilo katika Hadiyth ifuatayo..
2- ‘Urwah amesema: ((Nilimuuliza ‘Aaishah nikamwambia: Unasemaje kuhusu
Kauli ya Allaah Ta’aalaa:
((إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ ۖ فَمَنْ حَجَّ الْبَيْتَ أَوِ اعْتَمَرَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْهِ أَن يَطَّوَّفَ بِهِمَا))
..Basi Wa-Allaah, hakuna lawama kwa yeyote kama hakutufu As-Swafaa na Al-Marwah? Akasema: Maneno mabaya kabisa hayo umesema ee mtoto wa dada yangu! Hakika hili lau lingelikuwa kama ulivyoliawilisha, ingekuwa hakuna ubaya kwa mtu kama asingetufu vilima viwili. Lakini Aayah hii iliteremshwa kwa ajili ya Maanswaar. Walikuwa kabla hawajaingia katika Uislamu wakilinyanyulia sauti [sanamu la] Manaat At-Twaaghiyah ambalo walikuwa wanaliabudu eneo la Al-Mushallal. Akawa anayehiji anahisi ukakasi Kutufu As-Swafaa na Al-Marwah. Waliposilimu, walimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuhusu hilo. Wakasema: Ee Rasuli wa Allaah! Hakika sisi tulikuwa tunahisi ukakasi kutufu baina ya As-Swafaa na Al-Marwah [enzi ya ujahili]. Hapo Allaah Ta’aalaa Akateremsha:
إنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ
‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaweka sharia ya Kutufu baina ya vilima viwili, na yeyote hawezi kuacha Kutufu baina yao)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1562)]
3- Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((اسمعوا، فإن الله كتب عليكم السعي))
((Sikieni! Hakika Allaah Amewafaradhishieni Kusai)). [Swahiyh Bituruqihii. Imekharijiwa na Ahmad (6/421) na Al-Haakim (4/70). Angalia Al-Irwaa (1072)]
4- ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) amesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitufu na Waislamu walitufu –anakusudia baina ya As-Swafaa na Al-Marwah- ikawa ni Sunnah [ya Uislamu]. Na kwa uhai wangu, Allaah Haitimizi Hajj ya ambaye hakutufu baina ya As-Swafaa na Al-Marwah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1277) na Ibn Maajah (2986)]
5- Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia ‘Aaishah:
((طوافك بالبيت وبين الصفا والمروة يجزيك أو يكفيك لحجك وعمرتك))
((Kutufu kwako Nyumba, na [Kusai] kati ya As-Swafaa na Al-Marwah, kunakutosheleza au kunakutimizia Hajj yako na ‘Umrah yako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1897), Al-Bayhaqiy (5/106) na Al-Baghawiy (7/84). Kwa Muslim (1211) ina tamshi la ((Inakuenea Twawaaf yako kwa Hajj yako na ‘Umrah yako)).
Na kama isingelikuwa ni waajib, asingesema inakutosheleza. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
6- Toka kwa ‘Amri bin Diynaar amesema: ((Tulimuuliza Ibn ‘Umar kuhusu mtu ambaye ametufu Nyumba katika ‘Umrah na hakutufu kati ya As-Swafaa na Al-Marwah, je anaweza kumwingilia mkewe? Akasema: Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuja akatufu Nyumba mara saba, akaswali nyuma ya Maqaam rakaa mbili, akatufu kati ya As-Swafaa na Al-Marwah mara saba.
Na tukamuuliza Jaabir bin ‘Abdullaah akasema: Asimkurubie kabisa mpaka atufu kati ya As-Swafaa na Al-Marwah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1646). Na Muslim amekhariji (1234) athar ya Ibn ‘Umar]
‘Ulamaa wana kauli mbili nyingine kuhusu hukmu ya Kusai:
Ya kwanza: Abu Haniyfah, Ath-Thawriy na Al-Hasan Al-Baswriy wanaona kwamba Kusai ni waajib na si nguzo. Atakayeacha, basi ni lazima achinje mnyama, na Hajj yake ni sahihi.
Ya pili: Anas bin Maalik, ‘Abdullaah bin Az-Zubayr na Muhammad bin Siyriyna wanaona kuwa Kusai ni Sunnah na si wajibu, na hakuna lolote analodaiwa mtu kama ataacha. Na hili limesimuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas, na linafanana kuwa sawa na madhehebu ya Ubayya bin Ka-‘ab na Ibn Mas’uwd ambao katika maelezo ya pembeni ya Misahafu yao wameandika:
"فلا جناح عليه أن لا يطوف بهما"
((Hakuna ubaya kwake asipotufu vilima viwili)).
Ibn ‘Abdil Barri amesema: “Kilichodondoka katika (maelezo ya kando) Musw-haf wa jamaa hakichukuliwi kuwa hoja, kwa kuwa hakipitishwi kuwa kinatoka kwa Allaah ‘Azza wa Jalla, na wala hakihukumiwi kuwa ni Qur-aan ila tu kile kilichonukuliwa na jamaa kati ya vibao viwili (ndani ya Musw-haf). Na taawiyl bora kabisa iliyosimuliwa kwa Aayah hii ni yale aliyoyaeleza ‘Aaishah”. [At-Tamhiyd cha Ibn ‘Abdul Barri (2/98)]
Kutufu (Al-Ka’abah) na Kusai (kati ya As-Swafaa na Al-Marwah) kwa mwenye kufanya Qiraan na mwenye kufanya Tamattu’i
‘Ulamaa wamekhitalifiana kuhusu hili katika madhehebu matatu: [Az-Zaad (2/271), Tahdhiyb As-Sunan (5/243) na Majmuw’u Al-Fataawaa (26/104)]
La kwanza: Kila mmoja kati ya wawili atafanya Twawaaf mbili (Al-Ka’abah) na Kusai mbili (As-Swafaa na Al-Marwah).
Hili limesimuliwa toka kwa ‘Aliyy na Ibn Mas’uwd. Pia ni kauli ya Sufyaan Ath-Thawriy, Abu Haniyfah, watu wa Kuwfah, Al-Awzaa’iy na riwaya toka kwa Ahmad.
La pili: Kila mmoja kati ya wawili atafanya Twawaaf moja (Al-Ka’abah) na Kusai moja (As-Swafaa na Al-Marwah)
Haya yameelezwa na Al-Imaam Ahmad katika riwaya ya mwanaye ‘Abdullaah. Sheikh wa Uislamu na mwanafunzi wake Ibn Al-Qayyim wamelikhitari hili.
La tatu: Mwenye kufanya Tamattu’i atafanya Twawaaf mbili na Kusai mbili, na mwenye kufanya Qiraan atasai mara moja.
Ni kauli ya ‘Atwaa, Twaawuws na Al-Hasan. Ni madhehebu ya Maalik, Ash-Shaafi’iy na Ahmad.
Kauli ya madhehebu ya kwanza ni dhaifu kwa kuwa haikuthibiti toka kwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) linalohabarisha hilo. Kikubwa wanachoweza kukishikilia wenye kauli hii ni Kauli Yake Ta’aalaa:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
((Na timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah))
na hakuna ndani yake dalili katika hili. Utimilifu wa Hajj unapatikana hata kama –mwenye kufanya Qiraan- hakutufu isipokuwa Twawaaf moja kama inavyoonekana wazi katika dalili za makundi mawili mengine. Ama kauli mbili nyingine, sababu ya tofauti kati yao, ni kukinzana Hadiyth zilizokuja kuhusiana na hilo:
- Toka kwa Jaabir amesema: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakutufu wala Swahaba Zake kati ya As-Swafaa na Al-Marwah isipokuwa Twawaaf moja tu, Twawaaf ya kwanza)). Twawaaf hapa inakusudiwa Kusai. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1215), At-Tirmidhiy (947), Abu Daawuwd (1895), An-Nasaaiy (2986) na Ibn Maajah (2972)]
Toka kwa ‘Aaishah ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia:
((طوافك بالبيت وبين الصفا والمروة يكفيك لحجك وعمرتك))
((Ukitufu Nyumba, na [Kusai] kati ya As-Swafaa na Al-Marwah, kunakutosheleza Hajj yako na ‘Umrah yako)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
Bibi ‘Aaishah hapa alikuwa anafanya Qiraan kwa kauli swahiyh.
- Toka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) amesema: ((..Wakatufu Nyumba na [wakasai] baina ya As-Swafaa na Al-Marwah wale waliokuwa wamenuwia ‘Umrah, kisha wakavua Ihraam [wakatahalluli]. Kisha wakatufu Twawaaf nyingine baada ya kurudi kutoka Minaa. Ama wale waliokusanya Hajj na ‘Umrah, hakika walitufu Twawaaf moja)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1556) na Muslim (1211)]
Ibn Al-Qayyim amesema: “Ima isemwe: ‘Aaishah amethibitisha na Jaabir amekanusha, na kilichothibitishwa kinatangulizwa kabla ya kilichokanushwa. Au isemwe: Muradi wa Jaabir ni wale waliofanya Qiraan pamoja na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na wakaswaga wanyama –nao ni wachache- na hao walisai Sai [Kusai] moja tu na hakukusudia Swahaba wote. Au Hadiyth ya ‘Aaishah itolewe sababu ya kuwa neno lake: (akatufu …hadi mwisho) limepachikwa katika Hadiyth yake. Basi hizi ndizo njia tatu za watu katika Hadiyth yake. [Zaadul Ma’aadi kwa mabadilisho kidogo]
Ninasema: “Ama dai la kupachika, inalazimu kwalo kuwatia makosani vigogo wa hifdhw wenye kuaminika kama Az-Zuhriy na wengineo bila dalili bayana. Hadiyth yake imethibiti, hakuna shaka ndani yake, nayo ina Hadiyth nyingine zinazoipa mwega. [Angalia Kitabu cha Hijjah ya Nabiy cha Al-Albaaniy uk. 90]. Nayo ni dalili kuwa mwenye kufanya Tamattu’u ni lazima afanye Twawaaf mbili [Al-Ka’abah] na Sai mbili [As-Swafaa na Al-Marwah]. Na ‘Aaishah amehifadhi ambayo Jaabir hakuhifadhi. Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas inalitolea ushahidi kuwa aliulizwa kuhusiana na Tamattu’u ya Hajj akasema: ((Muhaajiruna na Answaar walihirimia Hajj pamoja na Wake wa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) katika Hijjah ya Kuaga. Tulipowasili Makkah, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alisema:
إجعلوا إهلالكم بالحج عمرة، إلا من قلد الهدي
Ifanyeni niya yenu ya Hajj ‘Umrah, isipokuwa kwa aliyemvisha mnyama wa kuchinjwa kigwe. Tukatufu Nyumba na [Kusai] As-Swafaa na Al-Marwah, tukawaingilia wake na tukavaa nguo. Akasema (Rasuli):
من قلد الهدي فإنه لا يحل حتى يبلغ الهدي محله
Aliyemvisha mnyama wa kuchinjwa kigwe, basi asivue Ihraam [asitahalluli] mpaka mnyama afike machinjoni mwake. Kisha akatuamuru usiku wa At-Tarwiyah tunuwie Hajj. Na tulipomaliza Manaasik, tulikuja tukaizunguka Nyumba, na As-Swafaa na Al-Marwah, na Hajj yetu ikatimia na tukalazimikiwa mnyama wa kuchinja…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy ikiwa Mu’allaq Majzuwm, na Muslim nje ya Swahiyh yake ikiwa Mawsuwl, na pia Al-Ismaa’iyliy katika Mustakhraji yake, na kutokea kwake Al-Bayhaqiy (5/23), na wapokezi wake ni watu madhubuti]
Na hili limethibiti kihakika kutokana na inavyoonyesha Hadiyth ya ‘Aaishah ya kuwa mwenye kufanya Tamattu’u ni lazima atufu na asai kwa ajili ya ‘Umrah, kisha avue Ihraam (atahalluli). Halafu atatufu na kusai tena baada ya kutoka ‘Arafah. Ama mwenye kufanya Qiraan, huyo ni lazima atufu mara moja na asai mara moja kwa mujibu wa maneno ya Jumhuri.
Je inajuzu kutanguliza Kusai kabla ya Kutufu Nyumba?
Maalik, Ash-Shaafi’iy, Abu Haniyfah na Maswahibu zao wanaona kwamba mwenye Kusai kabla ya Kutufu, hiyo haimtoshelezi na ni lazima arudie tena. Isipokuwa Maalik na Abu Haniyfah wamesema kuwa atatufu na kusai upya kwa yote mawili. Ash-Shaafi’iy amesema: Atasai tu tena ili kuwe baada ya kutufu. [At-Tamhiyd )6/12) na Al-Majmuw’u (8/105)]
Ninasema: Wanatolea dalili Hadiyth ya ‘Aaishah ya kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia –alipoingia hedhini-:
((افعلي ما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت حتى تطهري))
((Fanya (yote) ayafanyayo Hujaji isipokuwa tu usitufu Nyumba mpaka utwaharike)). [Hadiyth Swahiyh. Takhriyj yake imetajwa nyuma]
Kipengele cha dalili toka kwenye Hadiyth hii ni kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwamuru kufanya yote anayoyafanya mwenye kuhiji isipokuwa Kutufu Nyumba tu, na yeye (‘Aaishah) hakusai wala hakutufu. Na lau Kusai kusingelikuwa kumesimamia juu ya kutangulia Twawaaf kabla yake, basi asingelikuchelewesha na hususan pakizingatiwa kwamba mwenye hedhi hakatazwi Kusai -kwa mujibu wa kauli sahihi- kama itakavyobainishwa mbeleni kidogo.
Lakini mtu anaweza kusema: Kuchelewesha ‘Aaishah Kusai mpaka atufu kwanza hakumaanishi kwamba kufanya hivi ni lazima kwa wengine, na hasahasa tukizingatia kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakuulizwa kuhusu ‘amali yoyote iliyotangulizwa au iliyocheleweshwa Yawm An-Nahr [Tarehe 10 Dhul Hijjah] ila alisema:
((افعل ولا حرج))
((Fanya na hakuna ubaya))..
kama itakavyobainishwa mbeleni. Na huyu ni ‘Atwaa, Al-Awzaaiy na kundi la Asw-Haabu Al-Hadiyth.
Je inajuzu kwa mwenye hedhi asai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah?
Kuna ziada iliyosimuliwa katika Hadiyth iliyotangulia ya ‘Aaishah:
((افعلي كما يفعل الحاج غير أن لا تطوفي بالبيت [ولا بين الصفا والمروة] حتى تطهري))
((Fanya (yote) kama anavyofanya Hujaji isipokuwa tu usitufu Nyumba [wala baina ya As-Swafaa na Al-Marwah] mpaka utwaharike)).
Lakini neno lake (wala baina ya As-Swafaa na Al-Marwah) ni ziada isiyo ya kawaida na haifai. [Angalia Fat-hul Baariy (3/589) na Jaami’u Ahkaamin Nisaa (2/534)]
Na hata tukiijaalia kuwa ziada hii ipo kwenye Hadiyth, lakini pamoja na hivyo, haionyeshi kuwa kunashurutishwa kuwa twahara kwa mwenye Kusai, kwa kuwa Kusai kunasimamia juu ya kufanywa Twawaaf kabla yake –kwa mujibu wa Jumhuri-, hivyo kizuizi cha Kusai kikawa ni kutotufu.
Na hakuna pia dalili yoyote ya kushurutisha twahara kwa ajili ya Kusai, bali imepokewa kwa njia sahihi toka kwa Ibn ‘Umar kwamba amesema: ((Akitufu Nyumba, kisha akapata hedhi kabla hajasai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah, basi asai kati ya As-Swafaa na Al-Marwah)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah katika Al-Muswannaf (1/4/343)]
Mithili ya kauli hii zimepokewa kauli sahihi toka kwa Al-Hasan, ‘Atwaa, Al-Hakam, Hammaad na wengineo katika Masalaf, nayo ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy. [Muswannaf Ibn Abiy Shaybah (1/4/344) kwa Asaaniyd Swahiyh. Angalia Al-Majmuw’u (8/106)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
21-Ahkaam Za Sa’yi Baina Ya As-Swafaa Na Al-Marwah
Alhidaaya.com [3]
Shuruti za Sa’yi
Ili Kusai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah kuwe sahihi, ni sharti mambo yafuatayo:
1- Kufanyike baada ya Twawaaf sahihi –kwa mujibu wa Jumhuri- kama ilivyotangulia.
2- Iwe mizunguko saba. Kutoka As-Swafaa hadi Al-Marwah ni mzunguko, na kutoka Al-Marwaa hadi As-Swafaa ni mzunguko na kuendelea. Akifanya shaka kuhusu idadi kabla hajamaliza, ni lazima ajengee dhana katika idadi chache kama ilivyo katika Twawaaf (yaani akishakia kati ya nne na tano, basi afanye kuwa ni nne).
3- Aanzie toka As-Swafaa na amalizie Al-Marwah. Akifanya kinyume kwa kuanzia mzunguko wake wa kwanza toka Al-Marwah, basi mzunguko huu hauhesabiki. Lau ataianza mizunguko yake kutokea As-Swafaa na akaumalizia wa saba As-Swafaa, basi wa kwanza hauhesabiki, na atabakiwa na wa saba. [Ibn Hazm alipitikiwa na wazo lenye makosa akadai kwamba mtu atakwenda kasi katika mizunguko mitatu na atatembea kawaida mizunguko minne iliyobakia, na wengine katika hali hiyo hiyo, wameifanya mizunguko kumi na nne, na wote wana makosa kama alivyobainisha Ibn Al-Qayyim katika Az Zaad (2/231)]
4- Kusai kufanyike kwenye eneo lake maalum ambalo ni barabara iliyonyooka baina ya As-Swafaa na Al-Marwah.
Shuruti hizi zote ni kutokana na alivyofanya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) mwenye kusema:
((خذوا عني مناسككم))
((Jifunzeni kutoka kwangu matendo yenu ya Hajj)). [Al-Majmuw’u (8/95)]
Sunnah za Sa’yi
1- Mwenye Kusai awe na twahara, kwa kuwa ni dhikr kama ilivyo kwenye Twawaaf.
2- Aiguse nguzo kabla hajatoka kwenda sehemu ya Kusai kama ilivyo kwenye Hadiyth ya Jaabir.
3,4- Anapokurubia As-Swafaa asome:
إِنَّ الصَّفَا وَالْمَرْوَةَ مِن شَعَائِرِ اللَّـهِ
na atasema:
أبدأ بما بدأ الله به
Na hili liko katika Hadiyth ya Jaabir.
5,6- Aelekee Qiblah anapokuwa juu ya As-Swafaa na aseme:
((لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، لَا إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ وَحْدَه، اَنْجَزَ وَعْدَهُ وَنَصَرَ عَبْدَهُ وَهَزَمَ الأحْزابَ وَحْدَهُ))
Kisha aombe alitakalo. Atafanya hivi mara tatu.
7- Atembee kawaida kwenda Al-Marwah na anaweza kupanda (kipando) kama kuna haja. Katika Hadiyth ya Jaabir: ((Kisha aliteremka kuelekea Al-Marwah, na hata miguu yake ilipojikita barabara katika kitovu cha bonde alikwenda kasi kidogo, na miguu ilipopanda alitembea kawaida mpaka akafika Al-Marwah, akafanya juu ya Al-Marwah kama alivyofanya juu ya As-Swafaa)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1297), Abu Daawuwd (1970) na An-Nasaaiy (3062)]
Ibn ‘Abbaas amesema alipoulizwa kuhusu Kusai kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) baina ya As-Swafaa na Al-Marwah akiwa amepanda: ((Hakika watu wengi walimzonga Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) wakisema: Huyu Muhammad, huyu Muhammad, mpaka wakatoka wasichana vigori toka majumbani.. na walipozidi kumzonga, alipanda [mnyama]. Na kutembea kawaida na kwa kasi kidogo ni bora zaidi [kuliko kupanda])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1264) toka Hadiyth ya Abiy At-Twufayl].
8- Kwenda mchakamchaka wa nguvu kidogo kati ya alama mbili za kijani
Hili ni kwa wanaume tu na si kwa akina mama kama katika Twawaaf.
9- Kuomba du’aa baina ya As-Swafaa na Al-Marwah kama ilivyothibiti toka kwa Ibn Mas‘uwd kwamba alikuwa anasema:
((رب اغفر وارحم، إتك أنت الأعز الأكرم))
[Hadiyth Swahiyh Marfuw’u. Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (4/68) na At-Twabaraaniy katika Ad-Du’aa (870)]
10- Afanye juu ya Al-Marwah kama alivyofanya juu ya As-Swafaa kama kusoma, kuleta tahliyl na takbiyr, kuelekea Qiblah na kuomba du’aa.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
22-Kunyoa Na Kupunguza Kwa Mwenye Kufanya Tamattu’u
Alhidaaya.com [3]
Hujaji mwenye kufanya Tamattu’u akimaliza Kusai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah, atavua Ihraam ya (atatahalluli na) ‘Umrah yake kwa kunyoa au kupunguza. Ni bora apunguze nywele kuliko kuzinyoa, kwa kuwa atakuja kuzinyoa zote Siku ya An-Nahr (tarehe 10) baada ya kumaliza ‘amali za Hajj. Katika Hadiyth ya Jaabir, Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((حلوا من إحرامكم فطوفوا بالبيت وبين الصفا والمروة، وقصروا، وأقيموا حلالا حتى إذا كان يوم التروية فأهلوا بالحج...))
((Vueni Ihraam zenu, mtufu Nyumba na [msai] baina ya As-Swafaa na Al-Marwah, na punguzeni nywele, na kaeni mkiwa hamna Ihraam mpaka inapofika Siku ya At-Tarwiyah, hirimieni Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1568) na Muslim (1216)]
Akipunguza, anakuwa huru, na anaruhusiwa kufanya kila kitu hata kujimai mpaka Siku ya At-Tarwiyah.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
23-Sunnah Za Kutoka Kwenda Minaa
Alhidaaya.com [3]
1- Hujaji [mwenye kufanya Ifraad katika wakazi wa Makkah au aliyefanya Tamattu’u] ahirimie toka nyumbani kwake Siku ya At-Tarwiyah (Tarehe nane Dhul Hijjah).
2- Mahujaji wote waelekee Minaa Siku ya At-Tarwiyah kabla ya Adhuhuri.
3- Waswali Adhuhuri na Alasiri, na Magharibi na ‘Ishaa Siku ya At-Tarwiyah.
