Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن المنِّ بالعطية ونحوها
025-Mlango Wa Kukatazwa Kumsimanga Mtu kwa Ulichompa na Mfano Wake
Alhidaaya.com [1]
قال الله تَعَالَى :
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُبْطِلُوا صَدَقَاتِكُم بِالْمَنِّ وَالْأَذَىٰ ﴿٢٦٤﴾
Enyi walioamini! Msibatilishe swadaqah zenu kwa masimbulizi na udhia [Al-Baqarah: 264]
الَّذِينَ يُنفِقُونَ أَمْوَالَهُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ثُمَّ لَا يُتْبِعُونَ مَا أَنفَقُوا مَنًّا وَلَا أَذًى ۙ ﴿٢٦٢﴾
Wale wanaotoa mali zao katika Njia ya Allaah kisha hawafuatishii kwa waliyoyatoa masimbulizi wala udhia [Al-Baqarah: 262]
وعن أَبي ذَر رضي الله عنه ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ : (( ثَلاَثَةٌ لاَ يُكَلِّمُهُمُ اللهُ يَوْمَ القِيَامَةِ ، وَلاَ يَنْظُرُ إلَيْهِمْ ، وَلاَ يُزَكِّيِهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَليمٌ )) قَالَ : فَقَرَأَهَا رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم ثلاثَ مِرارٍ : قَالَ أَبُو ذرٍ : خَابُوا وخَسِرُوا مَنْ هُمْ يَا رسول الله ؟ قَالَ : (( المُسْبِلُ ، والمَنَّانُ ، وَالمُنْفِقُ سِلْعَتَهُ بالحَلِفِ الكَاذِبِ )) . رواه مسلم .
وفي روايةٍ لَهُ : (( المُسْبِلُ إزَارَهُ )) يَعْنِي : المُسْبِلَ إزَارَهُ وَثَوْبَهُ أسْفَلَ مِنَ الكَعْبَيْنِ لِلخُيَلاَءِ .
Imepokewa kutoka kwa Abu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Allaah Hatazungumza na watu aina tatu Siku ya Qiyaamah wala Hatawaangalia na wala Hatawatakasa na watakuwa na adhabu iumizayo." Akasema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliikariri kauli hii mara tatu." Akasema Abu Dharr: "Watu hao wamehasirika, ni kina nani ee Rasuli wa Allaah?" Akasema: "Mwenye kuburuza nguo kwa kiburi; na mwenye kujionyesha kwa fadhila aliyomfanyia mtu mwengine; na mwenye kuuza mali duni kwa kiapo cha uongo." [Muslim]
Na katika riwaayah yake nyengine: "Mwenye kuburuza kikoi chake." Yaani: "Mwenye kuburuza kikoi chake na nguo yake chini ya kongo mbili kwa kiburi."
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11316&title=025-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20Kumsimanga%20Mtu%20kwa%20Ulichompa%20na%20Mfano%20Wake