Riyaadhw Asw-Swaalihiyn
باب النهي عن قول الإنسان : مُطِرنا بنَوء كذا
072-Mlango Wa Kukatazwa kwa Mtu Kusema: Tumepata Mvua Kutokana na Nyota Kadha
Alhidaaya.com [1]
عن زيد بن خالد رضي الله عنه قال : صلَّى بنا رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم صَلاَةَ الصُّبْحِ بِالحُدَيْبِيَّةِ في إثْرِ سَمَاءٍ كَانَتْ مِنَ اللَّيْلِ ، فَلَمَّا انْصَرَفَ أقْبَلَ عَلَى النَّاسِ ، فقالَ : (( هَلْ تَدْرُونَ مَاذَا قالَ رَبُّكُمْ ؟ )) قالُوا : اللهُ وَرَسُولُهُ أعْلَمُ . قال : (( قالَ : أصْبَحَ مِنْ عِبَادِي مُؤْمِنٌ بِي ، وَكَافِرٌ ، فَأَمَّا مَنْ قَالَ : مُطِرْنَا بِفَضْلِ اللهِ وَرَحْمَتِهِ ، فَذلِكَ مُؤْمِنٌ بِي كَافِرٌ بِالكَوْكَبِ ، وأَما مَنْ قَالَ مُطِرْنَا بِنَوءِ كَذَا وَكَذَا ، فَذلكَ كَافِرٌ بِي مُؤْمِنٌ بِالكَوْكَبِ )) . متفق عليه .
Amesema Zayd bin Khaalid (Radhwiya Allaahu 'anhu): Alituswalisha sisi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Swalaah ya Asubuhi katika Hudaybiyah baada ya mvuaa zilizonyesha usiku uliopita. Alipomaliza akawaelekea watu na kuwauliza: "Je, mnaelewa Alichosema Rabb wenu?" Wakajibu: "Allaah na Rasuli Wake wanajua zaidi." Akasema: "Baadhi ya waja wangu wamepambazukiwa na asubuhi wakiwa Wananiamini na baadhi Wamenikufuru; ama aliyesema tumepata mvua kwa fadhila ya Allaah na Rehema Zake, basi huyo ni mwenye kuniamini na mwenye kukufuru nyota; ama mwenye kusema tumepata mvua kutokana na nyota kadha wa kadha huyo Amenikufuru na ni mwenye kuamini nyota." [Al-Bukhaariy na Muslim]
Links
[1] http://www.alhidaaya.com/
[2] https://www.addtoany.com/share#url=https%3A%2F%2Fwww.alhidaaya.com%2Fsw%2Fnode%2F11392&title=072-Riyaadhw%20Asw-Swaalihiyn%3A%20Mlango%20Wa%20Kukatazwa%20kwa%20Mtu%20Kusema%3A%20Tumepata%20Mvua%20Kutokana%20na%20Nyota%20Kadha