4- Walale Minaa ili waswalie Alfajiri huko na jua la Arafah liwachomozee huko.
5- Wahame katika maeneo haya kwa kutumia kipando (gari n.k), na kupanda ni bora kuliko kutembea.
6- Afunge Hujaji kijihema kidogo Namirah kama atataka kumwiga Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam).
Dalili ya Sunan hizi ni yaliyoelezewa katika Hadiyth ya Jaabir: ((..Na ilipokuwa Siku ya At-Tarwiyah, walielekea Minaa, wakahirimia Hajj. Na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipanda [mnyama], akaswalia huko Adhuhuri, ‘Alasiri, Magharibi, ‘Ishaa na Alfajiri. Halafu alikaa kidogo mpaka jua likachomoza, akaamuru ajengewe kijihema cha manyoya Namirah, na Rasuli wa Allaah akaenda mpaka akafika ‘Arafah..)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1218]
7- Alete Talbiyah au Takbiyr wakati anapotoka Minaa kuelekea ‘Arafah. Ni kwa Hadiyth ya Muhammad bin Abiy Bakr Ath-Thaqafiy kuwa alimuuliza Anas bin Maalik –nao wakirauka asubuhi kwenda ‘Arafah toka Minaa-: Vipi mlikuwa mnafanya katika siku hii pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)? Akasema: Alikuwa mmoja wetu analeta Tahliyl naye hamkatazi, na mwenye kuleta Takbiyr naye hamkatazi)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1659) na Muslim (1284)]
Na toka kwa Ibn ‘Umar amesema: ((Tulirauka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) toka Minaa kwenda ‘Arafah, baadhi yetu wakileta Talbiyah na wengine wakileta Takbiyr)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1284)]
8- Imamu awahutubie na awabainishie Manaasik za Hajj, na awahimize wakithirishe du’aa na kujinyenyekeza kwa Allaah. Awabainishie mambo muhimu ya lazima ya dini yao na utengemao wa hali zao kama ilivyo katika Hadiyth ya Jaabir. Khutbah hii ni Sunnah kwa makubaliano ya ‘Ulamaa wote, na imesuniwa iwe khutbah moja badala ya mbili ya kukaa kati yake. Ni mashuhuri katika vitabu vya sharia za kivitendo.
9- Aswali Adhuhuri na ‘Alasiri kwa kukusanya na kupunguza pamoja na imamu huko Namirah (Siku ya ‘Arafah), na asiswali kati ya Swalaah hizi mbili Swalaah nyingine yoyote. [Aliyekosa kuziswali pamoja na imamu, anaruhusiwa kuziswali peke yake kwa kuzikusanya kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri. Abu Haniyfah amesema haijuzu]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
24-Nguzo Ya Nne Ya Hajj: Kusimama ‘Arafah
Alhidaaya.com [3]
Muradi wa Kusimama ‘Arafah ni kuwepo Hujaji katika ardhi ya ‘Arafah kwa mujibu wa shuruti na ahkaam zilizotajwa.
Hukmu yake
Kusimama ‘Arafah ni nguzo ya kimsingi kati ya nguzo za Hajj. Sifa yake pekee tofauti na nguzo nyingine ni kuwa atakayepitwa na kisimamo hiki basi ameikosa Hajj.
Kuwa kwake nguzo kumethibiti kwa dalili zisizo na chembe ya shaka toka kwenye Qur-aan, Sunnah na Ijma’a.
(a) Kwenye Qur-aan
Allaah Ta’alaa Amesema:
((ثُمَّ أَفِيضُوا مِنْ حَيْثُ أَفَاضَ النَّاسُ))
((Kisha miminikeni kutoka pale wamiminikapo watu)). [Al-Baqarah (2:199)]
Aayah hii imethibiti kuwa iliteremka kuwaamuru watu wasimame ‘Arafah. Toka kwa ‘Urwah toka kwa baba yake toka kwa ‘Aaishah ((Kuwa Aayah hii iliteremka kuwazungumzia “Al-Hums”. Amesema: Walikuwa wanamiminika toka Jam-‘u [Muzdalifah], wakaamuriwa wamiminike toka ‘Arafaat)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1665) na Muslim (1219)]
“Al-Hums” ni Maqureysh na kizazi chao. Walikuwa enzi ya ujahilia wakimiminika toka Muzdalifah (Jam-‘u), na watu wakimiminika toka ‘Arafaat. Wameitwa hivyo kutokana na ushadidiaji na ukereketwa wa iymaan yao.
(b) Kwenye Sunnah
Kuna Hadiyth nyingi. Iliyo mashuhuiri zaidi ni Hadiyth ya ‘Abdur Rahmaan bin Ya-‘amar ((Kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwamuru mpiga mbiu anadi:
((الحج عرفة، من جاء ليلة جمع قبل طلوع الفجر فقد أدرك الحج))
((Hajj ni ‘Arafah. Atakayekuja usiku wa Jam-‘u [Muzdalifah] kabla ya kuchomoza Alfajiri, basi hakika ameipata Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1933), At-Tirmidhiy (590), An-Nasaaiy (5/264) na Ibn Maajah (3015)]
(c) Kwenye Ijma’a
‘Ulamaa wengi wamenukuu Ijma’a ya kuwa Kusimama ‘Arafah ni nguzo kati ya nguzo za Hajj, na mwenye kupitwa na kisimamo hicho, basi ni lazima ahiji mwaka kesho. [Bidaayatul Mujtahid (1/335)]
Wakati Wake
1- Jumhuri ya ‘Ulamaa wanasema wakati wa Kusimama ‘Arafah unaanzia baada ya kupinduka jua (Adhuhuri ya) Siku ya ‘Arafah (tarehe 9). [Al-Badaai’u (2/125) na Al-Mughniy (3/414)]
Ni kutokana na kitendo cha Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ambaye hakusimama ‘Arafah ila baada ya jua kupinduka kama ilivyoeleza Hadiyth ndefu ya Jaabir. Na Rasuli kasema:
((خذوا عني مناسككم))
((Jifunzeni kutoka kwangu matendo yenu ya Hajj)).
Lakini Imaam Ahmad (Rahimahu-Allaah) amesema kuwa wakati wa kusimama unaanzia tokea Alfajiri ya Siku ya ‘Arafah. Na dalili yake ni Hadiyth ya ‘Urwah bin Mudhwarras kuwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((من شهد صلاتنا هذه ووقف معنا حتى يدفع وقد وقف بعرفة قبل ذلك ليلاً أو نهاراً فقد تم حجه وقضى تفثه))
((Aliyehudhuria Swalaah yetu hii [Swalaatul Fajr], akasimama pamoja nasi mpaka akaondoka, na akawa alisimama ‘Arafah kabla ya hapo usiku au mchana, basi Hajj yake imetimia na ametimiza Nusuk zake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na
Abu Daawuwd (1950), At-Tirmidhiy (891), An-Nasaaiy (5/263) na Ibn Maajah (3016). Angalia Al-Irwaa (1066)]
Lakini neno lake “mchana” halikuainisha wakati maalum, na wakati huo unaainishwa na kitendo cha Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), na muradi unakuwa ni baada ya jua kupinduka. Na hili ndilo la akiba na salama zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
2- Mwenye kusimama ‘Arafaat mchana, basi ni lazima avute muda wa kubakia hapo hadi baada ya kuchwa jua. Na kama ataondoka hapo kabla ya Magharibi, basi Abu Haniyfah, Ash-Shaafi’iy na Ahmad wanasema kuwa Hajj yake ni sahihi lakini ni lazima achinje ili aunge sehemu ya usiku aliyoipunguza ambayo ilikuwa ijumuishwe na sehemu ya mchana ktk Kisimamo. [Al-Badaai’u (3/1098), Al-Majmuw’u (8/123) na Al-Mughniy (3/370)]
Riwaya toka kwa Ash-Shaafi’iy inasema si lazima achinje. Ahlu Adh-Dhwaahir wamesema hivyo hivyo. [Al-Muhallaa (7/8)]
Na hii ndio kauli yenye nguvu. Lakini Maalik amesema kuwa Hajj yake haiswihi mpaka akusanye baina ya usiku na mchana katika kusimama kwake. [Al-Mudawwanah, Bidaayatul Mujtahid (1/375)]
Na hoja yake ni Hadiyth ya Ibn ‘Umar amesema: ((Mwenye kuipata ‘Arafaat kwa usiku basi ameipata Hajj, na aliyepitwa na ‘Arafaat usiku, basi Hajj imempita. Basi huyo avue Ihraam kwa ‘Umrah, na ni lazima ahiji mwaka ujao)). [Hadiyth Swahiyh Marfuw’u. Imekharijiwa na Maalik katika Al-Muwattwa (886 ikiwa Mawquwf) na Ad-Daara Qutwniy (2/241) Marfuw’u]
Hadiyth hii imejibiwa ikiambiwa kuwa usiku umehusishwa kwa kuwa kupitwa na kisimamo kunafungamana nao. Na kiini cha inachodulisha ni:
3- Kiasi kinachotosheleza Kusimama ni Hujaji asimame sehemu ya usiku kabla ya Alfajiri –japo kwa muda mfupi- na kama Alfajiri itachomoza kabla hajasimama, basi ataikosa Hajj. Hili limegusiwa vile vile na Hadiyth iliyotangulia ya ‘Urwah bin Mudhwarras. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
Sunnah Na Adabu Za Kusimama ‘Arafah Na Kuondoka (kumiminika) Kutoka Hapo
1- Kusimama pembeni mwa miamba ya mawe
Hujaji anaruhusiwa kusimama sehemu yoyote ya eneo la ‘Arafah. Lakini imesuniwa asimame pembeni au mbele ya miamba ya mawe iliyotandazika chini ya Jabal Ar-Rahmah. Jabali hili liko katikati ya ardhi ya ‘Arafaat. Kufanya hivi ni kwa Hadiyth ya Jaabir: ((..mpaka akafika sehemu ya kisimamo, akamwelekeza ngamia wake Al-Qaswaa upande wa miamba ya mawe, na njia ya watembeao kwa miguu ikawa mbele yake..)).
An-Nawawiy amesema: “Na hiki ndicho Kisimamo kilichostahabiwa. Ama kitendo kilichozoeleka kufanywa na watu wa kawaida wasio na uelewa wa dini cha kupanda juu ya Jabali hilo na kudhani kuwa Hajj haiswihi ila kwa kufanya hivyo, basi hilo ni kosa”.
2,3- Kuelekea Qiblah na kunyanyua mikono miwili kuomba du’aa
Ni kwa Hadiyth ya Jaabir: ((Na akaelekea Qiblah…)). Na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((خير الدّعاء يوم عرفة، وخير ما قلت أنا والنبيّون من قبلي: لا إله إلّا الله وحده لا شريك له، له الملك وله الحمد، وهو على كلّ شيءٍ قدير))
((Du’aa bora na ya kheri zaidi ni ya Siku ya ‘Arafah. Na bora na la kheri zaidi nililolisema Mimi na Manabii walionitangulia ni: Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah Peke Yake Asiye na mshirika, ni Wake Ufalme, na ni Yake Himdi, Naye ni Mweza juu ya kila kitu)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (3585), na Ibn Abiy Shaybah (1/369). Angalia As-Swahiyhah (1503)]
Kuna matamshi mengi ya du’aa ya ‘Arafah yaliyopokelewa toka kwa Nabiy (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), lakini Asaaniyd Zake ni Layyin. [Angalia Zaadul Ma’aad (2/237)]
4- Kuleta Talbiyah
Ni kwa Hadiyth ya Sa’iyd bin Jubayr. Amesema: ((Tulikuwa pamoja na Ibn ‘Abbaas, akaniambia: Ee Sa’iyd! Mbona siwasikii watu wakileta Talbiyah? Nikamwambia: Wanamwogopa Mu’aawiyah. Ibn ‘Abbaas akatoka ndani ya hema lake akasema: “Labbayka Allaahumma Labbayka”, hakika wao wameiacha Sunnah kwa kumchukia ‘Aliyy (Radhwiya Allaah ‘anhu)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Haakim (1/464-465) na Al-Bayhaqiy (5/103). Angalia kitabu cha Hijjatun Nabiyy (uk. 74)]
Ninasema: “Ingawa Ibn Taymiyah (26/136) amesema kwamba kuleta Talbiyah ‘Arafah hakukuripotiwa toka kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) bali kumenukuliwa toka kwa Makhalifa Waongofu na wengineo, lakini Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas –ikiwa ni Swahiyh- inakuwa ni hoja dhidi yake. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Angalizo
Hivi ndivyo inavyotakikana iwe hali ya Hujaji anapokuwa ‘Arafah. Alete adhkaar na du’aa, ahudhurishe moyo, asome Qur-aan, awe mnyenyekevu, ajinyenyekeze na ajikurubishe kwa Allaah Subhaanah.
Hakika ni hasara kubwa kuwaona baadhi ya Mahujaji katika Siku hii ya ‘Arafah wakiipitisha Siku hii kwa kufanya mambo ya kipumbao yasiyo na faida, kucheza na kuzungumza na wenzi wao mambo yasiyo na ulazima. Na hata wengine wanafikia ujasiri wa kucheza karata, kuvuta sigara, kusikiliza nyimbo na muharramaat zingine. Tunajilinda kwa Allaah na hali hii ya kutojali kitu.
5- Hujaji asifunge Swawm
Ni kwa Hadiyth ya Maymuwnah: ((Kwamba watu walishakia kama Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amefunga Siku ya ‘Arafah. Nikampelekea maziwa –naye kasimama sehemu ya Kisimamo-, akayanywa na watu wanatizama)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1989) na Muslim (1124)]
6- Kuteremka toka ‘Arafah kwa utulivu na utaratibu baada ya kuchwa jua
Ni kwa neno lake Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) –wakati alipoteremka toka ‘Arafah baada ya kuchwa jua-:
((أيها الناس عليكم السكينة، فإن البر ليس بالابضاع))
((Enyi watu! Fanyeni utulivu, kwani wema si kwa kukimbizana)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1671), Muslim (1218) na An-Nasaaiy (5/257)]
Lakini kama atapata njia wazi mbele yake, basi anaweza kuchakarisha mwendo kidogo. Ni kwa Hadiyth: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anatembea mwendo wa hatua pana, na kama njia iko wazi, aliharakisha mwendo kidogo)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1666) na Muslim (1286)]
7- Kutembea kwa miguu kwenda Muzdalifah sambamba na kuleta Talbiyah
Hadiyth husika imelielezea hili nyuma kuzungumzia mwahala pa kuleta Talbiyah.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
25-Kulala Muzdalifah Usiku Wa Yawm An-Nahr
Alhidaaya.com [3]
Hukmu yake
Fuqahaa wamekhitalifiana kuhusu hukmu ya kusimama Muzdalifah (ambayo pia huitwa Jam-‘u) na kulala hapo katika kauli tatu:
Ya kwanza:
Ni nguzo, na atakayekosa kusimama hapo, basi kaikosa Hajj. Ni madhehebu ya Ibn ‘Abbaas, Ibn Az-Zubayr, An-Nakh-’iy, Ash-Sha-’abiy, ‘Alqamah na Ahlu Adh-Dhwaahir. Kuna kidokezo katika madhehebu ya Maalik kuhusu hili, na ni chaguo la Ibn Al-Qayyim (Rahimahu-Allaah). [Al-Mughniy (3/376), Al-Muhallaa (7/118), Bidaayatul Mujtahid (1/376) na Zaad Al-Ma’aad (3/253)]
Dalili zao ni:
1- Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَإِذَا أَفَضْتُم مِّنْ عَرَفَاتٍ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ عِندَ الْمَشْعَرِ الْحَرَامِ ۖ))
((Basi mtakapomiminika kutoka ‘Arafaat mdhukuruni Allaah kwenye Al-Mash-’aril Haraam)). [Al-Baqarah (2:198)]
Kuna ‘Ulamaa wanaosema kuwa Al-Mash-’arul Haraam ni Jabali ambalo liko Muzdalifah lijulikanao kama “Quzah”, na wengine wamesema ni eneo lote la Muzdalifah.
2- Hadiyth ya ‘Urwah bin Al-Mudhwarras kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((من شهد صلاتنا هذه ووقف معنا حتى ندفع وقد وقف بعرفة قبل ذلك ليلاً أو نهاراً فقد أتم حجه وقضى تفثه))
((Aliyehudhuria Swalaah yetu hii [Swalaatul Fajr], akasimama pamoja nasi mpaka tukaondoka, na akawa alisimama ‘Arafah kabla ya hayo usiku au mchana, basi ameitimiza Hajj yake na ametekelezaNusuk zake)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
3- Ni kitendo cha Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ambacho ni kama kibainisho cha aliloamuriwa katika Aayah Tukufu.
Ya pili:
Ni waajib, na mwenye kuacha ni lazima achinje na Hajj yake ni sahihi. Kauli hii ni madhehebu ya Jumhuri ya ‘Ulamaa. Dalili zao ni:
1- Kauli ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((الحج عرفة، من جاء قبل أن يطلع الفجر فقد أدرك))
((Hajj ni ‘Arafah. Atakayekuja kabla ya kuchomoza Alfajiri basi ameipata)). [Al-Mughniy (3/417) na Az-Zaad (2/253)]
Hii ina maana kuwa atakayesimama ‘Arafah kabla ya kuchomoza Alfajiri kwa kitambo kidogo, basi Hajj yake ni sahihi. Na kama kusimama Muzdalifah kungekuwa ni nguzo, basi Hajj yake isingeswihi.
2- Kama ingelikuwa ni nguzo, basi wanaume na wanawake wangeifanya wote kwa pamoja. Na kwa kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwaamuru akina mama watangulie mbele usiku, imejulikana kuwa si nguzo.
Wamejibu kuhusu Aayah (iliyotajwa 198 Al-Baqarah) na Hadiyth ya ‘Urwah bin Al-Mudhwarras wakisema kuwa kilichotamkwa ndani ya viwili hivyo si nguzo, kwani lau mtu atalala Muzdalifah, na asimdhukuru Allaah wala kuswali hapo, basi Hajj yake ni sahihi.. Kisha, kulala si lazimisho la kumdhukuru Allaah Ta’aalaa wala kuswali Swalaah ya Alfajiri, kwa kuwa ikiwa atateremka toka ‘Arafah mwishoni mwa usiku wa tarehe 10, ataweza hayo.
Hivyo basi, tunalazimika kulichukulia hilo [la kulala Muzdalifah] kama ima ni jambo la waajib, au jambo bora, au jambo mustahabu. [Ikhtiyaaraat Ibn Qudaamah Al-Fiqhiyyah cha Al-Ghaamidiy (1/678)]
Ninasema: “Kwa mujibu wa hoja hii, muradi wa kuitimiza Hajj katika Hadiyth ni utimizaji ambao hata kama haupo, basi jambo litakuwa ni sawa lakini pamoja na uharamu. Linalotoa mwega kwa hayo niyasemayo ni kuwa atakayeipata ‘Arafah na Muzdalifah lakini hakutufu Twawaaful Ifaadhwah, basi Hajj yake inakuwa haikutimia kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa. Allaah Ndiye Mjuzi Zaidi.
Na kauli isemayo kusimama na kulala Muzdalifah ni waajib, ndio kauli sawa na yenye nguvu zaidi. Lakini sitosema lolote kuhusu lazimisho la kuchinja mnyama wa kufidia kosa la kutosimama, kwa kuwa kiasli, mali ya Muislamu ni haramu isipokuwa kwa haki, na hili hujulikana kwa dalili. Na haiswihi kuleta Qiyaas cha kafara hata kama hili ni kinyume na Jumhuri ya ‘Ulamaa”.
Ya tatu:
Ni Sunnah. Hii ni kauli dhaifu, nayo ni riwaya toka kwa Ahmad.
Faida
Mpaka wa muda wa wajibu wa kulala
[Raddu Al-Mukhtaar (2/241), Haashiyatul ‘Adwaa (1/475), Mughnil Muhtaaj (1/498) Al-Mughniy (3/417) na Al-Furuw’u (3/510)]
Mahanafiy wanasema kuwa mwenye kupata kiasi cha kitambo kidogo cha kutokea kuchomoza Alfajiri –Yawm An-Nahr (Tarehe 10)- mpaka jua kutoka hapo Muzdalifah, basi amekipata kisimamo cha Muzdalifah, ni sawa kama alilala hapo au la. Na kama hakupata kitambo hicho, basi ni lazima achinje isipokuwa tu kama alishindwa kutokana na udhuru, hapo hatowajibikiwa kuchinja.
‘Ulamaa wa Kimaalik wanasema ni muda wa kumtua mnyama mzigo sehemu yoyote ya usiku kitambo cha kati ya kuwasili kwake hadi kuchomoza Alfajiri.
Ama Mashaafi’iy na Mahanbali, wao wanasema ni lazima asimame kiasi cha kitambo cha kuanzia anapowasili hadi usiku wa manane –kama atafika hapo kabla ya usiku wa manane- na ikiwa atafika hapo baada ya usiku wa manane basi kitamtosha kitambo kifupi kabla ya kuchomoza Alfajiri.
Ninasema: “Linaloonekana ni kuwa waajib ni kulala Muzdalifah mpaka Alfajiri, ni sawa alifika huko kabla ya usiku wa manane au baada yake, kwa kuwa kulala maana yake ni kusalia huko mpaka Alfajiri. Lakini wanawake madhaifu na wengineo, wanaruhusiwa kuondoka hapo baada ya usiku wa manane. Matamshi ya Hadiyth kadhaa yanadokeza hilo [la kuruhusiwa kuondoka] kama Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Tulishuka Muzdalifah, na Sawdah akamwomba ruksa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ili sisi [wanawake] tuondoke kabla ya mminyano wa watu. Yeye alikuwa mzito wa kutembea na Rasuli akamruhusu. Akaondoka kabla ya mminyano wa watu…)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1681) na Muslim (1290]
Hadiyth hii iko wazi ikibainisha kuwa ambaye hana ruksa [au udhuru], basi ni lazima abakie Muzdalifah mpaka asubuhi, kwa kuwa ni kitendo kwa mkabala wa ruksa.
