Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب كراهة الحلف في البيع وإنْ كان صادقاً
065-Mlango Wa Ukaraha wa Kula Yamini katika Biashara Hata Akiwa Mkweli
Alhidaaya.com [1]
Hadiyth – 1
عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قال : سَمِعتُ رسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقولُ : (( الحَلِفُ مَنْفَقَةٌ لِلسِّلْعَةِ ، مَمْحَقَةٌ لِلْكَسْبِ )) . متفق عليه .
Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Kuapa sana katika biashara huenda kukaongeza mauzo lakini inafuta faida yote uliyopata." [Al-Bukhaariy na Muslim].
Hadiyth – 2
وعن أبي قتادة رضي الله عنه : أنَّه سمعَ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم ، يقولُ : (( إيَّاكُمْ وَكَثْرَةَ الحَلِفِ فِي البَيْعِ ، فَإنَّهُ يُنَفِّقُ ثُمَّ يَمْحَقُ )) . رواه مسلم .
Imepokewa kutoka kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa amemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Jiepusheni na kuapa yamini sana katika kuuza (bidhaa zenu), kwani hilo mwanzo huboresha biashara na kisha huleta hasara." [Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11385&title=065-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Ukaraha%20wa%20Kula%20Yamini%20katika%20Biashara%20Hata%20Akiwa%20Mkweli