Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب تحريم لباس الحرير عَلَى الرجال ، وتحريم جلوسهم
عَلَيْهِ واستنادهم إِلَيْهِ وجواز لبسه للنساء
06-Mlango Wa Uharamu wa Kuvaa Hariri kwa Wanaume na Uharamu wa Kukaa Juu Yake na Kuegemea na Kujuzu Kuvaa kwa Wanawake
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن عمر بن الخَطَّابِ رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( لاَ تَلْبَسُوا الحَرِيرَ ؛ فَإنَّ مَنْ لَبِسَهُ في الدُّنْيَا لَمْ يَلْبَسْهُ في الآخِرَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa 'Umar bin Khatwaab (Radhwiya Allaah 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Musivae hariri, hakika mwenye kuvaa duniani hatovaa Aakherah." [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy na An-Nasai]
Hadiyth – 2
وعن عمر بن الخَطَّابِ رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : (( إنَّمَا يَلْبَسُ الحَرِيرَ مَنْ لاَ خَلاَقَ لَهُ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
وفي رواية للبخاري : (( مَنْ لاَ خَلاَقَ لَهُ في الآخِرَةِ )) .
Amesema 'Umar Al-Khatwaab (Radhwiya Allaahu 'anhu) akisema: "Hakika anayevaa hariri ni yule asiye na fungu (hatovaa) Aakherah." [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasai]
Na katika riwaayah ya Al-Bukhaariy: "Ni asiye na fungu lake Aakherah."
Hadiyth – 3
وعن أنس رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( مَنْ لَبِسَ الحَرِيرَ في الدُّنْيَا لَمْ يَلْبَسْهُ في الآخِرَةِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .
Imepokewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Mwenye kuvaa hariri duniani hatovaa Aakherah." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Hadiyth – 4
وعن علي رضي الله عنه ، قَالَ : رأيتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم أخَذَ حَريراً ، فَجَعَلَهُ في يَمِينهِ ، وَذَهَبَاً فَجَعَلَهُ في شِمَالِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( إنَّ هذَيْنِ حَرَامٌ عَلَى ذُكُور أُمّتي )) رواه أَبُو داود بإسنادٍ صحيحٍ .
Amesema 'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nilimuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akichukua hariri na kuiweka mkono wake wa kulia na dhahabu akaishika kwa mkono wake wa kushoto, kisha akasema: "Hakika hivi vitu viwili ni haramu kwa wanaume wa Ummah wangu." [Abu Daawuwd kwa Isnaad Hasan]
Hadiyth – 5
وعن أَبي موسى الأشْعَري رضي الله عنه : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : (( حُرِّمَ لِبَاسُ الحَرِير وَالذَّهَبِ عَلَى ذُكُورِ أُمَّتِي ، وَأُحِلَّ لإنَاثِهِمْ )) رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .
Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-'Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Imeharamishwa kuvaa hariri na dhahabu kwa wanaume wa Ummah wangu na ikahalalishwa kwa wanawake wao." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]
Hadiyth – 6
وعن حُذَيْفَةَ رضي الله عنه ، قَالَ : نَهَانَا النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم أنْ نَشْرَبَ في آنِيَةِ الذَّهَبِ وَالفِضَّةِ ، وأنْ نَأْكُلَ فِيهَا ، وعَنْ لُبْس الحَريرِ وَالدِّيبَاج ، وأنْ نَجْلِسَ عَلَيْهِ . رواه البخاري .
Amesema Hudhayfah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Ametukataza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kunywa katika vyombo vya dhahabu na fedha na kula ndani yake na pia kuvaa hariri na dibaji na kukaa juu yake." [Al-Bukhaariy]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11010&title=06-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Uharamu%20wa%20Kuvaa%20Hariri%20kwa%20Wanaume%20na%20Uharamu%20wa%20Kukaa%20Juu%20Yake%20na%20Kuegemea%20na%20Kujuzu%20Kuvaa%20kwa%20Wanawake