Vile vile Hadiyth ya Asmaa: ((Kwamba yeye alishuka Muzdalifah, akasimama muda hivi akiswali, kisha akasema: Ee mwanangu kipenzi! Je, mwezi umezama? Nikasema: Hapana. Akaswali tena muda hivi kisha akasema: Ee mwanangu kipenzi! Je, mwezi umezama? Nikasema: Na’am. Akasema: Basi ondokeni. Tukaenda mpaka tukatupia vijiwe Al-Jamarah, halafu akarejea, akaswali Alfajiri nyumbani kwake [Minaa]. Nikamwambia: We vipi! Mimi sioni ila tumewahi sana kuondoka [Muzdalifah]. Akasema: Ee mwanangu kipenzi! Hakika Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amewaruhusu wanawake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1679) na Muslim), na anayezungumza hapa na Asmaa ni mwachwa huru wake au mtumishi wake ‘Abdallah]
Na toka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) [akiwa kijana mdogo wakati huo] amesema: ((Mimi ni katika ambao Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwatanguliza mapema pamoja na wakeze ambao afya zao si imara)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1678) na Muslim (1293)]
Hadiyth hizi na nyinginezo zinatuhabarisha kuwa ulalaji wa wajibu ni mpaka Alfajiri isipokuwa kwa wanawake wenye afya dhaifu na nguvu kidogo. Hawa wanaruhusiwa kushuka toka hapo kabla ya Alfajiri baada ya mwezi kutoweka.
Faida
Ruksa ya kutolala Muzdalifah ni mahsusi kwa wanawake wenye afya dhaifu na nguvu kidogo pamoja na watoto wadogo. Je, wanawake kiujumla wanaingia kwenye ruksa hii, au ni kwa madhaifu tu kati yao?
Nukta hii ni ya kuitafiti. Inavyoonekana ni kuwa inawahusu wanawake madhaifu tu, kwa kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwatanguliza wake zake madhaifu na ‘Aaishah akabaki pamoja naye. Sawdah alimwomba ruksa ya kuondoka mapema kwa kuwa alikuwa mnene na mzito wa kutembea. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Mambo yaliyosuniwa Muzdalifah na kuondoka kutoka hapo
1- Ni kuswali Magharibi na ‘Ishaa kwa pamoja katika wakati wa ‘Ishaa (Jam-‘u Taakhiyr) hapo hapo Muzdalifah.
2- Adhana moja na Iqaamah mbili kwa Swalaah mbili.
3- Kuacha Sunnah zote baina ya Swalaah mbili.
4- Kulala mpaka Alfajiri bila kusimama usiku kuswali.
5- Kuswali Alfajiri mwanzoni mwa wakati wake kwa Adhana moja na Iqaamah moja.
6- Kusimama juu ya kilima cha Muzdalifah, kuelekea Qiblah na kuomba du’aa, pamoja na kuleta Tahmiyd, Takbiyr na Tahlilyl mpaka papambazuke kabisa.
7- Kuondoka kwa utaratibu toka Muzdalifah kabla jua halijachomoza.
8- Kukaza mwendo kidogo katika eneo la Batwn Muhassir isipokuwa kama amepanda gari ambayo yeye si dereva, hapo hawezi kufanya hivyo. Lakini inakuwa vyema anuwie kwa moyo wake lau angeliweza kuchakarisha mwendo hapo, basi angeuchakacharisha. [Batwn Muhassir ni eneo kati ya Minaa na Muzdalifah. Limeitwa hivyo kwa kuwa ndovu wa jeshi la Abrahah walinyon’gonyea hapo na kuishiwa nguvu kabisa. Na huenda kutokana na hilo, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akikaza mwendo kama ilivyo desturi yake mwahala pa watu walioshushiwa adhabu]
9- Aende Jamarah (kurusha vijiwe) kwa njia nyingine tofauti na ile aliyoipita akielekea ‘Arafaat (ikiwezekana).
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
26-Jamaraat (Kurusha Vijiwe) Minaa
Alhidaaya.com [3]
Taarifu yake
الرمي katika lugha ni kutupa kitu kwa kasi. Na الجمرات أو الجمار ni vijiwe vidogo.
Umoja wake (singular) ni جمرة ambazo ni changarawe.
Hukmu yake
Jumhuri ya ‘Ulamaa wanasema Kutupia Jamaraat ni waajib na haijuzu kuacha, na mwenye kuacha ni lazima achinje mnyama.
Dalili ya kuwa ni waajib
1- Hadiyth ya Jaabir aliyesema: ((Nilimwona Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) anatupia vijiwe akiwa juu ya mnyama wake Siku ya An-Nahr [tarehe 10] na anasema:
((لتأخذوا عني مناسككم، فإني لا أدري لعلي لا أحج بعد حجتي هذه))
((Jifunzeni kutoka kwangu Manaasik zenu, kwani hakika mimi sijui, huenda nisihiji baada ya Hijjah yangu hii)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1297), An-Nasaaiy (3062) na Abu Daawuwd (1970)]
2- Neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((إنما جعل الطواف بالبيت وبالصفا والمروة ورمي الجمار لإقامة ذكر الله))
((Hakika si jinginelo, Kutufu Nyumba, Kusai baina ya As-Swafaa na Al-Marwah na Kutupia vijiwe kumewekwa kwa ajili ya kumdhukuru Allaah)). [Isnaad yake ni Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1888), At-Tirmidhiy (902) na Ahmad (4/64)]
3- Ni ‘amali ambayo baada yake inafuatia kuvua Ihraam (Tahallul), hivyo imekuwa ni waajib ili iwe ni kitenganishi kati ya kuvua Ihraam na kuwa ndani ya Ihraam.
Sehemu Vilipo Viguzo Vinavyotupiwa Vijiwe Na Idadi Yake
Viguzo vinavyotupiwa vijiwe ni vitatu:
1- Jamarat Al-‘Aqabah Al-Kubraa (Guzo Kuu). Hili ni la kwanza upande wa Makkah, na linakuwa upande wa kushoto kwa anayeingia Minaa.
2- Al-Jamarat Al-Wustwaa (la kati). Linafuatia baada ya Jamarat Al-‘Aqabah upande wa Muzdalifah.
3- Al-Jamarat As-Swughraa (dogo). Linafuatia baada ya Masjid Al-Khayf Minaa.
Ukubwa wa vijiwe
Imestahabiwa ukubwa wa vijiwe vya kutupia uwe mfano wa kijiwe kinachorushwa kwa kidole (au manati), yaani ukubwa wa punje kubwa ya haragwe. Baadhi wamesema ni kubwa kuliko njegere (chickpeas) na chini ya hazeli (hazelnut).
Katika Hadiyth ya Jaabir: ((..Kisha akapita njia ya kati inayotokezea kwenye Al-Jamarat Al-Kubraa [Guzo kuu] mbele ya mti, akalitupia kwa vijiwe saba, analeta Takbiyr kwa kila kijiwe anachotupa mithili ya kijiwe cha kukivurumisha kwa kidole…)).
Na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliamuru aokotewe vijiwe vya kutupia, akaokotewa vijiwe saba vya ukubwa wa kuvurumisha kwa kidole, na akaanza kuvipangusa vumbi kwenye kiganja chake, na akasema:
((بأمثال هؤلاء فارموا، وإياكم والغلو في الدين، فإنما أهلك من كان قبلكم الغلو في الدين))
((Kwa mithili ya [ukubwa wa] hivi tupieni, na nawatahadharisheni na uchupaji mipaka na kufanya ifraatw katika Diyn, kwani uchupaji na ifraatw katika Diyn uliwaangamiza waliopita kabla yenu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (5/268), Ibn Maajah (3029) na Ahmad (1/215, 347)]
Sijui tuseme nini kwa wayafanyayo baadhi ya wajinga wanaotupia Jamaraat kwa viatu. Tunamwomba Allaah Ayatengeneze mambo ya Waislamu na Awaeleweshe Sunnah Tukufu ya Nabiy wao.
Ni wapi vijiwe huokotwa?
Hujaji anaweza kuokota vijiwe sehemu yoyote aitakayo, kwa kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakuainisha mahala maalumu pa kuokotea kama ilivyo katika Hadiyth iliyotangulia ya Ibn ‘Abbaas. Hii pia ni kauli ya Ahmad na ‘Atwaa, na imekhitariwa na Ibn Al-Mundhir na Ibn Taymiyah (Allaah Awarehemu).
Ash-Shaafi’iy amependelea Hujaji avichukue toka Muzdalifah. [Al-Majmuw’u (8/155)].
Hili limesimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar na Sa’iyd bin Jubayr.
Ninasema: “Lakini uzito bila shaka haufichiki, na jambo lina wasaa”.
Je, inajuzu kutumia vijiwe zaidi ya mara moja?
Jumhuri wanasema inajuzu kutumia vijiwe ambavyo ameshavitupia mwanzo lakini pamoja na ukaraha. Ibn Hazm amesema inajuzu bila ukaraha. Amesema (Rahimahul Laah) katika Al-Mughniy (7/288): “Ama kutupia kwake kwa vijiwe ambavyo ameshavitupia, hilo halikukatazwa na Qur-aan wala Sunnah”.
Na hii pia ni kauli ya Abu Haniyfah na Maswahibu wake.
Na ikisemwa kuwa imesimuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas akisema: ((Kuwa vijiwe vya kutupia viguzo vilivyotaqabaliwa kati yake huondoshwa [na Malaika], na ambavyo havikutaqabaliwa kati yake huachwa, na kama si hivyo, vingekuwa mlima wa kuziba njia))… Tunasema: “Na’am. Ikiwa utupaji wa vijiwe hivi wa mtu fulani haukutaqabaliwa na wa mwingine umetaqabaliwa, ni sawa na mtu aliyetoa swadaqah kitu fulani na Allaah Asimtaqabalie, kisha kitu kile kile akimiliki mtu mwingine akitolee swadaqah na Allaah Amtaqabalie”.
Vijiwe havioshwi
Ash-Shaafi’iy (Rahimahul Laah) amestahabisha kuviosha vijiwe vya kutupia Jamaraat, lakini hakuna dalili juu ya hilo. Ibn Al-Mundhir kasema: “Hakuna Hadiyth yoyote inayojulikana kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliviosha au kuamuru vioshwe, na hakuna faida yoyote kuviosha”.
Pia ‘Atwaa, Ath-Thawriy, Maalik na ‘Ulamaa wengi wanasema havioshwi.
Ash-Shaafi’iy amesema: “Tumesimuliwa toka kwa Twaawuws kuwa alikuwa anaviosha”.
Ninasema: “Linaloonekana ni kuwa hakuna usharia wa kuviosha. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Kutupia juu ya kipando
Inajuzu Hujaji kutupia viguzo akiwa juu ya kipando (mnyama, gari, pikipiki n.k). Ni kwa Hadiyth ya Qudaamah bin ‘Abdullaah amesema: ((Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akitupia Jamaratul ‘Aqabah Yawm An-Nahr [tarehe 10] juu ya ngamia wake mwekundu aliyechanganya weupe, hapigwi mtu [aliye mbele yake], wala hafukuzwi, wala haambiwi kaa kando, kaa kando)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (5/270), At-Tirmidhiy (903) na Ibn Maajah (3035)]
Wakati wa kutupia na idadi yake
Siku za kutupia ni nne.
Yawm An-Nahr (Tarehe 10 Dhul Hijjah), na masiku matatu yanayofuatia ambayo huitwa Masiku ya At-Tashriyq (11, 12 na 13 Dhul Hijjah).
Katika Yawm An-Nahr, Hujaji atatupia vijiwe saba kwenye Jamarat Al-‘Aqabah Al-Kubraa (Guzo kuu) peke yake.
Na katika Masiku Matatu ya At-Tashriyq, atatupia kwa mpangilio kwa kila siku Al-Jamarat As-Swughraa (Guzo dogo), kisha guzo la kati na kisha guzo kuu Jamarat Al-‘Aqabah. Kila guzo atatupia vijiwe saba. Hivyo idadi jumla ya vijiwe atakavyovitupia itakuwa ni 70; vijiwe saba Yawm An-Nahr, na 21 katika kila siku ya Masiku ya At-Tashriyq [7 + (21 × 3) = 70].
Ikiwa Hujaji ataharakia kuondoka (atafanya “Ta’ajjul”) kwa kutoweza kungojea hadi tarehe 13 –na hili anaruhusiwa- basi idadi ya vijiwe kwake itakuwa ni 49 [7 + (21×2) = 49].
1- Kutupia Yawm An-Nahr
Tushasema nyuma kuwa ni waajib kutupia Jamaratul ‘Aqabah tu Yawm An-Nahr kwa vijiwe saba. Lakini, ni kutokea wapi hutupiwa vijiwe?
Imesuniwa Hujaji atupie kutoka katikati ya Bonde (Batwn Al-Waadiy) ambapo Makkah inakuwa kushotoni kwake na Minaa kuliani mwake kama ataweza kufanya hivyo. Ni kwa kitendo cha Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kama ilivyoeleza Hadiyth ya Jaabir, na kwa Hadiyth ya Ibn Mas’uwd isemayo: ((Kwamba yeye alipotupia Jamaratul ‘Aqabah aliingia ndani ya bonde, na alipokuwa sambamba na mti, alisimama mbele yake, akatupia vijiwe saba, na kwa kila kijiwe akaleta Takbiyr, kisha akasema: Kutokea hapa –Naapa kwa Yule Ambaye hapana mola isipokuwa Yeye tu- alisimama ambaye aliteremshiwa Suwrat Al-Baqarah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1750) na Muslim (1296)]
Na kama haikuwa wepesi –na hususan katika zama zetu za sasa- basi hapana ubaya atupie toka mahala popote anapoweza.
Wakati wa kutupia
Toka kwa Jaabir (Radhwiya Allaah ‘anhu) amesema: ((Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akitupia Yawm An-Nahr wakati wa Dhuhaa, na ama baada ya hapo ni baada ya kupinduka jua)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy ikiwa Mu’allaq Majzuwman (3/677) na Muslim (1299).
Kwa hiyo Sunnah, asitupie Jamararul ‘Aqabah Yawm An-Nahr [tarehe 10] ila baada ya kuchomoza jua. Na hili si waajib kwa Jumhuri ya ‘Ulamaa.
Ama yaliyosimuliwa toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alitutanguliza mabarobaro wa Baniy Al-Muttwalib usiku wa Muzdalifah juu ya punda akawa anatupiga piga migongo yetu akituambia:
((أبني لا ترموا الجمرة حتى تطلع الشمس))
((Enyi wanangu! Msitupie vijiwe mpaka jua lichomoze)), Hadiyth hii ni Dhwa’iyf. [Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1940), An-Nasaaiy (5/271) na Ibn Maajah (3025). Ina Asaaniyd ambazo zina walakin. Al-Haafidh amesema ni Swahiyh katika Al-Fat-h (3/528) kwa Asaaniyd zake, na pia Al-Albaaniy katika kitabu cha Hijjatun Nabiy uk. 80.]
Kwani, ikiwa atachelewesha kutupia mpaka muda wa kabla ya kuchwa jua, basi inajuzu ingawa hilo kwa mujibu wa Ijma’a ya ‘Ulamaa halikustahabiwa. [At-Tamhiyd cha Ibn ‘Abdil Barr (17/255)]
Kama itamwia mtu uzito kutupia kabla jua kuchwa, basi anaruhusiwa kutupia japokuwa usiku. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anaulizwa [maswali] Yawm An-Nahr. Mtu mmoja akamuuliza akisema: Nimetupia baada ya kuingiliwa na jioni. Akamwambia: ((Hakuna ubaya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1735) na wengineo]
Kwa Fuqahaa wa Kimaalik na Kihanafiy, wakati wa kutupia huanza tokea kuchomoza Alfajiri ya Yawm An-Nahr. Ama wa Kishaafi’iy na Kihanbali, huanzia usiku wa manane wa kuamkia Yawm An-Nahr kwa aliyesimama ‘Arafah kabla yake.
Na wakati wa mwisho wa kutupia Jamaratul ‘Aqabah kwa Mahanafiy, ni mpaka Alfajiri ya siku ya pili (tarehe 11), kwa Wamaalik mpaka Magharibi. Wote wawili wamewajibisha kuchinja mnyama kwa kuchelewesha utupiaji nje ya wakati wake.
Ama Mashaaf’iy na Mahanbali, wakati wa mwisho wa kutupia kwao ni Siku ya mwisho ya Tashriyq.
Ni wakati gani madhaifu walioondoka Muzdalifah kabla ya Alfajiri wanatupia?
Hakuna makhitalifiano yoyote kuwa lililostahabiwa kwa wanawake madhaifu na wengineo, ni kutupia baada ya jua kuchomoza ili kumuiga Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Ama kutupia kabla jua kuchomoza, hili Ash-Shaafi’iy kalijuzisha walau kabla ya Alfajiri, na Jumhuri wamelijuzisha baada ya Alfajiri hadi kuchomoza jua.
Sheikh wetu amesema: [Jaami’u Ahkaamin Nisaa cha Sheikh wetu Mustwafaa bin ‘Adawiy (2/563) kwa mabadilisho kidogo)]:
“Ninaloona mimi kuhusiana hasa na wanawake ni kuwa wanaweza kutupia wanapowasili Minaa. Kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliwaruhusu kuondoka usiku. [Hadiyth kuhusu hili zimetajwa nyuma katika kipengele cha kulala Muzdalifah, nazo ni Swahiyh]. Na Asmaa (Radhwiya Allaah ‘anhaa alitupia kabla ya Swalaat As-Subh (kama ilivyoelezwa nyuma). Na nyuma Hadiyth ya Saalim imeeleza: ((Baadhi yao wapo wanaokuja Minaa kwa Swalaah ya Alfajiri, na wengine wanakuja baada ya hapo. Na wanapofika, hutupia Al-Jamarah. Na Ibn ‘Umar alikuwa anasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amewaruhusu hao hilo”. [Angalia nyuma]
Na’am, na hata kama Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas ni Swahiyh, basi katazo litakuwa ni kwa vijana wadogo na si wanawake. Au amri inaweza kuchukulika kama ni jambo manduwb katika kuoanisha dalili kama alivyosema Ibn Hajar katika Al Fat-h. Na Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Sunan Za Kutupia Viguzo Yawm An-Nahr
1- Kuacha Talbiyah kabla ya kuanza kutupia.
Ni kwa Hadiyth ya Al-Fadhwl bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaah ‘anhumaa): ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hakuacha kuleta Talbiyah mpaka alipofika Al-Jamarah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1670) na Muslim (1281)]
Jumhuri ya ‘Ulamaa wamelisema hili. [Fat-hul Baariy (3/623), Al-Majmuw’u (8/177), Nihaayatul Muhtaaj (3/303) na Al-Mubdi’u (3/340). Ama kwa upande wa Ibn Hazm katika Al-Muhallaa (7/180), Talbiyah hukatwa baada ya kumaliza kutupia]
2- Kuleta Takbiyr sambamba na kila kijiwe anachotupa.
Ni kwa yaliyomo kwenye Hadiyth ya Jaabir: ((..mpaka akafika kwenye Al-Jamarah [nguzo] iliyoko pembeni ya mti, akaitupia kwa vijiwe saba akileta Takbiyr kwa kila kijiwe kati yake..)).
3- Aitupie toka chini yake akiwa ndani ya bonde.
Hili limeelezwa nyuma kidogo.
4- Atupie baada ya jua kuchomoza.
Hili pia lishaelezwa.
5- Kuondoka baada ya kutupia bila kusimama. Ni kwa Hadiyth ya Jaabir: ((..alitupia toka ndani ya bonde kisha akaondoka kwenda mahala pa kuchinjia)). Asisimame mbele ya Jamaratul ‘Aqabah, si kwa kuomba du’aa wala kwa jingine lolote.
Al-Haafidh amesema kwenye Al Fat-h (3/679): “Jamaratul ‘Aqabah ina sifa nne mahususi kulinganisha na nguzo nyingine mbili: Ni peke yake inayotupiwa Yawm An-Nahr (tarehe 10), watu hawasimami mbele yake (baada ya kutupia), hutupiwa wakati wa Dhuhaa, na hutupiwa toka chini yake kama Sunnah”.
Amali zinazofanywa Yawm An-Nahr na mpangilio wake
‘Amali za kisharia kwa Hujaji katika Yawm An-Nahr baada ya kufika Minaa ni nne: Kutupia Jamaratul ‘Aqabah, kisha kuchinja, halafu kunyoa na mwisho kufanya Twawaaful Ifaadhwah. Mpangilio huu ni Sunnah na si Waajib. Na kama atatufu kabla ya kutupia, au akachinja wakati wa kuchinja kabla hajatupia, au akanyoa kabla ya kutupia na kutufu, basi inajuzu na hana fidia, lakini atakosa ubora. [Al-Majmuw’u (8/168)]
Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy, Jumhuri ya Salaf, ‘Ulamaa, na Fuqahaa Aswhaabil Hadiyth. [Fat-hul Baariy (3/668)]
Dalili ya hili ni Hadiyth ya Ibn ‘Abbaas: ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliulizwa kuhusu kuchinja, kunyoa na kutupia, na kutanguliza na kuchelewesha akasema: ((Hakuna ubaya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1734) na wengineo]
Na hii bila shaka ni kwa ajili ya kuondosha dhambi na fidia kwa pamoja, na hii ndio maana ya “Hakuna ubaya”.
Baadhi ya ‘Ulamaa kama Imaam Ahmad na wengineo wamesema kuwa ruksa ya kutopangilia ‘amali hizi inamhusu aliyesahau au asiyejua tu, na si kwa anayekusudia (kuvuruga utaratibu). [Al-Mughniy (3/447) na Fat-hul Baariy (3/668)]
Ni kwa Hadiyth ya ‘Abdullaah bin ‘Amri: ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alisimama katika Hijjah ya Kuaga na watu wakawa wanamuuliza. Mtu mmoja akasema: Sikuhisi [sikujua], nikanyoa kabla sijachinja. Akamwambia: Chinja na hakuna ubaya. Akaja mwingine akasema: Sikuhisi, nikachinja kabla sijatupia vijiwe. Akamwambia: Tupa na hakuna ubaya. Na hakuulizwa siku hiyo kuhusu jambo lolote lililotangulizwa au lililocheleweshwa isipokuwa alisema:
((افعل ولا حرج))
((Fanya na hakuna ubaya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1736, 1737) na Muslim (1306)]
Ibn Daqiyq amesema katika Sharhu ‘Umdatil Ahkaam (3/79): “Aliyoyasema Ahmad ni imara kwa upande kuwa dalili imehabarisha wajibu wa kumfuata Rasuli katika Hajj kwa neno lake:
خذوا عني مناسككم
((Jifunzeni kutoka kwangu Manaasik zenu)).
Na Hadiyth hizi zenye kuruhusu kutanguliza la kufanywa baadaye zimetanguliwa na kauli ya muulizaji “Sikuhisi” [Sikujua], hivyo hukmu hapa imehusishwa na hali ya kutokujua. Na kwa muktadha huo, hali ya kukusudia inabakia katika asili ya waajib wa kumfuata Rasuli kama alivyofanya katika Hajj. Kadhalika, hukmu ikifungamana na hali yenye uzito wa kuzingatiwa, haijuzu kuitupa hali hiyo kando. Na hakuna shaka kwamba kutokujua ni hali mwafaka ya kusameheka na kutoadhibiwa kwa kosa, nayo imefungamana na hukmu, hivyo haiwezekani kuiweka kando na kuifungamanisha na kukusudia”.
Ninasema: “Maneno haya yanakuwa katika kilele cha usahihi lau Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) angeishilia kusema “Hakuna ubaya” tu katika kumjibu muulizaji. Na aliposema: “Fanya na hakuna ubaya” na yakawa matamshi haya yanadulisha kuwa hakuna ubaya kwa siku zijazo, imejulikana kuwa hakuna tofauti kati ya aliyesahau, asiyejua, mwenye kukumbuka na mwenye kujua. Na hili likiwa kama hoja imara, linawafikiana na makusudio ya sharia na hususan katika zama zetu za leo. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”. [Al-‘Allaamah Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahul Laah) ameashiria hoja hii katika Al-Mumti’u (7/367)]
Tatizo linabakia katika kutanguliza kunyoa kabla ya kuchinja kutokana na Kauli Yake Ta’aalaa:
وَلَا تَحْلِقُوا رُءُوسَكُمْ حَتَّىٰ يَبْلُغَ الْهَدْيُ مَحِلَّهُ
((Na wala msinyoe vichwa vyenu mpaka mnyama afikie machinjoni pake)). [Al-Baqarah 196]
Hili limejibiwa kuwa muradi wa mnyama kufika machinjoni mwake ni kufika mahala ambapo ni halali kumchinja hapo, na hili lishafanyika. Na tatizo lingebakia lau Allaah Angesema: “Na msinyoe mpaka mchinje”.
Hivyo ni sahihi kuwa si wajibu kufuatanisha ingawa ni bora zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
27-Tahallul (Kujivua Ihraam) Ya Kwanza Na Ya Pili
Alhidaaya.com [3]
Hajj ina tahallul mbili; ya kwanza na ya pili, nazo zinafungamana na kutupia Jamaratul ‘Aqabah, kunyoa na Twawaaful Ifaadhwah. ‘Ulamaa wamekhitalifiana kuhusu je tahallul ya kwanza inapatikana kwa kutupia hata kama hakunyoa, au kutupia pamoja na kunyoa?
Asli ya hili ni Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Nilimtia manukato Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa mikono yangu hii miwili wakati alipohirimia, na kwa kuvua kwake Ihraam (tahallul) wakati alipovua Ihraam kabla hajatufu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1754) na Muslim (1189)]
Na ‘Aaishah hakuongozana naye wakati Rasuli alipoteremka toka Muzdalifah. Na imethibiti kiuhakika kuwa aliendelea kumpanda mnyama wake mpaka alipotupia Jamaratul ‘Aqabah, na hii inaonyesha kuwa ‘Aaishah alimtia manukato Rasuli baada ya kutupia. Lakini je, kumtia manukato kulikuwa kabla ya kunyoa au baada ya kunyoa?
Baadhi ya ‘Ulamaa wamesema: [Ash-Sharhul Mumti’u]
“Lau ingekuwa anavua Ihraam kwa kutupia tu, basi angelisema: “Na kwa kuvua kwake Ihraam kabla hajanyoa”. Yeye ameiweka tahallul baina ya Twawaaf na vitendo vya kabla yake ambavyo ni kutupia, kuchinja na kunyoa, na hususan Rasuli (Swallah Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((إن معي الهدي فلا أحل حتى أنحر))
((Hakika mimi nina mnyama wa kuchinja, sivui Ihraam mpaka nichinje)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1566) na Muslim (1229)
Kuna Hadiyth nyingineyo isemayo:
((إذا رميتم وحلقتم فقد حل كل شيء إلا النساء))
((Mkitupia na mkanyoa, basi kila kitu kimehalalika isipokuwa wanawake))…lakini Hadiyth hii si Swahiyh. [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na At-Twahaawiy (1/419), Al-Bayhaqiy (5/136) na Ahmad (6/143)]
Na wengine wamesema: Hujaji akitupia Jamaratul ‘Aqabah, kila kitu kinakuwa halali kwake isipokuwa wanawake hata kama hakunyoa. Wametoa dalili kwa riwaya ya Hadiyth iliyotangulia ya ‘Aaishah kwa tamko: ((Nilimtia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) manukato ya dhariyrah katika Hijjah ya Kuaga kwa mkono wangu kwa kuvua Ihraam na kuhirimia, wakati alipohirimia, na wakati alipotupia Jamaratul ‘Aqabah Yawm An-Nahr, kabla hajatufu Nyumba)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ahmad (6/200)]
Na kwa Hadiyth:
((إذا رميتم الجمرة فقد حل لكم كل شيء إلا النساء))
((Mkitupia Jamarah, basi kila kitu ni halali kwenu isipokuwa wanawake))..bila ziada ya ((وحلقتم)) na ((mkanyoa)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Angalia Al-Irwaa (4/236) na Asw-Swahiyhah (239)]
Haya ni madhehebu ya ‘Atwaa, Maalik, Abu Thawr na Abu Yuwsuf na riwaya toka kwa Ahmad. Ni chaguo la Ibn Qudaamah na mwelekeo wa Ibn Hazm ambaye pamoja na yote kasema: “Ni halali kwake hayo kwa kuingia tu wakati wa kutupia hata kama hakutupia”. [Al-Mughniy (3/439), Al-Muhallaa (7/139) na Hijjatun Nabiyy (uk. 81)]
Naye Ash-Shaafi’iy amesema kwamba tahallul ya kwanza inapatikana kwa mambo mawili kati ya matatu: Kutupia, kunyoa na kutufu, na tahallul ya pili inapatikana kwa la tatu (kutufu). [Al-Majmuw’u (8/205) na Fat-hul Baariy (3/684)]
Ama tahallul ya pili, hii hupatikana baada ya Twawaaful Ifaadhwah. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar: ((..kisha hakufanya [yaani Nabiy Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) jambo lolote marufuku kwake mpaka akamaliza Hajj yake, akachinja mnyama wake Yawm An-Nahr na akafanya Twawaaful Ifaadhwah kwenye Nyumba. Kisha akafanya kila kitu kilichozuiwa kwake….)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1227) na wengineo]
2- Kutupia Siku Ya Kwanza Na Ya Pili Ya Masiku Ya Tashriyq
Ni lazima katika siku hizi mbili za tarehe (11 na 12 Dhul Hijja) kutupia nguzo tatu kimpangilio; kwanza Al-Jamarat As-Sughraa (nguzo ndogo), kisha ya kati, na hatimaye Jamaratul Aqabah (nguzo kuu). Kila nguzo ataitupia vijiwe saba.
Wakati wa kutupia
Wakati wa kutupia katika siku hizi mbili unaanzia baada ya kupinduka jua, na haijuzu kabla yake kwa mujibu wa msimamo wa Jumhuri ya ‘Ulamaa. [Al-Mabsuwtw (4/23), Al-Muwattwa (1/409), Al-Furuw’u (3/518) na Al-Majmuw’u (8/211)]
Dalili ni:
1- Hadiyth ya Jaabir: ((Nilimwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) anatupia Yawm An-Nahr [wakati wa] Dhuhaa. Ama baada ya hapo, ni baada ya kupinduka jua)).
Na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((خذوا عني مناسككم))
((Jifunzeni kutoka kwangu matendo yenu ya Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma]
2- Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akisubiria jua lipinduke ili atupie. Toka kwa Wabrah: ((Nilimuuliza Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhu): Wakati gani nitupie vijiwe? Akasema: Akitupia kiongozi wako [wa Hajj] na wewe hapo tupia. Nikamuuliza tena swali hilo hilo. Akasema: Tulikuwa tunasubiria, na jua linapopinduka tunatupia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1746)]
Na lau ingejuzu kabla jua kupinduka, basi Rasuli angefanya angalau mara moja ili kuonyesha kuwa inajuzu.
3- Lau kutupia kungekuwa kunajuzu kabla jua kupinduka, basi Rasuli angefanya kwa kuwa kufanya hivyo, ni kuileta ‘ibaadah mwanzoni mwa wakati wake, ni kuwawepesishia watu ‘ibaadah na kuwarefushia wakati. [Ash-Sharhul Mumti’u (7/384)]
Wakati uliosuniwa unaanza tokea kupinduka jua mpaka kuchwa. Ikiwa itakuwa uzito kutupia kabla ya Magharibi, basi hapana ubaya kutupia usiku kama tulivyoeleza nyuma kuhusu kutupia Yawm An-Nahr.
Ama mwisho wa kutupia, madhehebu ya ‘Ulamaa ni mfano wa yale yale tuliyoyagusia katika kutupia Yawm An-Nahr.
Picha ya utupiaji katika siku mbili
Toka kwa Saalim kwamba Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa): ((Alikuwa anatupia Jamrat Ad-Dunyaa [iliyo karibu na Msikiti wa Khayf] kwa vijiwe saba na huleta Takbiyr kwa kila kijiwe, kisha husogea mbele mpaka akafika ndani ya bonde, halafu huelekea Qiblah kwa muda mrefu akiomba huku akinyanyua mikono yake miwili. Kisha hutupia Jamarat la kati halafu huelekea upande wa kushoto ndani ya bonde. Halafu hutupia Jamaratul ‘Aqabah tokea ndani ya bonde na wala hasimami mbele yake, na husema: Hivi ndivyo nilivyomwona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akifanya)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1751)]
An-Nafrul Awwal
Hujaji akitupia vijiwe siku ya kwanza na ya pili ya Tashriyq, basi anaruhusika kwenda Makkah kama atapenda kuharakia kuondoka toka Minaa (Ta’ajjul). Siku hii huitwa Yawmu An-Nafril Awwal (Siku ya mguro wa kwanza kwenda Makkah). Na kwa mguro huu, kutupia siku ya tatu ya Tashriyq kutakuwa hakuko tena kwa makubaliano ya ‘Ulamaa wote. Na hii ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَمَن تَعَجَّلَ فِي يَوْمَيْنِ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ وَمَن تَأَخَّرَ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ ۚ لِمَنِ اتَّقَىٰ))
((Atakayeharakisha kuondoka katika siku mbili, basi hakuna dhambi juu yake; na atakayetaakhari basi hakuna dhambi juu yake; kwa mwenye kuwa na taqwa)). [Al-Baqarah (2:203)]
Katika madhehebu ya Jumhuri, Hujaji anatakiwa agure au aondoke (mguro wa kwanza) kabla jua kuchwa siku ya pili ya Masiku ya Tashriyq (tarehe 12). Na Mahanafiy wanasema anaweza kuondoka siku ya tatu ya Tashriyq kabla Alfajiri haijawadia.
3- Kutupia Siku Ya Tatu Ya Tashriyq
Ni waajib kutupia Jamaraat tatu katika siku hii kwa aliyebakia Minaa na hakugura kwenda Makkah (katika Mguro wa kwanza) baada ya jua kupinduka kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri. Lakini Abu Haniyfah amesema inajuzu kutupia kabla jua kupinduka baada ya Alfajiri, na Hadiyth ya Jaabir inamjibu.
Na wamekubaliana kuwa wakati wa mwisho wa kutupia katika siku hii ni kuchwa jua, na kwamba wakati wa kutupia ili kulipia siku zilizotangulia unamalizikia pia kwa kuchwa jua la siku ya tatu ya Tashriyq, kwa kuwa wakati wa Manaasik unatoka kwa kuchwa jua.
An-Nafru Ath-Thaaniy
Hujaji akitupia Jamaraat tatu katika siku ya tatu ya Tashriyq, -nayo ni siku ya nne ya masiku ya kuchinja- ataondoka Minaa kwenda Makkah. Hatakiwi akae Minaa baada ya kutupia. Na hii huitwa Yawmu An Nafri Ath-Thaaniy (Siku ya mguro wa pili).
Kutupiwa vijiwe na mtu mwingine
Aliyeshindwa kutupia mwenyewe kutokana na ugonjwa, au kuzuiliwa na mfano wake, basi atamwomba mtu mwingine amtupilie, kwa kuwa wakati wake ni mfinyu. Na huyu atakayemtupilia ni lazima awe kwanza ameshajitupilia mwenyewe.
Na haiswihi kuwatupia wanawake wenye nguvu zao na uwezo wa kutupa wala watoto. Ama Hadiyth ya Jaabir isemayo: ((Tulihiji pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) tukiwa pamoja na wanawake na watoto, nasi tukawatupilia))…Hadiyth hii ni Dhwa’iyf [Imekharijiwa na Ahmad (3/314), na mfanowe kwa At-Tirmidhiy (927), Ibn Maajah (3038) na Al-Bayhaqiy (5/256)]
Kulala Minaa Masiku ya Tashriyq Ni Waajib
Ni waajib kulala Minaa nyusiku za siku tatu za Tashriyq (au nyusiku mbili za tarehe 11 na 12) kwa anayeta’ajjal (anayeharakia) kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri ya ‘Ulamaa. Wanasema ni lazima kuchinja mnyama kwa atakayeondoka huko bila udhuru kutokana na Hadiyth ya Ibn ‘Umar: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimruhusu ‘Abbaas alale Makkah siku za [kukaa] Minaa kwa ajili ya hodhi lake la kunyweshea maji [Mahujaji])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1745) na Muslim (1315)]
Hadiyth hii ni dalili kuwa ni waajib kulala Minaa, na kulala ni katika Manaasik za Hajj. Kwa kuwa kutolewa ruksa kunahukumia mkabala wake ambao ni zuio, na ruksa imetolewa kwa udhuru uliotajwa. [Al-Mughniy (3/449), Al-Furuw’u (3/518) na Ash-Sharhul Mumti’u]
Mahanafiy wamesema ni Sunnah. Ni kauli pia ya Ash-Shaafi’iy na riwaya toka kwa Ahmad. [Al-Hidaayah (2/2/186) na Al-Inswaaf (3/47)]
Kauli ya kwanza ya Jumhuri kuwa ni waajib ndio sahihi zaidi. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
28-Al-Hady Wanyama Wa Kuchinja
الهدي
Alhidaaya.com [3]
"الهدي" Ni kinachopelekwa Al-Haram kati ya wanyama na vinginevyo. Na muradi hapa ni wanyama maalum wanaopelekwa Al-Haram kwa ajili ya kujikurubisha kwa Allaah. Allaah Amesema:
((وَالْبُدْنَ جَعَلْنَاهَا لَكُم مِّن شَعَائِرِ اللَّـهِ لَكُمْ فِيهَا خَيْرٌ))
((Na ngamia na ng’ombe Tumekufanyieni kuwa ni miongoni mwa Ishara za Allaah; kwa hao mnapata khayr nyingi)). [Al-Hajj (22:36)]
Amesema tena:
((لَن يَنَالَ اللَّـهَ لُحُومُهَا وَلَا دِمَاؤُهَا وَلَـٰكِن يَنَالُهُ التَّقْوَىٰ مِنكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ ۗ وَبَشِّرِ الْمُحْسِنِينَ))
((Haimfikii Allaah nyama zake wala damu yake, lakini inamfikia taqwa kutoka kwenu. Hivyo ndivyo Älivyowatiisha kwenu ili mpate kumtukuza Allaah; “Allaahu Akbar, kwa yale Aliyokuongozeni; na wabashirie wafanyao ihsaan)). [Al-Hajj (22:37)]
Aina ya wanyama
‘Ulamaa wamekubaliana wote kuwa mnyama wa kuchinjwa ni lazima awe katika zile jozi nane Alizoziainisha Allaah Subhaanah (katika Aayah ya 143 ya Suwrat Al- An’aam), na mnyama bora kabisa ni ngamia, kisha ng’ombe, halafu kondoo na mbuzi. [Bidaayatul Mujtahid (2/559) na Al-Majmuw’u (8/368)]
Na kila mnyama anavyokuwa ghali, basi inakuwa ni bora zaidi, kwani Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipoulizwa kuhusu watumwa: Ni yupi bora zaidi [kwa kuachwa huru?] alisema:
((أغلاها ثمنا، وأنفسها عند أهلها))
((Ni mwenye bei ghali zaidi, na mwenye kuthaminiwa zaidi na watu wake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (2515), Muslim (136) na wengineo]
Yaliyoshurutishwa kwa mnyama wa kuchinjwa
1- Awe ni katika "بهيمة الأنعام"
[wanyama wa mifugo] ambao ni ngamia, ng’ombe, mbuzi na kondoo.
2- Kondoo awe amekomaa vizuri kwa kutimiza mwaka mmoja na zaidi, wa chini ya hapo hatoshelezi. Ngamia wa chini ya miaka mitano hatoshelezi, wala ng’ombe wa chini ya miaka miwili, wala mbuzi wa chini ya mwaka.
Toka kwa Jaabir kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((لا تذبحوا إلا مسنة، إلا أن تعسر عليكم فتذبحوا جذعة من الضأن))
((Msichinje isipokuwa Musinnah [ngamia aliyetimiza miaka mitano au ng’ombe aliyetimiza miaka mitatu], ila kama itakuwa vigumu kwenu, hapo mtachinja kondoo aliyetimiza mwaka)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslmi (1963), Abu Daawuwd (2797), An-Nasaaiy (7/218) na Ibn Maajah (3141)]
Na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwambia Abu Burdah kuhusiana na mbuzi mwenye miezi sita:
((تجزئ عنك، ولا تجزئ عن أحد بعدك))
((Anakutosheleza wewe [tu], na hamtoshelezi mwingine yeyote baada yako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5556) na Muslim (1961)]
3- Asiwe na kasoro yoyote kutokana na neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((أربع لا تجزئ في الأضاحي: العوراء البين عورها، والمريضة البين مرضها، والعرجاء البين ظلعها والكسيرة التي لا تنقي))
((Wanne hawafai katika wanyama wa kudhwahi: Mwenye chongo linaloonekana bayana, mwenye ugonjwa wa dhahiri, kiwete asiyeweza kutembea, na dhaifu [gofu] asiye na mifupa imara)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (2785), At-Tirmidhiy (1530), An-Nasaaiy (7/214) na Ibn Maajah (3144)]
Kasoro za wanyama zinaweza kugawanywa vigawanyo vitatu: [Ash-Sharhul Mumti’u ‘Alaa Zaadil Mustanqa’i (7/467-477)]
(a) Ziwe kasoro nne zilizoainishwa kwenye Hadiyth iliyotangulia. Kasoro hizi zinabatilisha utoshelezo.
(b) Ziwe zimetangaziwa katazo lakini zinaweza kutosheleza. Na hawa ni wanyama wenye kasoro kwenye masikio yao, pembe zao na mfano wa hivyo. Ni kama Hadiyth ya ‘Aliyy bin Abiy Twaalib:
((أَمَرَنَا رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم أَنْ نَسْتَشْرِفَ الْعَيْنَ وَالْأُذُنَ، وألا نُضَحِّي بِمُقَابَلَةٍ، ولا مُدَابَرَةٍ، ولا خَرْقَاءَ))
((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ametuamuru tukague macho na masikio [tunaponunua wanyama], na tusidhwahi aliyekatwa sikio kwa mbele likaachwa likining’inia, wala aliyekatwa sikio kwa nyuma, wala aliyepasuliwa sikio kwa urefu, wala aliyetobolewa sikio)). [Hadiyth Hasan. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (2804), At-Tirmidhiy (1543), An-Nasaaiy (7/217) na Ibn Maajah (3142)]
Wanyama wenye kasoro hizi ni makruhu kudhwahi lakini wanakidhi lengo.
(c) Ziwe kasoro ambazo hazikukatazwa lakini zinaharibu kidogo ukamilifu wa mnyama. Hizi hazina athari, lakini ni makruhu, na si haramu. Ni kama aliyevunjika meno na mfano wa hivyo. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Wanyama ni wa aina mbili
‘Ulamaa wamekubaliana wote kuwa mnyama anayeswagwa kwenye ‘ibaadah hii, yuko wa Waajib na yuko wa Sunnah.
1- Wa Waajib
Hawa wako katika vigawanyo vifuatavyo:
(a) Mnyama wa Tamattu’u na Qiraan. Huyu ni yule aliye waajib kwa Hujaji aliyefanya ‘Umrah kwanza kisha Hajj (Tamattu’u), au aliyefanya Hajj na ‘Umrah kwa pamoja (Qiraan). Na hii ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ ۚ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ))
((Basi mwenye kufanya Tamattu’u kwa kutekeleza ‘Umrah kwanza kisha Hajj, achinje mnyama aliye mwepesi. Na asiyepata afunge Swiyaam siku tatu katika Hajj na saba mtakaporejea)). [Al-Baqarah (2:196)]
Mnyama huyu ni waajib kwa mwenye kufanya Tamattu’u kwa Ijma’a, na kwa mwenye kufanya Qiraan kwa kauli ya Jumhuri.
(b) Mnyama wa fidia. Huyu ni yule aliye waajib kwa Hujaji akinyoa nywele zake kutokana na ugonjwa au wadudu wanaomsumbua. Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ بِهِ أَذًى مِّن رَّأْسِهِ فَفِدْيَةٌ مِّن صِيَامٍ أَوْ صَدَقَةٍ أَوْ نُسُكٍ))
((Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au ana vya kumuudhi kichwani mwake (ikambidi anyoe); basi atoe fidia kwa kufunga Swiyaam au kutoa swadaqah au kuchinja mnyama)). [Al-Baqarah (2:196)]
Hujaji huyu atakhiyarishwa baina ya kuchinja, au kulisha, au kufunga kama ilivyotangulia.
Jumhuri wameunganisha aina hii kuwajibisha kuchinja kwa mwenye kuacha waajib katika waajibaat za Hajj, na kwa mwenye kufanya katazo lolote kati ya makatazo ya Ihraam.
(c) Mnyama wa malipo. Ni yule ambaye ni waajib kwa Muhrim aliyeua mnyama wa kuwindwa wa nchi kavu, na hili lishaelezwa nyuma. Wamelifanyia hili Qiyaas kuchinja kwa mwenye kufanya marufuku yoyote kati ya marufuku katika Al-Haram kama kukata mti na mfano wake.
(d) Mnyama wa kuzuilika. Ni yule aliye waajib kwa aliyezuilika asiweze kukamilisha ‘amali za Hajj kutokana na ugonjwa au adui au mfano wa hayo, na hakuwa ameweka shuruti wakati wa kuhirimia –kama tulivyoeleza nyuma- kutokana na Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((Na kama mkizuilika basi chinjeni wanyama walio wepesi kupatikana)). [Al-Baqarah (2:196)]
(e) Mnyama wa kumwingilia mke. Ni yule aliye waajib kwa Hujaji anapomwingilia mkewe wakati wa Hajj. Na hili lishaelezwa nyuma.
(f) Mnyama wa nadhiri. Huyu ni waajib kwa aliyemwekea nadhiri.
2- Wa Kujitolea
Ni yule ambaye Hujaji mwenye kufanya Ifraad anajitolea tu (kama swadaqah) zaidi ya mnyama wa waajib.
Kumpeleka mnyama Haram kwa asiyetaka kwenda mwenyewe
Atakayekuwa kwenye mji wake na hakutaka kwenda Haram, basi imestahabiwa ampe mtu mwingine mnyama huyo ampelekee huko. Imestahabiwa pia amvishe vigwe na amtie alama kama tutakavyokuja kuona mbeleni. Na akimpeleka, hawi kwa kufanya hivyo Muhrim, na wala hakatazwi kufanya lolote katika mambo yaliyokatazwa kwa Muhrim. Hii ni kauli ya Jumhuri.
Toka kwa ‘Aaishah amesema:
((فَتَلْتُ قَلائِدَ بدن رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بيدي ثُمَّ أَشْعَرْتُهَا وَقَلَّدَهَا - أَوْ قَلَّدْتُهَا - ثُمَّ بَعَثَ بِهَا إلَى الْبَيْتِ . وَأَقَامَ بِالْمَدِينَةِ , فَمَا حَرُمَ عَلَيْهِ شَيْءٌ كَانَ لَهُ حِلاُّ))
((Nilivisuka vigwe vya ngamia wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwa mikono yangu miwili, kisha nikamtia alama na yeye akamvisha vigwe –au nilimvisha mimi vigwe- halafu akamtuma [mtu pamoja naye) kumpeleka kwenye Nyumba, naye akakaa Madiynah, na halikuwa katazo kwake jambo lolote lililokuwa ni halali)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1696) na Muslim (1321)]
Ni wanyama wangapi wanatosheleza?
Hakuna mpaka maalum wa wingi wa wanyama wa kuchinja. Wanyama aliochinja Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) walikuwa ni mia moja. Toka kwa ‘Aliyy: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alichinja ngamia mia..)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1718)]
Idadi ya chini kabisa inayomtosha mtu mmoja ni mbuzi mmoja. Toka kwa Abu Ayuuwb Al-Answaariyy: ((Mtu katika enzi ya Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa anajichinjia mbuzi mwenyewe na kwa watu wa nyumba yake, wanakula na wanalisha. Kisha watu wakajifaharisha, na wakawa kama unavyoona)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (1541) na Ibn Maajah. Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh]
Na katika Hadiyth ya ‘Aaishah, ni kuwa: ((Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimchukua kondoo dume akamlaza chini, kisha akasema:
((اللهم تقبل من محمد وآل محمد))
((Ee Allaah! Taqabal kutoka kwa Muhammad na ukoo wa Muhammad)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1967)]
Na hii ni kwa mnyama wa kudhwahi.
‘Ulamaa wote wamekubaliana kuwa kondoo mmoja hatoshelezi isipokuwa kwa mtu mmoja tu, tofauti na yaliyosimuliwa toka kwa Maalik kuwa anatosheleza ikiwa mtu atajichinjia mwenyewe na watu wa nyumba yake, lakini si kwa ushirika, bali akimnunua peke yake. [Bidaayatul Mujtahid (1/655)]
Watu saba wakishirikiana ngamia au ng’ombe mmoja itawatosheleza. Hii ni kauli mashuhuri ya Ash-Shaafi’iy toka kwa Ahmad. Ni kwa Hadiyth ya Jaabir aliyesema: ((Tulichinja pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) Mwaka wa Al-Hudaybiyyah ngamia jike kwa watu saba, na ng’ombe kwa watu saba)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1318)].
Na toka kwa Jaabir tena: ((Tulitoka pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) tukihirimia Hajj…na akatuamuru tushirikiane katika ngamia na ng’ombe, kila watu saba kati yetu ngamia mmoja)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1318)]
Ibn Rushd amenukuu Ijma’a ya kuwa haijuzu kushirikiana watu zaidi ya saba katika kuchinja mnyama. [Bidaayatul Mujtahid (1/656]
Ninasema: “Bali Is-Haaq ameelekea kusema kuwa ngamia mmoja na ng’ombe mmoja wanatosheleza watu kumi. Katika Hadiyth ya ‘Aaishah: ((..tulipokuwa Minaa, nililetewa nyama ya ng’ombe, nikasema: Hii ya nini? Wakasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amechinja ng’ombe kwa niaba ya wakeze)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1623) na Muslim (1211)]
Na wakeze ni tisa.
Na imeelezewa katika baadhi ya riwaya kuwa alikuwa ng’ombe mmoja baina yao. [Hadiyth Mursal. Imekharijiwa na Maalik (2/486-487]
Na imethibiti kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aligawa ghanima (ngawira) na akamlinganisha ngamia mmoja sawa na mbuzi kumi. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (2507), Muslim (1968) na wengineo]
Toka kwa Ibn ‘Abbaas: ((Tulikuwa pamoja na Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) katika safari, ikawadia [siku ya] Adhwhaa, tukashirikiana watu kumi ngamia, na watu saba ng’ombe)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (907), An-Nasaaiy (7/222) na Ibn Maajah (3131)]
Na Hadiyth hizi zinabambanuliwa (zinakharijiwa) katika moja ya njia tatu: [Zaad Al-Ma’aad cha Ibn Al-Qayyim (2/266-267)]
1- Ima isemwe: Hadiyth zinazosema watu saba washirikiane ngamia mmoja au ng’ombe mmoja ndizo nyingi zaidi na Swahiyh zaidi.
2- Au isemwe: Kumsawazisha ngamia mmoja na kondoo kumi, ni tathmini ya kuleta uwiano sawa katika mgawo wa ghanima. Ama kuwa kwa watu saba katika wanyama wa kuchinja kwenye Hajj, hayo ni makadirio ya kisharia.
3- Na ima isemwe: Kuwa hilo linatofautiana kwa kutofautiana zama, mahala na ngamia. Katika baadhi ya nyakati, ngamia mmoja alikuwa sawa na mbuzi kumi, akamfanya kwa watu kumi, na nyakati nyingine alikuwa sawa na mbuzi saba, akamfanya kwa watu saba. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
Wakati wa kuchinja
Imestahabiwa kuchinja Yawm An-Nahr (10 Dhul Hijjah) baada ya kutupia Jamaratul ‘Aqabah, na kabla ya kunyoa na kutufu kama ilivyotangulia. Ama wakati wa kujuzu, ‘Ulamaa wamekhitalifiana kwa kauli mbalimbali: [Al-Mabsuwtw (12/9), Al-Ummu (2/217), Al-Inswaaf (4/87), Al-Majmuw’u (8/390) na Az-Zaad (2/318)]
1- Inajuzu kuchinja Yawm An-Nahr na siku tatu baada yake. Hii ni kauli ya ‘Aliyy bin Abiy Twaalib, na madhehebu ya Al-Hasan Al-Baswriy, ‘Atwaa, Al-Awzaa’iy na Ash-Shaafi’iy. Ni chaguo la Ibn Al-Mundhir, Ibn Taymiyah na Ibn Al-Qayyim. Hoja yao ni Hadiyth:
((كل أيام التشريق ذبح))
((Masiku yote ya Tashriyq ni kuchinja)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Ahmad (4/82) na Ibn Hibaan (1008) kwa Sanad Munqatwi’u]
Na kwa kuwa siku tatu ni mahususi kama Siku za Minaa, Siku za Kutupia, Siku za Tashriyq, na ni haramu kuzifunga, hivyo siku hizi ni ndugu katika hukmu hizi, haziwezi kutenganishwa katika kujuzu kuchinja bila Aayah au Hadiyth au Ijma’a.
2- Wakati wake ni Yawm An-Nahr na siku mbili baada yake. Ni madhehebu ya Ahmad. Maalik na Abu Haniyfah. Pia ni kauli iliyosimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar, Ibn ‘Abbaas na Swahaba zaidi ya mmoja. Hoja yao ni kuwa imekatazwa kuzivundika nyama za Adhwaahiy kwa zaidi ya siku tatu.
Wamesema hii ni dalili kuwa siku za kuchinja ni tatu tu. Lakini kauli hii ina walakini, kwa kuwa katazo la kuvundika zaidi ya siku tatu, halizuii kuchinja baada ya siku tatu.
3- Wakati wa kuchinja ni siku moja tu, kwa kuwa siku imeambatika na jina lenyewe, na hivyo hukmu yake imeambatanishwa nayo. Ni kauli ya Ibn Siyriyna.
4- Ni siku moja tu kwa mijini na siku tatu kwa Minaa. Ni kauli ya Sa’iyd bin Jubayr na Jaabir bin Zayd. Kwa kuwa Minaa kuna matendo ya Manaasik kama kutupia Jamaraat, Kutufu na kunyoa. Hivyo yamekuwa ni siku za kuchinja kinyume na watu wa mijini.
5- Ni kuanzia Yawm An-Nahr hadi mwisho wa Dhul Hijjah. Kauli hii imesimuliwa toka kwa Abu Salamah bin ‘Abdur Rahmaan na An-Nakha’iy.
6- Hakuna wakati maalum. Ni mwono wa Ash-Shaafi’iy, na An-Nawawiy ameudhoofisha. [Al-Majmuw’u (8/348-349)]
Ninasema: “Inaonekana wazi kuwa siku za kuchinja ni nne: Yawm An-Nahr na siku tatu baada yake za At-Tashriyq. Hili limepitishwa kwa wingi na Baraza la Bodi ya ‘Ulamaa Wakuu wa Saudia (azimio no. 43 la tarehe 13/4/1396 Hijriyyah)”. [Tawdhwiyhul Ahkaam cha Bassaam (3/374)]
Mahala pa kuchinjia
Allaah Mtukufu Amesema:
((ثُمَّ مَحِلُّهَا إِلَى الْبَيْتِ الْعَتِيقِ))
((Kisha [mahala pa] kuhalalika kwake kuchinjwa ni kwenye Nyumba ya Kale)). [Al-Hajj (22:33)]
Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alichinja mahala pake pa kuchinjia Mina, na akasema:
((نحَرْتُ هَا هُنَا، وَمِنًى كُلهَا مَنْحَرٌ، فَانْحَرُوا فِي رِحَالِكُمْ))
((Nilichinja hapa, na Mina yote ni mahala pa kuchinjia, basi chinjeni majumbani mwenu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1218) toka kwa Jaabir]
Na katika tamko jingine:
((وكل منى منحر، وكل المزدلفة موقف، وكل فجاج مكة طريق ومنحر))
((Na Mina yote ni mahala pa kuchinjia, na Muzdalifah yote ni sehemu ya kisimamo, na barabara zote za Makkah ni njia na mahala pa kuchinjia)). [Isnaad Yake ni Hasan. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1937), Ibn Maajah (3048) na Ahmad (3/326)]
Hivyo basi, mnyama hachinjwi isipokuwa katika Al-Haram. Atakayechinja mahala popote ndani ya Al-Haram, -ndani ya Makkah au penginepo- basi itamtosheleza kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri. Lakini Maalik amesema haitoshelezi katika Al-Haram isipokuwa Makkah tu akishikimana na udhahiri wa Kauli Yake Ta’aalaa:
((هَدْيًا بَالِغَ الْكَعْبَةِ))
((Mnyama huyo afikishwe Ka’bah)).
Na kitendo cha Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ni hujja dhidi yake. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi.
Je, inajuzu kuhamisha nyama za adhwaahi nje ya Al-Haram?
Baraza la Bodi ya ‘Ulamaa wa Saudia katika azimio lake (nambari 77) tarehe 21/10/1400 Hijria limesema:
Wanyama anaochinja Hujaji ni wa aina tatu:
1- Mnyama wa kufanya Tamattu’u au Qiraan. Huyu inajuzu kuhamisha nyama yake nje ya Al-Haram. Swahaba (Ridhwaanu Allaah ‘alayhim) walichukua sehemu ya nyama za wanyama wao waliowachinja kwenda nazo Madiynah. Katika Swahiyh Al-Bukhaariy toka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah amesema: ((Tulikuwa hatuli nyama za ngamia wetu zaidi ya siku tatu Minaa, na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akaturuhusu akituambia:
((كلوا وتزودوا، فأكلنا وتزودنا))
((Kuleni na chukueni masurufu ya safari, tukala na tukabeba masurufu ya safari)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1719) na Muslim (1972)]
2- Mnyama anayemchinja Hujaji ndani ya Al-Haram kama malipo ya kuwinda, au fidia ya kuondosha adha, au kufanya lililokatazwa, au kuacha la waajib. Aina hii haijuzu kabisa kuhamisha nyama yake kupeleka kwengine, kwa kuwa nyama yote ni kwa masikini wa Al-Haram.
3- Mnyama aliyechinjwa nje ya mipaka ya Al-Haram kama wa fidia ya malipo, au wa kuzuilika, au mwingine wa kuwezekana kuchinjwa nje ya Al-Haram. Huyu nyama yake hugawiwa pale alipochinjwa, na pia haikatazwi kuihamisha toka mahala alipochinjwa kupelekwa kwengine. [Tawdhwiyhul Ahkaam (3/311-312)]
Kuwaswaga wanyama
Inajuzu kwa Hujaji amnunue mnyama wake katika eneo la Al-Haram. Pia inajuzu amlete (amswage) toka nje ya Al-Haram. Na akimswaga, imestahabiwa amfunge vigwe na amtie alama –kama ni ngamia au ng’ombe- bila makhitalifiano yoyote. Vigwe ni kamba au kipande cha ngozi ambacho hufungwa shingoni ili ajulikane kuwa ni mnyama wa kudhwahi. Ama kutiwa alama, ni kupasuliwa upande mmoja wa nundu ya ngamia au ng’ombe damu ikachuruzika, na hiyo inakuwa ni alama ya kuwa ni mnyama wa kudhwahi. Ash-Shaafi’iy na Ahmad wamestahabisha apasuliwe upande wa kulia.
Toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema:
صَلَّى رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم الظهْرَ بِذِي الْحُلَيْفَةِ، ثُمَّ دَعَا بِبدنة فَأَشْعَرَهَا من صَفْحَةِ سَنَامِهَا الأَيْمَنِ، وَسَلَتَ الدَّمَ عنها، وَقَلَّدَهَا بنَعْلَيْنِ، ثُمَّ رَكِبَ رَاحِلَتَهُ، فَلَمَّا اسْتَوَتْ بِهِ عَلَى الْبَيْدَاءِ، أَهَلَّ بِالْحَجَّ
((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliswali Adhuhuri Dhul Hulayfah, kisha akaitisha ngamia wake, akamtia alama upande wa kulia wa nundu yake, akampangusa damu yake, na akamfungia viatu viwili. Kisha alimpanda ngamia wake, na alipokaa sawa naye juu ya Al-Baydaa, alinyanyua sauti yake kuleta Talbiyah kwa ajili ya Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1234), Abu Daawuwd (1752) na An-Nasaaiy (5/170-171)]
Je. mbuzi na kondoo huvishwa vigwe?
Maalik na Abu Haniyfah wamesema mbuzi na kondoo hawavishwi vigwe. Na Ash-Shaafi’iy, Ahmad, Abu Thawr na Daawuwd wamesema wanavishwa kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah: ((Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipeleka mara moja kondoo wa kudhwahi, akamvisha vigwe)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1701) na Muslim (1331)]
Kuwasimamisha wanyama wa kudhwahi ‘Arafah (na kuwatambulisha)
[Al-Muhallaa (7/166/167) na Bidaayatul Mujtahid 1/561-562)]
Maalik anaona kuwa mnyama wa kudhwahi anayenunuliwa Haram hatoshelezi mpaka asimamishwe ‘Arafah. Na kama atanunuliwa sehemu ambayo marufuku za Ihraam zinaruhusika kisha akaingizwa Haram basi itatosha hata kama hakusimamishwa ‘Arafah.
Allayth kasema: Hawi mnyama wa kudhwahi ila aliyevikwa njuga, aliyepasuliwa alama na akasimamishwa ‘Arafah. Na huja yake ni Hadiyth ya Twaawuws: ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimtia alama ngamia)). Lakini Hadiyth si Swahiyh. [Hadiyth Dhwa’iyf. Angalia Al-Muhallaa (7/166)]
Ash-Shaafi’iy, Ath-Thawriy na Abu Thawr wamesema kuwa kusimama mnyama wa kudhwahi ‘Arafah ni Sunnah, na hakuna ubaya kumwacha, ni sawa akiwa ni mwenye kuingia toka sehemu iliyohalalishwa marufuku au hakuwa.
Abu Haniyfah kasema: Kumtia alama mnyama si Sunnah.
Ninasema: “La sawa ni kuwa akisimama na mnyama wa kudhwahi (‘Arafah) basi ni jambo jema, na kama hakusimama naye, basi hapana ubaya. Ibn Hazm kasema: “Haikuja amri yoyote ya kutia alama katika hilo kutoka kwenye Qur-aan au Sunnah. Na haliwi waajib ila Aliloliwajibisha Allaah katika moja ya mawili, na hakuna pia Qiyaas kinachowajibisha hilo, kwa kuwa Manaasik za Hajj ndizo zenye kuwawajibikia watu na si ngamia”.
Alaa kulli haal, utiaji alama na uvikaji wanyama vigwe katika nyakati zetu za sasa ni jambo lenye uzito na tabu kubwa, hivyo watu wasijibebeshe hilo. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Uchinjaji wa wanyama
‘Ulamaa wamekubaliana kuwa uchinjaji wa wanyama wa kufugwa ni "نحر" (chinjo la mwenye shingo ndefu kama ngamia) na "ذبح" (chinjo la mwenye shingo fupi kama ng’ombe), na kuwa "ذبح" ni Sunnah kwa mbuzi na kondoo, na "نحر" kwa ngamia. Tofauti kati ya "النحر" na "الذبح" itaelezwa kwa ubayana katika mlango wa wanyama wa kudhwahi. [Bidaayatul Mujtahid (1/670)]
Sunnah ya kumchinja mwenye shingo ndefu
Kati ya Sunnah ya kumchinja mwenye shingo ndefu ni kuchinjwa akiwa amesimamishwa na amefungwa. Allaah Amesema:
((فَاذْكُرُوا اسْمَ اللَّـهِ عَلَيْهَا صَوَافَّ))
Basi tajeni Jina la Allaah juu yao wanapopangwa safu (kuchinjwa). [Al-Hajj: 36]
Ibn ‘Abbaas kasema: Yaani wamesimama kwa miguu mitatu. [Al-Hajj (22:36)]
Na toka kwa Ziyaad bin Jubayr: ((Kwamba Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alimwendea mtu aliyekuwa anamchinja ngamia wake aliyepiga magoti akamwambia: Msimamishe akiwa amefungwa [mguu wake wa mbele wa kushoto], ni Sunnah ya Nabiy wenu (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1713), Muslim (1320) na Abu Daawuwd (1767)]
Na toka kwa Jaabir: ((Kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na Swahaba Zake walikuwa wakichinja ngamia akiwa amefungwa mguu wake wa mbele wa kushoto na kusimama kwa iliyobakia)). [Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1767)]
Ama ng’ombe, mbuzi na kondoo, hawa imestahabiwa kuwachinja kwa kuwalaza kwa ubavu wa kushoto, kuuacha huru mguu wa mbele wa kulia, na miguu mitatu ifungwe kamba kwa namna ambayo itabainishwa kwenye mlango wa wanyama wa kudhwahi.
Manufaa ambayo mwenye mnyama anaweza kunufaika nayo kutokana na mnyama wake
Nufaiko la kwanza: Kula nyama yake anapofika mahala halali pa kuchinjwa. Allaah Mtukufu Amesema:
((فَكُلُوا مِنْهَا وَأَطْعِمُوا الْبَائِسَ الْفَقِيرَ))
((Basi kuleni humo, na lisheni mwenye shida fakiri)). [Al-Hajj (22:28)]
‘Ulamaa wamekhitalifiana kuhusiana na kula nyama ya mnyama ambaye ni wa waajib. Abu Haniyfah amesema: “Haliwi mnyama wa waajib isipokuwa mnyama wa Tamattu’u na Qiraan”. [Al-Hidaayah (1/186)]
Na hii ni kauli ya Fuqahaa wengi wa Kihanbal. [Al-Mubdi’u (3/124), Al-Inswaaf (3/439), na Al-Furuw’u (3/378)]
Maalik kasema: “Wanyama wote wa waajib huliwa isipokuwa wa malipo ya kuwinda, nadhiri ya masikini na fidia ya adha”. [Bidaayatul Mujtahid (1/565) na Al-Kharshiy (2/378)]
Ash-Shaafi-’iy kasema: “Mnyama wa waajib haliwi wote, bali nyama yake yote ni kwa masikini”. [Rawdhwat At-Twaalibiyna (3/191)]
Ninasema: “Mnyama anayefanana na wa kafara, nyama yake hailiwi kwa kuwa ‘Ulamaa wamekubaliana kuwa mwenye kafara hali chochote cha mnyama wake. Na hili liko wazi katika mnyama wa malipo ya kuwinda, fidia ya adha na damu nyingine za kukarabati na kuunga kosa. Ama ambaye ni damu ya Nusuk, basi mnyama huyo kimsingi ni wa ‘ibaadah na si damu ya kukarabati na kuunga kosa, na huyu nyama yake huliwa. Na mnyama wa Tamattu’u na Qiraan, huyo ni wa Nusuk –kwa kauli yenye nguvu- ambaye amewajibishwa na sharia kwa ajili ya kumshukuru Allaah Ta’aalaa kwa neema Aliyomtunuku Hujaji kwa kumwepesishia kufanya Hajj na ‘Umrah katika safari moja. Na linalotilia nguvu hili ni kuwa tokea awali sababu ya kuunga kosa ilikuwa ni marufuku wakati ambapo Tamattu’u imeruhusiwa bila pingamizi yoyote. Na kama damu yake ingekuwa damu ya kuunga kosa, basi Tamattu’u isingelijuzu kabisa. Na haya ni madhehebu ya Mahanafiy na Mahanbali wengi, na chaguo la Ibn Taymiyah”. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/82)]
‘Ulamaa wa Kishaafi-’iy na Maalik wanasema ni damu ya kukarabati kosa isipokuwa Wamaalik wamejuzisha kula. Mwelekeo wa kwanza una nguvu zaidi, kwani imethibiti kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikula kidogo nyama ya mnyama wake na yeye alikuwa amefanya Qiraan. Na katika Hadiyth ya Jaabir: ((…kisha akaamuru kwa kila ngamia lichukuliwe fungu, nikayatia kwenye chungu, nikayapika, wakala nyama yake na wakanywa supu yake..)). [Al-Majmuw’u (7/176), Ar-Rawdhwah (3/47) na Ash-Sharhul Kabiyr ma’a Haashiyat Ad-Dusuwqiy (2/84)]. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Ama mnyama wa swadaqah, huyu huliwa sehemu ya nyama yake kwa Ijma’a ya ‘Ulamaa –akifikia mahala pa kuchinjwa- kama baki ya watu wengine.
Na ikiwa mnyama atapata adha hatarishi kwa maisha yake kabla hajafika sehemu ya kuchinjwa, basi atamchinja na atawaachia nyama yake watu wengine wale (na si watu wa msafara wake). Toka kwa Ibn ‘Abbaas kwamba Abu Qubayswah alimhadithia kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa akimtuma kumpelekea ngamia kisha humwambia:
((إن عَطِب منها شيءٌ، فخشيت عليها موتًا، فَانْحَرها، ثم اغْمِس نعلَها في دمِها، ثم اضرب صفحتها، ولا تَطْعَمها أنت ولا أحدٌ من أهل رُفْقَتِك))
((Kama ataumia sehemu yoyote ya mwili wake ukakhofia atakufa, basi mchinje, kisha kitoteshe kigwe chake ndani ya damu yake, halafu pakaza damu ubavuni mwake, na wala usile wewe wala yeyote katika watu wa msafara wako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1326), Ibn Maajah (1036) na Abu Daawuwd (1763)]
Sababu ya yeye na watu wa msafara wake kukatazwa kula nyama hiyo ni kuchelea wao kumjeruhi mnyama ili achinjwe wapate kula nyama kabla ya wakati wake.
Nufaiko la pili: Kumpanda kwa mwenye kuhitajia hilo
Inajuzu kumpanda mnyama wa kudhwahi kama Hujaji atahitajia kumpanda. Atampanda kwa mujibu wa hali inavyoruhusu bila kumuumiza au kumdhuru. Haya ni madhehebu ya Ash-Shaafi-’iy kutokana na Kauli Yake Ta’aalaa:
((لَكُمْ فِيهَا مَنَافِعُ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى ثُمَّ مَحِلُّهَا إِلَى الْبَيْتِ الْعَتِيقِ))
((Katika hao (wanyama) mnapata humo manufaa mpaka muda maalumu uliokadiriwa. Kisha kuhalalika kwake kuchinjwa ni kwenye Nyumba ya Kale. (Haram ya Makkah)). [Al-Hajj (22:33)]
Kati ya manufaa hayo ni kumpanda. Toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alimwona mtu anamswaga ngamia [naye kachoka sana], akamwambia: “Mpande”. Akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Huyu ni ngamia [wa kuchinjwa Ka’abah]. Akamwambia:
((اركبها ويلك))
((Mpande, we vipi wewe.)) katika mara ya pili au ya tatu. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1689), Muslim (1322) na wengineo]
Na toka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah –ambaye aliulizwa kuhusu kumpanda mnyama wa kudhwahi- akasema: ((Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) anasema:
((اركبها بالمعروف إذا ألجئت إليها حتى تجد ظهراً))
((Mpande bila kumdhuru ukilazimika kwa hilo mpaka upate mgongo [wa mnyama mwingine wa kupanda])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1324), Abu Daawuwd (1761) na An-Nasaaiy (2/147)]
Abu Haniyfah, Maalik, Ahmad, Is-Haaq na Adh-Dhwaahiriyyah wanasema kuwa atampanda hata kama hahitajii kupanda. Na Hadiyth ya Jaabir inawarudi. [Sharhu Muslim cha An-Nawawiy (4/806)].
Mchinjaji halipwi kutokana na mnyama
Haijuzu mchinjaji kupewa malipo yake ya kuchinja kutokana na mnyama aliyechinjwa, lakini inajuzu kumpa nyama kama swadaqah baada ya kumpa malipo yake. Ni kwa Hadiyth ya ‘Aliyy (Radhwiya Allaah ‘anhu): ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliniamuru nisimamie ngamia, nigawe ngozi yake na matandiko yake, na akaniamuru nisimpe mchinjaji chochote kutokana na mnyama. Akasema: Sisi tunampa kutoka kwetu)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1717), Muslim (1317) na wengineo]
Kufunga kwa asiyeweza kuchinja
Mwenye kufanya Qiraan na Tamattu’u ni lazima achinje kama ilivyotangulia nyuma, na kama hana fedha za kununulia mnyama au hakuweza kumpata, basi atafunga siku tatu akiwa Hajj na siku saba atakaporejea kwao nyumbani kama Alivyosema Ta’alaa:
((فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ ۚ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ))
((Basi mwenye kufanya Tamattu’u kwa kutekeleza ‘Umrah kwanza kisha Hajj, achinje mnyama aliye mwepesi. Na asiyepata afunge Swiyaam siku tatu katika Hajj na saba mtakaporejea)). [Al-Baqarah (2:196)]
Na katika Hadiyth ya Ibn ‘Umar, Nabiy (Swalla Allaah ‘ alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((فمن لم يجد هديا فليصم ثلاثة أيام في الحج وسبعة إذا رجع إلى أهله))
((Ambaye hakupata mnyama, basi afunge siku tatu katika Hajj na saba akirejea kwa watu wake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1691) na Muslim (1227)]
Ni wakati gani anafunga siku tatu?
‘Ulamaa wamekhitalifiana kuhusu siku hizi tatu zinazofungwa katika Hajj kwa kauli nyingi. Mashuhuri zaidi ni kauli mbili:
Ya kwanza: Inahalalika kuzifunga tokea anapohirimia ‘Umrah katika miezi ya Hajj, na imestahabiwa ziwe kuanzia tarehe saba Dhul Hijjah, Siku ya Tarwiyah na Siku ya ‘Arafah. Kauli hii imekhitariwa na Ibn Taymiyah, na ni madhehebu ya Mahanafiy na Mahanbali. Ahmad amenukuliwa akisema kuwa lililo bora zaidi ni siku ya mwisho iwe Siku ya Tarwiyah (tarehe nane). [Fat-hul Qadiyr (2/529), Al-Inswaaf (3/512) na Al-Mubdi’u (3/175)]
Na ikiwa mtu atasema, Allaah Ta’aalaa Amesema:
ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ
((Siku tatu katika Hajj)),
ataambiwa na’am, na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((دخلت العمرة في الحج))
((‘Umrah imeingia ndani ya Hajj)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma]
Ya pili: Haijuzu kufunga ila baada ya kuhirimia Hajj. Ni madhehebu ya Maalik, na Ash-Shaafi-iy. [Ash-Sharhul Kabiyr ma’a Haashiyati Ad-Dusuwqiy (2/84) na Al-Majmuw’u (7/186)]
Dalili ni Kauli Yake Ta’aalaa:
((ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ))
((Siku tatu katika Hajj)). [Al-Baqarah (2:196)]
Ni kauli iliyosimuliwa toka kwa Ibn ‘Umar.
Ninasema: “Kauli zote mbili zina mwelekeo murua unaobeba maana yumkinivu ya Aayah Tukufu. Kauli ya kwanza haina kipingamizi, lakini ni lazima kuzingatia yafuatayo: [Yamedokolewa toka kwenye Kitabu cha Ash-Sharhul Mumti’u (7/208)]
(a) Haitakikani kuhirimia Hajj kutangulizwe kabla ya Siku ya Tarwiyah (tarehe nane) kwa ajili ya kufunga, kwani hivi ni kinyume na Sunnah kama tulivyotangulia kuelezea. Na dhana topezi ni kuwa baadhi ya Swahaba waliohirimia na Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) Siku ya Tarwiyah, walikuwa ni masikini bila wanyama, na hawakutanguliza Ihraam ya Hajj.
(b) Haitakikani Hujaji afunge Siku ya ‘Arafah kwa kuwa ni kinyume na Sunnah kama ilivyoelezwa nyuma. Akitaka anaweza kufunga tarehe sita, saba na Siku ya Tarwiyah kama alivyosema Ahmad na kukhitariwa na Ibn Baaz (Rahimahuma-Allaah).
(c) Linaloonekana ni kuwa Swahaba walikuwa wakizifunga katika Siku za Tashriyq kama linavyofahamika hilo kutokana na Hadiyth ya Ibn ‘Umar na ‘Aaishah: ((Haikuruhusiwa katika Siku za Tashriyq kuzifunga isipokuwa kwa ambaye hakupata mnyama)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1997)]
Hili ndilo la akiba na salama zaidi, na kwalo Hujaji atajinasua toka kwenye mvutano.
(d) Haijuzu kuchelewesha kuzifunga siku hizo tatu baada ya Siku za Tashriyq, kwa kuwa siku zinazofuatia baada yake, si siku za Hajj.
(e) Akifunga kabla ya Siku za Tashriyq halazimishwi azifunge mfululizo, kwa kuwa Aayah haikuweka mabano ya kufunga mfululizo. Kiilivyo, Aliloliachilia Allaah na Rasuli Wake bila kuliwekea mpaka linaachiliwa kama lilivyo bila kuliwekea mpaka. Lakini kama ataanza kufunga katika Siku ya kwanza ya Tashriyq, hapo itamlazimu kufuatanisha ili Swawm yake iwe ndani ya Siku za Hajj. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Aliyezuilika kama hana mnyama
Tumeeleza nyuma kuwa aliyezuilika asiweze kukamilisha Hajj yake –na hakuwa ameweka shuruti katika Ihraam yake- basi huyo ni lazima achinje kutokana na Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((Na kama mkizuilika basi chinjeni wanyama walio wepesi kupatikana)). [Al-Baqarah (2:196)]
Mnyama huyo atamchinja mahala pale alipozuilika, halafu atanyoa nywele zake. Toka kwa Ibn ‘Umar amesema: ((Tulitoka na Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kwenda kufanya ‘Umrah, na makafiri wa Kiqureshi wakaizuia Nyumba. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akamchinja ngamia wake na akanyoa kichwa chake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1997)]
Na kama hakuweza au hakumpata, basi la sawa ni kuwa atavua Ihraam, na hatodaiwa chochote, si Swawm wala kingine. Ama mwenye kufanya Qiyaas kwa mnyama wa Tamattu’u, hili tunaweza kulipembua kwa njia hizi:
1- Katika ‘Umrah ya Hudaybiyah, Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa pamoja na Swahaba wake wengi wakiwemo masikini kati yao. Na haikuripotiwa kuwa aliwaamuru kufunga siku kumi wale ambao hawakuweza kupata mnyama. Hao kiasili hawadaiwi lolote.
2- Ni kuwa hukmu ya Tamattu’u na kuzuilika ipo kwenye Aayah moja [Al-Baqarah 196]. Allaah Ameitaja badali ya kutokuwa na mnyama wa kuchinja katika Tamattu’u [ambayo ni kufunga siku 10] na Hakuitaja katika kuzuilika, bali Amehamia kwenye hukmu nyingine Akisema
وَلَا تَحْلِقُوا رُءُوسَكُمْ
((Na wala msinyoe vichwa vyenu)),
na hivyo kuonyesha kuwa aliyezuilika ambaye hana mnyama, hadaiwi chochote. Hivyo Qiyaas kinakinzana na Aayah.
3- Ni kuwa Qiyaas hiki ni Qiyaas bila urari, kwani tofauti kati ya Tamattu’u na kuzuilika ni kubwa sana. Mwenye kufanya Tamattu’u lengo lake la Hajj anakuwa ashalipata baada ya kujivua na Ihraam ya ‘Umrah wakati mwenye kuzuilika hakukidhi lengo lake. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
29-Kunyoa Na Kupunguza
Alhidaaya.com [3]
Hukmu Yake
Jumhuri ya ‘Ulamaa wamekubaliana kuwa kunyoa nywele za kichwa au kuzipunguza ni waajib kati ya waajibaat za Hajj. Ni madhehebu ya Hanafiy, Maalik na Hanbal. [Fat-hul Qadiyr (2/178, 252), Sharhu Ar-Risaalati Bihaashiyatil ‘Adawiy (1/478), Al-Mughniy (3/435) na Al-Furuw’u (3/513)]
Kwa Ash-Shaafi’iy, kwa ilivyo mashuhuri kwake ni kuwa kunyoa au kupunguza ni nguzo ya Hajj. [Al-Mjmuw’u (8/189)]
Sababu ya kukhitalifiana kwao ni kukosekana dalili ya hili au lile pamoja na kuthibiti la kunyoa na kupunguza katika Qur-aan, Sunnah na Ijma’a. Allaah Amesema:
((لَّقَدْ صَدَقَ اللَّـهُ رَسُولَهُ الرُّؤْيَا بِالْحَقِّ ۖلَتَدْخُلُنَّ الْمَسْجِدَ الْحَرَامَ إِن شَاءَ اللَّـهُ آمِنِينَ مُحَلِّقِينَ رُءُوسَكُمْ وَمُقَصِّرِينَ لَا تَخَافُونَ))
((Kwa yakini Allaah Amemsadikisha Rasuli Wake ndoto kwa haki. Bila shaka mtaingia Al-Masjidal-Haraam In Shaa Allaah mkiwa katika amani, wenye kunyoa vichwa vyenu na wenye kupunguza, hamtakuwa na khofu)). [Al Fat-h (48:27)].
Na toka kwa Ibn ‘Umar kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
اللهم ارحم المحلقين
((Ee Allaah! Warehemu wenye kunyoa)).
Wakasema: Na wenye kupunguza ee Rasuli wa Allaah. Akasema:
اللهم ارحم المحلقين
((Ee Allaah! Warehemu wenye kunyoa)).
Wakasema: Na wenye kupunguza ee Rasuli wa Allaah. Akasema:
اللهم ارحم المحلقين
((Ee Allaah! Warehemu wenye kunyoa)).
Wakasema: Na wenye kupunguza ee Rasuli wa Allaah. Akasema:
والمقصرين
((Na wenye kupunguza)).
[Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1727) na Muslim (1301)]
Na kunyoa ni bora zaidi kuliko kupunguza. Ni kwa Hadiyth ya Ibn ‘Umar iliyotangulia. Na kunyoa si waajib isipokuwa kama atanadhiria kufanya hivyo. Na akipunguza, atakusanya nywele zake kisha atazikata kwenye mkusanyikio kiasi cha pingili ya kidole au chini yake au zaidi.
Ama wanawake, wao hupunguza na hawanyoi. Toka kwa Ibn ‘Abbaas: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alituambia)):
((ليس على النساء حلق، إنما على النساء التقصير))
((Si waajib kwa wanawake kunyoa, bali waajib kwa wanawake ni kupunguza)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1985), Ad-Daaramiy (1905) na wengineo]
Zaidi ya mtu mmoja wamesimulia Ijma’a ya kuwa wanawake hawanyoi bali wanapunguza.
Ni kiasi gani cha nywele anapunguza mwanamke aliyehirimia?
Hili halikugusiwa na Qur-aan wala Sunnah. Baadhi ya ‘Ulamaa wamesema kuwa atakata kiasi cha pingili ya kidole katika kila quruni (fundo la msuko). Waliosema hili ni Ibn ‘Umar, Ash-Shaafi’iy, Ahmad na Abu Thawr. Wengine wamesema: Atajichonga pembeni pembeni kidogo, na wengine wamesema msichana hatopunguza sana, lakini mama mzee atapunguza kwa kiasi kisichozidi robo ya nywele zake. [Angalia aathaar za hili katika Muswannaf Ibni Abiy Shaybah (1/4/115-117) na Jaami’u Ahkaamin Nisaa cha Sheikh wetu (2/566)]
Ninasema: “Inavyoonekana ni kuwa anaweza kupunguza kiasi anachopenda mwenyewe muhimu tu asifanane na wanaume. Na kama atafanana na wanaume, haitofaa. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Wakati wa kunyoa na kupunguza
Ni Sunnah kunyoa au kupunguza Yawm An-Nahr baada ya kutupia Jamaratul ‘Aqabah na kuchinja kwa kufuata kitendo cha Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam).
Jumhuri wanasema kunyoa au kupunguza hakuhusishwi na muda maalum au mahala maalum, lakini Sunnah ni kufanya hayo katika eneo la Al-Haram katika Siku za kuchinja.
Mahanafiy wanasema wakati wake ni katika siku za Kuchinja katika eneo la Al-Haram. Na lau Hujaji atakosea chochote katika mawili haya, basi ataipata tahallul (kuvua Ihraam) lakini ni lazima achinje. [Angalia vitabu rejea tulivyovitaja katika hukmu ya kunyoa]
Kati ya adabu za kunyoa
1- Asijinyoe mwenyewe bali anyolewe na mtu.
2- Kinyozi aanze kumnyoa upande wa kulia wa kichwa chake. Dalili ya mawili haya (1 na 2) ni Hadiyth ya Anas:
((أن رسول الله -صلى الله عليه وسلم- أتى مِنَى، فأتى الجَمْرَةَ فرماها، ثم أتى منزله بمِنَى ونحر، ثم قال للحلاق: «خُذْ» وأشار إلى جانبه الأيمن، ثم الأيسر، ثم جعل يعطيه الناسَ))
((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifika Mina, akaenda Jamarah akalitupia vijiwe, kisha akaenda sehemu yake aliyoshukia Mina akachinja. Kisha akamwambia mnyoaji: Kamata [kichwa ukinyoe], akamwashiria upande wake wa kulia, kisha wa kushoto, halafu akaanza kuwapa watu nywele zake [wazihifadhi ili watabaruku nazo])). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1305)]
[Riwaya nyingine inasema alimwita Abu Twalha Al-Answaariy (Radhwiya Allaah ‘anhu) akampa nywele zake hizo na akamwamuru azigawe kwa watu]
3- Akate kucha zake na sharubu zake baada ya kunyoa. Imesimuliwa kwa njia sahihi: ((Kuwa Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) alikuwa anaponyoa katika Hajj au ‘Umrah hukata kidogo ndevu zake na masharubu yake)).
Na Ibn Al-Mundhir amesema: “Imethibiti kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliponyoa kichwa chake, alikata kucha zake [pia]”. [Angalia Al-Majmuw’u (8/186, 195)]
Nini atafanya mwenye kipara?
Mwenye kipara kichwa kizima, hana cha kunyoa na hana fidia. Lakini imestahabiwa apitishe wembe (au mashine ya kunyolea) juu ya kichwa chake. Ibn Al-Mundhir amenukuu Ijma’a ya ‘Ulamaa kuwa mwenye kipara anapitisha wembe juu ya kichwa chake, lakini Jumhuri wanasema hilo si lazima. [Al-Majmuw’u (8/192, 193)]
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
30-Kupitwa Na Hajj Na Kuzuilika
Alhidaaya.com [3]
1- Kupitwa:
Ni kutenda jambo la kuikosa Hajj. Atakayepitwa na Kisimamo cha ‘Arafah mpaka ikachomoza Alfajiri ya Siku ya Kuchinja, basi huyo kaikosa Hajj. Dalili kuhusu hili imeelezwa nyuma wakati wa kuzungumzia nguzo ya Kusimama.
Aliyeikosa Hajj afanye nini?
Aliyepitwa na Kisimamo cha ‘Arafah basi ameikosa Hajj. Atavua Ihraam ya Hajj kwa ajili ya ‘Umrah ambapo atatufu, atasai, na atanyoa au kupunguza, na Manaasik nyingine zilizobakia kama kulala Muzdalifah, kutupia viguzo, kuwepo Minaa na mfano wake atakuwa hanazo tena, lakini itamlazimu ailipe Hajj yake mwaka unaofuatia, na achinje wakati wa kuilipa. Hii ni kauli ya Jumhuri kinyume na Mahanafiy ambao wanasema kuchinja si waaajib. [Al-Badaai’u (2/220), Al-Hidaayah (2/136), Al-Qawaaniynu Al-Fiqhiyyah (uk. 95), At-Taaju wal Ikliyl (3/200), Rawdhwat At-Twaalibiyna (3/182) na Al-Kaafiy (360)]
Ikiwa aliyeikosa Hajj ataonelea aendelee kubakia na Ihraam yake aje ahiji tena mwakani, basi anaruhusiwa hilo, kwa kuwa kurefuka muda baina ya kuhirimia na kufanya tendo la Hajj hakuzuii kulikamilisha. Ni kama ‘Umrah, au mtu aliyehirimia Hajj katika miezi isiyo ya Hajj.
Watu Wakikosea Tarehe Ya Kusimama ‘Arafah
Watu wakikosea wakasimama ‘Arafah tarehe nane au kumi, basi itawatosha, na si lazima walipe, kwa kuwa wamefanya waliloamuriwa. [Al-Majmuw’u (8/281)]
2- Kuzuilika:
Ni kushindikana aliyehirimia kukamilisha Hajj yake. Na asili ya hili ni Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((Na kama mkizuilika basi chinjeni wanyama walio wepesi kupatikana)). [Al-Baqarah (2:196)]
Sababu za zuio ni zipi?
[Al-Majmuw’u (8/283), Bidaayatul Mujtahid (1/528), na Al-Inswaaf (4/71)]
Kutokana na ‘Ulamaa kutofautiana katika kuifahamu Aayah iliyotangulia, wamekhitalifiana pia kwa upande wa sababu ya kimsingi ya kuleta zuio. Baadhi yao wamesema aliyezuilika ni aliyezuiliwa na maadui tu. Ni madhehebu ya Mashaafi’iy na Mahanbali. Kwa kuwa Aayah hii ilishuka baada ya washirikina kumzuia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) asifanye ‘Umrah ya Al-Hudaybiyah. Wametoa hoja pia kwa Kauli Yake (تعالى):
فَإِذَا أَمِنتُمْ
((mkipata amani))
baada ya Kauli Yake:
فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ
((Kama mkizuilika))
na Kauli Yake baada ya hapo:
فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا
((na atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu)).
Wamesema:
Kama aliyezuilika ni kwa sababu ya ugonjwa, basi kutajwa ugonjwa kusingelikuwa na faida baada ya hapo. Na haya ni madhehebu ya Ibn ‘Umar na Ibn ‘Abbaas.
Wengine wamesema, mwenye kuzuilika ni aliyezuilika kwa ugonjwa, adui na kila lenye kumzuia asiweze kutimiza Hajj yake. Ni kauli ya Maalik, riwaya toka kwa Ahmad na chaguo la Sheikh wa Uislamu, nayo ndiyo yenye nguvu. [Bidaayatul Mujtahid (1/529), Al-Inswaaf (4/71) na Al-Ikhtibaaraat (uk. 120)]
Na hii ni kwa ujumuishi wa Kauli Yake Ta’aalaa:
فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ
((Kama mkizuilika)).
Ama kuwa sababu ya kuteremka Aayah ni Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) kuzuiwa na adui, hii ni kuibania na kuifinyia dalili kwenye sababu yake tu [bila mtizamo mpana], na hili halifai. Ama kutolea dalili Kauli Yake Ta’aalaa:
فَإِذَا أَمِنتُمْ
((mkipata amani))
hili ni katika mlango wa kutaja hukmu ya baadhi ya vipengele vya jambo zima, na hii haihukumii takhswiys (uainisho wa kitu fulani tu) kama inavyoeleza taaluma ya Uswuwl. Na hapo hapo, Kauli Yake Ta’aalaa
فَإِذَا أَمِنتُم
inaonekana kwa nguvu kuwa haimhusu aliyezingirwa bali inahusiana na Tamattu’u ya kihakika, kana kwamba maana ya Aayah ni: Kama hamna hofu lakini mmefanya Tamattu’u kwa kuanza ‘Umrah kisha Hajj, basi chinjeni mnyama anayepatikana kwa wepesi. Taawili hii inaashiriwa na Kauli Yake Ta’aalaa:
((َٰذلِكَ لِمَن لَّمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ))
((Hayo ni kwa ajili ya yule ambaye watu wake hawaishi karibu na Al-Masjidil-Haraam))
Na mwenye kuzuilika anaweza kuwa yupo Al-Masjid Al-Haraam na mwengine kwa Ijma’a.
Ninasema (Abu Maalik): “Lililo wazi zaidi kuliko haya yote ni Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliingia kwa Dhwubaa’ah binti Az-Zubayr akamwambia: (([Huenda] ulitaka kuhiji)). Akasema: Wal-Laah, najihisi kuumwa sana. Akamwambia: ((Hiji, na ushurutishe, na sema:
اللهم محلي حيث حبستني
((Ee Allaah! Pangu pa kuvua Ihraam ni pale Utakaponizuia)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (5089) na Muslim (1207)]
Iko wazi kabisa bila utata kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amezingatia ugonjwa na maumivu ni sababu ya kuzuilika na Hajj. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.”
Aliyezingirwa afanye nini?
Aliyezingirwa akashindwa kutimiza Hajj yake, ikiwa alishurutisha (wakati wa kuhirimia) kuwa pahala pa kuvua Ihraam ni pale alipozuilika, basi atavua Ihraam na hatowajibikiwa na jambo lolote. Ni kwa Hadiyth ya ‘Aaishah iliyotangulia.
Na kama hakuwa ameshurutisha, basi atavua Ihraam na kufanya ‘Umrah, na itamlazimu achinje kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri. Ni kwa Kauli Yake Ta’aalaa:
((فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ))
((Na kama mkizuilika, basi chinjeni wanyama walio wepesi kupatikana)). [Al-Baqarah (2:196)]
Je ni lazima aliyezuilika alipe Hajj yake?
Jumhuri wanasema kuwa aliyezuilika si lazima alipe Hajj yake kama atavua Ihraam –kinyume na Mahanafiy- isipokuwa kama itakuwa tokea awali ni Hajj ya waajib kama Hijjah ya Uislamu. Atatakiwa uwajibu uliotangulia. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi.
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
31-Kutekeleza ‘Umrah Na Fadhila Zake
Alhidaaya.com [3]
Taarifu yake
Maana ya العمرة katika lugha ni ziara, au kupakusudia mahala paliposhamiri. Imeitwa hivi kwa kuwa inafanywa katika umri wote.
Ama kisharia, ni kuikusudia Al-Ka’abah kwa ajili ya Nusuk ambayo ni Kutufu na Kusai. [Mughnil Muhtaaj (1/460) na Kash-Shaaful Qina’a (2/436)]
Hukmu yake
‘Ulamaa wamekhitalifiana katika hukmu ya ‘Umrah kwa aliyewajibikiwa na Hajj katika kauli mbili:
Ya kwanza: ‘Umrah ni waajib mara moja tu katika umri wote
Ni madhehebu ya Ash-Shaafi’iy katika moja ya kauli zake mbili., na moja ya riwaya mbili toka kwa Ahmad. Imesimuliwa toka kwa ‘Umar, Ibn ‘Abbaas, Zayd bin Thaabit, Ibn ‘Umar na kundi la Masalaf. Ni kauli pia ya Ahlu Adh-Dhwaahir. [Al-Ummu (2/132), Al-Majmuw’u (7/3,7), Al-Mughniy (3/218), Al-Inswaaf (3/387) na Al-Muhallaa (7/360)]
Hoja zao ni:
1- Kauli Yake Ta’aalaa:
((وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ))
((Na timizeni Hajj na ‘Umrah kwa ajili ya Allaah)). [Al-Baqarah (2:196)]
2- Hadiyth ya ‘Aaishah aliyesema: ((Ee rasuli wa Allaah! Je ni waajib kwa wanawake Jihaad? Akasema:
((نعم عليهن جهاد لا قتال فيه: الحج والعمرة))
((Na’am, ni juu yao Jihaad isiyo na mapigano ndani yake; Hajj na ‘Umrah)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ahmad (6/71) na Ibn Maajah (2901). Al-Irwaa (981) amesema: “Na hii Isnaad yake ni Swahiyh juu ya sharti ya Masheikh wawili. Ninasema: “Hadiyth iliyopo kwa Al-Bukhaariy (1520) na An-Nasaaiy (5/86) haikutaja ‘Umrah, na matokeo ya Hadiyth ni mamoja, hivyo uthibiti wa tamko hilo utafitiwe. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”]
Neno lake (عليهن) linadulisha ulazima.
3- Hadiyth ya Adh-Dhubaa bin Ma’abad amesema: ((Nilimwendea ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhu) nikamwambia: Ee Amiyrul Muuminiyn. Hakika mimi nimesilimu. Na mimi nimekuta Hajj na ‘Umrah zimefaradhiwa kwangu, nami nimezinuwia. Akamwambia:
((هديت لسنة نبيك))
((Umehidiwa kwenye Sunnah ya Nabiy wako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na An-Nasaaiy (2/13-14), Abu Daawuwd (1799) na Ibn Maajah (2970). Angalia Al-Irwaa (2970)]
4- Jumhuri wanasema ‘Umrah ni Hajj ndogo. [Angalia Al Fat-h (6/322,8)/172) na Tafsiyr At-Twabariy (10/75)]
Ya pili: ‘Umrah ni Sunnah na si waajib
Ni madhehebu ya Abu Haniyfah na Maalik. [Al-Mudawwanah (1/370), Fat-hul Qadiyr (2/306) na Al-Badaai’u (3/1320)]
Ni kauli kongwe ya Ash-Shaafi’iy, riwaya nyingine toka kwa Ahmad, nayo imesimuliwa toka kwa Ibn Mas-‘uwd, na chaguo la Sheikh wa Uislamu Ibn Taymiyah. Hoja zao ni:
1- Yaliyosimuliwa toka kwa Jaabir: ((Kwamba Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) aliulizwa, je ‘Umrah ni waajib? Akasema:
((لا، وأن تعتمروا فهو أفضل))
((Hapana, mkifanya ‘Umrah, basi hilo ni bora kwenu)). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (939)]
2- Yaliyosimuliwa kwa njia Marfuw’u toka kwa Twalha:
((الحج جهاد، والعمرة تطوع))
((Hajj ni Jihaad, na ‘Umrah ni kujitolea [Sunnah])). [Hadiyth Dhwa’iyf. Imekharijiwa na Ibn Maajah (2989)]
3- ‘Umrah na Hajj ni ‘ibaadah mbili za jinsi moja. Ukiifanya kubwa, basi ndogo inakuwa si waajib. Ni kama kutawadha pamoja na kuoga, ingawa kutawadha pamoja na kuoga ni bora zaidi na ukamilifu zaidi. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/9)]
Na hivi ndivyo alivyofanya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), lakini aliwaamuru kufanya Tamattu’u, na akasema:
((دخلت العمرة في الحج إلى يوم القيامة))
((‘Umrah imeingia ndani ya Hajj mpaka Sikuya Qiyaamah)). [Hadiyth Swahiyh. Takhriyj yake imetajwa nyuma]
4- Kwamba ndani ya ‘Umrah hakuna tendo lolote zaidi ya matendo yaliyomo kwenye Hajj, na matendo hayo ya Hajj Allaah Ameyafaradhisha mara moja tu, na si mara mbili. Hivyo tunapata kujua kuwa Allaah Hakufaradhisha ‘Umrah. [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/8)]
Ninasema: “Ama Hadiyth ambazo kundi la pili limezitolea ushahidi, hakuna Hadiyth yoyote kati yake ambayo ni Swahiyh. Pamoja na hivyo, hoja za wenye kusema ‘Umrah ni waajib (ambao ni kundi la kwanza) pia haziko dhahiri bayana kuwajibisha ‘Umrah. Tukichukua Kauli Yake Ta’aalaa:
وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ
tutaona kwamba uwajibu wa hapa ni wa kutimiza matendo kwa aliyeanza kutekeleza ‘ibaadah hizo mbili. Ama katika kuanza, Allaah Amewajibisha Hajj tu Aliposema:
وَلِلَّـهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ
((Na kwa ajili ya Allaah, imewajibika watu watekeleze Hajj))
Na hakuwajibisha ‘Umrah. Ama kusema ‘Umrah ni Hajj ndogo, Ibn Taymiyah ameufanya usemi huu kuwa hoja dhidi ya wenye kusema ni waajib na si hoja ya kutilia nguvu usemi wao, kwa kuwa wanaposema Hajj ndogo, itamaanisha kuwajibishwa Hajj mbili (ndogo na kubwa), nalo ni jambo ambalo haliwezekani.
Muhimu, la salama na la akiba zaidi, ni kuitekeleza ‘Umrah bila kuiacha kutokana na uwezekaniko wa kuthibiti ziada ya neno “’Umrah” katika Hadiyth ya ‘Aaishah (iliyotangulia nyuma), na uwezekaniko wa kuwa muradi wa neno lake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
دخلت العمرة في الحج كهاتبن
((‘Umrah imeingia ndani ya Hajj kama viwili hivi))
Kuwa uwajibu wa ‘Umrah ni kama wa Hajj, na kwa kuwa kutenda kwa kutegemea dalili za uwajibu, dhima husalimika kwazo kwa mujibu wa Ijma’a. Allaah Ndiye Ajuaye Zaidi”.
Fadhila ya ‘Umrah
[Irshaadus Saariy ‘Anil Wajiyz (uk. 266)]
‘Umrah ni katika ‘Ibaadah zilizotukuka sana, na ni miongoni mwa vikurubisho bora kabisa ambavyo Allaah Huwapandishia kwavyo Waja Wake daraja na kuwaporomoshea kwavyo makosa. Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) ameihimizia kwa maneno na kivitendo.
1- Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((العمرة إلى العمرة كفارة لما بينهما))
((‘Umrah hadi ‘Umrah, ni kafara ya yaliyo kati yake)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1773) na Muslim (1349)]
2- Na amesema:
((تابِعُوا بَيْنَ الْحَجِّ وَالْعُمْرَةِ، فَإِنَّهُمَا يَنْفِيَانِ الْفَقْرَ وَالذُّنُوبَ كَمَا يَنْفِي الْكِيرُ خَبَثَ الْحَدِيدِ والذهب والفضة))
((Fatanisheni baina ya Hajj na ‘Umrah, kwani viwili hivi huondosha umasikini na madhambi, kama vile mivukuto [ya mhunzi] inavyoondosha uchafu wa chuma, dhahabu na silva)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na At-Tirmidhiy (807) na An-Nasaaiy (5/115). Angalia Swahiyh Al-Jaami’u (2899)]
3- Nabiy (‘Alayhis Swalaat was Salaam) alifanya ‘Umrah, na Swahaba wake wakafanya ‘Umrah pamoja naye wakati wa uhai wake na baada ya kufariki kwake.
Wakati wake
Inajuzu kufanya ‘Umrah katika siku zote za mwaka –kwa mujibu wa kauli ya Jumhuri- isipokuwa katika siku za Ramadhwaan inakuwa ni bora zaidi. Ni kwa kauli yake Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam)
((عُمرَةٌ في رمَضَانَ تَعدِلُ حجة - أو حَجَّةً مَعِي))
((‘Umrah katika Ramadhwaan inalingana [kwa thawabu] na Hijjah - au kuhiji pamoja nami)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1782) na Muslim (1256)]
‘Umrah inajuzu kabla ya Hajj
Toka kwa ‘Ikrimah bin Khaalid: ((Kwamba alimuuliza Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) kuhusu kufanya ‘Umrah kabla ya Hajj akajibu: Hakuna ubaya kuifanya, kwani Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifanya ‘Umrah kabla hajahiji)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1774)]
Je, ni sharia kufanya ‘Umrah mara kwa mara?
Kukariri ‘Umrah kunakuwa katika hali mbili:
Hali ya kwanza: Kuirudia rudia katika mwaka mmoja kwa safari za kwenda na kurudi
‘Ulamaa wamekhitalifiana kwa kauli mbili kuhusu hali hii: [Majmuw’u Al-Fataawaa (26/267) na kurasa zinazofuatia, na Al-Majmuw’u cha An-Nawawiy (7/140)]
Kauli ya kwanza: Ni makruhu. Ni kauli ya Hasan, Ibn Syriyna na An-Nakha’iy, ni madhehebu ya Maalik, na chaguo la Sheikh wa Uislamu.
Hoja yao ni kuwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na Swahaba wake hawakufanya ‘Umrah mara mbili kwa mwaka. Hivyo ni makruhu kuzidisha zaidi ya walivyofanya. Pia, ‘Umrah ni Hajj ndogo, na Hajj haifanywi katika mwaka ila mara moja tu, na hivyo hivyo ‘Umrah.
Kauli ya pili: Inajuzu na ni Sunnah. Ni madhehebu ya Jumhuri wakiwemo ‘Atwaa, Twaawuws, ‘Ikrimah, Ash-Shaafi’iy na Ahmad. Imesimuliwa pia toka kwa ‘Aliyy, Ibn ‘Umar, Ibn ‘Abbaas na ‘Aaishah.
Hoja yao ni kuwa ‘Aaishah kwa amri ya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifanya ‘Umrah mara mbili katika mwezi mmoja; ‘Umrah yake ambayo ilikuwa pamoja na Hajj, na ‘Umrah aliyoinuwia toka At-Tan-’iym (baada ya kumalizika Hajj).
Pia wametolea dalili Hadiyth isemayo:
((العمرة إلى العمرة كفارة لما بينهما))
((Umrah hadi ‘Umrah, ni kafara ya yaliyo kati yake)). [Hadiyth Swahiyh. Imetajwa nyuma kidogo]
Na Hadiyth ya ‘Aaishah: ((Kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alifanya ‘Umrah mbili: ‘Umrah katika Dhul- Qa-’adah, na ‘Umrah katika Shawwaal)). [Isnaad yake ni Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (1991) na Al-Bayhaqiy (5/11)]
Ninasema: “Ninaloliona linaniridhisha ni kuwa madhehebu ya Jumhuri ndiyo yenye nguvu. Kwani ‘Umrah ni ‘amali ya kheri, na halikuja katazo lolote la kuwa isirudiwe rudiwe. Na kuifanyia Qiyaas kwa Hajj –kuwa ni mara moja tu- hakufai, kwa kuwa ‘Umrah haikuwekewa wakati maalum kinyume na Hajj. Isitoshe, Hajj haiwezekaniki ikakariri katika mwaka mmoja. Hivyo kuilinganisha na ‘Umrah hakufai. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Hali ya pili: Kuirudia rudia kwa safari moja
Makhitalifiano katika suala hili ni mfano wa makhitalifiano yaliyo kabla yake. Na kauli yenye nguvu hapa ni kuwa si sharia mtu kufanya ‘Umrah nyingi katika safari moja kama wafanyavyo watu wengi leo ambao wanatoka kwenda hadi At-Tan-‘iym –baada ya Hajj mfano- kisha wanafanya ‘Umrah. Hili Rasuli hakulifanya, bali ((‘Umrah zote za Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alizifanya akiwa ndani ya Makkah. Na yeye alikaa Makkah baada ya wahyi kuanza kumshukia kwa miaka kumi na tatu, na haikunukuliwa kamwe toka kwake kuwa alifanya ‘Umrah akitoka nje ya Makkah katika muda wote huo. Na ‘Umrah aliyoifanya Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na akaiwekea sharia, ni ‘Umrah ya mtu anayeingia Makkah, na si ‘Umrah ya mtu aliye ndani ya Makkah, kisha akatoka kwenda nje ya mipaka ya Haram ili akahirimie. Na hili hakulifanya yeyote wakati wa uhai wake isipokuwa ‘Aaishah peke yake kati ya wengineo waliokuwa pamoja naye, kwa kuwa yeye alikuwa amehirimia ‘Umrah akapata hedhi, na Rasuli akamwamuru, akachanganya Hajj ndani ya ‘Umrah, na akawa ni mwenye kufanya Qiraan. Akahisi ukakasi wenzake kurudi wakiwa wamefanya Hajj kando na ‘Umrah kando, na yeye kafanya ‘Umrah ndani ya Hajj yake. Akamwomba kaka yake aende naye At-Tan-‘iym ili akahirimie ‘Umrah huko)). [Irshaadu As-Saariy ‘anil Wajiyz (uk. 266)]
Isitoshe, kihakika, Kutufu Nyumba ni bora zaidi kuliko Kusai, na ni vyema zaidi kuliko kutaabika kutoka kwenda hadi At-Tan-‘iym ili kuhirimia ’Umrah mpya. Na kwa sasa inajulikana vizuri kabisa kuwa muda ambao mtu anautumia katika kutoka kwenda At-Tan-‘iym ili ahirimie ‘Umrah mpya, anaweza kwa muda huo kuzunguka Al-Ka’abah mamia ya mizunguko.
Ninasema: “Hili ni kwa yule aliyefanya ‘Umrah kabla ya Hajj na akataka –baada ya Hajj- kuikariri tena ‘Umrah yake, au alikuwa amefanya ‘Umrah na akataka kufanya tena. Ama mwenye hali kama ya ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa) ambapo hakuweza kufanya ‘Umrah kabla ya Hajj, basi hakuna ubaya kufanya ‘Umrah baada ya kumaliza Hajj yake kwa kuzifanyia kazi dalili zote. [Haya kayasema Al-‘Allaamah Ibn Baaz (Rahimahul Laah) kama ilivyo katika Kitabu cha Tawdhwiyhul Ahkaam cha Bassaam (3/247)]. Na hii ni kauli wastani zaidi katika suala hili. Allaah Ndiye Ajuaye zaidi”.
Nguzo za ‘Umrah
1- Kuhirimia
2- Kutufu
3- Kusai
Mwenye kuacha nguzo yoyote kati ya hizi, basi ‘Umrah yake haitimu.
Waajibaat za ‘Umrah
1- Kuhirimia toka kwenye Miyqaat
Ni lazima kwa anayetaka kufanya ‘Umrah ahirimie toka kwenye Miyqaat kama anaishi nje ya eneo la Miyqaat. Na kama anaishi ndani ya eneo la Miyqaat, basi atahirimia toka nyumbani kwake. Ama mkazi wa Makkah, huyo atatoka kwenda nje ya mipaka ya Haram (At-Tan-‘iym au kwingineko) na atahirimia kutoka huko kama alivyofanya ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhaa).
2- Kunyoa au kupunguza
Swahiyh Fiqh As-Sunnah
Mlango Wa Hajj Na ‘Umrah
32-Ziara Madiynah
Alhidaaya.com [3]
Utukufu wa Madiynah
Toka kwa Jaabir bin Samurah amesema: “Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema:
((إن الله تعالى سمى المدينة طابة))
((Hakika Allaah Ta’aalaa Ameiita Al-Madiynah Twaabah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1385)]
Na toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((إِنَّ الْمَدِينَةَ كَالْكِيرِ تُخْرِجُ الْخَبِيثَ . لاَ تَقُومُ السَّاعَةُ حَتَّى تَنْفِيَ الْمَدِينَةُ شِرَارَهَا كَمَا يَنْفِي الْكِيرُ خَبَثَ الْحَدِيدِ))
((Hakika Madiynah ni kama mvukuto [wa mhunzi] ambao utamtoa mwovu toka humo. Haisimami Saa (Qiyaamah) mpaka Madiynah iwatoe wabaya wake kama mvukuto unavyotoa uchafu wa chuma)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1381)]
Ubora wa Msikiti wake na fadhla za kuswali ndani yake
Toka kwa Abu Hurayrah kwamba Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((لا تشد الرحال إلا إلى ثلاثة مساجد، مسجدي هذا، ومسجد الحرام، ومسجد الأقصى))
((Safari hazifungwi isipokuwa kwa Misikiti Mitatu; Msikiti wangu huu, Masjidil Haraam na Masjidil Aqswaa)). [Muttafaqun ‘Alayhi. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1189) na Muslim (1397)]
Na kasema tena Abu Hurayrah: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((صلاة في مسجدي هذا خير من ألف صلاة في غيره من المساجد، إلا المسجد الحرام))
((Swalaah moja katika Msikiti wangu huu ni bora kuliko Swalaah elfu moja kwenye Misikiti mingine isipokuwa Al-Masjidil Haraam)). [Muttafaqun ‘Alayhi. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1190) na Muslim (1394)]
Na toka kwa ‘Abdullaah bin Zayd kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam amesema:
((ما بين بيتي ومنبري روضة من رياض الجنة))
((Sehemu iliyo baina ya nyumba yangu na mimbari yangu ni kiwanja kati ya viwanja vya Jannah)). [Muttafaqun ‘Alayhi. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1195) na Muslim (1390)]
Adabu za kuzuru Msikiti wa Rasuli na Kaburi lake tukufu
Ubora uliohusishiwa Msikiti Mtukufu wa Rasuli, Al-Masjidul Haraam na Al-Masjidul Aqswaa, na Swalaah ndani yake kuwa na thawabu zaidi kuliko kwenye Misikiti Mingineyo, bila shaka hiyo ni takrima toka kwa Allaah Subhaanahu wa Ta’aalaa. Mwenye kuiendea, bila shaka anafanya hivyo kwa utashi wa kupata thawabu na kuitikia wito wa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alipohimizia watu wafunge safari kuiendea na kuizuru.
Misikiti hii Mitatu haina adabu maalum kulinganisha na Misikiti Mingine. Lakini baadhi ya watu hukanganyikiwa na kuufanyia Msikiti wa Rasuli adabu mahsusi kutokana na kuwepo kaburi lake ndani ya Msikiti.
Na ili Muislamu awe analijua jambo vizuri akija Madiynah na akataka kuuzuru Msikiti wa Rasuli, hapa sisi tunamhabarisha adabu hizo za ziyara.
1- Anapoingia aingie kwa mguu wake wa kulia, kisha aseme:
((اللهم صل على محمد وسلم، اللهم افتح لي أبواب رحمتك))
((Ee Allaah! Mswalie Muhammad na Mpe salaam. Ee Allaah! Nifungulie milango ya Rahmah Zako)).
Au:
((أعوذ بالله العظيم، وبوجهه الكريم، وسلطانه القديم، من الشيطان الرجيم))
((Najilinda kwa Allaah Al-‘Adhwiym, na kwa Uso Wake Al-Kariym, na kwa Uqahari Wake wa Azali, kutokana na Shaytwaan aliyewekwa mbali na rahmah)).
2- Kisha ataswali rakaa mbili za Maamkuzi ya Msikiti (Tahiyyatul Masjid) kabla hajakaa.
3- Atahadhari asiswali kwa kulielekea Kaburi Tukufu, au kulielekea wakati anapoomba du’aa.
4- Halafu atakwenda kwenye Kaburi Tukufu ili amtolee salaam Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), na atahadhari asiweke mikono yake kifuani, au kuinamisha kichwa, au kujinyenyekeza –ambako hakutakikani kwa yeyote isipokuwa kwa Allaah Pekee-, au kumlilia shida Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Amtolee salaam Rasuli kwa matamshi na maneno ambayo yeye mwenyewe alikuwa akiwasalimia kwayo Ahlul Baqiy’i. Kuna matamshi kadhaa swahiyh yaliyopokelewa toka kwake ambayo kati yake ni:
((السلام علي أهل الديار من المؤمنين والمسلمين ويرحم الله المستقدمين منا والمستأخرين، وإنا إن شاء الله بكم للاحقون))
((Amani iwe juu ya watu wa makazi haya kati ya Waumini na Waislamu, na Allaah Awarehemu waliotangulia kati yetu na wanaofuatia nyuma. Na sisi bila shaka Akipenda Allaah tutaungana nanyi)).
Kisha atawatolea salaam Maswahibu wake wawili Abu Bakr na ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa)) kwa salaam hiyo hiyo.
5- Asinyanyue sauti ndani ya Msikiti au mbele ya Kaburi Tukufu, sauti yake iwe ya chini. Kwa kuwa kumfanyia hishma Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akiwa maiti ni kama kumfanyia akiwa hai.
6- Afanye pupa kuswali Jamaa katika safu za mwanzo mwanzo kutokana na fadhla kubwa na thawabu nyingi zinazopatikana katika safu hizo.
7- Pupa ya kuswalia kwenye Rawdhwah isimfanye achelewe kuwahi safu za mwanzo, kwani kuswalia kwenye Rawdhwah hakuna tofauti na kuswalia sehemu nyingine yoyote ya Msikiti.
8- Si katika Sunnah mtu kupapia kuswali kwenye Msikiti Swalaah arobaini mfululizo kwa kutegemea Hadiyth Dhwa’iyf iliyotangaa kwa watu wengi isemayo:
((من صلى في مسجدي أربعين صلاة لا يفوته صلاة؛ كُتبت له براءة من النار، ونجاة من العذاب، وبرئ من النفاق))
((Mwenye kuswali kwenye Msikiti wangu Swalaah arubaini isimpite Swalaah yoyote, ataandikiwa kutoguswa na moto, kuokoka na adhabu, na atatakasika na unafiki)). [Hadiyth Dhwa’iyf, haifai. Angalia Adh-Dhwa’iyfah (364)]
9- Si katika sharia mtu kupita mara kwa mara kwenye Kaburi Tukufu ili kumtolea salaam Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam), kwani salaam humfikia toka sehemu yoyote hata ikitolewa toka mwisho wa dunia. Anayetoa salaam akiwa mbele ya Kaburi la Rasuli na aliyeko mwisho wa ncha ya ardhi, wote wanapata thawabu sawa za kumswalia Rasuli na kumtolea salaam.
10- Anapotoka Msikitini asitembee kinyume nyume, bali atoke kwa mguu wake wa kushoto akisema:
((اللهم صل على محمد، اللهم إني أسألك من فضلك))
((Ee Allaah! Mswalie Muhammad. Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba Fadhla Zako)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1193) na Muslim (1399)]
Masjid Qubaa
Imesuniwa kwa aliyekwenda Madiynah aukusudie na auendee Masjid Qubaa na aswali humo kufuata kitendo cha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam). Rasuli alikuwa ameuwekea ahadi ya kuuzuru, na anauendea kila siku ya Jumamosi na kuswali ndani yake rakaa mbili. Alikuwa anakwenda kwa miguu au kwa kupanda mnyama. [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1193) na Muslim (1399)]
Na alikuwa anasema:
((من تطَهَّرَ في بيتِهِ، ثمَّ أتى مسجدَ قباءٍ، فصلَّى فيهِ صلاةً، كانَ لَهُ كأجرِ عمرة))
((Mwenye kutawadha nyumbani kwake, kisha akauendea Masjid Qubaa, akaswali ndani yake Swalaah moja, basi anapata thawabu za mfano wa ‘Umrah)). [Al-Albaaniy kasema ni Swahiyh. Imekharijiwa na Ibn Maajah (1412)]
Al-Baqiy’u na Uhud
Al-Baqiy’u ni eneo la makaburi ya Waislamu huko Madiynah. Hapo wamezikwa Swahaba wengi, na bado Waislamu wanaendelea kuzikwa hapo hadi hivi leo. Wengi wanaozikwa hivi leo ni wale wanaokwenda Madiynah kwa utashi wa kufia huko ili wazikwe Al-Baqiy’u.
Na Uhud kama anavyosema Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam):
((وأحد جبل يحبنا ونحبه))
((Na Uhud ni Mlima, unatupenda na sisi tunaupenda)). [Muttafaqun ‘Alayhi. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (4083) na Muslim (1393)]
Katika uwanda wake walizikwa Shuhadaa sabini na kitu hivi waliouawa katika vita vilivyotokea hapo. Vita hivyo vimenasibishiwa Mlima huu na kujulikana kama Vita vya Uhud. Na yeyote aliyekwenda Madiynah na akataka kuzuru Al-Baqiy’u, au kuwazuru Shuhadaa hao, basi hakuna ubaya. Kwani Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) alikuwa amekataza kuyazuru makaburi kisha akaja kuruhusu ili yawakumbushe watu Aakhirah na wawaidhike na hatima ya waliomo ndani yake. Lakini ni lazima mtu atahadhari kutabaruku na makaburi, au kuwalilia shida maiti, au kuwaomba wamsaidie kutatua matatizo yake kwa walio hai, au kutawassal kwao kama njia ya kumfikia Mola wa waja.
Na hakuna usharia kwa anayekwenda Uhud akusudie kisemwacho kama "مصلى النبي" chini ya Mlima ili aswali hapo, au kupanda Mlima wa Uhud kupata barkah, au kupanda Mlima wa walenga mishale ili kufuatishia athari ya mabaki ya ukumbusho wa Swahaba hao. Hayo yote na mengineyo hayafai, ni mambo ya uzushi yaliyokatazwa. La muhimu hapo ni kuwatolea salaam na kuwaombea du’aa Shuhadaa hao. Na kuhusu hilo, Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) anasema:
((إنما هلك من كان قبلكم بتتبعهم آثار أنبيائهم))
((Hakika waliangamia waliopita kabla yenu kwa sababu ya kufuatilia kwao athari za mabaki ya kumbukumbu za Manabii wao)).
Basi tuyazingatie vyema maneno haya ya Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa)) na tuyatekeleze.
Mazaaraat
Kuna maeneo mengineyo Madiynah yajulikanayo kama Mazaaraat. Ni kama Al-Masaajidu As-Sab-‘at (Misikiti Saba) iliyo karibu na eneo la Vita vya Khandaq, Masjid Al-Qiblatayn, baadhi ya visima, Masjid Al-Ghamaamah, na Misikiti inayonasibishwa kwa Abu Bakr, ‘Umar na ‘Aaishah (Radhwiya Allaah ‘anhum). Maeneo haya yote, hayana lolote la kisharia linaloyahusisha kwa ziara, na mwenye kuyazuru asidhanie kabisa kuwa atapata thawabu za ziada kwa kuyatembelea. Kufuatisha athari ya mabaki ya kumbukumbu za Manabii na watu wema ilikuwa ndio sababu ya kuangamia umma zilizopita kabla yetu, na haiwi ni jambo zuri kwa Waislamu kukhalifu hadyi ya Nabii wao Muhammad (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) na hadyi ya Swahaba wake (Ridhwaanul Laah ‘alayhim). Kheri yote iko katika hadyi yake na hadyi yao, na shari yote iko katika kukhalifu hadyi yake na hadyi yao.
Maangalizi mawili muhimu sana
La kwanza: Mahujaji wengi hupupia kukaa Madiynah siku nyingi zaidi kuliko siku wanazokaa Makkah pamoja na kwamba Swalaah moja kwenye Al-Masjid Al-Haraam (Makkah) ni sawa na Swalaah laki moja kwenye Misikiti mingine. Ama Swalaah moja kwenye Al-Masjid An-Nabawiy (Madiynah) ni sawa na Swalaah elfu moja katika Misikiti mingine.
Tofauti hii kubwa ya malipo kati ya Swalaah kwenye Al-Masjid Al-Haraam na Al-Masjid An-Nabawiy ingebidi iwe chachu kwa Mahujaji hao ya kukaa zaidi Makkah kuliko Madiynah.
La pili: Mahujaji wengi wanadhani kuwa kuuzuru Msikiti wa Nabiy (Al-Masjid An Nabawiy) ni sehemu ya Manaasik za Hajj. Hivyo wanapapia hilo kama wanavyopapia Manaasik za Hajj kufikia hali ya kuona kwamba Hajj haikukamilika kwa ambaye hakwenda Madiynah.
Wanasimulia kuhusu hili Hadiyth kadhaa za kutungwa kama:
" من حج فلم يزرني فقد جفاني"
((Aliyehiji na hakunizuru, basi kanitupa mkono)).
Hivi wanavyodhani hawa ni kinyume kabisa. Kuuzuru Al-Masjid An-Nabawiy ni Sunnah aliyoiweka Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam kwa ajili ya kuswali ndani ya Msikiti, na hakuna mahusiano kati ya ziara hiyo na Hajj, na kuswihi Hajj hakuhusiani na ziara, bali ziara ni ‘ibaadah kando.
Yaliyo Marufuku Kwenye Haram Mbili (Makkah na Madiynah)
[Imenukuliwa toka Irshaadus Saariy cha Fadhwiylat baba Sheikh Muhammad Ibraahiym Shaqrah (uk. 260-261)]
Imekuja katika Swahiyh Mbili na kwengineko Hadiyth ya ‘Ibaad bin Tamiym toka kwa ami yake kuwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema:
((إنَّ إبراهيمَ حرَّم مكةَ، و دعا لها، و إنِّي حرَّمتُ المدينةَ ، كما حرَّم إبراهيمُ مكةَ))
((Hakika Ibraahiym aliiharamisha Makkah na akaiombea, na hakika mimi nimeiharamisha Madiynah kama Ibraahiym alivyoiharamisha Makkah)).
Uharamishaji huo bila shaka ni kwa Wahyi toka kwa Allaah Subhaanah kwa Manabii Wake na Mitume Wake hawa wawili Watukufu (Swalawaatul Laahi wa Salaamuhuu ‘alayhimaa). Tunaposema Al-Haramayn, basi tunakusudia Makkah na Madiynah, na haijuzu kisharia kuitwa kwa jina hilo isipokuwa Miji hii miwili tu. Hata Al-Masjid Al-Aqswaa, haufai kisharia kuitwa Al-Haram, wala kwa Msikiti wa Ibraahiym Al-Khaliyl, kwa kuwa Wahyi haukushuka na jina Haram isipokuwa kwa Makkah na Madiynah tu. Na hiyo ni sharia, akili ya binadamu hapo si uwanja wake.
Kuna mambo yaliyopigwa marufuku kuyafanya katika ardhi za Makkah na Madiynah kwa mkazi asili au kwa wenye kuitembelea kwa Hajj au ‘Umrah au kwa mengineyo. Mambo hayo ni:
1- Kuwinda wanyama au ndege, kuwatimua au kusaidia katika kuwadhuru.
2- Kukata mimea na miba isipokuwa kwa haja au dharura.
3- Kubeba silaha.
4- Kuokota alichoangusha au alichopoteza mtu katika Haram ya Makkah kwa Hujaji. Ama kwa mkazi wa Makkah, huyu anaruhusiwa kukiokota ili akitangazie. Na tofauti kati ya Hujaji na mkazi i wazi katika hilo.
Ninasema: “Dalili ya marufuku hizi ni neno lake Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) Siku ya Ukombozi wa Makkah:
((إنَّ هَذَا الْبَلَدَ حَرَّمَهُ اللَّهُ يَوْمَ خَلَقَ اللَّهُ السَّمَوَاتِ وَالأَرْضَ، فَهُوَ حَرَامٌ بِحُرْمَةِ اللَّهِ إلَى يَوْمِ الْقِيَامَةِ، وَإِنَّهُ لَمْ يَحِلَّ الْقِتَالُ فِيهِ لأَحَدٍ قَبْلِي، وَلَمْ يَحِلَّ لِي إلاَّ سَاعَةً مِنْ نَهَارٍ؛ فَهُوَ حَرَامٌ بِحُرْمَةِ اللَّهِ إلَى يَوْمِ الْقِيَامَةِ. لا يُعْضَدُ شَوْكُهُ، وَلا يُنَفَّرُ صَيْدُهُ، وَلا يَلْتَقِطُ لُقْطَتَهُ إلاَّ مَنْ عَرَّفَهَا، وَلا يُخْتَلَى خَلاهُ))، فَقَالَ الْعَبَّاسُ : يَا رَسُولَ اللَّهِ , إلاَّ الإِذْخِرَ ، فَإِنَّهُ لِقَيْنِهِمْ وَبُيُوتِهِمْ . فَقَالَ: إلاَّ الإِذْخِرَ .
((Hakika Allaah Ameuharamisha Mji huu Siku Allaah Alipoumba mbingu na ardhi. Basi Mji huu ni hifadhi isiyoguswa kwa Haramisho la Allaah hadi Siku ya Qiyaamah, na hakuruhusiwa yeyote kabla yangu kupigana ndani yake, na haikuruhusiwa kwangu isipokuwa saa moja ya mchana. Basi ni hifadhi isiyoguswa kwa Haramisho la Allaah mpaka Siku ya Qiyaamah. Mwiba wake haukatwi, wala wanyama wake wa kuwindwa hawatimuliwi, wala haokoti chenye kupotezwa humo isipokuwa mwenye kukitangazia, na wala manyasi yake hayakatwi)). Ibn ‘Abbaas akasema: Ee Rasuli wa Allaah! Isipokuwa “idh-khir” (aina ya mmea wenye harufu nzuri), kwani huo ni kwa mhunzi [kuwashia moto] na kwa [kuezekea paa za] nyumba zao. Akasema: ((Isipokuwa idh-khir)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Al-Bukhaariy (1834) na Muslim (1353)]
Toka kwa Jaabir amesema: Nimemsikia Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) akisema:
((لا يحل لأحدكم أن يحمل بمكة السلاح))
((Ni marufuku kwa mmoja wenu kubeba silaha Makkah)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Muslim (1356)]
Na toka kwa ‘Aliyy toka kwa Nabiy (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) amesema [yaani kuhusu Madiynah]:
((لَا يُخْتَلَى خَلَاهَا، وَلَا يُنَفَّرُ صَيْدُهَا، وَلَا تُلْتَقَطُ لُقَطَتُهَا إلَّا لِمَنْ أَشَادَ بِهَا، وَلَا يَصْلُحُ لِرَجُلٍ أَنْ يَحْمِلَ فِيهَا السِّلَاحَ لِقِتَالٍ وَلَا يَصْلُحُ أَنْ يقْطَعَ فِيهَا شَجَرَةٌ إلَّا أَنْ يَعْلِفَ رَجُلٌ بَعِيرَهُ))
((Manyasi yake hayakatwi, wala wanyama wake wa kuwindwa hawatimuliwi, wala hakiokotwi kiokotwa chake ila kwa atakayekitangazia, na wala haifai kwa mwanaume kubeba silaha kwa ajili ya mapigano, na wala haifai kukatwa humo mti isipokuwa mtu amkatie ngamia wake majani ya malisho)). [Hadiyth Swahiyh. Imekharijiwa na Abu Daawuwd (2018)]
Sheikh Shaqrah amesema: “Mwenye kufanya marufuku hizi basi atapata madhambi, na ni lazima atubie na kuomba maghfirah isipokuwa kwa mnyama. Ikiwa aliyehirimia atamwinda, basi ni lazima achinje mnyama wa malipo mbali na kutubia na kuomba maghfirah”.
Links
[1] https://www.alhidaaya.com/sw/taxonomy/term/284
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10436&title=06-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20%D9%83%D9%90%D8%AA%D8%A7%D8%A8%D9%8F%20%D8%A7%D9%84%D9%92%D8%AD%D9%8E%D8%AC%D9%91%20%D9%88%D9%8E%D8%A7%D9%84%D9%92%D8%B9%D9%8F%D9%85%D9%92%D8%B1%D9%8E%D8%A9%20-%20Kitabu%20Cha%20Hajj%20Na%20%27Umrah%20
[3] http://www.alhidaaya.com
[4] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10591&title=01-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Taarifu%20Ya%20Hajj
[5] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10592&title=02-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Hukmu%20Ya%20Hajj
[6] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10593&title=03-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Je%2C%20Ni%20Waajib%20Kuharakia%20Kuhiji%20Au%20Mtu%20Anaweza%20Kuchelewesha%3F
[7] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10594&title=04-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Miongoni%20Mwa%20Fadhila%20Za%20Hajj
[8] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10595&title=05-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Shuruti%20Za%20Kuwajibisha%20Hajj
[9] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10596&title=06-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Ni%20Vipi%20Vigezo%20Vya%20Uwezo%20Wa%20Kuhiji%3F
[10] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10597&title=07-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kumhijia%20Mwingine
[11] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10598&title=08-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Mawaaqiyt%20%28Nyakati%20Na%20Mahala%20Pa%20Kuhirimia%29
[12] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10599&title=09-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Picha%20Halisi%20Ya%20Hijjah%20ya%20Nabiy%20%28%D8%B5%D9%84%D9%89%20%D8%A7%D9%84%D9%84%D9%87%20%D8%B9%D9%84%D9%8A%D9%87%20%D9%88%D8%A2%D9%84%D9%87%20%D9%88%D8%B3%D9%84%D9%85%29%20%20%20
[13] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10600&title=10-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Muhtasari%20Wa%20Vitendo%20Vya%20Hajj%20Ya%20Mwenye%20Kufanya%20Tamattu%E2%80%99u
[14] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10601&title=11-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Nguzo%20Za%20Hajj%3A%20Nguzo%20Ya%20Kwanza%20Ya%20Hajj%3A%20Kuhirimia%20%28Al-Ihraam%29
[15] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10602&title=12-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Sunnah%20Za%20Kuhirimia
[16] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10603&title=13-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Tamko%20La%20Talbiyah
[17] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10604&title=14-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Marufuku%20Za%20Ihraam
[18] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10605&title=15-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Mambo%20Ambayo%20Muhrim%20Anaruhusiwa%20Kuyafanya%20Bila%20Tatizo
[19] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10606&title=16-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kuingia%20Makkah%20
[20] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10607&title=17-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Nguzo%20Ya%20Pili%20Ya%20Hajj%3A%20Twawaaf%20%E2%80%9CKutufu%E2%80%9D%20%28Twawaaful%20Ifaadhwah%29
[21] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10608&title=18-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Hukmu%20Kiujumla%20Kuhusu%20Twawaaf
[22] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10609&title=19-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Sunan%20Za%20Twawaaf
[23] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10610&title=20-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Nguzo%20Ya%20Tatu%20Ya%20Hajj%3A%20Sa%27yi%20Kati%20Ya%20As-Swafaa%20Na%20Al-Marwah%20
[24] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10611&title=21-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Ahkaam%20Za%20Sa%E2%80%99yi%20Baina%20Ya%20As-Swafaa%20Na%20Al-Marwah
[25] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10612&title=22-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kunyoa%20Na%20Kupunguza%20Kwa%20Mwenye%20Kufanya%20Tamattu%E2%80%99u
[26] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10613&title=23-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Sunnah%20Za%20Kutoka%20Kwenda%20Minaa
[27] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10614&title=24-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Nguzo%20Ya%20Nne%20Ya%20Hajj%3A%20Kusimama%20%E2%80%98Arafah
[28] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10615&title=25-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kulala%20Muzdalifah%20Usiku%20Wa%20Yawm%20An-Nahr
[29] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10616&title=26-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Jamaraat%20%28Kurusha%20Vijiwe%29%20Minaa
[30] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10617&title=27-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Tahallul%20%28Kujivua%20Ihraam%29%20Ya%20Kwanza%20Na%20Ya%20Pili
[31] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10618&title=28-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20
[32] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10619&title=29-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kunyoa%20Na%20Kupunguza
[33] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10620&title=30-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sun%20nah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kupitwa%20Na%20Hajj%20Na%20Kuzuilika
[34] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10621&title=31-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Kutekeleza%20%E2%80%98Umrah%20Na%20Fadhila%20Zake
[35] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F10622&title=32-Swahiyh%20Fiqh%20As-Sunnah%3A%20Mlango%20Wa%20Hajj%20Na%20%27Umrah%3A%20Ziara%20Ya%20Madiynah%20%20